Gone Too Soon: RIP JF Member.....Chetuntu!!!

Ndo kama hivi mkuu, kazi haziendi...........Am speechless!
 
Mkuu unataka kutuambia kuwa Shetani ndo hupanga vifo na wala si Mungu?............. Na kwanini Mungu amuache shetani apange kuteketeza viumbe vyake? Si amwangamize?...This is unfair!

Babu nilikaa pembeni kidogo kutafakari bila majibu yeyote.

Vipi hali ya mtoto aliyeachwa huyo aliyezaliwa eeh Mungu umsimamie.
 
So sorry for our beloved fellow, the late Chetuntu.

Mungu awape moyo wa ustahimilivu wanafamilia yake, wanajf na wote walioguswa na msiba huu.

Jambo la muhimu ni sisi tulio hai kujiandaa, kwakuwa hakuna ajuae siku wala saa ya kifo chake.
 
mmmmmmmmmmmmm so sad - oh God .... Mungu amsaidie na kumkuza mtoto wake mmoja aliyebaki - wote tuko njiani kuelekea huko.
 
Mungu amsamehe dhambi zake zote,amlaze mahal pema pepon.AMEN
 
OMG!..What a tragedy!! Ampumzike kwa amani mdogo, dada na rafiki mpendwa Chetuntu..Pole za kipekee kwa familia yake!

Really Gonna Miss You - Smokey Robinson.
 
Niliona hii habari mapema asubuhi nikashindwa kuchangia maana ilinifanya nianze kufikiria mambo mengi kweli.

For the first time imeniingia akilini kwamba i‘m not death proof and neither are you. Yeyote kati yetu anaweza akadondoka wakati wowote...ukilala tu waweza usiamke...ukiaga kwenda kazini usirudi nyumbani..ukipanda gari usishuke..ukipanda ndege usitue... ukienda hosp usitoke mzima na mengine mengi. Yani kila tunachofanya kuna uwezekano tusimalizane nacho tukiwa hai and that scares the hell out of me. Na hivi nimetoka kuspend weekend yangu hospitali ndo kabisa najiona mwenye bahati kurudi nyumbani nikiwa hai na bila machozi kama mtoto aliyeachwa na Chentutu.

Nasikitika kwamba tumempoteza member mwenzetu hapa jamvini...watoto walio katika eneo alilokua anafanya kazi wamepoteza mtu aliyewajali...ndugu zake wamempoteza ndugu yao ila zaidi nasikitika kwa mwanae aliyempoteza mama yake wakati bado anamhitaji kuliko sisi wengine wote pamoja.
I hope wapo ndugu zake watakaofanya maisha ya mtoto yaendelee kuwa as smooth as possible...asije akanyanyasika kama ambavyo wengi wamekua baada ya kupoteza mama zao. Kwa hili ntamwomba Mungu angalau ayabariki maisha yake maana mama hawezi kumrudishia.

Asante babu kwa taarifa na pole kwa msiba.
Pole nyingi kwa familia yake ila zaidi kwa mwanae.
Poleni wanaJF wote mlioguswa....
Chentutu Mungu akulaze mahali pema peponi dada mzuri.

BTW natamani tungekua tunaonyeshanaga mapendo namna hii wakati tukiwa hai na wazima. Si ajabu kuna watu aliwaona kama hawampendi hata hapa JF ila leo wamefunguka na kuonyesha kuguswa na kifo chake....laiti angekua anaona yanayoendelea huku chini (I hope she does) nadhani angekua analia na kutabasamu kwa wakati mmoja right now.

Kwaheri Chentutu...you‘ll be missed forever.
 
Well said Mshiki............ Na tuendelee kumwombea mpendwa wetu aendelee kupumzika kwa amani.............
 
Oooh my LORD!!!
kweli kifo hakina huruma. Mungu amlaze mahali pema peponi,na aipe faraja familia katika kipindi hiki cha majonzi.
 
Mkuu unataka kutuambia kuwa Shetani ndo hupanga vifo na wala si Mungu?............. Na kwanini Mungu amuache shetani apange kuteketeza viumbe vyake? Si amwangamize?...This is unfair!

....ni kweli kifo asili yake ni ule uasi pale Edeni, na Siyo kwamba Mungu anamuacha shetani laa hasha kwani hukumu yake naye ni ile siku ya mwisho!!
 
JF will always be with you in memories,untill such time,the almighty reunites us in heaven
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…