Gwajima, tekeleza ahadi yako kwa wakazi wa Basihaya

Gwajima, tekeleza ahadi yako kwa wakazi wa Basihaya

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Ukiamua kutaja maeneo ya jiji la Dar es salaam yanayo athirika na mvua za kila mwaka huwezi kusahau kutaja eneo la Basihaya linalopatikana jimbo la Kawe.

Basihaya ni miongoni mwa maeneo yanayojaa maji kila mwaka pindi msimu wa mvua unapofika. Barabara (Bagamoyo road) hufunikwa kabisa, maji na udongo hujaa na miundombinu mingine ikiathirika pia kwa kiasi kikubwa.

Chanzo cha tatizo hili ni nini?

Eneo hili halina mitaro ya maji hivyo maji yanayotoka upande wa Tegeta hujikusanya hapo. Aidha, kukosekana kwa udhibiti wa maji yanayotoka mlima wa wazo ambao huyatiririsha hadi barabarani ndiyo vyanzo vikubwa viwili vya tatizo hili.

Gwajima anahusikaje?

Pamoja na kutoa ahadi lukuki za kupeleka watu ulaya, kununua boti za uvuvi, Mchungaji Josephat Gwajima aliahidi kutatua tatizo hili sugu kwa wakazi wa Basihaya. Yeye ndiye mbunge wa eneo hili.

Miaka inakimbia, siku zinayoyoma. Gwajima haonekani.

Adha hii inazidi kuwa kubwa kila siku. Ni hadi watu hawa wafe kwa magonjwa ya mlipuko ndiyo wakumbukwe? Kwanini maoni na maombi yao hayasikilizwi? Lengo la Gwajima kusema uongo kuwa atashughulia kero hii lilikuwa ni lipi? Ufanisi wa bandari ya Bagamoyo utakuwaje kama sehemu ya barabara inayounganisha sehemu hii ina hali mbaya kiasi hiki?

Askofu Gwajima, tekeleza ahadi yako.
 
Tegeta inaingiaje katika kujaza maji Basihaya?.

Tatizo kubwa la kujaa maji lilitokana na barabara ya Bagamoyo kukosa karavati kubwa za kuvusha maji yanayotoka mlima wa Wazo hill.
 
Hata mgogoro wa ardhi Mbopo hajaweza kusimamia haki itendeke mwenye kustahili arejeshewe eneo lake.

Yani watu walikuwa na high expectations lakini matumaini naona yanapotea.

Ni kanakwamba anafurahishwa na dhuluma kitu ambacho sitaki kuamini .
 
Ukiamua kutaja maeneo ya jiji la Dar es salaam yanayo athirika na mvua za kila mwaka huwezi kusahau kutaja eneo la Basihaya linalopatikana jimbo la Kawe.

Basihaya ni miongoni mwa maeneo yanayojaa maji kila mwaka pindi msimu wa mvua unapofika. Barabara (Bagamoyo road) hufunikwa kabisa, maji na udongo hujaa na miundombinu mingine ikiathirika pia kwa kiasi kikubwa.

Chanzo cha tatizo hili ni nini?

Eneo hili halina mitaro ya maji hivyo maji yanayotoka upande wa Tegeta hujikusanya hapo. Aidha, kukosekana kwa udhibiti wa maji yanayotoka mlima wa wazo ambao huyatiririsha hadi barabarani ndiyo vyanzo vikubwa viwili vya tatizo hili.

Gwajima anahusikaje?

Pamoja na kutoa ahadi lukuki za kupeleka watu ulaya, kununua boti za uvuvi, Mchungaji Josephat Gwajima aliahidi kutatua tatizo hili sugu kwa wakazi wa Basihaya. Yeye ndiye mbunge wa eneo hili.

Miaka inakimbia, siku zinayoyoma. Gwajima haonekani.

Adha hii inazidi kuwa kubwa kila siku. Ni hadi watu hawa wafe kwa magonjwa ya mlipuko ndiyo wakumbukwe? Kwanini maoni na maombi yao hayasikilizwi? Lengo la Gwajima kusema uongo kuwa atashughulia kero hii lilikuwa ni lipi? Ufanisi wa bandari ya Bagamoyo utakuwaje kama sehemu ya barabara inayounganisha sehemu hii ina hali mbaya kiasi hiki?

Askofu Gwajima, tekeleza ahadi yako.
WAJINGA NDIO WALIWAO KANISA LAKE TU NI LA MABATI MPAKA LEO HAMKUJIULIZA LEO NDIO ATAHANGAIKA NA NYINYI?
 
Tegeta inaingiaje katika kujaza maji Basihaya?.

Tatizo kubwa la kujaa maji lilitokana na barabara ya Bagamoyo kukosa karavati kubwa za kuvusha maji yanayotoka mlima wa Wazo hill.
Niliwahi kuishi Msikitini jirani na Diwani Maji Safi ,mganga,mvua ikinyesha Ngoma ikishukatoka Wazo ilikuwa ni balaa.
 
Nasikia yeye huwa anaanza kuyafuta matatizo katika ulimwengu wa kiroho....mpeni muda🐒
 
Usitegemee lolote la maana toka kwa mkono wa baunsa
 
Hata mgogoro wa ardhi Mbopo hajaweza kusimamia haki itendeke mwenye kustahili arejeshewe eneo lake.

Yani watu walikuwa na high expectations lakini matumaini naona yanapotea.

Ni kanakwamba anafurahishwa na dhuluma kitu ambacho sitaki kuamini .
High expectations? huna akili kabisa
 
Hata mgogoro wa ardhi Mbopo hajaweza kusimamia haki itendeke mwenye kustahili arejeshewe eneo lake.

Yani watu walikuwa na high expectations lakini matumaini naona yanapotea.

Ni kanakwamba anafurahishwa na dhuluma kitu ambacho sitaki kuamini .
Pole mkuu. Mgogoro hauwezi kutatuliwa na wanasiasa. Wewe nenda mahakamani. Ni mbopo ipi hii?
 
Back
Top Bottom