Heparin
JF-Expert Member
- Sep 24, 2021
- 242
- 1,141
Rais wa 47 wa Marekani, Donald Trump, ameendelea kuonesha msimamo mkali kuhusu suala la wahamiaji. Katika sera zake, amesisitiza kuimarisha usalama wa mipaka, ikiwemo ujenzi wa ukuta mpakani na Mexico, pamoja na kuimarisha sheria za uhamiaji ili kupunguza wahamiaji wasio na vibali halali. Trump pia amependekeza sera za kuwaondoa wahamiaji haramu nchini na kubana vigezo vya kupata uraia kwa wahamiaji.
Hata hivyo, sera zake zimepokelewa kwa mitazamo tofauti: wafuasi wake wakiona juhudi hizo kama njia ya kulinda maslahi ya Marekani, huku wakosoaji wakizitaja kuwa za kibaguzi na zisizofuata haki za binadamu.
Katika mwendelezo wa sakata hili, nyaraka ya idara ya Uhamiaji ya Novemba 24, 2024 imeonekana mtandaoni ikiwa na orodha ya watu 1,445,549 wenye amri ya kuondoka nchini humo, huku watanzania wakiwa 301 kati yao.
Tutegemee kuona idadi hii ikiongezeka zaidi?
Hata hivyo, sera zake zimepokelewa kwa mitazamo tofauti: wafuasi wake wakiona juhudi hizo kama njia ya kulinda maslahi ya Marekani, huku wakosoaji wakizitaja kuwa za kibaguzi na zisizofuata haki za binadamu.
Katika mwendelezo wa sakata hili, nyaraka ya idara ya Uhamiaji ya Novemba 24, 2024 imeonekana mtandaoni ikiwa na orodha ya watu 1,445,549 wenye amri ya kuondoka nchini humo, huku watanzania wakiwa 301 kati yao.
Tutegemee kuona idadi hii ikiongezeka zaidi?