Hadithi: Mpangaji

Hadithi: Mpangaji

MPANGAJI 17


By CK Allan, 0746 266 267
Sasa Bwana Yahaya Kidude alikua akitabasamu huku akimpa mkono Sele ambaye hata hakushughulika kuushika,
“bwana Kidude, naomba kujua alipo mke wangu tafadhali” aliuliza Sele huku akisogea
“sikiliza Bwana Gift ni makosa kidogo yalitokea lakini nilitaka tu tuongee kidogo wewe na mke wako na kukupa pole kwa haya yote yaliyokukuta” alisema Bwana kidude akikaa chini
“tafadhali naomba kujua mke wangu alipo” alirudia tena Gift na sasa Bwana kidude akamkonyeza mlinzi wake mmoja ambaye aliingia chumba kingine na na kutoka na Esta,
Gift alimuona mke wake akiwa mzima kabisa na kumkimbilia na kisha wakakumbatiana
“Bwana Gift kama ujuavyo sisi tunatetea haki za watanzania nikaona walau nikuite ili kama kuna chochote naweza kukusaidia katika harakati zako hizi” alisema Bwana Kidude
“kunisaidia huko kwa kuniteka mimi na mke wangu ndio nini?” aliuliza Gift
“kama nilivyokuambia ni kuwa ni makosa madogo tu yamejitokeza lakini lengo tukae pamoja mimi na wewe”
“huu ni ujinga na tafadhali kaa mbali na maisha yangu” alisema Gift akimshika mke wake mkono na kutoka nje
“nafurahi sana kusikia hivyo Gift tuko pamoja” alipaza sauti Bwana kidude
Gift alitoka nje na kumfungulia mke wake mlango kisha akazunguuka haraka na kuondoa gari kwa kasi kuelekea nyumbani kwao
“imekuwaje kwani mbona sielewi” alianza Esta
“hata mimi pia Sielewi” alisema Gift
“ulipoondoka tu na wale jamaa hawa wakaja wakasema kuwa wamekuteka wewe na hivyo nikikataa kuongozana nao tu wanakuua kule kule, lakini pia nashangaa walikua wananilazimisha nitembee vizuri kana kwamba hakuna kitu!” Esta alisema
Sele nae alikumbuka walimuambia maneno hayo hayo
“tutajua tu lengo lao hawa watu,lakini siamini kama wametuchukua vile ili kutuambia ule upuuzi tu” alisema Sele

Tayari ilishafika majira ya saa 10 waliegesha katika mgahawa mmoja na kupata chakula cha mchana,
Sele alifungua sehemu aliyokua anahifadhi vitu vyake vidogo vidogo na ndipo akastuka kuona bahasha ya kaki ikiwa imekunjwa, kwakuwa tayari Esta alishatangulia hakuona ni busara kuifungua ile bahasha muda ule hivyo alichukua tu wallet yake na kushuka kisha wakaagiza chakula na baadae wakarudi kwenye gari kuendelea na safari yao kurudi nyumbani
“vipi kama hii bahasha ina mambo ambayo si Vyema Esta ayaone?” Sele aliwaza
“au pengine kuna kitu kibaya hapa nikifungua tunakufa wote?” aliwaza
Alikuwa na uhakika ile bahasha hakuweka yeye na hivyo lazima amewekewa na wale jamaa
“sele!”
“sele!” Sasa Esta alikua anamtingisha kumstua kwani tayari alikuwa mbali mawazoni
‘basi tu kuna jambo nawaza hapa” alisema Sele sasa akikaribia maeneo ya Mbweni kule wanapoishi
kwa mbali waliona gari la polisi karibu na nyumbani kwao
“itakuwa Mr K alinitafuta sana akanikosa ndio maana akatuma polisi” alisema Sele
“hapana ni mimi nilifanikiwa kumtumia ujumbe kuwa tumetekwa” alisema Esta
“kwa jinsi gani?” aliuliza
“tutaongea nyumbani nimechoka sana sele” alisema Esta sasa akitabasamu kufika kwake
Walifika getini kwao na kukuta tayari polisi wanne wakiwa mlangoni wanawasubiri
“kweli leo imekuwa siku mbaya” aliwaza Sele akishuka
“Bwana Sele sisi ni maafisa wa Polisi na huyu mwenzetu ni mwakilishi kutoka makao makuu ya taasisi ya kupambana na Rushwa, upo chini ya ulinzi kwa kupokea Rushwa ili kumchafua raisi mstaafu pamoja na familia yake, na hapa tuna kibali cha kupekua nyumba pamoja na gari yako!” alisema Yule polisi akitoa hati ya upekuzi
“subiri kwanza nimpigie mwanasheria wangu!” alisema Sele
“unaweza kumpigia tukutane kituoni lakini kwasasa wewe ni mtuhumiwa tayari” alisema sasa wakianza kupekua gari kuanzia kwenye buti ya gari kisha wakaingia ndani na kupekua na kutoa bastola na vitu kadhaa na ile bahasha!

‘Sele kitu gani kinaendelea” aliuliza Esta akihamaki
“sijui Esta”
Wale polisi sasa walisogea na kuanza kufungua ile bahasha ya kaki na kutoa mabunda matano ya fedha dola za kimarekani
“Ohh shit, kidude!’ aliwaza Sele sasa akiwa amekata tama
“Bwana Sele uko chini ya ulinzi”
Walisema sasa huku pingu zikipita mikononi mwa sele
Na kisha wakawaongoza kwenye gari la Polisi na safari ya kuelekea kituoni ilifika
Walifika kituo cha polisi huku sasa taarifa zikisambaa kila kona ya nchi na tayari waandishi wa habari walikua nje ya kituo kikuu cha polisi kwa ajili ya kusubiri wakati sele na mkewe wakiwa wanaletwa chini ya ulinzi mkali, mara baada ya kufika tu waliingizwa kwenye vyumba viwili tofauti na mahojiano yalianza huku Sele akikanusha kila hoja,
Baadae Sele alikataa kutoa ushirikiano akisubiri mwanasheria wake aje, na hivyo hakukua na budi kumsubiri ambaye alifika baada ya masaa matatu,
Aliingia huku akiwa akiwa na huzuni, tofauti na miaka yote ambayo Sele alimjua mwanasheria wake huyo katika baadhi ya kesi chache binafasi na zile za kampuni , leo sio Yule mwanasheria wake aliyekuwa akimjua siku zote
‘hei Rapha, kunani kitu gani kinaendelea?” aliuliza Sele akisimama
“usiwe na shida kaka, ninajaribu kufanya niwezalo lakini niambie ukweli broo” alisema Rapha akiweka begi lake chini lililokuwa na nyaraka zake
“tupishe!” alisema Rapha akimwambie Yule polisi aliyekuwa akimhoji Sele
‘kwa uhalisia unaweza kuona nimechelewa kuja, lakini nilikua nafuatilia kila jambo, Mpaka sasa jamaa wana ushahidi wa kutosha Sele” alianza kusema
“unasemaje wewe?” aliuliza sele alifoka
‘kamera za nyumbani kwako, na kamera za kule nyumbani kwa Kidude zinaonyesha kabisa hakukua na utekaji wowote!, na mbaya zaidi kidude hajulikani alipo mpaka sasa!’alisema Rapha

Sasa sele alifunguka akili zake na kumsimulia hadithi yote mwanzo mapka mwisho
“na mke wangu nae wakamwambia vile vile, kwahiyo walikua wanajua kabisa wanachokifanya ooh no!” alimalizia Sele
“ulishakutana na Bwana kidude au jamaa yoyote kabla ya leo?” aliuliza Rapha
“hapana”
“jamaa wametumia akili sana kutengeneza hii kesi”
“iko hivi, polisi wanasema walipata taarifa kuwa mheshimiwa kidude ndie aliyepanga mambo yote yale kwa kukutumia wewe ili aweze kujipatia umaarufu wa kisiasa, na kumbuka ni yeye aliibua hii kesi hata kipindi kile cha kampeni miaka kadhaa iliyopita, kwahiyo polisi wakawahi kule nyumbani kwake na wengine wakaenda nyumbani kwake,kwa bahati pale kulikua na jamaa yangu mmoja hivi ndio akanijulisha kuwa wewe unatafutwa,
Sasa jamaa wametengeneza mchoro mmoja mzuri sana,ila bado tunaweza kuwashinda, kwasasa tujaribu tuwezavyo upate dhamana” alisema Rapha
Ni kweli nje ya kituo cha polisi tayari watu walikuwa wamejaa na wengine wakifuatilia kwenye mitandao ya kijamii,
Mr K pamoja na watu wengine wa kampuni ya We4u Walifika polisi na kuangalia namna ya kuweza kumtoa Sele na mke wake kwa siku ile lakini jitihada zao ziligonga mwamba.
Kesho yake kupitia vyombo vya habari sasa mke wa raisi mstaafu mama Joan alikua akizungumza na waandishi kuhusu habari hizo
“Tangu siku ya kwanza nilikua nawaambia watu hizi ni tuhuma za Bwana Kidude na wenzake kuchafua yale mambo mazuri yaliyofanywa na Rais Tupa, mimi namjua mume wangu vizuri, hajawahi kuchepuka na wala hakuwahi kuwa na mahusiano yoyote nje na hakuwahi kuwa na mtoto, niwasihi polisi waendelee kumshikilia huyo mwanaharamu mpaka ataje wenzake wote na sheria kali zichukuliwe ili kuwa funzo kwa wengine, na vile vile huyo bwana Kidude aliyetoroka akamatwe haraka” alisema mama Joan huku akiondoka na walinzi wake
Mzee Tuppa wakati akifuatilia habari hiyo alijikuta akitetemeka na kutupa glasi ya maji aliyokua nayo mkononi mwake, kwa mara nyingine tena mke wake huyo alikua anachukua points tatu hivi hivi asingekubali kirahisi alimuita mlinzi wake Joshua
“sasa ni wakati wetu, siwezi kukubali upuuzi mwingine utokee, imetosha” alisema akimshika bega Joshua
 
MPANGAJI 18

By CK Allan

“niambie mzee tufanyaje” aliuliza Joshua
“mtumie mtu wako sasa tumalize hili jambo kabla mambo mengine hayajatokea zaidi” alisema mzee Tupa
Joshua alitoa simu yake ndogo na kubonyeza bonyeza kisha akakaa kwenye sofa akizunguusha zunguusha funguo yake baada ya dakika kama tatu hizi simu yake iliita na akaiweka sikioni
“ndio sasa hivi” kisha akakata simu
“unataka aje hapa?” aliuliza mzee Tuppa
“ndio hapa ndio salama zaidi na hatajulikana usijali mzee!” alisema sasa akitabasamu
“kwasasa ni wewe ninayekuamini Joshua” alisema mzee Tupa kisha wakaendelea kuongea mambo yao mengine wakati wakimsubiri kijana wao huyo
Ni kweli baada ya dakika 40 hivi alifika na mzee Tupa hakuweza kumtambua Yule kijana kabisa mpaka alipokaa kwenye Sofa bado hakuelewa chochote
“huyu ni nani?” aliuliza Mzee Tupaa
“ni Fred huyu mzee, kijana wetu!’ alisema Joshua huku akimkonyeza Fred ambaye alivua ile sura ya bandia aliyokua amevaa na sasa mzee Tupa akatabasamu, aisngekuwa Raisi labda angekuwa katika mshangao zaidi lakini kwa mtu wa cheo chake alishapitia makubwa zaidi ya hizo sura za bandia
“karibu Fred, nadhani Joshua amekuambia utupe abcd za huyo shetani wa kike” alisema mzee Tuppa
“ndio yeye ndio alipanga huo mpango na mzee Kidude alimuita siku ile wakati Gift anatoa ile hotuba yake, walikutana kule gimkana, akamuahidi dola laki mbili endapo atafanikisha zoezi na kisha akamuahidi kuwa atamlinda asikamatwe….”
“kwasasa yuko wapi huyo Kidude?” mzee Tuppa alimkatisha
“yupo kule kwenye nyumba ya madam kule bagamoyo mimi ndio nilimpeleka”
“huyu mwanamke mshenzi sana” alisema Tuppa
“lakini pia samahani mzee kuna jambo jingine!” alisema Fred akisita
“jambo gani, sema jambo gani!” aliuliza Tupa
“kidude anatoka na madam, yaani siku hizi kadhaa wanalala wote, ndio kama hivi nimempeleka huko madam, halafu namuacha namfuata asubuhi kesho! Alisema Fred
Kwa jinsi ambavyo hawakutegemea mzee Tuppa hakushtuka na wala hakujibu chochote baada ya mazungumzo na mikakati kabambe sasa Fred alirudi zake
Mzee Tuppa alikumbuka jinsi alivyomchukua kijana huyo akiwa Raisi wakati huo alienda kuzindua majengo ya chuo cha ufundi huko Tanga ambapo aliona bango la kijana huyo akiwa na umri wa miaka 15 hivi akiomba kuonana nae pamoja na kubanwa na walinzi lakini mzee Tuppa alionana nae na Kijana huyo alimsimulia jinsi wazazi wake walivyouwawa kwenye ugomvi wa shamba, na hivyo raisi akaagizwa kijana huyo aingie kwenye mafunzo ya ufundi veta kujifunza ufundi magari na baada ya muda akaenda JKT na hatimaye akamchukua rasmi kama dereva wa mtoto wake Joan, ni baada ya kuanza kutilia shaka nyendo za mkewe ndipo akamuua kumbadilishia dereva na kumuweka yeye ili amsaidie kumchunguza , Fredi aliifanya kazi hii kwa uaminifu mkubwa na bila mama Joan kuhisi jambo lolote, hata wakati anaenda kumuua mke mwenzake ni yeye Fred aliyempeleka na kisha kutoa taarifa kwa mzee Tupa
Na hii ndio ilisababisha daima mzee Tupa akawa hatua moja mbele ya mke wake mama Joan na hatimaye sasa alitamani kufikisha suala hili mwisho kabisa
Baada ya wiki moja sasa Sele alifunguliwa mashtaka rasmi na kesi yake ikapangiwa tarehe, kutokana na kelele za wanaharakati na kukosekana kwa mzee Kidude, Sele alikubaliwa dhamana yake na kutakiwa kuhudhuria siku ya kesi huku akitakiwa kutosafiri nje ya jiji la Dar es salaam,
Wakati huo huo mzee Tuppa alikua anapanga mipango ya namna ya kumtoa mwanae Gift katika sakata hilo.
Sele alifunguliwa mashtaka manne kwanza kosa la kumchafua Raisi mstaafu na familia yake, na pili kupokea rushwa ya million 200, kosa la kujipatia kipato kwa njia isiyo halali na kosa la nne la kupanga njama na kutenda uhalifu na kwa maelezo ya hakimu bwana Mwimbe ambaye ndie aliyepewa jukumu la kusimamia kesi hiyo kama akipatikana na hatia anaweza kufungwa miaka 20 hadi 30 pamoja na faini isiyopungua shilingi milioni 20.
Kwa mkakati ambao alishaupanga mama Joan, alikua tayari anaanza kusherehekea ushindi kwani aliamini tayari Gift anaishia Gerezani na hata ikibidi kumtumia watu wammalize huko huko Gerezani,
Kama alivyoomba Gift mke wake aliingizwa kwenye kosa moja tu la kushirikiana na mumewe kutenda uhalifu, hata hivyo kwake ilikuwa kesi ndogo tu kwakuwa hakuwa mshiriki wa moja kwa moja..
....................................................
“Kwahiyo huyo mwanamake ndio kaandaa huu upuuzi wote si ndio?” alikua ni mzee tupa sasa akijiweka vizuri pale kwenye kiti alipokuwa amekaa
“ndio mkuu” alijibu Joshua
“sasa sisi nadhani hakuna haja ya kuchelewa tulimalize” alisema mzee Tupa, siku hiyo walikuwa katika kikao kizito sana yeye na kijana wake huyo ambaye hakumchukulia kama mlinzi tu bali sasa alikuwa ni kijana wake kabisa maana hakika walitoka katika masaibu mengi sana
Mzee Tupa aliishakubali kwenda polisi na kuongea ukweli wote lakini asingeweza hata kidogo, kanuni na masharti ya Raisi mstaafu yalilindwa ipasavyo na sasa asingekuwa na namna isipokuwa kuchanga karata zake vizuri dhidi ya mke wake huyo ambaye alikuwa amembatiza jina la shetani,
‘Mimi naona tucheze nao tu hawawezi kutushinda’ alisema Joshua

Baada ya siku chache kabla ya kesi kusomwa polisi walitangaza kumkamata mheshimwa kidude akiwa katika harakati za kutoroka uwanja wa ndege, polisi walidai walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa mheshimiwa kidude anatoroka na hivyo kumshikilia
Jambo hili lilifanya kesi hii kuvutia watu wengi na kuzidi kuongeza umaarufu mkubwa wa Gift ndani na nje ya nchi
Kesi ilisomwa kama kawaida na ikawadia zamu ya mheshimiwa kizito kuhojiwa ambapo bila kupepesa macho aliongea mambo ambayo yalifanya watu waliokuwepo mahakamani kupigwa na butwaa
“kwanza sikuwa ninatoroka, nilikua katika safari zangu za kibiashara na siku zote nilikuwepo nyumbani kwangu na polisi wanajua ninapoishi, je walikuja wakanikosa?” alihoji mzee Kidude ambaye alitaka kusimama mwenyewe mahakamani kujitetea badala ya wakili wake
“mzee Kidude, tuambie wewe na Bwana Sele mlijuana wapi na siku ya tarehe 14, julai 2017 mlikuwa mnafanya nini pamoja?” mwendesha mashtaka aliuliza
“ Mimi nilipata taarifa kwa vijana wangu kuwa huyu Sele anahitaji kuonana na mimi, mimi nimfuate nyumbani kwake, lakini nikakataa na na badala yake nikamwambia yeye aje nyumbani kwangu, ndio siku hiyo akafika lakini hakutaka kuongozana na mkewe yeye alitangulia kwanza na mkewe akaja na vijana wangu wengine kwenye gari nyingine” aisema mzee Kidude
“tuambie mlifanya nini au mliongea nini baada ya yeye kufika hapo nyumbani kwako” aliuliza mwendesha mashtaka
“aliniambia alitaka nimsaidie kushinda kiti cha uraisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania”
“kwa jinsi gani?” aliuliza mwendesha mashtaka
“alisema atanipa kiasi kikubwa cha pesa na alinionyesha kiasi Fulani cha dola za kimarekani na kuniahidi zaidi endapo nitamsaidia kueneza hiyo habari kuwa yeye ni mtoto wa Raisi Tuppa na hivyo hii itamjengea umaarufu na kukubalika” alisema mheshimiwa kidude akiweka vizuri koti lake
“ni hayo tu mheshimiwa hakimu sina zaidi” alisema mwendesha mashtaka akikaa
Na sasa ilikua ni zamu ya wakili wa Sele Rapha kumuuliza maswali
“unasema ulipata taarifa kutoka kwa kijana wako kuwa sele anahitaji kuonana na wewe?”
“ndio” alijibu Kidude
“je unaweza kuiambia mahakama ni njia gani ilitumika wewe kupewa taarifa hiyo, alikupigia simu, alikuja mwenyewe ama ni njia gani hiyo?”
“nimesema nilipewa taarifa kutoka kwa vijana wangu, ama tuseme mlinzi wangu yeye ndio umuulize”
“je ulishawahi kuwasiliana na Sele kabla ya siku hiyo?” aliuliza Rapha
“hapana siku hiyo ndio ilikuwa ya kwanza kuonana nae”
“unaweza kuiambia mahakama ni namna gani mtu anaweza kuwa raisi wa Tanzania?” aliuliza Rapha
“ndio, mara baada ya kutimiza umri wa kisheria, na kupitishwa na chama chake, na kubainika kuwa hana matatizo yoyote ya kiakili anaweza kuchaguliwa kuwa raisi” alijibu mzee kidude
“vizuri sana, sasa kama ni hivyo kwanini Sele akufuate wewe ili umsaidie kuwa Raisi?” aliuliza tena Rapha
“kwakuwa nilisema kwamba alitaka mimi nimsaidie kueneza uvumi kuwa yeye ni mtoto wa Raisi”
“je uliwapigia polisi au taasisi ya kupambana na rushwa kuhusu hilo suala?” aliuliza tena Rapha
 
Back
Top Bottom