Goli ni Goli; la Mpendazoe nalo Goli!

Goli ni Goli; la Mpendazoe nalo Goli!

Huu ni mwanzo mzuri, sasa wale waliobaki nao wafunge magoli ya haraka haraka kabla mabeki wao hawajajipanga sawa

Wenye ujasiri huo sio wengi. Nimemshangaa sana Selelii remarks yake kwamba Mpendazoe angemtaka ushauri angemwambia asiondoke na kwamba yeye hatatoka CCM. Wengi ni aina hiyo ya kuganga njaa na hawajui wanatetea nini.

Big up Mpendazoe.
 
Hongera mpendazoe, uliyoyasema mwankijiji ni sahihi kabisa na kinachofanyika CCM sasa hivi wanajipanga ili kumshambulia aonekane mpumbavu, maneno ya Mwalimu nyerere yanatimia, Mungu amlaze pema peponi
 
Hilo goli la Mpendazoe kajifunga mwenyewe. Yaani imekula kwake.
 
Hongera sana mpendazoe kwa hatua uliyochukua..wengi watakusema watakavyo lakini simamia imani yako na hakika wengi watakuwa nguma yako..yako wapi ya Mutharika kuhama chama kilichomuingiza ofisini na bado walio wake wakamwelewa..
 
CCM haina jipya..wanaoitii wanafanya hivyo machoni kwa wanaotaka kuwaridhisha ilihali miiyo yao imeshakufa ganzi..sitoshangaa pia kumsikia bwana mkubwa akiomba kutoka 'chama chetu' na kujiunga na chama chochote..heri lawama kuliko fedheha!
 
Nadhani wenye akili wanaona na kuchambua mambo. Kwa vyovyote vile Mpendazoe kapiga bao CCM, wacha waseme visingizio kibao, bao limeshapigwa na nyavu zimetikisika na mpira upo kati tayari kutafuta bao lingine. Tusishangae kusikia Sitta naye katoka.....
 
Mpendazoe kaonyesha njia, tunasubiri na wengine wenye ujasiri wachomoke kutoka sisisem!
..Kweli kabisa mkuu, lakini isiwe ile hadithi ya kina Lamwai, Kabourou na Njeru Kasaka...Maana sisiem ni mafia kinyama.
 
Aminia Mpendazoe, lakini kwa nini amekwenda CCJ na sio chama kingine? Asije akakuta huko nako waliopo ndo kama wa CCM!
 
yaaani mpendazoe bonge la striker.....yaani kanikumbusha jana goli la pili la Bayern Munchen....eti alikuwa mzigo CCM bana yaani kama walevi wa ulanzi jinsi wanavojibu mambo ya msingi.....well done mpendazoe
 
yaaani mpendazoe bonge la striker.....yaani kanikumbusha jana goli la pili la Bayern Munchen....eti alikuwa mzigo CCM bana yaani kama walevi wa ulanzi jinsi wanavojibu mambo ya msingi.....well done mpendazoe

Sijui kwanini wanataka waendelee kuwa wao tu hawataki mabadiliko .....
 
Big up mkuu Mpendazoe. Umeonyesha njia..Najua tu wengi sana watafuata!
 
GOLI NI GOLI HATA LA MPENDAZOE NALO GOLI!




Na. M. M. Mwanakijiji


Kwenye kandakanda kuna magoli yanaudhi sana na yanakera. Kuna magoli ambayo mtu unakubali tu kuwa goli hilo "halina utata" na mnajitahidi kurudisha majibu.

Lakini, wakati mwingine magoli mengine yanamfanya mtu usikie donge kooni, presha ipande na kushuka na hata kuna mengine yanaweza kufanya timu nzima muende kumzonga mwamuzi kwani goli lililokubaliwa linaonekana kama limependelewa.

Bahati mbaya goli ni goli liwe la kuudhi au kukera lakini alimradi limekubaliwa basi wakati wengine wanasikia machungu wajue kabisa ipo timu nyingine inashangilia hata kama na wao wanaona kwa kweli lile goli lilikuwa baya.

Mbunge wa Kishapu Mhe. Fred Mpendazoe kawafunga bao CCM tena bao la kuudhi, kukera, kupandisha hasira na kwa kila kipimo bao ambalo CCM ile ya zamani isingeweza kufungwa kijinga hivi. Bao alilowafunga naweza kulilinganisha na bao la "tobo" au linakaribiana na bao la kipa "kupigwa kanzu"! Mwingine anaweza kusema "kapigwa kanzu halafu akapigwa tobo".

Kujiondoa kwa Mpendazoe kutoka Chama cha Mapinduzi kwa sababu yeyote ile kwa namna aliyotoka kunatufanya tusubiri kwa hamu maelezo ya CCM ya kutufafanulia kwanini goli hili siyo goli.Chama cha Mapinduzi bila ya shaka ambacho kina wasomi na watu waliobobea katika propaganda ya uzugaji kwa maneno kinakaribiwa na wakati mgumu wa kuelezea kujiondoa kwa Mpendazoe na bila ya shaka wanachama wengine huko mbeleni.

ref_cornerkick_shadowgram.gif
Mpendazoe hajaifungaCCM goli bali amejifunga mwenyewe kwenye mechi isiyokuwa na referee.Huo umaarufu wa mpendazoe unaodaiwa na watu si chochote kwani wanaoona kama ni maarufu ni watu wa aina yake na wale wengine wanaojiita mashujaa wa kupambana na ufusadi.Lakini kama ni mkweli mbona hawajaeleza hao wanatuhumiwa na ufisadi wamefanya nini na kuthibitisha tuhuma hizo.kilichosikika ni kelele za mbwa mwoga tuu.tena kwa mtuu yeyote makini hakuna mchango wowote wa maendeleo walioufanya aidha katika majimbo yao na hata katika chama chao katika ngazi ya wilaya.Hasara walioifanya katika majimbo yao ni kujenga makundi tuu.Let them go na hao wengine.
 
Angalizo zuri sana la Bwana Mpendazoe, huyu Tambwe ajulikana kwa kuendekeza NJAA
 
Wakuu, mimi naona kama ni "suicidal mission" kwa Mpendazoe?
Mimi naona wangetoka kama watano hivi kwa mkupuo impact ingekuwa kubwa sana kwa ccm!!
 
Mpendazoe hajaifungaCCM goli bali amejifunga mwenyewe kwenye mechi isiyokuwa na referee.Huo umaarufu wa mpendazoe unaodaiwa na watu si chochote kwani wanaoona kama ni maarufu ni watu wa aina yake na wale wengine wanaojiita mashujaa wa kupambana na ufusadi.Lakini kama ni mkweli mbona hawajaeleza hao wanatuhumiwa na ufisadi wamefanya nini na kuthibitisha tuhuma hizo.kilichosikika ni kelele za mbwa mwoga tuu.tena kwa mtuu yeyote makini hakuna mchango wowote wa maendeleo walioufanya aidha katika majimbo yao na hata katika chama chao katika ngazi ya wilaya.Hasara walioifanya katika majimbo yao ni kujenga makundi tuu.Let them go na hao wengine.
kama hakuwa maarufu kwanini wamjadili, Mpendazoe kaipiga Bao CCM, na ndio maana media yote TZ imehamia kwenye sakata hili, utatamani usiujue ukweli huo, lakini habari ndio hiyo.
 
Nampongeza kwa ku-sacrifice ubunge na marupuru yaliyobakia. Ni wachache wanaweza kujilipua hivi manake njaa ndo imetawala.
Taratibu tu asije akakosa ubunge, afu akarudi tena CCM. Ngoja tuwasikilize wengine, halafu na sera zao. Wasije wakaendeleza zilezile za kifisadi! Pengine kura yangu tis time itakua ya manufaa. im not raising my hopes though.
 
Nampongeza kwa ku-sacrifice ubunge na marupuru yaliyobakia. Ni wachache wanaweza kujilipua hivi manake njaa ndo imetawala.
Taratibu tu asije akakosa ubunge, afu akarudi tena CCM. Ngoja tuwasikilize wengine, halafu na sera zao. Pengine kura yangu tis time itakua ya manufaa. im not raising my hopes though.
huyu ni mwanaume wa shoka, anatambua thamani ya utu na mali, anajua kua vyoote viujazavyo ulimwengu ni ubatili na kujilisha upepo.
 
Back
Top Bottom