CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,781
- 6,139
- Thread starter
- #121
KESI YA MZEE MNYOKA 27
Mzee Mnyoka aliwahi ofisini kesho yake mapema sana akiwa na lile daftari alilichanganya na mafaili mengine ya pale ofisini,
Kisha mtendaji alipofika alimuagiza kutafuta vijana ambao wangefanya usafi pale ofisini na kutoa kila kitu nje,
"Nataka tufanye usafi na kutoa mafaili yote na yale ambayo hayafai tuyachome Moto"
Mzee Mnyoka alimuambia mtendaji,
"We Mzee Basi unajiona umefika, umetaka Sana iyo nafasi ila baadae utajilaumu Sana"
Mtendaji aliongea,
"Sikiliza Bwana Mdogo hebu uliza historia yangu hapa kijijini kabla hujaongea utumbo wako"
Alisema Mzee Mnyoka huku akianza kutoa meza nje,
Mtendaji hakuwa na namna akatafuta vijana na kuanza kufanya usafi ,
Walitoa vitu vyote nje Kisha wakafagia na kudeki,
Mzee Mnyoka sasa alikua bize akipekua Nyaraka moja baada ya nyingine na mwishowe akamuita mtendaji,.
"Hivi daftari la kahawa sio hili kweli?"
Alisema Mzee Mnyoka akimuonyesha mtendaji,
"Dah Ni lenyewe aisee Asante Mungu"
Aliongea mtendaji huku macho yakimtoka kwa furaha,
Yeye mwenyewe alikua amekalia kuti kavu kutokana na kupotea kwa daftari Hilo,
Hatimaye baada ya muda habari zilisambaa kuwa daftari limepatikana, Mzee Mnyoka sasa aliwaambia wananchi kuwa malipo yatafanyika kesho kutwa,
"Kuna watu wasio waadilifu walijaribu kuficha hili daftari ili wadhulumu pesa, lakini tunashukuru limepatikana!"
Mzee Mnyoka aliongea huku wenzake wakimshangilia,
Mwenyekiti aliyefururushwa alijisikia vibaya Sana na aliamua kwenda kumuona katibu tarafa Mzee Mkude ili waone namna ya kumkomesha Mzee Mnyoka
*********"""
Tito hakwenda Bungeni siku hiyo, badala yake, alibaki hotelini akiwaza,
Alimuelewa vyema Bwana Shida, na kutokana na mapato aliyokua akipata pale mgodini milioni 500 isingekuwa tatizo kwa mwezi,
Hata hivyo alielewa kuwa Shija baadae atataka kitu kingine
"Once a cheater , always a cheater"
Alikuwa akiwaza,
Alimtumia naibu wake ujumbe kuwa anajisikia mafua mafua na kichwa kinauma, hivyo aendelee kumuwakilisha kwenye kipindi Cha maswali na Majibu, halafu jioni atafika kwenye kikao Cha jioni ,
"Nimfanyeje huyu Mwanaharamu?"
Tito aliendelea kuwaza,
Asingeweza kumueleza Bwana Johnson kuhusu Hilo kwani angemuona Kama mzembe mtu aliyezembea,
Na kingine kilichomtia wasi wasi, Ni namna gani Bwana Shija alijua hizi taarifa na je Ni Nani na nani wanajua hizi taarifa?
Aliamua Bora amueleze mwenzake Majimbi,
Alitoa Simu yake ya kazi ambayo ilikua kwa ajili ya mambo yake ya Siri tu,
Kutokana na mazingira ya asubuhi hakuweza kujua askofu atakua mazingira gani hivyo alimtumia meseji Kwanza kwenye Simu yake ya kawaida,
"Askofu Mimi Ni waziri Tito nilikua nahitaji uniombee "
Askofu Majimbi alikua ofisini kwake, akitoa semina ya wanandoa ambao walitegemea kufunga ndoa jumamosi pale kanisani kwake, aliwahudumia Kisha akamwambia Katibu muhtasi wake asiruhusu mtu kwanza Ana maombi Binafsi,
Kisha akabonyeza kidude fulani sehemu ya ukuta ikafunguka akaingia na ikatokea sasa ofisi nyingine ambayo ilikua ya tofauti kabisa,
Alitoa Simu yake ya kazi nae akampigia Tito,
"Tito una nini asubuhi yote hii"
Alianza askofu Majimbi baada ya Simu kupokelewa,
"Kaka Kuna tuko matatizoni aisee"
Alisema Tito Kisha akamsimulia habari zote za waziri mwenzake Bwana Anthony shija,
"ah sasa hapo unakwama wapi jamaa yangu, huyo Ni kumpoteza tu kabla hili Jambo halijafika kwa Raisi"
Alisema Majimbi,
"Unajua kabisa ,yule Ni Waziri unadhani itakua simple kumpoteza bila kuacha alama?"
Aliuliza Tito,
"Sikiliza yeye si anataka millioni 500 kila mwezi?"
Aliuliza Majimbi
"Yeah"
Alijibu Tito,
"Sasa huyo tunaweza kutumia million 200 au 300 pekee kumpoteza huyo mjinga"
Alisema askofu Majimbi,
"Ninashangaa unaogopa eti, tumefanya kazi ngap? Hata kule mgodini tumeua wangapi? Sembuse mtoto mdogo tu huyo"
Alijitapa askofu Majimbi
"Tunamaliza kikao kesho, kwahiyo Mimi nitamjibu kuwa tutampa hizo pesa ila nikija Dar let's finish this son of bitch"
Alimalizia Tito Kisha akazima Simu halafu akachukua Simu yake nyingine,
Akampigia kimada wake mmoja Kisha akampigia dereva amfuate
"Nitakuonyesha kuwa Mimi Ni zaidi yako Shija"
Alijisemea sasa akijifunga taulo na kuelekea bafuni.
*************
"Sikiliza Mzee Mnyoka Hana ujanja mbele yetu, sisi tuliacha tu kumnyoosha kwahiyo tupe siku mbili ngoja amalizie malipo hizi siku mbili halafu siku ya tatu tunampoteza"
Aliongea Mzee Mkude
"Ila yule Mzee Ni mjanja mjanja hivi"
Aliongea mwenyekiti
"Hata Kama sisi Ni wajanja zaidi yake"
Wewe nenda kesho kutwa jioni hatuko nae Tena yule,"
Alisema Mzee Mkude,
Alishamchukia Mzee Mnyoka kabisa,
______ ___________
Mzee Mnyoka alishirikiana na kamati ya wilaya na alifanya malipo kwa wanakijiji na zoezi lilienda kwa weledi kabisa,
Ingawaje hakukuwa na maelewano mazuri na Mtendaji lakini zoezi lilikwenda vizuri,
Wakati Mzee Mnyoka anamalizia kufunga ofisi aliona gari dogo likiwa linajongea maeneo ya ofisini kwakuwa ofisi ilijitenga kidogo Mzee Mnyoka alijua bila Shaka ule Ni ugeni wa Kijiji,
Hivyo alisubiri bila kufunga mlango kwanza,
Gari ilisimama karibu Kisha mmoja wapo akashuka na kumueleza Mzee Mnyoka kuwa anaweza kufunga tu mlango hawana haraka,
Mzee Mnyoka alifunga mlango Kisha akaenda kuwasikiliza,
Wakati anainama alistuka kupigwa na kitu kizito akaanguka chini na kupoteza fahamu,
Kwa haraka jamaa walimuingiza ndani ya gari na kuondoka nae,
Baada ya masaa muda mwingi kupita Mzee Mnyoka alizinduka akiwa amelala sakafuni huku akiwa amefungwa kamba za mikono na miguu...
Mzee Mnyoka aliwahi ofisini kesho yake mapema sana akiwa na lile daftari alilichanganya na mafaili mengine ya pale ofisini,
Kisha mtendaji alipofika alimuagiza kutafuta vijana ambao wangefanya usafi pale ofisini na kutoa kila kitu nje,
"Nataka tufanye usafi na kutoa mafaili yote na yale ambayo hayafai tuyachome Moto"
Mzee Mnyoka alimuambia mtendaji,
"We Mzee Basi unajiona umefika, umetaka Sana iyo nafasi ila baadae utajilaumu Sana"
Mtendaji aliongea,
"Sikiliza Bwana Mdogo hebu uliza historia yangu hapa kijijini kabla hujaongea utumbo wako"
Alisema Mzee Mnyoka huku akianza kutoa meza nje,
Mtendaji hakuwa na namna akatafuta vijana na kuanza kufanya usafi ,
Walitoa vitu vyote nje Kisha wakafagia na kudeki,
Mzee Mnyoka sasa alikua bize akipekua Nyaraka moja baada ya nyingine na mwishowe akamuita mtendaji,.
"Hivi daftari la kahawa sio hili kweli?"
Alisema Mzee Mnyoka akimuonyesha mtendaji,
"Dah Ni lenyewe aisee Asante Mungu"
Aliongea mtendaji huku macho yakimtoka kwa furaha,
Yeye mwenyewe alikua amekalia kuti kavu kutokana na kupotea kwa daftari Hilo,
Hatimaye baada ya muda habari zilisambaa kuwa daftari limepatikana, Mzee Mnyoka sasa aliwaambia wananchi kuwa malipo yatafanyika kesho kutwa,
"Kuna watu wasio waadilifu walijaribu kuficha hili daftari ili wadhulumu pesa, lakini tunashukuru limepatikana!"
Mzee Mnyoka aliongea huku wenzake wakimshangilia,
Mwenyekiti aliyefururushwa alijisikia vibaya Sana na aliamua kwenda kumuona katibu tarafa Mzee Mkude ili waone namna ya kumkomesha Mzee Mnyoka
*********"""
Tito hakwenda Bungeni siku hiyo, badala yake, alibaki hotelini akiwaza,
Alimuelewa vyema Bwana Shida, na kutokana na mapato aliyokua akipata pale mgodini milioni 500 isingekuwa tatizo kwa mwezi,
Hata hivyo alielewa kuwa Shija baadae atataka kitu kingine
"Once a cheater , always a cheater"
Alikuwa akiwaza,
Alimtumia naibu wake ujumbe kuwa anajisikia mafua mafua na kichwa kinauma, hivyo aendelee kumuwakilisha kwenye kipindi Cha maswali na Majibu, halafu jioni atafika kwenye kikao Cha jioni ,
"Nimfanyeje huyu Mwanaharamu?"
Tito aliendelea kuwaza,
Asingeweza kumueleza Bwana Johnson kuhusu Hilo kwani angemuona Kama mzembe mtu aliyezembea,
Na kingine kilichomtia wasi wasi, Ni namna gani Bwana Shija alijua hizi taarifa na je Ni Nani na nani wanajua hizi taarifa?
Aliamua Bora amueleze mwenzake Majimbi,
Alitoa Simu yake ya kazi ambayo ilikua kwa ajili ya mambo yake ya Siri tu,
Kutokana na mazingira ya asubuhi hakuweza kujua askofu atakua mazingira gani hivyo alimtumia meseji Kwanza kwenye Simu yake ya kawaida,
"Askofu Mimi Ni waziri Tito nilikua nahitaji uniombee "
Askofu Majimbi alikua ofisini kwake, akitoa semina ya wanandoa ambao walitegemea kufunga ndoa jumamosi pale kanisani kwake, aliwahudumia Kisha akamwambia Katibu muhtasi wake asiruhusu mtu kwanza Ana maombi Binafsi,
Kisha akabonyeza kidude fulani sehemu ya ukuta ikafunguka akaingia na ikatokea sasa ofisi nyingine ambayo ilikua ya tofauti kabisa,
Alitoa Simu yake ya kazi nae akampigia Tito,
"Tito una nini asubuhi yote hii"
Alianza askofu Majimbi baada ya Simu kupokelewa,
"Kaka Kuna tuko matatizoni aisee"
Alisema Tito Kisha akamsimulia habari zote za waziri mwenzake Bwana Anthony shija,
"ah sasa hapo unakwama wapi jamaa yangu, huyo Ni kumpoteza tu kabla hili Jambo halijafika kwa Raisi"
Alisema Majimbi,
"Unajua kabisa ,yule Ni Waziri unadhani itakua simple kumpoteza bila kuacha alama?"
Aliuliza Tito,
"Sikiliza yeye si anataka millioni 500 kila mwezi?"
Aliuliza Majimbi
"Yeah"
Alijibu Tito,
"Sasa huyo tunaweza kutumia million 200 au 300 pekee kumpoteza huyo mjinga"
Alisema askofu Majimbi,
"Ninashangaa unaogopa eti, tumefanya kazi ngap? Hata kule mgodini tumeua wangapi? Sembuse mtoto mdogo tu huyo"
Alijitapa askofu Majimbi
"Tunamaliza kikao kesho, kwahiyo Mimi nitamjibu kuwa tutampa hizo pesa ila nikija Dar let's finish this son of bitch"
Alimalizia Tito Kisha akazima Simu halafu akachukua Simu yake nyingine,
Akampigia kimada wake mmoja Kisha akampigia dereva amfuate
"Nitakuonyesha kuwa Mimi Ni zaidi yako Shija"
Alijisemea sasa akijifunga taulo na kuelekea bafuni.
*************
"Sikiliza Mzee Mnyoka Hana ujanja mbele yetu, sisi tuliacha tu kumnyoosha kwahiyo tupe siku mbili ngoja amalizie malipo hizi siku mbili halafu siku ya tatu tunampoteza"
Aliongea Mzee Mkude
"Ila yule Mzee Ni mjanja mjanja hivi"
Aliongea mwenyekiti
"Hata Kama sisi Ni wajanja zaidi yake"
Wewe nenda kesho kutwa jioni hatuko nae Tena yule,"
Alisema Mzee Mkude,
Alishamchukia Mzee Mnyoka kabisa,
______ ___________
Mzee Mnyoka alishirikiana na kamati ya wilaya na alifanya malipo kwa wanakijiji na zoezi lilienda kwa weledi kabisa,
Ingawaje hakukuwa na maelewano mazuri na Mtendaji lakini zoezi lilikwenda vizuri,
Wakati Mzee Mnyoka anamalizia kufunga ofisi aliona gari dogo likiwa linajongea maeneo ya ofisini kwakuwa ofisi ilijitenga kidogo Mzee Mnyoka alijua bila Shaka ule Ni ugeni wa Kijiji,
Hivyo alisubiri bila kufunga mlango kwanza,
Gari ilisimama karibu Kisha mmoja wapo akashuka na kumueleza Mzee Mnyoka kuwa anaweza kufunga tu mlango hawana haraka,
Mzee Mnyoka alifunga mlango Kisha akaenda kuwasikiliza,
Wakati anainama alistuka kupigwa na kitu kizito akaanguka chini na kupoteza fahamu,
Kwa haraka jamaa walimuingiza ndani ya gari na kuondoka nae,
Baada ya masaa muda mwingi kupita Mzee Mnyoka alizinduka akiwa amelala sakafuni huku akiwa amefungwa kamba za mikono na miguu...