Hadhi ya Ubalozi ya Dkt. Slaa ilikuwa mzigo mkubwa kwake, hakupewa kwa maamuzi ya Mwenyenzi Mungu bali kwa maamuzi ya wanadamu. Sasa yupo huru

Hadhi ya Ubalozi ya Dkt. Slaa ilikuwa mzigo mkubwa kwake, hakupewa kwa maamuzi ya Mwenyenzi Mungu bali kwa maamuzi ya wanadamu. Sasa yupo huru

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Kama Dkt. Slaa amevuliwa hadhi ya ubalozi kwa kupigania rasilimali naamini yupo kwenye mwisho mwema wa maisha yake hapa Duniani. Kwamba ameanza kwa kupigania haki na amezeeka akiwa mtetezi wa haki; alianza kwa kuhubiri uzalendo na amezeeka akipigania haki.

Waliomvua Ubalozi ipo siku watasimama nakuhojiwa na watamtaja kwa wema na siyo ubaya kwa sababu naamini wanajua wazi kwamba kilichomvua ubalozi siyo kashfa ya ufisadi bali ni nguvu kubwa aliyonayo yakumtukuza Mwenyenzi kutumia ukweli na kuwa wazi pale ambapo anaona na kwa maarifa aliyopewa na Mwenyenzi Mungu kwamba hiki siyo sawa.

Hakuna balozi nchi hii ambaye amewahi kusimama kutetea haki; wote wapo kimya. Maana yake Dr. Slaa kuondolewa hadhi ya ubalozi ni kumwondoa kwa wasiotetea nchi na kumrejesha kwa watetezi wa nchi.

Kwa wapenda haki wanapaswa kushangilia kwamba Dkt. Slaa amekabidhi cheo alichopewa kwa kurubuniwa na ambacho hakupewa kwa sababu Mungu amepanga bali alipewa na wanadamu. Cheo kile kilikuwa ni mzigo kwake, sasa rasmi amekitua na yupo tayari kuzeeka akiwa hana madaraka yenye doa.
 
Ana matatizo, alianza kuvuliwa upadri na kanisa
Kanisani kazingua

Ccm akazingua

Chadema akazingua

kwa Mke kazingua

kwa Kimada kazinguliwa Yeye

Ubalozi kazinguliwa


Huyu Jamaa kwa usaliti ana PhD, hata ule Mgomo wake wa kutokula akiwa mahabusu aliusaliti akaanza kula tena

na sasa na hadhi wa ubalozi pia wanampora

Mzee Mwenzangu kapaisha penalt dakika ya 89 na yupo nyuma kwa goli mbili
 
Aruke ruke vyema

akihamasisha ghasia hilo halina mswalie Mtume

tunataka Wajukuu wa Slaa waishi kwa amani na Usalama nchini kama alivyoishi yeye hadi kuzeeka bila ya kujua mbu na kunguni wa kambi za wakimbizi wanaumaje?
Mkuu madaraka uliyonayo leo kuwatesa Watanzania yanaweza kubadirika kabla hata hujafa. Twende polepole. Tulisilewe sana na Madaraka.
 
Mkuu madaraka uliyonayo leo kuwatesa Watanzania yanaweza kubadirika kabla hata hujafa. Twende polepole. Tulisilewe sana na Madaraka.
Nataka watoto na wajukuu zangu waishi kwny Nchi ya amani kama niliyoishi mimi na wazeeke kama nilivozeeka mimi bila ya kujua turubai la kambi za Wakimbizi linafananaje bila ya kujalisha utaandika nini au utatunga story gani kuhalalisha uchochezi wa ghasia nchini
 
Wilbroad Slaa balozi wa wanaopinga matumizi mabaya ya rasilimali za Tanganyika.
 
nataka watoto na wajukuu zangu waishi kwny Nchi ya amani kama niliyoishi mimi na wazeeke kama nilivozeeka mimi bila ya kujua turubai la kambi za Wakimbizi linafananaje bila ya kujalisha utaandika nini au utatunga story gani kuhalalisha uchochezi wa ghasia nchini
Wewe ni mmoja wa Greater thinker nilifikiri Tanzania. Una madini, unajua historia ya taifa hili. Upo serikalini.

Usijishushe. Usibweteke, Unajua exactly Dr Slaa anasimamia maslahi yako, watoto wako, wajukuu wako.

Hawezi kufanya fujo yoyote 74 years old man.
 
Watesi wake wamepigwa na kitu kizito baada ya kusikia akisema SIPO TAYARI KUNYAMAZISHWA KWA KUHONGWA"

Dr. Slaa ana ukorofi na ubishi flan ambao kama huna pumzi unaweza kumrushia ngumi.........ana maudhi flan yakisomi
 
Nataka watoto na wajukuu zangu waishi kwny Nchi ya amani kama niliyoishi mimi na wazeeke kama nilivozeeka mimi bila ya kujua turubai la kambi za Wakimbizi linafananaje bila ya kujalisha utaandika nini au utatunga story gani kuhalalisha uchochezi wa ghasia nchini
Watoto na wajukuu zako maisha watakayoishi yatategemea jinsi gani ulisimama ukiwa na uwezo was kuhoji, unavyojikomba kutetea uuzaji wa rasilimali siku wananchi wakiamua hao watu wataadhibiwa kwa dhambi ulizofanya.
 
Wewe ni mmoja wa Greater thinker nilifikiri Tanzania. Una madini, unajua historia ya taifa hili. Upo serikalini.

Usijishushe. Usibweteke, Unajua exactly Dr Slaa anasimamia maslahi yako, watoto wako, wajukuu wako.

Hawezi kufanya fujo yoyote 74 years old man.
Mzee Slaa namfahamu tangu 1995 na ninazifahamu sana Siasa zake na Wengi wenye mawazo huru wanamjua!

nakupa mfano mmoja tu

Slaa alipigania sana Katiba Mpya wakati wa Jakaya hadi kwa njia za kuchochea ghasia

alipoingia John Magufuli Mzee Slaa akasema Katiba mpya sio Muhimu, cha muhimu ni maji, Umeme na barabara

Alipoingia Samia Suluhu Hassan akaondolewa Ubalozini akaja na hoja za Katiba Mpya tena

hapo Wewe una uhuru wa kuamini anapigania Katiba mpya na mimi nina uhuru wa kuamini Katiba mpya ni kisingizio cha kubeba wenye average mind

Wewe endelea kuamini anapigania Bandari nami niruhusu niamini anapigania agenda yake na wenzie kwa kisingizio cha Bandari


Nikumbushe hata jambo moja alilopinga utawala wa JPM au utawala wa JPM haukuwa na jambo lolote la kukosolewa? hata Tundu Lissu alivyopigwa Risasi alisema kupigwa Risasi ni jambo la kawaida na ni michezo ya ndani ya Chadema.

Mwanasiasa kupigwa Risasi ni jambo la kawaida Tanzania?

hata Wewe naamini unaijua agenda inayomsukuma Slaa ila pengine mna share agenda ndio maana unajaribu kuzuga zuga na kuzunguka


kuwa na agenda binafsi ni jambo moja lakini kuchochea ghasia na vurugu Nchin hilo ni la wote na kama ingekuwa vurugu anazochochea zingeishia kuathiri familia yake na watu wake pekee ningepuuza kama si kupotezea lakini najua Mimi na watoto, wajukuu na Watanzania wema wengi hawana mbadala wa amani na ndio sababu hata awe nani akichochea ghasia tutashawishi Serikali imshughulikie nguvu zote hata kama ni za kuazima potelea mbali
 
Mzee Slaa namfahamu tangu 1995 na ninazifahamu sana Siasa zake na Wengi wenye mawazo huru wanamjua!

nakupa mfano mmoja tu

Slaa alipigania sana Katiba Mpya wakati wa Jakaya hadi kwa njia za kuchochea ghasia

alipoingia John Magufuli Mzee Slaa akasema Katiba mpya sio Muhimu, cha muhimu ni maji, Umeme na barabara

Alipoingia Samia Suluhu Hassan akaondolewa Ubalozini akaja na hoja za Katiba Mpya tena

hapo Wewe una uhuru wa kuamini anapigania Katiba mpya na mimi nina uhuru wa kuamini Katiba mpya ni kisingizio cha kubeba wenye average mind

Wewe endelea kuamini anapigania Bandari nami niruhusu niamini anapigania agenda yake na wenzie kwa kisingizio cha Bandari


Nikumbushe hata jambo moja alilopinga utawala wa JPM au utawala wa JPM haukuwa na jambo lolote la kukosolewa? hata Tundu Lissu alivyopigwa Risasi alisema kupigwa Risasi ni jambo la kawaida na ni michezo ya ndani ya Chadema.

Mwanasiasa kupigwa Risasi ni jambo la kawaida Tanzania?

hata Wewe naamini unaijua agenda inayomsukuma Slaa ila pengine mna share agenda ndio maana unajaribu kuzuga zuga na kuzunguka
Mkuu Pohamba, Dr Slaa ananasimamilia
maslahi ya Taifa kama wewe. Tofouti zenu ni itikadi.
 
Aruke ruke vyema

akihamasisha ghasia hilo halina mswalie Mtume

tunataka Wajukuu wa Slaa waishi kwa amani na Usalama nchini kama alivyoishi yeye hadi kuzeeka bila ya kujua mbu na kunguni wa kambi za wakimbizi wanaumaje?
Mkubwa hatishiwi nyau.
 
Watoto na wajukuu zako maisha watakayoishi yatategemea jinsi gani ulisimama ukiwa na uwezo was kuhoji, unavyojikomba kutetea uuzaji wa rasilimali siku wananchi wakiamua hao watu wataadhibiwa kwa dhambi ulizofanya.
alipokuwa anasoma ule Msemo wa Fainali uzeeni alidhani lazima uwe mchezaji ?

wenzie tulipokuwa tunajenga familia zenye maadili na misingi ili tuje kuzeeka vyema yeye alijenga heshima kwny viuno vya makahaba …akidhani hatozeeka
 
Aruke ruke vyema

akihamasisha ghasia hilo halina mswalie Mtume

tunataka Wajukuu wa Slaa waishi kwa amani na Usalama nchini kama alivyoishi yeye hadi kuzeeka bila ya kujua mbu na kunguni wa kambi za wakimbizi wanaumaje?
Dp world haitakiwi , kesho Kanisani tunasomewa waraka na kuelezwa namna CCM inavyoumiza wananchi

Ni vita rasmi kati ya Kanisa la MITUME na CCM

Sent from my CPH2217 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom