Hadithi: My Soulmate

Hadithi: My Soulmate

MY SOULMATE SEHEMU YA 11.
Produced by : Equatorstory Specials.
Stela : "Nickson unaitwa na boss ofisini kwake."Alisema wakati Nickson yupo ana shughulika na mambo yake ya kawaida.
Nickson : "Sawa naenda."
Nickson alisimama mara moja na kuelekea ofisini kwa Boss wake.
Boss : "Karibu kijana kaa." Boss alisema akimuonesha kiti cha kukaa.
Nickson : "Asante Boss."
Boss : "Sasa kijana unajua kwa nini nimekuita hapa!?".
Nickson : "Hapana Boss sijajua bado yamkini ni mrejesho kuhusu ile barua pepe niliokutumia kuhusu budget ya mradi mpya?"
Boss : "Hapana ilo tutaongea wakati mwigine"
Nickson : "Sawa boss."
Bosss : "Kijana unajua mimi ni mtu wa sheria sana sipendi mtu ambae ana pindisha sheria."
Nickson : "Ndio Boss najua."
Boss : "Na unajua kabisa nilikutoa mbali sana kijana!?".
Nickson : "Ndio boss najua!"
Boss : "Sasa hmmmm". Boss ali shusha pumzi.
Nickson : "Ndio Boss!."
Boss : "Sasa kijana sijui nikufanyaje!"
Nickson : "Kwa nini Boss!?"
Boss : "Hujui kosa lako!?"
Nickson : "Hapana."
Boss : "Una mahusiano gani na Stela!?"
Nickson : "Una maaana gani boss!?". Hapo moyo wa Nickson ulipasuka. Alijua yamkini boss ashagundua kuhusu hili penzi la siri.
Boss : "Hujaelewa ama hujasikia!?".
Nickson : "Stela si si...."
Boss : "Nini!? Kijana umevunja masharti na ushahidi ninao!."
Nickson : "Ushahidi gani boss." Nickson alianza kuhisi kizunguzungu kwa mbali.
Boss : "Ninayo video ya wewe na Stela mkikumbatiana na kupigana mabusu huko jikoni kwani hujui kina camera humo ama."
Nickson : "Hapana Boss niliju....."
Boss : "Sasa nini una fanya yerro!?"
Nickson : "Boss ni bahati mbaya". Nickson alianza kuishiwa na pumzi alishindwa kumalizia hata sentensi yake alianza kuona kama sakafu inasogea kushoto na kulia.
Boss : "Yerro jielezeee."
Nickson : "Boss ni ....." Nickson alianza kuangusha machozi akishindwa hata kuongea akijua tayari ameshapoteza kazi yake ataishije!?
Boss : "Kijana HUNA KAZI TENA." Boss alisema kwa msisitizo huku akimpatia barua ya kufutwa kazi.
Nickson alinyanyuka akapokea hiyo barua akatoka ofisini kwa boss wake.
Boss : "Kijana fanya kukabidhi kila kitu kwa boss wako Angela. Na nisikuone tena humu ndani mjinga kabisa.."
Nickson : "Sawa boss.". Nickson alienda kwenye chumba jiko la ofisi hiyo akiangusha macozi. Alie muona akiwa katika hali hiyo ni Angela naye akamfuata huko.
Angela : "Nickson nini shida!?."
Nickson ali toa barua aliyopewa akampa Angela ajisomee . Nickson akafuta machozi na kunawa uso akawa kawaida tu alijisemea moyoni yamkini ni ishara ya Mungu niache kweli hii kazi japokuwa itakua ngumu lakini Mungu yupo.
Angela : "Weweeeeee jamani pole."
Nicskon : "Asante!!.."
Angela : "Sasa mbona kwenye barua imesema kuwa uikuwa ume onekana ukiwa ki mahaba na mfanyakazi wa hii ofisi lakini hawajasema ni nani ama ni mimi!?. "
Nickson : "Ah wewe unajua mahaba sasa!?". Wakacheka wote.
Angela : "Nickson acha utani bhana mi nina maanisha bhana eti ni ile siku ambayo uli ni kiss mdomoni kama ndo hivyo sema!.."
Nickson : "Hapana wala sio hapo!."
Angela : "Sasa je!?".
Nickson : "Boss amegundua nilikuwa natoka na Stela."
Angela "Weweee."
Nickson akamuelezea kinaga ubaga kila kitu kilichotokea. Angela hakuamini lakini pia alielewa kwanini ile siku Stela alimfyonza kisa Nickson.
Angela : "Jamani pole."
Nickson : "Nishapoa asante."
Nickson akatoka akamkabidhi kila kitu boss wake mpya Angela vitu vyote alivyotakiwa kukabidhi. Wakati huo wote boss alikua ofisini kwake na Stela wakionekana wakiongea maongezi ya kina.
Angela : "Jamani kwaheri mchungaji!. Ukatuombee huko Mungu anapokupeleka."Nickson ali cheka haku amini kama Angela ni Boss wake wamekua na ukaribu sana kana kwamba sio mtu na boss wake.
Nickson : "Nitafunga na kuwaombea."Nckson alianza kuondoka Angela akamuita,
Angela : "Pole shika hii jamani itakusaidia huko mbele ya safari si amini amini kama ndo unaondoka moja kwa moja. Kama ni uongo utanirudishia hela zangu mara mbili."
Nickson : "Hahaha haya bhana. Kwaheri."
Angela alimkumbatia mara ya mwisho lakini pia wafanyakazi wengine hawa amini kama Nickson hayupo katika ofisi hiyo tena.
Nickson ali rudi nyumbani kila mmoja aki mshangaa bila kuamini kwamba Nickson amerudi mapema .
Dulla : "NI vipi kaka!?"
Nickson : "Salama tu kaka niambie."
Dulla : "Ah mbona mapema hivyo unaumwa nini? "
Nickson : "Hapana mkuu ni majanga tu ya kawaida ."
Dulla : "Majanga gaani?".
Nickson : "Ndugu yangu nimefukuzwa kazi."
Dulla: "Sasa kisa kazi unataka kulia . Aaaaah mkuu wacha zako mi najua wewe mpambanaji sana wewe kazi yoyote unashika."
Nickson : "Hiyo kweli.."
Dulla : "Sasa wewe usiogope wewe ni mwana eti!. Usiwaze wala nini kufukuzwa kazi mimi nimefukuzwa mara tano!. Mpaka nikaona huuu ujinga wa kuomba kazi sio huu."
Nickson : "Acha utani!!".
Dulla : "Aaaaah wewe unanionaje!??? Mimi nimepigika nimekula matusi kwenye gereji za watu mara zingine nimeacha kazi sijaipwa lakini napambana."
Nickson : "Dah ndio maisha yalivyo."
Dulla : "Wewe usiwe na shaka mwana hapa nitasimama mwana huta lala njaa nikiwa ninacho kaka!." Dulla aliendelea kusema hivyo akiwa ana malizia kuvuta sigara yake.
Nickson : "Sawa ngoja nika weke huu mkoba wangu ."
Wakati Nickson anaingia akasikia sauti ya Bertha .
Bertha : "Maajabu leo kuona mwezi mchana."
Nickson :"Kivipi!?."
Bertha: "Mbona mapema nini kimekusibu au ulipotea kwenda ofisini kwako umepa sahau ama!?"
Nickson : "Kumbe leo kidato cha nne wanafanya mitihani.... Sikujua ". Nickson na Bertha wakacheka maana hiyo haihusiani.
Bertha :"Hahahaha wewe kaka kwanini usiwe kwenye vichekesho vya TV."
Nickson : "Ah hawalipi vizuri yani millioni nne!? Sasa nina fanyia nini!?"
Bertha : "Kwema lakini mbona mapema jaman unaumwa au!?"
Nickson : "Hapana. Inaonekana umetoka kuoga nenda kavae kabla hiyo kanga haijakaukia mwilini alafu nitakuja nikupe simulizi nzima."
Bertha : "Haya nivaaajae!? Au twende tukapate na ka soda kama hutojali ili stori inoge?".
Nickson : "Yote mema!".
Bertha : "Sawa."
Nickson na bertha walitoka hapo na kuelekea pahali walipopataka . Nickson akaumuelezea jinsi alivyo fukuzwa kazi . Na bertha aliamuwa kumuelezea Nickson kinaga ubaga jinsi alivyo gombana na mumewe. Hii ni baada ya Bertha kuona anaweza kumuamini Nickson.
Walikaa sehemu hiyo mpaka ilipofikia jioni wakijadili mambo tofauti tofauti kuhusiana na mada mbalimbali za maisha.
Nickson alipokea ujumbe mfupi wa maaandishi kutoka kwa Stela ukisema "Naomba tuachane sasa hivi hauna kazi hutoweza kunihudumia au hata kunimudu lakini pia utanifanya nipoteze kazi.". Nickson alishindwa kuamini inakuwaje Stela hajafukuzwa kazi?. Hakutaka kuwaza sana aliona litampotezea muda. Lakini alimtumia ujumbe mfupi wa simu.
Nickson : "Stela jamani wewe si mpenzi wangu unatakiwa unishikee mkono na kunipa ushirikiano wako niweze kusonga mbele."
Stela : "Koma kuniita mpenzi wako huelewi ama!?".
Nickson : "Jamani Stela muda huu ndo nakuitaji zaidi katika maisha yangu!."
Stela : "Hapana siwezi nikawa na mpenzi asie na mbele wala nyuma. Huna lolote utanisaidia nini? Utaleta changamoto gani za kimaendeleo katika maisha? Tafadhali sana unikome."
Nickson aliamua kukaa kimya hakujibu tena ujumbe aliotumiwa.
Maisha yaliendelea huku 'urafiki ' wa Nickson na Bertha ukizidi na Nickson hakua mtu wa kuchagua kazi yeye alikua akifanya kazi zozote anazo itiwa iwe ni zege,kuchimba mitaro kubeba mizigo alimradi mdomo unaenda kinywani. Nickson aliendelea ku sambaza maombi ya kazi kwa kampuni kadhaa ambazo anaweza kupata kazi bila mafanikio.Pamoja na kuwa Nickson anao ndugu wengine ambao wanaweza kumsaidia kifedha haku diriki kuwa omba aliona ni kheri apambane na afe ki sabuni.
Mr Mandoto alionekana akiendelea kumtafuta mke wake alipo potelea bila mafanikio lakini hakati tamaa!
Itaendelea.....
 
MY SOULMATE SEHEMU YA 13.
Produced by : Equatorstory Specials.
Ni mida ya saa kumi na mmoja jioni Nickson anakutana na rafiki yake kipenzi walio soma wote tokea shule ya msingi.
Nickson : "Ahh Erick za kupotea kaka!".
Erick : "Aisee kaka umekuwa ndugu yangu". Waliongea huku wakikumbatiana.
Nickson : "Man nili kumiss sana!."
Erick : "Hata mimi kaka khaa ni kama mwaka na zaidi tokea tuonane mara ya mwisho tulipokuwa chuo!."
Nickson : "Ahh mambo ya hapa na pale tu mkuu."
Erick : "Vipi shemeji yetu anasemaje!?."
Nickson : "Ah shemeji yako pasua kichwa mkuu anapenda sana hela kama wallet."
Erick : "Hahahah wewe jamaa bado tu unahongaga!? Mimi siwezagi kuonga kabisa yani mwanamke ntampa hela kama ntapenda na sio kumuhonga."
Nickson :"Aisee kaka nataka nikiwa mkubwa niwe kama wewe!."
Erick : "Hahahahaahaah utaweza wewe? Wanawake ukiwa endekeza watakuja kukuletea madharau."
Nickson : "Lakini kwani si unampa hata ya vocha ama nayo hairuhusu kwenye kitabu cha wahuni?"
Erick : "Wewe uwape vocha si uta baki na kucha zako tu!? Mimi nina ma dem watano na wote siwapi hata mia. Ukisema uwape vocha wata taka za elfu 5 na mara 5 hiyo si elfu 25 nani anataka kufiliska!?"
Nickson : "Duhh hapo kaka umenishinda."
Erick : "We mzoeshe hela uone kuwa mgumu atakuomba mwishowe ata puuzia tu. Niambie lakini."
Nickson : "Ndugu yangu mimi nina mpango wa kufanya mradi bhana."
Erick : "Enhee leta maneno....".
Nicskon walikaaa na wakajadili kwa kina na Erick kuhusiana na huo mradi Nickson aliopanga na waka shauriana mambo mawili ma tatu.
Nickson : "Kwa hiyo sasa mkuu vipi utaniunga ama?"
Erick : "Ndugu hapa hakuna kulaza damu twende tukajisajili kabisa BRELA kama kampuni tuanze kuchapa kazi mkuu. Hapa kijana ume nena yani naweza hata nikakupa dada yangu umuoe yule hapendagi hela sana!. "
Nickson : "Sawa basi kesho tutaaanza michakato. Nadhani itakua vyema Kama tungemtafuta Damian tumpe ashulikie maswala haya sis tuendelee na mengine ama vipi?"
Erick : "We jamaa mbona mvivu hivyo?"
Nickson : "Mhh sasa wewe unataka kufatilia ama?".
Erick :"Haya sawa tumpe Damian si ndo kazi yake!."
Nickson :"Eeeh mkuu nitawasiliana nae!."
Erick : "Sawa mkuu kwa heri!."
Basi tokea wakati huo Nickson na Erick wali ingia katika makubaliano ya kazi na waka anza ku haingaika huku na huku kwa ajii ya kuhakikisha mradi unafanikiwa.
Bertha : "Mambo Nickson."
Nickson : "Poa mzima wewe?"
Bertha : "Hapa nimekufa hujui tu!"
Nickson : "Nini shida!?"
Bertha : "Nilikumiss tu ."
Nickson : "Aaaah sasa si ungenipigia simu?"
Bertha : "We mwenyewe saivi upo bize sana!."
Nickson : "Yani huu mradi ninao fanya unanifanya niwe bize."
Bertha : "Bhana mimi nina njaa twende tukale chipsi ile sehemu yetu."
Nickson : "Sawa twende leo nitalipia."
Bertha : "Aaaah nakuona umesha anza na kupata vi hela bhana eeeh?"
Nickson : "Usha anza nita ghairi mimi?"
Bertha : "Ughairi una huo ubavu wewe?"
Nickson : "We twende bhana."
Nickson na Bertha walienda kula kama ilivyo kawaida yao wakienda wakicheka na kukombatiana na kushikana mikono kama mtu na mpenzi wake na jicho la Mpelelezi likiwa na wao bila wao kujua kuwa wanafuatiliwa kwa siku kadhaa na kila picha zao za furaha zinapokelewa na Mandoto akiwa huko alipo.
Upande mwingine Nyumbani kwa Mr Mandoto akiwa na dada yake ana angalia simu yake kwa hasira na kufyonza.
Mandoto : "Huyu mwanamke sijui nimfanyaje jamani."
Rose : "Kaka nini mbona una hasira sana?"
Mandoto : "Si huyo katuni naniliii mjinga huyu naniliii Bertha."
Rose : "Kwani kafanyaje kaka?"
Mandoto : "Bado yupo na yule mwanaume wake wapo barabarani wanacheka kama wajinga flani hivi."
Rose : "Kaka huyu mwanamke achana nae kalogwa huyo uyo mkaka atakuwa mchawi au kampa limbwata mwone anavyocheka cheka tu."
Mandoto : "Nitamuuuuuuuuuua mimi ngoja nitaenda huko Arusha watanijua mimi ni nani....."
Mara Mandoto simu yake ikaita akapokea aka gundua ni yule mchepuko wake waka anza kupiga story na aka anza kujisahau kuwa alikuwa amekasirika kuhusu Bertha na Nickson akaongea na kucheka na kulegeza macho na sauti kana kwamba sio mwanaume!.
Upande mwingine hotelini Bertha amefika na Nickson waka agiza walichokua wanataka kula.
Bertha : "Jamani Nickson saivi una mambo mengi Duuh"
Nickson : "Mradi najua utanipeleka mbali Mungu ata nijalia tu!."
Bertha : "Mmmmmh Sasa si bora uwe jambazi tu?."
Nickson : "Alafu nikuvamie wewe? Utanipa sh ngapi mimi naogopa kufa unaeza ukapigwa risasi ya kichwa ukafa wakati kuna mbinu zingine?"
Bertha : "Wapi wewe!!.... Sema tu ndo hivyo sina vifaa lakini ile meli ya kusafirshia pesa baharini ninge ivamia kama ningekua ni wale mabaharia wa bahari ya hindi."
Nickson : 'Hahaha kama uko serious si useme tuwape ramani afu watu tumie ka asilimia kidogo ile kitu unaeza vamia sawa lakini watakutafuta mpaka makaburini unacheza nini?."
Bertha : "Weewewe kwani tunawonesha sura? Si tunavaa maski bhana."
Nickson : "Eti eeeh afu unaifikiaje hiyo meli?"
Bertha : "Na mtumbwi..."
Nikcson : "Hahahah hahahahaha hahaha naona leo umeamua kunipa burudani..?"
Bertha : "Kwa nini."
Nickson : "Uvamie meli na mtumbwi si watailenga na jiwe izame!?"
Bertha : "Aaaah bhana sio kimtumbwi si tunatafuti boti nzuri."
Nickson : "Hiyo Idea nzuri lakini silaha hatuna pia hatuna vifaa labda tuwape hiyo idea."
Bertha : "Lakini kweli juzi bhana nilisikia wakisema wamefungua account mtandaoni labda tuwatumie ujumbe?"
Nickson : "Hahahah hao wapo na kazi nyingi sana ety wapate nafasi ya kukujibu?"
Bertha : "We tuwa andikie hivyo hivyo bhana sio mbaya hata tuwasiiane na watu wa huko nchi za nje."
Nickson : "Haya njoo tuwa andikie."
Nickson na Betha walikaaa wakiandika ujumbe huo kuwa shauri wa zamiaji wavamilie ile benki na wakiandika na mawazo yao hapa na pale wakijua hao wazamiaji wa meli hawa wezi kusoma sembuse kuwajibu walipo maliza walicheka na kuendelea na maakuli yao. Nickson aliendelea ku furahia wakati huo na kutokuwaza hata kuhusu Stela. ALikumbuka kwamba bila hela kwa hawezi ku fua dafu. Lakini mpelelezi bila kugundulika alikua anawanasa picha na akiwafatilia bila wao kujua. Yamkini Bertha hamjui mumewe vizuri ndio maaana hakuwa na hata wazo la mumewe kutumia wa pelelezi wa kujitegemea.
Upande mwingine tuna mwona Stela akiwa chumbani na Boss wake.
Stela : "Boss unajua Nickson anafanuya nini?"
Boss : "We nishakwambiaje kuhusu kuni ita ita Boss niite mpenzi bhana au unataka kunikera?"
Stela : "Aahhh wewe usiji chetue sana bhana."
Boss : "Unataka tugombane tena?"
Stela : "Jamani mpenzi nakutania."
Boss : "Enhee unasema yule yerro anafanyaje?"
Stea : "Ana anzisha mradi wa kutengeneza aplikesheni ya notes"
Boss : "Anajisumbua tu huyo"
Stela : "Yani ana pambana sana kuhusu ili swala."
Boss : "Enhee embu nielezee."
Stela : "Anataka kutengeneza aplikesheni ya kutunza notes za chuo na una weza kuwa nazo mahali popote unapotaka."
Boss : "Etyy?? Ilo wazo zuri!".Boss alisema huku anasimama akiwaza mambo kichwani mwake.
Stela ; "Ndio una dhani anaeza akafanikiwa anapoteza muda wake bure."
Boss : "Hapana hapana anaweza akapata mamilioni mengi sana!"
Stela :"Boss hahahahah hahaha ndo unamtania hapo?"
Boss : "Hapana... hapana..... huyu yerro ana fanya kazi nzuri sana yani nimeipenda."Boss alionekana akiwa kwenye mawazo yalio mpata ghafla.
Stela : "Sasa tunafanyaje tumu ajiri?"
Boss : "Hapana tukitaka kumuajiri ata kataaa."
Stela : "Sasa tuna fanyaje?"
Boss : "Sasa mwambie Angela atafute vijana kama waaaaa.. Kwani Nickson anafanya kazi na watu wangapi?"
Stela : "Yupo na best wake tu kama sijakosea."
Boss : "So wapo wawili?"
Stela : "Bhana mi sijui lakini nadhani hivyo."
Boss : "Mwambie Angela andae vijana sita kwa ajili ya hii kazi "
Stela : "We unataka kushindana na hiyo haitofanikiwa bhana!"
Boss : "We huna akili sana kwenye haya maswala hili wazo lina hela sana tukimwachia afanye mwenyewe atafaidika sana."
Stela : "Eeeenh kumbe enh?"
Boss :"Huu mradi unaweza pata takribani millioni nane kwa mwezi."
Stela : "Jamani mpenzi si uta ni nunulia ka gari kangu nikawaoneshe ma rafiki zangu?"
Boss : "We unawaza tu kula hela."
Stela : "Kwa hyo hunitaki?"
Boss : "Mpenzi jamani mama yeyo wangu lazima niku nunulie wewe tena?"
Boss alikusanya kikundi cha vijana na waka anza huo mradi wa kumuiga Nickson bila kuwa ambia watu kuwa ni mradi wa kuiga.
Stela alipo ona kuwa mambo yanaweza kumuendea vizuri Nickson na anaweza kukosa nafasi ya kuya furahia maisha aka anza kujipendekeza kwa Nickson.Kwa kutumia ujumbe mfupi akamwambia.
Stela : "Baby mambo?"
Nickson : "Poa Mambo?"
Stela : "Jamani nimekumis."
Nickson : "Hata mimi nimekumis. Tukutane basi ile hotel tunayoipenda japo nikuone."
Stela : "Hapana sasa hivi kazi zimenibana."
Nickson : "Sawa haina neno."
Stela : "MImi nataka kukuambia tu kitu kimoja Nickson."
Nickson : "Kitu gani nakusikiliza."
Stela : "Sio kwamba siamini kuwa utafanikiwa nina amini. lakini"
Nickson : "Niambie"
Stela : "Nataka kukuambia kuwa yote ninayo fanya ni kukusukuma uende mbele zaidi."
Nickson : "Kweli mpenzi?"
Stela : "Ndio mpenzi ukifanikiwa usinisahau kwa juhudi za kukufanya uende mbele Nickson ama utaniacha ukale na wanawake wengine?"
Nickson : "Hapana mpenzi wangu siezi kukuasaliti."
Stela : "Sawa Nickson pambana mimi nakungojea."
Nickson alifurahi na alipata nguvu na kujua kumbe kuna mtu anampenda? Na alijua kumbe Stela alikuwa mgumu kwake ili apambane kusonga mbele.?Nickson alijiona kama mwanaume kwa matumaini aliopewa ya uongo na Stela.Alifurahi kuona kuna mtu ana msapoti afike mbali alifurahi sana.

Itaendelea..........
Comment yako tu! ya muhimu!
 
MY SOULMATE SEHEMU YA 13.
Produced by : Equatorstory Specials.
Ni mida ya saa kumi na mmoja jioni Nickson anakutana na rafiki yake kipenzi walio soma wote tokea shule ya msingi.
Nickson : "Ahh Erick za kupotea kaka!".
Erick : "Aisee kaka umekuwa ndugu yangu". Waliongea huku wakikumbatiana.
Nickson : "Man nili kumiss sana!."
Erick : "Hata mimi kaka khaa ni kama mwaka na zaidi tokea tuonane mara ya mwisho tulipokuwa chuo!."
Nickson : "Ahh mambo ya hapa na pale tu mkuu."
Erick : "Vipi shemeji yetu anasemaje!?."
Nickson : "Ah shemeji yako pasua kichwa mkuu anapenda sana hela kama wallet."
Erick : "Hahahah wewe jamaa bado tu unahongaga!? Mimi siwezagi kuonga kabisa yani mwanamke ntampa hela kama ntapenda na sio kumuhonga."
Nickson :"Aisee kaka nataka nikiwa mkubwa niwe kama wewe!."
Erick : "Hahahahaahaah utaweza wewe? Wanawake ukiwa endekeza watakuja kukuletea madharau."
Nickson : "Lakini kwani si unampa hata ya vocha ama nayo hairuhusu kwenye kitabu cha wahuni?"
Erick : "Wewe uwape vocha si uta baki na kucha zako tu!? Mimi nina ma dem watano na wote siwapi hata mia. Ukisema uwape vocha wata taka za elfu 5 na mara 5 hiyo si elfu 25 nani anataka kufiliska!?"
Nickson : "Duhh hapo kaka umenishinda."
Erick : "We mzoeshe hela uone kuwa mgumu atakuomba mwishowe ata puuzia tu. Niambie lakini."
Nickson : "Ndugu yangu mimi nina mpango wa kufanya mradi bhana."
Erick : "Enhee leta maneno....".
Nicskon walikaaa na wakajadili kwa kina na Erick kuhusiana na huo mradi Nickson aliopanga na waka shauriana mambo mawili ma tatu.
Nickson : "Kwa hiyo sasa mkuu vipi utaniunga ama?"
Erick : "Ndugu hapa hakuna kulaza damu twende tukajisajili kabisa BRELA kama kampuni tuanze kuchapa kazi mkuu. Hapa kijana ume nena yani naweza hata nikakupa dada yangu umuoe yule hapendagi hela sana!. "
Nickson : "Sawa basi kesho tutaaanza michakato. Nadhani itakua vyema Kama tungemtafuta Damian tumpe ashulikie maswala haya sis tuendelee na mengine ama vipi?"
Erick : "We jamaa mbona mvivu hivyo?"
Nickson : "Mhh sasa wewe unataka kufatilia ama?".
Erick :"Haya sawa tumpe Damian si ndo kazi yake!."
Nickson :"Eeeh mkuu nitawasiliana nae!."
Erick : "Sawa mkuu kwa heri!."
Basi tokea wakati huo Nickson na Erick wali ingia katika makubaliano ya kazi na waka anza ku haingaika huku na huku kwa ajii ya kuhakikisha mradi unafanikiwa.
Bertha : "Mambo Nickson."
Nickson : "Poa mzima wewe?"
Bertha : "Hapa nimekufa hujui tu!"
Nickson : "Nini shida!?"
Bertha : "Nilikumiss tu ."
Nickson : "Aaaah sasa si ungenipigia simu?"
Bertha : "We mwenyewe saivi upo bize sana!."
Nickson : "Yani huu mradi ninao fanya unanifanya niwe bize."
Bertha : "Bhana mimi nina njaa twende tukale chipsi ile sehemu yetu."
Nickson : "Sawa twende leo nitalipia."
Bertha : "Aaaah nakuona umesha anza na kupata vi hela bhana eeeh?"
Nickson : "Usha anza nita ghairi mimi?"
Bertha : "Ughairi una huo ubavu wewe?"
Nickson : "We twende bhana."
Nickson na Bertha walienda kula kama ilivyo kawaida yao wakienda wakicheka na kukombatiana na kushikana mikono kama mtu na mpenzi wake na jicho la Mpelelezi likiwa na wao bila wao kujua kuwa wanafuatiliwa kwa siku kadhaa na kila picha zao za furaha zinapokelewa na Mandoto akiwa huko alipo.
Upande mwingine Nyumbani kwa Mr Mandoto akiwa na dada yake ana angalia simu yake kwa hasira na kufyonza.
Mandoto : "Huyu mwanamke sijui nimfanyaje jamani."
Rose : "Kaka nini mbona una hasira sana?"
Mandoto : "Si huyo katuni naniliii mjinga huyu naniliii Bertha."
Rose : "Kwani kafanyaje kaka?"
Mandoto : "Bado yupo na yule mwanaume wake wapo barabarani wanacheka kama wajinga flani hivi."
Rose : "Kaka huyu mwanamke achana nae kalogwa huyo uyo mkaka atakuwa mchawi au kampa limbwata mwone anavyocheka cheka tu."
Mandoto : "Nitamuuuuuuuuuua mimi ngoja nitaenda huko Arusha watanijua mimi ni nani....."
Mara Mandoto simu yake ikaita akapokea aka gundua ni yule mchepuko wake waka anza kupiga story na aka anza kujisahau kuwa alikuwa amekasirika kuhusu Bertha na Nickson akaongea na kucheka na kulegeza macho na sauti kana kwamba sio mwanaume!.
Upande mwingine hotelini Bertha amefika na Nickson waka agiza walichokua wanataka kula.
Bertha : "Jamani Nickson saivi una mambo mengi Duuh"
Nickson : "Mradi najua utanipeleka mbali Mungu ata nijalia tu!."
Bertha : "Mmmmmh Sasa si bora uwe jambazi tu?."
Nickson : "Alafu nikuvamie wewe? Utanipa sh ngapi mimi naogopa kufa unaeza ukapigwa risasi ya kichwa ukafa wakati kuna mbinu zingine?"
Bertha : "Wapi wewe!!.... Sema tu ndo hivyo sina vifaa lakini ile meli ya kusafirshia pesa baharini ninge ivamia kama ningekua ni wale mabaharia wa bahari ya hindi."
Nickson : 'Hahaha kama uko serious si useme tuwape ramani afu watu tumie ka asilimia kidogo ile kitu unaeza vamia sawa lakini watakutafuta mpaka makaburini unacheza nini?."
Bertha : "Weewewe kwani tunawonesha sura? Si tunavaa maski bhana."
Nickson : "Eti eeeh afu unaifikiaje hiyo meli?"
Bertha : "Na mtumbwi..."
Nikcson : "Hahahah hahahahaha hahaha naona leo umeamua kunipa burudani..?"
Bertha : "Kwa nini."
Nickson : "Uvamie meli na mtumbwi si watailenga na jiwe izame!?"
Bertha : "Aaaah bhana sio kimtumbwi si tunatafuti boti nzuri."
Nickson : "Hiyo Idea nzuri lakini silaha hatuna pia hatuna vifaa labda tuwape hiyo idea."
Bertha : "Lakini kweli juzi bhana nilisikia wakisema wamefungua account mtandaoni labda tuwatumie ujumbe?"
Nickson : "Hahahah hao wapo na kazi nyingi sana ety wapate nafasi ya kukujibu?"
Bertha : "We tuwa andikie hivyo hivyo bhana sio mbaya hata tuwasiiane na watu wa huko nchi za nje."
Nickson : "Haya njoo tuwa andikie."
Nickson na Betha walikaaa wakiandika ujumbe huo kuwa shauri wa zamiaji wavamilie ile benki na wakiandika na mawazo yao hapa na pale wakijua hao wazamiaji wa meli hawa wezi kusoma sembuse kuwajibu walipo maliza walicheka na kuendelea na maakuli yao. Nickson aliendelea ku furahia wakati huo na kutokuwaza hata kuhusu Stela. ALikumbuka kwamba bila hela kwa hawezi ku fua dafu. Lakini mpelelezi bila kugundulika alikua anawanasa picha na akiwafatilia bila wao kujua. Yamkini Bertha hamjui mumewe vizuri ndio maaana hakuwa na hata wazo la mumewe kutumia wa pelelezi wa kujitegemea.
Upande mwingine tuna mwona Stela akiwa chumbani na Boss wake.
Stela : "Boss unajua Nickson anafanuya nini?"
Boss : "We nishakwambiaje kuhusu kuni ita ita Boss niite mpenzi bhana au unataka kunikera?"
Stela : "Aahhh wewe usiji chetue sana bhana."
Boss : "Unataka tugombane tena?"
Stela : "Jamani mpenzi nakutania."
Boss : "Enhee unasema yule yerro anafanyaje?"
Stea : "Ana anzisha mradi wa kutengeneza aplikesheni ya notes"
Boss : "Anajisumbua tu huyo"
Stela : "Yani ana pambana sana kuhusu ili swala."
Boss : "Enhee embu nielezee."
Stela : "Anataka kutengeneza aplikesheni ya kutunza notes za chuo na una weza kuwa nazo mahali popote unapotaka."
Boss : "Etyy?? Ilo wazo zuri!".Boss alisema huku anasimama akiwaza mambo kichwani mwake.
Stela ; "Ndio una dhani anaeza akafanikiwa anapoteza muda wake bure."
Boss : "Hapana hapana anaweza akapata mamilioni mengi sana!"
Stela :"Boss hahahahah hahaha ndo unamtania hapo?"
Boss : "Hapana... hapana..... huyu yerro ana fanya kazi nzuri sana yani nimeipenda."Boss alionekana akiwa kwenye mawazo yalio mpata ghafla.
Stela : "Sasa tunafanyaje tumu ajiri?"
Boss : "Hapana tukitaka kumuajiri ata kataaa."
Stela : "Sasa tuna fanyaje?"
Boss : "Sasa mwambie Angela atafute vijana kama waaaaa.. Kwani Nickson anafanya kazi na watu wangapi?"
Stela : "Yupo na best wake tu kama sijakosea."
Boss : "So wapo wawili?"
Stela : "Bhana mi sijui lakini nadhani hivyo."
Boss : "Mwambie Angela andae vijana sita kwa ajili ya hii kazi "
Stela : "We unataka kushindana na hiyo haitofanikiwa bhana!"
Boss : "We huna akili sana kwenye haya maswala hili wazo lina hela sana tukimwachia afanye mwenyewe atafaidika sana."
Stela : "Eeeenh kumbe enh?"
Boss :"Huu mradi unaweza pata takribani millioni nane kwa mwezi."
Stela : "Jamani mpenzi si uta ni nunulia ka gari kangu nikawaoneshe ma rafiki zangu?"
Boss : "We unawaza tu kula hela."
Stela : "Kwa hyo hunitaki?"
Boss : "Mpenzi jamani mama yeyo wangu lazima niku nunulie wewe tena?"
Boss alikusanya kikundi cha vijana na waka anza huo mradi wa kumuiga Nickson bila kuwa ambia watu kuwa ni mradi wa kuiga.
Stela alipo ona kuwa mambo yanaweza kumuendea vizuri Nickson na anaweza kukosa nafasi ya kuya furahia maisha aka anza kujipendekeza kwa Nickson.Kwa kutumia ujumbe mfupi akamwambia.
Stela : "Baby mambo?"
Nickson : "Poa Mambo?"
Stela : "Jamani nimekumis."
Nickson : "Hata mimi nimekumis. Tukutane basi ile hotel tunayoipenda japo nikuone."
Stela : "Hapana sasa hivi kazi zimenibana."
Nickson : "Sawa haina neno."
Stela : "MImi nataka kukuambia tu kitu kimoja Nickson."
Nickson : "Kitu gani nakusikiliza."
Stela : "Sio kwamba siamini kuwa utafanikiwa nina amini. lakini"
Nickson : "Niambie"
Stela : "Nataka kukuambia kuwa yote ninayo fanya ni kukusukuma uende mbele zaidi."
Nickson : "Kweli mpenzi?"
Stela : "Ndio mpenzi ukifanikiwa usinisahau kwa juhudi za kukufanya uende mbele Nickson ama utaniacha ukale na wanawake wengine?"
Nickson : "Hapana mpenzi wangu siezi kukuasaliti."
Stela : "Sawa Nickson pambana mimi nakungojea."
Nickson alifurahi na alipata nguvu na kujua kumbe kuna mtu anampenda? Na alijua kumbe Stela alikuwa mgumu kwake ili apambane kusonga mbele.?Nickson alijiona kama mwanaume kwa matumaini aliopewa ya uongo na Stela.Alifurahi kuona kuna mtu ana msapoti afike mbali alifurahi sana.

Itaendelea..........
Comment yako tu! ya muhimu!
Hahhahaaaa nice story twasubir next episode
 
MY SOULMATE SEHEMU YA 14.
Produced by : Equatorstory Specials.
Ni mida ya saa sita Nickson na Eric wapo kwenye ofisi ya mkuu wa chuo wakimgojea wakutane nae kwa ajili ya kuweza kufanya maonyesho ya mradi wao mpya wa kuhidhi makala ya kujisomea.
Eric : "Mh kaka umemuona iyule mdada tulimwacha chuo wakati tunamaliza saivi amekuwa mzuri khaaa ndo maana nimeomba namba."
Nickson : "Kwa hiyo umempenda ama?".
Eric : "We jamaa utaelewa lini? huku duniani hamnaga kupenda ni ku fanya afu kila mtu ana shika hamsini zake. Mdadan mwenyewe nampeleka wapi zaidi ya kitandani?"
Nickson : "Duh we jamaa ume nishinda we jamaa kiwembe sana uwezi kutulia na mmoja?"
Eric : "Embu ngoja kwanza nikaongee na yule mdada aliopo kwenye ofisi ya mkuu wa chuo kwanza acha kuzubaa wewe."
Nickson : "Unaenda kumwambia nini wewe usije uka haribu tukakosa hii nafasi."
Eric : "We tullia niachie mtaaalamu."
Eric alinyanyuka kumuelekea secretary aliekuwepo kwenye ofisi ya mkuu wa chuo akimwacha Nickson amekaa wakiendelea kumsubiri mkuu wa chuo afike wakafanye kikao walichokuwa wakingoja.
Eric : "Dada mambo?"
Rita : "Salama kaka tafadhali subiri mkuu wa chuo atafika mda sio mrefu."
Eric : "Asante dada yangu ulisema unaitwa nani?"
Rita : "Naitwa Rita Mollel".
Eric : "Una jina zuri..."
Rita : "Asante."
Eric : "Sasa uyu mkuu wa chuo anachelewa sana ame enda kula kwanza nini?"
Rita :"Hapana najua atakuwa yupo njiani kuwa mvumilivu."
Eric : "Bas naomba namba yako akija utanipigia!."
Rita : "Kwani kaka unaondoka?"
Eric : "Hapana nimekaa pale mpaka nika anza kusinzia."
Rita : "Hahahahaha unachekesha. Nimekuelewa lakini mimi nina mpenzi yupo Uganda sasa hivi."
Eric : "Yani wewe mdada ni mjanja na mzuri sana."
Rita :"Asante."
Eric : "We weka namba bhana asiepo na lake halipo tuna weza hata kuwa marafiki au nikawa nakuliwaza uki misi."
Rita : "Sawa nakupa namba lakini kuwa rafiki tu."
Eric : "Wala usiogope."
Rita alimpatia Eric namba huku Nickson akishuhudia kila kitu naona asha zoea kumuona hivi rafiki yake.Wakati Eric anarudi kuket mkuu wa chuo ndo alikuwa aki ingia Eric alimsalimia na kumuita Nickson waka ingia na kuanza kikao wakiwa pamoja na Rita secretary amabyo macho ya Eric yalikua naye kila muda yakiwa yana mendea mapaja ya secretary aliekuwa amevaa sketi fupi.
Baada ya kuonesha walichokuwa wame unda na mkuu wa chuo pamoja na wadau wengine waliokuwepo walionekana kumpenda sana ubunifu wa hawa vijana basi muda wa kujadili maswala ya bei uliwadia na wali afikiana kwamba watauza haki zote za mradi huo kwa hicho chuo kwa kiasi cha milioni 150. Nicskon hakuamini alichosikia kutoka kwa mtu aliekuwa analipwa hela ambayo ilikuwa kidogo sana kukimu maisha yake sasa hivi ana lipwa millioni 150?.
Basi kikao kili ishia hapo na walikubaliana kuku tana mara ya pili ili wawekane sawa kuhusu mambo ya hela na pia waweke sawa mambo ya hela . Na watakapo kuja watakuja kuchuka cheki ya malipo yao.
Nickson alipotoka hapo wakati wanaelekea kutoka alimwona Eric akikazana kumpungia busu la hewani rita na kumkonyeza.
Nickson : "Kaka maisha yamejipa sasa mambo yamebadilika nitakuwa millonea na wewe pia. Ah Mungu ni mkubwa kweli."
Eric : "Kweli man nikipata hela ntanunua gari hapo wa dada watanikubali."
Nickson : "We jamaa yangu Mungu anakuona. "
Basi waka agana na kila moja akaondoka na njia yake kuelekea ma nyumbani. Nickson moja kwa moja akaenda kumtafuta Bertha aka mkumbatia kwa furaha sana akampa na busu kwenye paji la uso.
Bertha : "Vipi ume samehewa kodi ya nyumba ama?"
Nickson : "Bertha acha tu rafiki yangu!."
Bertha : "Niambie!..".Bertha alisema kwa mshangao akiwa ana muangalia Nickson alivyo kuwa akifurahi.
Nickson : "Nitakuwa millionea nashukuru sana kwa kuni support rafiki yangu". Alisema akimkumbatia kwa mara nyingine.
Bertha : "Usijali wangu ma rafiki ni kusaidiana umeona hata ushauri wangu wa kuku shauri ubadili zile nguo umesaidia?"
Nickson : "Yani bila wewe sijui ingekuwaje mwaa". Ali ongea kwa furaha na kumbusu tena .
Betha : "Nafurashi kwa ajili yako."
Nickson : "Twende basi tukale twende nkaku nunulie kuku wewe."
Bertha : "Siezi kwenda ngoja kwanza nika suke then tutaenda leo ntakununulia wine nzuri tusherekee au sio Baby yani Nickson!"Bertha alijikuta akimwita Nickson "Baby" wakati wao ni marafiki yamkini alikosea au furaha au asha anza kumpenda?
Nickson : "Okay sawa we nenda uje twende au ntakupitia saloon twende wote."
Bertha : "Sawa."
Nickson alienda ndani kwake akifurahi na alikumbuka Stela alimwambia kuwa atafute hela hataki maneno matupu. Nickson alimtafuta mpenzi wake stela kwa ujumbe mfupi..
Nickson : "Mambo Stela?"
Stela : "Nini?"
Nickson : "Jamani hivi ndo umekuwa hivyo kweli?"
Stela : "Hueleweki bhana mimi nipo kazini unasemaje?"
Nickson : "Nina habari njema ya kukuambia mpenzi wangu."
Stela : "Habari gani?"
Nickson : "Nime ongea na mkuu wa chuo chetu kwenda kumu uzia ule mradi wa aplikeshen ya makala."
Stela : "Kwayo kuongea na mkuu wa chuo mimi inanihusu nini?"
Nickson : "Jamani si usubiri nikuelezee."
Stela : "Enhee nielezee."
Nickson : "Amekubali niwauzie chuo aplikesheni hiyo kwa bei ya millioni mia na hamsini kwa ka hiyo nikigawana na Erick nakua na faida ya millioni 75."
Stela : "Unasemaaa? Acha uongo wewe kaka!."
Nickson : "Hapana sikutanii mpenzi wangu ntakua na hela ya kuweza kukuoa na kukupa maisha ya kusonga mbele."
Stela : "Wao jamani bebi mpenzi wangu si utani nunulia gari ya Range Rover?".
Nickson : "Range rover? Hela haitotosha lakini maisha yatakuwa mazuri."
Stela : "Sawa mpenzi wangu nakupenda sana!. Ndio maana nilikua mgumu kwako ili uweze kusonga mbele nilijua tu unaweza beby."
Nickson : "Asante mpenzi lakini wewe ulikua mgumu sana mpaka nikaona labda hunipendi."
Stela : "Aah usha anza!."
Nickson : "Hapana mpenzi jamani."
Stela : "Sawa baadae nakupenda na sitaki kukuona na mwanamke mwingine mkisha pata hela wanaume wengine mnakuwa na mambo mengi sana!."
Nickson : "Sawa."
Muda uliendelea kusonga na Bertha alimaliza kusuka alirudi nyumbani akavaa aka pendeza kana kwamba anaenda kwenye harusi ama hafla moja kubwa sana. Nguo ilikuwa inamchora vizuri sio kumbana sana na marashi yanayo nukia vizuri sana .Nickson ali baki kushangaa sana Bertha alimwona Nickson alivyo kuwa akimwangalia kwanzia chini hadi juu.
Bertha : "Kwahiyo utanishangaa kwanza ama tutaenda kwanza?"
Nickson : "Kushangaa nini nilikuwa tu nawaza nguo ntazo nunua nikiwa tajiri."
Bertha : "Hahaha wewe nae twende bhana!."
Bertha na Nickson waliondoka na kuelekea kwenda kula na kunywa wine kama walivyo kubaliana.
Upande mwingine Stela na Boss Sambeke wapo wanakula kwenye Hoteli ya kifahari kiasi.
Stela :"Mpenzi hauto amini nilicho kisikia leo".
Boss : "Ume sikia nini ni fashion nyingine ya nguo ama?"
Stela : "Wewe mwanaume ukoje? Unadhani mimi nafuatilia nguo tu?"
Boss : "Haya niambie."
Stela : "Ile aplikesheni ya Nickson amepata mteja kwa millioni 150."
Boss : "Unasema laki na nusu ama millioni 150?"
Stela : "Millioni 150!"
Boss : "Wacha utani!"
Stela : "Ndio aliniambia mwenyewe."
Boss : "Ah wapi wewe!."
Stela : "Alinitumia ujumbe wa maandishi leo."
Boss : "Bado mna wasiliana we si ulisema utamuacha?"
Stela : "Ndio tumeachana yule takataka haezi kunipa vitu unavyonipa Bhabaa!"
Boss : "Sawa nioneshe sms zake."
Stela : "Kwahyo huniamini!?"
Boss : "Nakuamini mi nataka kuona hiyo sms ya millioni 150!."
Stela : "Kama huamini nenda kuangalia kile chuo aliposomea Nickson utajua mimi sikuoneshi!."
Boss : "Sawa nina rafiki yangu pale ni secretary anaitwa Rita.". Hapo boss alikua anamuongelea yule Rita Eric aliokua akimwomba number.
Stela : "Utajua mwenyewe!"
Huku upande mwingine Bertha na Nickson walikuwa wana malizia kula na wakati wanatoka bertha aliomba aelekee chooni mara moja.Wakati Nickson amesimama karibu na gate aki mngoja Bertha atoke uani. Mara ghafla mbele ya Nickson yalisimama magari mawili na watu kama watatu waka shuka.
Mandoto : "Ah Nickson nakuona!". Ilikuwa Ni sauti ya Mandoto aliemtokea Nickson ghafla.
Itaendelea.......
 
MY SOULMATE SEHEMU YA 15.
Produced by : Equatorstory Specials.
############# Tulipo ishia ###########
Nickson amesimama hotelini karibu na geti akimsubiri Bertha atoke uwani. Mbele ya Nickson alipo simama magari mawili yalisamama mbele ya Nickson ambayo ni ya mumewe wake Bertha, Mzee Mandoto alishuka.
****** Twende sasa ***********
Mandoto : "Nickson nakuona!."
Nickson : "Nyie ni kina nani na mnapakije gari mbele yangu hapa sio parking bwana."
Mandoto : "Hahahahaha ina maaana hunijui mimi ni nani?"
Nickson : "We ni nani kwani?".
Wakati Nickson ana bishana nao yule mpelelezi alikuwa akimzunguka kwa nyuma kuelekea mgongoni kwake.
Mandoto : "Usiwe na kiburi wewe." Alisema akimpiga Nickson ngumi ya uso!
Nickson alitaka kupigana amrushie Mandoto ngumi wakati huo mpelelezi yupo nyuma yake akamgusa Nickson shingoni na Nickson alizimia gahfla.
Mpelelezi : "Oya tumuingize kwenye kwenye gari fasta tuondoke."
Mara ghafla Bertha alikuja na walinzi wakikimbilia kwenye eneo la tukio.
Mlinzi : "We mnafanyaje hapo?"
Mandoto : "Achana naye tuondoke sitaki kesi tuta mrudia."
Mandoto alisema huku akijiandaa kupanda gari waondoke lakin akawa ana mtizama Bertha . Mpelelezi na huyo mtu wa watatu wakao panda kwenye gari mbio mbio. Wakaondoka wakati walinzi wanafika hilo tukio walisha anza kuondoka wakimwacha Nickson akiwa amezimia.
Bertha : "Nickson Nickson..."
Bertha ali ita bila mafanikio aki jaribu kumuamsha. Walinzi walimchukua Nickson na kwenda kumpa huduma ya kwanza na baada ya masaa kama mawili Nickson alizinduka akiwa na maumivu makali ya shingo na kichwani alitaka kulala tu. Bertha alitafuta usafiri akampeleka mpaka chumbani kwake Bertha ili aweze kumuhudumia.
******************
Ni asubuhi ya siku inayo fuata. Boss Sambeke anaenda kukutana na Rita wa chuo cha kina Nickson kwa ajili ya maongezi.
Rita : "Habari za asubui Boss nakuona ume nenepa kidogo."
Boss : "Hhaaha ata mi enyewe naona wazidi kungara.". Walisema hayo wakikumbatiana.
Rita : "Asante Boss."
Boss : "Haina shida kabisa eeenh bhana au una mtu nini?"
Rita : ''Hapana niambie Boss unajua nime ji iba ety?"
Boss : "Sasa Binti nataka tuongee swala moja bhana"
Rita : "Ndio nakusikiliza.."
Wakati Boss haja anza kuoongea alikuja waiter waka agiza kifungua kinywa.
Boss : "Kuna huu mradi bhana nataka ni pate hiyo 'tenda' hapo"
Rita : "Tenda gani hiyo?". Alisema aki sogeza kichwa mbele kidogo asikie kwa makini.
Boss : "Ya kutengeneza aplikesheni ya kuhifadhi notes."
Rita : "Ah mbona umechelewa."
Boss : "Kivipi?"
Rita : "Kuna vijana walikuja na kitu kama hicho hicho.."
Boss : "Weweee embu nielezeee."
Rita : "Wakaka flani hivi walikua wanaitwa ....... Nickson na Eric."
Boss : "Enhee ikawaje?". Boss aliuliza kana kwamba hajui kinachoendelea.
Rita : "Ndio tena Dr Massoud ali ipenda sana wakakubaliana millioni 150 nafikiri watakua na kikao week ijayo."
Boss : "Wewe!!"
Rita : "Ndio kwa hiyo ume chelewa Boss tafuta nyingine tuna haja ya mifumo mingi sana!"
Boss : "Sasa hapo ndo nataka niongee na wewe ramani."
Rita : "Niambie mkuu."
Boss : "Mimi nataka niichukue hiyo nafasi hiyo nataka kui iba!"
Rita : "Kivipi mimi sijakwelewa"
Boss : "Yani nataka huyo asiuze huo mfumo hapo chuoni".
Rita :"Utafanyaje wakati mfumo aliuleta na unafanya kazi tayari wewe muda wa kwenda kuunda upya una pata wapi au unao tayari?"
Boss : "Hehehh hilo lisikupe shaka jambo dogo sana!"
Rita : "Eti eeh?".
Boss : "Ninao vijana wa tano wamekuwa waki unda huu mfumo karibumi mwezi sasa na wanafanya kazi vyema sana!"
Rita : "Sasa una dhani hapo mimi nina mchango gani?"
Boss : "Nataka ukawa vurugie mambo sema hata huo mfumo ali uiba alipo kuwa ana fanya kazi kwangu."
Rita :"Weweeee. Sio vizuri bhana mimi nikigundulika nitafutwa kazi."
Boss : "We shida yako nini utakosa hela?"
Rita : "Ndio una dhani nitaishije huku?. Hizi nguo sitoeza kumudu wala hata hivi viatu siwezi kuvaa tena!."
Boss : "Najua we mdada upo hali ya juu unasemaje ukifanikisha nkakupa zawadi?"
Rita : "Zawadi gani nayo weza kuiweka kazi yangu kwenye mashaka hiyo."
Boss : "Ntakunulia gari la millioni kumi alafu nakupa na zako kumi!."
Rita : "Mhhh we utanitapeli."
Boss : "Sasa pale ofisin si una toa cheki wewe?. Ukipewa wote tuna enda benki tunatoa hela nakupa hela yako kesi imeisha!."
Rita : "Wewe mi sikuamini!."
Boss : "We una taka hela au unataka ukweli eti we binti?"
Rita : "Mimi hela zinaongea sijaja huku kuremba macho!"
Boss : "Sawa we fanya hivyo tafuta akili."
Rita : "Hahah iyo kazi ndogo huyo rafiki yake Eric anapenda wanawake!."
Boss : "Kwa hiyo tuna fanyaje?."
Rita : "Hiyo niache anayo namba yangu namuona anajileta leta tu kwangu."
Boss : "Ah wapi wewe sema umemuelewa!"
Rita : "Kiasi ni mtanashati kwa hiyo nita pata faida mbili ntampata yeye ntapata na hela . Weweeeee chezea mimi?."
Boss : "Safi wewe mwanamke una akili nafikiri tuishie hapa ngoja niende kazini."
Rita : "Haya ngoja na mimi niende."
Boss : "Sawa kwaheri mamilo."Rita aliamka akaondoka huku Boss amekaaa akimtazama anavyo ondoka.
Rita aliondoka akiwa na mawazo je afanye hili swala kweli anajua ata muumiza Nickson lakini bila ya hivyo hatoweza kupata hizo millioni 20 labda afanye kazi miezi 24 ndo atafikisha hiyo hela . Lakini kwani Nickson ana muhusu nini?. Wakati akiwa ofisini anawaza hili swala mara ghafla Eric alipiga simu.
Rita :"Haloo". Alisema kwa sauti ya upole inayovutia kweli.
Eric : "Poa mambo mermbo?"
Rita : "Mi mzima bhaba." . Rita alisema akiwa anasokota nywele zake kana kwamba Eric yupo hapo.
Eric : "Mh mama hiyo sauti duh."
Rita : "Kwani ina nini?".Rita aliongeza maringo kwenye simu na alivyo kuwa amekaa.
Eric : "Hamna ume amkaje wewe mdada?".Eric alianza kuongea kwa sauti ya chini na ya utulivu kidogo.
Rita : "Salama tu sijui wewe jamani."
Eric : "Mi nipo salama kwanza unajua nini?"
Rita : "Nini niambie basii."
Eric : "Nimekuota mwenzio."
Rita : "Jamani umeota nini afu na mimi nitakwambia niliota nini."
Eric : "Nimeota umekuja kwangu kunisalimia wakati naenda kukufuatia soda mgeni wangu nikateleza nika anguka mpaka nilishtuka usingizini. Saivi nimeamka tu kwenda kukua angalia sebleni nikakukosa."
Rita : "Jamani usijali nitakuja jamani pole. Usihofu nitakuja!"
Eric : "Kweli?. Unajua nimemiss kukuona nitumie basi picha yako."
Rita : "Yani ume ni miss afu unataka picha tu? Wewe hujanimis wewe."
Eric : "Jamani sasa nitafanyaje?"
Rita : "Kama umeniss kweli mi sikutumii picha nataka tukutane."
Eric : "Unasema?". Eric alijikuta aki inuka ghafla kwa mshangao akipaza na sauti.
Rita : "Hutaki au?."
Eric : "Hapana nataka nataka. Saaa ngapi tuna kutana?". Eric alijua hapa asha daka mtu mwingine wa kumchezea.
Rita : "Saa moja jioni nitakwambia badae hoteli gani nataka kwenda au unaogopa hela?"
Eric : "Ivi una nionaje? Mimi nina hela ety umesahau kwamba nakaribia kupata mamillioni hapo? ".
Rita : "Sawa baadae."
Eric baada ya kukata simu alisamama na aka anza kushangilia ushindi wake kwa kucheza akiwa na kaptula yake ya kulalia.
Nickson aliamka baada ya kulala masaa kadhaa kwa sababu ya dawa pia alizopewa yamkini yalimuongezea usingizi. Aliamka akajikuta yupo chumbani kwa bertha aka angalia huku na huku na hakumwona Bertha popote alipo . Alikuta ujumbe kwenye simu yake kutoka kwa Bertha. "Samahani imenibidi niondoke.". Nickson hakuamini mach yake kama Bertha ameondoka aka anagalia ujumbe mwingine akakuta bertha amemwandikia. "Nime enda sokoni kuongeza vitu kuna chai na mikate niliokwandalia kula hiyo nafikiri ntakua nisharudi."
Nickson alishuha pumzi alidhania kuwa Bertha ameondoka kweli lakini aka dhani kua yamkini ni kweli ameondoka?.
Nickson akanywa chai na akatoka kwenda kuoga ili kujiweka vizuri . Alipo toka kuoga alikuta Bertha amerudi kutoka alipokuwa amekwenda.Bertha alimkubatia akilia kwa uchungu.
Bertha :"Jamani pole nisamehe jamani mkaka wa watu nikuweka majaribuni na huna hatia."
Nickson : "Mambo madogo sio kosa lako."
Bertha : "Jamani pole ".Bertha aliendelea kulia akiwa amemkumbatia Nickson aliekuwa akimbembeleza taaratibu.
Nickson : "Kaa hapo tuongee!."
Bertha alipunguza kulia aka keti na kufuta machozi .
Nickson : "Usilie bhana."
Bertha : "Sawa sawa. " Bertha alikuwa aki jikaza asiendelee kulia.
Nickson : "Yule ndo mume wako ulio niambia?"
Bertha :"Ndio na sijui amenipataje yule shetani."
Nickson : "Labda katumia mtandao."
Bertha : "Hapana mimi simu yangu nili iacha kwake na wala sija wasiliana na mtu. Wa kwetu ambaye anaeza kumwambia niko wapi itakuwa ametumia wapelelezi na sijui wame nipataje huku kote."
Nickson : "Inaonekana ana hela ? Mpaka kuajiri wapelelezi na wamekupata?"
Bertha : "Yule mbaba ana hela yule lakin simpendi kabisa."
Nickson :"Yani hata hela zake hutaki?."
Bertha : "Hapana Nickson tuhame hapa twende sehemu nyingine twende hata kenya nina marafiki zangu huko huko sio rahisi atupate tuta enda kujificha kijiji cha mbali ambako hamna hata umeme."
Nickson :"Usimwogope huyo hana matisho."
Bertha : "Wapi wewe umepigwa mpaka umezimia Nickson acha utani bhana."
Nickson : "Hamna sikuzimia alinipiga ngumi nikajifanya nimezimia kujitetea ."
Bertha : "Hahahahha ahahaha jamani Nickson unanifanya nicheke wewe mkaka Mungu akubariki jamani una roho nzuri sana."
Nickson : "We mwache akuje tena nitapambana nae we usimwogope bhana."
Bertha : "Nickson wacha zako yule anaeza kukua mara moja isingekua kukuwahi angeku beba Mungu ndo anajua alitaka kwenda kukufanyia nini yule Shetani."
Nickson : "Labda alitaka kwenda kuniuliza ushauri juu ya wanawake maana anaona mimi na wewe tunaelewana".
Bertha : "Hahahahahahahahaha ahahahahah ahahahaha"
Nickson : "Au alitaka kwenda kunipa hela nije nimwombee msamaha kwako huezi jua."
Bertha : "Hahahahaha bhana wewe una mambo jamani. "
Nickson : "Kawaida!."
Bertha : "Vipi umekula?."
Nickson : "Nimekunywa chai saa zile lakini pika basi maana nataka kwenda jimu nijiandae na Mr Mandoto na Mimi raundi ya pili."
Bertha : "Yani wewe. Haya ngoja nipike tule ushibe bhana."
Ilifika jioni Rita na Eric wanakutana kwa ajili ya chakula kama walivyo kubaliana. Eric amekuja amependeza kama ilivyo kawaida yake lakini Rita amechelewa kidogo. Eric yupo ana rusha macho huku na kule aki angalia amuone Rita.
Rita : "Mambo?"
Eric : "Poa umependeza!."
Rita : "Kawaida na uzuri unachangia."
Eric : "Hata mimi naona karibu nisha shika meza pale twende tukakae."
Eric aliongoza kueilekea meza na kumsogezea Rita kiti akae ndipo na yeye akaenda kukaa .
Walikaa waka piga stori hapa na pale walicheka walitumia muda kujuana na Rita ndipo alipo mwambia Eric alichokuwa ana muitia siku ya leo.
Rita : "Eric nataka nikwambie kitu .."
Eric : "Jisikie huru niambie niko hapa."
Rita : "Sijui utakubali."Alisema huku akiweka mkono wake juu ya mkono wa Eric.
Eric : "Sema mama nakupa masikio yangu yote."
Rita : "Nataka tuongee biashara."
Eric : "Enhee."
Rita : "Nataka nikwambie huku mjini akili."
Eric : "Najua."
Rita : "Sasa mimi nataka umgeuke huyo rafiki yako."
Eric : "Una sema.....????"
Rita : "Nisikilize kuna tajiri nimeongea nae anataka auzie hiyo aplikesheni chuo."
Eric : "Sasa mimi nakuablianaje wakati napata kama millioni 75 huoni kama ntakua nafanya ujinga ?"
Rita : "Sawa yule Boss amesema ataiuza kwa millioni 200 alafu mia zote ni zako."
Eric : "Enhee unataka nikubaliane na huo uongo?"
Rita : "Hapana sio uongo huyu mtu ni mashuhuri. Hana mambo ya kupinda alafu ukuibali."
Eric : "Enhee inakuaje?". Eric aliuliza akiwa ana dalili ya kuchukia kidogo.
Rita : "Tuliza jazba wangu."
Eric : "Inakuwaje?"
Rita : "Naku kubaliana na achana na mtu wangu wa aliepo Uganda nakubali niwe wako."
Eric : "Mhhhhh".
Rita : "Hiii yote itakua yako Eric."Rita ali simama aka zunguka akijionesha kwa Eric.
Eric alibaki akishangaa huku Rita akiondoka kwa madoido yote kama miss Tanzania vile. Eric hakuamini alichosikia yote yalimjia kwenye chake ghafla alibaki akiwaza millioni mia zinakuwa zake na atakuwa na RIta. Eric aliondoka na kwenda nyumbani akawaza na kuwaza akitafuta kitu cha kufanya kweli amgeuke rafiki yake kwa ajili ya hela na mwanamke?.
Itaendelea............
 
Nickson : "Hamna sikuzimia alinipiga ngumi nikajifanya nimezimia kujitetea ." 🙂 🙂 🙂 🙂
 
Back
Top Bottom