kweli hili nalo goli
Tuna miaka mitano sasa tunasikia jinsi baadhi ya Wabunge wanavyopambana na Ufisadi ndani ya CCM, kipi kimetendeka zaidi ya CCM kuwakejeli wale wanaotaka CCM ishughulikie ufisadi kwa nguvu zote?Mie kumsingi naamini Mpendazoe kachemsha. Ninazo sababu:-
- Alitakiwa kuupinga ufisadi akiwa ndani ya CCM. Nje ni kujimaliza kisiasa.
Mtu yeyote anayegombea ubunge huwa ana dhamira mbili. Moja ni kuwa na nafasi ya kupata kipato zaidi (kwa maana ya mshahara zaidi, heshima zaidi kwa kuitwa mheshimiwa na cheo zaidi ikiwa atapewa uwaziri au mamlaka mengine) na mbili ni "kuwatumikia wananchi". Sasa ku sacrifice haki ya kikatiba ya zaidi shilingi 40m/= kwa muda aliotumia kuwatumikia wananchi ni kuchemsha. Labda huko alikoenda amepata zaidi ya hizo (kitu ambacho kitakuwa ni rushwa).
You are just one of them, lol! Unawaza fedha tu zitakazopatikana kwa hili na lile. Uzalendo ng'o.
Katumia uhuru wake wa kidemokrasia kuhamia kwenye chama anachokiona kina katiba na mwelekeo anaoukubali yeye. Kuna shida gani?Kama alikuwa na dhamira halisi ya kuhama chama ili baadae aendelee kuwatumikia wanachi kwa kugombea tena ubunge akapata angehamia chama kingine cha kudumu, na sio kwenda kwenye chama ambacho hana uhakika kama kitapata isajili wa kudumu.
.Akumbuke mbunge sio kada wa chama. Makada wa chama wana wafuasi ndani ya chama husika. Chama huteua wanachama wake ili wakiwalishe katika uchaguzi fulani kulingana na upepo unavyovuma kwenye jimbo hilo la uchanguzi. Na moja ya sharti la kuteuliwa kugombea ni kuikitumikia, kukishabikia na kukubaliana na maamuzi yote ya chama. Ndio maana kina Wasira waliweza kuhama chama na waliporudi wakpokelewa kwa mikono miwili. Ni upepo tu. Kwa bahati mbaya hana influence ya kuwafanya wana Kishapu kuhamia CCJ. Heri Dan Makanga na UDP vs CCM kule Baridi enzi hizo
What is the problems with you guys? CCM wawashukuru sana waasisi wa nchi hii waliokuwa na akili za kizalendo wakaamua kujenga chama madhubuti. Kuna makada gani siku hizi zaidi ya waganga njaa tu?
Hizi kelele za kujimaliza kisiasa, kajifunga goli, kakimbia ni kelele za wivu na ukosaji tu. Nadhani baadhi ya watu hawakutegemea kwamba kuna watu wenye msimamo ambao hawajali ulaji.
- Kajifunga goli. atasononeka. atabaki peke yake.
- Kachemsha ile mbaya. Kimsingi huo ndio mwisho wake kisiasa.
Oh, kumbe unajua kwamba dola huwa inatisha watu? Hilo ndilo tatizo. Dola hii inayotamba kwamba imeongeza wigo wa demokrasia nchini inakuwaje na vitisho kwa wananchi wasio na hatia wenye mtazamo na mawazo tofauti na ambao hawajavunja sheria yoyote ya nchi? Twashukuru kwa kuligusia hilo kwa sababu endapo Mpendazoe atabughudhiwa makusudi tutajua dola inaendeleza vitisho vulivyovigusia.Hofu yangu ni moja. Inawezekana Mpendazoe alikuwa anatishwa kimya kimya na dola na vitisho vyenyewe alikuwa anajua vitamdhuru. Akaona akimbie
Mbona CCJ kinatisha watu hivi wakati ni Mbunge mmoja tu aliyetangaza kujiunga nacho? Hofu ya nini kwa mtu ambaye hana maana yoyote na ambaye keshajimaliza kisiasa?
Kwa hiyo wewe uko kundi la mafisadi unashangilia mafisadi kushinda sema tujue ili tusihangaike kujaza thread hapa uendelee kushangilia mwenyewe'Mechi' inawakilisha msimamo wa alichokuwa anakipigania akiwa bungeni huko. Kwa hiyo timu yake ni wale wote waliokuwa upande mmoja katika mpambano huo. Huko alikoenda hataweza kuendeleza mapambano, ni kakundi tu ka washangiliaji, hakuna impact. Yuko nje ya ulingo sasa, atakuwa mlalamishi tu, wale ambao lugha za mitaani tunawaita 'bush lawyers'. Katika hili mafisadi ndio wameshinda, ndio maana nasema kajifunga goli mwenyewe halafu akahamia jukwaa la washangiliaji.
Nakumbuka pale nyamagana tulimuzomea Nyerere alipoingia na Mkapa, lakini aliponyosha kafimbo kake kasi, mara kusi ,mara mangaribhi na mashariki, tukatuliza soka kumsikiliza.
Nimetonywa na mzee wa siasa za bongo kuwa Kina Sitta, Lucas Seleri, Mwakyembe n.k wana card mbili mbili za CCM na chama kingine cha upinzani mambo yakienda kumbo wanahamia CCJ ama CHADEMA pia uchaguzi mwaka huu kutakuwa na vurugu kama la kule Kenya tena si la kikabila bali ni la kati ya wakristo na waisilamu..
Ngoja nisubiri nione wapinzani wako je? hasa CCJ. Lakini waliopo hadi sasa hakuna cha vurugu na ccm itateleza tu. Hope zangu nazisikilizia kwa CCJ kuona hayo unayosema kama ni kweli.
Kwa hiyo wewe uko kundi la mafisadi unashangilia mafisadi kushinda sema tujue ili tusihangaike kujaza thread hapa uendelee kushangilia mwenyewe
CongoMtu yeyote anayegombea ubunge huwa ana dhamira mbili. Moja ni kuwa na nafasi ya kupata kipato zaidi (kwa maana ya mshahara zaidi, heshima zaidi kwa kuitwa mheshimiwa na cheo zaidi ikiwa atapewa uwaziri au mamlaka mengine) na mbili ni "kuwatumikia wananchi". Sasa ku sacrifice haki ya kikatiba ya zaidi shilingi 40m/= kwa muda aliotumia kuwatumikia wananchi ni kuchemsha. Labda huko alikoenda amepata zaidi ya hizo (kitu ambacho kitakuwa ni rushwa).
Nani kakuambia anataka ubunge huko CCJ afterall akiukosa wewe utamsaidia nini au utaisaidia nini familia yake hadi unasema ataujutia hivi ukisimama wewe na yeye mbele ya watu nani ataonekana mjutaji zaidi acheni hizo jamaniMpendazoe alijua hatapita kura ya maoni ndio maana amehamia upinzani.Sidhani kama atashinda uchaguzi .Zaidi ya kupiga makelele ametoa ushauri gani kuleta maendeleo ya taifa.Uamuzi alioufanya ataujutia maishani mwake.
Ningeshangaa sana kama angesema tofauti na hayo..................LIKE FATHER......LIKE SON............. msitegemee nyoka azae sungura....hata siku moja..............Mtoto wa Jakaya Kikwete, yaani Ridhiwan Kikwete amemponda aliyekuwa mbunge wa Kishapu kwa tiketi ya CCM, Fred Mpendazoe na kusema hakuwa na lolote acha aende zake.
Ridhiwan alikuwa leo mkoani Shinyanga kama ambako alialikwa kama mgeni Rasmi na Mjumbe wa baraza kuu la Umoja wa vijana wa chama cha Mapinduzi (UVCCM) kusimika makamanda 17 wa wilaya za mkoa wa Shinyanga.
Alisema kuondoka kwa mbunge huyo toka CCM na kukimbilia chama cha CCJ kinaonyesha viongozi ambao wamekuwa mzigo kwa chama lakini pia aina ya viongozi ambao wamekuwa wakichanguliwa katika uchaguzi na wananchi kumbe hawafai.
Alisema "Mwacheni aende Mpendazoe.... wala msihuzunike, kuondoka kwakwe kusiwafanye kukosa raha, wala CCM isisikitike, wapo wengi waliondoka na chama bado kipo imara, muhimu kusonga mbele na kuendelea kudumisha mshikamano wenu
Alisema alikuwa Mpendazoe alikuwa akifanya mambo mengi kinyume na kanuni za chama na kuwaomba wananchi kutulia na kuangalia viongozi wengine lakini akisisitiza kuwa walio makini na siyo wale wa kuja.
Hata hivyo Ridhiwan alisisitiza Hapa tunapaswa kuangalia, tunapochagua viongozi tuchague lakini tukichagua viongozi kwa kuangalia sura au hela za mtu, tukaacha wenye moyo na msimamo wa kukitetea na kuimarisha chama kwa vitendo , yatatokea kama ya mpendazoe".
Vijana nao walitoa Tamko lao kwa Ridhiwan wakisema;
kwa muda mrefu mwenendo mzima wa mbunge huyo ulikuwa na mwelekeo wa kukiangamiza chama ambao ulikuwa unakinzana na maadili ya Chama pia, na kuongeza kuwa alichokifanya ni uamuzi mzuri kwa vile umekipunguzia mzigo chama.
"Alikuwa kero, alishafanya mambo mengi kwa chama, siyo kwa chama tu hata katika jimbo lake lote kwa ujumla alikuwa mzigo mkubwa sana.
Hatukujua kama tuliteua mbunge asiyekuwa na uchungu na wapiga kura wake kiasi cha kuwatelekeza na kuwanyima haki yao ya kuwa na mwakilishi hasa katika kipindi hiki cha bajeti, tunaamini hakuna kitakachoharibika kwani tunatambua mshikamano wa watu Kishapu