President Elect
JF-Expert Member
- Aug 9, 2011
- 693
- 212
Mamlaka ya VETA inatoa elimu kwa wahitimu wa kidato cha nne (Form iv leavers) hata kama wamepata Divisheni 0! Pia VETA imetoa ithibati kwa vyuo mbalimbali nchini kutoa mafunzo ya aina hiyo kwa wahitimu wote wa kidato cha nne. Unapojiunga VETA, unahitimu Level 3 na kupata cheti kinachotambuliwa na vyuo vilivyosajiliwa NACTE. Hivyo, vijana kazeni buti, jiungeni VETA mpate elimu bora na kusonga mbele taratibu hadi chuo kikuu!