Hadithi: Mpangaji

Hadithi: Mpangaji

MPANGAJI 13

by CK Allan

“dokta James , Yule ni Mtoto wa Dokta james ambaye ndio alikua daktari wa Yule mama Doreen,” Alisema Yule muuza duka na kumfanya Sele sasa atake kuzimia
“ni kweli tarifa hua zipo tu zinaelea, unaweza kupaa kuzifuata au utume chombo kukuletea” aliwaza
“ah kwahiyo Yule Bwana mdogo ni Jose si ndio!” aliuliza Sele
“ndio Jose Yule, Dogo tangu dingi yake avute amekuwa kama teja hivi anaropoka tu, unajua bhana wakati mwingine kuna watu hawana huruma,”
“basi broo mi nipo hapa kuna pisi imenielekeza ipo mitaa hii ila naona nimefika mpaka hapa hola na simu hapokei”
“ah pisi za sinza nyingi pasua kichwa broo, itakuwa umepigwa” alisema Yule muuza duka
Sele alijifanya kusoma sms kwenye simu yake na kuaga
“ah amesema yuko kule juu kijiweni’ alisema akilipa pesa ya soda na kuondoka
Aliwaza na kuwazua na hakuona namna ya kumsaidia Jose kwa wakati ule ingawa aliamini kuwa lazima atafuatiliwa, hata hivyo alijua hawezi kudhurika mapema maana watu wataunganisha doti kwa urahisi
Mzee Lukas sasa alikua alikua akiwasubiri kwa hamu vijana wake ambao walirejea baada ya kuhakikisha mke wake ameondoka sasa vijana wake walimpa habari zote
“Yule ni kijana wa dokta James, anaitwa Jose, kama unavyojua alikua na urafiki kiasi na Gift, kwahiyo mara nyingine dokta James alipokuwa anaenda kwa mama Doreen alikua anaenda nae na akawa anacheza michezo ya video na Gift, inaonekana wakati baba yake anaondoka siku ile alijua anakokwenda au kuna kitu dokta alikua amemueleza mwanae”
Alisema Joshua
“vipi mnadhani kijana wangu Gift yuko hai kama alivyosema?” aliuliza Mzee
‘hapa tuweke hamsini kwa hamsini uhakika tunao sana kwa dada yake Doreen,”
“achana na Doreen, Doreen yupo kwa mume wake huko Italy unadhani mimi nilishindwa kumpata Doreen? Lakini unadhani ningemtazama vipi usoni? Wakati anajua kabisa mama yake ameuawa na mimi sijafaanya kitu?” alisema Mzee Tuppa machozi yakimtoka

“nisikilizeni Yule shetani ataenda kumuua Yule Jose na mama yake masikini, ili kufuta ushahidi wa ushetani wake safari hii sitamsamehe yeyote endapo hilo litatokea” alisema Mzee Tuppa
‘tumelizingatia hilo na tunafanya utaratibu wa kuhakikisha wanakuwa salama mzee” alisema Joshua huku akiondoka na wenzake kwenda sehemu zao za kupumzika
“yaani kuwa mlinzi wa raisi ni heka heka mwanzo mwisho, sijui mwisho wangu utakuwaje yaani” alijiwazia Joshua
Upande wa pili Mama Joan nae alikua anaongea na walinzi wake na kuweka mikakati yao
“kwahiyo kumbe ni mtoto wa dokta James eeh, aah sasa naelewa kwanini alikua anampigia chapuo mke wa marehemu’ aliwaza mama Joan akikumbuka jinsi mke wa dokta James alivyolipwa mafao mengi na fidia kubwa na vitu vingine vingi! Kumbe alikuwa na mtoto wa kiume yue mshenzi
‘nataka wiki hii isiishe huyo mpuuzi awe amefariki” sitaki mfanye upuuzi wowote na hakikisheni kama kuna kiumbe chochote cha Lukas kinaishi, nataka nimalizie uzee wangu kwa amani mimi” alisema mama Joan
“Lukas , utajilaumu sana” aliwaza mama Joan huku akizunguusha zunguusha simu yake
Alitoa maagizo hayo kwa vijana wake kisha aktoka sehemu hiyo ya makutano na kuondoka haraka kurejea nyumbani, alairudi na kumkuta mume wake huyo nae akiwa katika Lindi la mawazo alijua fika mke wake alitoka wapi na alipanga nini , lakini wanasema aliyetangulia ametangulia tu, Mzee Lukas alikua hatua kadhaa mbele ya mke wake
Akili yake ilijua kabisa mwanae Gift atakuwa hai, kama ilivyo kwa dada Yake Doreen, mara kadhaa alijaribu kumpigia simu Doreen, lakini alipopokea simu hakuongea chochote, pamoja na kwamba alitangazwa kuwa amekufa lakini kijana yake mmoja ambaye alimpenyeza kwa siri kumchunguza mkewe, ndie aliyekuja kumpa taarifa kuwa aliyeuawawa usiku ule alikua ni mlinzi pamoja na daktari na sio mlinzi na Gift katika ile miili minne kwa miaka Yote hiyo Mzee Tuppa alijitahidi kumtafuta mwanae kwa siri lakini aliona kila anavyokaribia anaweza kumpa nafasi mkewe pia kujua mwanae huyo alipo na pengine kabla yake, wasi wasi huu ndio ulimfanya mzee Lukas kusubiri mpaka majukumu haya makubwa yapite kisha “aingie mzigoni” mwenyewe kutafuta namna ya kurejesha familia yake hii
Aliwaza haya sasa akimuangalia mkewe wake huyo
“kwanini umemsamehe? Nakuuliza Lukas, hivi unaona watu wanatuzungumziaje huko kwenye mitandao? Hebu amka Lukas wewe bado ni Rais ujue” alisema mama Joan akiingia ndani akimpita mume wake pale nje
********************************
Sele alikua bize akiweka mikakati yake tayari alikua na sehemu ya kuanzia, hata hivyo hakutaka kufanya haraka ya kwenda kwa Dokta James kwani alijua fika sasa ile nyumba itakuwa inapigwa jicho kali alijaribu kusoma taarifa kadhaa za dokta James kupitia mtandao lakini hakupata taarifa za kumfaa sana
Siku hiyo aliamua liwalo na liwe alipanga kwenda usiku nyumbani kwa dokta James na kuonana na familia yake alifika na kupaki gari hatua kidogo mbali na nyumba yao kisha akashuka na kusogea mlangoni na kubonyeza kengele ya mlangoni , baada ya muda geti lilifunguliwa na na msichana mmoja hivi umri kati ya miaka 17 hivi, na kumkaribisha ndani,
“bila shaka ni mgeni wa kaka Jose,” alisema akitabasamu
“ah Ndio Ndio kwani vipi!? Sele aliuliza
“ah yaani kuanzia asubuh kila mtu anakuja, sijui wa online Tv, redio magazeti n.k” alisema huku akionyesha nae amechoka kufungulia wageni
“ah yupo, ndani?” sele aliuliza
“ndio yupo, lakini kwakweli sidhani kama atakubali kutoka nje maana amesema hataki tena kuonana na waandishi wa habari yaani” Alisem
“mimi sio mwandishi wa habadari dadaangu nina shida binafsi nay eye, tafdhali sana” alisema huku akiweka mikono yake kifuani ishara ya kuomba
Hata hivyo baadae alitoka akiwa na uso wa kukata tama
“amekataa kabisa na hata mama amesema kwa leo inatosha Tadhali naomba nifunge geti”
Alisema Yule msichana na sele akatoka nje ya geti,
Aliangalia saa yake tayari ilikua ni saa tatu kasoro usiku, hakutarajia kuwa Jose alikuwa anapata wageni wengi kiasi hicho, lakini hata hivyo tayari ilishakuwa story kubwa na waandishi wasingependa kukosa kila hatua ya skendo hiyo
Alitoka nje na kusogea mahali alipokuwa amepaki gari lake aliingia na kuanza kuondoka taratibu mara ghafla akapishana na gari aina ya noah iliyokuwa na vioo vyeusi alipunguza mwendo na kuanza kupaki pembeni kisha akageuza kulifuatilia lile gari sasa watu wawili walishuka na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea ilipokuwa nyumba ya akina Jose,
Aliamua kupitiliza kana kwamba hakuona chochote huku akitafuta upenyo wa kuzunguuka kurudi tena, wakati anajiuliza aliona gari nyingine ikiwa imepaki huku taa zimezimwa lakini kwa harakandani kulikuwa na watu,
“mmh hapa kuna kitu kinaendelea lazima” alisema akiipita na ile gari nyingine na kisha akatafuta upenyo na kuipaki gari kisha akarudi kwa miguu, wakati anakaribia kwenye ile gari aliona mtu mmoja akija kwa kasi na kuingia kwenye ile gari na kisha ikawashwa na kuondoka pale, bila kujiuliza mara mbili alirudi haraka na kuingia kwenye gari yake kujaribu kuwafuatilia, alipita pale kwa akina Sele na tayari watu walikua wameanza kukusanyika nje aliona kwa mbali Yule msichana aliyempokea muda mfupi akilia akiwa ameshikana na mama mmoja hivi
Aliongeza kasi na kweli kwa mbali aliona ile gari mbele yake,
Aliifuatilia na walipofika sinza kumekucha wakapinda kulia kuelekea mwenge Sele alizidi kufuatilia na mwishowe akawakaribia kabisa na sasa aliamini bila shaka gari iliyokuwa na Sele itakuwa mbele ya ile gari nyingine,
“vipi kama hawa ni kikosi kimoja nah ii gari moja ilikua kwa ajili yakuzuga tu?” aliwaza sele sasa akizidi kukanyaga mafuta, walipofika maeneo ya afrika sana, gari walielekea kushoto na kunyoosha hatimaye walitokea katika jengo moja la hoteli ambalo lilikuwa linajengwa na halikukamilika, lile gari likapunguza mwendo na kuingia, Sele kama kawaida alipitiliza na kisha akapaki gari na kuzima taa kisha akarudi mbio mbio kwa kunyata na kuingia kwenye lile jengo alizunguuka na kutafuta njia kwa mwanga hafifu na hatimaye akainama kwa kunyata huku akichungulia na akaanza kusikia sauti
“hamuendi popote na huyo dogo muacheni”
“bro nakuheshimu sana ondokeni hii misheni haiwahusu’
‘sikiliza T, unanijua vizuri, mzee hatawaacha salama amesema huyu dogo asiguswe”
“broo kama unatuchelewesha tupishe mama anamtaka huyu dogo ujue, hata hapa kupaki ni kwasababu ya heshima yako tuu”
“hebu kuwa muelewa wewe jamaa, mnazidi kumchafulia mzee hamjui tu wewe na huyo bi mkubwa wenu sasa hivi kesho magazeti na vyombo vyote vya habari watatangaza dogo amepotea unadhani nani wa kwanza kulaumiwa? Mmelifikiria hilo wewe na huyo mama yenu Shetani?”
Sasa sele akili zake zilikaa sawa alielewa kabisa haya ni makundi tofauti mama dhidi ya baba na mama yake ndie aliagiza Jose auwawe lakini baba yake ndie ameagiza kundi linguine kuzuia
Wakati akitafakari mara ghafla ukatokea mwanga mkali na kuwamulika pale
 
MPANGAJI 14

By CK Allan

Sele alijibanza ukutani na kisha akasogea tena tayari aliwe za kuona kundi lingine la watu wakiwa sasa wamewazunguuka pale na sasa walikua tunaweza kusema ni nusu huku na nusu kule, mara bila kukawia sasa milio ya Risasi ikarindima na Jose bila hiyana akaona upenyo na kutokea dirishani Sele alikua amechuchumaa huku akitafuta namna ya kutafuta upenyo wa kutokea na ndipo aliposikia kishindo nyuma yake, aligeuka na kumuona Jose pamoja na kuwa ilipita miaka mingi lakini alimtambua, hakukua na muda alimshika mkono na kukimbia huku wameinama kufuata mahali alipokua amepaki gari lake,
Milio ya risasi iliendelea kusikika na kulikua na vurumai na makelele kutoka huku na huku,
“twende!” sele alisema sasa akifungua mlango na kuingia
“Sasa walinyoosha barabara na kutokea stendi ya zamani ya mwenge na kisha wakatokea bara bara ya Morogoro , Sele hakujua kwanza anaenda wapi lakini baadae alipata wazo kuwa waende sehemu kwanza kuongea,
Alitafuta sehemu nzuri ambayo kulikua na uchochoro kisha akapaki gari
“Jose!’ aliita
“kaka!” Jose aliitika kisha akasogea kiti cha mbele, walitazamana kwa muda kisha wakakumbatiana
“gift”
“jose”
Walikumbatiana wakilia machozi mpaka walipodhani sasa wametosheka kulia Sele alitoa wazo
“mpigie simu bi mkubwa kwanza kuwa upo Salama halafu tutafute namna” alisema Sele sasa akimpa simu yake walimpata baada ya kurudia rudia sana kwani simu yake ilikua ikitumika sana na aliwajulisha kuwa tayari alikua kituo cha polisi akiripoti kuhusu kutekwa kwa mwanae
“sikiliza broo, ni suala rahisi tu ngoja tuwachezee mchezo” alisema Sele huku akiendesha gari kurudi tena Sinza kwa akina Jose, tayari ilishatimia saa 5 usiku na aliamua kumjulisha Esta kuhusu kuchelewa huko kisha akamuelekeza Jose kitu cha kufanya nap engine cha kusema pia kisha akaunganisha zake Mbweni
Sele alimueleza mke wake yote yaliyojiri na kile walichokubaliana kufanya na Jose kwanza kuweka ulinzi ili jambo baya lisitokee kwa kila namna na baadae walipue mazima, ingawa kwa jinsi Sele alivyoona baba yake alikua upande wao
Kesho yake asubuhi katika kipindi cha magazeti kupitia televisheni ya weupe Tv, walitangaza kutembelewa na mgeni katika kipindi chao hicho wakisema kuwa alikua na jambo la kupeleka ujumbe kwa serikali haswa mzee Tupa Raisi mstaafu
Baada ya kukaribishwa sasa Jose alisema vile vile kama alivyopangwa na Sele
“kwahiyo ninamshukuru sana Rais mstaafu kwa kunisamehe sana wiki moja iliyopita hata hivyo kama tujuavyo wapo watu ambao kwa dhamira zao pengine hawakukubaliana na mimi kusamehewa na Raisi wameendeleza chuki na mimi na siku ya jana walikuja nyumbani kwetu na kuniteka, hata hivyo nashukuru Mungu nimetoka salama, hata hivyo wakati wananiteka kuna mambo ambayo ambayo wale watu walikua wakiongea kwani walionekana kama ni makundi mawili hivi yanayokinzana, sasa yupo mtu ambaye nimemwambia kila kitu na kumkabidhi ushahidi wote ninaoujua kuhusu watu hao, kwa masharti kwamba siku yoyote nikipotea zaidi ya siku tatu bila mawasiliano yoyote basi aweze kuusambaza katika mitandao”
“sasa Bwana Jose, huo ushahidi upo katika mfumo gani, video, sauti, picha au nini?” aliluliza mtangazaji
“siku hiyo ikitokea wakaja kuniteka kama walivyoniteka jana au jambo baya kunitokea basi hata hapa weupe Tv mtaupata tu” alisema Jose baada ya maongezi hayo mafupi tayari taarifa zilienea kote na tayari Jose aligeuka maarufu ghafla
“umefanya vizuri” alipokea ujumbe mfupi kutoka kwa sele baada ya mahojiano hayo
Ni kweli baada ya mahojiano hayo sasa Mama Joan alitafuta mipango ya kufuta na kununua kila habari ambayo ingehusu mzee watoto na mke wa zamani wa mzee Tupa na kutafuta mbinu ziadi za kumnyamazisha Jose
Sele aliwasiliana na dada yake na kisha kwa kushirikiana na mr K Sasa waliandaa kikao cha siri na kufanya mikakati yote na namna ya kufungua shauri pamoja na kuangalia kila namna kuhusu suala lenyewe
“sisi hatutaki fidia, ni suala tu la mama yetu aliyeuliwa kikatili pamoja na watu wengine ambao hawakua na hatia kabisa,” yalikua ni mawazo kutoka kwa Doreen kupitia kundi sogozi la muda la mtandao wa whatsapp ambao walikuwa wamepatana kujadiliana humo
“ok, kwa hapo tunaweza kufanya vitu viwili, kuanzisha Shauri, ama sisi kuanzisha habari ili wao watengeneze shauri, inawezekana vyote tu”
“ nina wazo, kwakuwa kampuni yetu imeingia katika shindano la kampuni bora ya mwaka kwa upande wa teknolojia na kwa namna ilivyo kuna uwezekano mkubwa wa kushinda tuzo hiyo, wakati wa kutoa hotuba ya shukrani tuanzie hapo hapo” alisema sele

“Yes tufanye hivyo, na uzuri wenyewe Tuzo hizi hazifanyiki Tanzania kwahiyo tuanzie hapo hapo”
Basi walikubaliana na hatimaye hotuba ikaandaliwa na mazingira yote yakawekwa vizuri,
******************************
SEPTEMBA 12, 2018 NAIROBI
Sele akiwa ndani ya suti nzuri ya bluu pembeni yake alikua mke wake Esta ambaye nae alikuwa amevalia vazi lake lililomkaa vyema walikuwa wakicheka kila saa wakati mshereheshaji wa tuzo hizo Bwana Omondi akiwa anatamba jukwaani, hatimaye wakati wa tuzo ukafika na walioshinda tuzo mbali mbali ukawadia, kama ambavyo Sele alibashiri basi ilikua hivyo hivyo kwani baada ya kuchukua tuzo kulikua na dakika 10 za kusema jambo!
Sasa Sele alisubiri kwa hamu na tuzo yake ikawadia
“kampuni bora ya vifaa vya teknlojia kwa ulinzi na usalama wa majengo, kulikua na kampuni nne ambazo zilikua zimeshindanishwa kama ifuatavyo
Kampuni ya weCare kutoka Tanzania
Kampuni ya LIGHT kutoka Kenya
Kampuni ya we4u kutoka Tanzania na
Kampuni ya NEXT kutoka hapa Kenya
Na kutokana na kura kutoka kwa washiriki wa nchi hizi zote basi kampuni ya we4u kutoka Tanzania ndio wameibuka washindi na hapa Tunae mr Sele S, Sele ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa kampuni hii karibu sana uchukue tuzo hii” yalikua ni maneno ya mshereheshaji
“hii ni siku muhimu Sele, kila la kheri mume wangu” Esta alimnong’oneza Sele wakati sasa akisimama na kuweka suti yake vizuri na kusogea mbele
Alipokea tuzo yake kwa heshima kisha akasogea mbele sehemu iliyokuwa na kipaza sauti
“tuambie unajisikiaje kupokea tuzo hii ukizingatia kuwa kampuni yako ni mpya kabisa?’
“ah kwanza namshukuru sana Mungu kwa tuzo hii lakini pia namshukuru mke wangu ambaye ameendelea kuwa nami kila siku, najisikia furaha sana kwakweli” alisema sele huku mapigo yake ya moyo yakipiga kwa kasi
“tofauti na wenzako wengine ambao kwa uzito wa tuzo hii na hata katika ule mualiko ulitakiwa angalau uje na familia yako, vipi mr Sele labda unaweza kusema kidogo kuhusu familia yako kama hapa wapo na kama hawapo labda unawaambia nini kwasababu tuko live hapa na vyombo vingi vinaripoti tukio hili”
“yeah ni kweli, ningependa sana kuja na kila mtu hapa anayenihusu lakini kwasababu ambazo ziko nje ya uwezo wangu kabisa, nimekuja na mke wangu kipenzi tafadhali Esta simama kidogo, lakini bila shaka kuna watu watatu ambao wananitazama muda huu na ningependa kuwataja hawa ni muhimu sana yupo Mr Kibwana ambaye ni meneja katika kampuni hii ya we4u na bila shaka asingeweza kuja kwasababu ya majukumu, lakini niseme pia ninaye dada yangu Anaitwa Doreen Tris Falez huyu yuko Italia muda huu, lakini pia siwezi kuacha kumtaja baba yangu mzazi mr Lukas Tuppa , huyu yupo Tanzania bila shaka nasema kwamba nawependa sana” alisema Sele huku akifuta machozi ambapo mkewe Esta alimfuata na kumkumbatia na kushuka nae kwenye ngazi
Mara baada ya tuzo kumalizika sasa ilibidi Polisi kuingilia kati kwani tayari kundi la waandishi wa habari walikuwa wanataka kufanya mahojiano na Sele, na kutokana na sababu hiyo Sele na mkewe walipitishwa mlango wa nyuma na kuelekea hotelini alipofikia
Waliwahi haraka na kwenda chumbani kwao na kufungua televisheni na sasa tayari televisheni nyingi walikuwa wanatangaza habari za Sele mtoto wa Lukas Tuppa
Walikumbatiana kwa furaha huku wakikodoa macho kwenye kituo hiki cha weupe Tv wakifuatilia matangazo hayo ya moja kwa moja
“kwahiyo kwanza hapa kumbuka tulikua na habari za Jose juzi, na kama mnakumbuka alisema kama sio kweli kwamba mtoto wa Lukas yuko hai basi muda utasema, sasa kabla hili halijapoa sasa tunamuona mr Sele akisema yeye ni mtoto wa mheshimiwa Lukas, labda mimi najaribu kuotea kwamba bado kuna mengine yanakuja” yalikua ni maongezi ya watangazaji hao huku wakiendelea na mjadala
Tayari Sele alimtumia meseji mr K kuwa waendelee na mpango unaofuata kesho yake
Ilibidi sele kuzima simu yake pamoja kwani wasingeweza kulala usiku huo na walikataa kabisa kufanya mahojiano na waandishi wowote na hivyo wakajifungia ndani na kuchapa usingizi, pengine siku hiyo sele alipata usingizi mtamu kuliko siku zote kwani aliona kama kuna kitu tayari kilikuwa kimepungua katika ufahamu wake ule uzito ambao alikua anahisi upo basi uliondoka kabisa.
Kesho yake walijiandaa kurudi Tanzania ambapo ndipo wangemwaga mboga ,
 
Ndio story zangu zote zilivyo mkuu hata ukicheki madam president, Kesi ya Mzee Mnyoka pia
Madam President naionaga, nilikuwa nasubiri isogee mbele, siku nikifungua nisipate arosto.
 
Back
Top Bottom