Mkuu leo hamna kipande kingine Tulale tu?Ngoja uone mtiti wake kesho[emoji1787][emoji1787]
Mwanangu tufanyie mpango wa hata espode 2 tu tuishi nayo mpaka kesho tafadhar sana kakaNdio mkuu, tukutane Tena asubuhi,
Bando ni kipengele mkuu
WellMPANGAJI 05
Sasa Esta alitafuta namna ya kuanza mazungumzo yake yale aliyoyaita rasmi,
Aliweka komputa pembeni na kisha akamsogelea Sele pale kwenye sofa na kumshika bega,
“Sele, naomba kwanza nisamehe sana ila sina namna nyingine isipokuwa hii” alisema akianza
Alimsimulia Sele kuhusu historia yake ya maisha, elimu yake na mapenzi na kisha akamsimulia kuhusu mama Mwajuma na hadithi nyingine ambazo hakuona umuhimu wa kuzificha
“ mama Alikuja kutafuta maisha Dar miaka wakati huo aliniacha na bibi, kwa uhalisi mama alipata ujauzito akiwa darasa la saba, na mara baada ya kujifungua na mimi kuacha kunyonya ndio akaja huku Dar, alikuwa kila mwaka anakuja na kuniletea nguo na pesa za matumizi na hatimaye nikamaliza darasa la saba na kuchaguliwa kidato cha kwanza, wakati nikiwa likizo mwezi wa sita nakumbuka mama alikuja kijijini kwetu Moro goro akiwa na mtoto mwingine mdogo akasema anaitwa Mwajuma na ndio mama akatutambulisha rasmi kuwa ameolewa na mwanaume muislamu na kuamua kubadili na yeye” alisema Esta,
“kuna kitu nakiona kwako Sele, nilivyokuja nilisikia habari nyingi sana kuhusu wewe ndio maana hata siku ile nikasubiri kuonana na wewe , nimeona unahitaji msaada Sele ,na mimi ndio wa kukupa huo msaada Sele, tafadhali kama ulikua huna imani na mimi naomba sana uniamini, naomba sana Sele, naahidi kukutunzia siri yako yote kabisa utakayoniambia kuna kitu naona kabisa hakiko sawa Sele na mbaya zaidi hata wewe mwenyewe huna furaha na maisha haya unayoishi!” alisema Esta sasa na machozi yakaanza kumtoka
“tafadhali niambie sele, wewe ni nani hasa, umetokea wapi na familia yako iko wapi, sele, tafadhali nimeangalia mpaka usajili laini yako umeandika “sele sele sele” yaani majina yote matatu ni sele tu,” esta alizidi kumbananisha Sele
Sasa Sele machozi yalikua yanamelenga lenga tayari kabisa kutoka
Lakini alijikaza kiume na kuuondoa mkono wa Esta,
“kwanini nikueleze hayo yote Esta kwanini?” aling’aka sele
“ah kwasababu, ah kwasababu.. nimekupenda Sele” alimalizia Esta huku akisimama na kuweka mikono mdomoni kama mtu aliyesema jamboa ambalo hakutakiwa kusema,
Sele alipigwa na mshangao sasa , ndio hata yeye alishikwa na bumbuwazi na kujikuta sasa anatamani kuona kama yuko ndotoni ili aamke kutoka usingizini
“Esta wewe ni mwanamke pekee ambaye umeyabadili maisha yangu na nakupenda pia, lakini kuhusu historia Yangu, mimi ni nani nisingependa kukueleza Esta, kwakuwa inaniumiza mimi mwenyewe na itakuumiza wewe pia lakini kukueleza wewe ni hatari zaidi ya unavyofikiri wewe” alisema Sele,
“kumbukuka nimekuambia kila kitu Sele, na naapa kabisa Sele, nitatunza siri yako yoyote ile kuanzia leo hii na hata kama itakuwa ngumu kiasi gani basi siwezi kuachana na wewe Sele”
“Esta unajua wewe ni mzuri, una macho mazuri sana, lakini baada ya kusikia hayo yote hutakuwa hivi ulivyo Esta, tafadhali usitake kujua haya!’ alisema Sele kwa kumsihi sana Esta
“nakuahidi Sele usiponiambia basi hata Lindi siwezi kwenda Tena” alisema Esta
“Esta sikiliza kwa umakini, na naomba sana unisikilize nitakuambia kila kitu ila kwa masharti” alisema Sele
‘masharti yoyote Sele niko tayari” alisema Esta akikaa vizuri sasa kusikiliza hadithi ya Sele
“okay, kwanza hutamwambia mtu yoyote kwa namna yoyote ile, kwasababu yoyote ile utaendelea kuniita Sele , na hutanipigia simu popote mpaka mimi nianze kunitafuta, na hivyo hivyo kwenye meseji” alisema Sele
“hakuna shida Sele” nitaweza yote hayo
“okay sasa Esta mimi jina langu halisi ni GiFT Lukas Tupa”
Alisema akiweka kituo huku akimtazama vizuri Esta, ambaye hakuonyesha kustuka”
“narudia naitwa Gift Lukas Tupa esta” alisema tena akimwangalia Esta machoni na sasa Esta akili zake zilielewa haraka
“whaaat! Unasemaje Sele? Unataka kusema baba yako ni Mheshimiwa Lukas Tupa, the President?” aliuliza esta huku akiweka mikono mdomoni Sele alitingisha kichwa tu kukubali
“bado hadithi haijaanza Esta nilikuambia mapema !” alisema Sele sasa akimhurumia Esta
“Sele noo ,”
“okay sasa kwa mzee tuko wawili mimi na dada Yangu Doreen ambaye yeye yuko Italy ameolewa huko na alibadili kabisa na uraia, kwa ufupi iko hivi mzee Tupa alikua Mhadhiri mwandamizi pale udsm kabla hajateuliwa kuwa mbunge na Raisi aliyepita kama unakumbuka
Sasa mama yangu alikua ndio kwanza assistant lecturer pale kitengo cha sheria huko na huko akawa na mahusiano na mzee Tupa na ndio akazaliwa dada Doreen, na mimi ndio nikafuatia, mzee tupa alipoteuliwa kuwa Mbunge na hatimaye kuwa waziri wa Fedha akatupangia nyumba maeneo ya mikocheni, na mama alituambia wazi wazi kuwa mzee alikua na mke wake mkubwa na yeye alikua mke wake mdogo! Dada Doreen yeye alienda Kenya kusoma na mama akakataa mimi kwenda nje ya nchi kusoma na badala yake akasema nisome hapa hapa Tz ili niwe nae karibu” Sele aliendelea na story yake kisha akanywa maji kidogo na kuendelea
“mzee akikua anakuja kwa mwezi mara mbili, na kila siku aliyokuwa anakuja basi angeniletea zawadi mbali mbali, kiuhalisia tulikua na maisha mazuri sana”
“hata hivyo hatuweza kukutana na ndugu zetu wengine wa mama mkubwa na hatukupewa habari zao kabisa, nakumbuka kuna siku mama alisema kuwa mahusiano yao bado hajawa rasmi na endapo tungetambulishwa basi mzee angeweza kukosa kazi, na uteuzi wake ukaishia hapo kwakua ni kashfa ambayo ingeweza kumkosesha kibarua chake, unajua tena waziri haipendezi kuwa na mchepuko!” alisema Sele,
Maisha yaliendelea vizuri tu na dada Doreen akamaliza shule kule na mimi nikamaliza sekondari na nikaendelea na kidato cha tano na kumaliza vizuri kabisa kidato cha sita na kufaulu vizuri kwenye vyeti vyangu Jina langu ni Gift Jonathan Charles ambalo ndilo jina la babu yake mama, na hii ilifanyika makusudi ili k uficha ubini wangu, kumlinda mzee,
Hakukua na tatizo lolote kwani wakati ambao nilitaka kuongea na baba niliongea nae na hakuna kitu ambacho ningekosa
Nakumbuka siku hiyo nilikua najiandaa kwenda chuo kikuu majira ya saa moja usiku nilishangaa kuona gari la baba nje, nilistuka kidogo kwakuwa ilikua ni siku chache tu zimepita alikua pale,
“labda amekuja kuniaga” nilisema huku nikishuka ngazi haraka kutoka nje kumpokea baba,
Uso wake haukuwa na furaha kama siku zote lakini alionyesha bashasha,
“mama yako yupo?” alisema haraka akiingia ndani
“ndio yupo chumbani kwake” nilisema nikirudi zangu “juu” kupanga mizigo yangu kwani nilikuwa miongoni mwa wanafunzi watano tuliopata ufadhili wa masomo kusoma nje ya nchi
“mzee alipitiliza ndani huku walinzi wake wakibaki nje, namkumbuka mmoja aliitwa Joshua “
Baada ya masaa mawili hivi niliona baba akiondoka zake na mimi niliamua kushuka chini kumfuata mama na kumkuta Sebuleni analia
Sikujua hata pa kuanzia lakini mama aliniita na kuniambia yaliyojiri
“baba yako anateuliwa kuwa Raisi kwenye chama chake mwaka ujao, kutokana na ushindani uliopo kwenye Chama ni yeye na Waziri mkuu wa sasa ndio wanapewa nafasi kubwa sana hata hivyo mheshimiwa Raisi anataka kumuachia yeye kijiti”
Alisema mama
“sasa mbona unalia?” nilimuuliza mama
“iko hivi, mimi ni mchepuko tu mwanangu, mimi ni mchepukooo!” alisema kwa hasira akitupa glass ya maji sakafuni
“ah sijaelewa mama”
“iko hivi mwanangu Gift kuanzia sasa hivi baba yakao hatakuja tena hapa! Kwa ufupi hutakutana nae popote sio wewe tu lakini hata mimi pia” alisema akilia
“mama kwanini Lakini?” nilisema nikiwa sielewi
“mwanangu wewe ni msomi sasa unajua, Raisi hatakiwi kuwa na makando kando, kuanzia keshoa anaanza kufuatiliwa hata akienda chooni, anayetakiwa kuwa nae bega kwa bega ni mke wake wa ndoa” alisema mama
“naelewa mama, sasa bado nashindwa kuona kwanini unalia!’ nilisema
“leo amekuja kutupa tahadhari kuwa mkewe amejua tunapoishi hivyo tuwe makini na ikibidi tuhame kabisa hata nje ya nchi mapaka uchaguzi upite” alisema mama kwa uchungu
Sasa nilielewa uzito wa lile jambo, na sikuona namna ya kufanya, mama yangu hakuwa na ndugu tuliyeweza kumfahamu zaidi alituambia tu kuhusu baba yake ambaye alifariki alipokuwa mdogo na mama yake alifariki wakati akijifungua, na akaenda kulelewa katika kituo cha watoto Yatima cha Samaritan Morogoro ambapo alisomeshwa na wamisionari mpaka alipofika UDSM na kukutana na baba yangu,
Hata hivyo kwa macho na kwa vitendo baba yangu alinipenda sana na alimpenda mama yangu pia alishamfungulia miradi mikubwa sana na kumuachia pesa nyingi kabla ya uchaguzi na alimuahidi kuwa nae bega kwa bega
Wakati naondoka pale sebuleni mama alinipa barua ambayo ilikua imetoka kwa mzee
Daaah jmn mbna mie sizion lakini mama watotoshida tag hazifiki babe,story humu sasa hivi zipo nyingi balaa
hadithi njoo utamu koleaMPANGAJI 12
wenzetu hawa walimu wanakopeshwa basi akaenda huko akachukua mkopo na tukaingiza kwenye biashara zetu basi Mungu akajalia mama!”alisema Sele
“ooh kwakweli mwanangu hongereni sana kwakweli umetutoa kimaso maso kwakweli” alisema mama Mwajuma
Sele aliingia zake chumbani akiwaacha mama na mwanae hapo ambapo jioni walimsindikiza tena mpaka nyumbani
Sasa mama Mwajuma hakutaka kulala usiku ule aliwakusanya wapangaji wenzake na kuwaelezea huko nyumbani kwa Esta
“nakuambia ni Ikulu, ni ikulu!” alisema mama mwajuma akikazia “umbea” wake kama ilivyokuwa kawaida yake
----------------------------------------------------------------
BAADA YA MIAKA KADHAA
Uchaguzi nchini Tanzania ulimalizika salama na Mzee Lukas Tuppa akakabidhi kijiti kwa aliyekuwa waziri Mkuu wake Bwana Jeremiah Mdee,
Mara baada ya kustaafu Mzee Tuppa tofauti na watangulizi wake, aliamua kubaki jijini Dar es salaam, tayari Joan na Jesca walishakuwa mawaziri katika serikali yake huku wakitajwa kama mawaziri wadogo zaidi kuwahi kutokea Tanzania, Bwana Tuppa aliongoza kwa miaka 20 , tofauti kabisa na watangulizi wake, tetesi zilikua zilisambaa kuwa mkewe mama Joan ndie aliyekuwa akimlazimisha Mzee kuendelea kubaki madarakani
Alirudi nyumbani kwake Masaki na familia akijinasibu kuwa anaenda kuwa mfugaji wa kuku kumalizia wakati wake wa kuishi hapa duniani pamoja na “kucheza na wajukuu” kama viongozi wengi walivyopenda kuongezea hayo maneno wanapohojiwa
Mzee Tuppa alitengana na mkewe Rasmi siku alipogundua alimuua mke mke mwenzake mama Doreen,
Kilichoonekana kwa nje ilikua ni maigizo tu na kamwe hawakuwahi kulala tena chumba kimoja toka siku ile
Kila mmoja alikua na chumba chake au tuseme ‘nyumba yake” walinzi wake wa karibu walikua wanajua hayo yote lakini wakati walipokuwa wakitoka kwenda kwenye ziara za kikazi Mzee Tuppa na mkewe walikuwa wakishikana mikono na kutabasamu
Mara kadhaa mama Joan alijaribu kumuomba msamaha mume wake huyo lakini mzee Tuppa alikataa kata kata
“wewe ni muuaji Janet!, unathubutuje kumuua mama na mtoto kinyama kiasi kile kwa sababu za kijinga kama zile?” alikua anafoka mzee Tupa
“wangefanya nini wale eeh? Wangeweza kuzuia mimi kuwa Raisi? Ningekuwa tu! Walishaelewa ona umekatisha ndoto za kijana wangu! Mimi nitamtazama vipi huko kuzimu? Nakuuliza wewe?” Sasa Mr Tuppa alikuwa akikumbuka hayo yote akiwa ameshika picha ya mke wake mama Doreen waliyopiga wakati akiwa mhadhiri pale UDSM
“ twende mzee muda wa kipindi” ilikua ni sauti ya mlinzi wake Joshua ambaye sasa alikua akimsindikiza katika Televisheni ya Taifa ambapo kulikua na kipindi maalum cha “JIFUNZE KWAKE” ambacho kilikua maalum kuwahoji watu maarufu na kisha kupoke maswali machache kutoka kwa watazamaji mubashara baada ya kuwasili na ukaguzi kufanyanyika sasa mzee Tuppa alivalishwa kifaa maalum cha kukuzia sauti na kisha akaenda kukaa kwenye sofa kubwa iliyokuwa pembeni ya kamera nyingi nyingi
“habari mtazamajij wetu wa Televisheni yako ya taifa kama tulivyokuwa tukikujuza wiki hii nzima kuwa tutakuwa na Raisi mstaafu mheshimiwa Lukas Kaijage Tuppa, basi tayari ameshafika hapa studio tayari kabisa kukuletea mahojiano haya ya masaa mawili mimi ni mtangazaji wako Faraja Walter, na tutarejea baada ya muda mfupi!’
Kipindi hiki kilikua kipindi pendwa sana tayari watu wengi walikua wakifuatilia mahojiano hayo Sele akiwa nyumbani kwake na mke wake nao waliacha kula na kukodoa macho kwenye tv kuhakikisha wanasikia kila neno kutoka kwa mzee
“hebu sasa tuambie mheshimiwa unaona tofauti gani kati ya kuwa ofisini na ulivyo sasa nyumbani ukicheza na wajukuu?” aliuliza mtangazaji
“tofauti ipo kubwa sana, kwakweli ukiwa Raisi unapangiwa nini ufanye, nini ule, mpaka kitu gani uangalie kwenye Tv , tofauti na sasa hivi naweza kulala muda ninaotaka na hata kuamka pia, lakini pia naweza kula sasa hata vile vyakula ambavyo nisingekula kipindi nikiwa Raisi”
Waliendelea na mahojiano mpaka pale walipomaliza kisha wakaruhusu simu
Simu nyingi zilikua za kawaida na kupongeza mpaka baadae ilipopigwa simu moja hivi ambayo ilibadili kabisa mjadala
“mheshimiwa Raisi , kulikua na tetesi kuwa ulikua na mke mdogo ambaye alikua mwalimu pale chuo kikuu cha Dar, na mlijaliwa kuwa na watoto wawili,
nataka kujua kama je ni kweli na je baada ya kifo cha mke wako huyo katika ajali ya moto ulijisikiaje na huyo mtoto mwingine yuko wapi?
“tafadhali tutajie tena jina lako na unapiga simu ukiwa wapi?’ Faraja alijaribu kumkatisha Yule jamaa lakini tayari swali lilikua limeshasikika
‘basi tuendelee kuuliza maswali halafu mheshimiwa atayajibu kwa pamoja” alisema mtangazaji kwani tayari alishaona uso wa mzee Tuppa ukibadilika
“kama muuliza swali nimemsikia vizuri yeye amesema anawajua hao watoto kwahiyo nishauri jeshi la polisi lichukue hatua kwakuwa namba yake hii imeonekana basi ataeleza zaidi niwashi ndugu zangu watanzania tuachane na tetesi na habari za mitandao!” alimaliza mheshimiwa Raisi
“watamkamata huyo mtu” alisema Sele
“huyu mtu ni nani lakini? Amejuaje haya yote?” Aliuliza Esta
“sijui kwakweli” alisema sasa tayari alikua ameshaanza kuhisi kuna watu wengi tu wanajua sakata lake “ngoja tuone kesho wakimkamata nitafanya niwezalo kumuona” aliwaza sele
Ni kweli haikuchukua muda jeshi la polisi lilitangaza kumshikilia kijana huyo mapema sana kesho yake mchana kwa tuhuma za kutunga uongo na kuusambaza kuhusu familia ya Raisi mstaafu
“tunataka kutoa sampo kwa kijana huyu ili kukomesha kabisa tabia ya kusingizia na kuchafua watu kwa sababu za kisiasa, tutaanza na huyu na wengine watafuata” alisema polisi Mamboleo
Wakati huo Sele alikua jirani na kituo cha polisi hicho akijaribu kupenya penya ili amuone kijana huyo ni wakati anapaki gari na kusogea ndipo simu yake ikaita aliangalia mpigaji na kuweka simu chap sikioni
“baby niko hapa najitahidi..”
“usihangaike mume wangu, wamemuachia, Raisi amemsamehe ameamuru aachiliwe mara moja angalia whatsap nimekutumia clip’ Alisema Esta
Sele alirudi kwenye gari kisha akfungua mlango na kufungua ile video
“hatuwezi kumkamata kila mtu anayetunga uongo tutawakamata wangapi? Nimeamua kumsamehe Yule kijana na naomba jeshi la polisi kijana huyo aachiliwe” ilikua ni sauti ya mzee Tupa akiongea
“noo nooo something is wrong!” alijisemea Sele pamoja na muda mrefu aliokuwa nao lakini alijua baba yake amekasirika na sio kweli kuwa kijana huyo amesamehewa bali kuna jambo baya litamkuta, Sele aliendesha agari kusogelea kituo cha polisi na kweli alishuhudia kijana huyo akitoka, alimtazama kijana huyo angalau aone sura yake lakini hakuweza, tayari kulikua na msongamano wa waandishi wa habari na wapiga picha kadhaa hatimaye ilipaki gari ndogo pembeni na akashuka mama mmoja hivi akikimbilia kule ulipokuwa mlango na hatimaye
Baada ya muda mfupi akarudi kwenye gari akiwa na yule kijana, na gari ikaondoka
“fuata hiyo gari sele!” alijiambia wakati sasa anawasha gari kuifukuzia walitembea kutoka kituo cha polisi na kutokea barabara ya Shekilango na sasa waliingia kushoto na kufuata barabara ya sinza, halafu walipofika Mugabe wakaingia bara bara ya vumbi kulia, na sasa Sele alitabasamu baada ya kuangalia kwenye kioo cha gari cha kutazamania nyuma,
Naam hakuwa peke yake kulikua na gari nyingine nyuma yake ambayo alihisi nao walikua wakimfuatilia Yule kijana
“kumekucha” aliwaza akiendelea kusogea na walipita shule ya Msingi Mugabe, na kutokea kwenye nyumba moja iliyokuwa na geti jeusi baada ya kupiga honi geti likafunguliwa, sele alipaki pembeni na kusogea kwenye duka lililokuwa pembeni na sasa lile gari lililokuwa nyuma yake nao walifika na kupunguza mwendo kidogo kwenya ie nyumba kisha wakapitiliza
“naomba mirinda nyeusi” sele alisema huku akikaa kwenye benchi lilikokuwa pale nje
“hivi kumbe Yule dogo anakaa pale eeh” sele alianza maongezi
“ah Yule dogo bhana kajisababishia msala sana, ujue braza ukweli unaweza kukuua hivi hivi, Yule dogo juzi tu nilikua namwambia aache huo upuuzi wake lakini hakutaka kunielewa, wamemuachia lakini sijui kama wataamuacha yule maana ujue dogo ana siri nyingi sana za baba yake!”
“unataka kuniambia na wewe unaamini hizo tetesi?” Sele aliuliza
“broo wewe uko dunia gani, hata mtoto mdogo anajua kabisa Mzee aliua mke na watoto wake ili aupate uraisi nani asiyejua?”
“kwani Yule dogo ndio mtoto wa mzee nanilii ah nani Yule alikua …” sele alijifanya sasa kusahahu kidogo
Uniite 😄mdau toka madam Raisi Mzee mnyoka Steve Mollel kanishinda na Petty Magambo kaishia kubadili jina muendelezo hakuna 😄Kitu kipya kimeanza
Analyse
Half american
Watu8
Dr Restart
baby zu
Depal
Antonnia
Kalpana
Lovelovie
Glenn
Mamaya
Binadamu Mtakatifu
leadermoe
Darlin
Lloyd
munroe
mshamba_hachekwi
moneytalk
Dahan
Johnnie Walker
Leejay49
Amehlo
Palina am 4 real
Shunie Numbisa
Bantu Lady charlote
Luv
masai dada
Tayukwa
Kelsea
Antennah
Cee
Litro
Missy Gf
tag sasa hivi hazifiki dear,embu ingia jukwaa la entertained utazionaDaaah jmn mbna mie sizion lakini mama watoto