Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Mimi nilichokiona hapo ni huyo dada mweusi ndiye amembagua Biden, hapo wote walikuwa wakimshibokea Biden wakitoa simu zao wapige selfie lakini huyo dada yeye ni kama alikuwa hamuoni Biden.
Halafu unaposema rudini nyumbani huko nyumbani ni wapi? Kama wewe pamekufaa na ukayapatia huko basi huko ndiyo nyumbani kwenu, usitake kulazimisha watu warudi huko ili watekwe, wadhurumiwe na kunyanyasika, kwani huko kuna unafuu gani? Huko walipo ndiyo pamewapenda na kuwapa maisha, waacheni huko au waliwahi kuja kuwaombeni misaada.
haha haha haha hahaaaa!!! yuhyu dada mwenyewe anaonyesha rangi ya mkono wake wakati wa maongezi na yule mwanamke mzungu waliokuwa wakishangaa pamoja kitendo kile, angalia tena hiyo picha, "wamarekani wenzako" wasingeituma hiyo picha kama isingekuwa na tatizo. Manamba hajui kama ananyonywa bali anaangalia shida zake nyumbani zilizomsukuma kufanya kazi za kimanamba. Yaani analinganisha kazi na shida.
 
haha haha haha hahaaaa!!! yuhyu dada mwenyewe anaonyesha rangi ya mkono wake wakati wa maongezi na yule mwanamke mzungu waliokuwa wakishangaa pamoja kitendo kile, angalia tena hiyo picha, "wamarekani wenzako" wasingeituma hiyo picha kama isingekuwa na tatizo. Manamba hajui kama ananyonywa bali anaangalia shida zake nyumbani zilizomsukuma kufanya kazi za kimanamba. Yaani analinganisha kazi na shida.
Unaweza ukamuita manamba, lakini shida zake hakuletei wewe, ulitaka aje mkae naye ili iweje? Kuna mtu hawezi kuishi Mwenge au popote zaidi ya Temeke. Kila mtu akae panapomfaa, huyo akirudi huko, bado mtambagua tu, ajira zinayaka connections au uwe na card ya Chama fulani, akiingia kwenye siasa akawa upande wa upinzani bado mtamuibia kura au mtamteka au kumuua. Au unadhani huko mpo salama? Au kwa kuwa wewe hayakukuti?
Wakina Tundu Lissu walipigwa risasi Marekani na Ulaya? Roma, Ney wa na wengineo, hao wote walitekwa Marekani?
Angalia wasanii walivyo kama watumwa, wote hawana maamuzi binafsi, wanalazimika kisiasa kushabikia Chama fulani sanabu bila hivyo wajiandae kutengwabau kufilisiwa.
Bado mnajiona mpo sawa, only mwenye matatizo ya akili ndiye atadhani mpo sawa.
 
Inabidi kupajua nyumbani kwa kila mtu aliekua nje ndo uwashauri warudi
 
Unaweza ukamuita manamba, lakini shida zake hakuletei wewe, ulitaka aje mkae naye ili iweje? Kuna mtu hawezi kuishi Mwenge au popote zaidi ya Temeke. Kila mtu akae panapomfaa, huyo akirudi huko, bado mtambagua tu, ajira zinayaka connections au uwe na card ya Chama fulani, akiingia kwenye siasa akawa upande wa upinzani bado mtamuibia kura au mtamteka au kumuua. Au unadhani huko mpo salama? Au kwa kuwa wewe hayakukuti?
Wakina Tundu Lissu walipigwa risasi Marekani na Ulaya? Roma, Ney wa na wengineo, hao wote walitekwa Marekani?
Angalia wasanii walivyo kama watumwa, wote hawana maamuzi binafsi, wanalazimika kisiasa kushabikia Chama fulani sanabu bila hivyo wajiandae kutengwabau kufilisiwa.
Bado mnajiona mpo sawa, only mwenye matatizo ya akili ndiye atadhani mpo sawa.
kuna ilivyo na inavyotakiwa iwe. Kuna wakati traffics barabarani wanahangaika na kugombana na madereva na abiria ambao hawakufunga mikanda. Utajiuliza kwanini dereva hakufunga mkanda ambao uko kwaajili ya usalama wake mwenyewe? Kuna wakati najikuta nahangaika na watu wanaotumikishwa na mataifa mengine kwa kigezo cha tofauti umaskini na utajiri wa mataifa yao (manamba). Vijana hawa wananyonywa kunyonywa na kunyonjwa na mabepari kwa kuuza nguvu na ujuzi wao (labor). Nguvu na ujuzi ambao hata familia zao, ndugu, jamaa na mataifa yao wanazihitaji. yaani wanatengeza vicious cycle ya utajiri na umaskini kati ya mabepari na mataifa yao.

Mimi niko kama traffic kuhangaika na madereva wasiokuwa na vifaa vya kuzimia moto kwenye magari yao.
 
Mwaka Jana Kenya diaspora walichangia almost 4.5b USD kwenye uchumi wa nchi. Hiyo ni % ngapi ya total budget ya Tz?

Meanwhile kuna watu humu wameshiba uji wa chumvi wako busy kukwambia kwamba kuishi nje ni unamba! Bottomline, masikini tuna roho mbaya sana. Sijui kwa nini.

Poverty is a disease 🦠
 
Daah! umenena, nini nafahamu kuwa furahi ya mtu haitokani na kuwa na pesa nyingi tu bali mjumuiko wa mambo mengi na hela ikiwemo. Nimekutana na kijana ambae huko majuu ambae analala kwenye gari yake maisha, nilipomuuliza kwanini kwanini huna chumba chako aliniambia ninafanya kazi shift 3 kwa siku hivyo muda wa kulala sina, hata hiyo nyumba naona nitapoteza pesa zangu bure wakati silali humo. Akanambia ana madeni mengi yanayohitaji ku service (kulipa) hivyo lazima afanye kazi zaidi ya 1 ili apate ziada. kaka kijana huyu hajawahi kula chakula cha nyumbani kwake zaidi ya kule fast foods mitaani, makato mengi na anashindwa kutuma pesa nyumbani maana wafyeka hela nyingi sana. kaka kuna mitaa/maduka/malls ukiingia mwenye ngozi nyeusi wanadhani huna pesa ya kuingia hapo bali unataka kuiba, ubaguzi bado haujakwisha tunalazimisha tu.

Nguvu, muda, juhudi, maarifa na akili mnazozitumia kumudu kuishi huko hata zingewekezwa japo nusu tu kwenye jangwa zingetoa matunda. Vijana wetu huku ni wavivu sana ni wavivu sana na ni wavivu sana ndio maana wanapata tamaa ya green card wakidhani huko US pesa ziko kwenye viroba tu ni za kuzoa na kutumia.

Kama asili na chanzo kikuu cha ushoga huko ni maisha magumu, watu wanaunganisha nguvu ili kumudu maisha bila kulazimika kuwa na watoto wa kutunza, yaani kuona mwanamke ni kuongeza ugumu kwenye ugumu. bahati mbaya mimi nimeishi huko sana tena vijijini kabisa ambako maisha ni kama haya hapa ya tandika na kwamtogole, kuchafu na idadi kubwa ya ombaomba wazungu mitaani ambao wanapatiwa nguo kule salvation army na kwingineko kwenye malls kama vile Walmart zenye madirisha ya watu maskini (wazungu) kupatiwa misaada.

kaka usiwadanganye watu ukawapa hope na kuja kuishia kuolewa na wanaume wenzao, wanaofanikiwa ni watu kidogo sana kati ya hao wahamianji. Wengi wao wanaishia kwenye vyombo vya usalama kufungwa na hata kuuliwa.
Nafikiri wewe ulienda huko kwa kuzamia. Elimu yako ilikuwa duni na uwezo wa kwenda (kiakili) shule hukuwa nao. USA ukiomba kazi wanataka high school diploma na wewe huenda ni darasa la saba. Watanzania wengi walioenda USA na elimu zao wana nafasi nzuri. Waliyo na bidii wanafanya kazi viwandani ingawaje kazi za nguvu lakini wanaanzia $15 (Tsh 42,000) kwa saa. Kama wewe ulikuwa vijijini basi huenda ni darasa la aba na kazi pekee ungeweza kupata ni ya kuvuna mazao mashambani, na mtu kama huyo hata kujaza green card lottery haruhusiwi/ha"qualify". Minimum qualification ni form six au forn four with two-year work experience.
 
Nafikiri wewe ulienda huko kwa kuzamia. Elimu yako ilikuwa duni na uwezo wa kwenda (kiakili) shule hukuwa nao. USA ukiomba kazi wanataka high school diploma na wewe huenda ni darasa la saba. Watanzania wengi walioenda USA na elimu zao wana nafasi nzuri. Waliyo na bidii wanafanya kazi viwandani ingawaje kazi za nguvu lakini wanaanzia $15 (Tsh 42,000) kwa saa. Kama wewe ulikuwa vijijini basi huenda ni darasa la aba na kazi pekee ungeweza kupata ni ya kuvuna mazao mashambani, na mtu kama huyo hata kujaza green card lottery haruhusiwi/ha"qualify". Minimum qualification ni form six au forn four with two-year work experience.
Hiyo haikuondolei jina lako la cheap labor kwao. Yaaani kazi hiyohiyo unayofaanyia ina malipo tofauti kwa watu wa rangi na asili tofauti. Africans are the lowest in payment rates. Mimi saloon nanyoa kwa sh.2000 huku, je huko unalipa ngapi?

Wanaolipa sana na wanazichukua Tena kwanjia ya Kodi na mapato na high prices. Najua wewe unavizia clearance paleee kwenye kona ya Mall,
 
Unaweza ukamuita manamba, lakini shida zake hakuletei wewe, ulitaka aje mkae naye ili iweje? Kuna mtu hawezi kuishi Mwenge au popote zaidi ya Temeke. Kila mtu akae panapomfaa, huyo akirudi huko, bado mtambagua tu, ajira zinayaka connections au uwe na card ya Chama fulani, akiingia kwenye siasa akawa upande wa upinzani bado mtamuibia kura au mtamteka au kumuua. Au unadhani huko mpo salama? Au kwa kuwa wewe hayakukuti?
Wakina Tundu Lissu walipigwa risasi Marekani na Ulaya? Roma, Ney wa na wengineo, hao wote walitekwa Marekani?
Angalia wasanii walivyo kama watumwa, wote hawana maamuzi binafsi, wanalazimika kisiasa kushabikia Chama fulani sanabu bila hivyo wajiandae kutengwabau kufilisiwa.
Bado mnajiona mpo sawa, only mwenye matatizo ya akili ndiye atadhani mpo sawa.
Kaka wao tayari wako huko, haina neno wacha watafute liziki maana hawakujuwa kuwa kuna mateso yake. Uzi huu ni kwaajili ya wale wanaotamani kwenda kuhaso kule wakifikiri kila kitu ni tambarare, Hapana, angalia hiki


View: https://youtube.com/shorts/1u_MG5vFrbc?si=ZXPYiGcOLDQa3KUM
 
Kaka wao tayari wako huko, haina neno wacha watafute liziki maana hawakujuwa kuwa kuna mateso yake. Uzi huu ni kwaajili ya wale wanaotamani kwenda kuhaso kule wakifikiri kila kitu ni tambarare, Hapana, angalia hiki


View: https://youtube.com/shorts/1u_MG5vFrbc?si=ZXPYiGcOLDQa3KUM

Kwani shida nini? Kukamatwa ni mateso? Mbona bongo kutekwa na kuuawa na wanausalama ni jambo la kawaida mno?
Sasa hiyo clip haionyeshi chanzo wala nini. Inaonyesha mtu anatakiwa kuwa arrested na yeye ana resist, lakini wakamkamata na watu wanachikua video bila kubughudhiwa au na huyo walienda kumuua?
 
Mwaka Jana Kenya diaspora walichangia almost 4.5b USD kwenye uchumi wa nchi. Hiyo ni % ngapi ya total budget ya Tz?

Meanwhile kuna watu humu wameshiba uji wa chumvi wako busy kukwambia kwamba kuishi nje ni unamba! Bottomline, masikini tuna roho mbaya sana. Sijui kwa nini.

Poverty is a disease 🦠
Wakenya ni wakimbizi ndani na nje ya nchi yao hata baaa ya uhuru, sio mfano sahihi.
 
Kwani shida nini? Kukamatwa ni mateso? Mbona bongo kutekwa na kuuawa na wanausalama ni jambo la kawaida mno?
Sasa hiyo clip haionyeshi chanzo wala nini. Inaonyesha mtu anatakiwa kuwa arrested na yeye ana resist, lakini wakamkamata na watu wanachikua video bila kubughudhiwa au na huyo walienda kumuua?
Omba Mungu Kamala ashinde, la sivyo tutaona mengi.
 
Nafikiri wewe ulienda huko kwa kuzamia. Elimu yako ilikuwa duni na uwezo wa kwenda (kiakili) shule hukuwa nao. USA ukiomba kazi wanataka high school diploma na wewe huenda ni darasa la saba. Watanzania wengi walioenda USA na elimu zao wana nafasi nzuri. Waliyo na bidii wanafanya kazi viwandani ingawaje kazi za nguvu lakini wanaanzia $15 (Tsh 42,000) kwa saa. Kama wewe ulikuwa vijijini basi huenda ni darasa la aba na kazi pekee ungeweza kupata ni ya kuvuna mazao mashambani, na mtu kama huyo hata kujaza green card lottery haruhusiwi/ha"qualify". Minimum qualification ni form six au forn four with two-year work experience.
Nilikuwa nagombaniwa nibaki, na social security number yao ninayo. Lakini kwani nataka nini hasa? Madeni kila sehemu kwa kila kitu?
 
Wakoloni walitusafirisha kwa majahazi kama watumwa kwenda kwao kuwafanyia kazi bure (manamba) kwenye mashamba, viwanda na majumbani kwao, history mbaya sana hii kukumbukwa, maana sio tu kwenda kuwafanyia kazi wazungu bure lakini wengi wao walikufa njiani wakati wakisafirishwa kwa kutoswa majini, msongamano mkubwa, njaa na ugonjwa njiani.

LEO hii miaka 60 baada ya uhuru sababu zilezile za kusafirisha manamba kwenda Marekani, Ulaya na uarabuni ndio sababu hizihizi za watu kwenda huko kwa Green card lottery, Jamani hali hii ni mpaka lini? what are you looking for? Kilichobadilika tu leo ni kitu kimoja tu kutoka manamba walionunuliwa kwenye masoko ya watumwa hadi kwenda kwa green card na baadhi ya sifa za watu wanaohitajika kusafirishwa na aina ya usafiri. Wakati ule walihitaji watu vijana wenye nguvu za kufanya kazi za wakati ule na sasa hivi kwa kutumia green card wanahitaji watu vijana wenye afya wenye elimu na ujuzi maalum kwaajili ya kufanya kazi za wakati huu.

Hii ni kujitafutia balaa wewe mwenyewe na familia yako kwa matumaini feki kabisa huku ukijua kuwa utakwenda kule kufanyakazi kubwa na nyingi sana ili upate chochote kitu wakati nguvu, juhudi na akili hizo ungeweza hata kuziwekeza hapahapa nchini kwako na kupata mafanikio makubwa sana ya ajabu pamoja na kutoa mchango kwenye ujenzi wa taifa lako kwa njia za kodi, tozo na huduma kwa jamii yako.

Jaamaani, Si shauri uombe hiyo kitu, nyambafu!!!!
Mi nilidhani kazi za majumbani kumbe za kitaaluma, basi mshauri Ndugulile kapata kazi WHO
Wakoloni walitusafirisha kwa majahazi kama watumwa kwenda kwao kuwafanyia kazi bure (manamba) kwenye mashamba, viwanda na majumbani kwao, history mbaya sana hii kukumbukwa, maana sio tu kwenda kuwafanyia kazi wazungu bure lakini wengi wao walikufa njiani wakati wakisafirishwa kwa kutoswa majini, msongamano mkubwa, njaa na ugonjwa njiani.

LEO hii miaka 60 baada ya uhuru sababu zilezile za kusafirisha manamba kwenda Marekani, Ulaya na uarabuni ndio sababu hizihizi za watu kwenda huko kwa Green card lottery, Jamani hali hii ni mpaka lini? what are you looking for? Kilichobadilika tu leo ni kitu kimoja tu kutoka manamba walionunuliwa kwenye masoko ya watumwa hadi kwenda kwa green card na baadhi ya sifa za watu wanaohitajika kusafirishwa na aina ya usafiri. Wakati ule walihitaji watu vijana wenye nguvu za kufanya kazi za wakati ule na sasa hivi kwa kutumia green card wanahitaji watu vijana wenye afya wenye elimu na ujuzi maalum kwaajili ya kufanya kazi za wakati huu.

Hii ni kujitafutia balaa wewe mwenyewe na familia yako kwa matumaini feki kabisa huku ukijua kuwa utakwenda kule kufanyakazi kubwa na nyingi sana ili upate chochote kitu wakati nguvu, juhudi na akili hizo ungeweza hata kuziwekeza hapahapa nchini kwako na kupata mafanikio makubwa sana ya ajabu pamoja na kutoa mchango kwenye ujenzi wa taifa lako kwa njia za kodi, tozo na huduma kwa jamii yako.

Jaamaani, Si shauri uombe hiyo kitu, nyambafu!!!!
Mimi nilidhani kazi za majumbani kumbe za kitaaluma, basi mshauri Dk. Faustine Ndugulile Mkurugenzi kikanda wa Afrika katika Shirika la Afya Duniani (WHO). asitishe ajira yake abaki na aendelee na kuitumikia nchi kama Mbunge kabla hajajiuzulu, maana sharti aache kazi nchini ili akaitumikie nafasi yake hiyo.
 
American life is harder, Tanzania life is harder too, so choose your hard but I will do whatever it takes to get better life this is my slogan. Umaskini ni mbaya sana halafu masikini Hana kiapo
 
Back
Top Bottom