Gibbons Mwaikambo

Gibbons Mwaikambo

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2008
Posts
4,768
Reaction score
2,361
MODS mmeondoa thread hiyo hapo juu, ambayo kuna member aliulizia.
Nampa ukweli wa Gibbons Mwaikambo kwa ufupi.
Hii mada hata leo ina somo kubwa.



Watoto waliozaliwa majuzi hawawezi kumfahamu.


Gibbons Mwaikambo alizaliwa 1938 huko Tukuyu, Mbeya na alisomea Economics mpaka kiwango cha shahada ya Masters huko Moscow ,Urusi, 1967.
Gibbons alioana na Ester Mariki, binti wa kichagga.

Baada ya mashirika mengi kutaifishwa Gibbons alikuwa General Manager wa muda mrefu NIC, National Insurance Corporation.
Alisifika kwa kulipaisha kiuchumi shirika hilo na kufikia kuwa shirika moja lenye nguvu kiuchumi.

Baada ya kustaafu, miaka ya 80 akaona ajaribu mkono wake katika siasa.
Awali alikuwa kama sikosei, aidha wadhamini wa chama au idara ya chama ,WAZAZI, hili sina uhakika, lakini alikuwa kiongozi CCM.

Hata hivyo kwa sababu zisizojulikana alifanyiwa ile kitu inaitwa figisu na jina lake katika changuzi za ndani ya CCM halikupitishwa.
Mgombea mwenza wa nafasi hiyo alikuwa Emmanuel Mwabulukutu, afisa aliyekuwa wa muda mrefu wa Idara ya Usalama.

Kuiona hiyo figisu, na kwamba alikuwa kiongozi ndani ya CCM, kwa ghadhabu Gibbons alitaka kufanya maamuzi magumu kujitoa ndani ya chama na kujiunga na TLP, chama chenye nguvu, kilichokuwa cha upinzani kikiongozwa na Lyatonga Mrema.
Siri hiyo aliwaambia rafiki zake wa karibu.

Kosa kubwa.

Hakuna siri ya watu wawili. Na miaka ya Mwalimu kila mtu alikuwa anamchunguza mwenziwe.

Muda si mrefu siri iliwafikia wana Usalama kuwa kesho yake Gibbons anajitoa CCM.
Usiku huo huo Gibbons alitekwa.
Asubuhi yake gari lake lilikutwa limegonga ukuta wa nyumba moja ya kibalozi pale Upanga, naye amekufa ndani yake.
Ni wazi ilikuwa assasination.
 
Ulichokosea ni kwamba hakutaka kujiunga na TLP , TLP wakati huo haikuwa na Mrema ilikuwa na watu wengine moja wapo alikuwa Lekamwa,Mrema alikuwa NCCR. bali Mwaikambo alitaka kujiunga na CHADEMA ya kina Bob Makani, Brown Ngwilulupi na Edin Mtey. Mbowe wakati huo alikuwa kidampa tu.
 
Ulichokosea ni kwamba hakutaka kujiunga na TLP , TLP wakati huo haikuwa na Mrema ilikuwa na watu wengine moja wapo alikuwa Lekamwa,Mrema alikuwa NCCR. bali Mwaikambo alitaka kujiunga na CHADEMA ya kina Bob Makani, Brown Ngwilulupi na Edin Mtey. Mbowe wakati huo alikuwa kidampa tu.
Asante kwa masahihisho, lakini ndo ukweli wenyewe Mwaikambo alikuwa ana defect.
Tujazie historia .
 
Ulichokosea ni kwamba hakutaka kujiunga na TLP , TLP wakati huo haikuwa na Mrema ilikuwa na watu wengine moja wapo alikuwa Lekamwa,Mrema alikuwa NCCR. bali Mwaikambo alitaka kujiunga na CHADEMA ya kina Bob Makani, Brown Ngwilulupi na Edin Mtey. Mbowe wakati huo alikuwa kidampa tu.
Mkuu umefahamu vipi kuwabilikuwa ahamie CHADEMA maana kwa kumbukumbu zangu haikuwahi kutajwa.
 
MODS mmeondoa thread hiyo hapo juu, ambayobkuna member aliulizia.
Nampa ukweli wa Gibbons Mwsikambonkwa ufupi.
Hii mada hata leo ina somo kubwa.



Watoto waliozaliwa majuzi hawawezi kumfahamu.


Gibbons Mwaikambo alizaliwa 1938 huko Tukuyu, Mbeya na alisomea Economics mpaka kiwango cha shada ya Masters huko Moscow Urusi, 1967.
Gibbons aliona na Ester Mariki, binti wa kichagga.

Baada ya mashirika mengi kutaifishwa Gibbons alikuwa General Manager wa muda mrefu NIC, National Indurance Corporation.
Alisifika kwa kulipaisha kiuchumi shirika hilo na kufikia kuwa shirika moja lenye nguvu kiuchumi.

Baada ya kustaafu, miaka ya 80 akaona ajaribu mkono wake katika siasa.
Awali alikuwa kama sikosei, aidha wadhamini wa chama au idara ya chama ,WAZAZI, hili sina uhakika, lakini alikuwa kiongozi CCM.

Hata hivyo kwa sababu zisizojulikana alifanyiwa ile kitubinsitwa figisu na jina lake katika changuzi za ndani ya CCM halikupitishwa.
Mgombea mwenza wa nafasi hiyobalikuwa Emmanuel Mwabulukutu, afisa aliyekuwa wa muda mrefu wa Idara ya Usalama.

Kuiona hiyo figisu, na kwamba alikuwa kiongozi ndani ya CCM, kwa ghadhabu Gibbons alitaka kufanya maamuzi magumu kujitoa ndani ya chama na kujiunga na TLP, chama chenye nguvu, kilichokuwa cha upinzani kikiongozwa na Lyatonga Mrema.
Siri hiyo aliwaambia rafiki zake wa karibu.

Kosa kubwa.
Hakuna siri ya watu wawili. Na miaka ya Mwalimi kila mtu alikuwa anamchunguza mwenziwe.

Muda si mrefu siri iliwafikia wana Usalama kuwa kesho yake Gibbons anajitoa CCM.
Usiku huo huo Gibbons alitekwa.
Asubuhi yake gari lake lilikutwa limegonga ukuta wa nyumba moja ya kibalozi pale Upanga, naye amekufa ndani yake.
Ni wazi ilikuwa assasination.

Hapo kwenye NIC; I = INSURANCE na sio INDURANCE
 
Usiwe mvivu wa kutumia ubongo.
Google and check out the facts.
Hata hivyo kutokushirikisha ubongo wako kufikiri(ujinga) ni haki yako ya msingi.
Kwa bahati mbaya una utoto mwingi! Makosa katika andiko lako linadiscredit andiko na kutua andiko ambalo halikufanyiwa utafiti ni umbea. Kwanini utake ni google? Mwaikambo alipata ajali akapoteza uhai hakuuawa kama unavyodai.
 
Mzee Gibbons Mwaikambo almaarufu kama GBM inasemekana alizaliwa tarehe 14 Oktoba, 1938. Mzee huyu wa Kinyakyusa alibobea katika Masuala ya Uchumi akiwa amesoma Shahada ya Umahiri ya Sayansi ya Uchumi kwenye Chuo Kikuu cha Friendship kilichopo Moscow Urusi Mwaka, 1967.
Aidha, alihudhuria Kozi mbalimbali za Utawala wa Bima kikiwemo Cheti cha Utaalamu yaani Certified Insurance Certificate (CIC) na kusomea Masomo hayo Chuo cha BIMA kilichopo Mjini New York Marekani Mwaka, 1970. Aidha, alikuwa Mwanachama aliyebobea kwenye Asasi inayoundwa na Wakurugenzi wa Bima nchini Uingereza (Fellow Institute of Directors-United Kingdom) katika masuala ya utafiti na utawala.
Alibahatika kuoana na Mama Esther Mariki Mwaikambo Mwaka, 1967 ambaye ni Mchaga wa Mwika Kilimanjaro na kubahatika kupata watoto watano akiwemo James aliyerithi jina la Babu yake, Gwamaka na Nkundwe. Mke wake Esther Mwaikambo kwa sasa ni Profesa katika Chuo Kikuu Cha Tumaini Makumira. Ni Daktari Bingwa wa fani ya Udaktari akiwa Daktari Bingwa wa Kwanza Tanzania toka Mwaka, 1969 na amebobea kwenye fani hiyo kwa kumaliza Shahada ya Umahiri ya Udaktari na ya Uzamivu na kufanya Utafiti na Machapisho kadhaa hadi kuwa Profesa. Amepata pia kutunukiwa tuzo ya Dr Martin Luther King na balozi wa Marekani nchini Tarehe 6 Machi, 2013.
Mzee Gibbonce Mwaikambo alianzia kazi kama Meneja wa Bima Iringa mnamo Mwaka, 1970 wakati huo Dkt Amon James Nsekela akiwa Meneja Mkuu wa Shirika la Bima lililokuwa chini ya Wakoloni; Alimrithi Amon James Nsekela Mwaka, 1972 na Kuunda Shirika la Bima la Taifa, wakati Shirika hilo lina Mtaji wa kiasi cha Shillingi milioni 5.5 za Tanzania hadi GBM anaondoka mwaka 1989 inadaiwa aliliacha Shirika likiwa na vitega uchumi vya zaidi ya Sh. 31 bilioni za Tanzania.
Baadaye GBM akahamishiwa Benki ya Rasilimali (TIB) iliyoanzishwa mwaka, 1970 ikimilikiwa na Serikali wakati Asilimia 60% zilikuwa za Serikali moja kwa moja, Asilimia 30% zilikuwa hisa za NBC na asilimia 10% zilikuwa Hisa za NIC; GBM alifanya TIB hadi Mwaka, 1985 akiwa Meneja Mkuu; alifanya kazi na akina Iddi Simba akiwa Mwenyekiti wa Bodi, Amoafo, J. akiwa Mshauri wa Masuala ya Sera, Ndugu A. Kibona akiwa Meneja wa Idara ya Maendeleo na Ndugu Malaki akiwa Mkurugenzi wa Miradi. Mhe Chief Gibbons Mwaikambo, aliteuliwa kuwa Mbunge wa Taifa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwaka, 1980 na kutumika hadi Mwaka, 1985.
Moja ya Mapendekezo yake Bungeni ilikuwa kuishauri Serikali kuunda baadhi ya Kanuni za Kusimamia Ugawanyaji wa fedha za kigeni kwenye Mashirika na Kampuni. Alibainisha kuwa zipo kampuni ambazo utendaji wao mbovu unaathiri Kampuni zingine zinazotegemea Kampuni hizo zisizo na tija katika ufanisi wao. Akatoa Mfano wa Kampuni ya kutengeneza Matairi ya General Tyre ambayo alisema inakaribia kufungwa huku Matairi ya Kampuni zingine hayapewi kipaumbele. Alibainisha kuwa kuna migao mingine ya fedha isiokuwa na Umuhimu.
Ifahamike pia kuwa kwa ubobezi wake wa Masuala ya Bima alikuwa ndiye Mwafrika wa Kwanza kuwa Meneja wa Shirika la Bima kwa Afrika chini ya Wakoloni walioitawala Tanzania na Kuunda Shirika la Bima la Taifa; Kukubalika na Wakoloni haikuwa kazi nyepesi wakati huo. Aidha, Mhe Chief Gibbons Mwaikambo alikuwa ni mmoja ya Wadhamini wa Chama cha Mapinduzi na Mlezi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi.
GBM alipendwa na Mungu, alifariki mnamo Tarehe 4 Septemba, 1995 baada ya madai kuwa gari yake iligonga mti wengine wakidai ilipinduka na kuzua utata wa Kifo chake.
GBM mbali na usomi wake bado aliheshimika kuwa Chief wa kabila la Wanyakyusa ambapo ililazimika azikwe usiku kama zilivyo desturi za Kabila la Wanyakyusa kuenzi Mazishi ya Machifu yaani “Wanyafyale”.
MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI MHE. CHIEF GIBBONS .J MWAIKAMBO (GBM).
Hiyo ndo historia (kwa ufupi) ya Mzee Gibbons Mwaikambo ambayo nimeikuta sehemu jioni hii, nimetamani nikushirikishe na wewe ili kama ulikuwa na hamu ya kujua mawilimatatu kuhusu Mwaikambo uisome kabla ya kulala usiku huu. Mungu akitupa uzima simulizi kamili kuhusu Mzee GBM zitakujia kupitia kitabu cha "Wanyakyusa Mashuhuri", ambacho nitatamani nikiandike kama itampendeza Mungu.
Huyu ndo Mnyakyusa aliyetuhumiwa kuwa alikuwa na upendeleo sana kwa kuwaajiri kwa upendeleo watu wengi wa Mbeya na hasa Wanyakyusa kwenye Shirika la Bima, na baadaye akatungiwa utani wa kuwa amewahi kusema "Kazi hamna, ila Imbombo jilipo"
 
Kwa bahati mbaya una utoto mwingi! Makosa katika andiko lako linadiscredit andiko na kutua andiko ambalo halikufanyiwa utafiti ni umbea. Kwanini utake ni google? Mwaikambo alipata ajali akapoteza uhai hakuuawa kama unavyodai.
Damage control.
 
Mzee Gibbons Mwaikambo almaarufu kama GBM inasemekana alizaliwa tarehe 14 Oktoba, 1938. Mzee huyu wa Kinyakyusa alibobea katika Masuala ya Uchumi akiwa amesoma Shahada ya Umahiri ya Sayansi ya Uchumi kwenye Chuo Kikuu cha Friendship kilichopo Moscow Urusi Mwaka, 1967.
Aidha, alihudhuria Kozi mbalimbali za Utawala wa Bima kikiwemo Cheti cha Utaalamu yaani Certified Insurance Certificate (CIC) na kusomea Masomo hayo Chuo cha BIMA kilichopo Mjini New York Marekani Mwaka, 1970. Aidha, alikuwa Mwanachama aliyebobea kwenye Asasi inayoundwa na Wakurugenzi wa Bima nchini Uingereza (Fellow Institute of Directors-United Kingdom) katika masuala ya utafiti na utawala.
Alibahatika kuoana na Mama Esther Mariki Mwaikambo Mwaka, 1967 ambaye ni Mchaga wa Mwika Kilimanjaro na kubahatika kupata watoto watano akiwemo James aliyerithi jina la Babu yake, Gwamaka na Nkundwe. Mke wake Esther Mwaikambo kwa sasa ni Profesa katika Chuo Kikuu Cha Tumaini Makumira. Ni Daktari Bingwa wa fani ya Udaktari akiwa Daktari Bingwa wa Kwanza Tanzania toka Mwaka, 1969 na amebobea kwenye fani hiyo kwa kumaliza Shahada ya Umahiri ya Udaktari na ya Uzamivu na kufanya Utafiti na Machapisho kadhaa hadi kuwa Profesa. Amepata pia kutunukiwa tuzo ya Dr Martin Luther King na balozi wa Marekani nchini Tarehe 6 Machi, 2013.
Mzee Gibbonce Mwaikambo alianzia kazi kama Meneja wa Bima Iringa mnamo Mwaka, 1970 wakati huo Dkt Amon James Nsekela akiwa Meneja Mkuu wa Shirika la Bima lililokuwa chini ya Wakoloni; Alimrithi Amon James Nsekela Mwaka, 1972 na Kuunda Shirika la Bima la Taifa, wakati Shirika hilo lina Mtaji wa kiasi cha Shillingi milioni 5.5 za Tanzania hadi GBM anaondoka mwaka 1989 inadaiwa aliliacha Shirika likiwa na vitega uchumi vya zaidi ya Sh. 31 bilioni za Tanzania.
Baadaye GBM akahamishiwa Benki ya Rasilimali (TIB) iliyoanzishwa mwaka, 1970 ikimilikiwa na Serikali wakati Asilimia 60% zilikuwa za Serikali moja kwa moja, Asilimia 30% zilikuwa hisa za NBC na asilimia 10% zilikuwa Hisa za NIC; GBM alifanya TIB hadi Mwaka, 1985 akiwa Meneja Mkuu; alifanya kazi na akina Iddi Simba akiwa Mwenyekiti wa Bodi, Amoafo, J. akiwa Mshauri wa Masuala ya Sera, Ndugu A. Kibona akiwa Meneja wa Idara ya Maendeleo na Ndugu Malaki akiwa Mkurugenzi wa Miradi. Mhe Chief Gibbons Mwaikambo, aliteuliwa kuwa Mbunge wa Taifa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwaka, 1980 na kutumika hadi Mwaka, 1985.
Moja ya Mapendekezo yake Bungeni ilikuwa kuishauri Serikali kuunda baadhi ya Kanuni za Kusimamia Ugawanyaji wa fedha za kigeni kwenye Mashirika na Kampuni. Alibainisha kuwa zipo kampuni ambazo utendaji wao mbovu unaathiri Kampuni zingine zinazotegemea Kampuni hizo zisizo na tija katika ufanisi wao. Akatoa Mfano wa Kampuni ya kutengeneza Matairi ya General Tyre ambayo alisema inakaribia kufungwa huku Matairi ya Kampuni zingine hayapewi kipaumbele. Alibainisha kuwa kuna migao mingine ya fedha isiokuwa na Umuhimu.
Ifahamike pia kuwa kwa ubobezi wake wa Masuala ya Bima alikuwa ndiye Mwafrika wa Kwanza kuwa Meneja wa Shirika la Bima kwa Afrika chini ya Wakoloni walioitawala Tanzania na Kuunda Shirika la Bima la Taifa; Kukubalika na Wakoloni haikuwa kazi nyepesi wakati huo. Aidha, Mhe Chief Gibbons Mwaikambo alikuwa ni mmoja ya Wadhamini wa Chama cha Mapinduzi na Mlezi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi.
GBM alipendwa na Mungu, alifariki mnamo Tarehe 4 Septemba, 1995 baada ya madai kuwa gari yake iligonga mti wengine wakidai ilipinduka na kuzua utata wa Kifo chake.
GBM mbali na usomi wake bado aliheshimika kuwa Chief wa kabila la Wanyakyusa ambapo ililazimika azikwe usiku kama zilivyo desturi za Kabila la Wanyakyusa kuenzi Mazishi ya Machifu yaani “Wanyafyale”.
MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI MHE. CHIEF GIBBONS .J MWAIKAMBO (GBM).
Hiyo ndo historia (kwa ufupi) ya Mzee Gibbons Mwaikambo ambayo nimeikuta sehemu jioni hii, nimetamani nikushirikishe na wewe ili kama ulikuwa na hamu ya kujua mawilimatatu kuhusu Mwaikambo uisome kabla ya kulala usiku huu. Mungu akitupa uzima simulizi kamili kuhusu Mzee GBM zitakujia kupitia kitabu cha "Wanyakyusa Mashuhuri", ambacho nitatamani nikiandike kama itampendeza Mungu.
Huyu ndo Mnyakyusa aliyetuhumiwa kuwa alikuwa na upendeleo sana kwa kuwaajiri kwa upendeleo watu wengi wa Mbeya na hasa Wanyakyusa kwenye Shirika la Bima, na baadaye akatungiwa utani wa kuwa amewahi kusema "Kazi hamna, ila Imbombo jilipo"
Sensa ya wafanyakazi wa Bima iliyofanyika baada ya kuulizwa Bungeni suala hilo ,ilitoa majibu kuwa kwa uwingi, kabila la Wasukuma lilishika namba moja, pili Wachagga na tatu ndo Wanyakyusa.
 
Kwa bahati mbaya una utoto mwingi! Makosa katika andiko lako linadiscredit andiko na kutua andiko ambalo halikufanyiwa utafiti ni umbea. Kwanini utake ni google? Mwaikambo alipata ajali akapoteza uhai hakuuawa kama unavyodai.
Mkuu mzee yule alikuwa baba yetu.
Kwamba ajali aliyopata ni fake, hilo halina ubishi.
Wataalam wa kutengeneza ajali wapo.
Inakuwaje mtu alipata ajali lakini mifukoni mwake kukutwe michanga?
Waulize waliokutuma!
 
Mkuu mzee yule alikuwa baba yetu.
Kwamba ajali aliyopata ni fake, hilo halina ubishi.
Wataalam wa kutengeneza ajali wapo.
Inakuwaje mtu alipata ajali lakini mifukoni mwake kukutwe michanga?
Waulize waliokutuma!
Jenga hoja si kubwabwaja, una uhakika nimetumwa na nani? Hapo ndipo huwa mnakosea sana
 
Kwa bahati mbaya una utoto mwingi! Makosa katika andiko lako linadiscredit andiko na kutua andiko ambalo halikufanyiwa utafiti ni umbea. Kwanini utake ni google? Mwaikambo alipata ajali akapoteza uhai hakuuawa kama unavyodai.
Wala sikuti mkuu maana we ndio mtoto hapa.
Mtu ana defect(hata kama uamuzi huo haukuwa mzuri) kesho yake akutwa amekufa kwa "ajali"?

Whom are you kidding?
Kawaambie hilo chekechea wezio!
 
Asante kwa masahihisho, lakini ndo ukweli wenyewe Mwaikambo alikuwa ana defect.
Tujazie historia .
Sisi wengine ni wachanga kwenye historia ya nchi hii.
Jee Mzee Mwaikambo alikuwa na cheo gani katika CCM? Jee alikuwa na influence kubwa ya kisiasa?.
Nilivyosikia mimi kuhusu huyu mzee ni kwamba alikuwa ni mkabila aliyepitiliza kwani pale NIC lugha ya kinyakyusa ndiyo ilikuwa ndiyo lugha rasmi iliyokuwa inatumika kazini. Niliambiwa pia, kuanzia mfanya usafi, mpika chai karani na viongozi wengi walikuwa wanatoka uchaggani mwa nyanda za juu kusini. Mwisho wa yote hata vyeo vilikuwa vinatoka kikanda. Jee hali halisi ilikuwaje???
 
Mzee Gibbons Mwaikambo almaarufu kama GBM inasemekana alizaliwa tarehe 14 Oktoba, 1938. Mzee huyu wa Kinyakyusa alibobea katika Masuala ya Uchumi akiwa amesoma Shahada ya Umahiri ya Sayansi ya Uchumi kwenye Chuo Kikuu cha Friendship kilichopo Moscow Urusi Mwaka, 1967.
Aidha, alihudhuria Kozi mbalimbali za Utawala wa Bima kikiwemo Cheti cha Utaalamu yaani Certified Insurance Certificate (CIC) na kusomea Masomo hayo Chuo cha BIMA kilichopo Mjini New York Marekani Mwaka, 1970. Aidha, alikuwa Mwanachama aliyebobea kwenye Asasi inayoundwa na Wakurugenzi wa Bima nchini Uingereza (Fellow Institute of Directors-United Kingdom) katika masuala ya utafiti na utawala.
Alibahatika kuoana na Mama Esther Mariki Mwaikambo Mwaka, 1967 ambaye ni Mchaga wa Mwika Kilimanjaro na kubahatika kupata watoto watano akiwemo James aliyerithi jina la Babu yake, Gwamaka na Nkundwe. Mke wake Esther Mwaikambo kwa sasa ni Profesa katika Chuo Kikuu Cha Tumaini Makumira. Ni Daktari Bingwa wa fani ya Udaktari akiwa Daktari Bingwa wa Kwanza Tanzania toka Mwaka, 1969 na amebobea kwenye fani hiyo kwa kumaliza Shahada ya Umahiri ya Udaktari na ya Uzamivu na kufanya Utafiti na Machapisho kadhaa hadi kuwa Profesa. Amepata pia kutunukiwa tuzo ya Dr Martin Luther King na balozi wa Marekani nchini Tarehe 6 Machi, 2013.
Mzee Gibbonce Mwaikambo alianzia kazi kama Meneja wa Bima Iringa mnamo Mwaka, 1970 wakati huo Dkt Amon James Nsekela akiwa Meneja Mkuu wa Shirika la Bima lililokuwa chini ya Wakoloni; Alimrithi Amon James Nsekela Mwaka, 1972 na Kuunda Shirika la Bima la Taifa, wakati Shirika hilo lina Mtaji wa kiasi cha Shillingi milioni 5.5 za Tanzania hadi GBM anaondoka mwaka 1989 inadaiwa aliliacha Shirika likiwa na vitega uchumi vya zaidi ya Sh. 31 bilioni za Tanzania.
Baadaye GBM akahamishiwa Benki ya Rasilimali (TIB) iliyoanzishwa mwaka, 1970 ikimilikiwa na Serikali wakati Asilimia 60% zilikuwa za Serikali moja kwa moja, Asilimia 30% zilikuwa hisa za NBC na asilimia 10% zilikuwa Hisa za NIC; GBM alifanya TIB hadi Mwaka, 1985 akiwa Meneja Mkuu; alifanya kazi na akina Iddi Simba akiwa Mwenyekiti wa Bodi, Amoafo, J. akiwa Mshauri wa Masuala ya Sera, Ndugu A. Kibona akiwa Meneja wa Idara ya Maendeleo na Ndugu Malaki akiwa Mkurugenzi wa Miradi. Mhe Chief Gibbons Mwaikambo, aliteuliwa kuwa Mbunge wa Taifa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwaka, 1980 na kutumika hadi Mwaka, 1985.
Moja ya Mapendekezo yake Bungeni ilikuwa kuishauri Serikali kuunda baadhi ya Kanuni za Kusimamia Ugawanyaji wa fedha za kigeni kwenye Mashirika na Kampuni. Alibainisha kuwa zipo kampuni ambazo utendaji wao mbovu unaathiri Kampuni zingine zinazotegemea Kampuni hizo zisizo na tija katika ufanisi wao. Akatoa Mfano wa Kampuni ya kutengeneza Matairi ya General Tyre ambayo alisema inakaribia kufungwa huku Matairi ya Kampuni zingine hayapewi kipaumbele. Alibainisha kuwa kuna migao mingine ya fedha isiokuwa na Umuhimu.
Ifahamike pia kuwa kwa ubobezi wake wa Masuala ya Bima alikuwa ndiye Mwafrika wa Kwanza kuwa Meneja wa Shirika la Bima kwa Afrika chini ya Wakoloni walioitawala Tanzania na Kuunda Shirika la Bima la Taifa; Kukubalika na Wakoloni haikuwa kazi nyepesi wakati huo. Aidha, Mhe Chief Gibbons Mwaikambo alikuwa ni mmoja ya Wadhamini wa Chama cha Mapinduzi na Mlezi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi.
GBM alipendwa na Mungu, alifariki mnamo Tarehe 4 Septemba, 1995 baada ya madai kuwa gari yake iligonga mti wengine wakidai ilipinduka na kuzua utata wa Kifo chake.
GBM mbali na usomi wake bado aliheshimika kuwa Chief wa kabila la Wanyakyusa ambapo ililazimika azikwe usiku kama zilivyo desturi za Kabila la Wanyakyusa kuenzi Mazishi ya Machifu yaani “Wanyafyale”.
MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI MHE. CHIEF GIBBONS .J MWAIKAMBO (GBM).
Hiyo ndo historia (kwa ufupi) ya Mzee Gibbons Mwaikambo ambayo nimeikuta sehemu jioni hii, nimetamani nikushirikishe na wewe ili kama ulikuwa na hamu ya kujua mawilimatatu kuhusu Mwaikambo uisome kabla ya kulala usiku huu. Mungu akitupa uzima simulizi kamili kuhusu Mzee GBM zitakujia kupitia kitabu cha "Wanyakyusa Mashuhuri", ambacho nitatamani nikiandike kama itampendeza Mungu.
Huyu ndo Mnyakyusa aliyetuhumiwa kuwa alikuwa na upendeleo sana kwa kuwaajiri kwa upendeleo watu wengi wa Mbeya na hasa Wanyakyusa kwenye Shirika la Bima, na baadaye akatungiwa utani wa kuwa amewahi kusema "Kazi hamna, ila Imbombo jilipo"

Kwa kumbukumbu zangu.

Kabla ya kifo chake alikuwa amechukua form ya kugombea urais kupitia chama chake CCM na pia alipata kuwa Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi ya CCM.
 
Sisi wengine ni wachanga kwenye historia ya nchi hii.
Jee Mzee Mwaikambo alikuwa na cheo gani katika CCM? Jee alikuwa na influence kubwa ya kisiasa?.
Nilivyosikia mimi kuhusu huyu mzee ni kwamba alikuwa ni mkabila aliyepitiliza kwani pale NIC lugha ya kinyakyusa ndiyo ilikuwa ndiyo lugha rasmi iliyokuwa inatumika kazini. Niliambiwa pia, kuanzia mfanya usafi, mpika chai karani na viongozi wengi walikuwa wanatoka uchaggani mwa nyanda za juu kusini. Mwisho wa yote hata vyeo vilikuwa vinatoka kikanda. Jee hali halisi ilikuwaje???

Jibu la hilo swali tayari huyu jamaa Jidu kakupa mwanga.
👇
Sensa ya wafanyakazi wa Bima iliyofanyika baada ya kuulizwa Bungeni susla hilo ,ilitoa majibu kuwa kwa uwingi, kabila la Wasukuma lilishika namba moja, pili Wachagga na tatu ndo Wanyakyusa.

00
Kwa kumbukumbu zangu.

Kabla ya kifo chake alikuwa amechukua form ya kugombea urais kupitia chama chake CCM na pia alipata kuwa Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi ya CCM.
Hakuwahi kujaribu kugombea urais bali ubunge wa Wilaya ya Rungwe.
 
Back
Top Bottom