CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,781
- 6,139
- Thread starter
- #101
MPANGAJI 07
Niliona watu watatu wakiwa wamefunika nyuso zao ila kwa muonekano mmojawapo alikuwa mwanamke, walikuwa wamemtoa mama yangu pamoja na daktari na mlinzi na dada wa kazi na kuwafunga kamba na kuwawekea vitambaa mdomoni ispokuwa mama yangu ambaye walikua wakimuuliza nilipo
“yuko wapi Gift?’ Alikuwa akiuliza Yule mwanamke akimpiga mateke mama
“Gift yupo na baba yake kwenye kampeni!”mama alijibu huku akilia,
Sitaki kukumbuka Esta, ila ni kwamba walimpiga mama risasi na wale wengine walifariki pale pale kisha wakatoka nje na kuchoma moto nyumba”
Sele sasa alikuwa Analia kama mtoto mdogo,
Esta nae alijikuta akilia kwa nguvu na na mara wakajikuta wamekumbatiana wote wakilia kama watoto wadogo
“inauma sana Esta, sasa kesho yake jambo baya zaidi likatokea, magazeti na vyombo vya habari walitangaza kuwa mama yangu, pamoja na mimi wote tulifariki katika ajali ya moto iliyotokea usiku ule,
“kwa maana hiyo ule mwili wa dokta ndio ukaonekana ni wewe au?” aliuliza Esta
“nilikuja kugungua baadae mama mkubwa ndio alimuua mama yangu mzazi na alifanya vile makusudi ili hata kama nikiwa hai nisiwe na namna yoyote ya kujitokeza kuwa mimi ni mtoto wa mzee Tupa kwakuwa tayari nilishafariki kwenye ule moto” alisema Sele
“loh kwanini lakini Binaadamu ni wanyama kiasi hiki,?”alisema Esta sasa huku akijifuta machozi
“Vipi sasa baada ya kutoka hapo ilikuwaje na ule usiku ulienda wapi na ikawaje sasa hadi ukaishi hivi unavyoishi leo Sele?”
“niligundua kwamba tayari nilishafika maeneo ya koko beach kwahiyo nilirudi kwenye gari na kwa bahati nilikuta pesa kama laki mbili hivi kwenye ile gari ya Dokta, nikaenda kutafuta chumba gest nikalipia siku tatu, ili nitafakari cha kufanya”
Nilifanya mawasiliano na dada Doreen ambaye hakuamini kama anaongea na mimi maana alijua nimeshafariki, kwahiyo akanisisitiza kuhakikisha waliofanya haya yote wanakuja kupata haki yao hapo baadae, nilisubiri usiku sana nikaenda kwenye nyumba yetu na kujaribu kutafuta kama nitapata kitu cha maana
Kitakachonisaidia, vitu vingi tayari vilikua vimeshachukuliwa na nadhani ilikua ni njia mojawapo ya kuficha siri, nilifanikiwa kuokota baadhi ya picha za mama na za kwangu na vitu kadhaa tu
“Sele kwahiyo hii ilikua ni mwaka 2000 sio?”
“yap, kipindi kile kile cha…” sele alikatishwa na sauti ya mhudumu ambaye alikuwa ameleta chakula kutokana na oda zao walizokuwa wameagiza, hakika walijikuta wamepiga story sana kwa muda mrefu na hata hawakusikia njaa mhudumu aliweka chakula mezani na kisha waliamua kula
Hadithi ziliendelea mpaka jioni Tayari Sele alikua amemsimulia kila kitu ambacho alidhani alipaswa kumhadithia,
“sasa ulipata vipi tena vitambulisho vyako?” Esta aliuliza
“kutokana na vitambulisho vile havikuwa feki yaani vilitoka mamlaka husika, nilienda tu polisi nikachukua loss riport na kisha nikarudisha kimoja baada ya kingine” alisema Sele
“Sele nataka uniamini mimi, kwakweli hadithi yako inahuzunisha sana, kwa mtu yoyote Yule kama nilivyokuahidi Sele, kuanzia leo hii mimi nitakuwa upande wako katika kila jambo ambalo unapanga kulifanya, nipo Sele kwa ajili yako..’ alisema Esta akimkumbatia Sele kwa nguvu, Sele alijisikia msisimko wa ajabu pale matiti ya Esta yalipokuwa yakigusa kifua chake kipana cha wastani taratibu na yeye alianza kumshika Esta kwenye kiuno na kifuani, hatimaye wakaanza kupunguza nguo kwenye miili yao waliendelea kutomasana kama wapenzi waliokuwa hawajakutana muda mrefu na pole pole wakahamia kwenye mahaba mazito, hakika ilikua ni vurumai mle ndani kwa vita ile isiyoumiza hadi kila mmoja akabaki hoi kabisa.
“Esta wewe ni mwanamke Jasiri na nakushukuru kwa kunibadilisha leo hii najisikia Sele mpya kabisa!” alisema sele akiwa bado anachezea nywele za Esta
“Sele nakuahidi kuanzia siku hii sitakubali tena uishi maisha ya huzuni” tafadhali ngoja niende Lindi kesho halafu nasubiri uniambie nifanye utakachotaka Sele, chochote kile Sele” alisema Esta akiwa amelala juu ya kifua cha Sele.
Usiku ule ulikuwa wa furaha sana kwa wawili wale na ipofika asubuhi Esta alilipa Bili yote ya pale kisha safari ikaanza.
Esta alipata Gari ya Masasi kisha Sele alienda “kazini kwake” kwa siku zote kisha jioni akarejea kama kawaida
*********************************
Wiki mbili zilikatika na taratibu Sele alianza kubadilika, alikua amenyoa nywele zake na kuchonga ndevu zake vizuri , siku hiyo alienda mpaka kwenye kaburi la mama yake maeneo ya sinza akiwa na shada la maua, Sele aliweka yale maua kisha akapiga magoti pale
“mama najua umeona mwanao nimesimama tena, mama nimampata mwanamke anaitwa Esta Chilambo, ni mwanamke mzuri mama ana upendo kama wewe, anasema ananipenda mama, kama ulivyokuwa unanipenda mama, baada ya kuwakamata wale washenzi wote waliofanya ukatili huu mama, basi nitamuoa mama, angalia mama mwanao nimebadilika kabisa mama hata naomba mama niombee msamaha kwa dada Doreen, nimekua kaka mbaya” alisema sele sasa akilia machozi pale kaburini
Alikaa zaidi ya nusu saa kisha akasimama na kujifuta machozi na kusimama na kuondoka,
Sele alikumbuka jinsi alivyokuwa amezinguana na dada yake baada ya kumtaka asichukue hatua kwanza za kulipiza kisasi mpaka pale wakati ukifika
“haiwezekani Gift, huwezi kufanya sasa, watakuua , Wataniua na mimi, jifiche hivyo hivyo mdogo wangu vuta subra kidogo tuu!” alikumbuka maneno ya dada yake huyo, lakini Gift hakukubali, Gift hawezi kusahau siku hiyo akiwa maeneo ya mwenge alimuona mama yake mkubwa huyo mke wa Raisi akiwa katika matembezi yake, alikua amejiandaa kwa siku kadhaa akiwa na bastola yake kuwa popote atakapomuona Yule mama basi angempiga risasi ili kumlipizia kisasi mama yake, wakati msafara unakaribia mama yake mkubwa alishuka huku akiwa amezunguukwa na walinzi alielekea kituo cha watoto yatima kilichokuwa karibu ili agawe misaada Gift alijichanganya kati kati ya watu huku bastola yake ikiwa kiunoni tayari kufanya mauaji, wakati anakaribia kabisa alishtuka kuhisi mikono iliyokua na nguvu zaidi yake ikimshika vizuri kiunoni na bastola yake ikachukuliwa! Halafu akavutwa pole pole kuelekea kwenye gari
Alitupiwa kwenye gari na safari ikaanza aliwekwa kati kati ya watu wawili na watu wengine wawili walikua mbele ambao hawakugeuka na hivyo hakuona sura zao gari ilishika kasi kuelekea nje ya mji na baadae gari ilisimama kisha wakashuka watu wote na Yule mmoja aliyekuwa mbele akarudi sasa Siti ya nyuma na kukaa na Gift akiwa na ile bastola
“nisikilize Gift” alisema Yule jamaa ambaye Gift alikua hamjui kabisa
“unafanya jambo la kipuuzi kuliko upuuzi wenyewe! Usifanye tena huu upuuzi kama unataka kulipa kisasi cha mama yako!”
“wewe ni nani na umejuaje haya yote?” aliuliza Gift
“mimi ni mjomba wako!” alisema
‘lakini mama yangu hajawahi kuniambia chochote kuhusu kuwa na mjomba mwingine!” alisema Gift
“ni kweli , iko hivi Unakumbuka siku ile ukiwa pale Mlimani city na wenzako na ikatokea vurugu?”
“ah nakumbuka ndio kuna mtu akaja haraka na kutuingiza kwenye gari kisha akatupeleka kila mtu nyumbani kwao na akakataa kuchukua pesa?’ sasa Gift alianza kumbuka Yule jamaa
‘ulipomaliza tu kidato cha sita mama yako aliniajiri niwe mlinzi wako kuhakikisha unakuwa Salama, nasikitika sana maana siku ile pengine badala ya kukufuatilia ulipoenda kutafuta dawa ningebaki pale nyumbani!” pengine wasingemuua mama yako
Alisema na yeye sasa akifuta machozi
“najua una hasira lakini nataka kukuhakikishia kuwa siku ukitoa bastola yako tu mbele ya mama yako mkubwa bila hata hujafyatua watakuwa wameshakuwahi na habari za mama yako zitakuwa zimeishia hapo!” alisema
Kuanzia siku ile Gift alilikubali rasmi jina la Sele na kisha akaanza kuishi maisha yake, alikata mawasiliano na dada yake Doreen kabisa kwani alijua ingeweza kuwa njia rahisi ya kumkamata yeye, jambo ambalo alilifanya alimtumia Yule jamaa kusimamia miradi ya mama yake na kisha faida ya ziada alimuingizia Gift katika akaunti zake za Sele, na kama kulikua na ulazima basi walikutana kwa siri nyumbani kwa Yule jamaa,
Sele alifanikiwa kutojiingiza katika ulevi na wanawake, kwani kwa pesa alizokuwa nazo angeweza kuishi maisha ya pombe na kubadili wanawake atakavyo lakini alijua kuwa siku ambayo angeanza kuishi maisha ya kujulikana basi ndio siku ya kukamatwa kwake, kwahiyo Sele alitoka kwenye jumba lao zuri kule mbezi beach akalitafutia mpangaji kwa msaada wa Yule jamaa kisha yeye akaenda kuishi uswazi katika maisha ya chini kabisa ili kusubiri Uraisi huu wa baba yake upite, hata hivyo wakiwa mwishoni kabisa kumaliza mhula wa mwisho wa urasi
Mzee Tuppa alinogewa na madaraka na kubadili katiba kisha akaongezewa tena miaka 10!
Sele alishindwa kuvumilia zaidi na ndipo kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu wakakutana Nairobi yeye na dada Yake Doreen, ambapo dada yake alisema wasubiri miaka hiyo 10 iishe na Gift akasema walianzishe tuu kwa kutumia vyombo vya kimataifa, walipingana na kutoleana maneno makali na kikao chao kikaishia hapo!
Kila mmoja akaenda njia yake na hawakusalimiana wala kuwasiliana tena!
Miaka zaidi ya 7 ilipita wakati leo hii Sele akikumbuka haya akitoka makaburini kwa mama yake
Niliona watu watatu wakiwa wamefunika nyuso zao ila kwa muonekano mmojawapo alikuwa mwanamke, walikuwa wamemtoa mama yangu pamoja na daktari na mlinzi na dada wa kazi na kuwafunga kamba na kuwawekea vitambaa mdomoni ispokuwa mama yangu ambaye walikua wakimuuliza nilipo
“yuko wapi Gift?’ Alikuwa akiuliza Yule mwanamke akimpiga mateke mama
“Gift yupo na baba yake kwenye kampeni!”mama alijibu huku akilia,
Sitaki kukumbuka Esta, ila ni kwamba walimpiga mama risasi na wale wengine walifariki pale pale kisha wakatoka nje na kuchoma moto nyumba”
Sele sasa alikuwa Analia kama mtoto mdogo,
Esta nae alijikuta akilia kwa nguvu na na mara wakajikuta wamekumbatiana wote wakilia kama watoto wadogo
“inauma sana Esta, sasa kesho yake jambo baya zaidi likatokea, magazeti na vyombo vya habari walitangaza kuwa mama yangu, pamoja na mimi wote tulifariki katika ajali ya moto iliyotokea usiku ule,
“kwa maana hiyo ule mwili wa dokta ndio ukaonekana ni wewe au?” aliuliza Esta
“nilikuja kugungua baadae mama mkubwa ndio alimuua mama yangu mzazi na alifanya vile makusudi ili hata kama nikiwa hai nisiwe na namna yoyote ya kujitokeza kuwa mimi ni mtoto wa mzee Tupa kwakuwa tayari nilishafariki kwenye ule moto” alisema Sele
“loh kwanini lakini Binaadamu ni wanyama kiasi hiki,?”alisema Esta sasa huku akijifuta machozi
“Vipi sasa baada ya kutoka hapo ilikuwaje na ule usiku ulienda wapi na ikawaje sasa hadi ukaishi hivi unavyoishi leo Sele?”
“niligundua kwamba tayari nilishafika maeneo ya koko beach kwahiyo nilirudi kwenye gari na kwa bahati nilikuta pesa kama laki mbili hivi kwenye ile gari ya Dokta, nikaenda kutafuta chumba gest nikalipia siku tatu, ili nitafakari cha kufanya”
Nilifanya mawasiliano na dada Doreen ambaye hakuamini kama anaongea na mimi maana alijua nimeshafariki, kwahiyo akanisisitiza kuhakikisha waliofanya haya yote wanakuja kupata haki yao hapo baadae, nilisubiri usiku sana nikaenda kwenye nyumba yetu na kujaribu kutafuta kama nitapata kitu cha maana
Kitakachonisaidia, vitu vingi tayari vilikua vimeshachukuliwa na nadhani ilikua ni njia mojawapo ya kuficha siri, nilifanikiwa kuokota baadhi ya picha za mama na za kwangu na vitu kadhaa tu
“Sele kwahiyo hii ilikua ni mwaka 2000 sio?”
“yap, kipindi kile kile cha…” sele alikatishwa na sauti ya mhudumu ambaye alikuwa ameleta chakula kutokana na oda zao walizokuwa wameagiza, hakika walijikuta wamepiga story sana kwa muda mrefu na hata hawakusikia njaa mhudumu aliweka chakula mezani na kisha waliamua kula
Hadithi ziliendelea mpaka jioni Tayari Sele alikua amemsimulia kila kitu ambacho alidhani alipaswa kumhadithia,
“sasa ulipata vipi tena vitambulisho vyako?” Esta aliuliza
“kutokana na vitambulisho vile havikuwa feki yaani vilitoka mamlaka husika, nilienda tu polisi nikachukua loss riport na kisha nikarudisha kimoja baada ya kingine” alisema Sele
“Sele nataka uniamini mimi, kwakweli hadithi yako inahuzunisha sana, kwa mtu yoyote Yule kama nilivyokuahidi Sele, kuanzia leo hii mimi nitakuwa upande wako katika kila jambo ambalo unapanga kulifanya, nipo Sele kwa ajili yako..’ alisema Esta akimkumbatia Sele kwa nguvu, Sele alijisikia msisimko wa ajabu pale matiti ya Esta yalipokuwa yakigusa kifua chake kipana cha wastani taratibu na yeye alianza kumshika Esta kwenye kiuno na kifuani, hatimaye wakaanza kupunguza nguo kwenye miili yao waliendelea kutomasana kama wapenzi waliokuwa hawajakutana muda mrefu na pole pole wakahamia kwenye mahaba mazito, hakika ilikua ni vurumai mle ndani kwa vita ile isiyoumiza hadi kila mmoja akabaki hoi kabisa.
“Esta wewe ni mwanamke Jasiri na nakushukuru kwa kunibadilisha leo hii najisikia Sele mpya kabisa!” alisema sele akiwa bado anachezea nywele za Esta
“Sele nakuahidi kuanzia siku hii sitakubali tena uishi maisha ya huzuni” tafadhali ngoja niende Lindi kesho halafu nasubiri uniambie nifanye utakachotaka Sele, chochote kile Sele” alisema Esta akiwa amelala juu ya kifua cha Sele.
Usiku ule ulikuwa wa furaha sana kwa wawili wale na ipofika asubuhi Esta alilipa Bili yote ya pale kisha safari ikaanza.
Esta alipata Gari ya Masasi kisha Sele alienda “kazini kwake” kwa siku zote kisha jioni akarejea kama kawaida
*********************************
Wiki mbili zilikatika na taratibu Sele alianza kubadilika, alikua amenyoa nywele zake na kuchonga ndevu zake vizuri , siku hiyo alienda mpaka kwenye kaburi la mama yake maeneo ya sinza akiwa na shada la maua, Sele aliweka yale maua kisha akapiga magoti pale
“mama najua umeona mwanao nimesimama tena, mama nimampata mwanamke anaitwa Esta Chilambo, ni mwanamke mzuri mama ana upendo kama wewe, anasema ananipenda mama, kama ulivyokuwa unanipenda mama, baada ya kuwakamata wale washenzi wote waliofanya ukatili huu mama, basi nitamuoa mama, angalia mama mwanao nimebadilika kabisa mama hata naomba mama niombee msamaha kwa dada Doreen, nimekua kaka mbaya” alisema sele sasa akilia machozi pale kaburini
Alikaa zaidi ya nusu saa kisha akasimama na kujifuta machozi na kusimama na kuondoka,
Sele alikumbuka jinsi alivyokuwa amezinguana na dada yake baada ya kumtaka asichukue hatua kwanza za kulipiza kisasi mpaka pale wakati ukifika
“haiwezekani Gift, huwezi kufanya sasa, watakuua , Wataniua na mimi, jifiche hivyo hivyo mdogo wangu vuta subra kidogo tuu!” alikumbuka maneno ya dada yake huyo, lakini Gift hakukubali, Gift hawezi kusahau siku hiyo akiwa maeneo ya mwenge alimuona mama yake mkubwa huyo mke wa Raisi akiwa katika matembezi yake, alikua amejiandaa kwa siku kadhaa akiwa na bastola yake kuwa popote atakapomuona Yule mama basi angempiga risasi ili kumlipizia kisasi mama yake, wakati msafara unakaribia mama yake mkubwa alishuka huku akiwa amezunguukwa na walinzi alielekea kituo cha watoto yatima kilichokuwa karibu ili agawe misaada Gift alijichanganya kati kati ya watu huku bastola yake ikiwa kiunoni tayari kufanya mauaji, wakati anakaribia kabisa alishtuka kuhisi mikono iliyokua na nguvu zaidi yake ikimshika vizuri kiunoni na bastola yake ikachukuliwa! Halafu akavutwa pole pole kuelekea kwenye gari
Alitupiwa kwenye gari na safari ikaanza aliwekwa kati kati ya watu wawili na watu wengine wawili walikua mbele ambao hawakugeuka na hivyo hakuona sura zao gari ilishika kasi kuelekea nje ya mji na baadae gari ilisimama kisha wakashuka watu wote na Yule mmoja aliyekuwa mbele akarudi sasa Siti ya nyuma na kukaa na Gift akiwa na ile bastola
“nisikilize Gift” alisema Yule jamaa ambaye Gift alikua hamjui kabisa
“unafanya jambo la kipuuzi kuliko upuuzi wenyewe! Usifanye tena huu upuuzi kama unataka kulipa kisasi cha mama yako!”
“wewe ni nani na umejuaje haya yote?” aliuliza Gift
“mimi ni mjomba wako!” alisema
‘lakini mama yangu hajawahi kuniambia chochote kuhusu kuwa na mjomba mwingine!” alisema Gift
“ni kweli , iko hivi Unakumbuka siku ile ukiwa pale Mlimani city na wenzako na ikatokea vurugu?”
“ah nakumbuka ndio kuna mtu akaja haraka na kutuingiza kwenye gari kisha akatupeleka kila mtu nyumbani kwao na akakataa kuchukua pesa?’ sasa Gift alianza kumbuka Yule jamaa
‘ulipomaliza tu kidato cha sita mama yako aliniajiri niwe mlinzi wako kuhakikisha unakuwa Salama, nasikitika sana maana siku ile pengine badala ya kukufuatilia ulipoenda kutafuta dawa ningebaki pale nyumbani!” pengine wasingemuua mama yako
Alisema na yeye sasa akifuta machozi
“najua una hasira lakini nataka kukuhakikishia kuwa siku ukitoa bastola yako tu mbele ya mama yako mkubwa bila hata hujafyatua watakuwa wameshakuwahi na habari za mama yako zitakuwa zimeishia hapo!” alisema
Kuanzia siku ile Gift alilikubali rasmi jina la Sele na kisha akaanza kuishi maisha yake, alikata mawasiliano na dada yake Doreen kabisa kwani alijua ingeweza kuwa njia rahisi ya kumkamata yeye, jambo ambalo alilifanya alimtumia Yule jamaa kusimamia miradi ya mama yake na kisha faida ya ziada alimuingizia Gift katika akaunti zake za Sele, na kama kulikua na ulazima basi walikutana kwa siri nyumbani kwa Yule jamaa,
Sele alifanikiwa kutojiingiza katika ulevi na wanawake, kwani kwa pesa alizokuwa nazo angeweza kuishi maisha ya pombe na kubadili wanawake atakavyo lakini alijua kuwa siku ambayo angeanza kuishi maisha ya kujulikana basi ndio siku ya kukamatwa kwake, kwahiyo Sele alitoka kwenye jumba lao zuri kule mbezi beach akalitafutia mpangaji kwa msaada wa Yule jamaa kisha yeye akaenda kuishi uswazi katika maisha ya chini kabisa ili kusubiri Uraisi huu wa baba yake upite, hata hivyo wakiwa mwishoni kabisa kumaliza mhula wa mwisho wa urasi
Mzee Tuppa alinogewa na madaraka na kubadili katiba kisha akaongezewa tena miaka 10!
Sele alishindwa kuvumilia zaidi na ndipo kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu wakakutana Nairobi yeye na dada Yake Doreen, ambapo dada yake alisema wasubiri miaka hiyo 10 iishe na Gift akasema walianzishe tuu kwa kutumia vyombo vya kimataifa, walipingana na kutoleana maneno makali na kikao chao kikaishia hapo!
Kila mmoja akaenda njia yake na hawakusalimiana wala kuwasiliana tena!
Miaka zaidi ya 7 ilipita wakati leo hii Sele akikumbuka haya akitoka makaburini kwa mama yake