Uchaguzi 2020 Gwajima ni Mgombea anayezungumziwa sana. Je, ni kwanini?

Uchaguzi 2020 Gwajima ni Mgombea anayezungumziwa sana. Je, ni kwanini?

dindilichuma

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2015
Posts
1,736
Reaction score
2,699
Kila siku nikifuatilia nyuzi hapa JF nakutana na nyuzi nyingi zikimzungumzia Mgombea wa Ubunge Jimbo la Kawe askofu Josephat Gwajima.

Nabaki najiuliza kwa majimbo yote ya Tanzania na hata majimbo tu ya Dar kwanini yeye tu anazungumziwa zaidi Kwanini nguvu kubwa inatumika kumzungumzia?

Nimefuatilia na kukuta Hoja nyingi anazosemwa Gwajima ni mambo binafsi na ya kazi zake Za kila Siku binafsi. Sioni akipigwa kwa Sera zake Kama mgombea ubunge. Anafunguliwa nyuzi nyingi Sana kuliko mgombea ubunge yeyote.

Nimeanza kuamini Gwajima inawezekana anauwezo mkubwa na kama asingekuwa nao wapinzani wake wangempuuza na wasingehangaika nae. Ila Gwajima ni tishio Sana kwa nafasi aliyogombea.

Unaweza kuona mtu anaanzisha uzi kuhoji ujenzi wa kanisa linaloongozwa na Gwajima na mtu huyohuyo akashindwa pengine kuhoji ujenzi wa ofisi ya Chama chake kianachopokea ruzuku. Hapo unapata picha ni nini kinaendelea kwa anaehoji.

Tujaribu kuwahoji wagomhea wetu kwa sera na ahadi zao bila kuwabagua. Ubunge ni kuhakikisha wananchi wa Tanzania na Jimbo lako wanajipatia maendeleo na Maisha yao yanakua rahisi. Mbunge ashirikiane na kuiambia serikali na taasisi na yeyote mwenye Masaada juu ya kero na mambo Mazuri yanayopaswa kufanyika jimboni kwake.

Baada ya Tarehe 28/10/2020 tunaweza kupata jibu ni kwanini Gwajima anazungumzwa Sana hasa na wasio penda awe mbunge na wanaopenda awe mbunge hawazungumzi Sana.

Hamkani Shwari si Shwari tena.

Naamini tutaenda kupiga Kura.
 
Siasa na ...
>Mwanasiasa akikwambia nje kuna giza, usichukue uamuzi wa kutaka kulala hapo hapo, ILA toka nje uhakikishe kweli kuna giza!.
 
Hahaha matapeli huwa yanaongelewa sana.

Hasa kama haya yanayofufua wafu feki. Mzee Mkapa kafa juzi sijui kwanini hawakumuita UNO boy aje amfufue?
 
Anazungumziwa kwa sababu kampeni anazopiga ni zauongo mwingi sana labda kama mtu haujaenda shule ndio unaweza usitambue uongo wake anatoa ahadi ambazo ata magufuli akiwa mbunge hawezi kuzitekeleza
 
Anazungumziwa kwa sababu kampeni anazopiga ni zauongo mwingi sana labda kama mtu haujaenda shule ndio unaweza usitambue uongo wake anatoa ahadi ambazo ata magufuli akiwa mbunge hawezi kuzitekeleza

Vitabu vitano vya Kijapani duu asalale Mtume simama dunia ipite
 
Mpondaji mkuu Ni mmoja tu .Halima Mdee.Ana ID tofauti tofauti nyingi
 
Na hapo ndo hajaingia mjengoni!

... akiingia mjengoni, kwa vibweka vyake, vyombo vya habari, YouTube, Jamii Forums ... etc, vitafurika habari zake!
😅
👊 ✌✌✌💥
 
Kwa sababu ni muhuni na tapeli aliyetapeli watu kwa kigezo cha dini na sasa ameingia kutapeli kupitia siasa
 
Unaweza kuzungumziwa sana kwa sababu umekuwa wa hovyo sana au kwa sababu ni bora sana.

Gwajima, wengi wanamzungumzia kwa kuishangaa CCM inakuwaje kumteua mtu wa ajabu na wa hovyo kabisa kama Gwajima kuwa mgombea wao!!

Mtu tapeli, mwongo, asiye na maadili hata yale kawaida tu, mcheza picha za ngono! Au tuseme CCM wamerogeka ni hiyo misukule ya Gwajima? Lakini siyo ajabu - CCM huabudu sana ushirikina na washirikina. Walikuwa na mganga wao Majimarefu, baadaye wakampa na ubunge.
 
Kila siku nikifuatilia nyuzi hapa JF nakutana na nyuzi nyingi Zikimzungumzia mgombea wa ubunge jimbo la Kawe askofu Josephat Gwajima....
kwa wee hujui kuwa hata mtandaoni site zinazotizamwa sana ni zile za ngono na udaku? gwaj boy ni udaku kwa hiyo pni lazima wananchi wa kawe tujilinde dhidi ya udaku
 
Unaweza kuzungumziwa sana kwa sababu umekuwa wa hovyo sana au kwa sababu ni bora sana.

Gwajima, wengi wanamzungumzia kwa kuishangaa CCM inakuwaje kumteua mtu wa ajabu na wa hovyo kabisa kama Gwajima kuwa mgombea wao!!

Mtu tapeli, mwongo, asiye na maadili hata yale kawaida tu, mcheza picha za ngoni!! Au tuseme CCM wamerogeka ni hiyo misukule ya Gwajima? Lakini siyo ajabu - CCM huabudu sana ushirikina na washirikina. Walikuwa na mganga wao Majimarefu, baadaye wakampa na ubunge.
msiwalaumu sana ccm inawezekana hawana watu sasa wafanyaje? Jiji la Arusha eti kapelekwa gambo kushindana na Kamanda🤣🤣🤣🤣🤣
 
Mmesahau kipindi kile Rais Clinton kidogo afurushwe kwenye ofisi ya urais kutokana na skendo yake na Monica Lewinsky.

Kabla ya kumchagua mtu tunamu-assess kwanza kwamba ni mtu wa aina gani.

reputation matters
 
Ugumu wa kawe kwa chadema ni kuwaambia walifanya nini na watafanya nini Halima akirudishwa bungeni.
Gwajima yeye ni kazi rahisi sana kuwapa ahadi wananchi kua wakimchagua atafanya nini. Inampa urahisi wa kuaminiwa kuliko huyu aliyekaa miaka 10 harafu hana la maana.
Lakini gwajima alishajitambulisha kiasi hakuna mtu nchi anayefuatilia siasa hamfahamu gwajima. Wababa, wamama, wazee na watoto wanamjua gwajima
.
 
Back
Top Bottom