Hadithi: Kesi ya Mzee Mnyoka

Hadithi: Kesi ya Mzee Mnyoka

KESI YA MZEE MNYOKA 36

Mzee Mnyoka alitoka chumbani kuelekea sebuleni ambapo mgeni wake alikuwepo...

"Kumbe ulisema unaitwa Bwana Nani vile, "

Mzee Mnyoka alianza...

"George , George Paul Mzee wangu"
Alisema George huku akitoa mkono Tena kumpa Mzee Mnyoka....

"Sawa sasa Kuna chumba Cha mdogo wako hapa bila Shaka utavumilia mazingira yake , si unajua Tena vijana"

Alisema Mzee Mnyoka akichukua begi la George na kutoka nae kuelekea chumbani kwa James,

Alifungua Kisha akamkabidhi ufunguo ...


George alitoa begi lake na kuunganisha baadhi ya vifaa vyake muhimu Kisha vingine akavificha sehemu sehemu mpaka usiku alipoitwa kula chakula Cha jioni alirudi kuendelea na mipango yake kwa ajili ya kesho...


*************

Oscar alikuwa sasa Yuko bize popote alipokuwapo Tito Oscar angekuwa pembeni yake,


Baada ya kuwa na ratiba ya waandishi wa habari Tito alipanga kufanya maandalizi ya kuelekea Mgodini ambapo shughuli kubwa zingefanyika kule ikiwemo makabidhiano....

Waliamini kule kungekuwa na usalama wa kutosha,


Siku hii ya leo Bwana Johnson alialikwa kutembelea makao makuu ya Kanisa la uzima wa milele kwa askofu Majimbi


Askofu Majimbi alimpokea mgeni wake huyo na kusema Ni rafiki wa Kanisa lao na amekuwa hata akifadhili baadhi ya huduma za pale kanisani ikiwemo ujenze wa hosteli kwenye chuo Chao Cha Kanisa pamoja na mradi wa maji...


Tofauti na Tito , Askofu Majimbi alishamtembelea zaidi ya Mara tatu Bwana Johnson akiwa uingereza hivyo walifahamiana vyema ..


Baada ya maongezi ya kawaida walihamia "ofisini" ambapo walifanya mazungumzo yao kuhusu biashara zao....

Kikubwa walijadiliana namna ya kutoa mzigo salama nchini Tanzania na kuondoka nao bila kuathiri uhusiano wa nchi hizi mbili...

Majimbi alimuhakikishia kuwa kupitia Tito Mambo yote yatakaa vizuri ..


***************

Bwana Allan nae hakuwa nyuma aliweka kikosi chake Cha watu kumi ili kusaidiana na Oscar endapo Mambo yatakwama

Hapo nyuma alikua na mjadala mzito pamoja na wenzake kuhusu kumuingiza mtu mwingine katika oparesheni hii, wenzake walisema kuwa mtu huyo asingefaa kutokana na umri wake, lakini pia hata mahusiano yake na mtuhumiwa...

Hata hivyo Bwana Allan alisema mtu huyo bado anaweza kufaa Ni Bora wamtumie ashindwe kuliko kuacha kabisa kumtumia,

Ndipo sasa wakaona wampe taarifa Mhusika mwenyewe....


Jambo la ajabu Ni kuwa mpelelezi wao huyo alisema Yuko tayari kufanya kazi hiyo kwa asilimia 100 na yupo tayari kurudi nchini....


Ndipo sasa akafanyiwa mipango yote ya usafiri kurudi nyumbani Tanzania..


Ni suala Hili lilimfanya Bwana Allan kujaribu kufanya uchunguzi wake kwanini binti yule alikubali kufanya kazi Ile kwa urahisi mkubwa

Jioni hii akiwa ofisini kwake alikua akipitia picha mbali mbali kwenye komputa yake,


Ndipo sasa alijikuta akirudia rudia kuangalia hii picha..


Alitabasamu Kisha akatoa Simu yake ya kazi na kumtafuta Oscar....


***************************

George alitoka asubuhi na mapema alifika mpaka mgodini Kinjeki ambapo alijitambulisha Kama mwandishi mwanafunzi kutoka chuo Cha uandishi wa habari Arusha ..


Baada ya kutoa vitambulisho vyake aliruhusiwa kupita na kuonyeshwa Mambo mbali mbali ya mgodini hapo, ..

Alitoa kamera na notebook yake Kisha akachukua maelezo kidogo na kuungana na waandishi wengine waliokua wanaendelea kuingia mgodini...

Ni tukio kubwa la kihistoria nchini Tanzania na hivyo kwa muda mfupi habari za Kinjeki zilikua zinaandikwa Sana....

**************


Baada ya ratiba zote kukamilika sasa Bwana Johnson alikua amemaliza mizunguuko yote na sasa Safari ya kwenda Kinjeki iliwadia .

****************

Bwana Allan alionana na mpelelezi wake huyo aliyewasili siku hiyo kwa ajili ya kuonana nae ...


Bwana Allan alitaka kumuona ili ajihakishe Kama kweli Ni yeye aliamua mwenyewe kuwemo kwenye misheni hii,


Bwana Allan alikumbuka sasa jinsi alivyomshawishi msichana yule alivyokuwa mdogo kabisa pale Saint Rock international School Kenya, mwaka 98 wakati ambapo Bwana Allan alipewa jukumu la kutafuta watoto wa viongozi ambao wangekuwa tayari kuwa wapelelezi baadae, kwa faida ya nchi,


Siku hiyo akiwa Kenya alikua amemfuata mtoto wa waziri mkuu mstaafu ambaye alikua shuleni hapo,


Na baada ya kufika shuleni, na kuuliza habari zake aliambiwa tayari alishahamishwa siku mbili zilizopita kwenda uingereza,

Kwakua lilikuwa Ni Jambo la Siri hakukua na sababu ya kulaumu mtu na ndipo wakati anataka kutoka hapo shuleni akatambulishwa mtoto wa waziri Tito,

Joyce ambaye alikua na miaka 10 wakati huo nae akisoma shuleni hapo,


Ni wakati anaongea nae na kumuuliza masomo anayopenda na kupitia ripoti zake ndipo sasa Bwana Allan akaanza kumuhusudu binti huyo aliyekuwa mahiri katika masomo ya tehama

Na ndipo alifanikiwa kumueleza taratibu na hatimaye alipofikisha miaka 15 serikali ikamchukua moja kwa moja!

Na ndipo sasa kila Mara akawa anapata udhamini wa masomo nje ya nchi , baba yake Mzee Tito kutokana na kuwa mtu wa shughuli nyingi alijua tu mwanae yupo masomoni nje ya nchi akisomea Mambo ya komputa mengine alijua serikali inagharamia,


Bwana Allan alikuwa anawaza yote haya akiegesha Gari yake pembeni mwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere...


Ni wakati muafaka ndipo alipomuona mtu wake akitoka alimpungia mkono na Kisha akamkumbatia..


"Oh my daughter"

Alisema huku akimpokea begi kuelekea kwenye Gari...
Noma na nusu
 
Good, Ingawa kama jina la hadithi linavyojinasibu, ilitakiwa iishie kwa mzee MNYOKA kama MAIN CHARACTER, hatima yake ni nini?, je na yeye alipewa bahasha na nyumba na namba moja??
 
Back
Top Bottom