LGE2024 Godbless Lema, mlishatwambia kuwa kushiriki chaguzi kwa sheria hizi za sasa ni Ujinga

LGE2024 Godbless Lema, mlishatwambia kuwa kushiriki chaguzi kwa sheria hizi za sasa ni Ujinga

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
..itakuwa rahisi kuwadhibiti, au hata kuwadhuru, maana watakuwa nje ya taratibu za kisheria.
Hakuna mtu atakayeweza kuwadhibiti vijana walio tayari kufa kulinda taifa, rasilimali, mustakabali wa Taifa.

Kwa sasa naona viongozi wa ukweli ni Mwabukusi na Mpina wenye uchungu na Taifa na maslahi ya Taifa.

Wapo viongozi wengine vijana wanaweza kuwakabidhi uongozi baada ya mapinduzi Kama Mzee Warioba, Dr Shivji nk
 
Hakuna mtu atakayeweza kuwadhibiti vijana walio tayari kufa kulinda taifa, rasilimali, mustakabali wa Taifa.

Kwa sasa naona viongozi wa ukweli ni Mwabukusi na Mpina wenye uchungu na Taifa na maslahi ya Taifa.

Wapo viongozi wengine vijana wanaweza kuwakabidhi uongozi baada ya mapinduzi Kama Mzee Warioba, Dr Shivji nk

..kwanini vijana wafe wakati Babu zao walileta uhuru wa Tanganyika bila kumwaga damu.
 
..kwanini vijana wafe wakati Babu zao walileta uhuru wa Tanganyika bila kumwaga damu.
Kila kizazi inabidi kipambane. Uhuru unapambaniwa kwa aina yoyote ile kwa wakati wote. Kuishi bila haki, kama mtumwa nchini mwako kwa kijana anayejitambua kuna tofauti gani na kuwa marehemu?

Unalipa kodi ili familia chache zitumbue jasho lako hadi unakufa, kununua V8, kuongeza posho kwa wenza, kuhonga wapinzani, kuuza nchi na rasilimali zake muhimu, kukuteka ukisema haya sio sawa, kuna maisha hapo?
 
Ingewezekana japo kwa mbinde kama ingekuwepo angalau minimum respect ya hizo chaguzi. Kwa sasa hata zile minimums hazipo. Ndiyo maana energy ielekezwe kwenye kukata mzizi wa fitina.
Uzuri kwenye hili wananchi tumesimama kidete, hatuwezi kuendelea kushiriki chaguzi za kihuni. Na ccm na serekali wameshaupata ujumbe. Cdm kama chama tumeshawasadia wangesimama na sisi kuwa hakuna uchaguzi, ujumbe huu ungefika kwa usahihi na mbali zaidi. Na huu ni mwanzo tu, hata uchaguzi mkuu tutashusha mahudhirio ya wapiga kura kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea.

Mabadiliko hayakwepeki, ni aidha machafuko au mapinduzi ya kijeshi. Iwe iwavyo mabadiliko ni lazima.
 
Hakuna mtu atakayeweza kuwadhibiti vijana walio tayari kufa kulinda taifa, rasilimali, mustakabali wa Taifa.

Kwa sasa naona viongozi wa ukweli ni Mwabukusi na Mpina wenye uchungu na Taifa na maslahi ya Taifa.

Wapo viongozi wengine vijana wanaweza kuwakabidhi uongozi baada ya mapinduzi Kama Mzee Warioba, Dr Shivji nk
Mwabukusi wangalau, lakini Mpina hamna kitu hapo. Ukiacha nongwa yake dhidi ya Msoga gang, hana uthubutu wowote wa kupambana nje ya siasa za mbeleko ya vyombo vya dola.
 
Mwabukusi wangalau, lakini Mpina hamna kitu hapo. Ukiacha nongwa yake dhidi ya Msoga gang, hana uthubutu wowote wa kupambana nje ya siasa za mbeleko ya vyombo vya dola.
Unafikiri ukiwa na timu ya Mwabukusi, Mpina, Polepole, Lissu,Heche,Warioba kama kiongozi wao itafika wapi?

Wakishapambana wanamkabidhi Warioba kuongoza serikali ya mpito kupata katiba mpya, kuweka mambo sawa kama miaka mitatu hivi.

Vyama vipya vinasajiliwa kwa uhuru, uchaguzi huru na haki unafanyika. Technocrats wanapewa vitengo husika.
 
..itakuwa rahisi kuwadhibiti, au hata kuwadhuru, maana watakuwa nje ya taratibu za kisheria.
Kwani CCM na serikali yake ni lini walikuwa ndani ya sheria! Haya yote yanayo jadiliwa kwenye mada hii ni kwa sababu CCM hawafanyi mambo yao ndani ya sheria.
This is just friendly fire. Usijali sana.
 
Uzuri kwenye hili wananchi tumesimama kidete, hatuwezi kuendelea kushiriki chaguzi za kihuni. Na ccm na serekali wameshaupata ujumbe. Cdm kama chama tumeshawasadia wangesimama na sisi kuwa hakuna uchaguzi, ujumbe huu ungefika kwa usahihi na mbali zaidi. Na huu ni mwanzo tu, hata uchaguzi mkuu tutashusha mahudhirio ya wapiga kura kwa kiwango ambacho hakijawahi kutokea.

Mabadiliko hayakwepeki, ni aidha machafuko au mapinduzi ya kijeshi. Iwe iwavyo mabadiliko ni lazima.
Mstari huo wa mwisho pekee ndio umebaki ukituweka pamoja. Hayo ya kususia toka mwanza hadi sasa ni kukubali CCM waendelee hadi watakapo choka, sijui itakuwa lini hiyo!

Lilikuwa na bado linaendelea kuwa jukumu la hivi vyama vya upinzani kuhimiza na kutoa elimu, waTanzania wengi kuliko ilivyo wahi kutokea wajitokeze kupiga kura ya kuwakataa CCM. CCM wakikaza shingo na kuvuruga uchaguzi hiyo ni sababu tosha ya kuutumia huo mstari wako wa mwisho tunao kubaliana.

Lakini, kwa bahati mbaya sana CHADEMA na vyama vingine, na waTanzania kwa ujumla ni kama sote tumejisalimisha kwa CCM hiyo hiyo, itufanye vyovyote inavyo taka. Hii ni pamoja na nyinyi mnao susa kuwaruhusu waendelee bila pingamizi.
 
Mkuu 'Missile', na wasomaji na wachangiaji wa mada yako hii muhimu, binafsi sioni sababu ya kuwalaumu akina Lemma, Lissu na viongozi wengine wa CHADEMA kwa hayo uliyo yaeleza kwenye mada yako.

Hayo uliyo yataja ya "Kutoshiriki uchaguzi bila uwepo wa Katiba Mpya na Tume Huru", yalisemwa mwanzoni kabisa baada ya uchafuzi ule uliofanyika 2020, na baada ya mchafuzi mkuu kuondoka kwenye picha. Matarajio ya wakati huo, na uwepo wa muda wa kutosha kufanya marekebisho hayo ulikuwepo. Huyo kiongozi mpya aliyeingia na kushika nafasi, naye alionyesha dalili za mwelekeo wa hayo kufanyika.

Kwa hiyo, kabla ya kuyang'ang'ania hayo kuwa sababu ya kulaumu na kuanza kuhimiza watu wasipige kura ni muhimu kuyapima vizuri kwenye mizani.

Ni lini hasa kauli ya kususia uchaguzi endapo hapatakuwepo na Katiba Mpya na Tume huru iligeuzwa na viongozi hawa na chama chao?
Mimi nadhani ni baada ya kubainika wazi kwamba Samia katekwa na wahafidhina ndani ya CCM. Akatupilia mbali ule ulaghai wa mazungumzo ya maridhiano; wakati akisha mteka nyara Mbowe! Baada ya hapo, habari ya ufinyu wa muda unaotakiwa kutengeneza Katiba Mpya ukawa ni kizingiti. Tume Huru wakaona urahisi wa kutengeneza mazingaombwe, kama walivyo fanya.

Nirudi nyuma kidogo: baadhi yetu toka mwanzo kabisa tulikuwa tukiwahimiza CHADEMA kwamba kama hapatakuwepo na mabadiliko ya Katiba na uwepo wa tume huru, CHADEMA na wengine wajiandae KUZUIA UCHAGUZI kwa njia yoyote ile iwezekanayo, na siyo kususia tu uchaguzi.

Sasa tumefika hapa, Oktoba, tayari CCM ikijiandaa kufanya yale yale ya siku zote, tena waziwazi kabisa bila ya kificho.
CHADEMA wasusie uchaguzi. Itasaidia kitu gani? CCM itatakaza matokeo tena siyo ya namba ya waliowapa kura; watatangaza Asili mia ya ushindi walio upata; bila shaka si chini ya asili mia 90!
Kususia uchaguzi kutakuwa kumesaidia kitu gani!

Hebu tutazame huo upande wa ;pili; ambao wanawahimiza wananchi wajiandikishe kwa wingi zaidi na wajitokeze kupiga kura kuliko wakati mwingine wowote.
Tukikubaliana kuwa hawa watakao pata hamasa ya kujiandikisha na kupiga kura watakuwa ni wanaotaka mabadiliko, ni kuwa kura hizo nyingi zitakuwa ni za kuwakataa CCM

Sasa hapa litakuwa jukumu la CCM kuzikataa/kuzificha hizi kura nyingi zilizo wakataa. Hiyo moja.

Pili, lengo la ushauri wetu kwa CHADEMA kuwahimiza wananchi wengi kushiriki, ni kuwa wananchi hawa watakuwa wamepata elimu ya kutosha kuhusu HAKI zao na uhalali wa kura zao walizo piga. Kwamba wananchi hawa waandaliwe kukataa uvunjwaji wa sheria unaofanywa na CCM, huko huko kwenye vituo vyao vya kupigia kura na kuhesabu na kutangaza kura hizo. CHADEMA na vyama vingine wanao wananchi na wanachama wao karibu kila mahala nchini, kwa hiyo kituo chochote cha kupigia kura nchi nzima pasinge wezekana kukosa wananchi wa kukataa kura zao zisiharibiwe, huko huko kwenye vituo na kwenye ngazi nyinginezo katika hatua za kutangaza matokeo.

Bahati mbaya sana ninayo walaumu viongozi wa CHADEMA, kazi ya maandalizi ya wananchi kufanya kazi hii iliwashinda toka mwanzo. Sijui kwa kweli kilicho tokea ndani ya chama hiki kilicho anza kuweka matumaini kwa wananchi.

Nime tiririka tu, bila mpangilio maalum, lakini ni matumaini yangu kwamba nitaeleweka ukinifuatilia vizuri nilicho jaribu kueleza hapa.

Mkuu, 'Missile' naheshimu sana mada zako unazoleta hapa jamvini. Ni mada ulizo ziandaa na kuzipa wakati wa kutosha kuzipangilia vizuri.
 
Mkuu 'Missile', na wasomaji na wachangiaji wa mada yako hii muhimu, binafsi sioni sababu ya kuwalaumu akina Lemma, Lissu na viongozi wengine wa CHADEMA kwa hayo uliyo yaeleza kwenye mada yako.

Hayo uliyo yataja ya "Kutoshiriki uchaguzi bila uwepo wa Katiba Mpya na Tume Huru", yalisemwa mwanzoni kabisa baada ya uchafuzi ule uliofanyika 2020, na baada ya mchafuzi mkuu kuondoka kwenye picha. Matarajio ya wakati huo, na uwepo wa muda wa kutosha kufanya marekebisho hayo ulikuwepo. Huyo kiongozi mpya aliyeingia na kushika nafasi, naye alionyesha dalili za mwelekeo wa hayo kufanyika.

Kwa hiyo, kabla ya kuyang'ang'ania hayo kuwa sababu ya kulaumu na kuanza kuhimiza watu wasipige kura ni muhimu kuyapima vizuri kwenye mizani.

Ni lini hasa kauli ya kususia uchaguzi endapo hapatakuwepo na Katiba Mpya na Tume huru iligeuzwa na viongozi hawa na chama chao?
Mimi nadhani ni baada ya kubainika wazi kwamba Samia katekwa na wahafidhina ndani ya CCM. Akatupilia mbali ule ulaghai wa mazungumzo ya maridhiano; wakati akisha mteka nyara Mbowe! Baada ya hapo, habari ya ufinyu wa muda unaotakiwa kutengeneza Katiba Mpya ukawa ni kizingiti. Tume Huru wakaona urahisi wa kutengeneza mazingaombwe, kama walivyo fanya.

Nirudi nyuma kidogo: baadhi yetu toka mwanzo kabisa tulikuwa tukiwahimiza CHADEMA kwamba kama hapatakuwepo na mabadiliko ya Katiba na uwepo wa tume huru, CHADEMA na wengine wajiandae KUZUIA UCHAGUZI kwa njia yoyote ile iwezekanayo, na siyo kususia tu uchaguzi.

Sasa tumefika hapa, Oktoba, tayari CCM ikijiandaa kufanya yale yale ya siku zote, tena waziwazi kabisa bila ya kificho.
CHADEMA wasusie uchaguzi. Itasaidia kitu gani? CCM itatakaza matokeo tena siyo ya namba ya waliowapa kura; watatangaza Asili mia ya ushindi walio upata; bila shaka si chini ya asili mia 90!
Kususia uchaguzi kutakuwa kumesaidia kitu gani!

Hebu tutazame huo upande wa ;pili; ambao wanawahimiza wananchi wajiandikishe kwa wingi zaidi na wajitokeze kupiga kura kuliko wakati mwingine wowote.
Tukikubaliana kuwa hawa watakao pata hamasa ya kujiandikisha na kupiga kura watakuwa ni wanaotaka mabadiliko, ni kuwa kura hizo nyingi zitakuwa ni za kuwakataa CCM

Sasa hapa litakuwa jukumu la CCM kuzikataa/kuzificha hizi kura nyingi zilizo wakataa. Hiyo moja.

Pili, lengo la ushauri wetu kwa CHADEMA kuwahimiza wananchi wengi kushiriki, ni kuwa wananchi hawa watakuwa wamepata elimu ya kutosha kuhusu HAKI zao na uhalali wa kura zao walizo piga. Kwamba wananchi hawa waandaliwe kukataa uvunjwaji wa sheria unaofanywa na CCM, huko huko kwenye vituo vyao vya kupigia kura na kuhesabu na kutangaza kura hizo. CHADEMA na vyama vingine wanao wananchi na wanachama wao karibu kila mahala nchini, kwa hiyo kituo chochote cha kupigia kura nchi nzima pasinge wezekana kukosa wananchi wa kukataa kura zao zisiharibiwe, huko huko kwenye vituo na kwenye ngazi nyinginezo katika hatua za kutangaza matokeo.

Bahati mbaya sana ninayo walaumu viongozi wa CHADEMA, kazi ya maandalizi ya wananchi kufanya kazi hii iliwashinda toka mwanzo. Sijui kwa kweli kilicho tokea ndani ya chama hiki kilicho anza kuweka matumaini kwa wananchi.

Nime tiririka tu, bila mpangilio maalum, lakini ni matumaini yangu kwamba nitaeleweka ukinifuatilia vizuri nilicho jaribu kueleza hapa.

Mkuu, 'Missile' naheshimu sana mada zako unazoleta hapa jamvini. Ni mada ulizo ziandaa na kuzipa wakati wa kutosha kuzipangilia vizuri.

Asante mkuu Kalamu kwa input yako nzuri sana.

Kiufupi CCM ya sasa haina haya, haina aibu. CCM hii ya sasa, chini ya sheria hizi na katiba hii haiwezi kuleta hata "SEMBLANCE YA UCHAGUZI". Itaendelea kuleta UCHAFUZI na UCHAFUZI. Sasa ni kuwa irresponsible kuwahimiza wananchi kushiriki uchafuzi.

CCM siku hizi haihitaji kura, inahitaji wanaohesabu!. It is just kwamba Wanahitaji watu wengi wajitokeze ili waweze kudanganya kuwa wanananchi wana imani nao zaidi, ila beyond that they dont give a damn!

Nape hakuongea kwa bahati mbaya kule Bukoba!.

Turudi katika misingi ambayo ni kutengeneza mazingira ya fair and credible elections kabla ya kutaka watu washiriki mazoezi haya ya uchaguzi.
 
Mstari huo wa mwisho pekee ndio umebaki ukituweka pamoja. Hayo ya kususia toka mwanza hadi sasa ni kukubali CCM waendelee hadi watakapo choka, sijui itakuwa lini hiyo!

Lilikuwa na bado linaendelea kuwa jukumu la hivi vyama vya upinzani kuhimiza na kutoa elimu, waTanzania wengi kuliko ilivyo wahi kutokea wajitokeze kupiga kura ya kuwakataa CCM. CCM wakikaza shingo na kuvuruga uchaguzi hiyo ni sababu tosha ya kuutumia huo mstari wako wa mwisho tunao kubaliana.

Lakini, kwa bahati mbaya sana CHADEMA na vyama vingine, na waTanzania kwa ujumla ni kama sote tumejisalimisha kwa CCM hiyo hiyo, itufanye vyovyote inavyo taka. Hii ni pamoja na nyinyi mnao susa kuwaruhusu waendelee bila pingamizi.
Siaimini katika njia ya kura maana hapo ni kupoteza wakati.
 
Mtu mwerevu akikuambia kitu huku anajua kitu hicho ni uongo na wewe ukakubali basi anakuona boya

CCM kukuambia ushiriki uchaguzi, huku na wewe unajua wazi kuwa hakuwezi kuwepo uchaguzi wowote credible kwa sheria, kanuni na katiba hii. Lakini kwa sababu ya Tamaa zako tu na wewe unaenda kushiriki Uchafuzi huo. Basi CCM wanakuona boya kwelikweli na watakuendesheni kiboyaboya siku zotei!
 
Wafuasi wa CHADEMA pamoja na baadhi ya viongozi wao walishirikiana kuwarushia matusi ACT sababu eti walishiriki baadhi ya chaguzi na kuwaita wasaliti vibaraka na majina mengine, hivi sasa naona wanzirusha kabisa. Niliwahi zungumza zile zilikuwa ni drama tu mda ukifika na wao watashiriki.
 
Turudi katika misingi ambayo ni kutengeneza mazingira ya fair and credible elections kabla ya kutaka watu washiriki mazoezi haya ya uchaguzi.
Tulipo fikia na CCM hi,i haya ya kurudi kwenye misingi hayawezekani tena bila ya matumizi ya nguvu za wananchi kuyadai.
Na wakati mzuri ilikuwa ni kuanzia sasa kwenye huu uandikishaji na kuendelea mbele hadi baada ta uchaguzi mkuu mwakani.
Lakini fursa hii nzuri nayo sasa inapita, kwa sababu wananchi hawajaandaliwa vyema watimize wajibu wao huo muhimu. Kwa hiyo, CCM naona wataendelea na mipango yao kama kawaida bila ya pingamizi lolote la maana.
 
Back
Top Bottom