Giza totoro kituo cha mabasi ya mwendo kasi Kimara, je serikali imeshindwa kuweka backup power?

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Muda huu giza limetamalaki kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Kimara.

Msongamano wa abiria ni mkubwa mno, magari ni kama vile yamegoma.

Hii ni aibu kwa taifa , yaani mama aite wageni wake kupitia Royal Tour, halafu wageni wapande mwendo kasi uliojaa kunguni na huduma mbovu, sijui kwenye nchi zao wanaenda kuiongelea vipi Tanzania ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ?

Tumeshindwa mwendo kasi je tutaiweza treni ya umeme?
 
Wageni wamekuja kutalii kuona kumbe kunguni bado wapo duniani na wanaishi kwenye mwendokasi
 
Wanunue sola pannel wasituchoshe ๐Ÿ™ƒ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ