GUMZO: Al Ahly ageuka kibonde baada ya mechi na Simba

GUMZO: Al Ahly ageuka kibonde baada ya mechi na Simba

Leo hoja hii inatetewa lakini kipindi Yanga anacheza na tp mazembe mlidai tp mazembe kashuka kiwango😂😂
Alishuka haswaa na ndio maana aliangukia Shirikisho baada ya kufurushwa kombe la Klabu Bingwa na Vipers ya Uganda iliyokuja kushika mkia kwenye group stage
 
Nimependa Matumizi yako ya neno Mbumbumbu, Ila ngoja tuone;

Katika League ya Misri, wapo round ya nne(4). Al Ahly anashika nafasi ya Saba(7) sio tatu(3) kama ulivyosema huku akiwa amecheza michezo miwili pekee, ambayo yote ameshinda.

Pamoja na kuwa imecheza michezo miwili pekee ila ni timu inayoongoza kwa goal difference katika ligi hiyo.

Hizo mechi tano ni mchanganyiko wa CAFCL, Ligi Kuu na Egypt Cup.

Kama mambo madogo kama haya unashindwa kuyajua au kuelewa, Wakikuita Mbumbumbu watakua wanakosea?
Vipi na USM Alger?
Alafu nilijua utakuja kuthibitisha kua Al-ahal kabla ya kucheza na Simba kashinda mechi tano mfululizo!![emoji23][emoji23][emoji23].... kumbe umekuja kuthibitisha umbumbumbu wako kwa mala nyingine.
Punguza kitambi kwanza hicho.
 
BIG UP

@Bestdady.

Andiko Bora kabisa LILILO tukuka
Wenda huwajui.
FB_IMG_1697548664677.jpg
 
Alishuka haswaa na ndio maana aliangukia Shirikisho baada ya kufurushwa kombe la Klabu Bingwa na Vipers ya Uganda iliyokuja kushika mkia kwenye group stage
Basi na Al ahly kwasasa ameshuka kiwango
 
Mimi ni shabiki wa wana lunyasi lakini naomba niseme kwamba mpira wa sasa umebadilika mkubwa sasahiv watu wanacheza kitu kinaitwa Economic Football kwa maana ya kuwa Kama uliangalia mechi vizuri kwa % kubwa sana National Ahly hawakuwa na presha sana ya mchezo sababu walikuwa wana uhakika kwamba Simba ndio mwenye mlima mkubwa kupindua matokeo yale na kuwafanya wavuke.

Siku hizi mkubwa ni kwamba haijalishi timu inavukaje muhimu na cha kuzingatia tu ni kwamba imevuka kwenda hatua inayofata hizo zingine ni mbwembwe tu.

Tazama Mamelod Sandowns yuko home home na Petro de Luanda ametoka suluhu ya bila bila na hapo utasemaje?

Robertinho mwenyewe huwa anasema yeye hataki kujua timu inacheza vipi muhimu na anachojali ni je, timu inapata matokeo? Ukielewa hili utakuwa umepiga hatua kiakili.

Siku hizi kila timu inaingia uwanjani na game plan ya mechi husika kulingana na matokeo yanayohitajika. Ukitaka kuamini subiri mechi inayokuja ya Al Ahly na Mamelod ndio utaelewa ninachomaanisha kwa kuwa umewakosea sana heshima National Ahly eti kisa tu hizo draw mbili na Simba na kuvuka kwao kwa mgongo wa goli la ugenini.

Kilichotokea kwa Simba ni bahati tu na wala si zaidi ya hapo
 
Leo hoja hii inatetewa lakini kipindi Yanga anacheza na tp mazembe mlidai tp mazembe kashuka kiwango😂😂
Ahly hajafikia level za mazembe mpka kuja kumsajili singano na ambokile mazembe hawako vxuri huo ndio ukweli lkn Ahly bdo anaendelea kusajili mpka epl ligi kuu ujerumani huko akijisikia anasajili unamfananishaje na mazembe
 
Ahly hajafikia level za mazembe mpka kuja kumsajili singano na ambokile mazembe hawako vxuri huo ndio ukweli lkn Ahly bdo anaendelea kusajili mpka epl ligi kuu ujerumani huko akijisikia anasajili unamfananishaje na mazembe
Soma kilichoandikwa acha kukurupuka hakuna mtu kamlinganisha Al ahly na mazembe hapo
 
Je, Simba SC kutolewa na Al Ahly SC ilipaswa kuwa story kubwa?.

Majibu ya swali hili yanaweza ibua mijadala mingi sana, ambayo si yataleta tofauti kwa mashabiki (watu kushikana mashati) bali italeta hisia tofauti kuanzia kwa ngazi ya uwekezaji, uongozi hata wachezaji kwa ujumla.

Lakini kuna baadhi ya vichekesho vinaendelea Tanzania ya kuwa Al Ahly sasa wapo "Unga", wakimaanisha Al Ahly ni timu mbovu kwa sasa.

Ila mbona Imekua mapema sana. kwanini tume-shift haraka hivyo kutoka kusema kuwa Simba atapigwa kama ngoma wengi wakisema 3+ (anaenda kuliaibisha Tanzania) hadi Al Ahly ni wabovu. Mbona imekua ghafla hivyo?

Je, hizi kauli mlikua mnasema wakati hamjamuona Al Ahly akicheza?
Je, mlikua mnasema kitu ambacho hamkijui? Tukiwaita waropokaji tutakua tunawakosea?
Tukianza kuwapuuza kile mnachokisema, tutaonekana tuna dharau?
Maana tuliwaamini zile kauli zenu za kumpamba Al Ahly...mbona sasa mmetugeuka? Tushikilie yale mliyotuambia wakati ule au haya ya Sasa? Tunaomba majibu .

Well...Sasa ngoja niwape takwimu ya Al Ahly kabla ya mechi ya Simba.
Al Ahly katika mechi zake tano(5) za mwisho kabla ya kukutana na Simba ameshinda mechi zote, amefunga mabao kumi na saba (17) na kuruhusu goli moja (1) pekee.

Why ageuke kuwa unga baada ya hizi mechi mbili na Simba?

Let me whisper something; Hizi kauli sio mara yao ya kwanza, Ni kama script inajirudia vile. Katika comment moja ya mashabiki wa Al Ahly aliyejaribu kuwapa moyo mashabiki wenzake waliolalamika kuwa wanahitaji kubadilishwa mishipa ya damu baada ya kuhisi kupasuka kutokana na pressure ya mchezo. Hii ni lugha ya picha. (Unaweza pita kwenye ukurasa wa Al Ahly kuthibitisha hili).

Ila huyo shabiki wa Al Ahly alisema bora yetu sisi, huku akiwauliza wenzake mliona kilichotokea Mohamed V? Kwa wenzetu kilikuwa ni kiwanda cha machozi, yalikua ni mateso. Akimaanisha mashabiki wa Wydad walilia sana katika mechi ile. I hope wewe unayesoma andiko hili ulishuhudia kilichotokea, kama hukuona basi nikuambie mambo yalikua hivyo japo Wydad alifanikiwa kuvuka kupitia Mikwaju ya penati(4-3).

Ila Tanzania baada ya mechi hizo mbili na Simba, tuliambiwa Wydad wa sasa ni wabovu ila chakushangaza Wydad alifika hatua ya Fainali, japo Bingwa alikua Al Ahly. Na hakuna aliyekuja kubadilisha kauli yake, mambo yakaisha hivyo.

Kuna kitu katika Kauli ya Kocha Al Ahly (Koller) kuhusu Simba;

Baada ya mchezo wa Kwanza, Koller alijinasibu kuwa yeye ndiyo kocha aliyepata matokeo bora zaidi dhidi ya Simba, maana kila Kocha aliyekuja na Al Ahly kucheza na Simba kwa Mkapa alifungwa. Hapa akimaanisha Simba sio wa kawaida kawaida kama watu wanavyosema. Ila baada ya mechi ya pili: Japo hii kauli inatamfanya awe na wakati mgumu pale Al Ahly Sc (Huwezi bishana na Mashabiki wa Al Ahly ukabaki salama, muulize Pisto) ila yeye aliwapinga vikali kusema kauli ya kusema amecheza vibaya, ila yeye anaona amecheza vizuri sana kulingana na mpinzani aliyekutana nae. Hii ina maanisha nini? Majibu unayo.

Hata alipoulizwa issue ya kufanya mabadiliko ya wachezaji, alisema alishindwa kufanya Sub za Wachezaji sababu hakutaka wachezaji wapya waingie na kutumia muda ku-adapt tempo ya mchezo..."ambapo akiamini katika muda huo ambao yeye wachezaji wake wangetumia ku-adapt mchezo, mpinzani wake (Simba) angetumia nafasi hiyo kupata matokeo". Hapa Jamaa anamaanisha nini? Japo tuliona amemuingiza modeste jioni kabisa. Ila naamini Kocha wa Al Ahly (Koller) itamchukua muda mrefu sana hili jinamizi la Robertinho na Simba yake kutoka kichwani mwake.

Mashabiki wa Mamelodi wanasemaje:
Ukipita katika comment ambazo zimeigusia Simba, wanasema afadhali wamempata Al Ahly "Babe" wao, maana Simba ni timu ambayo utajidanganya unacheza mpira, unafika final third lakini hutaliona goli. Labda kwa maneno machache hii mbinu inafahamika "Haram Ball". Hii kauli inaweza thibitika katika mechi za Simba na Yanga (Ngao), wengi walisema Yanga alipaswa kushinda hata goli tano ila takwimu zinaonesha tofauti, Yanag alikua na Shot on Target moja pekee, huku zikiwa mbili pekee kwenye mechi na Al Ahly Sc katika mechi ya jana.

Huku wengine wakisema, katika hizi mechi mbili, Simba imebadilisha mentality ya Timu za chini ya ukanda wa jangwa la sahara kuwa hawa vigogo wa Africa ambao ni Timu namba moja Africa " Al Ahly" na namba mbili "Wydad", kuwa ni kweli wanakila kitu ila wakati wa timu zetu kufanya vitu umefika na nyakati za kuteswa sana zimeisha.

Turudi kwenye kosa kosa za Al Ahly, Unahisi kwanini wali-opt kupiga mashuti ya mbali baada ya kufika final third? ambapo hii labda inawafanya wengi wamaanini Al Ahly wapo unga, ambayo mengi yalikuwa ni off target. Mambo yapo hivi, tuliona kazi/clearance zilizokua zinafanyika na Che pamoja na Inonga. It was like, nikweli utamlambisha nyasi Che lakini Mimi(Inonga) nitakua nyuma ku-clear(vice versa), Hii ilifanya wa-opt kupiga mashuti ya mbali sababu ya Strength za beki za Simba.

Je hii nguvu ya kuishusha Al Ahly ili kui-discredit Simba mnafanya kwa manufaa ya nani?
Je ni hasira za kumpa 3+ Al Ahly katika betting?

Je mlitamani kuona Simba amefungwa zaidi ya 5 ndio kuthibitisha ubora wa Al Ahly?

Je kuna boss mnamtumikia, so mnaogopa kumkosea kwa kusema kile alichokifanya Simba?

Nashindwa kupata majibu kabisa. Why Wydad na Al Ahly wageuke wabovu wakikutana na Simba pekee? Katika hizi mechi mbili nilitegemea watanzania wata-ipongeza Simba kwa kuweza kuonesha ushindani dhidi ya Al Ahly Sc kama ninavyoona watu kutoka mataifa ya Africa(Nje ya Tanzania) waliokua wakifuatilia AFL wakifurahia na kushangazwa na kile kilichooneshwa na Simba, wakisema ni beyond their expectation. Kuna shabiki mmoja baada mechi ya kwa mkapa alisema and I qoute "...I think this should be a derby of Africa". (Anaweza akawa anatania, ila kitu amemaanisha, kuna radha anaipata wanapokutana hawa wiwili maana hadi sasa ni 50- 50).

Tukubali tukatae hadi kufikia sasa, japo anaitwa Mwakarobo na timu ambayo haijafika mafanikio yake kimataifa ila Simba ni timu iliyonesha ushindani mkubwa sana kimataifa.
Pia kwa Yanga I hope itakuwa the same, wapambane kuonesha walichonacho kimataifa ili kile kilichofachanyika msimu uliopita isionekane ni "fluke" I mean walibahatisha tu.​
giphy.gif
 
Je, Simba SC kutolewa na Al Ahly SC ilipaswa kuwa story kubwa?.

Majibu ya swali hili yanaweza ibua mijadala mingi sana, ambayo si yataleta tofauti kwa mashabiki (watu kushikana kuonesha walichonacho kimataifa ili kile kilichofachanyika msimu uliopita isionekane ni "fluke" I mean walibahatisha tu.​
A failed team, aka Nkima waza na bhupe wayinyela inghana. Acheni excuse na mbambamba....
 
Kama hili punga hapa linajua kurembua macho tuView attachment 2792299

Jamaa kajishushia heshima sana. Binafsi nilishaacha kusikiliza hawa wacha mbuzi wa mchingo.

Unasemaje finalists wa juzi tu champions lg ni wabovu. Inamaana Wydad mbovu, ameshuka kiwango,
Al alhly nae mbovu ameshuka kiwango. Kisa tu wametifuana na Simba. Haya watuambie ni nani sasa aliyebora?
 
Jamaa kajishushia heshima sana. Binafsi nilishaacha kusikiliza hawa wacha mbuzi wa mchingo.

Unasemaje finalists wa juzi tu champions lg ni wabovu. Inamaana Wydad mbovu, ameshuka kiwango,
Al alhly nae mbovu ameshuka kiwango. Kisa tu wametifuana na Simba. Haya watuambie ni nani sasa aliyebora?
Kakishushia heshima pia kituo chake kazi,sasa hivi Wasafi FM imekuwa ni kitengo cha propaganda cha Yanga. Au ndiyo maelekezo ya mmiliki wake aliyemfuata mvuta bangi mwezake Haji Manara aliyehamia Yanga toka Simba.
 
Nimependa Matumizi yako ya neno Mbumbumbu, Ila ngoja tuone;

Katika League ya Misri, wapo round ya nne(4). Al Ahly anashika nafasi ya Saba(7) sio tatu(3) kama ulivyosema huku akiwa amecheza michezo miwili pekee, ambayo yote ameshinda.

Pamoja na kuwa imecheza michezo miwili pekee ila ni timu inayoongoza kwa goal difference katika ligi hiyo.

Hizo mechi tano ni mchanganyiko wa CAFCL, Ligi Kuu na Egypt Cup.

Kama mambo madogo kama haya unashindwa kuyajua au kuelewa, Wakikuita Mbumbumbu watakua wanakosea?
Al Ahly si juzi tu alifungwa na USM ALGER waliocheza na Yanga fainali confederation? Na hao USM ALGER walifungwa na Yanga kwao fainali? kubali tu Al,Ahly imeshuka kiwango.
 
Back
Top Bottom