Hadithi: Mpangaji

Hadithi: Mpangaji

MPANGAJI 22
By CK Allan

“Mshtakiwa tafadhali jibu, unaweza kutaja majina ya hao watu waliokuwa kwenye hii video?” hakimu sasa aliingilia kati baada ya kuona ukimya usiokuwa wa kawaida kutoka kwa mama Joan
“aah mmmh ah sio mimi na hao watu siwajui!” alisema tena mama Joan na kupelekea watu pale mahakamani kuangua kicheko
“haya tuambie unamfahamu Yule pale?” Mwendesha mashtaka alisema sasa akimnyoshea mkono Fred
“ahhh ndio, Hapana!” alisema mama Joan kwa kusita sita
“Hapana au ndio ?” aliuliza tena
“aaaah, mmhhh” aliongea mama Joan kisha akaanguka chini, hakimu aliahirisha kesi tena na mama Joan akakimbizwa Hospitali huku akisisitiza Mzee Kidude na Sele wasitoke nje Ya jiji la Dar es salaam wakati wote kesi ikiwa inaendelea

“asante sana Baba, sikujua utafanya hivyo! Alisema Doreen sasa walipokuwa nyumbani kwa Mr K kuangaliwa mwenendo wa kesi yao
“kwasasa kesi ya msingi tunakaribia kuimaliza, mzizi wa yote haya ni hii kesi ya msingi, kama mambo yakienda hivi tunashinda hii kesi asubuhi sana” alisema Rapha huku akimalizia soda yake kwenye glas
“unadhani wanaweza kuja na hoja gani?” aliuliza Sele
“hawana hoja zaidi watang’ang’ania validility tu” alisema Rapha
“ndio nini iyo validility?”aliuliza Doreen
“ni muda wa huu ushahidi , kuwa ulikaa muda mrefu bila kutolewa, lakini hoja hii inakufa kwa kuzingia sheria ya ushahidi namba 213 ya mwaka 2005 kuwa ushahidi utaendelea kutumika na kuhesabika ni hai kuanzia siku shauri lilipofunguliwa hadi mwisho wa kesi” alisema Rapha
“hivi kwasasa Mama Joan atakuwa chini ya ulinzi wa Polisi ama bado hajapatikana na hatia?” aliuliza Sele
“Yule ni mtuhumiwa na kutokana na kilichotokea pale lazima atakuwa chini ya ulinzi ili asiharibu upelelezi, lakini tu hatalazimika kutoa ushahidi mpaka daktari athibitishe kwa maandishi kuwa anaweza kufanya hivyo” alisema Rapha
‘oooohoo basi kama ni hivyo mambo ni tofauti na tunavyofikiria” alisema Sele akisimama huku wenzake wakimshangaa tu
“huyu mama anafanya mchezo hizo siku kadhaa za kuwa hospitali inaweza kuwa ni janja yake kufanya jambo Fulani” alisema Sele akijishika shika ndevu zake
“kwani yupo hospitali gani?” alisema Mr K
“Hatujui ngoja tupeleleze mpaka jioni tutakuwa tumepata jibu” alisema Rapha huku akisimama na kuaga wenzake na kutoka nje ya nyumba ya Mr K,
Ni kweli majira ya jioni Sele alipata kujua kuwa mama Joan alikuwa amelazwa katika hospitali ya Mtakatifu Emmaus iliyokuwa kigamboni, Sele alichukua simu yake kisha akaingia kwenye mtandao na kutafuta taarifa za hospitali hiyo pamoja na kuangalia mazingira yake jinsi yalivyo
“naona kuwa kuna jambo haliko sawa kuhusu mama Joan ni kama anaficha kitu Fulani hivi na hata kule kuumwa sidhani kama ni kwa kawaida” alisema Esta sasa akimstua Sele katika mawazo yake hayo
“ah Yule haumwi ninachofikiria ni kuwa anajaribu kwenda kupanga mikakati yake zaidi ili kwamba aweze kutoka katika kesi inayomkabili” alisema Sele
Hata hivyo baada ya siku kadhaa waliitwa tena mahakamani na kuelezwa kuwa kesi yao inaahirishwa tena kwakuwa mama Joan, bado alikua hayupo katika hali nzuri ya kiafya
Hata hivyo baada ya siku chache tu wakili wa utetezi wa mama Joan na mzee Kidude alijitoa kwenye Kesi! Na hivyo ikabidi mzee Kidude ajitafutie wakili wake,
Siku hiyo mzee Kidude akiwa anatoka hospitali kumjulia hali mama Joan akiwa na derava wake ghafla gari moja ilikatisha mbele yake na kusimama kwa ghafla, kitu ambacho kilisababisha kidude kushtuka ghafla na derava wake kufunga breki za papo kwa papo, wakati wakiwa wanashangaa walishuka watu wanne haraka haraka wakiwa na bunduki na kumtoa mzee kidude na kumuingiza kwenye gari yao halafu mmoja wao akaenda kuendesha ile gari na kutokomea, kilikuwa ni kitendo cha dakika mbili tu na sekunde kadhaa,
“semeni jamani mnataka kiasi gani cha pesa semeni jamani!” alisema mzee Kidude
“kaa kimya mzee” walisema wale vijana na sasa safari ikaendelea na kisha wakamfunika kitambaa na kuingia nae kwenye “nyumba yao” ya siku zote, baada ya dakika kadhaa sasa walimfungua kitambaa mzee Kidude

Sasa mzee Kidude aliomba bora awe anaota kuliko kutazamana uso kwa uso na Yule mtu aliyekuwa mbele yake
“pole mzee Kidude naona vijana wamekusumbua kidogo, karibu tuketi rafiki yangu!” alisema mzee Tupa
“kumbe, kumbe, ku-mbe,ni, we-we,’ alisema Mzee Kidude kwa tabu
“usijali,” aliongea mzee Tupa huku akitabasamu kisha akakonyeza walinzi wake ambao waliondoka na kuwaacha wenyewe
“haya mbona hutaki kuniua, niue sasa” alisema mzee Kidude
“mimi sio muuaji , ningetaka kukuaa ningekuwa kule kule bagamoyo, tangu siku ile umelala na mke wangu!” alisema Mzee Tupa na kumuacha mzee Kidude akitapata kutafuta maneno
“usihangaike nisikilize” alianza mzee Tupa
“najua ni wewe unasababisha kesi isisomwe mpaka sasa ukidhani kwamba utaweza kuwanunua mahakimu na hivyo unamuambiaYule shetani mwenzako kuwa azidi kujifanyisha huko hsopitali, sasa nisikilize unatakiwa ufanye mambo mawili tu,
Jambo la kwanza
Upeleke taarifa rasmi kuwa mko tayari kwa kesi kesho kutwa, halafu jambo la pili eleza pesa za Gift ulitoa wapi, na eleza ukweli mahakamani, ni hayo tu, najua unajua nitakachokufanya endapo hutafanya kama ninavyokulekeza” alisema mzee Tupa sasa akimkonyeza Mlinzi wake ambaye alikua mbali kidogo na hapo
“haya warudisheni” aliwaambia
“mpaka kesho asubuhi nitaona uaminifu wako mzee Kidude” alisema mzee Tupa
Sasa mzee Kidude alijikuta akipagawa, kabisa sasa alianza kuamini akili zake zile za mwanzo wakati anatamani kujiingiza katika mchezo huyu, mara kadhaa alikua anajiambia kuwa anacheza na kifo chake mwenyewe “unacheza na mke wa raisi Kidude” ni maneno ambayo yalikua yanamjia mara kwa mara kichwani kwake kabla hajaanza huu ujasiri wake wa kipumbavu
“bossi uko sawa?’ sasa dereva wake alikua akijaribu kumuongelesha bosi wake huyo
“twende nyumbani” alisema tu bila kujibu swali

Walifika na moja kwa moja mzee Kidude alifungua friji na kutoa kilevi na kujimiminia
“kwa mara nyingine tena umalaya umeniponza” alijisemea kidude
Sasa alikua na saa 13 tu kuamua hatima yake,

Mzee tupa alikua amepata simu kutoka kwa Raisi , kama angehitaji msaada wake bila kutambulikana, Mzee Tupa hakutaka msaada uliopilitiliza zaidi tu alitaka kujua mwenendo wa kesi na jinsi mkewe anavyojaribu kujitoa , angekuwa na uwezo hata wa kuomba kesi hiyo ifutwe ama apangiwe hakimu yoyote amtakaye lakini mzee Tupa alisema haki itendeke kwa asilimia mia
Na hivyo siku hiyo ndipo alipopata taarifa kuwa mama Joan alikuwa haumwi bali alikua anavuta muda ili kununua mahakimu na kuweka mambo mengine sawa, na tayari mzee Kidude alipokuwa kule hospitali sasa aliweza kujulishwa kila hatua na kuamua kumchukua jioni ile, mzee Tupa alikuwa na video kadhaa na mauza uza ya mkewe na Bwana Kidude, hakutaka zisambae haraka kwani zilikua zinamchafua yeye pia na sasa akafikiri njia pekee ni kumkaanga mama Joan na mafuta yake mwenyewe, ilikua kazi ndogo tu kumshawishi wakili wake kujitoa na sasa ilikua ni zamu ya Mzee Kidude
Kesho yake hakimu alipokea taarifa kuwa mama Joan anaweza kuendelea na kesi baada ya kupona na hivyo ikapangwa wiki iliyofuata huku wote wakisisitizwa waje na vielelezo vya msingi
Siku hiyo ya hukumu,
Kama kawaida siku hiyo mahakama ilikua imefurika watu kutoka sehemu mbali mbali kwani tayari kesi hiyo ilikua miongoni mwa kesi maarufu sana zilizovutia
Upekee wa siku hiyo mzee Tupa pamoja na watoto wake walikuwepo kushuhudia hukumu ya kesi hiyo
Baada ya kusoma utangulizi na maelezo ya msingi sasa hakimu aliwapa tena nafasi ya pande zote mbili kutoa hoja zao za kuhitimisha na kisha mzee Kidude akapewa nafasi na kutoa ushahidi wake,
Wakati anaingia kizimbani macho yake yalitazamana na mzee Tupa ambaye alimkonyeza na yeye akamkonyeza kisha akaanza kutoa ushahidi wake
“mheshimiwa hakimu, zile pesa nilipewa na mama Joan kuwa niziweke kwenye Gari la Sele kusudi kwamba tumtengenezee kesi ya uhujumu uchumi na ndio nasikitika sana nimedanganya mahakama
Mzee Kidude aumbuka😀
Umalaya umemponza😂
 
Kumbe mambo ni moto Hivi lol ubarikiwe mkuu ngoja niendelee nilipoishia!
 
MPANGAJI ----- MWISHO WA MWISHO

BY CK ALLAN
“ kwahiyo ninaomba sana mheshimiwa Hakimu mahakama inisamehe tu maana nilitishiwa maisha yangu, kuwa nisipofanya hivi maisha yangu yatakuwa hatarini”
Alimaliza kujieleza mzee Kidude huku wakili wake akipigwa na butwaa na kujaribu kuingilia kati
“Mheshimiwa Hakimu mteja wangu hayuko sawa kisaikolojia hivyo naiomba mahakama yako tukufu isitoe uamuzi leo hii” alisema wakili
“napinga mheshimiwa Hakimu” aliingia Kati Rapha
“ mahakama yako tukufu ikubali maelezo ya mshtakiwa kwakuwa hakuna vielelezo vya daktari kuwa ana tatizo la kisaikolojia” alisema Rapha akikaa
“nakubaliana na wewe, maelezo yake yamechukuliwa na mahakama” alisema Hakimu na kisha akajiweka sawa ili kutoa hukumu ya kesi,
Mwendesha mashtaka alisoma maelezo ya kesi na ushahidi wa maelezo ya pande zote mbili na kisha akatoa ushauri wake kuhusu mwenendo wa kesi kisha akamkaribisha hakimu ambaye alisoma tena maelezo na kurejea vifungu kadhaa vya sheria kisha akatoa hukumu yake
“kwahiyo basi, Mahakama imeona kwamba ndugu Sele Selemani Sele hana kesi ya kujibu na mahakama imemuachia huru, hata hivyo kuhusu kesi yake ya madai kuhusu kuwa na undugu na ndugu Lukas Tuppa, mahakama inaruhusu mdai kuleta vielelezo ikiwemo kupima vipimo vya nasaba na mdaiwa, hata hivyo mahakama imemuona kuwa na hatia mshtakiwa Janet Lukas Tuppa , na kutoa adhabu ya miaka 25 gerezani kwa kupanga na kutekeleza mauaji , na vile vile mahakama inamhukumu kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kupanga na kutekeleza utakatishaji wa fedha na uhujumu uchumi, na vifungo hivi vinaenda kwa pamoja, vile vile Mahakama inamhukumu Kidude James Tito miaka 8 gerezani kwa kupanga na kutekeleza njama za uhalifu wa kifedha pamoja na kuidanganya mahakama..”
Sele alipiga magoti chini huku akimshukuru Mungu na kisha akatazama huko na huko na kukumbatiana na wakili wake kisha akakumbatiana na watu wengine huku akisogea sasa kumuelekea mama Joan
Wakati huo mama Joan alikuwa akilia huku askari wakiwa wamemzunguuka katika harakati za kumtia pingu, ni wakati akiwa amenyoosha mikono ili wamfunge pingu kwa haraka alichomoa bastola ya askari mmoja na kujiwekea kichwani, taharuki ilizuka kwa ghafla huku sasa polisi wakimsihi asifanye alichokuwa akitaka
Hata hivyo bila kusita alifyatua risasi na kumpasua kichwa na kuanguka chini..
BAADA YA WIKI MOJA
Doreen alirudi zake Italy huku akiwa amemaliza kabisa kuweka mambo yote sawa,
Siku hiyo Sele alikuwa nyumbani na mke wake wakicheza mchezo wa mpira wa miguu kwenye komputa huku wakitaniana wakati kengele ya mlangoni ilipolia kuashiria kuna ugeni Haraka Sele alifungua simu yake na kufungua program maalum na kuangalia kamera ya nje
“mmhhh mbona kazi ipo!”alisema Sele akimuonyesha mkewe hao wageni wenyewe
“loh, Lukas, waziri Joan, Na Jesca’ mh
Alisema huku akimuangalia mumuwe, wakati huo tayari mzee Lukas alikua akijiandaa kubonyeza kengele kwa mara ya pili, ndipo Sele alimshika mkono mke wake na kutoka nje kwenda kuwapokea,
Alifungua geti kisha akamsogelea mzee Lukas na kumkumbatia kisha akawasalimia Joan na Jesca na kuwakaribisha ndani,
Walitulia zaidi ya dakika tano huku kila moja akishindwa namna ya kuanza mpaka pale mzee Tupa lipovunja ukimya
“usishangae Gift, damu ni nzito kuliko maji, yaliyotokea yametokea, hawa ni dada zako!” alisema mzee Lukas akiwaangalia akina Joan ambao walisimama tena kukumbatiana huku machozi yakiwatoka kisha wakamkumbatia na Esta pia
Baada ya maongezi kiasi sasa waliaga na kusimama
“sasa nataka kuja tena kucheza na wajukuu hapa Gift, wajukuu!” alisema mzee Lukas kwa utani huku akipanda gari na kuondoka
Hakika ilikua siku ya furaha sana kwa Gift na Esta siku hiyo alirudi ndani haraka na kumshika mkono mke wake na kumvuta
“nini tena Gift!’ alisema Esta
“hujamsikia Mzee anasema anataka wajukuu!’’
Alisema Gift huku wote wakiangua kicheko.
MWISHO_____
Asanteni sana kwa uvumilivu wenu na kusoma hadithi hii!
Siwez kuwataja wote lakini niseme mmenitia moyo sana, ni hadithi yangu ya 3 kuleta humu baada ya Kesi ya Mzee Mnyoka na Madam president,
Kwasasa nitaweka pozi kidogo kwakuwa kifaa nilichokua natumia (laptop) nimekisukuma! Kutokana na sababu za hapa na pale!
Basi niseme Tena nawashukuru sana na in shall Allah tutaonana Tena kwenye MZAHA WA DAMU, Huko mbeleni , panapo majaaliwa
Wabilah towfiq
CK Allan
0746 266 267
 
MPANGAJI ----- MWISHO WA MWISHO

BY CK ALLAN
“ kwahiyo ninaomba sana mheshimiwa Hakimu mahakama inisamehe tu maana nilitishiwa maisha yangu, kuwa nisipofanya hivi maisha yangu yatakuwa hatarini”
Alimaliza kujieleza mzee Kidude huku wakili wake akipigwa na butwaa na kujaribu kuingilia kati
“Mheshimiwa Hakimu mteja wangu hayuko sawa kisaikolojia hivyo naiomba mahakama yako tukufu isitoe uamuzi leo hii” alisema wakili
“napinga mheshimiwa Hakimu” aliingia Kati Rapha
“ mahakama yako tukufu ikubali maelezo ya mshtakiwa kwakuwa hakuna vielelezo vya daktari kuwa ana tatizo la kisaikolojia” alisema Rapha akikaa
“nakubaliana na wewe, maelezo yake yamechukuliwa na mahakama” alisema Hakimu na kisha akajiweka sawa ili kutoa hukumu ya kesi,
Mwendesha mashtaka alisoma maelezo ya kesi na ushahidi wa maelezo ya pande zote mbili na kisha akatoa ushauri wake kuhusu mwenendo wa kesi kisha akamkaribisha hakimu ambaye alisoma tena maelezo na kurejea vifungu kadhaa vya sheria kisha akatoa hukumu yake
“kwahiyo basi, Mahakama imeona kwamba ndugu Sele Selemani Sele hana kesi ya kujibu na mahakama imemuachia huru, hata hivyo kuhusu kesi yake ya madai kuhusu kuwa na undugu na ndugu Lukas Tuppa, mahakama inaruhusu mdai kuleta vielelezo ikiwemo kupima vipimo vya nasaba na mdaiwa, hata hivyo mahakama imemuona kuwa na hatia mshtakiwa Janet Lukas Tuppa , na kutoa adhabu ya miaka 25 gerezani kwa kupanga na kutekeleza mauaji , na vile vile mahakama inamhukumu kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kupanga na kutekeleza utakatishaji wa fedha na uhujumu uchumi, na vifungo hivi vinaenda kwa pamoja, vile vile Mahakama inamhukumu Kidude James Tito miaka 8 gerezani kwa kupanga na kutekeleza njama za uhalifu wa kifedha pamoja na kuidanganya mahakama..”
Sele alipiga magoti chini huku akimshukuru Mungu na kisha akatazama huko na huko na kukumbatiana na wakili wake kisha akakumbatiana na watu wengine huku akisogea sasa kumuelekea mama Joan
Wakati huo mama Joan alikuwa akilia huku askari wakiwa wamemzunguuka katika harakati za kumtia pingu, ni wakati akiwa amenyoosha mikono ili wamfunge pingu kwa haraka alichomoa bastola ya askari mmoja na kujiwekea kichwani, taharuki ilizuka kwa ghafla huku sasa polisi wakimsihi asifanye alichokuwa akitaka
Hata hivyo bila kusita alifyatua risasi na kumpasua kichwa na kuanguka chini..
BAADA YA WIKI MOJA
Doreen alirudi zake Italy huku akiwa amemaliza kabisa kuweka mambo yote sawa,
Siku hiyo Sele alikuwa nyumbani na mke wake wakicheza mchezo wa mpira wa miguu kwenye komputa huku wakitaniana wakati kengele ya mlangoni ilipolia kuashiria kuna ugeni Haraka Sele alifungua simu yake na kufungua program maalum na kuangalia kamera ya nje
“mmhhh mbona kazi ipo!”alisema Sele akimuonyesha mkewe hao wageni wenyewe
“loh, Lukas, waziri Joan, Na Jesca’ mh
Alisema huku akimuangalia mumuwe, wakati huo tayari mzee Lukas alikua akijiandaa kubonyeza kengele kwa mara ya pili, ndipo Sele alimshika mkono mke wake na kutoka nje kwenda kuwapokea,
Alifungua geti kisha akamsogelea mzee Lukas na kumkumbatia kisha akawasalimia Joan na Jesca na kuwakaribisha ndani,
Walitulia zaidi ya dakika tano huku kila moja akishindwa namna ya kuanza mpaka pale mzee Tupa lipovunja ukimya
“usishangae Gift, damu ni nzito kuliko maji, yaliyotokea yametokea, hawa ni dada zako!” alisema mzee Lukas akiwaangalia akina Joan ambao walisimama tena kukumbatiana huku machozi yakiwatoka kisha wakamkumbatia na Esta pia
Baada ya maongezi kiasi sasa waliaga na kusimama
“sasa nataka kuja tena kucheza na wajukuu hapa Gift, wajukuu!” alisema mzee Lukas kwa utani huku akipanda gari na kuondoka
Hakika ilikua siku ya furaha sana kwa Gift na Esta siku hiyo alirudi ndani haraka na kumshika mkono mke wake na kumvuta
“nini tena Gift!’ alisema Esta
“hujamsikia Mzee anasema anataka wajukuu!’’
Alisema Gift huku wote wakiangua kicheko.
MWISHO_____
Asanteni sana kwa uvumilivu wenu na kusoma hadithi hii!
Siwez kuwataja wote lakini niseme mmenitia moyo sana, ni hadithi yangu ya 3 kuleta humu baada ya Kesi ya Mzee Mnyoka na Madam president,
Kwasasa nitaweka pozi kidogo kwakuwa kifaa nilichokua natumia (laptop) nimekisukuma! Kutokana na sababu za hapa na pale!
Basi niseme Tena nawashukuru sana na in shall Allah tutaonana Tena kwenye MZAHA WA DAMU, Huko mbeleni , panapo majaaliwa
Wabilah towfiq
CK Allan
0746 266 267
Daaaaah THANKS A LOT BRO I LIKE IT
 
MPANGAJI ----- MWISHO WA MWISHO

BY CK ALLAN
“ kwahiyo ninaomba sana mheshimiwa Hakimu mahakama inisamehe tu maana nilitishiwa maisha yangu, kuwa nisipofanya hivi maisha yangu yatakuwa hatarini”
Alimaliza kujieleza mzee Kidude huku wakili wake akipigwa na butwaa na kujaribu kuingilia kati
“Mheshimiwa Hakimu mteja wangu hayuko sawa kisaikolojia hivyo naiomba mahakama yako tukufu isitoe uamuzi leo hii” alisema wakili
“napinga mheshimiwa Hakimu” aliingia Kati Rapha
“ mahakama yako tukufu ikubali maelezo ya mshtakiwa kwakuwa hakuna vielelezo vya daktari kuwa ana tatizo la kisaikolojia” alisema Rapha akikaa
“nakubaliana na wewe, maelezo yake yamechukuliwa na mahakama” alisema Hakimu na kisha akajiweka sawa ili kutoa hukumu ya kesi,
Mwendesha mashtaka alisoma maelezo ya kesi na ushahidi wa maelezo ya pande zote mbili na kisha akatoa ushauri wake kuhusu mwenendo wa kesi kisha akamkaribisha hakimu ambaye alisoma tena maelezo na kurejea vifungu kadhaa vya sheria kisha akatoa hukumu yake
“kwahiyo basi, Mahakama imeona kwamba ndugu Sele Selemani Sele hana kesi ya kujibu na mahakama imemuachia huru, hata hivyo kuhusu kesi yake ya madai kuhusu kuwa na undugu na ndugu Lukas Tuppa, mahakama inaruhusu mdai kuleta vielelezo ikiwemo kupima vipimo vya nasaba na mdaiwa, hata hivyo mahakama imemuona kuwa na hatia mshtakiwa Janet Lukas Tuppa , na kutoa adhabu ya miaka 25 gerezani kwa kupanga na kutekeleza mauaji , na vile vile mahakama inamhukumu kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kupanga na kutekeleza utakatishaji wa fedha na uhujumu uchumi, na vifungo hivi vinaenda kwa pamoja, vile vile Mahakama inamhukumu Kidude James Tito miaka 8 gerezani kwa kupanga na kutekeleza njama za uhalifu wa kifedha pamoja na kuidanganya mahakama..”
Sele alipiga magoti chini huku akimshukuru Mungu na kisha akatazama huko na huko na kukumbatiana na wakili wake kisha akakumbatiana na watu wengine huku akisogea sasa kumuelekea mama Joan
Wakati huo mama Joan alikuwa akilia huku askari wakiwa wamemzunguuka katika harakati za kumtia pingu, ni wakati akiwa amenyoosha mikono ili wamfunge pingu kwa haraka alichomoa bastola ya askari mmoja na kujiwekea kichwani, taharuki ilizuka kwa ghafla huku sasa polisi wakimsihi asifanye alichokuwa akitaka
Hata hivyo bila kusita alifyatua risasi na kumpasua kichwa na kuanguka chini..
BAADA YA WIKI MOJA
Doreen alirudi zake Italy huku akiwa amemaliza kabisa kuweka mambo yote sawa,
Siku hiyo Sele alikuwa nyumbani na mke wake wakicheza mchezo wa mpira wa miguu kwenye komputa huku wakitaniana wakati kengele ya mlangoni ilipolia kuashiria kuna ugeni Haraka Sele alifungua simu yake na kufungua program maalum na kuangalia kamera ya nje
“mmhhh mbona kazi ipo!”alisema Sele akimuonyesha mkewe hao wageni wenyewe
“loh, Lukas, waziri Joan, Na Jesca’ mh
Alisema huku akimuangalia mumuwe, wakati huo tayari mzee Lukas alikua akijiandaa kubonyeza kengele kwa mara ya pili, ndipo Sele alimshika mkono mke wake na kutoka nje kwenda kuwapokea,
Alifungua geti kisha akamsogelea mzee Lukas na kumkumbatia kisha akawasalimia Joan na Jesca na kuwakaribisha ndani,
Walitulia zaidi ya dakika tano huku kila moja akishindwa namna ya kuanza mpaka pale mzee Tupa lipovunja ukimya
“usishangae Gift, damu ni nzito kuliko maji, yaliyotokea yametokea, hawa ni dada zako!” alisema mzee Lukas akiwaangalia akina Joan ambao walisimama tena kukumbatiana huku machozi yakiwatoka kisha wakamkumbatia na Esta pia
Baada ya maongezi kiasi sasa waliaga na kusimama
“sasa nataka kuja tena kucheza na wajukuu hapa Gift, wajukuu!” alisema mzee Lukas kwa utani huku akipanda gari na kuondoka
Hakika ilikua siku ya furaha sana kwa Gift na Esta siku hiyo alirudi ndani haraka na kumshika mkono mke wake na kumvuta
“nini tena Gift!’ alisema Esta
“hujamsikia Mzee anasema anataka wajukuu!’’
Alisema Gift huku wote wakiangua kicheko.
MWISHO_____
Asanteni sana kwa uvumilivu wenu na kusoma hadithi hii!
Siwez kuwataja wote lakini niseme mmenitia moyo sana, ni hadithi yangu ya 3 kuleta humu baada ya Kesi ya Mzee Mnyoka na Madam president,
Kwasasa nitaweka pozi kidogo kwakuwa kifaa nilichokua natumia (laptop) nimekisukuma! Kutokana na sababu za hapa na pale!
Basi niseme Tena nawashukuru sana na in shall Allah tutaonana Tena kwenye MZAHA WA DAMU, Huko mbeleni , panapo majaaliwa
Wabilah towfiq
CK Allan
0746 266 267
Hongera sana chief, wewe ni mwandishi mzuri sana . Jaribu kuweka hizi kazi kwenye vitabu

Asante

Sent from my CPH2219 using JamiiForums mobile app
 
MPANGAJI ----- MWISHO WA MWISHO

BY CK ALLAN
“ kwahiyo ninaomba sana mheshimiwa Hakimu mahakama inisamehe tu maana nilitishiwa maisha yangu, kuwa nisipofanya hivi maisha yangu yatakuwa hatarini”
Alimaliza kujieleza mzee Kidude huku wakili wake akipigwa na butwaa na kujaribu kuingilia kati
“Mheshimiwa Hakimu mteja wangu hayuko sawa kisaikolojia hivyo naiomba mahakama yako tukufu isitoe uamuzi leo hii” alisema wakili
“napinga mheshimiwa Hakimu” aliingia Kati Rapha
“ mahakama yako tukufu ikubali maelezo ya mshtakiwa kwakuwa hakuna vielelezo vya daktari kuwa ana tatizo la kisaikolojia” alisema Rapha akikaa
“nakubaliana na wewe, maelezo yake yamechukuliwa na mahakama” alisema Hakimu na kisha akajiweka sawa ili kutoa hukumu ya kesi,
Mwendesha mashtaka alisoma maelezo ya kesi na ushahidi wa maelezo ya pande zote mbili na kisha akatoa ushauri wake kuhusu mwenendo wa kesi kisha akamkaribisha hakimu ambaye alisoma tena maelezo na kurejea vifungu kadhaa vya sheria kisha akatoa hukumu yake
“kwahiyo basi, Mahakama imeona kwamba ndugu Sele Selemani Sele hana kesi ya kujibu na mahakama imemuachia huru, hata hivyo kuhusu kesi yake ya madai kuhusu kuwa na undugu na ndugu Lukas Tuppa, mahakama inaruhusu mdai kuleta vielelezo ikiwemo kupima vipimo vya nasaba na mdaiwa, hata hivyo mahakama imemuona kuwa na hatia mshtakiwa Janet Lukas Tuppa , na kutoa adhabu ya miaka 25 gerezani kwa kupanga na kutekeleza mauaji , na vile vile mahakama inamhukumu kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kupanga na kutekeleza utakatishaji wa fedha na uhujumu uchumi, na vifungo hivi vinaenda kwa pamoja, vile vile Mahakama inamhukumu Kidude James Tito miaka 8 gerezani kwa kupanga na kutekeleza njama za uhalifu wa kifedha pamoja na kuidanganya mahakama..”
Sele alipiga magoti chini huku akimshukuru Mungu na kisha akatazama huko na huko na kukumbatiana na wakili wake kisha akakumbatiana na watu wengine huku akisogea sasa kumuelekea mama Joan
Wakati huo mama Joan alikuwa akilia huku askari wakiwa wamemzunguuka katika harakati za kumtia pingu, ni wakati akiwa amenyoosha mikono ili wamfunge pingu kwa haraka alichomoa bastola ya askari mmoja na kujiwekea kichwani, taharuki ilizuka kwa ghafla huku sasa polisi wakimsihi asifanye alichokuwa akitaka
Hata hivyo bila kusita alifyatua risasi na kumpasua kichwa na kuanguka chini..
BAADA YA WIKI MOJA
Doreen alirudi zake Italy huku akiwa amemaliza kabisa kuweka mambo yote sawa,
Siku hiyo Sele alikuwa nyumbani na mke wake wakicheza mchezo wa mpira wa miguu kwenye komputa huku wakitaniana wakati kengele ya mlangoni ilipolia kuashiria kuna ugeni Haraka Sele alifungua simu yake na kufungua program maalum na kuangalia kamera ya nje
“mmhhh mbona kazi ipo!”alisema Sele akimuonyesha mkewe hao wageni wenyewe
“loh, Lukas, waziri Joan, Na Jesca’ mh
Alisema huku akimuangalia mumuwe, wakati huo tayari mzee Lukas alikua akijiandaa kubonyeza kengele kwa mara ya pili, ndipo Sele alimshika mkono mke wake na kutoka nje kwenda kuwapokea,
Alifungua geti kisha akamsogelea mzee Lukas na kumkumbatia kisha akawasalimia Joan na Jesca na kuwakaribisha ndani,
Walitulia zaidi ya dakika tano huku kila moja akishindwa namna ya kuanza mpaka pale mzee Tupa lipovunja ukimya
“usishangae Gift, damu ni nzito kuliko maji, yaliyotokea yametokea, hawa ni dada zako!” alisema mzee Lukas akiwaangalia akina Joan ambao walisimama tena kukumbatiana huku machozi yakiwatoka kisha wakamkumbatia na Esta pia
Baada ya maongezi kiasi sasa waliaga na kusimama
“sasa nataka kuja tena kucheza na wajukuu hapa Gift, wajukuu!” alisema mzee Lukas kwa utani huku akipanda gari na kuondoka
Hakika ilikua siku ya furaha sana kwa Gift na Esta siku hiyo alirudi ndani haraka na kumshika mkono mke wake na kumvuta
“nini tena Gift!’ alisema Esta
“hujamsikia Mzee anasema anataka wajukuu!’’
Alisema Gift huku wote wakiangua kicheko.
MWISHO_____
Asanteni sana kwa uvumilivu wenu na kusoma hadithi hii!
Siwez kuwataja wote lakini niseme mmenitia moyo sana, ni hadithi yangu ya 3 kuleta humu baada ya Kesi ya Mzee Mnyoka na Madam president,
Kwasasa nitaweka pozi kidogo kwakuwa kifaa nilichokua natumia (laptop) nimekisukuma! Kutokana na sababu za hapa na pale!
Basi niseme Tena nawashukuru sana na in shall Allah tutaonana Tena kwenye MZAHA WA DAMU, Huko mbeleni , panapo majaaliwa
Wabilah towfiq
CK Allan
0746 266 267
shukran sana allan
 
Back
Top Bottom