Habib Kyombo apewe nafasi zaidi kucheza hapo Simba

Habib Kyombo apewe nafasi zaidi kucheza hapo Simba

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Katika tathmini yangu ya Habib Kyombo, namuona ni mchezaji mzuri sana anayestahili kupewa nafasi zaidi.

Sitaongelea mikimbio yake wala mbwembwe zingine, ni mchezaji anayeonekana ana IQ nzuri ya soka halafu ni mpambanaji.

Changamoto kubwa ya Simba pale mbele ni kasi ndogo, Okrah akitaka kuwakimbiza, akigawa mpira tu wenzake wanapunguza kasi na kurudisha mipira nyuma. Kyombo anaweza kwenda na kasi hiyo pale mbele.

Pia ufupi wa safu ya mbele nalo ni tatizo. Mipira mingi ya juu, asilimia kubwa Simba wanapoteza. Kyombo pekee pale mbele anaweza kupambania hii mipira.
 
Kwanza niwe muwaza kabisa kuwa sihafurahishwa na haya matokeo, tumecheza vizuri ila siwezi kujivunia sare mbele ya team isiyokuwa na malengo.

Israh Mwenda ameonyesha kukua kimpira na kama atalata muda wa kucheza zaidi, basi hatukuwa na wasiwasi juu ya mbadala wa Kapombe tena. Uongozi utafute mzawa wa kumsaidia Zimbwe pia.

Kyombo akipewa muda atakuja kuwa hatari sana, ni swala la kupewa muda tu kama jinsi ambavyo Israh kapewa, yani badala ya kuanza na Sakho ni bora tuwe tunaanza na Kyombo ili Sakho asugue benchi mpaka pale atakapojua kuwa yeye si mkubwa kama anavyodhani.

Tutafute mshambuliaji mwingine wa maana pale mbele atakaesaidiana na Phiri ili tuzitumie vizuri nafasi ambazo tumekuwa tukizitengeneza.

Hii mentality ya uchoyo inataka kukomaa sana na hili lipo sawa kwa Sakho, Banda na Okhra, itafutwe namna sahihi ya kuwashauri hawa jamaa, ni wachezaji wazuri ila wamejaa ubinafsi sana.


Vinginevyo team imekuwa vizuri sana kwa maoni yangu, na nampongeza sana Mgunda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza niwe muwaza kabisa kuwa sihafurahishwa na haya matokeo, tumecheza vizuri ila siwezi kujivunia sare mbele ya team isiyokuwa na malengo.

Israh Mwenda ameonyesha kukua kimpira na kama atalata muda wa kucheza zaidi, basi hatukuwa na wasiwasi juu ya mbadala wa Kapombe tena. Uongozi utafute mzawa wa kumsaidia Zimbwe pia.

Kyombo akipewa muda atakuja kuwa hatari sana, ni swala la kupewa muda tu kama jinsi ambavyo Israh kapewa, yani badala ya kuanza na Sakho ni bora tuwe tunaanza na Kyombo ili Sakho asugue benchi mpaka pale atakapojua kuwa yeye si mkubwa kama anavyodhani.

Tutafute mshambuliaji mwingine wa maana pale mbele atakaesaidiana na Phiri ili tuzitumie vizuri nafasi ambazo tumekuwa tukizitengeneza.

Hii mentality ya uchoyo inataka kukomaa sana na hili lipo sawa kwa Sakho, Banda na Okhra, itafutwe namna sahihi ya kuwashauri hawa jamaa, ni wachezaji wazuri ila wamejaa ubinafsi sana.


Vinginevyo team imekuwa vizuri sana kwa maoni yangu, na nampongeza sana Mgunda.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kweli kabisa Mgunda ameleta kujiamini kwa Simba. Leo Nabi imebidi afanye sub ya mshambuliaji na kuleta kiungo mkabaji Hapo ndio ujie Mgunda ni tactitian mzuri.
 
Back
Top Bottom