Hadithi: Mpangaji

Hadithi: Mpangaji

MPANGAJI 05

Sasa Esta alitafuta namna ya kuanza mazungumzo yake yale aliyoyaita rasmi,
Aliweka komputa pembeni na kisha akamsogelea Sele pale kwenye sofa na kumshika bega,
“Sele, naomba kwanza nisamehe sana ila sina namna nyingine isipokuwa hii” alisema akianza
Alimsimulia Sele kuhusu historia yake ya maisha, elimu yake na mapenzi na kisha akamsimulia kuhusu mama Mwajuma na hadithi nyingine ambazo hakuona umuhimu wa kuzificha
“ mama Alikuja kutafuta maisha Dar miaka wakati huo aliniacha na bibi, kwa uhalisi mama alipata ujauzito akiwa darasa la saba, na mara baada ya kujifungua na mimi kuacha kunyonya ndio akaja huku Dar, alikuwa kila mwaka anakuja na kuniletea nguo na pesa za matumizi na hatimaye nikamaliza darasa la saba na kuchaguliwa kidato cha kwanza, wakati nikiwa likizo mwezi wa sita nakumbuka mama alikuja kijijini kwetu Moro goro akiwa na mtoto mwingine mdogo akasema anaitwa Mwajuma na ndio mama akatutambulisha rasmi kuwa ameolewa na mwanaume muislamu na kuamua kubadili na yeye” alisema Esta,
“kuna kitu nakiona kwako Sele, nilivyokuja nilisikia habari nyingi sana kuhusu wewe ndio maana hata siku ile nikasubiri kuonana na wewe , nimeona unahitaji msaada Sele ,na mimi ndio wa kukupa huo msaada Sele, tafadhali kama ulikua huna imani na mimi naomba sana uniamini, naomba sana Sele, naahidi kukutunzia siri yako yote kabisa utakayoniambia kuna kitu naona kabisa hakiko sawa Sele na mbaya zaidi hata wewe mwenyewe huna furaha na maisha haya unayoishi!” alisema Esta sasa na machozi yakaanza kumtoka
“tafadhali niambie sele, wewe ni nani hasa, umetokea wapi na familia yako iko wapi, sele, tafadhali nimeangalia mpaka usajili laini yako umeandika “sele sele sele” yaani majina yote matatu ni sele tu,” esta alizidi kumbananisha Sele
Sasa Sele machozi yalikua yanamelenga lenga tayari kabisa kutoka
Lakini alijikaza kiume na kuuondoa mkono wa Esta,
“kwanini nikueleze hayo yote Esta kwanini?” aling’aka sele
“ah kwasababu, ah kwasababu.. nimekupenda Sele” alimalizia Esta huku akisimama na kuweka mikono mdomoni kama mtu aliyesema jamboa ambalo hakutakiwa kusema,
Sele alipigwa na mshangao sasa , ndio hata yeye alishikwa na bumbuwazi na kujikuta sasa anatamani kuona kama yuko ndotoni ili aamke kutoka usingizini
“Esta wewe ni mwanamke pekee ambaye umeyabadili maisha yangu na nakupenda pia, lakini kuhusu historia Yangu, mimi ni nani nisingependa kukueleza Esta, kwakuwa inaniumiza mimi mwenyewe na itakuumiza wewe pia lakini kukueleza wewe ni hatari zaidi ya unavyofikiri wewe” alisema Sele,
“kumbukuka nimekuambia kila kitu Sele, na naapa kabisa Sele, nitatunza siri yako yoyote ile kuanzia leo hii na hata kama itakuwa ngumu kiasi gani basi siwezi kuachana na wewe Sele”
“Esta unajua wewe ni mzuri, una macho mazuri sana, lakini baada ya kusikia hayo yote hutakuwa hivi ulivyo Esta, tafadhali usitake kujua haya!’ alisema Sele kwa kumsihi sana Esta
“nakuahidi Sele usiponiambia basi hata Lindi siwezi kwenda Tena” alisema Esta
“Esta sikiliza kwa umakini, na naomba sana unisikilize nitakuambia kila kitu ila kwa masharti” alisema Sele
‘masharti yoyote Sele niko tayari” alisema Esta akikaa vizuri sasa kusikiliza hadithi ya Sele
“okay, kwanza hutamwambia mtu yoyote kwa namna yoyote ile, kwasababu yoyote ile utaendelea kuniita Sele , na hutanipigia simu popote mpaka mimi nianze kunitafuta, na hivyo hivyo kwenye meseji” alisema Sele
“hakuna shida Sele” nitaweza yote hayo
“okay sasa Esta mimi jina langu halisi ni GiFT Lukas Tupa”
Alisema akiweka kituo huku akimtazama vizuri Esta, ambaye hakuonyesha kustuka”
“narudia naitwa Gift Lukas Tupa esta” alisema tena akimwangalia Esta machoni na sasa Esta akili zake zilielewa haraka
“whaaat! Unasemaje Sele? Unataka kusema baba yako ni Mheshimiwa Lukas Tupa, the President?” aliuliza esta huku akiweka mikono mdomoni Sele alitingisha kichwa tu kukubali
“bado hadithi haijaanza Esta nilikuambia mapema !” alisema Sele sasa akimhurumia Esta
“Sele noo ,”
“okay sasa kwa mzee tuko wawili mimi na dada Yangu Doreen ambaye yeye yuko Italy ameolewa huko na alibadili kabisa na uraia, kwa ufupi iko hivi mzee Tupa alikua Mhadhiri mwandamizi pale udsm kabla hajateuliwa kuwa mbunge na Raisi aliyepita kama unakumbuka

Sasa mama yangu alikua ndio kwanza assistant lecturer pale kitengo cha sheria huko na huko akawa na mahusiano na mzee Tupa na ndio akazaliwa dada Doreen, na mimi ndio nikafuatia, mzee tupa alipoteuliwa kuwa Mbunge na hatimaye kuwa waziri wa Fedha akatupangia nyumba maeneo ya mikocheni, na mama alituambia wazi wazi kuwa mzee alikua na mke wake mkubwa na yeye alikua mke wake mdogo! Dada Doreen yeye alienda Kenya kusoma na mama akakataa mimi kwenda nje ya nchi kusoma na badala yake akasema nisome hapa hapa Tz ili niwe nae karibu” Sele aliendelea na story yake kisha akanywa maji kidogo na kuendelea
“mzee akikua anakuja kwa mwezi mara mbili, na kila siku aliyokuwa anakuja basi angeniletea zawadi mbali mbali, kiuhalisia tulikua na maisha mazuri sana”
“hata hivyo hatuweza kukutana na ndugu zetu wengine wa mama mkubwa na hatukupewa habari zao kabisa, nakumbuka kuna siku mama alisema kuwa mahusiano yao bado hajawa rasmi na endapo tungetambulishwa basi mzee angeweza kukosa kazi, na uteuzi wake ukaishia hapo kwakua ni kashfa ambayo ingeweza kumkosesha kibarua chake, unajua tena waziri haipendezi kuwa na mchepuko!” alisema Sele,
Maisha yaliendelea vizuri tu na dada Doreen akamaliza shule kule na mimi nikamaliza sekondari na nikaendelea na kidato cha tano na kumaliza vizuri kabisa kidato cha sita na kufaulu vizuri kwenye vyeti vyangu Jina langu ni Gift Jonathan Charles ambalo ndilo jina la babu yake mama, na hii ilifanyika makusudi ili k uficha ubini wangu, kumlinda mzee,
Hakukua na tatizo lolote kwani wakati ambao nilitaka kuongea na baba niliongea nae na hakuna kitu ambacho ningekosa
Nakumbuka siku hiyo nilikua najiandaa kwenda chuo kikuu majira ya saa moja usiku nilishangaa kuona gari la baba nje, nilistuka kidogo kwakuwa ilikua ni siku chache tu zimepita alikua pale,
“labda amekuja kuniaga” nilisema huku nikishuka ngazi haraka kutoka nje kumpokea baba,
Uso wake haukuwa na furaha kama siku zote lakini alionyesha bashasha,
“mama yako yupo?” alisema haraka akiingia ndani
“ndio yupo chumbani kwake” nilisema nikirudi zangu “juu” kupanga mizigo yangu kwani nilikuwa miongoni mwa wanafunzi watano tuliopata ufadhili wa masomo kusoma nje ya nchi
“mzee alipitiliza ndani huku walinzi wake wakibaki nje, namkumbuka mmoja aliitwa Joshua “
Baada ya masaa mawili hivi niliona baba akiondoka zake na mimi niliamua kushuka chini kumfuata mama na kumkuta Sebuleni analia
Sikujua hata pa kuanzia lakini mama aliniita na kuniambia yaliyojiri
“baba yako anateuliwa kuwa Raisi kwenye chama chake mwaka ujao, kutokana na ushindani uliopo kwenye Chama ni yeye na Waziri mkuu wa sasa ndio wanapewa nafasi kubwa sana hata hivyo mheshimiwa Raisi anataka kumuachia yeye kijiti”
Alisema mama
“sasa mbona unalia?” nilimuuliza mama
“iko hivi, mimi ni mchepuko tu mwanangu, mimi ni mchepukooo!” alisema kwa hasira akitupa glass ya maji sakafuni
“ah sijaelewa mama”
“iko hivi mwanangu Gift kuanzia sasa hivi baba yakao hatakuja tena hapa! Kwa ufupi hutakutana nae popote sio wewe tu lakini hata mimi pia” alisema akilia
“mama kwanini Lakini?” nilisema nikiwa sielewi
“mwanangu wewe ni msomi sasa unajua, Raisi hatakiwi kuwa na makando kando, kuanzia keshoa anaanza kufuatiliwa hata akienda chooni, anayetakiwa kuwa nae bega kwa bega ni mke wake wa ndoa” alisema mama
“naelewa mama, sasa bado nashindwa kuona kwanini unalia!’ nilisema
“leo amekuja kutupa tahadhari kuwa mkewe amejua tunapoishi hivyo tuwe makini na ikibidi tuhame kabisa hata nje ya nchi mapaka uchaguzi upite” alisema mama kwa uchungu
Sasa nilielewa uzito wa lile jambo, na sikuona namna ya kufanya, mama yangu hakuwa na ndugu tuliyeweza kumfahamu zaidi alituambia tu kuhusu baba yake ambaye alifariki alipokuwa mdogo na mama yake alifariki wakati akijifungua, na akaenda kulelewa katika kituo cha watoto Yatima cha Samaritan Morogoro ambapo alisomeshwa na wamisionari mpaka alipofika UDSM na kukutana na baba yangu,
Hata hivyo kwa macho na kwa vitendo baba yangu alinipenda sana na alimpenda mama yangu pia alishamfungulia miradi mikubwa sana na kumuachia pesa nyingi kabla ya uchaguzi na alimuahidi kuwa nae bega kwa bega
Wakati naondoka pale sebuleni mama alinipa barua ambayo ilikua imetoka kwa mzee
Well
 
MPANGAJI 12
wenzetu hawa walimu wanakopeshwa basi akaenda huko akachukua mkopo na tukaingiza kwenye biashara zetu basi Mungu akajalia mama!”alisema Sele
“ooh kwakweli mwanangu hongereni sana kwakweli umetutoa kimaso maso kwakweli” alisema mama Mwajuma
Sele aliingia zake chumbani akiwaacha mama na mwanae hapo ambapo jioni walimsindikiza tena mpaka nyumbani
Sasa mama Mwajuma hakutaka kulala usiku ule aliwakusanya wapangaji wenzake na kuwaelezea huko nyumbani kwa Esta
“nakuambia ni Ikulu, ni ikulu!” alisema mama mwajuma akikazia “umbea” wake kama ilivyokuwa kawaida yake
----------------------------------------------------------------
BAADA YA MIAKA KADHAA
Uchaguzi nchini Tanzania ulimalizika salama na Mzee Lukas Tuppa akakabidhi kijiti kwa aliyekuwa waziri Mkuu wake Bwana Jeremiah Mdee,
Mara baada ya kustaafu Mzee Tuppa tofauti na watangulizi wake, aliamua kubaki jijini Dar es salaam, tayari Joan na Jesca walishakuwa mawaziri katika serikali yake huku wakitajwa kama mawaziri wadogo zaidi kuwahi kutokea Tanzania, Bwana Tuppa aliongoza kwa miaka 20 , tofauti kabisa na watangulizi wake, tetesi zilikua zilisambaa kuwa mkewe mama Joan ndie aliyekuwa akimlazimisha Mzee kuendelea kubaki madarakani
Alirudi nyumbani kwake Masaki na familia akijinasibu kuwa anaenda kuwa mfugaji wa kuku kumalizia wakati wake wa kuishi hapa duniani pamoja na “kucheza na wajukuu” kama viongozi wengi walivyopenda kuongezea hayo maneno wanapohojiwa
Mzee Tuppa alitengana na mkewe Rasmi siku alipogundua alimuua mke mke mwenzake mama Doreen,
Kilichoonekana kwa nje ilikua ni maigizo tu na kamwe hawakuwahi kulala tena chumba kimoja toka siku ile
Kila mmoja alikua na chumba chake au tuseme ‘nyumba yake” walinzi wake wa karibu walikua wanajua hayo yote lakini wakati walipokuwa wakitoka kwenda kwenye ziara za kikazi Mzee Tuppa na mkewe walikuwa wakishikana mikono na kutabasamu
Mara kadhaa mama Joan alijaribu kumuomba msamaha mume wake huyo lakini mzee Tuppa alikataa kata kata
“wewe ni muuaji Janet!, unathubutuje kumuua mama na mtoto kinyama kiasi kile kwa sababu za kijinga kama zile?” alikua anafoka mzee Tupa
“wangefanya nini wale eeh? Wangeweza kuzuia mimi kuwa Raisi? Ningekuwa tu! Walishaelewa ona umekatisha ndoto za kijana wangu! Mimi nitamtazama vipi huko kuzimu? Nakuuliza wewe?” Sasa Mr Tuppa alikuwa akikumbuka hayo yote akiwa ameshika picha ya mke wake mama Doreen waliyopiga wakati akiwa mhadhiri pale UDSM
“ twende mzee muda wa kipindi” ilikua ni sauti ya mlinzi wake Joshua ambaye sasa alikua akimsindikiza katika Televisheni ya Taifa ambapo kulikua na kipindi maalum cha “JIFUNZE KWAKE” ambacho kilikua maalum kuwahoji watu maarufu na kisha kupoke maswali machache kutoka kwa watazamaji mubashara baada ya kuwasili na ukaguzi kufanyanyika sasa mzee Tuppa alivalishwa kifaa maalum cha kukuzia sauti na kisha akaenda kukaa kwenye sofa kubwa iliyokuwa pembeni ya kamera nyingi nyingi
“habari mtazamajij wetu wa Televisheni yako ya taifa kama tulivyokuwa tukikujuza wiki hii nzima kuwa tutakuwa na Raisi mstaafu mheshimiwa Lukas Kaijage Tuppa, basi tayari ameshafika hapa studio tayari kabisa kukuletea mahojiano haya ya masaa mawili mimi ni mtangazaji wako Faraja Walter, na tutarejea baada ya muda mfupi!’
Kipindi hiki kilikua kipindi pendwa sana tayari watu wengi walikua wakifuatilia mahojiano hayo Sele akiwa nyumbani kwake na mke wake nao waliacha kula na kukodoa macho kwenye tv kuhakikisha wanasikia kila neno kutoka kwa mzee
“hebu sasa tuambie mheshimiwa unaona tofauti gani kati ya kuwa ofisini na ulivyo sasa nyumbani ukicheza na wajukuu?” aliuliza mtangazaji
“tofauti ipo kubwa sana, kwakweli ukiwa Raisi unapangiwa nini ufanye, nini ule, mpaka kitu gani uangalie kwenye Tv , tofauti na sasa hivi naweza kulala muda ninaotaka na hata kuamka pia, lakini pia naweza kula sasa hata vile vyakula ambavyo nisingekula kipindi nikiwa Raisi”
Waliendelea na mahojiano mpaka pale walipomaliza kisha wakaruhusu simu
Simu nyingi zilikua za kawaida na kupongeza mpaka baadae ilipopigwa simu moja hivi ambayo ilibadili kabisa mjadala
“mheshimiwa Raisi , kulikua na tetesi kuwa ulikua na mke mdogo ambaye alikua mwalimu pale chuo kikuu cha Dar, na mlijaliwa kuwa na watoto wawili,
nataka kujua kama je ni kweli na je baada ya kifo cha mke wako huyo katika ajali ya moto ulijisikiaje na huyo mtoto mwingine yuko wapi?
“tafadhali tutajie tena jina lako na unapiga simu ukiwa wapi?’ Faraja alijaribu kumkatisha Yule jamaa lakini tayari swali lilikua limeshasikika
‘basi tuendelee kuuliza maswali halafu mheshimiwa atayajibu kwa pamoja” alisema mtangazaji kwani tayari alishaona uso wa mzee Tuppa ukibadilika
“kama muuliza swali nimemsikia vizuri yeye amesema anawajua hao watoto kwahiyo nishauri jeshi la polisi lichukue hatua kwakuwa namba yake hii imeonekana basi ataeleza zaidi niwashi ndugu zangu watanzania tuachane na tetesi na habari za mitandao!” alimaliza mheshimiwa Raisi

“watamkamata huyo mtu” alisema Sele
“huyu mtu ni nani lakini? Amejuaje haya yote?” Aliuliza Esta
“sijui kwakweli” alisema sasa tayari alikua ameshaanza kuhisi kuna watu wengi tu wanajua sakata lake “ngoja tuone kesho wakimkamata nitafanya niwezalo kumuona” aliwaza sele
Ni kweli haikuchukua muda jeshi la polisi lilitangaza kumshikilia kijana huyo mapema sana kesho yake mchana kwa tuhuma za kutunga uongo na kuusambaza kuhusu familia ya Raisi mstaafu
“tunataka kutoa sampo kwa kijana huyu ili kukomesha kabisa tabia ya kusingizia na kuchafua watu kwa sababu za kisiasa, tutaanza na huyu na wengine watafuata” alisema polisi Mamboleo
Wakati huo Sele alikua jirani na kituo cha polisi hicho akijaribu kupenya penya ili amuone kijana huyo ni wakati anapaki gari na kusogea ndipo simu yake ikaita aliangalia mpigaji na kuweka simu chap sikioni
“baby niko hapa najitahidi..”
“usihangaike mume wangu, wamemuachia, Raisi amemsamehe ameamuru aachiliwe mara moja angalia whatsap nimekutumia clip’ Alisema Esta
Sele alirudi kwenye gari kisha akfungua mlango na kufungua ile video
“hatuwezi kumkamata kila mtu anayetunga uongo tutawakamata wangapi? Nimeamua kumsamehe Yule kijana na naomba jeshi la polisi kijana huyo aachiliwe” ilikua ni sauti ya mzee Tupa akiongea
“noo nooo something is wrong!” alijisemea Sele pamoja na muda mrefu aliokuwa nao lakini alijua baba yake amekasirika na sio kweli kuwa kijana huyo amesamehewa bali kuna jambo baya litamkuta, Sele aliendesha agari kusogelea kituo cha polisi na kweli alishuhudia kijana huyo akitoka, alimtazama kijana huyo angalau aone sura yake lakini hakuweza, tayari kulikua na msongamano wa waandishi wa habari na wapiga picha kadhaa hatimaye ilipaki gari ndogo pembeni na akashuka mama mmoja hivi akikimbilia kule ulipokuwa mlango na hatimaye
Baada ya muda mfupi akarudi kwenye gari akiwa na yule kijana, na gari ikaondoka
“fuata hiyo gari sele!” alijiambia wakati sasa anawasha gari kuifukuzia walitembea kutoka kituo cha polisi na kutokea barabara ya Shekilango na sasa waliingia kushoto na kufuata barabara ya sinza, halafu walipofika Mugabe wakaingia bara bara ya vumbi kulia, na sasa Sele alitabasamu baada ya kuangalia kwenye kioo cha gari cha kutazamania nyuma,
Naam hakuwa peke yake kulikua na gari nyingine nyuma yake ambayo alihisi nao walikua wakimfuatilia Yule kijana
“kumekucha” aliwaza akiendelea kusogea na walipita shule ya Msingi Mugabe, na kutokea kwenye nyumba moja iliyokuwa na geti jeusi baada ya kupiga honi geti likafunguliwa, sele alipaki pembeni na kusogea kwenye duka lililokuwa pembeni na sasa lile gari lililokuwa nyuma yake nao walifika na kupunguza mwendo kidogo kwenya ie nyumba kisha wakapitiliza
“naomba mirinda nyeusi” sele alisema huku akikaa kwenye benchi lilikokuwa pale nje
“hivi kumbe Yule dogo anakaa pale eeh” sele alianza maongezi
“ah Yule dogo bhana kajisababishia msala sana, ujue braza ukweli unaweza kukuua hivi hivi, Yule dogo juzi tu nilikua namwambia aache huo upuuzi wake lakini hakutaka kunielewa, wamemuachia lakini sijui kama wataamuacha yule maana ujue dogo ana siri nyingi sana za baba yake!”
“unataka kuniambia na wewe unaamini hizo tetesi?” Sele aliuliza
“broo wewe uko dunia gani, hata mtoto mdogo anajua kabisa Mzee aliua mke na watoto wake ili aupate uraisi nani asiyejua?”
“kwani Yule dogo ndio mtoto wa mzee nanilii ah nani Yule alikua …” sele alijifanya sasa kusahahu kidogo
hadithi njoo utamu kolea
 
MPANGAJI 19
By CK Allan

“ndio niliwatuma vijana wangu na ndio maana muda mfupi tu alikamatwa” alisema mheshimiwa Kidude. Sasa Sele alikata tamaa ya kutoka salama katika kesi hii, kama alivyokuwa ametarajia, mke wa Raisi alikuwa amejipanga vilivyo kuhakikisha kuwa hachomoki katika kesi hii ,akili yake ilimwambia kuwa mheshimiwa kidude hakukamatwa bali alijikamatisha makusudi baada ya kupanga mikakati yake ipasavyo
Ilifika zamu yake akasomewa mashataka yake na hakutakiwa kujibu chochote na kesi ikaahirishwa tena

Doreen sasa aliona kama mbwai na iwe mbwai tu alishauriana na mumewe na kisha akaaomba likizo ya mwezi mmoja kazini kwake na kupanda ndege kuelekea Tanzania , Doreena asingeweza kukaa kimya huku mdogo wake akiozea gerezani hata hivyo alitaka kulifanya jambo hili bila kumshirikisha Sele, tayari alishakuwa na mawasiliano na mr K na sasa alimuomba msaada wa kupata mawasiliano ya mzee Tuppa, Mr K alijitahidi na mwishowe akapata namba ya mlinzi wake mmoja ambaye alimtumia Doreen haraka.
Doreen alishuka uwanja wa ndege wa Julias Nyerere na kuita tax iliyokuwa jirani na kumuelekeza ampeleke rombo hotel, ni miaka zaidi ya 15 sasa Doreen hajawahi kukanyaga ardhi hii
“hakika nchi imebadilika sana, lakini watu ni wale wale!” aliwaza akiweka miwani yake vizuri huku akitazama mazingira mazuri ya jiji la Dar
Alifika hotelini na kuchukua chumba chake kisha akafanya mawasiliano na mumewe na kisha akaanza kutoa vitu vyake na kuvipanga vizuri
“Gift, dada yako niko hapa pamoja na wewe”
Tayari alitoa laptop yake na kufungua fungua baadhi ya picha na video zilizokuwemo kisha akajilaza kitandani
Wakati huo Sele , Rapha na Mr K walikuwa katika kikao kizito cha kujadiliana namna ya kutoka kwenye kesi ile,
Kilichokuwa kinasumbua ni kesi ya rushwa, lakini kesi yao ya msingi ya kuwa mtoto wa Lukas walikuwa na ushahidi wa kutosha tu katika hilo
‘tuangalie namna ya kuwarudishia hii kesi , alisema Rapha huku macho yake yakiwa katika video ya ulinzi wa kamera katika nyumba ya Sele
“hebu rudisha nyuma hapo weka pause” alisema Rapha akisogea kwa makini
“mwangailieni huyu jamaa, huyu ,huyu!” alisema Rapha huku mr K na Sele wakimtazama tuu
“hii sura ya huyu jamaa hamjawahi kuiona kweli? Hebu fungua youtube niwaonyeshe kitu” alisema rapha na sele haraka akafungua tovuti iyo
‘andika msafara wa mke wa raisi mama Tuppa” alisema rapha sasa akiamini akili zake hazijamdanganya
“fungua hiyo video ya pili hapo” alisema akionyeshea
Na sasa wote walipigwa na mshangao , sura pamoja naumbo la mlinzi mmojawapo wa mama Joan lilifanana kabisa na Yule mtu alikuwa amesimama pale nje kwenye zile video za nyumbani kwa Sele, ambaye alikua amemteka Esta
‘kwahiyo hapa asilimia mia moja huu ni mkakati wa mama joan na huyu mzee Kidude” alisema Sele
“yeah na inavyoonekana hapa kuna kila dalili huyu mama amekusudia mambo makubwa huko mbele” alisema Mr K,
“ukishagundua mtu unayepambana nae hakuna shida” alisema Sele
Wakati wao wakiendelea kujadili huku mzee Tuppa sasa alikuwa amepumzika nje ya nyumba yake kwenye bustani za maua akicheza na ndege wake aina ya kanga wakati mlinzi wake Joshua alipomfuata na kumnong’oneza waliingia ndani kisha kama kawaida yao wakapitia mlango wa uani na kutokea nje na kuingia kwenye gari ya kawaida kabisa na kuondoka kwa kasi,
Mzee Tuppa alipenda kwenda sehemu mbali mbali na kufanya starehe zake kwa kupitia njia hii ya uani ili kuwakimbia walinzi wake, aliondoka na dereva wake na Joshua tu
“una uhakika yupo?” aliuliza tena mzee Tupa
“ndio mzee yupo anatusubiri” alisema Joshua sasa wakikata uchochoro na kutokea barabara ya moro goro kisha wakaiacha kimara mwisho na kuingia kimara temboni NA kuingia kwenye barabara ya vumbi na kisha wakapaki gari yao mbele ya kanisa la KKT
“vaa hii” alisema Joshua sasa akitoa kofia moja inayofunika masikio wengine walipenda kuiita pama mzee Tupa alitabasamu na kuivaa kisha wakazunguuka nyuma ya kanisa hilo na kutokea kwenye viti maalum vilivyotengenezwa kwa Zege na kukaa
“yuko wapi sasa?’ aliuliza mzee Tupa

“anakuja mzee muda ….” Alikatishwa na mlio wa gari Joshua alitabasamu na kuzunguuka kule nyuma akiwa tayari kumpokea mgeni wake huyo
Baada ya dakika kadhaa alirudi akiwa ameongozana na mwanamke mmoja hivi aliyekuwa amejifunika mtandio
Sasa mzee Tupa alijikuta akisimama na kusogea hata kabla mgeni huyo hajafika mahali alipokuwepo
Doreen alivua miwani yake pamoja na kutoa ule mtandio wake kichwani na sasa alikua akitazamana uso kwa uso na binti yake huyo, ambaye hakukumbuka mara ya mwisho walionana lini
“dad!”
“daughter” alisema mzee Tupa akimkumbatia binti yake Yule walibaki wamekumbatiana kwa zaidi ya dakika tano huku kila mmoja akitoa machozi hatimaye waliachiana na kisha Doreena akamkumbatia uncle Joshua
Sasa waliketi chini na kuanza kuongea mzee Tupa alijieleza yote yaliyokuwa moyoni mwake huku akimtaka radhi binti yake huyo kwa mambo yote yaliyotokea
“Mungu ni shahidi sihusiki kabisa na yale yote na hata haya yanayoendelea kutokea katika jambo hili la Gift”
“Baba ni wakati wako wa kuonyesha Dunia kwamba wewe ni baba wa namna gani, vile vile ni wakati wako wa kutuonyeshea mimi na Gift kuwa ni kweli huhusiki kabisa na mambo yote haya yanayoendelea kutokea” alisema Doreen
“niambie mwanangu unataka mimi nifanyeje? Sema mwanangu?” aliuliza mzee Tuppa akimuangalia binti yake huyo
“turn yourself in” alisema Doreen
Mzee Tupa alikumbuka pia ushauri aliopata kutoka kwa rafiki yake jaji mstaafu kuwa ulikuwa sawa na huo huo kuwa ajiingize rasmi kwenye kesi hiyo
“nakuahidi nitafanya niwezavyo kuhakikisha mambo haya yanakwisha kabisa na kila mmoja atavuna alichopanda” alisema mzee Tupaa
“vizuri sasa mimi niondoke” alisema Doreena akiondoka
“Doreen, nakupenda mwanangu, nisameheni sana!” alisema akisimama na kuondoka
Doreen alisimama na kuondoka zake na kurudi kwenye Taksi iliyokuwa inamsubiri na kurudi hotelini kwake, sasa aliamini mambo yataisha kabisa katika kesi ile alifanya mawasiliano na mzee K kisha akakutana na Rapha na kuweka mikakati sawa namna ya kuweza kuweka ushahidi sawa, kulikua na ile video ya mauaji, pamoja na picha kadhaa za utotoni za akina Gift akiwa pamoja na mzee Lukas Tupa na ile picha maarufu ya familia ambayo walipiga wote wanne
“mzee ameonyesha nia?” aliuliza Rapha
“yeah lakini hatabiriki sana” alisema Doreen
“okay tujipange sisi kama Sisi, labda nikuulize swali moja, wakati unasoma Kenya kuna siku baba yako alishawahi kukutembelea na mkapiga walau picha ukiwa shuleni na walimu au wanafunzi wenzako?” aliuliza Rapha
“mzee alikuja kama mara tatu hivi, na siku zote alifika shuleni na kusema alikua anatembelea watanzania waliokuwa wanasoma nchi humo, nadhani tulikuwa kama wanne hivi wawili katika ile shule na wawili walikuwa katika shule nyingine, so alikua anatukusanya na kutupeleka lunch au dina, na nilishaambiwa kuwa nisiseme kuwa yeye ni baba yangu nikiwa kule Kenya, kwa ajili ya usalama wangu, nakumbuka mama aliniambia Kenya kuna magaidi na kama wakijua mimi ni mtoto wa waziri basi wataniteka” alisema Doreen akifuta machozi
“hakuna shida, sasa tuanze na hiki kilichopo halafu tubadili kesi na tumfungulie rasmi kesi ya mauaji madam” alisema Rapha
Hatimaye siku ya kesi ilifika na kama kawaida gift alipewa nafasi ya kujitetea na kama alivyofundishwa na wakili wake alikuwa sasa anatoa utetezi wake kabla ya hukumu kutolewa
‘tuliishi mikocheni na baadae tukahamia mbezi beach, wakati wote huo mama alikua anafanya kazi chuo kikuu cha Dar es Salaam, kwahiyo baba yetu mzee Lukas Tuppa alikua na kawaida ya kututembelea nyumbani kila…..” sasa Gift alikua akieleza maisha yake binafsi na ya dada yake na jinsi mpaka alivyofanikiwa kuona mama yake akiuwawa”
“sasa kwanini unahisi kuwa kesi hii imepangwa na watu wabaya wakati wewe umekamatwa na ushahidi ndugu yangu?’ alikua anauliza sasa wakili upande wa mashtaka
‘Pesa hiyo niliwekewa baada ya kutekwa kule na watu wa mzee Kidude ndio walioweka bahasha hiyo” alisema Gift
Waliendelea kuuliza maswali na sasa wakili wa Gift akaanza kuita mashahidi wake kwa mshangao wa wengi Shahidi wa kwanza alikua Doreen baada ya kuapa na kupanda kizimbani nae akatoa maelezo yake
 
MPANGAJI 20
By CK Allan

“Tuliishi kwa furaha mpaka siku ile ambapo baba alikuja kutuambia anataka kujiingiza kwenye mbio za uraisi, na kusema kuwa hatakuja tena pale nyumbani, baba yetu alitupenda sana na kulikua na kila dalili alikua anampenda mama yetu zaidi kuliko mama Joan na ndio maana mama Joan akamuua mama yetu mzazi…”
“haaaaaaaaaaaaa” sasa kulikuwa na mguno mkubwa pale mahakamani na minong’ono ilikua dhahiri na ikabidi mwendesha mashtaka kuingilia kati
“binti, hizo tuhuma za mauji ni kubwa sana, unaweza kuthibitisha?” aliuliza mwendesha mashataka kwa utulivu
“ndio, tulifanikiwa kuondoka na kipande kidogo cha video kutoka kwenye nyumba yetu kabla vitu vinginme havijachukuliwa na mheshimiwa hakimu ushahidi huo unaonesha wazi wazi mama Joan akiwa na watu wake wakimshambulia mama kwa risasi” alisema Doreen
“haaaaaaaaaaaaaaa” miguno iliendelea tena pale mahakamani
“sio hivyo tu, nyumba yetu haikuwa na uthibitisho wowote wa kuwa na tatizo lililosababisha shoti ya umeme, ama gesi ama chochote kile, badala yake moto ule uliwashwa makusudi kupoteza ushahidi” alisema Doreen
“tunaomba hiyo video tafadhali” alisema mwendesha mashtaka na kisha wakaingia kwenye chumba maalum pamoja na mawakili wa pande zote mbili na kuangalia sasa ile video huku kila mmoja akiandika vitu muhimu
Na baadae walirudi tena mahakamani na Doreen akatoa ushahidi wa picha na vitu kadhaa vingine
“kwakuwa tayari tumeshapata mtuhumiwa mwingine naagiza sasa mama joan, aletwe hapa mahakamani kwani tayari hatuwezi tena kuendelea kusikiliza mashahidi wengine na kuendelea na kesi hii bila mtuhumiwa kuwepo” alisema hakimu huku akiahirisha kesi tena
Gift na dada yake walibaki nyuma huku wakikumbatiana na kuongea kwa fuaraha
“asante kwa kuja dada” alisema Gift
“asante sana mdogo wangu siwezi kukuacha nyuma” alisema Doreen
“haya tupite njia hii” alisema Mr K akiwaongoza kupita njia ya pembeni kwani tayari waandishi walikuwa wanawasubiri nje na wasingeweza kuwakwepa bila kupitia mlango wa nyuma

“Nashauri tusitumie gari moja” alisema rapha
“na mimi naona hivyo pia” alisema Gift
“Sele na Mr K Mtatumia gari langu, mimi na Doreen tutatumia gari la Mr K , halafu gari la Sele liwe backup na james na Ali wakitufanyia backup” alisema Rapha na kisha wakatoka nje ya jengo
“mtanifuata mimi kila kichochoro ninachopita” alisema Mr K na sasa safari ikaanza mara moja wakitoka mahakamni kisutu na kuelekea huko Mr K alipokusudia
Waliendelea kuwa kuwasiliana kwenye magari yote matatu
“mbona tunaenda ofisini” aliuliza Sele
“ndio tunaenda huko ila kuna kitu nataka ukaone” alisema Mr K
Walifika mpaka ofisini kwao na kumkuta Esta ambaye alikua amekaa kwa muda akishikilia majukumu ya Sele kutokana na yeye kuwa katika ubize wa kesi walipitiliza na kuingia kwenye ofisi ya Mr K
“Mr K sidhani kama mahali hapa ni salama sana” alisema Rapha
‘subirini muone” alisema sasa akichukua simu iliyokuwa pale mezani
“Njoo” alisema kisha akakata simu akina Sele walikua wakimtazama tu sasa Mr K
Baada ya muda aliingia katibu muhtasi wake, Aisha
“tuna kikao kirefu sana kwa siku mbili mfululizo kutokana na jambo ambalo unalijua kwahiyo mtu yoyote akiulizia huduma basi muone namna ya kumsaidia na usimruhusu yoyote , narudia yeyote, kuja ofisini kwangu, nipigie simu yangu ya mkononi tu ikibidi sana” alisema.
Baada ya Aisha kuondoka sasa Gift alishindwa kuvumilia
“mr K Hapa hatuwezi kukaa angalia kwanza ni ofisini chumba kidogo na inabidi sehemu ya kupumzika bhana” alisema Sele ,
Mr K hakujibu alisimama na kwenda kuufunga mlango kabisa kisha akasogelea kwenye shelfu kubwa la vitabu na mafaili na kusogeza mafaili kadhaa kisha akatumbukiza mkono na kubonyeza kidude Fulani na sasa lile shelu likaanza kupanda juu pole pole na hatimaye mlango mkubwa ukatokea mbele yao
“haya njooni huku!” alisema Mr K Na sasa wote wakasimama wakiwa wamepigwa na butwaa

Mr K aliifungua ule mlango na sasa wakatokea kwenye sebule moja kubwa iliyokuwa na Tv kubwa mbili na samani nzuri za kisasa
“haya sasa hapa tupo nyumbani kwetu kabisa tunaweza kuendelea” alisema Mr K akiwakaribisha wageni wake hao
“hakika hii inapendeza sana sikujua kama Mr K unaweza kubuni kitu kama hiki, haya tunafanyaje sasa hapa kujua yanayoendelea huko nje!” alisema Sele na kama alivyotegemea aliwasha Tv mojawapo aliyohisi na kweli ilikua inaonyesha matukio kadhaa yaliyokuwa yakiendelea kule ofisini na nje kidogo ya ofisi na kuzunguuka jengo zima
“haya sasa wanaotaka kupumzika kwa muda wanaweza, kuna vyumba viwili vikubwa vinatosha kabisa na jiko dogo lipo hapa na nimeweka vyakula vya kutosha kwa wiki kadhaa, kwakweli niliweka hiki chumba maalum kabisa kipindi kile vugu vugu lilipoanza nikahisi chochote kinaweza kutokea sasa” alisema Mr K,
Sasa walikaa na kujadili mipango yao yote huku wakifuatilia kila kitu kilichokuwa kinaendelea pale ofisini ni mpaka jioni sana sasa Doreen aliondoka kurudi hotelini kwake akisindikizwa na Rapha huku sele Na Esta wakirudi nyumbani kwao na kumuacha Mr K ofisini kwake
Hatimaye Mama Joan aliamua kujipeleka Polisi huku mzee Lukas akigoma kata kata kumsindikiza
“kila mmoja apambane na hali yake Vivian!’ alipenda kutumia jina lake halisi alipokuwa akiongea na mke wake huyo
“nilikulinda wakati wote lakini sio sasa Vivian! Sio sasa!” alisema mzee Lukasi asubuhi hiyo wakati mke wake huyo akienda kituo cha polisi
Mama Joan alikua aliwakilishwa na wakili wake ambaye alimpa matumaini makubwa ya kushina kesi hiyo asubuh kabisa
Wakati kesi ikisomwa sasa wakili wake huyo alikua akisimama mara kadhaa na kupinga baadhi ya maelezo au ushahidi uliokuwa katika upande wa mashtaka
“mheshimiwa hakimu mdai katika kesi ya msingi ni mtaalamu wa Tehama, tena anamiliki kampuni ya kuuza vifaa vya ulinzi wa mifumo, ikiwemo kamera za ulinzi, je kwa weledi wake mkubwa huu pamoja na tuzo alizoshinda anashindwa kutengeneza video kama hii? Mheshimiwa hakimu, lakini pia tunajiuliza kwanini wakae na ushahidi wote huu wa mauaji kwa miaka yote hii kwa kigezo tu cha kumlinda baba yao?” aliuliza wakili wa mama Joan
“napinga mheshimiwa..napinga!” aliingilia kati Rapha
“kuwa na kampuni ya vifaa na kujua tehema hakuzuii mahakama hii tukufu kuchukua ushahidi huu, video hii inaonyesha muda mwaka na tarehe ya matukio halisi ya wakati ule mheshimiwa hakimu” alisema Rapha huku akiweka Joho lake vizuri na kurudi kukaa
“je unao mashahidi wengine tafadhali?” aliuliza hakimu
“ndio mheshimiwa,’ alisema Rapha akimkonyeza mwendesha mashtaka ambapo baada ya muda aliingia Jose
Baada ya kupanda kizimbani sasa alianza kutoa ushahidi wake
“naitwa Josep James Kimei, baba yangu alikuwa daktari katika hospitali ya taifa muhimbili na baadae akwa daktari Binafsi wa familia ya Mzee Lukas, mara nyingi alikuwa akienda kuwahudumia akina mama Doreen na watoto wake kule Mikochoni au mbezi Beach mara kadhaa nilikua nakwenda nae kule hususani wakati wa likizo, ama siku moja moja wakati wa Wikiendi”
“hebu sasa tuambie siku ambayo baba yako alikuwa anakwenda kwa marehemu mama Doreen na baadae na hakurudi tena ilikuwaje hiyo siku?’ Rapha alikuwa anamuuliza
“ilikua ni majira ya saa tatu kasoro na tulikua tunakula chakula cha usiku wakati baba alipopigiwa simu kuwa aende haraka kwa mama Doreen, nilitaka kwenda na baba Siku ile lakini baba alinisihi nimalizie kula chakula kwani hatachukua muda kurudi, ilikua ni siku moja kabla ambapo alituambia kuwa kuna uwezekano akabadilishiwa majukumu ya kazi yake na hivyo pengine kazi zake zikaongezeka zaidi , baada ya kumaliza kula tulikaa mpaka majira ya saa tano usiku lakini baba hakurudi , hivyo mama ayangu alijaribu mara kadhaa kupiga simu yake lakini haikupokelewa na kwakuwa hapakuwa na umbali mrefu tulitoka na kupanda bajaji kuelekea kule kwa mama Doreen, wakati tunakaribia pale kwenye nyumba yao tuliona gari ikitoka kwa kasi na kuacha geti likiwa wazi na hivyo tuliongeza mwendo lakini tayari moto ulikua ukiwaka karibia shemu zote za nyumba na tayari watu walikuwa wanatoka majumbani kusogea pale,tulikuwa wa kwanza kufika pale lakini ghafla mama yangu alianza kulalamika moyo na presha na akazimia, sikua na namna isipokuwa kumkimbiza hospitali haraka na kisha kurudi tena kwenye tukio ambapo polisi walikuwa wameshatoa miili na kuzima moto na kesho yake tulitangaziwa kuwa mama Doreen amefariki na mtoto wake na mlinzi, baada ya mama kutoka hospitali hakuwa sawa mpaka leo hii,
Tulijaribu kutoa taarifa polisi lakini hakukuwa na taarifa zozote hata pamoja na kueleza kuwa baba alikuwa kwa mama Doreen hakuna polisi aliyetilia maanani na baada ya siku chache tukasikia gari ya baba imeonekana karibu na bahari ikiwa imetelekezwa, na baba hakuwemo!
 
Back
Top Bottom