Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,743
- 25,564
- Thread starter
- #21
MTUNZI: NYEMO CHILONGANI.
MAHALI: DAR ES SALAAM.
SIMU: 0718 069 269.
NITAKAPOKUFA 12
Katika kipindi chote Samiah hakuonekana kuwa na furaha kabisa, kitendo cha kupewa talaka na mume wake, Yusufu kilionekana kumuumiza kupita kawaida. Kila siku akawa mtu wa kulia tu, hakujua sababu ambayo ilimfanya mume wake kupinga kwa nguvu zote kupata ujauzito. Wakati mwingine alikuwa akijuta kile ambacho alikuwa amekifanya cha kuruhusu ujauzito.
Mtoto alionekana kuwa baraka katika familia nyingine lakini kwake akaonekana kuwa kama laana. Muda wote Samiah alikuwa mtu wa kulia tu. Wazazi wake, Bwana Hussein pamoja na mama yake, Bi Warda walikuwa na kazi kubwa ya kumbembeleza kila siku. Moyoni aliumia kupita kawaida, maumivu makali ambayo wala hakuwa akiyategemea kabla.
Mara zote alikuwa akijifungia chumbani. Kutokana na kuwa na msongo mkubwa wa mawazo huku akiwa na ujauzito, mara kwa mara Samiah alikuwa akiumwa. Kila alipokuwa akipelekwa hospitalini madaktari walikuwa wakimwambia apunguze mawazo na pia awe anakula sana lakini maneno ya madaktari wale hayakubadilisha kitu chochote kile.
Mwili wake ukanyong’onyea, kila wakati alikuwa akimfikiria mtalaka wake, Yusufu ambaye katika kipindi hicho alikuwa ameamua kuishi maisha ya peke yake. Siku ziliendelea kukatika mpaka katika kipindi kile ambacho akaanza kujisikia uchungu na kupelekwa katika hospitali ya mkoa ya Dodoma na kisha kujifungua salama mtoto wa kiume.
Kwa kiasi fulani furaha yake ikaonekana kurudi tena moyoni mwake, mtoto wake huyo ambaye aliamua kumpa jina la Nasri ambaye alionekana kumpa furaha katika kipindi hicho. Kila alipokuwa akimwangalia, alifanana nae sana huku baadhi ya maeneo akiwa amefanana na Yusufu. Samiah akapokea zawadi mbalimbali kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao walikuja hospitalini pale.
Waandishi wa habari hawakutaka kupitwa, mara baada ya kupata taarifa kwamba Samiah alikuwa amejifungua, wakasafiri mpaka Dodoma na kisha kuchukua habari na kuwapiga picha. Taarifa hiyo ndio ambayo ilionekana kuuza sana magazeti hasa pale watu ambapo wangesikia na hatimae kutaka kumuona mtoto huyo, Nasri.
Kama ilivyotarajiwa na ndivyo ilivyotokea. Magazeti yakanunuliwa sana mitaani kiasi ambacho kiliwashangaza hata wamiliki wa magazeti hayo. Kila mtu alikuwa akitaka kumuona mtoto wa Yusufu au The Ruler kama jinsi ambavyo alivyokuwa akijuliakana katika kipindi hicho.
Mwezi wa kwanza ukapita, mwezi wa pili ukapita. Yusufu hakuacha mawasiliano pamoja na mtalaka wake, Samiah kwani mara kwa mara alikuwa akipeleka fedha za matumizi kama kuepuka lawama lakini huku moyo wake ukiwa na hasira na Samiah kwani aliona muda si mrefu angeweza kunyang’anywa kila alichokuwa nacho.
****
Yusufu akaamka kutoka usingizi, jasho lilikuwa likimtoka kupita kawaida. Akaanza kuangalia huku na kule, alikuwa akiweweseka sana. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kupita kawaida. Macho yake akayapeleka katika simu yake, ilikuwa saa tisa usiku. Hofu ikaanza kumjia moyoni, hakuelewa sababu yoyote ambayo ilimpelekea kuwa katika hali ile.
Huku akiwa anajiuliza, ghafla chumba kikawa na giza kubwa, taa ambayo mara kwa mara alikuwa akiiwasha ikajizima, mwanga mkali ukaanza kumulika kutoka katika kile kioo ambacho kilionekana kuwa kama mlango wake wa kuingilia katika ulimwengu wa giza. Yusufu alizidi kuogopa kupita kawaida, hali ambayo ilikuwa imetokea katika kipindi kile haikuwahi kumtokea hata siku moja.
Ghafla, sauti kali na nzito ikaanza kusikika kutoka katika kioo kile ambacho hakukuwa na mtu ambaye angeweza kukiona zaidi yake. Sauti ile ilikuwa ikimtaka kuelekea katika ulimwengu ule wa giza. Bila kujiuliza au kuleta mgomo wowote ule, akainuka na moja kwa moja kuanza kukifuata kioo kile.
Mianga kama ya radi nangurumo za ajabu zikaanza kusikika, kwa sababu ngurumo zile alikuwa amekwishazizoea, hakuogopa, akaelekea katika kioo kile na kisha kutokea katika upande wa pili. Mwendo wa Yusufu ambao alikuwa akitembea siku hiyo ulikuwa ni wa tofauti sana, kichwa chake kilikuwa kikijua wazi kwamba kitendo cha kuvunja moja ya masharti ndicho ambacho kilisababisha yale yote.
Mara baada ya mwendo fulani akaifikia nyumba ile na kisha kuingia ndani. Muonekano wa nyumba ile siku hiyo ulikuwa ni wa tofauti kabisa. Kwanza nyumba ilionekana kubwa sana kwa ndani siku hiyo, hata idadi ya watu ambao walikuwa ndani ya nyumba ile siku hiyo walikuwa wameongezeka zaidi.
Watu zaidi ya themanini walikuwa ndani ya nyumba ile, mavazi yao yalikuwa yametofautiana. Wapo ambao walikuwa wamevaa nguo nyeusi na wengine nyekundu. Mavazi yao hazikuwa suruali, zilikuwa kama mashuka makubwa ambayo walikuwa wakiyavaa kuanzia chini mpaka kufunika vichwa vyao.
Yusufu akabaki akiwa amesimama mlangoni, katikati ya watu wale kulikuwa na chombo ambacho kilikuwa kikiwaka taa huku pembeni kukiwa na kisu ambacho kilionekana kuwa na ncha kali sana. Yusufu hakutaka kupiga hatua zaidi, alichokifanya ni kuanza kuelekea mbele kabisa huku watu wote ambao walikuwa mahali pale wakiwa wameinamisha vichwa vyao huku kwa mbali sauti zao zikisikika mahali pale.
Mara baada ya kufika mbele kabisa, mtu mmoja ambaye alionekana kutisha sana akaanza kumfuata pale alipokuwa amesimama na kisha kuanza kumwangalia usoni. Macho ya mtu yule hayakuwa ya kawaida kabisa, yalikuwa mekundu kabisa huku meno yake yakiwa na ncha kali kupita kawaida.
Alichokifanya mtu yule mara baada ya kumwangalia Yusufu kwa muda fulani, akaanza kuelekea kule kulipokuwa na kisu na kisha kukichukua na kumgawia Yusufu. Yusufu hakujua kazi ya kisu kile, alibaki akitetemeka huku akijua kwamba alitakiwa ajichome na kujiua kama adhabu ambayo aliambiwa angepewa.
“Umevunja moja ya masharti yetu” Mwanaume yule alimwambia Yusufu kwa sauti nzito iliyokuwa na utetemeshi mkubwa.
Watu wote ambao walikuwa wameinama chini wakainua vichwa vyao na kisha kuanza kumwangalia Yusufu. Yusufu aliwaangalia watu wale, alikuwa akiwatambua sana huku akionekana kushtuka, hakuamini hata viongozi wengine wa nchi pamoja na matajiri wengine nao walikuwa katika ulimwengu ule.
“Tunakuadhibu” Mtu yule alimwambia Yusufu.
Mara ghafla mbele ya Yusufu kikatokea kioo kimoja kikubwa, kilikuwa mara mbili zaidi ya kile kioo ambacho kilikuwa chumbani kwake. Yusufu hakuelewa maana ya kioo kile, alibaki akikiangalia tu. Baada ya sekunde kadhaa, sura za wazazi wake, mzee Kessi na Bi Fatuma zikaonekana katika kioo kile kitu ambacho kilimfanya Yusufu kushtuka.
“Tunakuadhibu. Tunamtaka mtu mmojawapo” Mtu yule alimwambia Yusufu.
Yusufu akaanza kutetemeka, hakuamini kama adhabu ambayo alikuwa akipewa kwa wakati huo ilikuwa ni kumuua mmoja wa wazazi wake. Ule ukaonekana kuwa mtihani mkubwa sana kwake, hakujua ni mzazi gani ambaye alitakiwa kumuua katika kipindi hicho. Akabaki akiwaangalia wazazi wake kwa muda hata kabla hajaamua ni yupi alitakiwa kumuua kwa mkono wake katika kipindi hicho.
Mawazo yake yakaanza kurudi nyuma kabisa. Akaanza kukumbuka katika kipindi ambacho wazazi wake hao walivyokuwa wakiangaika sana kila siku kwa ajili yake. Hakuamini kama siku hii ya leo alitakiwa kufanya uamuzi mmoja mgumu, uamuzi wa kumuua mmoja wa wazazi wake ambao walikuwa wamejitoa sana katika maisha yake.
Alibaki kwa muda wa dakika tano akawa bado hajatoa uamuzi wowote ule. Alikuwa akiendelea kukumbuka mambo mengi ambayo yalikuwa yametokea katika maisha yake ya nyuma ambayo alikuwa amelelewa sana na wazazi wake hao. Japokuwa uamuzi ulikuwa mgumu sana kwake lakini alitakiwa kufanya kitu kimoja tu, kumuua mtu mmojawapo.
Yusufu hakuwa na jinsi, alitakiwa kufanya kile ambacho alitakiwa kukifanya mahali hapo. Akaunyanyua mkono wake ulioshika kisu. Machozi yalikuwa yakitiririka mashavuni mwake, maumivu makubwa sana yakaukumba moyo wake. Alichokifanya mahali hapo ni kuchoma taswira ya baba yake, mzee Kessi ambayo ilikuwa ikionekana katika kioo kile.
Mzee Kessi akaonekana akianza kuangaika katika kioo kile, damu nyingi zikaanza kumtoka kwa sekunde kadhaa na kisha kutulia. Yusufu akabaki akilia, hakuamini kama katika kipindi hicho alikuwa amemuua baba yake kwa mikono yake mwenyewe. Adhabu ile ikaonekana kuwa kubwa kwake, hakuamini kama baba yake ambaye alikuwa amemlea katika kipindi chote kile ndiye ambaye alikuwa amemuua kwa mkono wake mwenyewe.
Hapo hapo akapokonywa kisu kile. Yusufu akapiga magoti chini na kuanza kulia kwa uchungu mkubwa. Japokuwa watu wengine walikuwa wamekwishaanza kuondoka mahali hapo lakini Yusufu hakuondoka, bado alikuwa amepiga magoti chini huku akiendelea kulia. Ghafla akajikuta akisafirishwa kutoka katika ulimwengu ule na kutokea katika kitanda chake huku akiwa amepiga magoti vile vile. Yusufu alibaki akilia tu, hakuonekana kuamini kile ambacho alikuwa amekifanya kipindi kile, kumuua baba yake kwa mkono wake mwenyewe.
****
Siku hiyo usiku ukaonekana kuwa usiku mgumu kuliko siku zote alizowahi kuishi ndani ya dunia hii. Alijitahidi sana ili aweze kupata usingizi lakini usingizi ukagoma kabisa kuja. Mawazo yake yalikuwa yakimfikiria baba yake tu, mzee Kesy ambaye alikuwa akiishi mjini Bagamoyo. Moyo wake ulikuwa ukimuuma sana, hakuamini kama utajiri, umaarufu na mvuto ambao alikuwa nao ndio ambao ulikuwa umesababisha siku hiyo kumuua baba yake.
Yusufu alilia sana usiku huo, japokuwa hakuwahi kwenda msikitini lakini kwa kufikia hatua hiyo akaanza kumuomba Mungu aweze kumnusuru baba yake ili kile ambacho alikuwa amekifanya kule kwenye ulimwengu wa giza, kitendo cha kumuua baba yake kisiweze kufanikiwa. Hakujua angeishi vipi baada ya hapo, hakujua ni hali gani ambayo angekuwa nayo mara baada ya kusikika kwamba baba yake, mzee Kessi alikuwa amefariki.
Masaa yalizidi kwenda mbele mpaka kulipopambazuka, bado Yusufu alikuwa macho na wala hakuwa na nguvu za kutoka kitandani ambako alikuwa amelala tu. Kwa upande wake mmoja wa moyo wake ulionekana kujuta kwa kile ambacho alikuwa amekifanya lakini upande mwingine ulikuwa ukimpongeza kutoka na kitendo kile ambacho kingeufanya utajiri wake, umaarufu na hata mvuto kubaki navyo vile vile.
Saa 1:07 asubuhi, simu yake ikaanza kuita. Alichokifanya ni kuichukua na kisha kuangalia kioo cha simu ile. Jina lala ‘Dear Mom’ lilikuwa likionekana katika kioo cha simu ile. Hata kabla ya kupokea simu ile Yusufu akajua ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea. Kinyonge akabonyeza kitufe cha kijani na kisha kuipeleka simu sikioni.
“Baba yako amefariki” Ilisikika sauti ya mama yake simuni hata kabla ya salamu.
Japokuwa alikuwa akijua kwamba kitu kile kingetokea lakini kwa wakati huo baada ya kupewa taarifa ile moyo wake ukamlipuka, mapigo ya moyo yakaanza kudunda kwa kasi kupita kawaida, mzunguko wa damu yake ulikuwa ukizunguka kwa kasi sana. Yusufu hakuongea kitu, machozi yalikuwa yakitiririka katika mashavu yake, moyo wake ulijisikia uchungu kupita kawaida.
“Ninakuja huko huko” Yusufu alisema na kisha kukata simu.
Akabaki akiwa amepigwa na butwa kitandani pale, moyo wake ulikuwa ukifikiria zaidi kuhusiana na baba yake, kosa alilolifanya mke wake ambaye alimpa talaka, Samiah likaonekana kuwa kubwa kwake na ndilo ambalo ilikuwa limesababisha yale yote kutokea. Alichokifanya Yusufu ni kumpigia simu Kelvin na kumtaarifu kile ambacho kilikuwa kimetokea kwamba baba yake alikuwa amefariki.
Ndani ya dakika ishirini, Kelvin akafika mahali hapo huku akitangulizana na marafiki wengine na kisha kuanza safari ya kuelekea Bagamoyo huku wakiwa pamoja na Yusufu. Kila mmoja ndani ya gari alikuwa akimfariji, hawakujua kwamba huyo huyo Yusufu ndiye ambaye alikuwa amemuua baba yake kwa mikono yake mwenyewe.
Walichukua dakika arobaini na tano mpaka kufika Bagamoyo ambapo wakaanza kuelekea katika sehemu ilipokuwa na nyumba hiyo. Tayari watu walikwishaanza kufika mahali hapo, vilio vilikuwa vikisikika katika eneo la nyumba hiyo. Yusufu akashindwa kujizuia, akaanza kulia tena jambo ambalo liiwafanya hata marafiki zake kulengwa na machozi.
Yusufu akaanza kuelekea ndani ya nyumba yao ambapo akakutana na mama yake, Bi Fatuma na kisha kumkumbatia. Wote walikuwa wakilia, walionekana kuumia kupita kawaida. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo watu walivyozidi kujaa ndani ya eneo la nyumba hiyo. Waandishi wa habari hawakuwa mbali, nao wakafika mahali hapo na kisha kuanza kupiga picha kila kilichokuwa kikiendelea.
Taarifa zikatangazwa kwenye vituo vya redio pamoja na televisheni. Kila mtu ambaye aliisikia taarifa ile alishtuka. Hawakuamini kama Yusufu yule yule ambaye alikuwa amepata sana umaarufu ndiye ambaye alikuwa akipitia katika mambo magumu namna ile. Wananchi wakaanza kuamini ushirikina kwa kuona kwamba kulikuwa na mtu ambaye alikuwa amesababisha hayo yote.
“Mmmh! Miezi mitano iliyopita alitalikiana na mke wake, leo hii baba yake amefariki. Nina wasiwasi kuna mkono wa mtu hapa. Kuna mtu ambaye hapendi kumuona akipata mafanikio haya” Mwananchi mmoja alisikika akimwambia mwenzake.
“Yaani na mimi nilitaka niseme hivyo hivyo. Yaani sjui kwa nini Watanzania tuna roho za kwa nini, yaani hatutaki kuwaona watu wakifanikiwa maishani mwao” Jamaa mwingine alimwambia mwenzake.
Mapenzi kwa Yusufu yalikuwa makubwa sana, hakukuwa na mtu yeyote ambaye alifahamu kwamba Yusufu huyo huyo ndiye ambaye alikuwa katika kila kilichoendelea mahali pale. Machoni mwa watu alionekana kuwa mtu asiye na hatia yoyote ile. Uso wa majonzi ambao alikuwa akiuonyesha siku hiyo ndio ndio ambao uliwaonyeshea watu kwamba alikuwa hausiki kabisa na kile ambacho kilikuwa kimetokea.
Vitu vingine viliendelea kama kawaida mhali hapo mpaka pale ambapo Shekhe Oswald alipofika msibani hapo na kisha kuongea maneno machache na mwili kupelekwa msikitini kuswaliwa na kisha kuruudishwa nyumbani ambapo harakati zote za mazishi zikaanza kufanyika mahali hapo.
Ilipofika saa 10:15 watu zaidi ya mia saba ambao walikuwa wamekusanyika mahali hapo wakaanza kuupeleka mwili wa mzee Kessi makaburini kwa ajili ya kuzikwa. Wakinamama walibaki majumbani wakilia, Bi Fatuma hakuamini kama mume wake ambaye alikuwa akimpenda kwa wakati huo alikuwa amefariki dunia na mwili wake ulikuwa njiani ukipelekwa makaburini.
Je nini kitaendelea?
Je nini kitatokea katika maisha ya Yusufu?
Umaarufu atakuwa nao zaidi au utampotea?
Je ataweza kuishi bila kuvunja masharti?
MAHALI: DAR ES SALAAM.
SIMU: 0718 069 269.
NITAKAPOKUFA 12
Katika kipindi chote Samiah hakuonekana kuwa na furaha kabisa, kitendo cha kupewa talaka na mume wake, Yusufu kilionekana kumuumiza kupita kawaida. Kila siku akawa mtu wa kulia tu, hakujua sababu ambayo ilimfanya mume wake kupinga kwa nguvu zote kupata ujauzito. Wakati mwingine alikuwa akijuta kile ambacho alikuwa amekifanya cha kuruhusu ujauzito.
Mtoto alionekana kuwa baraka katika familia nyingine lakini kwake akaonekana kuwa kama laana. Muda wote Samiah alikuwa mtu wa kulia tu. Wazazi wake, Bwana Hussein pamoja na mama yake, Bi Warda walikuwa na kazi kubwa ya kumbembeleza kila siku. Moyoni aliumia kupita kawaida, maumivu makali ambayo wala hakuwa akiyategemea kabla.
Mara zote alikuwa akijifungia chumbani. Kutokana na kuwa na msongo mkubwa wa mawazo huku akiwa na ujauzito, mara kwa mara Samiah alikuwa akiumwa. Kila alipokuwa akipelekwa hospitalini madaktari walikuwa wakimwambia apunguze mawazo na pia awe anakula sana lakini maneno ya madaktari wale hayakubadilisha kitu chochote kile.
Mwili wake ukanyong’onyea, kila wakati alikuwa akimfikiria mtalaka wake, Yusufu ambaye katika kipindi hicho alikuwa ameamua kuishi maisha ya peke yake. Siku ziliendelea kukatika mpaka katika kipindi kile ambacho akaanza kujisikia uchungu na kupelekwa katika hospitali ya mkoa ya Dodoma na kisha kujifungua salama mtoto wa kiume.
Kwa kiasi fulani furaha yake ikaonekana kurudi tena moyoni mwake, mtoto wake huyo ambaye aliamua kumpa jina la Nasri ambaye alionekana kumpa furaha katika kipindi hicho. Kila alipokuwa akimwangalia, alifanana nae sana huku baadhi ya maeneo akiwa amefanana na Yusufu. Samiah akapokea zawadi mbalimbali kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao walikuja hospitalini pale.
Waandishi wa habari hawakutaka kupitwa, mara baada ya kupata taarifa kwamba Samiah alikuwa amejifungua, wakasafiri mpaka Dodoma na kisha kuchukua habari na kuwapiga picha. Taarifa hiyo ndio ambayo ilionekana kuuza sana magazeti hasa pale watu ambapo wangesikia na hatimae kutaka kumuona mtoto huyo, Nasri.
Kama ilivyotarajiwa na ndivyo ilivyotokea. Magazeti yakanunuliwa sana mitaani kiasi ambacho kiliwashangaza hata wamiliki wa magazeti hayo. Kila mtu alikuwa akitaka kumuona mtoto wa Yusufu au The Ruler kama jinsi ambavyo alivyokuwa akijuliakana katika kipindi hicho.
Mwezi wa kwanza ukapita, mwezi wa pili ukapita. Yusufu hakuacha mawasiliano pamoja na mtalaka wake, Samiah kwani mara kwa mara alikuwa akipeleka fedha za matumizi kama kuepuka lawama lakini huku moyo wake ukiwa na hasira na Samiah kwani aliona muda si mrefu angeweza kunyang’anywa kila alichokuwa nacho.
****
Yusufu akaamka kutoka usingizi, jasho lilikuwa likimtoka kupita kawaida. Akaanza kuangalia huku na kule, alikuwa akiweweseka sana. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kupita kawaida. Macho yake akayapeleka katika simu yake, ilikuwa saa tisa usiku. Hofu ikaanza kumjia moyoni, hakuelewa sababu yoyote ambayo ilimpelekea kuwa katika hali ile.
Huku akiwa anajiuliza, ghafla chumba kikawa na giza kubwa, taa ambayo mara kwa mara alikuwa akiiwasha ikajizima, mwanga mkali ukaanza kumulika kutoka katika kile kioo ambacho kilionekana kuwa kama mlango wake wa kuingilia katika ulimwengu wa giza. Yusufu alizidi kuogopa kupita kawaida, hali ambayo ilikuwa imetokea katika kipindi kile haikuwahi kumtokea hata siku moja.
Ghafla, sauti kali na nzito ikaanza kusikika kutoka katika kioo kile ambacho hakukuwa na mtu ambaye angeweza kukiona zaidi yake. Sauti ile ilikuwa ikimtaka kuelekea katika ulimwengu ule wa giza. Bila kujiuliza au kuleta mgomo wowote ule, akainuka na moja kwa moja kuanza kukifuata kioo kile.
Mianga kama ya radi nangurumo za ajabu zikaanza kusikika, kwa sababu ngurumo zile alikuwa amekwishazizoea, hakuogopa, akaelekea katika kioo kile na kisha kutokea katika upande wa pili. Mwendo wa Yusufu ambao alikuwa akitembea siku hiyo ulikuwa ni wa tofauti sana, kichwa chake kilikuwa kikijua wazi kwamba kitendo cha kuvunja moja ya masharti ndicho ambacho kilisababisha yale yote.
Mara baada ya mwendo fulani akaifikia nyumba ile na kisha kuingia ndani. Muonekano wa nyumba ile siku hiyo ulikuwa ni wa tofauti kabisa. Kwanza nyumba ilionekana kubwa sana kwa ndani siku hiyo, hata idadi ya watu ambao walikuwa ndani ya nyumba ile siku hiyo walikuwa wameongezeka zaidi.
Watu zaidi ya themanini walikuwa ndani ya nyumba ile, mavazi yao yalikuwa yametofautiana. Wapo ambao walikuwa wamevaa nguo nyeusi na wengine nyekundu. Mavazi yao hazikuwa suruali, zilikuwa kama mashuka makubwa ambayo walikuwa wakiyavaa kuanzia chini mpaka kufunika vichwa vyao.
Yusufu akabaki akiwa amesimama mlangoni, katikati ya watu wale kulikuwa na chombo ambacho kilikuwa kikiwaka taa huku pembeni kukiwa na kisu ambacho kilionekana kuwa na ncha kali sana. Yusufu hakutaka kupiga hatua zaidi, alichokifanya ni kuanza kuelekea mbele kabisa huku watu wote ambao walikuwa mahali pale wakiwa wameinamisha vichwa vyao huku kwa mbali sauti zao zikisikika mahali pale.
Mara baada ya kufika mbele kabisa, mtu mmoja ambaye alionekana kutisha sana akaanza kumfuata pale alipokuwa amesimama na kisha kuanza kumwangalia usoni. Macho ya mtu yule hayakuwa ya kawaida kabisa, yalikuwa mekundu kabisa huku meno yake yakiwa na ncha kali kupita kawaida.
Alichokifanya mtu yule mara baada ya kumwangalia Yusufu kwa muda fulani, akaanza kuelekea kule kulipokuwa na kisu na kisha kukichukua na kumgawia Yusufu. Yusufu hakujua kazi ya kisu kile, alibaki akitetemeka huku akijua kwamba alitakiwa ajichome na kujiua kama adhabu ambayo aliambiwa angepewa.
“Umevunja moja ya masharti yetu” Mwanaume yule alimwambia Yusufu kwa sauti nzito iliyokuwa na utetemeshi mkubwa.
Watu wote ambao walikuwa wameinama chini wakainua vichwa vyao na kisha kuanza kumwangalia Yusufu. Yusufu aliwaangalia watu wale, alikuwa akiwatambua sana huku akionekana kushtuka, hakuamini hata viongozi wengine wa nchi pamoja na matajiri wengine nao walikuwa katika ulimwengu ule.
“Tunakuadhibu” Mtu yule alimwambia Yusufu.
Mara ghafla mbele ya Yusufu kikatokea kioo kimoja kikubwa, kilikuwa mara mbili zaidi ya kile kioo ambacho kilikuwa chumbani kwake. Yusufu hakuelewa maana ya kioo kile, alibaki akikiangalia tu. Baada ya sekunde kadhaa, sura za wazazi wake, mzee Kessi na Bi Fatuma zikaonekana katika kioo kile kitu ambacho kilimfanya Yusufu kushtuka.
“Tunakuadhibu. Tunamtaka mtu mmojawapo” Mtu yule alimwambia Yusufu.
Yusufu akaanza kutetemeka, hakuamini kama adhabu ambayo alikuwa akipewa kwa wakati huo ilikuwa ni kumuua mmoja wa wazazi wake. Ule ukaonekana kuwa mtihani mkubwa sana kwake, hakujua ni mzazi gani ambaye alitakiwa kumuua katika kipindi hicho. Akabaki akiwaangalia wazazi wake kwa muda hata kabla hajaamua ni yupi alitakiwa kumuua kwa mkono wake katika kipindi hicho.
Mawazo yake yakaanza kurudi nyuma kabisa. Akaanza kukumbuka katika kipindi ambacho wazazi wake hao walivyokuwa wakiangaika sana kila siku kwa ajili yake. Hakuamini kama siku hii ya leo alitakiwa kufanya uamuzi mmoja mgumu, uamuzi wa kumuua mmoja wa wazazi wake ambao walikuwa wamejitoa sana katika maisha yake.
Alibaki kwa muda wa dakika tano akawa bado hajatoa uamuzi wowote ule. Alikuwa akiendelea kukumbuka mambo mengi ambayo yalikuwa yametokea katika maisha yake ya nyuma ambayo alikuwa amelelewa sana na wazazi wake hao. Japokuwa uamuzi ulikuwa mgumu sana kwake lakini alitakiwa kufanya kitu kimoja tu, kumuua mtu mmojawapo.
Yusufu hakuwa na jinsi, alitakiwa kufanya kile ambacho alitakiwa kukifanya mahali hapo. Akaunyanyua mkono wake ulioshika kisu. Machozi yalikuwa yakitiririka mashavuni mwake, maumivu makubwa sana yakaukumba moyo wake. Alichokifanya mahali hapo ni kuchoma taswira ya baba yake, mzee Kessi ambayo ilikuwa ikionekana katika kioo kile.
Mzee Kessi akaonekana akianza kuangaika katika kioo kile, damu nyingi zikaanza kumtoka kwa sekunde kadhaa na kisha kutulia. Yusufu akabaki akilia, hakuamini kama katika kipindi hicho alikuwa amemuua baba yake kwa mikono yake mwenyewe. Adhabu ile ikaonekana kuwa kubwa kwake, hakuamini kama baba yake ambaye alikuwa amemlea katika kipindi chote kile ndiye ambaye alikuwa amemuua kwa mkono wake mwenyewe.
Hapo hapo akapokonywa kisu kile. Yusufu akapiga magoti chini na kuanza kulia kwa uchungu mkubwa. Japokuwa watu wengine walikuwa wamekwishaanza kuondoka mahali hapo lakini Yusufu hakuondoka, bado alikuwa amepiga magoti chini huku akiendelea kulia. Ghafla akajikuta akisafirishwa kutoka katika ulimwengu ule na kutokea katika kitanda chake huku akiwa amepiga magoti vile vile. Yusufu alibaki akilia tu, hakuonekana kuamini kile ambacho alikuwa amekifanya kipindi kile, kumuua baba yake kwa mkono wake mwenyewe.
****
Siku hiyo usiku ukaonekana kuwa usiku mgumu kuliko siku zote alizowahi kuishi ndani ya dunia hii. Alijitahidi sana ili aweze kupata usingizi lakini usingizi ukagoma kabisa kuja. Mawazo yake yalikuwa yakimfikiria baba yake tu, mzee Kesy ambaye alikuwa akiishi mjini Bagamoyo. Moyo wake ulikuwa ukimuuma sana, hakuamini kama utajiri, umaarufu na mvuto ambao alikuwa nao ndio ambao ulikuwa umesababisha siku hiyo kumuua baba yake.
Yusufu alilia sana usiku huo, japokuwa hakuwahi kwenda msikitini lakini kwa kufikia hatua hiyo akaanza kumuomba Mungu aweze kumnusuru baba yake ili kile ambacho alikuwa amekifanya kule kwenye ulimwengu wa giza, kitendo cha kumuua baba yake kisiweze kufanikiwa. Hakujua angeishi vipi baada ya hapo, hakujua ni hali gani ambayo angekuwa nayo mara baada ya kusikika kwamba baba yake, mzee Kessi alikuwa amefariki.
Masaa yalizidi kwenda mbele mpaka kulipopambazuka, bado Yusufu alikuwa macho na wala hakuwa na nguvu za kutoka kitandani ambako alikuwa amelala tu. Kwa upande wake mmoja wa moyo wake ulionekana kujuta kwa kile ambacho alikuwa amekifanya lakini upande mwingine ulikuwa ukimpongeza kutoka na kitendo kile ambacho kingeufanya utajiri wake, umaarufu na hata mvuto kubaki navyo vile vile.
Saa 1:07 asubuhi, simu yake ikaanza kuita. Alichokifanya ni kuichukua na kisha kuangalia kioo cha simu ile. Jina lala ‘Dear Mom’ lilikuwa likionekana katika kioo cha simu ile. Hata kabla ya kupokea simu ile Yusufu akajua ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea. Kinyonge akabonyeza kitufe cha kijani na kisha kuipeleka simu sikioni.
“Baba yako amefariki” Ilisikika sauti ya mama yake simuni hata kabla ya salamu.
Japokuwa alikuwa akijua kwamba kitu kile kingetokea lakini kwa wakati huo baada ya kupewa taarifa ile moyo wake ukamlipuka, mapigo ya moyo yakaanza kudunda kwa kasi kupita kawaida, mzunguko wa damu yake ulikuwa ukizunguka kwa kasi sana. Yusufu hakuongea kitu, machozi yalikuwa yakitiririka katika mashavu yake, moyo wake ulijisikia uchungu kupita kawaida.
“Ninakuja huko huko” Yusufu alisema na kisha kukata simu.
Akabaki akiwa amepigwa na butwa kitandani pale, moyo wake ulikuwa ukifikiria zaidi kuhusiana na baba yake, kosa alilolifanya mke wake ambaye alimpa talaka, Samiah likaonekana kuwa kubwa kwake na ndilo ambalo ilikuwa limesababisha yale yote kutokea. Alichokifanya Yusufu ni kumpigia simu Kelvin na kumtaarifu kile ambacho kilikuwa kimetokea kwamba baba yake alikuwa amefariki.
Ndani ya dakika ishirini, Kelvin akafika mahali hapo huku akitangulizana na marafiki wengine na kisha kuanza safari ya kuelekea Bagamoyo huku wakiwa pamoja na Yusufu. Kila mmoja ndani ya gari alikuwa akimfariji, hawakujua kwamba huyo huyo Yusufu ndiye ambaye alikuwa amemuua baba yake kwa mikono yake mwenyewe.
Walichukua dakika arobaini na tano mpaka kufika Bagamoyo ambapo wakaanza kuelekea katika sehemu ilipokuwa na nyumba hiyo. Tayari watu walikwishaanza kufika mahali hapo, vilio vilikuwa vikisikika katika eneo la nyumba hiyo. Yusufu akashindwa kujizuia, akaanza kulia tena jambo ambalo liiwafanya hata marafiki zake kulengwa na machozi.
Yusufu akaanza kuelekea ndani ya nyumba yao ambapo akakutana na mama yake, Bi Fatuma na kisha kumkumbatia. Wote walikuwa wakilia, walionekana kuumia kupita kawaida. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo watu walivyozidi kujaa ndani ya eneo la nyumba hiyo. Waandishi wa habari hawakuwa mbali, nao wakafika mahali hapo na kisha kuanza kupiga picha kila kilichokuwa kikiendelea.
Taarifa zikatangazwa kwenye vituo vya redio pamoja na televisheni. Kila mtu ambaye aliisikia taarifa ile alishtuka. Hawakuamini kama Yusufu yule yule ambaye alikuwa amepata sana umaarufu ndiye ambaye alikuwa akipitia katika mambo magumu namna ile. Wananchi wakaanza kuamini ushirikina kwa kuona kwamba kulikuwa na mtu ambaye alikuwa amesababisha hayo yote.
“Mmmh! Miezi mitano iliyopita alitalikiana na mke wake, leo hii baba yake amefariki. Nina wasiwasi kuna mkono wa mtu hapa. Kuna mtu ambaye hapendi kumuona akipata mafanikio haya” Mwananchi mmoja alisikika akimwambia mwenzake.
“Yaani na mimi nilitaka niseme hivyo hivyo. Yaani sjui kwa nini Watanzania tuna roho za kwa nini, yaani hatutaki kuwaona watu wakifanikiwa maishani mwao” Jamaa mwingine alimwambia mwenzake.
Mapenzi kwa Yusufu yalikuwa makubwa sana, hakukuwa na mtu yeyote ambaye alifahamu kwamba Yusufu huyo huyo ndiye ambaye alikuwa katika kila kilichoendelea mahali pale. Machoni mwa watu alionekana kuwa mtu asiye na hatia yoyote ile. Uso wa majonzi ambao alikuwa akiuonyesha siku hiyo ndio ndio ambao uliwaonyeshea watu kwamba alikuwa hausiki kabisa na kile ambacho kilikuwa kimetokea.
Vitu vingine viliendelea kama kawaida mhali hapo mpaka pale ambapo Shekhe Oswald alipofika msibani hapo na kisha kuongea maneno machache na mwili kupelekwa msikitini kuswaliwa na kisha kuruudishwa nyumbani ambapo harakati zote za mazishi zikaanza kufanyika mahali hapo.
Ilipofika saa 10:15 watu zaidi ya mia saba ambao walikuwa wamekusanyika mahali hapo wakaanza kuupeleka mwili wa mzee Kessi makaburini kwa ajili ya kuzikwa. Wakinamama walibaki majumbani wakilia, Bi Fatuma hakuamini kama mume wake ambaye alikuwa akimpenda kwa wakati huo alikuwa amefariki dunia na mwili wake ulikuwa njiani ukipelekwa makaburini.
Je nini kitaendelea?
Je nini kitatokea katika maisha ya Yusufu?
Umaarufu atakuwa nao zaidi au utampotea?
Je ataweza kuishi bila kuvunja masharti?