Hadithi: Mpangaji

Hadithi: Mpangaji

Hapa kuna la kujifunza enyi wanawake

Usiku ule ulikuwa wa furaha sana kwa wawili wale na ipofika asubuhi Esta alilipa Bili yote ya pale kisha safari ikaanza.
 
Yes hii wakati nauguza mguu wangu, nashuka nayo. Hivi unajua baridi hii ya asubuhi, mguu ndio unauma kama unakatwa duh. Asante acha niianze...

Yeah kwenye baridi inauma inavutaa balaaa!!
Pole dear hii asubuhi usisahau kuchuaa
anaekuchuaa asikuonee hurumaa asugue kwanguvu dawa ipenye vizuri!!
Hayo maumivu yake ni balaa!!
Ugua pole kipenzi!
 
Yeah kwenye baridi inauma inavutaa balaaa!!
Pole dear hii asubuhi usisahau kuchuaa
anaekuchuaa asikuonee hurumaa asugue kwanguvu dawa ipenye vizuri!!
Hayo maumivu yake ni balaa!!
Ugua pole kipenzi!
Asante sana na kwa maelekezo. Ubarikiwe sana mrembo Antonnia 😘😘😘
 
Yeah kwenye baridi inauma inavutaa balaaa!!
Pole dear hii asubuhi usisahau kuchuaa
anaekuchuaa asikuonee hurumaa asugue kwanguvu dawa ipenye vizuri!!
Hayo maumivu yake ni balaa!!
Ugua pole kipenzi!
Juzi nilikua napitia profile yangu ya Jf nikaona wewe upo kwenye thread zangu za kuanzia mwaka 2013-14 huko!

Kwa Bahati mbaya umefunga PM Yako ila namba yangu unayo naomba nitafute aisee!! Antonnia
 
Juzi nilikua napitia profile yangu ya Jf nikaona wewe upo kwenye thread zangu za kuanzia mwaka 2013-14 huko!

Kwa Bahati mbaya umefunga PM Yako ila namba yangu unayo naomba nitafute aisee!! Antonnia
Akhsaaannteeeeehhh ! Kumbe ni longtime number one big fan eeh auweeehhh🕺✌️!!

Wee Namba yako sina mkuu!
 
Hii Story nimeanza leo nikiwa MAKOLE - DOM, now napita Kibaha nimeshaimaliza
 
MPANGAJI 16

By CK Allan
Jengo lilionekana kama lipo chini ya ardhi hivi na Sele aliangaza huku na huku ili kuweza angalau kuhisi kama alishawahi kuwepo kwenye jengo lile kabla, akili zake sasa zilikiri kabisa kuwa ile iikuwa ni mara ya kwanza kwa yeye kuwepo katika jengo lile walishuka ngazi kuelekea chini zaidi na kutokea kwenye eneo moja hivi kama ukumbi na kisha wakasimama hapo huku Sele akionyeshwa chumba cha kuingia na wale jamaa wakasimama nje Sele alisogea na kuvuta kitasa cha mlango na kuingia ndani, kwa sekunde kadhaa hivi alisimama akiduwaa baada ya kuona sura iliyokuwa mbele yake, hakuamini lakini ilikuwa ni kweli,
Ndio, baba yake mzee Lukas Tuppa alikuwa amesimama mbele yake wakitazamana macho kwa macho! Hatimaye baada ya sekunde chache, mzee Lukas sasa alishindwa kujizuia na kuanza kutoa machozi kisha akamsogelea na kumkumbatia
“I’m so sory Gift, I’m so sory!” alisema mr Lukas sasa akiwa amemkumbatia mwanae huyo, gift nae alijikuta machozi yakimtiririka na kuna namna Fulani alijikuta hasira alizokuwa nazo zikiyeyuka,
Baada ya muda kidogo Gift alikaa kwenye kiti na mzee Tuppa nae akakaa kwenye kiti kingine kisha akaanza hotuba yake fupi
‘najua sina haki yoyote katika hili lakini naomba sana unisikilize Gift, kipindi kile ulikua mdogo sana, nisingeweza kukuambia kila kitu, but only God knows jinsi nilivyoishi kwa kipindi chote hiki bila uwepo wenu’ alianza mzee Lukas sasa hotuba yake huku akimuangalia Gift ambaye alikua ameinama tu huku mikono ikiwa kwenye mashavu
“but why, kwanini lakini baba? Kwanini?” alisema Gift
“nilijitahidi sana kuwa na ninyi lakini mama yako mkubwa alizuia jitihada zangu zote, najua wewe ni smart, unajua mambo mengi na katika hili naomba ujue kuwa vyovyote ilivyo sikuagiza na wala sihusiki na kifo cha mama yako!” alisema Mzee Lukas
“kwanini umenileta hapa?” aliuliza Gift sasa akisimama
“nimekuita hapa kukueleza jambo moja tu kuwa, nipo pamoja na wewe katika kila hatua utakayoamua kuchukua mwanangu, sijui itakavyokuwa na itatokea nini lakini naamini jambo hili litakuwa na mwisho mzuri, je unapanga kufanya nini?” aliuliza mzee Lukas
“hata mimi sijui nitafanya nini ila naamini nitafanya jambo!’ alisema Gift
“sikiliza Gift, aliyemuua mama Yako ana mkono mrefu sana na vita hii haitakuwa Rahisi kwako ingawa nakutakia kila la kheri!” alisema mzee Lukas akimkumbatia tena mwanae huyo
“nitahakikisha unashinda katika hili Gift” alisema mzee Tuppa, Gift alitoka nje na wale jamaa bila kuuliza walitoka na kutoka nae mpaka nje ya jengo kisha wakamfunga tena kile kitambaa na kuingia kwenye gari baada ya mwendo kama wa dakika kumi hivi walimtoa tena kile kitambaa na kumrudishia simu zake kisha wakamuacha maeneo ya Tazara njia panda,
Gift alisimama barabarani na kisha akawasha simu zake na kusoma jumbe mbali mbali pamoja na kuangalia waliomtafuta katika masaa hayo kadhaa ambayo hakuwa hewani
Ni sekunde chache tu tayari simu yake ilionyesha ishara ya jumbe kuingia, alisoma zote haraka haraka huku sasa akiwa katika hali ya tahadhari kwanza alikuta taarifa kuwa mke wake alikua amempigia lakini jambo ujumbe mmoja ni ule uliomshangaza kuwa kuna mtu anajaribu kufungua mlango wake nyumbani kwake!
“haiwezekani! Haiwezekani!” alisema sasa akijaribu kumpigia Esta ,
Hakupatikana! Alijaribu zaidi ya mara mbili na tayari alijihakikishia kuwa hakupatikana!
Sasa alichanganyikiwa akipungia mkono boda boda iliyokuwa mbele yake..
‘twende haraka,!” alisema

Gift alifika nyumbani na kukuta geti lake liko wazi, haraka sana alijitosa ndani huku akiita jina la mke wake, ni sasa aligundua bado mtu wa boda boda alikua anampigia honi nje kuashiria malipo yake, aliingia ndani na kutoa elfu 10 na kumpa huku akirudi ndani haraka, aliingia kwenye chumba chake cha ulinzi na kuanza kuangalia matio yaliyopita,
Kumbe wakati wakiwa wanatoka na akina Michael gari nyingine iliingia muda mfupi na walionekana na alishuka mwanamke mmoja na mwanaume kisha waliingia ndani na Esta alionekana kwenda kufungua geti waliongea kidogo huku Esta akiwakaribisha ndani ambapo baada ya muda aliingia Yule mwanamke pekee huku Yule mwingine akiangalia huku na huko bila shaka alihisi kulikua na kamera eneo hilo baada ya dakika kadhaa Esta alionekana akitoka na Yule mwanamke kisha akarudi mlangoni na kuufunga na kupiga hatua moja kisha wakaingia kwenye gari, hakukua na purukushani yoyote, na kisha wakaingia kwenye gari na kuondoka
“inamaana hajatekwa?” aliwaza Sele
“lakini hawa ni akina nani?” alisema huku akirudisha nyuma kipande cha video wakati Esta anafunga mlango aliangalia kwa muda kidogo kisha akatoa simu yake alikagua ule muda ambao alitumiwa ujumbe mfupi kuwa kuna mtu anajaribu kufungua mlango wa nyumba yake akaona ni muda ule ule wakati Esta anafunga mlango!
Haraka wazo likamjia Esta alifanya makusudi kukosea zile password ili sele apate ujumbe huo vile vile alijua kabisa wale jamaa walikuwa wanajua wanaonekana kwenye kamerza za ulinzi ndio maana wakafanya waliyoyafanya “kumteka Esta Kistaarabu’ aliwaza sasa Sele akienda kwenye kabati lake na kutoa bastola yake na kuiweka kiunoni kisha akatoka nje na kuingia kwenye gari lake na kuliwasha hakufika mbali sana simu yake ikaita na haraka aliichukua na kuiweka sauti kubwa
“hello Gift tuko na mke wako hapa, naamini unataka kumuona akiwa hai tena” sauti ya upande wa pili ilisikika
“nyie ni akina nani, na kwanini mmemteka mke wangu?’ Gift aliuliza akiwa amehamaki
“wewe fuata maelekezo yetu tu na mke wako atakuwa salama” ile sauti ya kiume upande wa pili ilisikika
Haya semeni mnataka nini!” alisema sasa Gift huku akipunguza mwendo wa gari
“njoo hapa makumbusho kuna baa inaitwa TULIP iko pembeni ya kituo cha kuuza mafuta ukifika hapo ingia kama unataka kuweka mafuta hapo sisi utakuta mtu anakusubiri hapo atakuelekeza cha kufanya”
Gift hakujibu aliindoka kwa mwendo wa haraka kama alikua anacheza sinema vile na baada ya dakika arobaini tu alikua makumbusho akauliza ilipo baa ya TULIP na baada ya muda mfupi alikuwa kwenye kituo cha mafuta alisogeza gari kana kwamba anataka kujaza mafuta wakati akiwa anashangaa shangaa alisikia kioo cha gari yake kikiwa kinagongwa ikabidi ashushe vioo na kumuangalia, Yule mtu alitoa simu yake na kubonyeza bonyeza kisha akamuonyesha Gift ambaye haraka alifungua gair na kutoka, niambie yuko wapi, alisema Sele sasa akimshika shati Yule jamaa
“ahaaa toa mkono wako jamaa” alisema Yule jamaa kwa dharau
“rudi kwenye gari” alisema sasa akiuondoa mkono wa sele
Sele hakuwa na namna isipokuwa kurudi kwenye gari na kuingia ndani Yule jamaa nae aliingia kisha akavuta mkanda wake kuuweka vizuri
“twende” alisema
“wapi sasa mbona kama unanizingua wewe jamaa!” Sele alisema akiwa amekasirika
‘nyosha hapo kwenye huo uzio kama unaenda Bar halfu nitakuelekeza” alisema na sele akatii na kisha wakapita kwenye uzio mmoja hivi baada ya ile bar na kutokea kwenye geti moja jeusi hivi na Yule jamaa akabonyeza Honi mara mbili na gei likafunguliwa
“Karibu sana bwana Gift naomba acha kila kitu chako kwenye gari” alisema Yule jamaa akiwa sasa anashuka kwenye gari
“sikiliza, ujinga wako mmoja tu utasababisha mke wako auwawe , unatakiwa utembee bila kuonyesha mashaka kabisa wakati tukiingia kwenye iyo nyumba” Yule jamaa alisema
Sele sasa aligundua hawa jamaa kuna kitu kingine cha ziada wanapanga maana alikumbuka kule kwenye kamera za usalama nyumbani kwake Esta nae alikua anatembea kawaida kutoka pale nyumbani kwake!
“ngoja tuone huu mwisho wa huu mchezo” aliwaza akitoa bastola yake na simu zake na kuacha ndani ya gari kisha akashuka nje ya gari na kumfuata Yule jamaa kuingia ndani ilikua ni sebule nzuri yeny samani za kisasa baada ya dakika kadhaa walitokea watu watatu mmojawapo akiwa mzee hivi ambaye sura yake haikuwa ngeni sana na Sele alimtambua mara mmoja alikua mgombea wa Uraisi kwa tiketi ya upinzani katika uchaguzi uliopita kupitia chama cha TAI bwana Yahaya Kidude alikua akionyesha tabasamu na Sele hakujali aliuliza tu alipo mke wake
Leo nimeishia hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom