LGE2024 Goba: Mgombea wa CCM licha ya kutokuwa na kazi (jobless) amepitishwa lakini mgombea wa CHADEMA ambaye alikuwa ni dereva ameenguliwa

LGE2024 Goba: Mgombea wa CCM licha ya kutokuwa na kazi (jobless) amepitishwa lakini mgombea wa CHADEMA ambaye alikuwa ni dereva ameenguliwa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu

Huko Goba, wagombea wa CHADEMA wenye kazi rasmi wameenguliwa kwa madai kwamba shughuli zao hazitambuliwi kama kazi rasmi za kiuchumi.

Hii ni tofauti na wagombea wa CCM ambao, licha ya kujitangaza kuwa hawana ajira (jobless), wamepitishwa kugombea. Hivi karibuni, mgombea wa CHADEMA katika mtaa wa Kisauke ambaye ni dereva, aliwekewa vikwazo na kuenguliwa kwa sababu udereva haukutambulika kama kazi rasmi.

PC 1.jpg


Soma Pia: Mgombea wa CCM aliyeandika amezaliwa mwaka 2024 kwenye fomu, aripotiwa kupitishwa kugombea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Hali kadhalika, mgombea mwingine wa ujumbe wa serikali ya mtaa eneo hilo hilo, ambaye ni mfanyabiashara wa Kariakoo, aliwekewa kizingiti kwa sababu ujasiriamali pia haujatambuliwa kama kazi.

Cha kushangaza, mgombea wa CCM ambaye alitangaza hadharani kuwa hana ajira yoyote, alipitishwa kugombea, kinyume na Kanuni za uchaguzi za Serikali za Mitaa, hasa Kanuni ya 15(d) na 17(5), zinazotaka mgombea awe na shughuli rasmi ya kumwingizia kipato.

PC 2.jpg

Inaonekana msimamizi wa uchaguzi wa Goba anaona udereva sio kazi, ujasiriamali sio kazi, lakini kukosa ajira ni kazi!

Na bado Waziri Mchengerwa, licha ya kufahamu changamoto hizi, ameshauri wagombea walioenguliwa wakate rufaa iwapo wanaona wameonewa.
 
Kutokuwa na kazi si disqualification ya kugombea uongozi.

Kufanya kukosa kazi ni disqualification ya kugombea uongozi ni kinyume na katiba, kunamnyima mtu haki yake ya kikatiba ya kugombea uongozi kwa sababu hana kazi tu.

Kuwa na kazi nayo ni haki ya kikatiba.

Ukimnyima mtu haki ya kikatiba ya kugombea uongozi kwa sababu hana kazi ni kumnyima mtu haki moja ya kikatiba (kugombea uongozi) kwa sababu umemnyima haki nyingine (ya kuwa na kazi).
 
Jana nilikua Mbezi nimekaa akaja jamaa mmoja Mgombea wa chama huko mbezi Mpiji Magoe anaitwa Karata wa chama cha TADEA ametolewa Kwa sababu ya ameandika ni Mjasiriamali. Alienda kukuata refaa ameambiwa Mjasiriamali ni mziruraji hivyo hawakubali ombi lake. Kwa maelezo yake aliambatanisha sehemu mbalimbali wa CCM waliopitishwa na wameandika kazi Yao ya ujasiriamali
 
Ewe Mwenyezi tunakushtakia huyu aliyebariki huu ushenzi mhukumu kama ulivyomhukummu yule aliyevuruga 2019-2020 na hukumu ikatoka March 17 2021.
 
Wakuu

Huko Goba, wagombea wa CHADEMA wenye kazi rasmi wameenguliwa kwa madai kwamba shughuli zao hazitambuliwi kama kazi rasmi za kiuchumi.

Hii ni tofauti na wagombea wa CCM ambao, licha ya kujitangaza kuwa hawana ajira (jobless), wamepitishwa kugombea. Hivi karibuni, mgombea wa CHADEMA katika mtaa wa Kisauke ambaye ni dereva, aliwekewa vikwazo na kuenguliwa kwa sababu udereva haukutambulika kama kazi rasmi.



Soma Pia: Mgombea wa CCM aliyeandika amezaliwa mwaka 2024 kwenye fomu, aripotiwa kupitishwa kugombea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Hali kadhalika, mgombea mwingine wa ujumbe wa serikali ya mtaa eneo hilo hilo, ambaye ni mfanyabiashara wa Kariakoo, aliwekewa kizingiti kwa sababu ujasiriamali pia haujatambuliwa kama kazi.

Cha kushangaza, mgombea wa CCM ambaye alitangaza hadharani kuwa hana ajira yoyote, alipitishwa kugombea, kinyume na Kanuni za uchaguzi za Serikali za Mitaa, hasa Kanuni ya 15(d) na 17(5), zinazotaka mgombea awe na shughuli rasmi ya kumwingizia kipato.


Inaonekana msimamizi wa uchaguzi wa Goba anaona udereva sio kazi, ujasiriamali sio kazi, lakini kukosa ajira ni kazi!

Na bado Waziri Mchengerwa, licha ya kufahamu changamoto hizi, ameshauri wagombea walioenguliwa wakate rufaa iwapo wanaona wameonewa.
Nimesikitika sana mfano huku mtaani kwetu Kuna Jamaa wa chadema anakubalika sana na wananchi ila ameuza ushindi wake kwa mwenzie wa CCM kwa kupewa pesa kwa Siri halafu amekiuka masharti ya uchaguzi makusudi. Ili ionekane smeonewa na ccm
 
Nitafuatilia
Ufuafilie halafu ufanye nini kwa mfano? Hujawahi kukiri hata siku Moja upuuzi unaosimamiwa na mwenyekiti wako au kusimama against, just by nature if human existence!
 

Attachments

  • 1731344173133.jpg
    1731344173133.jpg
    303.1 KB · Views: 4
Back
Top Bottom