Mtazamo wangu ni kwamba, ajira zina competition kubwa na kwa hiyo uwezo wa ku-compete ndo utakuwezesha kuajiriwa. lakini pia uwezo wa kumudu mazingira ya kazi ndo utakusaidia kuendelea mbele (growing) sehemu ya kazi na kufanya waajiri mbali mbali watamani kupata mtu mwenye skills kama wewe au hata mwajiri wako asitamani kukuachia.
Ajira pia ni njia mojawapo kutengeneza network itakayakusaidia badae kama utaamua kujiajiri.
Kama unadhani uwezo wako wa kushindana kutafuta ajira ni mdogo (hii ni taswira ya output ya vyuo vingi kwa sasa) basi ni bora uanze kujipanga kujiajiri. la kukumbuka ni kwamba kujiajiri ni kazi ngumu pia pengine kuliko hata kuajiriwa.
Mfano, kule kazini unaweza kutegea na ukiwa na mwajiri ambaye hafuatilii sana utendaji kazi wa watu wake, you can get away with it mna ukapata mshahara wako. Lakini kama umejiajiri mathalani kwenye mradi wa kuuza chakula ama kufyatua matofali, siku ukizembea kidogo mkono hauendi kinywani na biashara yako itakufa huku unaangalia.
kwa hiyo kazi zote, za kuajiriwa ama kujiajiri zinahitaji commitment ya muhusika kama unataka ikufikishe mbali. Hapa sizungumzii zile za "mission town" za kupiga porojo. namanisha zile genuine cases only.
kazi zote zinahitaji skills ambazo vyuo vyetu vingi havitoi. chuo/shule zetu zinafundisha general concepts tu ambazo kuziweka kwenye mazoezi ni kazi ingine ngumu sana.
Kwa hiyo basi, kwa namna yoyote itakavyokuwa, kuajiriwa ama kujiajiri ni zote ni kazi na zote pia zahitaji skills ambazo mhusika ni lazima azitafute deliberately huku akifanya ile elimu ya chuo. how? talk to people wa mtaani, pitia huku kwenye blogs na social forums, observe, omba chance ya kushiriki kufanya bila malipo mahali flani, soma stories za waliofanikiwa, jaribu namna nyingi. tafuta skills nyingi kama customer service (hii ni ile lugha nzuri kwa wateja), usafi, basic financial skills (hii itasaidia kutunza hesabu zako mwenyewe na kuhakikisha huli mtaji), communication skills (mawasiliano ndo kila kitu hasa written maana inaacha mark ama audit trail), team work (wengi wetu tunakwama mahali kwa vile tunapenda individualism). na zaidi ya yote tamani kila siku ku-improve your self. kila siku jifunze skill mpya na uifanyie kazi, uwe na uwezo wa kufanya zaidi kwa muda ule ule au kufanya kitu kile kile kwa muda kidogo
Cha mwisho kwa sasa, fahamu kwamba mazingira yanabadilika, technologia inabadilika, mahitaji ya watu na hali ya mazingira inabadilisha how we work. hata ukiajiriwa ama ukijiajiri ni hivyo hivyo. For you to remain relevant, ni lazima ubadilike kulingana na mazingira. Mfano; internet cafe zilikuw maarufu sana miaka ya mwanzoni mwa 2000, lakini unaona sa hivi kila mtu ana internet mkononi. jana nilikuwa mahali fulani watu wakawa wanalalamika kwamba mpambaji wa ukumbi katumia baloons kupamba wakati hiyo imepitwa na wakati, watu wanatumia roses. hiyo ni mifano miwili kwamba change ipo na inatu-affect wote. To remain relevant, whether tumeajiriwa ama kujiajiri ni lazima twende na pace ya mabadiliko.