Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 16,003
Mtandao wa Google umetoa ripoti inayobaini kwa undani upekuzi na maswali ambayo Wakenya waliuliza mtandaoni mwaka 2016.
Katika kitengo cha maswali yanayoanza na 'jinsi ya', "jinsi ya kupunguza unene haraka" liliulizwa na Wakenya wengi zaidi.
"Jinsi ya kulainisha nywele asili" lilikuwa swali la tatu kwenye orodha. Maswali mengine yaliyoulizwa ni "Jinsi ya kufanya ngozi iwe nyeupe kitaalamu", "jinsi ya kutongoza wasichana", "jinsi ya kupata tumbo bapa" miongoni mwa mengine.
Wakenya wengi walitafuta maelezo kuhusu afya yao. Maswali yaliyoongoza ni "jinsi ya kupunguza unene haraka" na "jinsi ya kupata tumbo bapa" .
"Jinsi ya kuhesabu siku za ujauzito," lilikuwa la tatu.
Maswala mengine ya kiafya yaliyotafutwa na Wakenya ni "jinsi ya kuzuia uvundo wa miguu" , "jinsi ya kupunguza msukumo wa damu", "jinsi ya kuhesabu siku salama za kushiriki ngono bila kupata mimba" "jinsi ya kuwa mnene kwa siku moja".
Wakenya pia walitaka kujua "Nini kinachotokea Aleppo". Wengi walitaka kujua hali ilivyo katika mji wa Aleppo uliokumbwa na mapigano makali kati ya wapiganaji na vikosi vya serikali.
Wakenya pia walitaka kujua "Nini kinachotokea Ethiopia?"
Hii inafuatia maandamano ya jamii za Amhara na Oromia nchini Ethiopia, ambayo yamesababisha mauaji ya takriban watu 100.
Katika kitengo cha maswali yanayoanza na 'jinsi ya', "jinsi ya kupunguza unene haraka" liliulizwa na Wakenya wengi zaidi.
"Jinsi ya kulainisha nywele asili" lilikuwa swali la tatu kwenye orodha. Maswali mengine yaliyoulizwa ni "Jinsi ya kufanya ngozi iwe nyeupe kitaalamu", "jinsi ya kutongoza wasichana", "jinsi ya kupata tumbo bapa" miongoni mwa mengine.
Wakenya wengi walitafuta maelezo kuhusu afya yao. Maswali yaliyoongoza ni "jinsi ya kupunguza unene haraka" na "jinsi ya kupata tumbo bapa" .
"Jinsi ya kuhesabu siku za ujauzito," lilikuwa la tatu.
Maswala mengine ya kiafya yaliyotafutwa na Wakenya ni "jinsi ya kuzuia uvundo wa miguu" , "jinsi ya kupunguza msukumo wa damu", "jinsi ya kuhesabu siku salama za kushiriki ngono bila kupata mimba" "jinsi ya kuwa mnene kwa siku moja".
Wakenya pia walitaka kujua "Nini kinachotokea Aleppo". Wengi walitaka kujua hali ilivyo katika mji wa Aleppo uliokumbwa na mapigano makali kati ya wapiganaji na vikosi vya serikali.
Wakenya pia walitaka kujua "Nini kinachotokea Ethiopia?"
Hii inafuatia maandamano ya jamii za Amhara na Oromia nchini Ethiopia, ambayo yamesababisha mauaji ya takriban watu 100.