Habari Njema: TRC wanapanga kuweka injini za Diesel kuimarisha huduma

Habari Njema: TRC wanapanga kuweka injini za Diesel kuimarisha huduma

Joined
Apr 5, 2024
Posts
81
Reaction score
117
1734072499918.png

Habari wanajamvi,
Natumaini mmeamka salama na wenye afya tele. Ijumaa hii na iwe mbaraka kwako.

Jumatano mbili zilizopita nilitoka dar-es-salaam kuja Moro. Sasa, siku kabla treni iliniacha. Nilichelewa kwa dakika mbili (treni ilipaswa kuondoka saa 10 kamili. Nlifika 9.57, nkakuta milango ya treni ishafungwa). Nikalazimika kukata treni ya siku inayofuata.

Jumatano nkafika saa moja kabla, nkaketi kwenye siti yangu. Safari.

Tulipofika Ruvu, mtangazaji akatwambia kuwa tungebakia hapo kwa "dakika kadhaa" kwa sababu ya tatizo la ufundi. Nkajua hazitazidi 30, kwa maana nlishampigia mke wangu aniandalie chakula nnachokipenda cha ugali, mboga fulani hivi na kachumbari ilopikwa yenye nyanya nyingi.

Bwana wee. Nusu saa ikageuka kuwa saa zima, masaa 2,3,4... Tulitoka saa nane asubuhi.

Habari Njema
Nilisoma ripoti njema leo kuwa TRC washaagiza injini za diesel. Kwa mujibu wa gazeti la "The Guardian", injini hizi zinatarajiwa kusaidia wakati ambapo kuna changamoto ya umeme, ili wananchi mambo yao yasikwame.

Akizungumza jijini Dar-es-Salaam, meneja mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa, alidokeza kuwa kuna mkandarasi kutoka ulaya ambaye tayari anafanyia kazi injini hizo. Hii ni baada ya Bw. Masanja kuwahakikishia wananchi kuwa mfumo wa umeme wa SGR ni tofauti na mkonga wa taifa.

Faraja inayokuja ni kwamba gharama za injini hizo zipo tayari kwenye bajeti ya shirika hilo (kwa hiyo tutegemee kuwa utekelezwaji utakuwa wa haraka).

Ifahamike kuwa mfumo wa treni za SGR inaruhusu utumiaji wa mafuta ya diesel na umeme pia. (Hybrid engine).

isitoshe, shirika hilo lipo mbioni kuwezesha engine ambazo zina battery zinazotunza chaji ili kusaidia endapo umeme utakuwa na hitilafu.

Kuimarisha Usalama
Imebainika kuwa kuna watu fulani ambao wamekwisha kukamatwa kwa wizi wa mali za shirika (pamoja na kwamba hatujui kuwa gharama ya vifaa vilivyoibiwa havijulikani).

TRC wameweka CCTV katika maeneo yenye usalama mdogo, na wanazidi kufanya hivyo hadi watakapofunika njia nzima kutoka Dar hadi Dodoma.

Chanzo: The Guardian, December 12, 2024.
 
View attachment 3175562
Habari wanajamvi,
Natumaini mmeamka salama na wenye afya tele. Ijumaa hii na iwe mbaraka kwako.

Jumatano mbili zilizopita nilitoka dar-es-salaam kuja Moro. Sasa, siku kabla treni iliniacha. Nilichelewa kwa dakika mbili (treni ilipaswa kuondoka saa 10 kamili. Nlifika 9.57, nkakuta milango ya treni ishafungwa). Nikalazimika kukata treni ya siku inayofuata.

Jumatano nkafika saa moja kabla, nkaketi kwenye siti yangu. Safari.

Tulipofika Ruvu, mtangazaji akatwambia kuwa tungebakia hapo kwa "dakika kadhaa" kwa sababu ya tatizo la ufundi. Nkajua hazitazidi 30, kwa maana nlishampigia mke wangu aniandalie chakula nnachokipenda cha ugali, mboga fulani hivi na kachumbari ilopikwa yenye nyanya nyingi.

Bwana wee. Nusu saa ikageuka kuwa saa zima, masaa 2,3,4... Tulitoka saa nane asubuhi.

Habari Njema
Nilisoma ripoti njema leo kuwa TRC washaagiza injini za diesel. Kwa mujibu wa gazeti la "The Guardian", injini hizi zinatarajiwa kusaidia wakati ambapo kuna changamoto ya umeme, ili wananchi mambo yao yasikwame.

Akizungumza jijini Dar-es-Salaam, meneja mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa, alidokeza kuwa kuna mkandarasi kutoka ulaya ambaye tayari anafanyia kazi injini hizo. Hii ni baada ya Bw. Masanja kuwahakikishia wananchi kuwa mfumo wa umeme wa SGR ni tofauti na mkonga wa taifa.

Faraja inayokuja ni kwamba gharama za injini hizo zipo tayari kwenye bajeti ya shirika hilo (kwa hiyo tutegemee kuwa utekelezwaji utakuwa wa haraka).

Ifahamike kuwa mfumo wa treni za SGR inaruhusu utumiaji wa mafuta ya diesel na umeme pia. (Hybrid engine).

isitoshe, shirika hilo lipo mbioni kuwezesha engine ambazo zina battery zinazotunza chaji ili kusaidia endapo umeme utakuwa na hitilafu.

Kuimarisha Usalama
Imebainika kuwa kuna watu fulani ambao wamekwisha kukamatwa kwa wizi wa mali za shirika (pamoja na kwamba hatujui kuwa gharama ya vifaa vilivyoibiwa havijulikani).

TRC wameweka CCTV katika maeneo yenye usalama mdogo, na wanazidi kufanya hivyo hadi watakapofunika njia nzima kutoka Dar hadi Dodoma.

Chanzo: The Guardian, December 12, 2024.
Ndoto zimeanza kuzima taratibu taratibu
 
Yaani kutoka gari Moshi la umeme Hadi kuwa guta la mafuta ya diesel.awamu ya mama kilakitu hajakamikisha chochote
 
  • Kicheko
Reactions: EEX
Dizeli?
Ifue umeme labda ndani kwa ndani Kama zamani ila gusi Iwe hii mchongoko
 
Itungwe adhabu kali ambayo itaamuru anayehujumu miundo mbinu ya train anyongwe au kufungwa maisha!.... utaleta u serious na discipline kwenye utunzaji wa miundo mbinu yetu ya SGR na ya miradi mingine!!
 
Hapo kwenye betri ni uongo,wangezungumzia tu diesel engine ingetosha

Kulala porin kupo pale pale hata zikija hzo engine
 
Wizi mwingine bana...kwanini wasiweke matanga kama ya kwenye ngalawa kwenye vichwa cya treni tujue moja...
 
Wala hatushangai. Wabongo bado hatujafikia ile hatua ya kuonekana smart upstairs kama ilivyo kwa wenzetu ngozi nyeupe.
 
Haya yote hawakujua toka awali, walishindwa nini kuagiza vichwa vyenye betri ya kuhifadhi umeme, na mbona yule kadogosa alisema hata umeme ukikatika sio kesi.
Kwakuwa nchi hii ni ya KIPUUZI hawatowajibishwa.
 
Akizungumza jijini Dar-es-Salaam, meneja mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa, alidokeza kuwa kuna mkandarasi kutoka ulaya ambaye tayari anafanyia kazi injini hizo. Hii ni baada ya Bw. Masanja kuwahakikishia wananchi kuwa mfumo wa umeme wa SGR ni tofauti na mkonga wa taifa.
Kinachoshindikana kwenye umeme ni kitu gani?
Mbona kwa wenzetu hatusikii habari hizo iweje kwetu tu?
Kwanini wasitatue hilo tatizo la umeme permanently wao wanatengeneza fursa za procurement kwa lengo la 10%?
 
View attachment 3175562
Habari wanajamvi,
Natumaini mmeamka salama na wenye afya tele. Ijumaa hii na iwe mbaraka kwako.

Jumatano mbili zilizopita nilitoka dar-es-salaam kuja Moro. Sasa, siku kabla treni iliniacha. Nilichelewa kwa dakika mbili (treni ilipaswa kuondoka saa 10 kamili. Nlifika 9.57, nkakuta milango ya treni ishafungwa). Nikalazimika kukata treni ya siku inayofuata.

Jumatano nkafika saa moja kabla, nkaketi kwenye siti yangu. Safari.

Tulipofika Ruvu, mtangazaji akatwambia kuwa tungebakia hapo kwa "dakika kadhaa" kwa sababu ya tatizo la ufundi. Nkajua hazitazidi 30, kwa maana nlishampigia mke wangu aniandalie chakula nnachokipenda cha ugali, mboga fulani hivi na kachumbari ilopikwa yenye nyanya nyingi.

Bwana wee. Nusu saa ikageuka kuwa saa zima, masaa 2,3,4... Tulitoka saa nane asubuhi.

Habari Njema
Nilisoma ripoti njema leo kuwa TRC washaagiza injini za diesel. Kwa mujibu wa gazeti la "The Guardian", injini hizi zinatarajiwa kusaidia wakati ambapo kuna changamoto ya umeme, ili wananchi mambo yao yasikwame.

Akizungumza jijini Dar-es-Salaam, meneja mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa, alidokeza kuwa kuna mkandarasi kutoka ulaya ambaye tayari anafanyia kazi injini hizo. Hii ni baada ya Bw. Masanja kuwahakikishia wananchi kuwa mfumo wa umeme wa SGR ni tofauti na mkonga wa taifa.

Faraja inayokuja ni kwamba gharama za injini hizo zipo tayari kwenye bajeti ya shirika hilo (kwa hiyo tutegemee kuwa utekelezwaji utakuwa wa haraka).

Ifahamike kuwa mfumo wa treni za SGR inaruhusu utumiaji wa mafuta ya diesel na umeme pia. (Hybrid engine).

isitoshe, shirika hilo lipo mbioni kuwezesha engine ambazo zina battery zinazotunza chaji ili kusaidia endapo umeme utakuwa na hitilafu.

Kuimarisha Usalama
Imebainika kuwa kuna watu fulani ambao wamekwisha kukamatwa kwa wizi wa mali za shirika (pamoja na kwamba hatujui kuwa gharama ya vifaa vilivyoibiwa havijulikani).

TRC wameweka CCTV katika maeneo yenye usalama mdogo, na wanazidi kufanya hivyo hadi watakapofunika njia nzima kutoka Dar hadi Dodoma.

Chanzo: The Guardian, December 12, 2024.
Dizeli ni kujirudisha nyuma tu…. Labda inakuja kufanya shunting na boost kwenye zole end route like bandari
 
Kinachoshindikana kwenye umeme ni kitu gani?
Mbona kwa wenzetu hatusikii habari hizo iweje kwetu tu?
Kwanini wasitatue hilo tatizo la umeme permanently wao wanatengeneza fursa za procurement kwa lengo la 10%?
I think trc wanakosea
 
I think trc wanakosea
Kuna jambo wanalifanya kujinufaisha wao binafsi, kama siyo 10% kwenye diesel basi wanatengeneza another big procurement ili wajinufaishe
 
Back
Top Bottom