Salama wakuu,naombeni msaada kwani kuna rafiki yangu yuko kwa Bibi (Uingereza) anataka kunitumia gari la kutumia hapa mjini.ni Toyota Collora 1997,(Saloon), lakini gharama za kuikomboa gari Bandarini ni juu yangu,Kwa hiyo naomba kujua Gharama za kuikomboa hapa Bandarini (Dar) natanguliza shukrani.
mkuu nahisi umekosea jukwaa peleka kule kwenye biashara pande hizi ni full uongo, kujipambanua, malumbano, wenye uchungu na nchi, mafisadi, kampeni, mwisho wa siku kitu kinaitwa siasa so jukwaa hili ni la siasa zaidi,
Ngoja wataalam waje, maana mimi layman gari yoyote iliovuka zaidi ya miaka 10 iliyopita gharama yake inakua juu sana pale bandarini, coz nikama vile unaleta takataka hapa bongo. Hivyo cost itakua ya juu kidogo.Hem njooni mumpe huyu