Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Green card lottery ni Umanamba mamboleo

Hoja yenu ni kuwa Tanzania hakufai kuishi, hakuna social services nzuri kama huko hivyo unapiga debe vijana waichukie hadi kuikimbia nchi yao waje huko kufanyakazi za umanamba.

Kaka mimi nakumbuka hata tz manamba kwenye mashamba ya mkonge, mpira, ngano, chai, kahawa, ranch za mifugo walikuwa wanalipwa hela za kuwawezesha kuishi, kulipa kodi ya mkoloni bila shida na hata kusomesha watoto wao hadi ngazi ya middle schools shida sana. Japo walikuwa wanapunjwa lakini manamba walikuwa na nafuu kiuchumi kuliko wale ambao hawakufanya kazi za umanamba. Ambao walikuwa hawafanyi kazi za umanamba walikuwa wanalala porini kujificha kukamatwa kwa kushindwa kulipa mkodi.

Kwahiyo unachosema wewe ndio tabia na sababu halisi ya umanamba. Unaweza sasa kujengea wazazi, kulipia ada za wadogo zako, nk kwa kufanyakazi za watu wengi, kulipa kodi kwa nchi nyingine, kukuza uchumi wa nchi nyingine halafu wewe unaambulia kulipwa posho inayokatwa kodi kubwa, kodi ambayo anaenda kuzikopesha nchi nyingine ikiwemo tz kwa riba kubwa na kugharamia vita vya dhuluma kwa nchi changa, nk. Shida yetu kwenye mitaala yetu hakuna somo la Critical thinking kwa watoto wetu.
Hivi wewe una critical thinking! Ama kweli! Critical thinking mngeishia kukimbiza Mwenge! Critical thinking ingekufanya kukosa umeme, maji ya mgao kuona sawa tu!
In short you thinking is in Primitive mode! Na wewe unawakilisha Watanzania wengi! Hamuoni mbele mnabakia mabeberu! Mabeberu! Mabeberu! Inasikitisha!
 
IQ yako ni ndogo sana, Ukraine imenyang'anywa na Urusi mikoa 4, kwahiyo unataka kusema Ukraine ni mazuzu?

DR Congo wanaporwa mali zao kwa mtutu wa bunduki na wazungu kwa mgongo wa Rwanda na Uganda. Msumbiji wanataka kunyang'anywa gesi yao, Sudan Kusini wamenyang'anywa mafuta yao na wazungu kwa mgongo wa vita ya wenyewe kwa wenyewe wanaopatiwa silaha na wazungu. Nani kakwambia kuwa M23 wana uwezo wa kupigana na serikali DRC?
Urusi kakimbia Kharkiv,Kherson
Maana alichukua mkoa 1 tu wa Kherson na kakimbia
 
hata umeme huko umekuja kwa mapambano makubwa kati ya wananchi na wanasiasa,. Hivi ni kweli unataka wajukuu na vitukuu vyako vije vikujue kama mtu aliyekimbia nchi yake kwasababu ya kukosa umeme na maji ya uhakika. Hakika watakukuona kama babu ambae hakuwa na maono, muoga, asiyeaminika, na asiyekuwa mzalendo na mwaminifu?
Kila watakapoona nchi mnapoipeleka watanishukuru milele! Miaka 60 ya uhuru mnachombiwa vyoo vya shimo! Watu ambao mnajiona na Critical thinking mnakwenda kuzindua!
In short mpaka Sasa wananishukuru, maana wameanza kuwatumia pesa wenzao ambao bado hawana kazi lichacya kumaliza chuo kuu!
Just this week my son provided $ 1000/ kwa mtu aliyekwama kabisa huko bongo! Ameahidi kurudisha, tunajua hawezi.
Mpaka they respect me a lot kwa kuwaleta US, singoji kufa wanienzi!
 
Nadhani mtoa maada dhumuni lake la namna mchakato wa Green card lottery umegubikwa na utumwa. kama una nia ya dhati ya kuishi usa kwanini usubiri bahati nasibu? utumwa tu
 
hata umeme huko umekuja kwa mapambano makubwa kati ya wananchi na wanasiasa,. Hivi ni kweli unataka wajukuu na vitukuu vyako vije vikujue kama mtu aliyekimbia nchi yake kwasababu ya kukosa umeme na maji ya uhakika. Hakika watakukuona kama babu ambae hakuwa na maono, muoga, asiyeaminika, na asiyekuwa mzalendo na mwaminifu? Mimi na wenzangu tutabaki hapahapa na kuzikwa hapahapa, tutayabadilisha mambo kuwa bora kwa mikono na akili zetu tukiwa hapahapa bila kulikimbia tatizo. Nikiwa hapa sauti yangu ni kubwa na inayojiamini kuliko ningekuwa kwa waarabu. Siku moja nilikuwa ninamuona jamaa yangu yuko ulaya eti nae anaandamana bei za vitu zimepanda huko maisha yamekuwa magumu, nikamwangaliaaaaaaaaaa hadi nikashikwa na mkojo nikaenda chooni kukojoa na kwenda chumbani kulala.
Mnasafari ya kupambana kubwa! Umeme umekuja kwa kupambana! Miaka 60 toka kupata uhuru! Critical thinker anaandika kwa ujasiri badala ya aibu! Mtambana na maji! Mtapambana ukosefu wa vyoo mashuleni! Mtapambana na opposition parties! Iko kazi
 
Mkuu tuna safari ndefu! Katika karne hii bado kuna upofu mkubwa namna hii wa kufikiri! Hebu niambie jamaa kama huyu awe wizarani na anatengeneza curriculum ya taifa!
Watu kama huyu mleta maada usiombe awe bank halafu una tatizo lako technical na yeye ndio anatakiwa kukupa huduma. Unaweza kulia.

The only reason ilinifanya nikaacha kutumia local banks ni kwa sababu ya uwepo wa wafanya kazi ambao wana akili kama za mtoa maada.
 
Mkuu usidanganyike na takwimu, wengi wanapigika hawawezi kutuma hata mia mbovu, wanaishia kutumikia mfumo na kuambulia pesa ya kulipia pango na bill mbalimbali. Mimi nimekaa moja ya nchi ya ulaya wakati nasoma, hata wazungu wenyewe wanapigika na wanaomba mitaani sembuse wewe wa kuja. Kwa hiyo usiwaaminishe kwamba huko mambo ni mteremko, wasiamini sana wanachokiona kwenye picha na TV, uhalisia unaweza kuwa tofauti na matarajio yao.​
Kama ulifeli kutake chances zako usilalamikie watu kuwa maisha ni magumu.
 
kaka hakuna ku negotiate, hata kama unaonekana umenegotiate lakini utanetiate ndani ya confidence interval fulani, yaani wao wanao ukomo (ceiling) wao kwa kila kazi, kila qualification na kwa kila aina ya mtu (race, nationality and citizenship status). Umepunjwa kaka lakini huoni kama unapunjwa kwakuwa reference point yako ni bongo. yaani unaona hicho ulichokipata ni kingi kuliko kazi hiyo ukiwa Tz/Africa, unaona kama vile umeukata lakini in fact wajua kuwa wewe ni cheap labor/nafuu sana kama wangekuwa wamemuajili Mmarekani halisi kwenye nafasi hiyohiyo (umanamba uko palepale bro!), kusanyeji mitaji huko mrudi huku tuijenge nchi yetu sisi wenyewe. Ni upuuzi kukimbilia mahala ambako tayari wenzako walishahenya kufika hapo walipo kwakuwa eti kwenu kunanuka mavi.
Wewe ni mjinga sana.
 
Mnasafari ya kupambana kubwa! Umeme umekuja kwa kupambana! Miaka 60 toka kupata uhuru! Critical thinker anaandika kwa ujasiri badala ya aibu! Mtambana na maji! Mtapambana ukosefu wa vyoo mashuleni! Mtapambana na opposition parties! Iko kazi
Kaka sababu ya msingi (basic cause) kwanini Tanzania hakuna umeme ni ukoloni mamboleo. Western countries, marekani na our former colonialists ndio sababu hasa ya mataifa ya afrika kuonekana kama yalivyo sasa. Afrika chini ya jangwa la sahara inafanana kiuchumi na kihuduma, na Afrika juu ya jangwa la sahara pia inafanana kwa maendeleo yao. Hii haiwezi kuwa ni coincidence tu, au useme viongozi wote wa afrika ni wajinga na wapumbavu kwa wakati mmoja muda wote na mara zote. Lazima wanakutana na a common factor inayozaliza matokeo yanayofanana. Kujua hili kunahitaji mtu mwenye akili nyingi na critical thinkers. Hawa wazungu huko uliko mzee ndio wanaopanga nani awe rais wetu na nani asiwe rais wetu Afrika, wanapanga bei za vitu vyetu na wanapanga bei za vitu vyao, wanaamua sisi tumiliki nini na wao wamiliki nini kwa bara lote. Wanafanya haya yote kwa kuzingatia maslahi yao wao.

Kiongozi mwenye akili, mjanja, jasiri, mpenda nchi yake, na mwenye maono kama mimi hawamtaki na hawataruhusu atawale, watamuondoa atake asitake kwa kutumia sababu na njia mbalimbali. Juzi juzi wakatuambia tusijenge bwawa la mwl Nyerere, tusijenge barabara kupitia hifadhi za wanyama, tusijenge bomba la mafuta, tusijenge hoteli kwenye mbuga, turuhusu ushoga laa sivyo....Lakini sisi hatuwashauri kwa lolote. Hivi wee jamaa uwezo wako wa kufikiria uko sawasawa?

Hii ni elimu ambayo mtu kama wewe hupendi kuisikia kwakuwa tayari umeshachagua upande.
 
Hivi mgao wa umeme ni sababu ya msingi (sufficient) itakayonifanya mimi niihame nchi yangu na kwenda kujenga nchi za watu wengine? Kwamfano, kama wewe ni daktari wa binadamu, mgao wa umeme unatosha mimi kuwaacha kuwatibu ndugu zangu tz na kwenda kuwatibu wazungu wa nchi nyingine ili wasife na kuishi maisha marefu? eti nipate fedha kichele. Mbona watu wako haapa na wanamudu kusomesha wana wao?
Kwa sababu akili hauna ndio maana unaona mgao wa umeme siyo tatizo.
 
hata umeme huko umekuja kwa mapambano makubwa kati ya wananchi na wanasiasa,. Hivi ni kweli unataka wajukuu na vitukuu vyako vije vikujue kama mtu aliyekimbia nchi yake kwasababu ya kukosa umeme na maji ya uhakika. Hakika watakukuona kama babu ambae hakuwa na maono, muoga, asiyeaminika, na asiyekuwa mzalendo na mwaminifu? Mimi na wenzangu tutabaki hapahapa na kuzikwa hapahapa, tutayabadilisha mambo kuwa bora kwa mikono na akili zetu tukiwa hapahapa bila kulikimbia tatizo. Nikiwa hapa sauti yangu ni kubwa na inayojiamini kuliko ningekuwa kwa waarabu. Siku moja nilikuwa ninamuona jamaa yangu yuko ulaya eti nae anaandamana bei za vitu zimepanda huko maisha yamekuwa magumu, nikamwangaliaaaaaaaaaa hadi nikashikwa na mkojo nikaenda chooni kukojoa na kwenda chumbani kulala.
Nairudia hoja yako inatisha hasa kwa mtuu ayejiita critical thinker! Nakuuliza tu mwisho wa mapambano yako ni lini! Kila mwaka lazima utoe mchango wa Mwenge! Bado mapambano ya kupata pensheni yako uzeeni!
Bado watoto wako watakua hawana ajira! Anyway labda wewe ni kama wa Chama wanaweza kujishikiza Lumumba!
Mwenyezi Mungu angetupunguzia makali ya Jehanamu sisi Waafrika!
 
Watu kama huyu mleta maada usiombe awe bank halafu una tatizo lako technical na yeye ndio anatakiwa kukupa huduma. Unaweza kulia.

The only reason ilinifanya nikaacha kutumia local banks ni kwa sababu ya uwepo wa wafanya kazi ambao wana akili kama za mtoa maada.
huwa mara zote nina compare na ku contrast kati ya green card na manamba, similarities ni nyingi kuliko differences, naama zote zilikuwa zinatafuta basically wafanyakazi wa bei rahisi, zote zilikuwa zinahusisha kuhama kutoka kwenye homeland yako, yaani Waha, wanyamwezi, wasukuma walihamishwa kutoka kwao kwenda kufanyakazi kwenye mashamba makubwa ya mkonge, wanyama na migodi, wote wanalipwa kwa kupunjwa, wote wanakuwa mbali na kwao, wote wanalipa kodi kulekule ugenini waliko, wote wakifa wanazikwa hukohuko unambani, wote wana maendeleo kuliko familia zao walikotoka. Lakini tofauti zao kubwa ni kwamba Manamba walikuwa wanapelekwa kwa nguvu lakini green card wanaenda wenyewe, green card wanatakiwa awe na elimu na ujuzi kwaajili ya kufanyakazi za wakati huu lakini Sifa kuu ya manamba ilikuwa kuwa na nguvu na umbo kubwa kwasababu ya kufanyakazi za wakati ule, na tofauti nyingine green card anaweza akaishi mtaani lakini manamba walikuwa wamejengewa kambi waishi hapohapo karibu na kazi husika.
 
umeme huko umekuja kwa mapambano ]makubwa kati ya wananchi na wanasiasa,. Hivi ni kweli unataka wajukuu na vitukuu vyako vije vikujue kama mtu aliyekimbia nchi yake kwasababu ya kukosa umeme na maji ya uhakika. Hakika watakukuona kama babu ambae hakuwa na maono, muoga, asiyeaminika, na asiyekuwa mzalendo na mwaminifu?

Kavulata: Watoto wangu wananiona ni super dad! genius dad! Kila mara wananiuliza niliwazaje kuwatoa Tanzania
Almost 75% ya wenzao hawana kazi, wanangu walichukua P3 zao na kutuma kwa mtu ambaye ni graduate ili awe anachezesha game kupata pesa!
Huwa wanashangaa kuna baadhi ya ndugu zao hawako Wassup, kisa hawana smart phone, na wakiwa na smart phone hawana bundle! Inakuwa ni kazi kuwaeleza!
Nimekwambia single kufa wanipongeze! Wanaona wenyewe nimewaepusha na maisha gani!
Pambana mkuu!
 
Japo sijawahi kuishi huko lakini mzee bongo life ni tough sana.

Huenda wewe ni mwenyeji wa dar, huko vijijini hujaenda kuona watu wana maisha magumu kiasi gani.

Sikiliza tu story ya majaliwa, uone maisha ya familia ya dogo yalivyo magumu, pesa anapata kwa kuanika dagaa ambayo huenda hata yeye tu haimtoshi.

Ajira hakuna, wati viwandani wanalipwa buku 3 kwa siku ndgu yangu, si bora huko walau ela unaiona japo gharama za maisha zipo juu lakini somehow haki za binadamu zinafuatwa.
Mkuu najua bongo ni tough, nina ndugu Dar hadi vijijini, kila siku ni vilio, naangalia exchange rate ya $ kwa Tanzania shilling, inaniumiza sana, yaani nikimpa mtu dola 47,tayari ni laki.
Sasa kwangu hiyo ni kitu kidogo sana!
Nikiwatumia nakua kama mfalme!
Kinachoumiza ni huu upumbuvu wa Watanzania wenzetu,tunapotoa options za kujaribu nje wanaona ni umanamba! Na hawa wanadai wasomi! Critical thinker, unabakia unashangaa kama wanajua maumivu ya Watanzania.
Labda wako katikati ya jezi ya kijani, hawaoni maumivu ya Watanzania!
 
huwa mara zote nina compare na ku contrast kati ya green card na manamba, similarities ni nyingi kuliko differences, naama zote zilikuwa zinatafuta basically wafanyakazi wa bei rahisi, zote zilikuwa zinahusisha kuhama kutoka kwenye homeland yako, yaani Waha, wanyamwezi, wasukuma walihamishwa kutoka kwao kwenda kufanyakazi kwenye mashamba makubwa ya mkonge, wanyama na migodi, wote wanalipwa kwa kupunjwa, wote wanakuwa mbali na kwao, wote wanalipa kodi kulekule ugenini waliko, wote wakifa wanazikwa hukohuko unambani, wote wana maendeleo kuliko familia zao walikotoka. Lakini tofauti zao kubwa ni kwamba Manamba walikuwa wanapelekwa kwa nguvu lakini green card wanaenda wenyewe, green card wanatakiwa awe na elimu na ujuzi kwaajili ya kufanyakazi za wakati huu lakini Sifa kuu ya manamba ilikuwa kuwa na nguvu na umbo kubwa kwasababu ya kufanyakazi za wakati ule, na tofauti nyingine green card anaweza akaishi mtaani lakini manamba walikuwa wamejengewa kambi waishi hapohapo karibu na kazi husika.
Unapotaka kubadili hali yako ya maisha, inabidi ufanye uamuzi mgumu, mojawapo ni ka kuondoka nchini kwako, jamaa zangu hawaoni hilo!
 
Mkuu najua bongo ni tough, nina ndugu Dar hadi vijijini, kila siku ni vilio, naangalia exchange rate ya $ kwa Tanzania shilling, inaniumiza sana, yaani nikimpa mtu dola 47,tayari ni laki.
Sasa kwangu hiyo ni kitu kidogo sana!
Nikiwatumia nakua kama mfalme!
Kinachoumiza ni huu upumbuvu wa Watanzania wenzetu,tunapotoa options za kujaribu nje wanaona ni umanamba! Na hawa wanadai wasomi! Critical thinker, unabakia unashangaa kama wanajua maumivu ya Watanzania.
Labda wako katikati ya jezi ya kijani, hawaoni maumivu ya Watanzania!
Kabisa mzee, kuna wana wanahustle kichizi mlo wanapata kwa tabu.
Watu wakifanya biashara za umachinga wanatimuliwa wengine wanapigwa na polisi na migambo mpaka wanapata ulemavu wa kudumu.

Mzee mbele ni mbele tu aisee, japo naskia kuna ubaguzi lakini ubaguzi hauui kama hawa polisi na migambo wetu.
 
Kwa sababu akili hauna ndio maana unaona mgao wa umeme siyo tatizo.
Mkuu jamaa hana laptop,kindle au tablet,au hana project yoyote akirudi nyumbani! Kaenda shule but he still a cave man! Primitive to the core! Na rafiki yangu ni Architect, yuko nyuma mno katika projects zake! Mara ofisini haupo mara nyumbani haupo!
Lakini anayejiita critical thinker haoni tabu kuwasha mshumaa!
Bado DNA ya mababu zake waliotumia kuni iko kwenye damu!
Unategemea mtu kama huyu atawavusha Watanzania katika karne hiii?Thubutu!
 
Kabisa mzee, kuna wana wanahustle kichizi mlo wanapata kwa tabu.
Watu wakifanya biashara za umachinga wanatimuliwa wengine wanapigwa na polisi na migambo mpaka wanapata ulemavu wa kudumu.

Mzee mbele ni mbele tu aisee, japo naskia kuna ubaguzi lakini ubaguzi hauui kama hawa polisi na migambo wetu.
Mkuu nina miaka US, sijabaguliwa! Watu wanasahau kabisa sheria za US ni kali sana kuhusu ubaguzi wowote ule! Ukiwa na evidence mtu kakubagua kazini kwa dini, rangi, jinsia ni ngumu sana.
Na jamaa zangu Waarabu, saa za swala wanatoa Mike kama yao wanapiga swala zao hakuna anayewabughuzi!
Achana na media. Kama ubaguzi upo wangapi wangeondoka Marekani!
 
Mkuu nina miaka US, sijabaguliwa! Watu wanasahau kabisa sheria za US ni kali sana kuhusu ubaguzi wowote ule! Ukiwa na evidence mtu kakubagua kazini kwa dini, rangi, jinsia ni ngumu sana.
Na jamaa zangu Waarabu, saa za swala wanatoa Mike kama yao wanapiga swala zao hakuna anayewabughuzi!
Achana na media. Kama ubaguzi upo wangapi wangeondoka Marekani!
Sasa mbona jamaa anaktisha tamaa watu kwenda huko akidai huku ni bora kuliko huko!??

Wabongo tuna roho za wivu sana sijui kwanini asiee, kisa ye kafeli basi hataki mwingine ajaribu akiamini akifaulu basi yeye ataonekana hamnazo.
 
Sasa mbona jamaa anaktisha tamaa watu kwenda huko akidai huku ni bora kuliko huko!??

Wabongo tuna roho za wivu sana sijui kwanini asiee, kisa ye kafeli basi hataki mwingine ajaribu akiamini akifaulu basi yeye ataonekana hamnazo.
Kwa kifupi sijui lengo lake! Sijasema kila mtu lazima akitaka kufanikiwa aje US, nalosema ukiona options za nyumbani ngumu jaribu nje! Wanageria, Wakenya na watu nje ya Afrika wanafanya hivyo!
Jamaa hataki kabisa kusikia, na anakuja na very primitive arguments! Eti uzalendo! Uzalendo utasomesha watoto wako? Uzalendo utakupa mahitaji yako unayotafuta maishani?
Ukishindwa jambo unatafuta options nyingine,ndio nacho jaribu kusema hapa! Lakini naona nazungumza Kichina!
 
Back
Top Bottom