Gone Too Soon: RIP JF Member.....Chetuntu!!!

MAY YOU R. I. P

Let God give you strength when you need it. Let Him give you peace and restoration with his love for you.
This is just another example that proves that the world is not our permernent home. In this imperfect world we live in, we must trust God who is always perfect.
 
Kiukweli taarifa hii nimeipokea kwa masikitiko mkaubwa sana,
  1. Kifo chochote kinauma lakini cha mtu unayemfahamu kinauma zaidi. Hivyo marehemu ameacha majonzi mengi kwa familia yake na wanaJF kwa ujumla.
  2. Safari hii ya kifo ina maswali mengi ya kiimani hivyo kuleta majibu mengi ya kinadharia, lakini kwa mimi nanukuu " Kheri wafao sasa katika Yesu Kristo"
  3. Mwisho ni angalizo kwa sisi tuliobaki duniani kuelewa kuwa kifo tunatembea nacho hivyo ni bora tukajiandalia makazi mema kwa kufanya yaliyo mema. Mwisho mtume Muhammad katika hadithi fulani anasema " Kifo chatosha kabisa kuwa mawaidha kwa mwanadamu"
Chituntu hatunaye tena, Eeeeeh Mungu Muumba mbingu na ardhi mpokee mwanaJF mwenzetu aliyetangulia mbele ya haki. Kwa hakika kila nafsi itaonja mauti, nasi tunakuja. Amen.
 
....ni kweli kifo asili yake ni ule uasi pale Edeni, na Siyo kwamba Mungu anamuacha shetani laa hasha kwani hukumu yake naye ni ile siku ya mwisho!!
Kwa hiyo kifo si mpango wa Mungu mkuu?..........Hata mtu anapozeeka na kufikia ukomo bado ni mpango wa shetani? Hili ni fumbo la imani aisee.....
 
Ni huzuni kubwa sana ila hatuna jinsi ni kukubaliana na hali. Yeye katangulia nasi tuko nyuma yake. Twamuombea apate mapumziko mema. Aaamiin.
 
Kwa hiyo kifo si mpango wa Mungu mkuu?..........Hata mtu anapozeeka na kufikia ukomo bado ni mpango wa shetani? Hili ni fumbo la imani aisee.....

Mkuu;
....ni mpango wa shetani,
....hivi ukomo wa maisha ya bnadam ni miaka mingapi? kumbuka hapo mwanzo watu waliishi hadi miaka 900 na usheee,
Anyway ni fumbo la imani kwa njia moja au nyingine!!
 
Mkuu;
....ni mpango wa shetani,
....hivi ukomo wa maisha ya bnadam ni miaka mingapi? kumbuka hapo mwanzo watu waliishi hadi miaka 900 na usheee,
Anyway ni fumbo la imani kwa njia moja au nyingine!!
Lakini mkuu, mbona hata wanyama ambao shetani hana time nao nao wanakufa? Mbona mimea pia inafikia ukomo?
 
Ifike wakati wenye theory zao za kiimani wazihifadhi kwa siku nyengine.

Yakuhusisha kifo na shetani kwenye thread kama hii tungeepuka.
 
Asprin kwanza nitumie nafasi hii kukushukuru kwa niaba ya member wengine wa JF kwa kutuhabarisha na kutupa walau wasifu wake hapa JF. Maelezo yako yametufanye wengi tuhisi kama mtu tuliyewahi kuonana naye (kwa michango yake) ingawaje si ana kwa ana.

R.I.P Chetuntu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…