Habari njema kwa nchi, gesi nyingine ya Helium yagunduliwa Bonde la Ziwa Nyasa. Tanzania kuwa muuzaji kinara Duniani

Hawezi gundua mwingine afu mkagawana sawa ,tunachokipata ndio stahiki zetu'.

Ukitaka kikubwa weka teknolojia,staff na mtaji ugundue mwenyewe
Uko sahihi wenzetu pesa wawekezazo sio.cha mtoto sisi hatuwezi pesa zinazohitajika mara ingine kwa utafiti tu zaweza kula bajeti ya miaka mitano ya serikali yote

Na pia zaweza wekezwa hizo.pesa mwisho wa siku ukagunduo huo.mradi hauna maana yoyote pesa za wananchi zote zikaishia utafiti tu
 
Kwan habar njema ya gesi ya kwanza iko wapi, mbona gunduzi zinafanyika nyingi tu tatizo sijajua liko wapi
 
Conc:Kuna wizi mkubwa umefanywa kwenye shirika la Tanesco kwa muda mrefu.Kuna watu wamekuwa Marais wa Tanzania lakin wanawaza kuiba pesa ili ziwasaidie wajukuu.Juzi bilion 350 zimelipwa kampuni ya Symbion .Lakin ipo siku Mungu atawapa pigo kuu.
Sasa hii Ni kesi nyingine mkuu Ila hili swala wahusika wanatakiwa kujibia.
 
Binafsi napendekeza Kama kampuni inakuja kufanya Utafiti Basi Serikali ikubali kuweka mtaji wake ili kitakachopatikana kiweze kugawiwa vizuri.
 
Kabla ya kutuletea porojo za gesi ya Helium, kwanza tuambieni kama taifa tumepata faida gani kutokana na gesi ya Mtwara?
 
Tanzania ukichukua bandari,madini na utalii tu unaweza kuifanya nchi kula MTU alipwe mshahara-tatizo viongozi wetu upstair kama zero,uzalendo zero wote wamehaa rushwa na kujinufaisha wenyewe.
Ukirudi kwa sisi Wananchi ndio matahira na mazezeta kabisa,wacha twende hivyo hivyo labda baada ya miaka 200 ijayo vizazi vyetu vitaikomboa Nchi-ambapo rasimali Nazi zitakuwa zimeisha.

Sisi tuna bahati Nyerere alikuwa na akilini akaziacha kwa ajili yetu,sasa rasilimali alizo acha Nyerere akitegemea labda kizazi chetu kitakuja kuzibadilisha kumbe ndio janga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…