Hadi sasa tumekopa Trillion 8, nashauri tupunguze kasi

Hadi sasa tumekopa Trillion 8, nashauri tupunguze kasi

Moja ya vitu ambavyo watu wengi wanapuuzia ni hili suala la mikopo kwa nchi yetu.

Lakini hawajui kuwa mikopo hii ndio inayofanya miradi ya Maendeleo. Watu wanafurahia miradi Ila hawajui pesa inatoka wapi.

Utawala wa awamu ya 5 ulikopa na taarifa zilitolewa kila mwezi pale BOT lakini hakuna aliyejali, Leo tunakuja kuelezwa Deni lilipofikia watu wanakuwa wakali.

Hivyo ni vyema sasa tukawa tunakumbushana hali ya Deni linavyoendelea ili baadae tusije kusema hatukujua.

Kutokea April hadi November, Deni limeongezeka kwa Trillion 8
Hivyo kwa miezi 7 Tumekopa Trillion 8 ni wastani wa zaidi ya Trillion 1 kwa mwezi.
Nashauri speed hii ipungue kidogo.

Mama aajikite zaidi na kuongeza makusanyo maana kwa sasa watu hawatumii sana mashine za EFD, ni kama wameambia wafanye wanachotaka.

View attachment 2043640View attachment 2043641
Kwanza Kukopa hakujawahi kuwa tatizo ikiwa uwezo wa kulipa upo na mikopo kuwekezwa kwenye productive sectors.Pili kuongezeka kwa deni hakutokani tuu na mikopo mipya bali madeni ya nyuma yaliyoiva na kuongezeka kwa riba ya mikopo.

Hata hivyo kama deni limeongezeka ni sawa kwa sababu Nchi ina sera za mikopo kwa kila mwaka.Kwa bajeti hii serikali ilipanga Kukopa til.10 hasa kutoka vyanzo vya nje.
 
CCM watu wa fix sana, wanasema uchumi unakua, tunajenga miradi kwa pesa zetu wenyewe - kumbe wanatoka usiku wanakwenda kukopa kwa mabeberu .

Sasa matokeo yake ndiyo haya kila mtanzania anadaiwa laki 6 na deni bado linaongezeka uchao.
Ni kweli kabisa
 
Kwanza Kukopa hakujawahi kuwa tatizo ikiwa uwezo wa kulipa upo na mikopo kuwekezwa kwenye productive sectors.Pili kuongezeka kwa deni hakutokani tuu na mikopo mipya bali madeni ya nyuma yaliyoiva na kuongezeka kwa riba ya mikopo.

Hata hivyo kama deni limeongezeka ni sawa kwa sababu Nchi ina sera za mikopo kwa kila mwaka.Kwa bajeti hii serikali ilipanga Kukopa til.10 hasa kutoka vyanzo vya nje.
Mimi nimeshauri tu speed ipungue kidogo
 
Tumekopa na nani ? Sema mmekopa au wamekopa kwa (ingawa ni kwa kisingizio cha niaba kwa wananchi ) lakini hata hao wananchi hawana habari hivyo let's make it clear..., wamekopa au kama mpo nao mmekopa...., Mimi simo na hii ibaki kama kumbukumbu kwa vizazi vijavyo (mimi sikuwepo kwenye mikopo yenu)
 
Tumekopa na nani ? Sema mmekopa au wamekopa kwa (ingawa ni kwa kisingizio cha niaba kwa wananchi ) lakini hata hao wananchi hawana habari hivyo let's make it clear..., wamekopa au kama mpo nao mmekopa...., Mimi simo na hii ibaki kama kumbukumbu kwa vizazi vijavyo (mimi sikuwepo kwenye mikopo yenu)
Kwenye kukopa awatushirikishi bali kwenye ulipaji
 
Mimi nimeshauri tu speed ipungue kidogo
Mkuu speed kupungua itategeana na uchumi kukua Ili kupata vyanzo vipya vya mapato kutokana na biashara na uwekezaji.

As for me nashauri wajikite kwenye mikopo ya masharti nafuu na ya mda mrefu maana mkuu bila mikopo mzigo wa Kodi utakuwa mkubwa kwa wananchi.
 
Utalia sana tu kwa sababu umekubali nchi kuendeshwa bila Bunge.Haya unayoyasema yalipaswa kusemwa na kukemewa na Bunge.

Ulipaswa upambane nchi iwe na Bunge kwanza na siyo kuja kulialia kwenye matokeo ya nchi kuendeshwa bila Bunge.

Tatizo kubwa la Mtanzania ni upunguani.The worst is yet to come!
Sasa ulitaka yeye peke yake ndio apige kelele za kulitaka bunge?
We ni hatua gani uliyo chukua, na wapi ulipo fikia katika kulitaka bunge?

Watanzania mukishiba tu hamuchagui cha kuongea.
 
Sasa ulitaka yeye peke yake ndio apige kelele za kulitaka bunge?
Hujanielewa.Point yangu ni kwamba huwezi kurukia kusolve secondary problem ambayo imesababishwa na primary problem bila kusolve kwanza primary problem.

Alichofanya mtoa uzi ni kujaribu kutatua secondary problem ambayo iko linked na primary problem ambayo haikuwahi kutatuliwa kitu ambacho ni kupoteza muda kusolve secondary problem.
We ni hatua gani uliyo chukua, na wapi ulipo fikia katika kulitaka bunge?
Kazi yangu mimi ni kutoa elimu kwa uma kama nilivyofanya leo.Katika kutatua tatizo lolote lile msingi ni elimu na mimi nimejikita hapo.
Watanzania mukishiba tu hamuchagui cha kuongea.
Huwezi kunipangia cha kuongea.
 
Mmekopa na nani?

Sisi maskini hizo fedha hazijawahi kutufikia hasa ukizingatia huduma za kijamii tunazilipia kila mahala.

Waliokopa ni hao hao viongozi na familia zao kwani wanafaidika wao.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Kuna wabunge kama nape wanasubiri mama amalize muda wake waanze kulaumu. Mbaya zaidi fedha nyingi za mikopo zinaenda zanzibar
 
Back
Top Bottom