Graduates wengi tunapitia wakati mgumu sana, sema jamii inaona kama hatujielewi

Graduates wengi tunapitia wakati mgumu sana, sema jamii inaona kama hatujielewi

Nilipitia hali kama hiyo. 2011-2014, nimefanya Freelancing Bayport ServiceTz,Cliend Adviser Advans Bank.... orodha ni ndefu. All in all fanya chochote kiko kwenye uwezo wako upate kitu cha kufanya, muaminj MUNGU wako utashinda. Bottom line haijalishi unapitia changamoto gani, lakini hakuna kukata tamaaa
 
1594582183636.png
 
Jaman tusikatae ukweli wala kutupiana lawama, ajira za serikalini na kuajiliwa sehemu binafsi kwa kipato,/mshahara mkubwa Ni tatizo.
Vijana tufanye kazi, tujitume kujiajili wenyewe, na mtaji wa kwanza Ni nguvu zako mwenyewe.

Uhalisia wa Maisha Ni tofauti ukiingia mtaani, hakuna Cha bure Wala Cha dezo, Ni kukomaa tu na Maisha.

Shida graduate tunachagua Sana kazi za kufanya halafu tunataka kutusua mapema.
 
Andiko zuri mkuu, ni kweli kung'ang'ania dar ni shida zaidi maana unaingia katika utumwa ambao sio rahisi kutoka......Kukosa ajira nilipitia kwa kipindi kifupi miezi miwili tu ila niliteseka sana na kujifunza kitu kikubwa sana maishani......chamsingi ni kumuomva Mungu afungue milango ya baraka na kuwa na nidhamu ya matumizi.....
aiseeh kuna watu wana bahat, miez miwil tu, mi huu ni mwaka wa 5 bilabila daaah!
 
Nilipitia hali kama hiyo. 2011-2014, nimefanya Freelancing Bayport ServiceTz,Cliend Adviser Advans Bank.... orodha ni ndefu. All in all fanya chochote kiko kwenye uwezo wako upate kitu cha kufanya, muaminj MUNGU wako utashinda. Bottom line haijalishi unapitia changamoto gani, lakini hakuna kukata tamaaa
Ukweli Mkuu, kukata tamaa mwiko
 
Jaman tusikatae ukweli wala kutupiana lawama, ajira za serikalini na kuajiliwa sehemu binafsi kwa kipato,/mshahara mkubwa Ni tatizo.
Vijana tufanye kazi, tujitume kujiajili wenyewe, na mtaji wa kwanza Ni nguvu zako mwenyewe.
Uhalisia wa Maisha Ni tofauti ukiingia mtaani, hakuna Cha bure Wala Cha dezo, Ni kukomaa tu na Maisha.
Shida graduate tunachagua Sana kazi za kufanya halafu tunataka kutusua mapema.
Kweli mkuu.
 
Kwanza kushindwa biashara moja hakumaanishi kushindwa biashara zote.

Hata huko mkoani hakuna 'guarantee' ya kwamba utafanikiwa.

Jambo la msingi ni kujaribu "Tena na Tena"
Mkoani hakuna hela ya mzunguko kama Dar. Ndio maana makampuni yamejazana Old Bagamoyo road hapo kama HQ zao!
 
Umeongelea jambo la msingi sana juu ya mahitaji yetu kwenye service fulani na idadi inayozalishwa ya wahitimu.

Kuna kitu kingine wahitimu wengi wanaozalishwa ni wale wanaohitajika kwenye service industry ambayo haijakomaa kuweza kuchukua idadi kubwa.

Wengi wa graduates wanamatarajia makubwa ya kupata kazi katika public sector kuliko private sector ambayo pamoja sharp growth yake bado haijawa na uwezo mkubwa sana wa kujaza gap linaloachwa na public sector.

Trend ya 2015 kurudi nyuma ilikuwa inatia matumaini sana kwa kada nyingi kupata ajira au kujiajiri kwa mfano service industry ilikua kwa haraka sana na kuwa na watu wengi waliojiajiri huko vivyo hivyo sector zingine zilianza kuvutia watu wengi sana kuwekeza na kuanza kuzalisha ajira nyingi kwa watu wenye kada mbalimbali.


Nini kifanyike.

1 kwa graduates walioko mtaani tayari wakubaliane na hali kuwa hii itawasaidia kupata mawazo mapya on how to survive the battle

2 kwa walioko vyuoni wanapaswa kujiandaa kisaikolojia at the same time try to learn new skills hasa hasa MARKETING na entrepreneurship wanapaswa kutumia muda wao mwingi creating connections zitakazowasaidia kuingia kwenye soko la ajira with Hopes

3. We have to swallow our pride tufanye kazi yoyote inayoweza kuzalisha kipato while while looking for best options.

4 we shouldn't expect too much kuwa degree ni ultimate source of economic success hii ndiyo inayotufanya tushindwe kufikiria nje ya box.

5 kukwepa mazingira ya aibu na kuchekwa mitaani huko tunakotoka ni vyema tukatafuta sehemu we are least known and start from the bottom inaweza kusaidia kutupa dimensions nyingi za kuweza kuona fursa.

Etc

6.
Ukiwa msomi utajificha wapi Tanzania hii?

Ukikimbilia ruvuma huko ndani ndani unauza miwa iko siku afisa vijiji umesoma nae atakuona tu
 
Sijui kwanini Dar kunalemaza Sana .yaani unahis huwezi survive kwingine!
Kiukweli mikoani maisha sio magumu kama Dar. Ila patakuchukua muda sana kusogea kimaisha tofauti na Dar. Ni ngumu sana kukusanya laki1 kama faida mkoani kama ilivyo kwa Dar.

Inabidi uwe na hesabu kali tu utumie hela kwa kubana ili ubakiwe na nyingi ya kusave ukiwa dar.
 
We acha tu mkuu, heshima huja kwa kuwa na kitu ktk haya maisha yetu ya kibongo
Ukikosa kazi bora hata uwe na kabiashara unaonekana unafanya, ila ukiwa unakula kulala tu aisee hata paka anaweza kukukojolea tu bila kuwaza.🤣🤣🤣

Kukosa kazi bongo ni kama gunia la msumari. Hamna mtu atakuheshimu hata uwe na PhD as long as haizalishi pesa umeisha.
 
Kaka umegusa Maisha ya wengi hata wachumba tunaogopa kutongoza yani ni shida mnoo
Ukitongoza mchumba utaishia kuachwa tu mkuu kwa fedheha nzito maana kila akiwaza utatusua umuoe wewe ndio unazidi kula mitama kwenye interviews na kazi hupati kabisa.🤣🤣🤣🤣🤣
 
Mkoani hakuna hela ya mzunguko kama Dar. Ndio maana makampuni yamejazana Old bagamoyo road hapo kama HQ zao!
Asee mkoani hapana acha tubanane hapa hapa dar nyoso

Nilienda likizo juzi nikacheki mishe naona chenga tu, hadi nikajiuliza watu huku wanamake vip money

Arachuga hiyoo
 
Back
Top Bottom