Hadithi: Mpangaji

MPANGAJI 11

By CK Allan
Esta sasa alishatembelea karibia miradi yote na kuona kila kitu ambacho kinaendelea
siku hiyo usiku walikuwa wanajadiliana namna ya kurudi kwa kasi katika kuhakikisha kisasi kinalipwa ipasavyo
β€œnina wazo Sele”alisema Esta
β€œtutengeneze historia ya Sele Selemani Sele” alianza Esta
β€œsijakuelewa’
β€œSikiliza Sele, kwanza tutengeneze uhuru wako kwanza, uwe huru kutembea popote wakati wowote na saa yoyote, halafu ujikite katika biashara mojawapo ambayo utaichagua uindeleze ukue nayo kabisa na kutambulika duniani kote, halafu ukishajulikana sasa ndio itakuwa rahisi wewe kuongea chochote na kikasikilizwa na Dunia, kuliko ilivyo sasa”
β€œmhh una mpango gani?” aliuliza sele
β€œkwasasa una vitambulisho vyote, lakini huna shule ya msingi wala sekondari wala chuo ulichosoma, nina wazo kwanza tutafute shule ya msingi, baadae Sekondari halafu huko juu tutajua” alisema Esta
β€œbonge la wazo ila kumbuka tunakimbizana na Muda, na inabidi mzee akimaliza tu muda wake kesi iishe, kwasababu kama ujuavyo sasa hivi hakuna mahakama itakubali kupokea kesi yoyote ya mke wa Raisi aliye madarakani, hakuna hata sehemu moja unaweza kufungua kesi” alisema Sele huku akichukua simu yake,
β€œuncle, huna mtu unafahamiana nae pale wizarani au baraza?” alisema baada ya simu kupokelewa
β€œnina kijana pale nilishawahi kufanya nae kazi kipindi Fulani ila naweza kuipata namba yake baada ya nusu saa, vipi?” alisema mr K
β€œbasi fanya mpanga kesho tukutane nae”
Waliweka miadi vizuri nakesho wakakutana na mtu huyo wa baraza na kuweka nae utaratibu
β€˜inawezekana sana kwahiyo umri wa sele inabidi awe amemaliza shule kati ya mwaka 1997-1999 hivi, mnapendekeza awe amemaliza mkoa gani,
β€œhapa dar s salaam” walisema kwa pamoja

β€œokay sasa hii kazi itachukua wiki mbili kwasababu inahitaji umakini tusije kumpa shule ambayo kipindi hicho ilikua hata haipo, kama unavyojua ni kizazi cha google hiki” alisema Yule jamaa aliyeonekana kuwa mtaalamu wa β€œdili” kama hizo
β€œsasa kuhusu cheti cha form four inabidi kutafuta shule ambayo mkuu wake wa shule amefariki, yaani hayupo kabisa hapa duniani! Ili tunapochomeka jina basi mambo yote yatakuwa vizuri kabisa!” alisema Yule jamaa huku akipiga funda la juice
β€œsikia lengo letu sisi tunataka mtu anapotafuta taarifa hizi za mfanyabiashara maarufu Sele basi aweze kuona alisoma wapi hivyo tu, tunakutegemea sana ndugu yetu, si unajua wakati mwingine tunakosa Dili kutokana na Vyeti tuu” alisema Mr K akitabasamu
β€œsikilizeni hapa ndio kwenyewe ndugu zangu, siwezi kuwaangusha sema tu kama mjuavyo kazi hii sifanyi mwenyewe niko na wenzangu kwahiyo sijajua mmejipanga vipi!’ alisema Yule jamaa sasa akiweka miwani yake vizuri
β€œwewe unataka tukupe ngap?” aliuliza Sele ambaye alikua kimya muda wote
β€œkwa primary kikubwa ni matokeo ya mwisho na vyeti vya primary ni rahisi tu, cheti cha form four ndio kidogo kina mlolongo kwasababu inabidi kuonyesha pia matokeo ya form two kwahiyo kuna kamzunguuko kidogo kuwapoza watu hapa na pale n.k, sasa kwasababu najua sisi sote tunatafuta, toeni million 6 hii nimewasaidia sana ndugu zangu” alisema Yule jamaa
β€œna kazi yote inaweza kukamilika kwa lini?’ aliuliza Mr k
β€œhaizidi wiki mbili kama kila kitu kikiwa sawa!”
β€œbasi jioni utapata milioni 4 na ukimaliza kazi tutakupa iliyobaki tunakushuru sana tukiamini mambo yatakaa sawa!”
Waliagana kisha wakaendelea na mazungumzo yao huku Nyuma kati ya Mr K na Sele
β€œ ni wazo zuri sana, baada ya kupata vyeti hivi na kila mtu akijiaminisha Sele ndio Sele, na mheshimiwa atakuwa ameshamaliza muda wake wa kukaa madarakani na sisi tutaibuka pale juu” alisema Mr K akimgeukia Sele
β€œsasa ni biashara gani ambayo unataka kupanda nayo!” aliuliza Mr K
β€œ kwakuwa tayari nilishasomea mambo ya mifumo, tufungue kamupuni ndogo ya mifumo ya ulinzi wa kiteknolojia ambapo tutadeal na kufunga mifumo kwenye majengo, hotel, benk, n.k pamoja na kuuza vifaa vya ulinzi nadhani kwa Tanzania bado hakuna kampuni maalum ya kudeal na vitu hivi” alisema Sele na mr k alikubalina na wazo lake na sasa kampuni ikawa tayari imeanzishwa kwenye makaratasi

Hatimaye baada ya mwezi mmoja kampuni ilifunguliwa na kupata usajili wa awali kampuni illitwa β€œWE4U” ambapo ilihusika na kufunga vifaa vya ulinzi kwenye majengo na vile vile kuuza spea za vifaa vya ulinzi wa kiteknlojia,
kutokana na uhitaji wa vitu hivyo haikuchukua muda mrefu kampuni yake ikaanza kufahamika na kuanza kutumika kufunga vifaa katika majengo mbali mbali. Sasa ungeweza kukuta wakipokea oda nyingi kutoka sehemu tofauti, kama isingekuwa kufunga mifumo basi kuuza vifaa ,
pamoja na kuwa ilikua ni sehemu ya kupandia tu kufikia ndoto zao lakini na Faida kubwa pia Sele aliipata kwani alitanua wigo na kufanya kazi na makampuni mengine ya vifaa ndani na nje ya nchi
kila ambavyo mama Mwajuma alikua akitaka kumtembelea mwanae Esta, walikwepesha na wao wakaamua kumtembelea, hawakutaka kabisa mama Mwajuma ajue maisha halisi ya Sele kabla hawajaweka sawa hivyo baada ya kila kitu kukamilika siku hiyo walitaka kumfanyia mama Mwajuma Saprise sasa
β€œnadhani ni wakati sahihi sasa tumkaribishe mama!” alisema Esta maana kila siku anataka kuona tunapokaa!
β€œhaha ni kweli ni mwaka kasoro sasa nadhani inabidi tufanye hivyo!” alisema Sele huku akimalizia kuvaa viatu vyake,
β€œsikia kuna mchoro mmoja wa benki ya Acb tawi la mwenge naenda kuchukua wanataka tuwafungie cctv camera, nikitoka hapo nitaenda ofisini nitapitia Sokoni pia, wewe mfuate mama si ushazoea sasa hivi kwenye mataa!” alisema Sele akitabasamu
β€œhaha hakuna shida kabisa sasa hivi napiga gia hatari!” alisema Esta kwani tayari nae alikua na gari yake aina ya β€œvitz”
Baada ya Sele kuondoka Esta nae alimalizia kuandaa chakula na kukihifadhi vizuri kisha akamfuata mama mwajuma, kwa muda wa saa 4 asubuhi foleni haikua kubwa sana na masaa mawili tu yalitosha yeye kufika mwananyamala na kisha kuingia vichochoroni mpaka nyumbani kwao kwa zamani, alipaki gari yake nje kisha akaingia ndani na kumkuta mama yake na wapangaji wengine kama kawaida, aliwasalimia na eye akasogea kukaa kwenye mkeka
β€œwe mwanamke nikajua umeshajiandaa jamani, kumbe tunaongea kwenye simu nikajua umeshamaliza!” Esta alianza kulalamika
β€œsasa mimi nikajua utakuja jioni ngoja nijiandae haraka’ alisema mama Mwajuma akinyanyuka na kujiandaa
β€˜haya sasa na hili wigi mpaka tutembee mpaka steni si nitakuwa nimeloa jasho mama Mwajuma mimi!” alisema
β€œmama utembee wapi jamani nimekuja na Gari!” alisema Esta
β€œkha! Gari, wewe umekuja na Gari?” alisema mama Mwajuma sasa huku akitoka mbio nje , ilibidi wapangaji wengine watoke kuchungulia
β€œjamani mke wa Sele, amekuja na gari loh!”
Esta sasa alikua anajizuia kucheka lakini alijikaza na kufungua mlango wa gari
β€œhuu mkanda unafungwa hivi, halafu unavuta hapa!” alisema Esta akimfunga mkanda mama Mwajuma na safari ikaanza
β€œkwahiyo huyo mumeo Sele amekununulia gari na wewe unajua kuendesha gari? Mbona kama niko ndotoni mimi mama Mwajuma!”
β€œmama bhana hujaacha tu vituko vyako” alisema Esta sasa wakiingia kwenye barabara kubwa ya lami

Walifika nyumbani kwa Sele na mama Mwajuma alishikwa na kigugumizi baada ya kuona nyumba nzuri vile ya sele
Alikua na maswali mengi kuliko majibu alikaa pale hadi Sele alipowasili na kuingia ndani ambapo alimsalimia kwa ufupi kisha akaingia chumbani na kubadili nguo na kisha akarudi tena Sebuleni
β€œaah mama Mama karibu sana sisi tupo hapa jamani, mambo yalikua mengi na kazi kila tukisema uje tunajikuta wote tuko bize, sasa tulipopata hii nafasi ndio tukaona uje upaone nyumbani mama” alisema sele baada ya kukaa kwenye Sofa
β€œsasa mwanangu maisha haya mmeyapata lini kwa haraka hivi mwanangu? Eeh, mbona hujawahi kusema unaishi vizuri hivi mpaka watu wakawa wanakudharau sele!” alisema mama mwajuma kama kwa kufoka hivi!
β€œmama Kwakweli namshukuru sana Esta, unajua kipindi kile nilikua nafanya biashara ndogo ndogo za kuuza vifaa vya komputa, sasa nilipokua na mwenzangu huyu kama unavyojua
 
MPANGAJI 12
wenzetu hawa walimu wanakopeshwa basi akaenda huko akachukua mkopo na tukaingiza kwenye biashara zetu basi Mungu akajalia mama!”alisema Sele
β€œooh kwakweli mwanangu hongereni sana kwakweli umetutoa kimaso maso kwakweli” alisema mama Mwajuma
Sele aliingia zake chumbani akiwaacha mama na mwanae hapo ambapo jioni walimsindikiza tena mpaka nyumbani
Sasa mama Mwajuma hakutaka kulala usiku ule aliwakusanya wapangaji wenzake na kuwaelezea huko nyumbani kwa Esta
β€œnakuambia ni Ikulu, ni ikulu!” alisema mama mwajuma akikazia β€œumbea” wake kama ilivyokuwa kawaida yake
----------------------------------------------------------------
BAADA YA MIAKA KADHAA
Uchaguzi nchini Tanzania ulimalizika salama na Mzee Lukas Tuppa akakabidhi kijiti kwa aliyekuwa waziri Mkuu wake Bwana Jeremiah Mdee,
Mara baada ya kustaafu Mzee Tuppa tofauti na watangulizi wake, aliamua kubaki jijini Dar es salaam, tayari Joan na Jesca walishakuwa mawaziri katika serikali yake huku wakitajwa kama mawaziri wadogo zaidi kuwahi kutokea Tanzania, Bwana Tuppa aliongoza kwa miaka 20 , tofauti kabisa na watangulizi wake, tetesi zilikua zilisambaa kuwa mkewe mama Joan ndie aliyekuwa akimlazimisha Mzee kuendelea kubaki madarakani
Alirudi nyumbani kwake Masaki na familia akijinasibu kuwa anaenda kuwa mfugaji wa kuku kumalizia wakati wake wa kuishi hapa duniani pamoja na β€œkucheza na wajukuu” kama viongozi wengi walivyopenda kuongezea hayo maneno wanapohojiwa
Mzee Tuppa alitengana na mkewe Rasmi siku alipogundua alimuua mke mke mwenzake mama Doreen,
Kilichoonekana kwa nje ilikua ni maigizo tu na kamwe hawakuwahi kulala tena chumba kimoja toka siku ile
Kila mmoja alikua na chumba chake au tuseme β€˜nyumba yake” walinzi wake wa karibu walikua wanajua hayo yote lakini wakati walipokuwa wakitoka kwenda kwenye ziara za kikazi Mzee Tuppa na mkewe walikuwa wakishikana mikono na kutabasamu
Mara kadhaa mama Joan alijaribu kumuomba msamaha mume wake huyo lakini mzee Tuppa alikataa kata kata
β€œwewe ni muuaji Janet!, unathubutuje kumuua mama na mtoto kinyama kiasi kile kwa sababu za kijinga kama zile?” alikua anafoka mzee Tupa
β€œwangefanya nini wale eeh? Wangeweza kuzuia mimi kuwa Raisi? Ningekuwa tu! Walishaelewa ona umekatisha ndoto za kijana wangu! Mimi nitamtazama vipi huko kuzimu? Nakuuliza wewe?” Sasa Mr Tuppa alikuwa akikumbuka hayo yote akiwa ameshika picha ya mke wake mama Doreen waliyopiga wakati akiwa mhadhiri pale UDSM
β€œ twende mzee muda wa kipindi” ilikua ni sauti ya mlinzi wake Joshua ambaye sasa alikua akimsindikiza katika Televisheni ya Taifa ambapo kulikua na kipindi maalum cha β€œJIFUNZE KWAKE” ambacho kilikua maalum kuwahoji watu maarufu na kisha kupoke maswali machache kutoka kwa watazamaji mubashara baada ya kuwasili na ukaguzi kufanyanyika sasa mzee Tuppa alivalishwa kifaa maalum cha kukuzia sauti na kisha akaenda kukaa kwenye sofa kubwa iliyokuwa pembeni ya kamera nyingi nyingi
β€œhabari mtazamajij wetu wa Televisheni yako ya taifa kama tulivyokuwa tukikujuza wiki hii nzima kuwa tutakuwa na Raisi mstaafu mheshimiwa Lukas Kaijage Tuppa, basi tayari ameshafika hapa studio tayari kabisa kukuletea mahojiano haya ya masaa mawili mimi ni mtangazaji wako Faraja Walter, na tutarejea baada ya muda mfupi!’
Kipindi hiki kilikua kipindi pendwa sana tayari watu wengi walikua wakifuatilia mahojiano hayo Sele akiwa nyumbani kwake na mke wake nao waliacha kula na kukodoa macho kwenye tv kuhakikisha wanasikia kila neno kutoka kwa mzee
β€œhebu sasa tuambie mheshimiwa unaona tofauti gani kati ya kuwa ofisini na ulivyo sasa nyumbani ukicheza na wajukuu?” aliuliza mtangazaji
β€œtofauti ipo kubwa sana, kwakweli ukiwa Raisi unapangiwa nini ufanye, nini ule, mpaka kitu gani uangalie kwenye Tv , tofauti na sasa hivi naweza kulala muda ninaotaka na hata kuamka pia, lakini pia naweza kula sasa hata vile vyakula ambavyo nisingekula kipindi nikiwa Raisi”
Waliendelea na mahojiano mpaka pale walipomaliza kisha wakaruhusu simu
Simu nyingi zilikua za kawaida na kupongeza mpaka baadae ilipopigwa simu moja hivi ambayo ilibadili kabisa mjadala
β€œmheshimiwa Raisi , kulikua na tetesi kuwa ulikua na mke mdogo ambaye alikua mwalimu pale chuo kikuu cha Dar, na mlijaliwa kuwa na watoto wawili,
nataka kujua kama je ni kweli na je baada ya kifo cha mke wako huyo katika ajali ya moto ulijisikiaje na huyo mtoto mwingine yuko wapi?
β€œtafadhali tutajie tena jina lako na unapiga simu ukiwa wapi?’ Faraja alijaribu kumkatisha Yule jamaa lakini tayari swali lilikua limeshasikika
β€˜basi tuendelee kuuliza maswali halafu mheshimiwa atayajibu kwa pamoja” alisema mtangazaji kwani tayari alishaona uso wa mzee Tuppa ukibadilika
β€œkama muuliza swali nimemsikia vizuri yeye amesema anawajua hao watoto kwahiyo nishauri jeshi la polisi lichukue hatua kwakuwa namba yake hii imeonekana basi ataeleza zaidi niwashi ndugu zangu watanzania tuachane na tetesi na habari za mitandao!” alimaliza mheshimiwa Raisi

β€œwatamkamata huyo mtu” alisema Sele
β€œhuyu mtu ni nani lakini? Amejuaje haya yote?” Aliuliza Esta
β€œsijui kwakweli” alisema sasa tayari alikua ameshaanza kuhisi kuna watu wengi tu wanajua sakata lake β€œngoja tuone kesho wakimkamata nitafanya niwezalo kumuona” aliwaza sele
Ni kweli haikuchukua muda jeshi la polisi lilitangaza kumshikilia kijana huyo mapema sana kesho yake mchana kwa tuhuma za kutunga uongo na kuusambaza kuhusu familia ya Raisi mstaafu
β€œtunataka kutoa sampo kwa kijana huyu ili kukomesha kabisa tabia ya kusingizia na kuchafua watu kwa sababu za kisiasa, tutaanza na huyu na wengine watafuata” alisema polisi Mamboleo
Wakati huo Sele alikua jirani na kituo cha polisi hicho akijaribu kupenya penya ili amuone kijana huyo ni wakati anapaki gari na kusogea ndipo simu yake ikaita aliangalia mpigaji na kuweka simu chap sikioni
β€œbaby niko hapa najitahidi..”
β€œusihangaike mume wangu, wamemuachia, Raisi amemsamehe ameamuru aachiliwe mara moja angalia whatsap nimekutumia clip’ Alisema Esta
Sele alirudi kwenye gari kisha akfungua mlango na kufungua ile video
β€œhatuwezi kumkamata kila mtu anayetunga uongo tutawakamata wangapi? Nimeamua kumsamehe Yule kijana na naomba jeshi la polisi kijana huyo aachiliwe” ilikua ni sauti ya mzee Tupa akiongea
β€œnoo nooo something is wrong!” alijisemea Sele pamoja na muda mrefu aliokuwa nao lakini alijua baba yake amekasirika na sio kweli kuwa kijana huyo amesamehewa bali kuna jambo baya litamkuta, Sele aliendesha agari kusogelea kituo cha polisi na kweli alishuhudia kijana huyo akitoka, alimtazama kijana huyo angalau aone sura yake lakini hakuweza, tayari kulikua na msongamano wa waandishi wa habari na wapiga picha kadhaa hatimaye ilipaki gari ndogo pembeni na akashuka mama mmoja hivi akikimbilia kule ulipokuwa mlango na hatimaye
Baada ya muda mfupi akarudi kwenye gari akiwa na yule kijana, na gari ikaondoka
β€œfuata hiyo gari sele!” alijiambia wakati sasa anawasha gari kuifukuzia walitembea kutoka kituo cha polisi na kutokea barabara ya Shekilango na sasa waliingia kushoto na kufuata barabara ya sinza, halafu walipofika Mugabe wakaingia bara bara ya vumbi kulia, na sasa Sele alitabasamu baada ya kuangalia kwenye kioo cha gari cha kutazamania nyuma,
Naam hakuwa peke yake kulikua na gari nyingine nyuma yake ambayo alihisi nao walikua wakimfuatilia Yule kijana
β€œkumekucha” aliwaza akiendelea kusogea na walipita shule ya Msingi Mugabe, na kutokea kwenye nyumba moja iliyokuwa na geti jeusi baada ya kupiga honi geti likafunguliwa, sele alipaki pembeni na kusogea kwenye duka lililokuwa pembeni na sasa lile gari lililokuwa nyuma yake nao walifika na kupunguza mwendo kidogo kwenya ie nyumba kisha wakapitiliza
β€œnaomba mirinda nyeusi” sele alisema huku akikaa kwenye benchi lilikokuwa pale nje
β€œhivi kumbe Yule dogo anakaa pale eeh” sele alianza maongezi
β€œah Yule dogo bhana kajisababishia msala sana, ujue braza ukweli unaweza kukuua hivi hivi, Yule dogo juzi tu nilikua namwambia aache huo upuuzi wake lakini hakutaka kunielewa, wamemuachia lakini sijui kama wataamuacha yule maana ujue dogo ana siri nyingi sana za baba yake!”
β€œunataka kuniambia na wewe unaamini hizo tetesi?” Sele aliuliza
β€œbroo wewe uko dunia gani, hata mtoto mdogo anajua kabisa Mzee aliua mke na watoto wake ili aupate uraisi nani asiyejua?”
β€œkwani Yule dogo ndio mtoto wa mzee nanilii ah nani Yule alikua …” sele alijifanya sasa kusahahu kidogo
 
Kuhusu kujua mambo ya kisheria nilifuatilia sana
Kipindi kile Cha "kesi ya mbowe" na wenzake
Nilijua sana mambo mengi kupitia ule Uzi!!

Kwahiyo mtakuta episodes za mahakamani utadhani ni kibatala!!

🀣🀣🀣🀣
 
Kuhusu kujua mambo ya kisheria nilifuatilia sana
Kipindi kile Cha "kesi ya mbowe" na wenzake
Nilijua sana mambo mengi kupitia ule Uzi!!

Kwahiyo mtakuta episodes za mahakamani utadhani ni kibatala!!

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kongole sana .
 
Kuhusu kujua mambo ya kisheria nilifuatilia sana
Kipindi kile Cha "kesi ya mbowe" na wenzake
Nilijua sana mambo mengi kupitia ule Uzi!!

Kwahiyo mtakuta episodes za mahakamani utadhani ni kibatala!!

[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Nimecheka jamani ,,hongera kwa kujifunza jambo
 
Naweka kitanda kabisa hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…