Hadithi: Nitakupata Tu

Hadithi: Nitakupata Tu

Jackal

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2012
Posts
9,971
Reaction score
13,608
NITAKUPA TU
SEHEMU YA 001

*********
Alihisi ilikuwa sauti ya mwanamke, sauti ambayo mwanzo alidhani haikuwa ya mwanamke kutoka na usiku ule kuwa vigumu. Lakini sauti ile bado ilikuwa ikisikika katika ngoma za masikio yake. Sauti ya mwanamke akilia na kuomba msaada, sauti ikipiga kelele za hali ya juu kuonyesha kwanba kunakitendo kiovu kinatendeka. Bado hakuijali sauti ile, alichukulia kwamba labda atakuwa ni malaya amekula pesa za watu sasa analazimishwa kulipa. Bado akapuuza akitembea kuelekea nyumbani kwake.

Licha ya kupuuza lakini safari hii, sauti ikasikika tena kwa karibu. Sauti ambayo ilipita masikioni na kwenda kuweka kituo ndani ya kina cha moyo wake. Sauti nayo ikazidi kuhanikiza, lakini safari hii kwa aina ambayo ili msisimua. Aina ambayo ilifanya kengele za hatari kugonga kichwani. Binti anayefukuzwa kulitaja jina lake usiku ule kulimpa mashaka makubwa. Kwa mara ya kwanza mkono wake ukashuka mpaka alipoihifadhi bastola yake. Kitendo cha kuitwa jina katika mazingira yale kulimpa hisia kuwa kulikuwa na namna, namna ambayo ilitengenezwa kwa aina fulani ya kutaka kitu kutoka kwake.

Wamejuaje niko hapa? Walijuaje nitapita njia hii tena katika muda huu? Yalikuwa maswali yaliokisumbua kichwa chake, yalikuwa maswali yaliomfanya aziamini hisia zake, hisia ambazo hazikuwahi kumuangusha. Sasa akatembea kwa umakini mkono ukiwa juu ya Bastola. Hakujali tena kelele za mwanadada yule. Licha ya kutokuwa na ulahai wowote katika sauti yake, lakini hakutaka kuliamini hilo, akaendelea kutembea.. lakini hakufika popote akausikia mlio wa bastola, mlio ambao uliambatana na yowe, yowe kutoka kwa mwanadada yule. Kwa mara ya kwanza akageuka nyuma, akageuka kukiangalia kilichotokea nyuma.. naam akamuona mwanadada amelala chini tena barabarani.

Hakuonekana kama alikuwa hai. Mbele kidogo ya ulipoangukia mwili wa binti yule, aliwaona wanaume wawili waliovalia makoti meusi wamesimama. Walikuwa wanaume hasa kwa kuwaangalia. Hakutaka kuupoteza muda, hakutaka kuupoteza muda kuwepo eneo lile. Akatokomea akiwaacha wanaume wale wamesimama wakimuangalia. Alitembea akijiuliza maswali mengi sana. Kama lengo lilikuwa ni yeye kwa nini wamemuua yule msichana? Walitaka nishuhudie kitu gani na kwa madhumuni yapi?

Haiwezekani watoke huko kisha waje wamuulie mtu mbele yangu harafu mimi wasinifanye kitu, kuna zaidi ya hili. Alijisemea peke yake akiufungua mlango wa nyumba yake, akaingia ndani moja kwa moja akaenda kujibweteka kwenye kiti. Sauti ya mwanamke yule bado ilikuwa ikijirudia kichwani mwake, bado aliisikia bado masikioni mwake. Akajaribu kuivuta kumbukumbu ya sauti ile kuona kama angeugundua ulahai katika sauti ya mwanamke yule, lakini hakukuwa na kitu chochote kilichoashiria kwamba mwanamke yule alikuwa akimrahai. Ilikuwa sauti iliokatika ukweli, haikuwa na hata shaka ndani yake.

Lakini sasa kwa nini mazingira yake yalikuwa ya kutilia mashaka? Hilo likamfanya ainuke na kuelekea bafuni ambapo alijimwagia maji kisha akarudi chumbani kwake. Akachagua mavazi ya kimichezo akavaa na baada ya hapo akachukua bastola yake na kutoka pale kuelekea kule alipoangukia yule mwanamke. Muda wote aliutamani ukweli wa jambo lile. Haikuwahi kutokea mtu kuuawa mbele ya macho yake. Hii ilikuwa mara ya kwanza na ilimtia mashaka sana. Alitaka kwenda kumuona marehemu, alitaka kumuona kwa kuwa aliamini angekipata kile ambacho kingemsaidia katika kumfahamu marehemu.

Akaurusisha mlango kisha akalifunga geti kwa ndani kisha yeye akauparamia ukuta na kuangukia upande wa nje. Hii ndio ilikuwa njia yake awapo katika shughuli ambayo alihisi ilikuwa na hatari mbele yake. Alipotua akachepuka na kutafuta njia mbadala tofauti na ile alioipita mwanzo. Alitembea usiku sambamba na vivuli vya miti, hata alipotokea sehemu ile bado palikuwa kimya na hata mwili wa mwanamke yule bado ulikuwepo ukionyesha kutokuwa na uhai. Macho yake yaliozoea giza yalikuwa yakizunguka maeneo yote, bado hakuiona dalili ya uwepo wa mtu katika eneo lile. Hakuiona dalili ya kufuatiliwa wala kuwekewa mtego. Mkono wake ulikuwa juu ya bastola akipiga hatua kuufuata mwili uliolala chini bila uhai. Damu ilikuwa imeunda dimbwi kubwa. Akaufikia mwili ule na kuanza kuuangalia kwa makini.

Kwa kuwa hakutaka kuupoteza ushahidi, alichokifanya ni kutoa gloves na kuzivaa mikononi. Akaushika mwili wa binti yule na kuugeuza. Cha kwanza kukiona ni matundu matatu ya Risasi kifuani. Lakini kilichomchanganya katika matundu yale ni jinsi matundu yale yalivyo. Mpigaji alionekana kusimama kwa mbele na sio nyuma kama alivyokuwa akidhani. Hilo likampa picha, picha ya kuwa yeye ndie alikuwa mlengwa. Alikuwa mlengwa kutokana na ukweli kwamba marehemu alionekana hakuwa akikimbia. Bali alikuwa ameshikwa na alikuwa akilazimishwa kukifanya kitu.

Alikuwa akilazimishwa kumuita yeye. Hapo akapata picha nzima kuwa alikuwa akihitajika yeye na sio huyu msichana. Alichokifanya nikuupekua ule mwili, hapo akakutana na vitamburisho vitatu, pamoja na kadi moja kubwa ambayo hii iliikuta kwenye Mkoba, pamoja na Simu yake ya mkononi. Akavichukua vyote na kuvisunda mifukoni. Baada ya hapo akapata wasaa wa kuiangalia sura ya mwanadada huyu. Hapo akakutana na sura nzuri na yakuvutia.

"Watu wanaroho ngumu, ya nini kumuua mtoto mzuri kama huyu? Alinong'ona huku akiinuka tayari kwa kurudi kwake.

***********

Chumba chote kilikuwa kimya, kila mmoja alikuwa ametulia akitizama mbele kuliko na Tv kubwa. Walikuwa wakiangalia taarifa ya habari kutoka shirika la utangazaji nchini. Kila mmoja alikuwa akitarajia kutangazwa kwa habari fulani ambazo zingewafurahisha. Kila mmoja ndani ya chumba kile alikuwa akiisubiri taarifa hiyo kwa hamu. Alikuwa akisubiri kile ambacho kingewafanya wao wawe katika kiwango cha juu katika biashara zao. Lakini ilikuwa kinyume wa kile walichokitarajia.

Taarifa ambayo walikuwa wakiisubiri kwa hamu haikuja kama vile walivyotarajia. Bali vijana wao wanne walikuwa wamekamatwa wakiwa na mzigo wa madawa ya kulevya. Walikamatwa na maafisa wa usalama uwanjani hapo. Kila mmoja akapagawa, kila mmoja akahisi labda yupo ndotoni. Mzigo wao wenye thamani ya bilioni ishirini na mbili za kitanzania ulikuwa umekamatwa. Wakawaona vijana wao wakisukumwa kuelekea katika chumba maalum kwa ajili ya mahojiano zaidi. Chumba kikazizima kwa taharuki. Mmoja akaiendea simu yake na kupiga namba fulani. Muda mfupi simu ya upande wa pili ilikuwa ikiita. Iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa. Hata aliporudia bado hali ilikuwa pale pale.. hilo likawafanya watu wale watizamane.
"Haiwezekani!! Mmoja akanguruma.

"Kuna mchezo, huyu mwingine aliongea huku akishindwa kuuhimili presha. "Jimmy hawezi kutufanyia hivi!!!" Mwingine akaongeza. Lakini bado haikuondoa ukweli kwamba Mzigo wao ulikuwa umekamatwa na kulikuwa na uwezekano hata wao wenyewe wakatajwa. Bado simu haikupokelewa, bado iliendelea kuita kwa muda mrefu. Wajumbe wote wakazidi kushangazwa na hali ile. Lakini kabla hawajakaa sawa wakaisikia simu ikiita. Safari hii ilikuwa ikipigwa.
"Jimmy!!" Aliita.

"Jackson!!" Naye akaita..
"Atafutwe Teddy Harryson!!" Aliongea Jimmy kisha bila kusubiri maelezo yoyote akakata simu. Wajumbe wote wakaangaliana, hakuna alieamini maneno ya Jimmy. Kila mmoja alikuwa akiwaza mzigo wao uliokamatwa. Kitendo cha kuambiwa wamtafute Teddy Harryson bila kupewa maelezo yoyote kuliwakera baadhi ya wajumbe. Lakini wakiwa bado kwenye Mshangao wa kutokumuelewa Jimmy, simu ikatoa mliokuonyesha kuna ujumbe umeingia.

"Mpigie Teddy Mwambie akailete Roho ya Binti mmoja ambaye alikuwa chanzo cha kukamatwa kwa mzigo wetu. Nataka nikikupigia simu kwa mara nyingine unipe taarifa ya Roho Ya huyo Binti kuwasili hapo." Ulisomeka Ujumbe Ule.

ITAENDELEA
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 002
*******
Ilihitajika Roho ya Binti aliesababisha kukamatwa kwa mzigo wao. Mzigo ambao ulikuwa wa mamilioni ya shilingi. Ilikuwa ni lazima wampigie simu Teddy kwa kuifanya kazi ya kuileta roho ya mwanamke huyo. Ilikuwa ni amri kutoka Kwa Jimmy, amri ambayo ilitakuwa kutekelezwa katika usiku ule.

Hilo likafanyika na Roho ya mwanamke alietakiwa ikaletwa sehemu husika. Licha ya kumuua mwanamke yule lakini bado hawakuridhika kwa hilo kutokana na kutokuupata mzigo wao. Wajumbe wote waliokuwepo ndani ya Chumba, wakaufanya mkutano wa kujadili kipi cha kuufanya ili kuupata mzigo wao. Ni ndani ya mkutano huo likapitishwa Jina la Masimba. Alitakiwa kutafutwa kwa lazima, alitakiwa kutafutwa ndani ya muda ule.

Kutafutwa kwa kazi maalum. Kazi ya kujua nani alikuwa nyuma ya ukamatwaji wa Mzigo wao wa madawa. Hawakuamini kuwa mwanamke yule pekee anaweza kuwa chanzo cha kupotea kwa mzigo wao. Walitambua kuna mchezo mchafu, mchezo ambao ulikuwa ukichezwa nyuma ya pazia. Muda mfupi kijana mmoja alitoa simu yake na kutafuta namba, alipoipata akabonyeza batani ya kijani, muda wa sekunde tano simu ikaanza kuita.

"Dogo!" Ilisikika sauti upande wa pili.
"Yeah Mkuu!!" Alijibu kijana Yule.
"Kuna nyekundu au kijani?" Lilikuwa swali kutoka kwa masimba. Alitambua simu nyingi za usiku kutoka kwa kijana huyo hazikuwa za usalama hata kidogo.

"Nyekundu Mkuu, kuna kitu tunahitaji ukifanyie kitu, lakini hatuwezi kuongea kwenye simu. Tukutane coco beach muda huu kama muda upo." Akajibu dogo.

"Nitakuwa hapo muda mfupi, mtanikuta pale kwenye mishkaki." Akajibu Masimba huku akikata simu. Hakutaka kupoteza muda, alichofanya ni kumuamsha Mpenzi wake, akamuaga kuwa anakwenda coco beach na asingechelewa kurudi. Akaruhusiwa huku akiombwa kutozidisha masaa mawili. Alitoka nyumbani kwake kinondoni manyanya, akaelekea kituo cha pikipiki, hapo akamueleza dereva wapi anaelekea. Muda mfupi alikuwa juu ya pikipiki akielekea coco beach kuitikia wito. Kuambia kuwa kuna nyekundu ni dalili ya kuwepo kwa kazi ya umwagaji damu.

Alikuwa ni mtu wa kutumainiwa katika mipango mbalimbali. Alishapewa kazi nyingi na zote alizifanya katika weledi wa hali ya juu. Siku zote aliishi kutokana na kufanyakazi ambazo ni tofauti na kazi yake ya halali. Licha ya kuwa afisa usalama wa Taifa tena wa kutegemewa, lakini upande mwingine alikuwa akishiriki mipango mingi ya hatari. Baada ya Dakika tano walikuwa wamewasili eneo la coco beach.

Akashuka kwenye pikipiki, akaingiza mkono mfukoni akatoa noti ya Elfu tano akampa dereva, kisha bila kusubiri chenji akapiga hatua kuelekea pale alipowaambia wakutane. Alitembea kama mtu wa kawaida, suruali ya Jeans, tshirt nyeupe na raba nyeupe miguuni zilimfanya abadirike na kuonekana kama kijana. Akaendelea kutembea macho yake yakitembea huku na huko. Mbele kidogo akaiona gari ambayo aliifahamu. Ilikuwa gari inayotumiwa na watu wake.

Hii ilimaanisha kuwa wao walishafika kabla yake. Akaendelea kutembea akiipita gari ile kama hakuiona, alipoipita akainama na kuzuga kama anafunga viatu. Lakini muda huo huo macho yake yakitembezwa kwa ustadi mkubwa. Ni hapo alipokiona kitu ambacho kwanza kilimshangaza na pili kilimtia hofu. Wakati ameinama akifunga viatu, alimuona mtu kama Mpenzi wake. Alimuona mwanamke kama Teddy akitembea kwa kificho ndani ya fukwe za coco. Hilo lilimshangaza, halikuishia kwenye kumshangaza tu, bali lilimpa hisia tofauti. Hakuwa amemfananisha Na haitatokea amfananishe Teddy. Lakini amefuata nini hapa? Mbona kama alikuwa akinifuatilia? Yalikuwa maswali, maswali ambayo alihitaji kupata majibu katika wakati ule.

Akaendelea bila kugeuka nyuma, hakutaka kufanya hivyo kuogopa kumshtua Teddy. Hatua kama tano kabla hajawafikia watu wake, masimba akaitoa Ishara kwa watu ambao walikuwa wamekaa mbele yake. Ishara ambayo ilijibiwa haraka na watu wale, kilichofuatia ni kuingia ndani ya gari na muda ule gari likaondoshwa pale coco na kurudi katikati ya mji. Ulikuwa mchezo ambao hakuna ambaye aliuelewa mapema. Wote walijua kwamba lazima wangezungumza palepale ufukweni. Lakini haikuwa hivyo, kila mmoja alishangazwa na mabadiliko ya Masimba.

"Nipeni kazi nishukie hapa." Ilikuwa sauti kutoka kwa masimba. Wajumbe wote wakashangazwa na haraka ile. Mmoja akataka kuhoji lakini alipoangaliana na macho ya Masimba akafumba mdomo na hakukumbuka tena kutaka kuuliza.

"Tuokoeni muda, aliongea tena masimba, safari hii akitaka kuufungua mlango.. lakini akashikwa bega na kijana yule. "Nadhani umeisikia taarifa habari ya jana kuhusu kukamatwa kwa mzigo wa madawa ya kulevya? Akauliza huku akimuangalia masimba usoni.

"Yeah nimeona na nilikuwepo eneo hilo." Akajibu akiangalia nyuma. "Basi ule mzigo ni wa kwetu na tunahisi kuna mmoja wetu atakuwa ameivujisha taarifa za kukamatwa kwa mzigo wetu kwa faida zake." Alieleza kijana yule kwa kirefu kisha akaongeza "Tuna mashaka na Jimmy Lambert, tuna mashaka kwa kuwa anaonyesha kutokuwa na uchungu na mabilioni yetu yaliopotea.
"Umesema mnamuhisi kuwa amewageuka? Akauliza masimba.

"Ndio, tunahisi kwa kuwa hana uchungu na Bilioni ishirini na mbili. Safari alijibu mtu mwingine tofauti na kijana. Masimba akakaa kimya kwanza akionekana kuwaza kitu. Alipokuja kuinua kichwa chake akatingisha kichwa kuonyesha kubaliana na kazi ile. "Tambueni hii kazi ni ngumu na ya hatari sana, ninakwenda kuifanya kwa kuwa pesa iliopotea ni nyingi. Lakini pia naenda kinyume na kazi yangu. Hivyo basi naomba nitakapoanza kuifanya kazi hii sitaki kusikia chochote kikizungumzwa. Pia pesa yangu nusu niingizieni kwenye account yangu.

Kisha tukutane Mbagala rangi tatu baada ya sikutano nitakuwa na chochote cha kuwaeleza!!" Akaongea masimba akishuka ndani ya gari tayari kwa kuelekea kwake. Ule wasiwasi wa kumuona mkewe pale coco beach ndio kwanza ukaanza baada kushuka kwenye gari. Kila alipojaribu kutafuta sababu ya mkewe kumfuatilia nyuma nyuma hakuipata. Hakuwahi kumuhisi mkewe tofauti lakini kwa kitendo cha leo akahisi kuna kitu mpenzi wake amekihisi ama labda wivu ndio unamsumbua.

*******

Aliingia nyumbani akiwa hana wasiwasi, baada ya kuingia akaongoza chumbani ambapo alimkuta mkewe akiwa amelala. Akamuangalia kwa muda mrefu bila kufanya lolote. Alimuangalia mpenzi wake huyu kwa muda mrefu bila kufanya kitu chochote. Hakutaka kwenda pale kitandani, kuna kitu alitaka kukifanya kwa wakati ule.alivikumbuka vitamburisho na mkoba wa yule dada alieuawa usiku wa jana. Akatembea mpaka sehemu yake ya siri ambayo ndio huhifadhi mambo yake mengi.

Akavichomoa vitu alivyovichukua kwa marehemu yule, akatoka nje kabisa na kuanza kuvitizama. Jina lake mwanamke yule lilisomeka kama Asteria Paul. Alikuwa mfanyakazi wa Uwanja wa ndege. Akahisi kitu kama kengele zikigonga kichwani mwake. Alihisi kuna kitu kipo nyuma ya mauaji yale. Akarudisha vitambulisho na kuiwasha simu ya binti yule. Baada ya muda akaenda kwenye majina ya watu waliompigia.. Hakuamini Macho yake Pale alipokutana na namba ya Mpenzi wake ikiwa ndio namba ya mwisho kumpigia marehemu..
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 003

********
Namba ya Mwisho kumpigia marehemu ilikuwa namba ya Mpenzi wake. Hilo likamsisimua mwili wake, ile hisia kwamba mpenzi wake ndiye aliemuona kule coco beach sasa ilikuwa imeupata ushahidi wake. Lakini bado kichwa chake kilikuwa kizito kupindukia kuamini kwamba Teddy ni Mhusika katika tukio la kuuawa kwa mwanamke yule. Hilo halikumpa mashaka zaidi lakini alijiuliza ni vipi ameweza kufanya hilo wakati alikuwa naye ndani kwa kipindi chote.

Ni katika kuyawaza hayo ndipo akaikumbuka siku iliopita pale alipoagwa na Teddy kuwa anakwenda kwao na hatarudi kwa siku hiyo. Kulikumbuka hilo kulizidi kuusisimua Mwili wake. Alitanbua kuna kila dalili za mpenzi wake kuhusika na kifo cha mwanamke yule. Lakini alijiuliza sababu za kumuua mwanamke mbele yake kulikuwa na maana gani kwake? Walikuwa wakimpa ujumbe gani kwake. Hapo akaipata hamu ya kuendelea kuichunguza simu ya marehemu Asteria. Jina la pili kukutana nalo ni la Mtu ambaye aliambiwa amchunguze. Lilikuwa jina la Jimmy Lambert. Alikuwa mmoja kati ya watu waliowasiliana na Asteria Muda Mfupi kabla ya kifo chake. Kila alichokuwa akikiona kilikuwa kama ndoto asioiamini.

Kwa nini jina la Teddy kisha Jimmy? Teddy yupo wapi katika hili? Ana husika vipi katika kifo cha mwanamke huyu? Yalikuwa maswali mazito sana, maswali ambayo hayakuwa na majibu kwa wakati ule. Hakuwa na jibu kwa wakati ule lakini ilikuwa lazima kulitafuta jibu kabla hakujapambazuka. Aliinuka na kuvirudisha vitu vyake sehemu yake, alipohakikisha kila kitu kipo sawa akaanza kutembea kuelekea nje ya nyumba yake. Hakupata hamu ya kulala kwa wakati ule. Uhusiano wa kifo cha mwanamke yule na urafiki wa Jimmy na Teddy kilikuwa kitu kilichomtia shaka na kuvuruga kichwa chake. Safari hii hakutaka kutumia usafiri wa kukodi, aliamua kutumia gari yake mwenyewe. Alikuwa amekata shauri ya kuelekea magomeni Mikumi nyumbani kwa rafiki wa mpenzi wake.

Alitambua huko anaweza akaupata Ukweli kuhusu mauaji ya Binti yule na Uhusiano uliokuwepo kati ya Jimmy na Teddy. Kwa kuwa barabara haikuwa na magari, hapakuwa na ugumu wowote. Aliendesha gari kwa mwendo wa kawaida huku akiwa makini kuangalia kama alikuwa akifuatiliwa. Lakini hapakuwa na kitu chochote kilichomtia wasiwasi. Baada ya muda alikuwa akiegesha gari umbali mfupi kutoka iliponyumba ananyoishi Rafiki wa mpenzi wake. Ilikuwa nyumba kubwa ya vyumba sita, sebule, choo sambamba na jiko. Hakuwa akiishi na mtu kutoka na mumewe kutokuwepo hapa nchini. Masimba alishuka na kuufunga mlango wa gari kisha akaongoza kuelekea getini kwa nyumba ile.

Giza lilikuwa limechukua sehemu kubwa huku ukimya nao ukitawala kuonyesha kwamba watu wengi walikuwa wameshalala. Alitembea taratibu huku akiwa makini na kila kitu, alipolifikia geti akataka kuligonga lakini akagundua kuwa lilikuwa wazi. Hilo likamstaabisha, tokea amfahamu mwanamke huyu hakuwahi kumuona ama kukuta geti hili likiwa wazi. Kitendo cha leo kilimstaabisha sana. Akakata shauri aingie pasipokuligonga geti. Akalisukuma taratibu na kuzama ndani.

Hapo pia akashangazwa kwa ukimya ambao aliukuta ndani. Taa zote zilikuwa zikiwaka, mlango wazi lakini hakukuwa na sauti yoyote kuashiria kama kulikuwa na mtu ama lah. Hilo likampa machale, akajivuta zaidi kuufuata mlango.. akaukuta ni kweli ulikuwa uko wazi. Akaingia na kusogea ndani, bado alipokewa na ukimya. Ukimya ambao hakuwahi kukutana nao katika jumba lile. Ukimya uliomfanya aichomoe bastola yake na kuishikilia mkononi. Akatembea kwa makini huku macho yake yakicheza pande zote. Bado hakuiona dalili ya kuwepo kwa mtu. Akaendelea kutembea huku umakini ukiongezeka. Akatokea sebuleni, kutokea sebuleni tu akahisi mwili ukisisimka.. sebule ilikuwa ilikuwa imevurugwa na vitu kutupwa huku na huko.

Akaikamata bastola yake vizuri kisha akaanza kusogea mbele zaidi na zaidi. Hatua saba mbele akaiona michirizi ya damu. Umakini ukaongezeka zaidi na Zaidi. Akatembea mdomo wa bastola ukitangulia. Alikuwa akitembea kuifuata michirizi ile ya damu. Alikuwa amejiweka tayari kwa kila kitu. Akaendelea kuifuatilia michirizi ile nyuma nyuma, mbele kidogo Akaiona ikiwa imeishia mlangoni mwa chumba fulani mle ndani. Hapo akasimama kwanza, baada ya hapo akausukuma mlango kisha kujitoma ndani. Hapo akajikuta akitizamana na Mwili wa Rafiki Wa Teddy Ukiwa umelala chini huku damu zikionekana kutuama.

Akatembea mpaka pale ulipo mwili wa dada yule. Hakuonekana kuwa na uhai, hakuonekana kama alikuwa hai. Masimba akautazama mwili wa mwanadada yule kwa muda wa kama sekunde tano bila kufanya lolote. Kichwa chake kilikuwa kimevurugika, asteria, na sasa alikuwa ameuawa mwanamke huyu. Kipi kipo nyuma katika mauaji haya? Bado alitaka kujua kiundani zaidi, wakati akiwa bado ameduwaa asijue nini anatakiwa kufanya, akaisikia miguu ya watu ikitembea kisha minong'ono ikafuatia.

Akatulia tuli huku mdomo wa bastola akiuelekeza mlangoni. Bado hatua za miguu na minong'ono ikaendelea kusikika, Sasa zilikuwa sasa hatua zile zilikuwa zikiukaribia mlango ule, punde akakiona kitasa kikitikiswa, wakati huo huo mlango ukasukumwa.. hakusubiri chochote kitokee, hakusubiri chochote kivuruge plani yake, mlio mdogo mfano wa chafya ukasikika, bastola ikakohoa mara mbili.. Hapakuwa na kelele. Ilikuwa miguno tu, miguno ilioambatana na kutambarajika kwa watu.

Masimba akaurudia umakini wake, akatembea mpaka pale ilipolala ile miili ya watu wale wawili, akainama na kuigeuza miili. Zilikuwa sura ngeni machoni, hakuwahi kuwaona popote watu hawa. Alichokifanya nikuwapekua watu wale nakuchukua kila alichokiona kinafaa, kisha akatoweka eneo lile kwa kupitia mlango wa nyuma wa nyumba Ile.
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 004

Aliondoka kwa kupitia mlango wa nyumba ile. Kichwa chake kilishavurugwa kama sio kuvurugikiwa. Hakuamini kama tukio la kuuawa kwa mwanamke yule lingeyavumbua mambo makubwa kama yale tena kwa muda mfupi. Lakini ni nani waliomuua Rafiki huyu wa Teddy? Kwa nini wamuue? Au waliniona nikiondoka nyumbani wakaamua kunifuatilia? Kama walinifuatilia kwa nyuma ni vipi damu ilikuwa imeganda kuonyesha mauaji yalifanyika muda mrefu kidogo? Maswali hayo yakampa hamu ya kumchunguza mkewe, sio mkewe tu bali hata na Jimmy.

Kwani aliondoka nyumbani akiwa peke yake, hakuona kitu chochote kilichompa wasiwasi kama alikuwa akifuatiliwa, sasa ilikuwaje kufika tu nyumbani kwa mtu aliekuwa akimuhitaji amkute ameuawa? Hilo likampa kile ambacho hakuwahi kukiwaza, tukio la coco beach lilibeba tukio zima la kuuawa kwa mwanamke huyu. Akatambua kuwa alitakiwa kuwa makini, alitambua kama atakwenda ndivyo sivyo basi anaweza asiimalize kazi hii. Alijua kama mkewe ni mshirika wa Jimmy na kama ni kweli ni yule aliemuona coco beach, basi alijua kuwa lazima atakuwa akitembea na macho ya watu kila mahali.

Akairudia gari yake kwa kutokea uelekeo tofauti, baada ya kuikuta gari yake akawasha kitufe fulani cha kucheki usalama, aliporidhika muda mfupi alikuwa barabarani akielekea nyumbani kwake huku akiubeba utulivu wa Hali ya Juu. Hakutaka kumpa mashaka mpenzi wake, alitaka kumchunguza chini kwa chini. Muda mfupi alikuwa akiingiza gari ndani ya geti la nyumba yake. Akashuka na kurudi getini tena, baada ya kulifunga akaongoza kuingia ndani. Ile anaufungua mlango akapokewa na macho ya Teddy yakimtizama katika namna ya kuvutia. Yalikuwa macho malegevu, macho yanayohitaji kitu fulani.

Masimba alilijua hilo, lakini hakutaka litendeke. Akapiga hatua mbili tatu mpaka aliposimama mwandani wake. Akamkumbatia kwa upendo wa hali ya juu. Walibaki wamesimama katika kumbatio lile, kumbatio ambalo lilidumu kwa muda wa dakika mbili. Kila mmoja akiliwaza lake. Punde walikuwa wakiachiana lakini huku wakiwa wanatizama.. kila mmoja alikuwa akimuangalia mwenzake kwa upendo. Lakini upendo ambao haukubeba maana nzima ya kutizamana kwao. Kwa mbali Masimba alikigundua kile ambacho kilifichika katika mtizamano ule. Kulikuwa na wasiwasi Machoni kwa mpenzi wake.

Hakusubiri zaidi kumuangalia, aliushika mkono wake na kuelekea naye chumbani, hapo wakapokewa na kitanda, kitanda ambacho leo hili kilichelewa kuupumzisha mwili wa Masimba. Akaendelea kupiga hatua kuelekea pale kitandani. Alipofika alimlaza teddy kisha naye akayatoa mavazi yake kisha kujilaza kando ya Teddy. Wakauvuta usingizi kwa muda, usingizi ambao haukua rahisi kwa masimba. Sauti ya mwanamke alieuawa usiku wa juzi bado iliendelea kusikika masikioni mwake, bado hakujua kwa nini ilikuwa vile, bado hakujua wauaji walikuwa na lengo gani. Akapanga siku inayofuata kuelekea nyumbani kwa marehemu. Alitaka kwenda kupeleleza na kujua nini ambacho kipo nyuma. Alitaka kuujua ukweli juu ya kifo cha Asteria, alitaka kujua kuna uhusiano gani na Jimmy. Akaivuta shuka usoni, kisha kuutafuta usingizi.

*******
"Lazima Tumuue." Ilisikika sauti kutoka ndani ya chumba fulani. "Hawezi kucheza na sisi, hata hao waliomtuma tutawamaliza kabla ya jua la kesho kutwa." Aliendelea kuunguruma mwanaume yule. Alikuwa mwanaume wa makamo, mweusi na mwenyekitambi ambacho kilimfanya aonekane kama mkurugenzi au waziri katika wizara fulani. Ukimuondoa mwanaume huyo pembeni alikaa Jimmy na kushoto kwake alikaa mwanaume mwingine ambaye muda wote alikuwa kimya. Kilikuwa kikao ambacho hakikuwa rasmi. Kikaa ambacho kiliitishwa na watu watatu baada ya kupata taarifa ya kuuawa kwa vijana wao wawili. Hilo liliwapa mashaka makubwa sana, mashaka ambayo hapo mwanzo hawakuwa nayo. Ukweli waliujua na walimjua muuaji.

Licha ya kumjua muuaji lakini hawakuwaza kama lingefika huko. Hawakujua kama Masimba angeanza kwa kuwatia Hasara, hawakujua kama wangewapoteza watu wao ambao walikuwa ni msaada mkubwa kwao, kwa mara ya kwanza wakajikuta wakikijutia kitendo cha kumuua Asteria Mbele ya Masimba. Walijua kitendo hicho ndicho kilichosababisha yote ambayo yalitokea usiku wa jana. Kila mmoja akatulia akihitaji kuipa utulivu akili yake ili kupata majibu sahihi juu ya kudili na mtu huyu ambaye ameonekana kuwa kikwazo kwao. Hakuna ambaye aliinua mdomo ama kuufumbua kuzungumza na mtu mwingine. Walinyamaza kumsubiri mtu ambaye ndie mtu wa mipango, walikuwa wakimsubiri Teddy Kupata majibu ya kipi ambacho kilitokea na kipi ambacho kifanyike. Kila mmoja

NITAKUPATA TU SEHEMU YA 003
********

Namba ya Mwisho kumpigia marehemu ilikuwa namba ya Mpenzi wake. Hilo likamsisimua mwili wake, ile hisia kwamba mpenzi wake ndiye aliemuona kule coco beach sasa ilikuwa imeupata ushahidi wake. Lakini bado kichwa chake kilikuwa kizito kupindukia kuamini kwamba Teddy ni Mhusika katika tukio la kuuawa kwa mwanamke yule. Hilo halikumpa mashaka zaidi lakini alijiuliza ni vipi ameweza kufanya hilo wakati alikuwa naye ndani kwa kipindi chote. Ni katika kuyawaza hayo ndipo akaikumbuka siku iliopita pale alipoagwa na Teddy kuwa anakwenda kwao na hatarudi kwa siku hiyo. Kulikumbuka hilo kulizidi kuusisimua Mwili wake. Alitanbua kuna kila dalili za mpenzi wake kuhusika na kifo cha mwanamke yule. Lakini alijiuliza sababu za kumuua mwanamke mbele yake kulikuwa na maana gani kwake?

Walikuwa wakimpa ujumbe gani kwake. Hapo akaipata hamu ya kuendelea kuichunguza simu ya marehemu Asteria. Jina la pili kukutana nalo ni la Mtu ambaye aliambiwa amchunguze. Lilikuwa jina la Jimmy Lambert. Alikuwa mmoja kati ya watu waliowasiliana na Asteria Muda Mfupi kabla ya kifo chake. Kila alichokuwa akikiona kilikuwa kama ndoto asioiamini. Kwa nini jina la Teddy kisha Jimmy? Teddy yupo wapi katika hili? Ana husika vipi katika kifo cha mwanamke huyu? Yalikuwa maswali mazito sana, maswali ambayo hayakuwa na majibu kwa wakati ule. Hakuwa na jibu kwa wakati ule lakini ilikuwa lazima kulitafuta jibu kabla hakujapambazuka. Aliinuka na kuvirudisha vitu vyake sehemu yake, alipohakikisha kila kitu kipo sawa akaanza kutembea kuelekea nje ya nyumba yake.

Hakupata hamu ya kulala kwa wakati ule. Uhusiano wa kifo cha mwanamke yule na urafiki wa Jimmy na Teddy kilikuwa kitu kilichomtia shaka na kuvuruga kichwa chake. Safari hii hakutaka kutumia usafiri wa kukodi, aliamua kutumia gari yake mwenyewe. Alikuwa amekata shauri ya kuelekea magomeni Mikumi nyumbani kwa rafiki wa mpenzi wake. Alitambua huko anaweza akaupata Ukweli kuhusu mauaji ya Binti yule na Uhusiano uliokuwepo kati ya Jimmy na Teddy. Kwa kuwa barabara haikuwa na magari, hapakuwa na ugumu wowote. Aliendesha gari kwa mwendo wa kawaida huku akiwa makini kuangalia kama alikuwa akifuatiliwa.

Lakini hapakuwa na kitu chochote kilichomtia wasiwasi. Baada ya muda alikuwa akiegesha gari umbali mfupi kutoka iliponyumba ananyoishi Rafiki wa mpenzi wake. Ilikuwa nyumba kubwa ya vyumba sita, sebule, choo sambamba na jiko. Hakuwa akiishi na mtu kutoka na mumewe kutokuwepo hapa nchini. Masimba alishuka na kuufunga mlango wa gari kisha akaongoza kuelekea getini kwa nyumba ile. Giza lilikuwa limechukua sehemu kubwa huku ukimya nao ukitawala kuonyesha kwamba watu wengi walikuwa wameshalala. Alitembea taratibu huku akiwa makini na kila kitu, alipolifikia geti akataka kuligonga lakini akagundua kuwa lilikuwa wazi. Hilo likamstaabisha, tokea amfahamu mwanamke huyu hakuwahi kumuona ama kukuta geti hili likiwa wazi. Kitendo cha leo kilimstaabisha sana. Akakata shauri aingie pasipokuligonga geti.

Akalisukuma taratibu na kuzama ndani. Hapo pia akashangazwa kwa ukimya ambao aliukuta ndani. Taa zote zilikuwa zikiwaka, mlango wazi lakini hakukuwa na sauti yoyote kuashiria kama kulikuwa na mtu ama lah. Hilo likampa machale, akajivuta zaidi kuufuata mlango.. akaukuta ni kweli ulikuwa uko wazi. Akaingia na kusogea ndani, bado alipokewa na ukimya. Ukimya ambao hakuwahi kukutana nao katika jumba lile. Ukimya uliomfanya aichomoe bastola yake na kuishikilia mkononi. Akatembea kwa makini huku macho yake yakicheza pande zote. Bado hakuiona dalili ya kuwepo kwa mtu.

Akaendelea kutembea huku umakini ukiongezeka. Akatokea sebuleni, kutokea sebuleni tu akahisi mwili ukisisimka.. sebule ilikuwa ilikuwa imevurugwa na vitu kutupwa huku na huko. Akaikamata bastola yake vizuri kisha akaanza kusogea mbele zaidi na zaidi. Hatua saba mbele akaiona michirizi ya damu. Umakini ukaongezeka zaidi na Zaidi. Akatembea mdomo wa bastola ukitangulia. Alikuwa akitembea kuifuata michirizi ile ya damu. Alikuwa amejiweka tayari kwa kila kitu. Akaendelea kuifuatilia michirizi ile nyuma nyuma, mbele kidogo Akaiona ikiwa imeishia mlangoni mwa chumba fulani mle ndani. Hapo akasimama kwanza, baada ya hapo akausukuma mlango kisha kujitoma ndani.

Hapo akajikuta akitizamana na Mwili wa Rafiki Wa Teddy Ukiwa umelala chini huku damu zikionekana kutuama. Akatembea mpaka pale ulipo mwili wa dada yule. Hakuonekana kuwa na uhai, hakuonekana kama alikuwa hai. Masimba akautazama mwili wa mwanadada yule kwa muda wa kama sekunde tano bila kufanya lolote. Kichwa chake kilikuwa kimevurugika, asteria, na sasa alikuwa ameuawa mwanamke huyu. Kipi kipo nyuma katika mauaji haya? Bado alitaka kujua kiundani zaidi, wakati akiwa bado ameduwaa asijue nini anatakiwa kufanya, akaisikia miguu ya watu ikitembea kisha minong'ono ikafuatia. Akatulia tuli huku mdomo wa bastola akiuelekeza mlangoni. Bado hatua za miguu na minong'ono ikaendelea kusikika, Sasa zilikuwa sasa hatua zile zilikuwa zikiukaribia mlango ule, punde akakiona kitasa kikitikiswa, wakati huo huo mlango ukasukumwa.. hakusubiri chochote kitokee, hakusubiri chochote kivuruge plani yake, mlio mdogo mfano wa chafya ukasikika, bastola ikakohoa mara mbili.

Hapakuwa na kelele. Ilikuwa miguno tu, miguno ilioambatana na kutambarajika kwa watu. Masimba akaurudia umakini wake, akatembea mpaka pale ilipolala ile miili ya watu wale wawili, akainama na kuigeuza miili. Zilikuwa sura ngeni machoni, hakuwahi kuwaona popote watu hawa. Alichokifanya nikuwapekua watu wale nakuchukua kila alichokiona kinafaa, kisha akatoweka eneo lile kwa kupitia mlango wa nyuma wa nyumba Ile. alikuwa akiitizama saa yake. Muda ulikuwa muda ulikuwa ukienda bila kumuona Teddy, kila mmoja akashangazwa na kitu kile, kila mmoja lishangazwa na kuchelewa kufika kwa Teddy, mmoja akaona aipige namba yake japo kumuuliza. Lakini kinyume chake namba haikuwa inapatikana. Hilo likawashangaza wote, liliwashangaza kwa kuwa taarifa alikuwa nayo na aliahidi kufika hapo katika muda husika. Lakini muda huu alikuwa hapatikani kabisa. Kila mmoja akasonya, akasonya huku akitukana matusi ya nguoni.

*****

Wakati akisubiriwa kule na watu wake, teddy alionekana akiingia katika maeneo ya nyumba ya rafiki yake. Ni ile nyumba ya rafiki yake alieuawa jana.aliukuta umati wa watu umezunguka eneo lote huku polisi wakiwa wamezungusha utepe kuonyesha kuwa hapakutakiwa mtu kupita hapo. Alipenya katikati ya watu mpaka karibu kabisa na waliposimama askari wa usalama. Akawasogelea kisha kuongea nao mawili matatu, wakaonekana askari wale wakimruhusu kupita kuingia ndani ya nyumba ya Rafiki yake.

Alitembea bila kuonyesha wasiwasi wowote mpaka sebuleni ambapo aliwakuta wataalam wa picha wakiendelea kupiga picha mbali mbali, pia walikuwepo wanausalama kadhaa wakitizama hiki na kile, akawapita na kuelekea kule ambapo ilielekea michirizi ya damu. Akatembea akiangalia hiki na kile. Hatua tano akamuona mtu ameinama akiichunguza miili ya watu wawili ambao walikuwa wamelala katikati ya damu. Alimtambua mtu huyo na alimjua. Alikuwa mpenzi wake. Alikuwa masimba akiitizama miili ya wanaume wawili aliowauaa Jana. Akataka kusimama lakini alijikuta akiendelea kutembea baada ya masimba kugeuka na macho yao kukutana.
 
NITAKUPATA TU

SEHEMU YA 005

Alitaka kusimama asiendelee na safari yakuelekea pale alipochuchumaa Masimba. Kitendo cha kumkuta mpenzi wake kulimpa picha mbili tofauti. Picha ambazo hazikuonyesha kumfurahisha yeye. Hata masimba alipogeuka na macho yao kukutana, bado alitembea na bado alikuwa akimuangalia kwa mashaka. Hata masimba alikitambua kitendo kile, lakini hakutaka kumshtua, hakutaka kumuonyesha kama anajua kitu. Baada ya Teddy kusogea pale, kwa mara ya pili masimba akainua uso na macho yake kumtizama Teddy.

Alimuangalia kwa muda kisha kurudisha macho yake kwenye mwili wa Marehemu, alimuona jinsi alivyolala uso wake ukiwa umekunjamana kutokana na maumivu ambayo aliyapata wakati anauawa. Kila alipokuwa akimuangalia marehemu ndipo hasira juu ya mpenzi wake ziliongezeka. Alitambua kuuawa kwa mwanamke huyu ilikuwa ni kuzibwa mdomo juu ya kitu fulani ambacho hata yeye alihisi kuwa labda utakuwa ule mzigo. Kwa mara nyingine akajiapiza kuyafikia makazi ya Jimmy Lambert.

Matundu mawili ya risasi kifuani na mawili shingoni ikikuwa ni kithibisho kuwa marehemu huyu hakutakiwa kuachwa hai. Baada ya kuridhika na kile alichokifanya pale akainuka, akaongea mawili matatu na mpenzi wake, alipomuacha hapo akaongea na wana usalama kisha akaondoka maeneo yale kuelekea nyumbani kwa Marehemu Esteria. Kwa kuwa hapakuwa mbali na eneo ambalo alikuwepo, masimba hakuona tatizo kutembea kwa miguu.. alitembea huku sura ya wasiwasi ilionyesha mpenzi wake ikijirudia. Hakuwa na wasiwasi pale alipotembea hapa na kutokea pale.

Hakuwa na mashaka kuwa anafuatiliwa kwa kuwa walikuwepo vijana ambao walikuwa wakimfuatilia kwa nyuma kuangalia nani ambaye alikuwa nyuma yake. Bado alitambua mkewe alikuwa nyuma ya matukio haya, alijua Teddy alikuwa katika hili. Hilo lilimpa matumaini ya kugundua kuhusu mzigo uliokamatwa, na hata kuugundua ukweli mwingine ambao umefichwa kwa njia moja ama nyingine. Akaifikia nyumba ya marehemu Asteria.

Askari walikuwa wengi wakilinda eneo lote. Kila mmoja alikuwa makini kwa kila hatua. Masimba akawafikia na kuongea nao mawili matatu, punde alikuwa akipiga hatua kuelekea ndani ya nyumba ile iliojaa waombolezaji. Kila mtu alionekana ni mwenye uchungu sana. Kila mmoja alikuwa akilia kwa uchungu wa hali ya juu. Hilo likampa Masimba wakati mgumu. Wakati wakupata maelezo kutoka kwa ndugu wa marehemu Asteria. Alitembea macho yakitizama kila sura ya mtu aliekuwepo pale, siku zote alitambua kuwapo katika tukio lile na umati wa watu kiasi kile, ni njia moja wapo ya kuweza kumtambua ama kumshuku kwa macho, vile tu hisia zake zitakavyo. Kila sura ilionyesha majonzi, kila mmoja alionyesha kuumizwa na kifo cha Asteria.

Hilo likamfanya masimba aikumbuke sauti ya msichana yule wakati alipokuwa akimuita. Hapo akahisi kitu kikimkaba kwenye koo. Kwa nini hakusimama kumsaidia binti huyu anayeonyesha kupendwa na watu? Alipewa kazi ya kuchunguza mzigo uliokamatwa, mzigo ambao haijulikani kama ni wote ambao umekamatwa. Lakini sasa alikuwa amebeba uchunguzi wa vifo vya watu wengine wawili. Vifo ambavyo vinaonyesha kuwepo na uhusiano wa kupotea kwa mzigo ambao alipewa kazi ya kuuchunguza. Alitembea kwa utulivu mpaka sehemu moja ambayo walikaa wakina mama wengi wakionyesha kumshika mama mmoja ambaye alionekana hajiwezi kwa kilio. Baada ya kufika hapo akaongea na dada mmoja ambaye alifanana sawia na marehemu Asteria.

"Wamemuua mdogo wangu, wamemuaa kwa sababu ya uaminifu wake kazini!" Alianza kuongea dada yule huku akiangua kilio. "Najua una uchungu, najua unaumia, lakini hatuna lakufanya kwa kuwa limeshatokea. Naomba ufute machozi kwa kuwa niko hapa kwa kazi yakutaka kujua nani wapi nyuma ya kifo hiki. Futa machozi. Kisha nataka unijibu maswali kwa uchache. Aliongea masimba huku sasa akitoa kijitabu kidogo.
"Tunaweza kuanza mazungumzo.. nataka kujua kila kitu unachokijua wewe kuhusu marehemu.' Akaongea masimba huku akijiandaa.

Dada wa Asteria alimuangalia Masimba, kisha kwa sauti ya upole akaanza kumueleza.
"Asteria ni Mdogo wangu na mimi ndio msiri wake. Hakuwa akinificha chochote katika maisha yake. Wiki mbili zilizopita alinipigia simu akiniambia kwamba kuna kitu anataka kunieleza, lakini kitu chenyewe ni Cha hatari na hatuwezi kuzungumza kwenye simu. Baada ya kuniambia hivyo nilimshauri aje nyumbani anieleze kisha tuangalie hatua za kuchukua. Kweli Asteria alikuja siku ya pili yake usiku, tena akiwa katika mavazi ya ajabuajabu ambayo yalifunika mpaka uso wake.

Ki ukweli aina ile ya mavazi na uingiaji wake ndani, ulinifanya nihisi kuwa kweli mdogo wangu alikuwa katika hatari. Basi sikutaka kumhoji kuhusu yale mavazi na hata uingiaji wake, nilimtaka aniambie tatizo lake. Ndipo hapo aliponieleza kuwa kuna watu matajiri wanataka wasaidiwe kuingiza madawa ya kulevya yenye thamani ya mamilioni ya shilingi. Lakini sasa wanataka wawasaidie kuingizwa na kama yakifanikiwa Basi kila mmoja katika kitengo chao angepewa shilingi milioni mia tano.

Na wenzake wotw wamekubali na anayesubiriwa ni yeye. Baada ya maelezo hayo nikamwambia wewe unaamua nini? Akasema yeye hayupo tayari, na aliongeza kuwa alitaka kukutana na mpelelezi aitwaye masimba amueleze hicho kitu kwa kuwa kulikuwa na mtu wake wa karibu anashirikiana na mtu anayeitwa Jimmy pamoja na viongozi wa serikali. Siku ambayo aliondoka hapa kumfuata Huyo mpelelezi, mdogo wangu hakurudi Tena akiwa hai. Amerudi akiwa marehemu." Alimaliza kuongea yule dada wa marehemu huku akiangua tena kilio.

Mishipa ya hasira na uchungu ilikuwa usoni kwa masimba. Kumbe marehemu alikuwa akimtafuta yeye, kumbe marehemu alikufa akitaka kuikabidhi siri mikononi mwake. Kwa nini hakusimama kumsikiliza. Masimba akatulia akifikiria kwa uchungu. TEDDY mpenzi wake alikuwa akihusika katika kifo cha Asteria. Akainuka akitaka kuondoka lakini akashikwa bega. Alipoinua kichwa alikutana na sura ya mama mzaZi Wa Asterina, akimuangalia kwa macho makali, macho ambayo hayakuonyesha woga. Wakaangaliana tena na tena.. Mama akataka kuongea kitu lakini sauti haikutoka.
*********
Walikaa kwa muda mrefu wakiisubiri simu kutoka kwa Teddy. Lakini bado simu yake haikuwa ikipatikana. Kila mmoja alikuwa akichanganywa na Ukimya ule. Lakini wakati wakiendelea kusubiri wakauona mlango ukifunguliwa. Teddy alikuwa akiingia akionekana hana tabasamu lake. Kila mmoja akabaki ameduwaa akimuangalia mwanadada huyu usoni.

"Kuna watu wawili wanatakiwa kufa". Akaongea Tedy kisha ukimya na hamaniko kutoka kwa watu wale likionekana. Kila mmoja alikuwa amekanganywa na maneno ya Teddy. Huna ambaye aliinua kinywa chake kuongea chochote. Mshangao bado uliwazubaisha. Wakiwa bado katika hilo teddy akaingeza.

"Hili Suala lipo mikononi mwa Idara ya Usalama wa Taifa. Vijana wanafanyakazi kubwa sana kutokana na vifo hivi. Masimba amelishikia bango hili suala na muda sio mrefu tunaweza kuumbuka." Teddy akaeleza mienendo yote ya masimba, mazungumzo yake na ndugu wa asteria. Na kuhusu watu wao waliouawa usiku wa kuamkia leo na kutoweka kwa Simu zao. "Sasa ni lazima mama wa Asteria na dada yake wauawe katika njia yoyote. Tukiwaachia hapa kisha wakakutana tena Na masimba kamwe hatutaweza kupona. Ni lazima wafe na ikibidi Hata Masimba Naye atawafuata.

No photo description available.
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 006

Lazima tuwaondoe duniani, na ikibidi hata masimba atawafuata huko huko kuzimu. Hili suala bado gumu sana. Kukutana kwa masimba na wenzetu kule coco beach, kutoweka simu ya Marehemu Asteria pamoja na simu za vijana wetu, ni moja kati ya vitu hatari sana. Ninachoamini mimi Dada wa marehemu Asteria kuna kitu atakuwa anakijua kuhusu kifo cha mdogo wake, nilazima asteria alimpa siri kuhusu sisi. Kwa hiyo ilikujiweka katika mazingira sahihi nilazima tuwaondoe hawa watu. Nina amini hata masimba kuna kitu amekigundua kwangu, nadhani hata pale coco beach aliniona ndio maana hawakukaa sana. Sasa ni wajibu wetu kufanya kile ambacho kitatuweka salama zaidi. Kwani hata watu wa Idara ya Usalama Wa Taifa wamecharuka katika hili, nahawa ndio wanaompa nguvu huyu mwanaume, kwahiyo kwangu mimi nimemaliza na hii ndio mipango yangu." Aliongea Teddy kwa kirefu huku akiwaangalia wanaume wale wa tatu kwa zamu.

Kila mmoja alionekana yupo mbali kimawazo, kila mmoja alionekana akitafakari kuhusu jambo hili. Ukimya ukachukua nafasi katika eneo la chumba chote. Ni kweli hakikuwa kitu kidogo, lakini licha ua ukubwa wa kitu hiki hauwezi kuzuia mapambano. Mapambano sababu ya kupigania mamilioni yao ya Shilingi. Walikuwa tayari kumuua mtu yoyote kwa sababu ya pesa. Kila mmoja alikuwa akiutafakari ujumbe ulioletwa pale. Walihitajika kuawa watu wawili, na ikibidi watu watatu. Watu ambao watawafanya wao waishi kwa usalama zaidi. Watu ambao watakifanya kitendawili cha mzigo wao kubaki katika usiri nzito. Lakini watamuuaje masimba?

Nani atainua bastola na kulenga kichwa ama kifua cha masimba? Hayo yalikuwa maswali ambayo yalikuwa yakipita vichwani mwao. Bado ukimya ulitawala na bado hapakuwa ni mtu wa kuzungumza. Kama Idara ya usalama imecharuka nini hatima yao katika hili. Walijua hapakuwa panahitajika nguvu, wakajua kutumia nguvu nikutafuta kushindwa katika hili pambano. Kila mmoja alitaka kuwa huru katika hilo. Kama simu za vijana wale zimetoweka, na simu zenyewe zilikuwa na mawasiliano walioyafanya na vijana hawa, nini ambacho kingewaponyesha.. hapo ndio walipouona Umuhimu wa kumuondoa Masimba kwanza kabla ya dada na mama wa Asteria. Kwa mara ya kwanza Jimmy aliamua kusimama kuzungumza kuhusu hilo. Kila mmoja alikuwa akimtizama akisubiria kusikia kile alichotaka kukizungumza.

******
Baada ya kumaliza kuongea na mama wa Asteria sambamba na dada yake, masimba akaona ni muda wa kuelekea nyumbani kwake huku akifikiria ni kipi ambacho atakifanya kuhusu mpenzi wake. Hakutaka kukurupuka katika hilo lakini kule kuambiwa na dada wa asteria kuhusu ukaribu wake na mmoja ya watu wenye mzigo huo, kulizidi kuitoa picha kuwa bado Teddy ni mhusika katika matukio yote ya mauaji. Ukianzia kuikuta mamba yake kuwa namba ya mwisho kuwasiliana na marehemu Asteria, kumuona coco beach usiku ule, kuonyesha wasiwasi alipomkuta akikagua miili ya watu wale mawili ni matukio ambayo yalimuaminisha na kuzifanya hisia zake kuwa sahihi.

Licha ya kutembea pasipo na tahadhali, lakini bado alitanbua kuwa alikuwa na vijana wake wakimuangalia kila hatua. Alitambua umuhimu wa vijana wake. Wakati anataka kutokea kituo cha magomeni Hospital, akavutiwa na kitu fulani ambacho alikiona upande wa pili wa barabara. Licha ya kitu hicho pia hata simu yake ilipokea ujumbe kutoka kwa vijana wake. "Kuna vichwa viwili Vimeunda Urafiki nawe" ulisomeka ujumbe huo.

Haikuwa kazi ngumu kuijua maana halisi ya ujumbe ule. Hata macho yake yalipoangaza katika maeneo yale ni kweli yakakutana watu wawili ambao walikuwa katikati ya umati wa watu ambao walikuwa wakisubiri usafiri wa kuelekea makwao. Ingawa watu hawa walijichanganya na abiria, lakini bado muonekano wao ulikuwa ni wakipekee, bado hawakuonekana kutulia hasa machoni mwao. Kila wakati walikuwa wakimwangalia Masimba kwa namna fulani ya kipekee. Aina ambayo haiwezi kufichika machoni kwa watu wenye fani ya ujasusi. Watu wale wawili, wakike na kiume bado walisimama wakionekana wakisubiri kitu, hata pale magari yaliposimama bado hawakupanda, bado hawakuonyesha kama walihitaji kupanda. Masimba akatabasamu kisha kupiga hatua akielekea pale waliposimama.

Alitembea sawa na watu wengine waliokuwa wakiivuka barabara. Hata walipofika kituoni, gari ya kwanza kusimama masimba akapanda akiwaacha watu hawa wakihamanika. Lakini bahati nzuri konda aliwaona na kumuomba dereva asimame. Ni wakati watu wale wakipanda ndipo masimba alipoisikia miluzi na mayowe kutoka nje, watu waliokuwa wakishangilia kitu walichokiona. Akaruhusu macho yake yaelekee huko. Hapo hata yeye akashikwa na butwaa la muda, butwaa huku macho yakivutika kwa kile kinachopita nje.

Alikuwa akitembea kama twiga nyikani, alikuwa akitembea kama anaiogopa ardhi. Miguu ilitua kwenye ardhi kanakwamba haitaki. Alitembea akijitupa huku na huko. Kivazi chake kifupi kilikuwa kikiwavuta na kuwakata shingo wanaume kwa wanawake. Hata alipokuja kuingia kwenye daladala bado masimba alikuwa akimtizama, bado alikuwa akimuangalia twiga huyu, twiga alietoroka mbugani na kuja mitaani. Binti alikuwa haonyeshi kujali, haonyeshi aibu na kingine hakuonyesha kwamba labda angemuonea yoyote aibu. Ndio kwanza alikuwa akijipinda na Kujigeuza. Alikuwa akijishika hapa na kujiachia hapa. Hata pale alipokuwa akimtizama alihisi alikuwa akitizamana na Heaven Sent, ama alikuwa akiitizama picha yake. Alikuwa mzuri, alikuwa ameumbwa na alikuwa akivutia hata kutizamwa. Ni hapo binti yule alipotupa macho yake usoni kwa Masimba. Hata masimba alipomtupia jicho na hata macho yao kukutana, Kuna kitu kilionekana machoni kwa mwanamke yule. Kitu ambacho hakikuwa kigeni wala kipya machoni kwa Masimba.

WAKATIZAMANA ZAIDI NA ZAIDI.
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 007

Wakatizamana tena na tena. Masimba hakuwa mjinga katika kile ambacho kilikuwa kikitokea pale. Muda wote alimuangalia yule msichana akikitafuta kile ambacho kilifichwa upande wa pili. Alikitafuta kile ambacho kingempa picha huyu alikuwa nani. Macho pekee ya mwanadada yule hayakuweza kumpa jibu la kwamba huyu alikuwa nani. Jicho legevu kama mtu alieupoteza usingizi kwa muda mrefu halikuweza kumpa majibu alioyataka. Kwa jicho la mwanamke huyu hata jasusi ama mpelelezi wa kiwango cha aina yoyote asingeweza kuligundua hilo.

Akakumbuka kuwa kulikuwa na watu wengine, watu ambao walikuwa wakimuandama kila hatua. Aliwatambua na kuwajua, alihitaji kuutafuta ukweli kutoka kwa hawa na yule mwanamke alievaa mavazi ya kutamanisha. Alitaka kujua kama kunakujuana, kutambuana na hata kufahamiana. Alitaka kuifanyakazi kwa kutumia akili zake. Macho yake yakatembea taratibu yakizibwa na gazeti. Muda wote alihitaji kupata ujumbe kutoka kwa wenzake wakimjulisha kuhusu huyu mwanamke. Lakini hilo halikuwezekana kwa wakati ule, si kuwezekana kwa kuwa hawawezi, la hasha! Hata vijana hawakuwa wamemjua huyu mwanamke.

Akatulia na kutulia tena, punde konda akatangaza kituo kinachofuata. Akili yake ikachemka kwa haraka, kilikuwa kipimo sahihi cha kugundua kama yule mwanamke ni abiria ama alikuwa mmoja kati yao. Akainuka naye akijiandaa kushuka.. macho yake muda wote yalikuwa machoni kwa watu ambao waliambatana naye, kuambatana kwa maana ya kumfuatilia. Bado alikikosa kile ambacho alikuwa akikitafuta. Bado hakufanikiwa kugundua kama walikuwa wakifahamiana ama lah. Akatembea akisogea mlangoni. Alikuwa makini kwa kila hatua, mikono yake ilikuwa tayari kuifanya kazi kama ingebidi. Daladala ikasimama kituo cha kinondoni mkwajuni. Masimba akashuka akiwa pamoja na abiria wawili watatu. Baada ya kushuka hakutaka kuangalia nyuma. Alitembea akiingia hapq na kutokea pale.

Safari yake Hiyo ikaishia Eneo la kinondoni studio. Licha ya kutambua kuwa alikuwa akifuatiliwa tokea pale magomeni, cha kushangaza hakuwaona tena watu wale. Alitumia mbinu zake zote lakini bado hakufanikiwa kugundua chochote. Akatembea sasa akiivuka barabara fulani katika mitaa ile ya kinondoni, wakati anakikaribia kituo fulani cha teksi, mara akaisikia sauti ya mtu ikimuita, sauti ambayo ilikuwa ngeni kwake. Akaipuuza kama hakuwa amesikia. Lakini kwa mara nyingine sauti ile ilikuwa ikimuita tena. Sasa alionekana mtu yule akimuita tena huku akimfuata kule alipokuwa akielekea. Ilikuwa sauti ya mwanamke, sauti ya mtu ambaye hakuwahi kumuona achilia mbali kuisikia sauti ile.

Akajipa kazi ya kugeuka, ni kweli akageuka.. macho yake yakamuona mtu, mtu yule yule ambaye alipanda pale kwenye daladala, mtu yule yule ambaye alimuacha ndani ya daladala. Lakini sasa alikuwa akimuita tena kwa jina lake, jina ambalo halitumii sana. Hakuuficha mshangao, hakuuficha kwa mtu kama yeye kugundua. Amenijulia wapi? Kwa nini anifuate mpaka huku? Nini anakitaka kwangu? Alijiuliza maswali mengi huku akisimama kumsubiri mwanamke yule.

Mwanamke yule akatembea kwa mwendo ule ule wa kuogopa kuikanyaga ardhi. Bado masimba alikuwa akipata kukitafuta kile ambacho alikikosa kule alipotoka. Bado mwanamke yule hakuonyesha uhatari na vilevile hakuonyesha kama alikuwa ni mtu wa misukosuko. Wakakutana na kwa mara ya kwanza wakishikana mikono. Wakasalimiana wakiangaliana. Masimba alimuangalia machoni kwa muda mrefu akikitaka kile ambacho alikihisi. Lakini bado huyu hakuonyesha kama ni mmoja kati ya hao. Bado jicho lake legevu lilitengeneza urembo wa kumvutia mwanaume yoyote lijali. Akataka kusema kitu, lakini kabla hajafanya hivyo akausikia mlio wa simu yake. Akaichomoa kutoka mfukoni na kukutana na kiboksi cha Ujumbe mfupi wa maneno, kuonyesha kuna ujumbe umetumwa. Kidole kikashuka na kuruhusu ujumbe ule kufunguka.

"Ni mmoja wao kuwa makini." Ulisomeka ujumbe ule. Ujumbe uliomfanya atabasamu na kucheka. Kwa mara ya kwanza alikuwa amekutana na mtu ambaye amefanikiwa kuyarahai macho yake. "Ni Mmoja Kati yao" neno lile likajirudia kichwani. Akahamisha macho kwa mwanamke huyu. Bado akakutana na jicho legevu, jicho ambalo liliuficha uhalisia wa kikazi.

"Nadhani hatutaweza kuongea kwa sasa. Chukua mawasiliano yangu nitafute saa mbili usiku. Bila shaka unanifahamu sana hivyo na mimi nataka nikufahamu." Aliongea Masimba huku akitoa business card yake na kumkabidhi mwanamke yule, huku akiondoka katika eneo hilo.

*********

Alishuka na kuingia nyumbani kwake. Akili yake ilikuwa imevurugwa kutokana na mambo kuonekana kuharibika mapema sana. Kitendo cha kuingia kwa masimba katika sakata hili, hakikuwa kitu kizuri kwake na kwa wengine. Hakutakiwa masimba kuijua hii mipango. Lakini kuuawa kwa Asteria wakati akitaka kuonana na masimba kumeharibu kila kitu. Kifo cha Asteria ndicho kikichomuibua masimba. Kutoweka kwa simu ya marehemu na mazungumzo yale, alihisi masimba atakuwa amegundua kuwa yeye ni mshirika wa Mpango ule. Teddy alijikuta kichwa chake kikiwa kizito. Teddy alijikuta katika wakati ambao hakuwahi kuwa nao. Akaelekea chumbani kwao, akaongoza mpaka sehemu anapoweka bastola yake.

Akafungua na kuichukua kisha kuishika mkononi. Aliitizama huku akiwaza. Alikuwa tayari kumuua Masimba iwapo atagundua kama anaijua siri yao. Alikuwa tayari kumuua mpenzi wake kwa sababu ya pesa. Akasimama akiiangalia bastola. Hapo akakumbuka penzi lao lilipoanzia. Alikumbuka mengi.. moyo ukakosa ujasiri. Muda ule ule akahisi mikono ikimshika kiunoni kisha sauti nzito ikasikika. "Usiogope Mpenzi Nakupenda Sana... ilikuwa sauti ya Masimba. Teddy hakutegemea, hata alipogeuka na macho yao kukutana.. Hakuweza tena kumuangalia MASIMBA.
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 008

Usiogope nakupenda sana mpenzi. Ilikuwa sauti ya masimba, sauti ambayo ilitokea nyuma yake.hakuwa amejiandaa na hilo, hakuwa amelitegemea lile la masimba kuwepo pale ndani. Hili likamnyong'onyeza. Akatamani kuongea kitu lakini maneno hayakutoka. Hakujua muda ambao masimba alifika nyumbani, hakutegemea uwepo wake hapo, na hata pale alipokumbuka kitendo alichokifanya, alichoka kwa kuwa alitambua kuwa masimba alikuwa amekishuhudia kitendo kile.

Akaiona akili yake ikishindwa kumsaidia katika kulitatua hili ambalo lilikuwa mwisho wake. Hata pale mikono ya masimba ilipokuwa akipapasa kiuno chake, bado Teddy hakuweza kumjibu. Bado bastola yake ilikuwa mkononi, bado hasira zilionekana usoni, na hata dhamira ya mauaji ilijengeka kupitia macho yake. Hakuweza tena kumuangalia masimba, hakuweza tena kuuinua uso wake kumtizama. Alitazama pembeni na alikuwa ameinamia chini. Mwili ulikuwa unatetemeka, alijikuta kwenye wakati mgumu kupambana na moyo wake. Moyo uliojaa mapenZi juu ya masimba, moyo ambao haukuwahi kumpenda mwingine zaidi ya huyu mwanaume. Mwanaume ambaye alichukua asilimia mia moja katika moyo wake?

Ni vipi ataweza kuitumia bastola kumlenga huyu mwanaume? Ni vipi angeweza kukiruhusu kidole chake kutekenya kitufe kuruhusu risasi imuue Masimba? Ni vipi pale atakapoiona Risasi ikimtupa masimba chini huku damu zikisambaa? Hapo akauona ugumu, ugumu wa kufanya kile ambacho alitaka kukifanya, lakini vilevile aliyafikiria mabilioni ya shilingi. Kwa mara nyingine akakiona kichwa chake kikitaka kupasuka. Lakini mpapaso wa mikono ya masimba ukamfanya teddy aachie mguno.

Mpapaso ambao ulipanda mpaka kwenye kifua chake kilichobeba viazi vidogo. Mikono hiyo ikatulia hapo kwa muda ikitomasa na kuchezea kwa ustadi mkubwa. Hilo likaanza kumlegeza teddy, likamuacha teddy akisinzia na kulegea. Masimba akamgeuza na kufanya wote watazamane. Watazamane katika namna ya kuhitajiana. Jicho lilikuwa usingizini na hata midomo ikawa tayari kupokea zawadi. Wakatizamana zaidi, muda huu nguo zilikuwa zikitupwa chini baada ya kuvuliwa.

Bastola ilianguka pasipo hata teddy kugundua. Alikuwa akihema kama mwizi, alikuwa akihema kama ametoka kukimbia mbio ndefu. Hakuwa teddy yule aliekuwa ameapa kumpoteza masimba. Hakuwa teddy yule mwenye uwezo wa kunyoosha mkono kumuua masimba. Huyu alikuwa kondoo, kondoo anayetii mamlaka ya bwana. Akasogezwa kitandani, hata yeye mwenyewe akasogea, akakalishwa kitandani, hata mwenyewe akakaa, na hata kulala, akalala huku macho yake yakiwa yamefumbwa na kufumbika. Midomo bado ilihitaji kupokea kitu, kitu ambacho kingeianzisha safari nyingine. Ilikuwa hivyo.

*****
Alishtuliwa na mlio wa simu yake, akaupeleka mkono pembeni yake ambapo alikuwa amelala masimba. Lakini akashangaa kutokuwepo kwake. Bado simu yake iliita, lakini aliendelea kuipuuza. Sasa alikuwa akiinuka kutoka pale kitandani na kuelekea kule sebuleni. Akalifunua pazia akidhani atakutana na masimba hapo, lakini hapakuwa na mtu. Hilo likamshangaza tena na tena. Haikuwa kawaida ya masimba kumuacha kitandani. Wakati akiendelea kuumizwa na hilo bado simu chumbani iliendelea kuita.

Safari hii mpigaji alikuwa akipiga kwa mara ya tatu. Akakata shauri kurudi chumbani kwenda kuipokea simu hiyo. Akazivuta hatua zake taratibu akiwa mtupu kama alivyozaliwa.akasogea na kuingia chumbani huku mawazo yakiwa ni wapi alipoelekea masimba. Akaifikia simu na kuichukua, macho yakatua juu ya kioo.. akakutana na jina la mtu alieufanya moyo wake upige kwa haraka. Jimmy Lambert ndiye aliekuwa akiipiga simu. Akakipeleka kidole chake na kupokea simu.

"Jimmy." Aliita tedy kwa sauti ndogo yenye kuonyesha uchovu.
"Vipi umelala au?" Lilikuwa swali kutoka kwa Jimmy.
"Yeah! Nilikuwa nimelala, kuna lolote? Alijibu kisha kuuliza.

"Naomba Uje Tegeta muda mfupi ujao, kuna mtu nataka mkutane, mfahamiane na mtambuane. Tumeona tukutafutie mtu wa kusaidiana naye." Alijibu Jimmy kisha akakata simu bila kusubiri jibu kutoka kwa Teddy. Hilo la kutafutwa kwa mtu likaupa mashaka moyo wake. Ni kweli pesa alizitaka na kuzihitaji. Ni kweli anampenda masimba kuliko maelezo. Lakini hata kama atamuua masimba, wapo wanaume wengine ambao watamuoa. Kinachotakiwa ni kupanga njia ipi sahihi ya kumuua. Kwa mara nyingine roho yake, akili yake ilikuwa tayari tena kumuua masimba. Alikuwa amedhamilia na alikuwa ameamua kumpoteza. Alichokifanya ni kujiandaa kwa safari ya kuelekea huko tegeta huku akiwa na nguvu na maamuzi sahihi.

Wakati yeye akitoka na kulifunga geti, masimba alikuwa nyumba ya tatu kutoka pale. Alikuwa amesimama hapo kwa muda mrefu akitizama kila kitu ambacho kiliendelea pale. Muda mfupi akamuona mpenzi wake akilifunga geti na baada ya hapo akamuona akiondoka pale kwa kutembea kwa miguu. Bado alitulia akiendelea kuangalia kila kitu ambacho kilikuwa kikitendeka pale. Bado mpenzi wake aliendelea kutembea akielekea kituo cha daladala. Hilo pia lilimpa nafasi ya kumfuatilia pasipokuonekana. Simu ilikuwa sikioni akiwasiliana na vijana wake, alikuwa akiwaeleza kila kitu cha kufanya. Aliwaaachia wao kazi ya kumfuatilia Teddy. Alichokuwa akipokea ni maelezo ya nini kinaendelea katika hilo.

******

Teddy alitembea mpaka kituo cha daladala, alipofika hapo akatulia akiangaza macho yake huku na huko. Alikuwa ametulia kwa muda akitizama kila mienendo ya watu. Alikuwa na hisia za kufuatiliwa, lakini kila alipopitisha macho yake sehemu zote, hakuweza kumuona mtu ambaye labda angepata mashaka naye. Baada ya kuhakikisha hilo, akaingia kwenye daladala na muda mfupi gari likaondoka likielekea Tegeta. Ilikuwa safari ambayo kwake ilikuwa muhimu sana.

Walikuwa na mzigo wa mamilioni ya shilingi lakini bado haikuwezekana kuuza kutokana na matukio haya yanayoendelea kutokea hakuwa tayari kuiacha pesa ile kwa sababu ya mwanaume. Moyoni alijisemea kwamba labda angekuwa mama yake ndipo angefanya hivyo. Wakati akiwaza hakujua kwamba kuna watu walikuwa siti ya nyuma yake wakimtizama. Walikuwa vijana wawili wadogo kiumri, vijana ambao kwa kuwaona ungedhani labda ni wanafunzi wa sekondary.

Lakini haikuwa hivyo, hawa walikuwa vijana kutoka kitengo nyeti katika nchi hii. Walikuwa wakiendelea kuzungumza hili na lile, huku mara moja moja wakimtupia jicho mwanadada huyu. Kilikuwa kitu kizuri sana kumfuatilia mtu ambaye hajui kuwa anafuatiliwa. Gari ilipofika tegeta kwa ndevu vijana wale wakasimama tayari kwa kushuka. Hata teddy naye alikuwa akishuka hapo. Alitangulia yeye kushuka, kisha wakafuatia wao kushuka. Baada yakushuka vijana wale wakangoza kuelekea barabara fulani. Hata teddy alikuwa nyuma yao akifuata barabara ile. Hakujua kuwa waliombele yake hawakuwa mabishoo kama alivyodhania, bali walikuwa makachero wakifuatilia kila hatua yake na kila kitu anachokifanya.

ITAENDELEA

May be an image of 1 person
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 009
Hakujua kuwa alikuwa njia moja na wanausalama. Hakujua kuwa vijana waliombele
yake walikuwa wanausalama, tena wakimfuatilia yeye. Bado aliongoza akitembea kwa umakini, akichungulia na kuangalia kila sehemu kwa chati.

Alikuwa tayari kumuua mwanaume anayempenda kwa sababu ya pesa. Licha ya kuwa tayari lakini hakuujua mwisho wa mambo yale utakuwa nini. Kingine kilichomtatiza ni mtu ambaye ameambiwa kuwa ameongezwa katika kazi ile ya kumfuta masimba katika uso huu wa dunia. Kilikuwa kitu kigumu mwanzo lakini kila alipokumbuka kifo cha Asteria na Rafiku yake, alijikuta akinong'ona mwenyewe. Muda nfupi
baadae alikuwa akiingia ndani ya Bar moja maeneo yale ya tegeta. Baada ya kuingia, akaongoza mpaka moja kwa moja katika vyumba vya eneo lile. Akauendea mlango wa chumba ambacho huwa wanakutaniana. Akaugonga mlango katika namna ambayo ilitambulika ama kuzoeleka miongoni mwao. Mlango ukafunguliwa
kisha akaruhusiwa kupita. Alipoingia mlango ukafungwa tena.

Macho yake yakatembea usoni kwa kila mmoja, shauku yake ilikuwa ni kumuona mtu ambaye aliambiwa atakuwa nao katika sakata lile. Kila mmoja ndani ya chumba kile alikuwa kimya, ukimya ambao uliyaruhusu
macho yao kutizamana. Sura ya mwanamke mrembo ndio sura pekee ngeni ambayo ilimpa majibu kuwa huyu alikuwa ndie mtu alieletewa ili kusaidiana naye. Akasogea macho yake yakilazimisha kutizamana na mwanamke huyu. Alikuwa akifanya hivyo kutaka kujua kama huyu mwanamke atakuwa mmoja kati ya watu wa aina yake. Ni kweli walitizamana, ni kweli waliangaliana na kuangaliana tena na tena. Lakini hakufanikiwa kukiona kile alichokuwa akikitafuta.

Macho ya mwanamke huyu hayakumuonyesha kile alichokuwa anakitafuta. Hayakumjulisha kama yeye alikuwa nani. Bado yalikuwa macho ya kulegea, macho ya kusinzia na kibaya zaidi hayakumuonyesha chochote kile. Hilo likaonyesha kumpa mashaka. Akatafuta mahala puzuri na kukaa. Bado macho yake
hayakuacha kuonyesha mashaka. Bado hakumuamini mwanamke yule. Ndio alikuwa mrembo, ndio alikuwa mzuri na alivutia katika kutizamwa na hata kuwekwa ndani na wanaume. Lakini licha ya uzuri huo bado hakukiona kile ambacho kingempa picha, picha kwamba anaweza kuzimudu kashkash zote za
wanausalama. Akauvuta muda huku akimtizama Jimmy na wengine waliokuwepo pale ndani.

Alitaka kusikia kutoka kwake, alitaka kusikia kwamba huyu ni nani, na ni vipi atamudu kupambana na masimba. Jimmy ni kama aliyasoma mawazo ya Jenipher. Akasimama kutoka pale alipokaa kisha kupiga hatua kusogea
mpaka pale alipokaa Jenipher. Akamuangalia kwa muda kisha akanena. "Nimekuletea Shetani yule akusaidie kumuondoa masimba katika uso wa dunia hii.." yalikuwa maneno yaliozunguka kichwani kwa teddy.
Hakuuamini ushetani wa mwanadada yule. Alimuona ni kama wadada wa mjini na asingeweza chochote. "Jimmy unadhani ataiweza hii kazi? Tambua tunachokifanya ni kazi ya kifo. Na hii kazi tunaifanya kwa siri sana. Pia tambua watu tunaopambana nao hawana masihara. Una uhakika yule mrembo ni shetani kweli?" Aliongea
Jenipher akionyesha kuwa na mashaka. Tabasamu likachanua usoni kwa Jimmy, kisha likafuatiwa na kicheko, kicheko ambacho kilitumika kama jibu kwa maswali ya Teddy.

Wote wakasimama kwa pamoja kisha kushikana mikono. Mkataba ukaingiwa na makubaliano
kufikiwa. Kilichobaki ilikuwa kazi ya kumuondoa Masimba, kisha wabia wenzao, harafu kugawana
mzigo wao.

********
Wakati Vijana Wake wakiwa tegeta, masimba ndio kwanza alikuwa akiiisimamisha gari mtaa
wa pili kutoka nyumba anayoishi Jimmy. Baada ya kushuka akaufunga mlango. Baada ya kuufunga mlango akaangaza huku na huko, aliporidhika akatembea bila wasiwasi kuelekea ilipo nyumba ya Jimmy. Hakuwa na wasiwasi juu ya kuingia katika jumba hilo kwani vijana wake walikuwa wakimpa taarifa za kile kilichokuwa kikiendelea kule tegeta. Alijua ndani ya muda huo alikuwa na uwezo wa kuingia na kutoka pasipo
wasiwasi wowote. Alitembea kama mwananchi wa kawaida akiangalia hiki na kangalia kile. Mtaa wote ulikuwa kimya, hapakuwa na watu ambao wangemsumbua ama kumtilia mashaka.

Mzigo umekamatwa na kutangazwa katika vyombo vya habari. Lakini cha ajabu mzigo huu unaonyesha
kutokukamatwa, unaonyesha kuna mchezo nyuma ya sakata hilo. Nani yupo nyuma ya jambo hili? Ndio kitu peke ambacho alijiuliza masimba pasipo kupata majibu. Akaendelea kutembea huku mazingira yakimpa uhuru wa kufanya kitu. Sasa alikuwa akiangaliana na jumba la Jimmy Lambert. Lilikuwa jumba la kifahari, likiwa limezungushiwa Uzio, uzio ambao ulikuwa mrefu kiasi chake.

Ukiondoa hilo pia jumba hilo lilizungushiwa nyaya maalum za umeme ambazo zilisaisia kuongeza usalama wa jumba lile. Pia licha ya hivyo vitu, lakini pia hapakuwa na walinzi. Mlinzi alikuwa mmoja ambaye alikaa kwenye geti la mbele. Baada ya kuliangalia vyakutosha sasa aliamua kuingia ndani. Huyu aliamulia kuingia katika Geti la mbele. Akasogea akitembea kawaida sana. Mlinzi wa kampuni binafsi alikuwa mlangoni mkononi akiwa
ameshikilia bunduki aina ya gobole. Masimba akasogea zaidi na zaidi mpaka karibu kabisa na mlinzi yule. Kabla hajazungumza naye chochote. Masimba akachomoa simu kisha kumpa mlinzi yule. Mlinzi akasita kwanza kuipokea.

Akamwangalia mtu huyo usoni, mtu ambaye alikuwa akimpa simu pasipokuongea naye chochote. Macho yake yakakutana na tabasamu, tabasamu ambalo liliitoa hofu ya mlinzi yule. "Ongea Na Jimmy Lambert ana maagizo anataka kukupa." Akaingea Masimba pasipo masihara. Mlinzi yule akalifanya kosa la kupiga hatua
kumsogelea Masimba. Hakufanikiwa kusogea tena kwani pigo moja la karate likatua Shingoni.

Mlinzi akatambarajika chini. Akamvuta na kumuweka kando ya maua ya jumba lile. Alipohakikisha hawezi kuonwa na watu, alilisukuma geti na kujitoma ndani. Alitembea kwa tahadhari kubwa mpaka uani mwa jumba
lile. Akasimama hapo akiangalia zilipo camera za usalama za jumba la Jimmy. Baada ya kuhakikisha hamna chochote kile, akachomoa funguo zake malaya kisha kuichomeka sehemu, punde mlango ulikuwa ukifunguka na kumruhusu Masimba Kuingia.

Baada ya kuhakikisha ameingia, masimba akaichomoa bastola yake na kuanza kuingia kila sehemu akipekua. Kwa kuwa alikuwa akipewa taarifa na vijana wake juu ya uwepo wa jimmy na washirika wake, hakuwa na wasiwasi katika kupekua. Alifungua vyuma karibia vyote kwa kutumia funguo malaya na kuvipekua. Hakuweza
kupata kitu chochote. Wakati anaingia kwenye chumba anacholala jimmy, ndipo hapo alipouona
mlango mdogo, mlango ambao alizani labda ni wachoo ama bafu lakini alipoutingisha ulikuwa
mgumu na haukuwa unafunguka kwa Funguo

Malaya. MASIMBA AKATULIA
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 10
Mlango ulikuwa mgumu na haukuweza
kufunguka hata kwa funguo malaya. Hilo
likamfanya masimba atulie kwanza. Alitulia
akiwaza ni kipi cha kufanya ili kuufungua
mlango. Akawaza na kuwazua huku akijaribu
mara kwa mara kuufungua mlango. Lakini bado mlango ulikuwa mgumu kufunguka. Akaachana
na kimlango hicho kisha kuiendea droo ya
kitanda. Hapo pia akatumia funguo malaya
kufungua, safari hii alifanikiwa. Baada ya
kuifungua droo ile, akayatupa macho yake kwa
chati ndani yake. Cha kwanza kukiona zilikuwa funguo kama tano, funguo ambazo mara moja
alitambua kuwa ni zile ambazo huwenda
zinatumika kuufungua mlango ule. Akazitwaa
kisha kurudi pale mlangoni. Zoezi la kufungua
likaanza tena. Safari hii haikumchukua muda,
kimlango kile kikafunguka.. macho yake yakapokewa na mabegi matano, mabegi ambayo
aliyatambua kuwa ndio ule mzigo ambao
ulitangazwa kukamatwa uwanja wa ndege.
Kichwa chake kikachemka kwa haraka sana,
alitakiwa kuondoka na mabegi yale katika muda
ule. Alitaka kuliacha hili suala katika kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe. Lakini kuna kitu kimoja
kilikuwa kikimtatiza.. mzigo huu usingeweza
kutoka pale airport kwa nguvu ya Jimmy pekee.
Jimmy hakuwa na uwezo wa kuishawishi Idara
ya Usalama pasipo kuwepo kwa msaada wa mtu
mwingine hapa. Mtu huyo ni nani? Lilikuwa swali pekee lililosumbua kichwani mwake. Alitambua
lazima kuna uwepo wa mtu tena mkubwa sana
katika sakata lile. Kwa mara ya kwanza
majukumu yakaendelea kuongezeka. Sasa
alikuwa akimuhitaji huyu mtu wa tatu. Lakini pia
alitambua ahadi ya kupigiwa simu na mwanamke yule mrembo. Baada ya kufikiria kwa muda
mrefu pasipokupata majibu sahihi, akaona huu
ulikuwa wakati wa kuondoka pale ndani, lakini
akajiapiza kwamba ni lazima atoke pale akiwa na
mzigo ule. Akavuta begi la kwanza kisha la pili,
alipotaka kuvuta begi la tatu, masikio yake yakainasa michakato ya miguu ya mtu,
ikionyesha kusogea pale mlangoni. Masimba
akainuka haraka na kujisogeza pembeni kidogo
ya mlango. Punde akauona mlango ukifunguliwa
kisha mdomo wa bastola ukatangulia Mbele, bado
akaendelea kutulia, hata mtu yule alipoingia bado hakujitoa pale. Alitaka kumfahamu huyu alikuwa
nani.akamsubiri mtu yule aurudishie mlango
ndipo amkabili. Hilo likafanyika, muda mfupi mtu
yule alikuwa akitizamana na mdomo wa bastola
huku macho yasio na mzaha yakimtizama. Mtu
yule hakulitegemea hilo, akajikuta akiupoteza umakini, sasa alikuwa akitetemeka. Hakuonekana
kama ni mjuzi katika misukosuko, bali huyu
alionekana kuwa mgeni katika medani hii ya
mapambano. Masimba akaendelea kumtizama
huku bastola yake ikiwa imelengwa kwenye paji
la uso la mwanaume yule. Mara tukio la ajabu likatokea, tukio ambalo lilimfanya masimba
aamini kuwa huyu mtu alikuwa mbwa koko.
Mkojo ulikuwa ukimtoka na kulowanisha mavazi
yake. Hilo lilimfanya masimba apange kumtumia
katika kuyaondoa mabegi katika chumba kile.
Punde alikuwa akiishusha bastola na kuanza kumtizama mateka wake. Hakuongea naye
chochote zaidi ya kumpa Ishara ya kufanya kile
ambacho alitaka kukifanya. Muda mfupi
walikuwa wakitoka nje huku wameongozana,
mateka yule akiwa na mabegi mawili makubwa,
hata masimba naye ilikuwa hivyo. Bastola ilikuwa mkononi akimuongoza mtu yule njia za kupita.
Wakafanikiwa kutoka getini pasipo na ugumu
wowote kwani bado mlinzi yule hakuwa
amerudiwa na fahamu. Alimuongoza mateka
wake mpaka mahali alipoiacha gari yake.
Wakapakia mabegi yao na muda mfupi walikuwa wakiondoka hapo kwa pamoja huku bado
bastola ikizigusa mbavu zake. ****** Ilikuwa yapata majira ya saa nne usiku wakati
Teddy akiwa njiani kuelekea kimara nyumbani
kwa dada wa Asteria tayari kwa kwenda
kuifanyakazi. Wakati anayavuka mataa ya
ubungo, simu yake ya kiganjani ikawa inaita.
Akasonya huku akiitoa simu yake kutoka mfukoni. Jina la Jimmy likasomeka kwenye kioo
cha simu yake. Haraka akapokea na kuipeleka
simu sikioni. "Rudi mikocheni Haraka." Baada ya maneno hayo
simu ikakatwa, rudi mikocheni haraka kisha simu
kukatwa ni kitu ambacho kilimchanganya akili
yake. Atumwe akawaue ndugu wa Asteria,
wakati bado hajakamilisha hilo aambiwe arudi
mikocheni tena! Ulikuwa ujumbe ulioonyesha hapakuwa na usalama. Akaavunja sheria za
barabarani kwa kugeuza gari sehemu ambayo
haikuruhusiwa. Watu waliokuwa pembeni mwa
barabara sambamba na askari wa usalama
barabarani walikishuhudia kitendo kile kwa
karibu sana. Hata walipomsogelea kutaka kumsimamisha, Teddy akawapelekea gari kwa
kasi sana, askari wakaruka na kuangukia
pembeni. Teddy akakanyaga mafuta gari ikawa
inatembea kwa mwendo wa hatari. Kila mmoja
alikuwa akiiangalia gari kwa mshangao. Wengine
waliahangilia na hata kupiga miluzi, lakini wachache walilaani huku wakitukana matusi
mazito. Teddy hakusikia ndio kwanza alikuwa
akiipita Changanyikeni na sasa alikuwa akiitafuta
mwenge. Kila mmoja aliekuwa akiitizama gari ile
ilivyokuwa ikiendeshwa, alifumba macho
akiogopa kutizama. Wakati anafika maeneo ya Mwenge mataa, mbele yake akakiona kile
ambacho kilimfanya aupunguze mwendo. Mbele
yake kurukuwa na diffender tano za palisi na
Askari wasiopungua Ishirini, kila mmoja akiwa na
Sub Machine Gun akiwa ameilekeza kule lilipo gari
la TEddy. Amri ikatolewa akitakiwa kushuka akiwa amenyoosha mikono juuu.. Teddy akatii
huku bastola akiiacha ndani ya gari. Aliposhuka
chini tu huku akiwa amenyoosha mikono askari
wengi walimtambua kuwa alikuwa ni mwenzao,
lakini licha ya kumtambua huko hawakuacha
kumuuliza hili na lile. Baada ya kama dakika tano walimuachia na kumtaka kuwa muangalifu. ******** Alisimamisha gari nje ya jumba la Jimmy,
akashuka na kuingia ndani. Hapo akapokelewa
na mwili ambao haukuonekana kama una Uhai.
Mbele yake alisimama Jimmy sambamba na
washirika wao kila mmoja akionekana
kuchanganyikiwa. Tedy bado hakuwa amekielewa kile kilichokuwa kikiendelea humo
ndani. Hata pale alipoambiwa aingie chumbani
hakuwa bado anatambua kile ambacho
kimetokea. Alipoingia chumbani kisha kutupa
macho yake pale kwenye hazina yao, Teddy
akaporomoka chini akiwa ameishiwa nguvu. Mzigo wao wao wa Mamilioni ya Shilingi ulikuwa
umetoweka. Mzigo uliomfanya awe tayari
kumuua Mpenzi wake haukuwepo tena. Mzigo
uliomfanya amuue Asteria haukuwepo tena.
Umeenda wapi? Nani amewazunguka? Masimba?
Hapana!! Juma Kitumbe? Inawezekana!!! Yalikuwa mawazo yaliopishana kichwani mwake.
Alipoinua kichwa kuwatizama Wenzake, alijikuta
Akitizamana na Midomo Miwili Ya Bastola. NGOMA NDIO KWANZA NI MBICHI
May be an image of 1 person

 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 11
Alikuwa akitizamana na midomo miwili ya
bastola. Washikaji wakiwa katika umakini wa hali
ya juu. Teddy hakuamini kile alichokuwa
akikitizama. Akataka kujaribu kumuuliza Jimmy
kinachoendelea, lakini sauti haikutoka, akabaki
akiitizama midomo ya bastola ambayo ilikuwa umbali mfupi kutoka usawa wa paji la uso wake.
Akili yake ikaganda, ikashindwa kufanya kazi
kwa wakati, mzigo umepotea, harafu tena
anashikiwa bastola! Hilo likamchanganya kama
sio kumshangaza. Akakitamani kitendo kile kiwe
ndoto, lakini bado haikuwa hivyo. Mzigo haukuwepo na kibaya zaidi alikuwa akitizamana
na midomo ya bastola. Akainamisha kichwa chini
akijaribu kukiamini kile kinachoendea pale. Kwa
mara nyingine akainua kichwa kutizama tena,
lakini safari hii hakukiona kile ambacho alikiona
mwanzo. Hakuwa akitizamana tena na midomo ya bastola, hapakuwepo na watu wawili
waliokuwa wameshika bastola. Walipotea na
kutokuonekana kabisa. Mbele ya macho yake
alisimama Jimmy pekee. Hata Jimmy hakuwa yule
wa tabasamu. Huyu alionekana kuchanganyikiwa
na hata kukata tamaa. Uso ulikunjamana kwa hasira, sasa alikuwa akimtizama Teddy kwa
macho yake makali. Uso wake ulikuwa ukiongea
kifo, macho yake yalikuwa yakiitangaza shali. Kila
alipokuwa akimuangalia Teddy mishipa ya hasira
ilikuwa ikizidi kuharibu taswira yake. Alikuwa
akihitaji kuongea na Teddy. Alitambua teddy hakuwa mhusika wa kilichotokea, alimjua tena na
pia aliufahamu uaminifu na hata msimamo wake.
Asingeweza kukifanya kile. Hilo likampa ugumu
kuongea, kitendo cha watu wao kumnyooshea
Bastola kilimpa wakati mgumu sana. Alimjua fika
katika medani ya mapambano, alimjua fika katika medani ya mapigano, huyu alikuwa ni zaidi ya
Jean Claude Van Damme na hata zaidi ya Don Yen
na Hata Jet lee. Kitendo cha kumnyooshea bastola
ni kumkosea sana. Hilo likamfanya Jimmy awe
mnyenyekevu mbele ya mwanadada huyu.
Lakini kile alichokitegemea hakikuwa hivyo.uso wa teddy haukuwa katika masihara tena,
alimuangalia Jimmy kwa macho yenye maswali
lukuki. Akatamani kuongea neno moja lakini
hakuipata nafasi hiyo. Teddy alisimama na
kupiga hatua bila hata kumuangalia Jimmy.
Alitembea akitoka katika jumba lile akiwa ni mwenye hasira sana. Aliuhisi mchezo mzima
kuchezwa na watu wake hao ili kumzunguka. Hilo
hakuwa tayari kuliona likitokea. Alikuwa tayari
kumuua yoyote katika hilo. Alishakubali kumuua
masimba sababu ya mzigo ule, sasa kwa nini
hawa wanataka kunizunguka? Lilikuwa swali ambalo lilikivuruga na
kukichanganya kichwa cha teddy. Bado Jimmy
hakuweza kuongea kitu. Bado jmmy alikuwa
akimkodolea macho. Teddy akakiinua kichwa
chake kwa mara ya pili kisha kumuangalia tena
jimmy. Macho yake yalikuwa yakiongea kitu kingine kabisa. Hakuwa teddy yule mrembo na
mwenye tabasamu, huyu alikuwa teddy tofauti
kabisa. Bado hakuyaondoa macho yake usoni
kwa Jimmy. "Huu ndio Wema wangu? Haya ndio
malipo ya kuwasaidia mzigo wenu? Umenisahau
mimi ni nani? Umesahau kuwa ninauwezo wa kuwaua kwa muda mfupi tu? Sasa naomba
uniambie ukweli, nataka kuujua mzigo uko wapi
na nani ameuondoa hapa. Usipokuwa mkweli
maiti yako itakutwa humu ndani. Aliongea teddy
akimuangalia jimmy pasipo kupepesa macho
bastola ikiwa mkononi. Jimmy alijikuta midomo ikimkauka, akajikuta mate yakishindwa kupita
kooni. Alimtizama teddy machoni kwa muda
mrefu akitamani kuongea kitu. Hakupata neno la
kuongea, alijikuta akianza kutetemeka. Jimmy leo
alikuwa akimuogopa teddy. Akaona kukaa kimya kutasababisha makubwa.
Kwa sauti ya uoga akaanza kuelezea kila kitu
tokea waliporudi na kuikuta maiti ya mlinzi,
akaeleza walivyoingia ndani wakishuhudia
mzigo wao ukiwa haupo. Hakuficha chochote
kile. Baada ya Jimmy kumaliza kuongea teddy hakuongea kitu. Alipiga hatua mpaka nje pale
ulipolazwa mwili wa mlinzi yule. Akaufunua na
kuuangalia kwa makini. Cha kwanza kukiona ni
jeraha shingoni kwa marehemu yule. "Masimba!" Lilikuwa neno pekee kutoka kwa
teddy. Hili likamfanya jimmy aliekuwa
amesimama nyuma kidogo ya teddy asogee na
kuonyesha kushangazwa. "Masimba aliingia hapa
na ndiye aliefanya hiki kitu. Na kama kweli ni
yeye alieuchukua mzigo, itabidi uwasiliane na mwamvita muda huu, ili watakapo kutana ajue
anatakiwa kufanya nini." Aliongea teddy akitoka
pale akionyesha ni mwenye mawazo. *********
Ulikuwa usiku wa saa mbili na nusu pale simu ya
Masimba ilipotoa sauti kuonyesha kulikuwa na
ujumbe mfupi wa maneno. "Upo wapi Masimba?
Uliuliza ujumbe ule. Masimba akatulia kwanza
kujipa muda wa kufikiria. "Nipo nyumbani!" Alijibu nakutulia tena. 'Bila shaka utakuwa upo tayari kwa sasa
kukutana na mimi?" Ujumbe mwingine
ukaonyesha kuuliza. "Yeah! Naomba tukutane Ngamia Pub kigamboni,
nadhani panafaa kwa aina ya maongezi yetu.".
Alituma ujumbe huo ambao ulipokewa kwa
ukimya wa muda mrefu. Kwa mtu aina ya
Masimba aliutambua ukimya ule. Aliutambua kwa
maana moja. Mwanamke yule alikuwa akifanya mawasiliano na watu wengine, watu ambao
alitambua lazima watakuwa wameshaanza
kuelekea sehemu ya mkutano wao. Hakuwa na
shaka kwa kuwa Charty John alikuwepo sehemu
ya tukio akimuangalia kila aingiaye na kutoka.
Hakuwa na shaka kuhusu hilo. Muda mfupi alikuwa akiingia maliwatoni,
akajimwagia maji, kisha kutoka na kuyaendea
mavazi yake. Baada ya kuvaa na kujiangalia
akachukua bastola zake mbili revolver colt na
dernng up automatically na kuziweka sehemu
yake. Baada ya kumaliza hapo akaweka vitu vyake sawa pale ndani. Muda mfupi alikuwa
akiliacha jumba lake akielekea sehemu ya tukio
akiwa katika tabasamu la aina yake. Siku zote
alipenda kucheza na watu wa aina yake, alipenda
kucheza na watu walioupenda mchezo ule.
Alitaka kumalizana na hawa kisha kurudi kwa teddy. Alitaka kumfanya kuwa wa mwisho. ***** Sehemu kubwa ya eneo hili la mjimwema lilikuwa
limechangamka watu wakionyesha kuifurahia
siku hii. Muziki ilikuwa ukisikika, muziki ambao
ulikuwa ukiwa burudisha vijana kwa wazee.
Sehemu yote ilikuwa katika hali ya kupendeza na
hata kuvutia. Charty alikuwa pembeni kabisa macho yake yakiwa busy kutizama kila tukio
linaloendelea hapo. Muda mfupi akaiona gari aina
ya Toyata ikisimama eneo la maegesho. Macho
yake yakavutiwa na watu walioshuka kwenye
gari ile. Hayakuvutiwa kwa uzuri wa mavazi yao
ama sura zao, bali alivutiwa kwa kuwa ndio wale aliowaona mchana wakimfuatilia masimba. Hilo
likamuweka kwenye utayari. Muda mfupi
akamuona mwanamke yule akiingia pale, alikuwa
katika mavazi ya aina yake. Sketi fupi ilioishia juu
ya magoti kwa juu kabisa. Sketi ya kubana na
kusababisha mistari ya chupi aliovaa kuonekana kwa uwazi zaidi. Wateja wote wakageuka
kutizama kule alipokuwa akitokea mwanamke
yule. Miluzi ikasikika na shangwe kutamalaki.
Wakati mwanamke yule akiendelea
kuwahenyesha wanaume na kuzivunja shingo
zao, masimba ndio kwanza alikuwa akiwasili eneo la tukio, bastola mbili zikiwa kiunoni,
akitembea kuelekea pale pale.
May be an image of 1 person

 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 012
Wakati masimba akishuka eneo la
Ngamia Pub, macho yake yalikuwa
yakiangaza huku na kule kuangalia
nani na nini walikuwa wakimtiza. Kila
aliemuona alikuwa kwenye mambo
yake, hakuna ambaye alikuwa
akimtizama. Hilo halikumfanya ajiamini
kabisa, bado akatembea akiangalia
huku na huko. Hata pale macho yake
yalipomuona mwanamke mrembo
alieketi pembeni, bado masimba
hakuvutika kumtizama. Macho yake
yalikuwa yakitizama upande mwingine
kabisa. Hakutazama huko kwa
makusudi, bali alikuwa akimtizama
mtu ambaye alikuwa akimfananisha.
Alifanana kabisa na mpenzi wake,
alifanana kabisa na teddy. Akahitaji
kufanya kitu ambacho
kingemuaminisha kwamba mtu yule
alikuwa mpenzi wake. Kengele ya
tahadhali ikagonga kichwani pale
alipowaona watu watatu wengine
wakimtizama. Tabasamu mubashara
likachomoka usoni kwake, halikuwa
tabasamu la kufurahi wala kuwavutia
wasichana waliojazana pembeni. Hili
lilikuwa tabasamu la kukubali kile
ambacho alikiwaza. Kile ambacho
alijua lazima kitendwe na yule
mwanamke. Alitambua baada ya
kuwasiliana na kumwambia sehemu
ambayo wangekutana, ni lazima naye
angeisambaza taarifa ile. Hilo aliliamini
na hapa alikuwa akilithibitisha. Vichwa
vitano vilivyokaa sehemu tofauti
vilikuwa vikimtizama yeye.
Vikimuangalia na hata kumshuti basi
wangefanya hivyo. Akaendelea
kusogea akimuangalia yule mtu
anayefanana na mpenzi wake. Ni kweli
alikuwa teddy, ni kweli alikuwa yeye!
Kwa nini yeye? Kwa nini hapa muda
huu? Yupo kwenye hili? Hilo
likamshangaza tena na tena. Lakini
kwakuwa alikuwa na watu wake eneo
lile, alijua kila kitu kingewekwa wazi,
ingawa hakupewa taarifa ya uwepo wa
Teddy, hilo halikumsumbua kwa kuwa
alimjua teddy. Aliutambua uwezo
wake wakijasusi, alitambua uwezo
wake wakujibadilisha. Hilo
halikumfanya Awalaumu vijana wake.
Akaifikia meza ambayo ilikaa
mwanamke yule. Hakusubiri
kukaribishwa, bali alivuta kiti na kukaa.
"Bila shaka sikatazwi kukaa hapa!"
Aliongea huku akimtupia mwanamke
yule jicho. Bado akakutana na jicho lile
lile la ulaghai, jicho ambalo bado
liliendelea kumdanganya Masimba.
Jicho la usingizi, jicho la kuvutia na
hata kubadilisha mtazamo wa watoto
wakiume.
Kabla hajajibu, akaliachia tabasamu,
tabasamu ambalo liliendelea kuufanya
uso wake ung'are na uzuri
kuongezeka.
"Sio hapa tu, hata nyumbani, tena
chumbani kabisa ungekaribishwa."
Akajibu mwanamke yule akiendelea
kutabasamu.
"Kumbe hata chumbani nakaribishwa,
kwanini tumekuja hapa? Akauliza
masimba huku macho yake
yakiendelea kutembea usoni kwa
mwanamke huyu. Kuna kitu alikuwa
akikitafuta, lakini usoni kwa
mwanamke huyu bado hapakuonekana
kile ambacho alikuwa akikitafuta. Sura
ya mwanamke huyu ilipambwa na
uzuri wa haja, uzuri wa kuvutia na
kuwavutia wengi.
"Nimekuita hapa ili tufahamiane, pia
kuna mawili matatu nahitaji tuongee!"
Baada ya maneno hayo, mwanamke
yule akaonekana kuwa tofauti, safari
hii hapakuwa na tabasamu wala
mbwembwe. Uso wake ulikuwa uso
wa kazi. Hilo likamfanya Masimba naye
abadilike. Lakini ubadilikaji wake
haukuwa ubadilikaji ule. Huu ulikuwa
ubadilikaji wa kuiteka akili ya
mwanamke yule. Wakatizamana kwa
muda kila mmoja akitafuta kilichopo
ndani ya mwenzake.
"Naitwa Mwamvita Rajabu, ni ndugu
wa binti alieuawa juzi usiku. Nimekuja
hapa jijini leo asubuhi kufuatilia kile
ambacho kimesababisha kifo cha
ndugu yangu." Aliongea mwanamke
yule huku akiendelea kuivaa sura ya
Huzuni. Licha ya sura hiyo lakini kwa
Masimba bado sura ile haikuwa katika
huzuni hiyo, bali ilikuwa katika huzuni
ya kulazimishwa.
'"Wewe ni Polisi, afisa usalama ama?
Na kwa nini umeniona mimi pekee
ndiye wakuongea nawe? Sasa aliuliza
masimba safari hii ikiwa makini
kumuangalia mwanamke yule usoni.
Bado sura yake iliendelea kuwa na
huzuni, lakini kitu kingine mwanamke
yule alikuwa kimya akionyesha
kupatwa na huzuni zaidi. Kwa jasusi
aina ya masimba hakuwa mgeni wa
mbinu zile, hakuwa mgeni kwa kuwa
alijua mwanamke yule hakuwa na jibu
kwa wakati ule. Ukimya wake
haukusababishwa na huzuni bali swali
aliloulizwa halikuwa na majibu. Safari
hii mwanamke yule akainua uso wake
na kumwangalia masimba. Hata macho
yao yalipokutana, safari hii Masimba
alikiona kile ambacho alikuwa
akikitafuta. Macho yao yalikuwa
yakielezana kwamba wote ni watu
katika fani moja. Wote walikuwa
majasusi wa kiwango cha hali ya juu.
"Nadhani umenitambua sasa, nadhani
ulichokuwa unakitafuta umekiona."
Akaongea mwanamke yule akiendelea
kumuangalia masimba.
Tabasamu likachanua usoni, tabasamu
ambalo lilifuatiwa na kicheko.
Hakikuwa kicheko cha furaha, hiki
kilikuwa kicheko cha ushindi. Ni rahisi
kumuua adui unayemjua kuliko
usiemjua. Kitendo cha mwanamke
huyu kuongea kile alichokuwa
anakitafuta kikampa kuamini kwamba
hata huyu ni mmoja wao.
"Yeah! Nimekiona na nimepata majibu.
Lakini bado hujaniambia wewe ni nani?
Na umeniita hapa kutaka nikujue ama
kuniambia ulichoniitia? Safari hii
masimba aliongea kwa ukali huku
macho yako ya kibadilika.
"Hupaswi kujua masimba, hupaswi
kunijua. Lakini nakuomba uachane na
hili ulilolianzisha. Hutafika popote
masimba." Safari hii aliongea
akichezesha midomo.
"Bahati mbaya aliekuelekeza kwangu
amekosea. Kamwambia mimi huwa
sitishwi na wala siogopagi. Sitaacha na
sitarajii kuacha, lakini nadhani leo kuna
kitu umesikia. Basi ile ni kazi yangu
mimi." Alijibu masimba kwa kejeli.
Alishajua adui zake washakuwa waoga,
wameshaanza kumhofia. MASIMBA
akasimama na kuanza kuondoka eneo
lile. Alimuacha mwanamke yule
akijisonya, akitamani kumlipua.. lakini
haikuwa amri kwa siku hiyo.
May be an image of 1 person

 
SEHEMU YA 013
Akamuangalia masimba alipokuwa
akiondoka katika eneo lile, akatamani
kuichomoa bastola yake ili
ikiwezekana airuhusu risasi, lakini
hakutaka kufanya hivyo kwa kuamini
kuwa masimba hawezi kuwa pale peke
yake. Akashuhudia akitembea na
kupotelea katika upeo wake.
Kuondoka kwa masimba kukampa
nguvu ya kuamini kuwa masimba
hakuwa mtu wa kutishwa. Aliamini hilo
baada ya maneno yake. Akatamani
kusimama kuwapa ishara watu wake
ambao walikuwa katika maeneo
tofauti. Lakini bado alisita akiamini
kuna macho yapo mahali yakimtizama
kwa kila alichokuwa akikitenda.
Akajipa uvumilivu huku akishusha
kinywaji kinywani. Masimba baada ya
kuachana na mwanamke yule
alitembea akitoka eneo la pub ile.
Macho yake bado yalikuwa yakiangaza
kuhakikisha kama kwelu mwanamke
aliyekaa pembeni kabisa mwa Pub ile
alikuwa Mpenzi wake. Lakini safari hii
macho yake hayakumuona Teddy,
hayakumuona mwanamke ambaye
alidhani ni Mpenzi wake, bali
yalimuona mtu mwingine, tena
mwanamke harafu alikuwa amevaa
mavazi kama yale yale aliokuwa
amevaa Teddy. Hilo likampa tafsiri
kwamba ulikuwa mchezo, ulikuwa
mchezo ambao ulichezwa kwa kipindi
kile. Ni kweli mwanzo alimuona Teddy,
nikweli alikuwa na uhakika huo, lakini
cha ajabu safari hii alikuwa akimuona
mwanamke mwingine, mwenye sura
nyingine, lakini alievaa mavazi
yanayofanana na yale aliovaa Mpenzi
wake. Lakini huyu hakuwa teddy!
Mshangao kilikuwa kitu cha kwanza
kutokea usoni kwake. Akaona ni wakati
wakuondoka hapo kwa kuwa alikuwa
akihitaji kwenda kuongea na Mama wa
Marehemu Asteria, sambamba na dada
yake. Akatoka akaelekea sehemu
ambayo aliipaki gari yake. Alitembea
macho yake yakiangalia kila kitu, hatua
kadhaa kabla ya kufika kwenye
maegesho ya magari akakiona kivuli,
kivuli kuonyesha uwepo wa mtu karibu
na alipoipaki gari yake. Kengele za
hatari zikagonga kichwani kwake,
hakujua kwa nini lakini alijikuta
akiushusha mkono wake pale
alipohifadhi bastola yake. Hakutaka
kukiamini kile alichokiona. Akaendelea
kutembea akikiangalia kile kivuli..
lakini kabla hajagundua chochote
akausikia mlipuko mkubwa, mlipuko
ambao ulisababisha hata yeye kutupwa
pembeni kabisa na kuanguka mfano
wa furushi. Gari yake na magari
mengine yalikuwa yakiwaka moto
kuonyesha kuwa alitegewa bomu
kwenye gari yake. Eneo lote la
mjimwema likawa katika taharuki,
watu walikuwa wakikimbia huku na
huko kila mmoja akipigania kuiokoa
nafsi yake. Sehemu yote ikageuka vilio,
iligeuka somalia kwa muda mfupi. Pale
alipoangukia masimba ndio kwanza
alikuwa akirudiwa na akili zake,
alikuwa akifumbua macho huku
akijaribu kuvuta kumbukumbu.
Kumbukumbu ambayo haikuwezekana
kurudi kutokana na mkanganyiko na
vilio vya watu. Akatambaa na tumbo
mpaka pembeni kidogo. Muda mfupi
alikuwa akisimama huku akishuhudia
gari yake ikiteketea, gari ambayo
alipewa kama zawadi na mwanamke
mmoja hivi baada ya kumfanyia kazi
yake ipaswavyo.
Bado hakuamini kama amesalimika...
akaituliza akili yake, alitaka kuirudisha
kumbukumbu kabla ya mlipuko ule.
Kivuli cha mtu kilikuwa kitu pekee
alichokiona. Kivuli ambacho
hakufanikiwa kumuona mhusika halisi
wa kivuli kile. Kwa mara ya kwanza
akashukuru. Ilikuwa ni lazima aondoke
pale, ilikuwa ni lazima apotee hapo,
akaipima nguvu katika mwili wake.
Alipoiona inatosha akaanza kupiga
hatua huku hisia kuwa teddy alikuwa
mmoja kati ya wapangaji washambulie
lile. Akatembea akijichanganya na
watu waliokuwa wakipita katika eneo
hilo wakikimbia. Naye alikuwa
akikimbia sambamba nao, ni wakati
akikimbia ndipo alipomuona tena
Teddy akitokea upande ule ambao
alikiona kivuli kabla ya mlipuko.. Hata
yeye alikuwa akikimbia, hata yeye
alionyesha kufadhaika, Alionyesha
kutafuta kitu, hakuwa teddy yule
kiburi, hakuwa teddy yule gaidi na
mwenye usiri. Huyu alikuwa teddy
aliechanganyikiwa. Hili likamvutia
Masimba kulitizima. Lakini wakati hilo
halijafika popote akaishuhudia gari
ikisimama pale alipokuwa amesimama
teddy. Gari iliposimama milango
ikafunguliwa, teddy akaingia kisha gari
kuwashwa. Kilikuwa kitendo
kilichofanyika kwa sekunde mbili,
kitendo ambacho kilimfanya masimba
aduwae. Kitendo ambacho kilimpa
picha na kumuaminisha kuwa teddy
hakuwa Teddy yule walioanzana akiwa
ndio kwanya yupo kwenye mafunzo ya
awali ya kijeshi. Hakuwa Teddy Yule
wa Ifakara, hakuwa Teddy yule
mwenye kutangaza mapenzi ya kweli.
Huyu sio teddy yule anayetoka Idara ya
usalama wa Taifa, hakuwa teddy yule
alietoka urusi katika mafunzo ya juu ya
Ujasusi. Huyu alikuwa Teddy Muuaji,
teddy msaliti. "NITAKUPATA TU" Ndio
kauli pekee aliotamka wakati gari ile
ikimpita kwa mwendo wa kasi.
*********
Palikuwa na ukimya wa ajabu, ukimya
ambao kwa mbali ulikuwa
ukiondolewa na mbwa waliokuwa
wakibweka. Alikuwa hapo kwa minajili
ya kuongea na dada wa marehemu
Asteria. Alitembea kama kama kawaida
akielekea mlangoni mwa nyumba ile.
Muda wote macho yake yaliozoea giza
yalikuwa yakiangaza huku na huko.
Akaufikia mlango, akasimama kwa
muda kisha akaanza kuangalia eneo
lote, alipoona hakuna mtu wa kumtilia
mashaka, akaugonda mlango kwa
mara ya kwanza, hakujibiwa, kwa mara
ya pili hapakuwa na majibu tena..
alipogonga kwa mara ya tatu, akasikia
nyayo za mtu zikisogea pale mlangoni,
wakati akiusubiri mlango ufunguliwe
akashangaa kumuona mtoto mdogo
akilia kwa ndani. Hilo hakulitarajia,
mkono wake ukashuka na kuichomoa
bastola.. kabla hajaingia mlango
ukafunguliwa kisha sura ya mtoto
mdogo wa miaka kumi alietapakaa
damu mwili mzima akatokea. Masimba
hakutaka kuuliza, akamuweka mtoto
pembeni kisha kuingia ndani, sebuleni
akapokelewa na damu iliosambaa kila
sehemu, huku miili ya watu wawili
ikiwa imelala ikionyesha haina uhai.
Masimba akaisogelea miili iliokuwa
imelala katikati ya damu. Godfrey
Maboba akiwa na mkewe Irene Charles
walikuwa wamelala katikati ya dimbwi
la damu wakiwa maiti. Walikuwa
wamepigwa risasi vifuani mwao.
Masimba akainama kwa uangalifu,
akawaangalia marehemu. Bado
walikuwa wa moto kuonyesha
hawakuawa muda mfupi uliopita.
Wakati ameinama hapi akakisikia kitu
mfano wa chafya, kitu ambacho
kilitokea dirishani. Aliujua mlio ule,
aliujua haukuwa mlio mwingine bali
wa bastola. Masimba akawahi kuchupa
huku akisahau uwepo wa mtoto wa
marehemu. Wakati anatua nyuma ya
kiti pale sebuleni, akajikuta akitua
sambamba na mwili wa Mtoto Yule
ukiwa hauna Uhai....
MASIMBA AKAISHIWA NGUVU
No photo description available.

 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 014
Alikuwa akiitizama maiti ya mtoto yule.
Mwili wake ulikuwa na matundu
mawili ya risasi maeneo ya kifuani.
Alikuwa amelala huku damu zikishuka
taratibu ba kuanza kuilowesha sakafu.
Masimba akaduwaa kwa muda wa
sekunde tano akishindwa kuamini kile
anakitizama. Mtoto asiye na hatia
alikuwa ameuawa kifo kibaya, kifo
ambacho hakupaswa kuuawa hivyo.
Hakuwahi kulia na hakuwa mtu wa
kulia katika maisha yake, lakini mwili
wa mtoto huyu ulimliza na
kumuumiza. Macho yake yalikuwa
yamemtazama yeye kana kwamba
yalikuwa yakimuuliza. Yakimuuliza ni
lipi kosa lake ambalo amelitenda
mpakq kuuawa, alikuwa akimuukiza
kwa nini alimuachia mpaka risasi zile
zikapenya? Masimba chozi
likadondoka, kiganja cha mkono
kikayafunika macho ya mtoto yule.
Ndio kwanza akakumbuka kuwa
alikuwa mbele ya maiti watatu, mbele
ya maiti ya Godfrey Maboba mkewe
pamoja na mtoto wao. Mikoni ikawa
inamtetemeka huku hasira juu ya watu
wale zikipanda. Ni wakati akiendelea
kuangalia hapo akashuhudia mlango
ukipigwa teke kisha watu zaidi ya kumi
wenye silaha nzito wakaingia.
Walikuwa ni askari wa kikosi maalum
(special forces) askari ambao walikuwa
na mafunzo ya kupambana na watu wa
aina yoyote. Bunduki zao zilikuwa
mbele zikimtizama Masimba.
Hawakuonekana kuwa na utani,
hawakuonekana kuwa ni wenye
masihara. Walionekana walikuwa
tayari kufanya chochote. Amri
ikatolewa ya kumtaka masimba kutupa
silaha yake chini. Hilo masimba akalitii,
alilitii huku akili yake akifanyakazi ya
zaida. Alijua kikosi hiki kimekuja hapa
kwa sababu ya kumuangamiza.
Ulikuwa ni mpango ambao
umepangwa makusudi kwa sababu ya
kumkwamisha. Mpango ambao
ulitengenezwa mahususi na mtu mzito
katika serikali. Special forces hawawezi
kuja sehemu kirahisi, special forces
hawawezi kutumwa kwenda
kumkamata mtu mmoja. Hata kama
mtu mwenyewe ni yeye, special forces
hutumika katika sehemu ngumu
ambazo sio za kawaida. Sasa nani
ambaye ametoa orders ya wao kuja
hapa katika jumba hili? Kengele ya
hatari ikalia kichwani mwake,
alitambua kuwa lazima ameuziwa kesi
ya mauaji. Akaitupa bastola yake chini.
Kiongozi wa kikosi kile ambaye
alikuwa na cheo cha Luteni Kanali
akasogea pale aliposimama masimba.
Bado bunduki zilimtizama yeye, bado
bunduki zilikuwa zikicheza na mikono
yake na hata uelekeo wa macho yake.
Kiongozi wa kikosi kile maalum
akasogea. Akasogea tena na tena, sasa
alikuwa akitizama uso kwa macho na
masimba. Punde mkono wa kiongozi
yule ukazama mfukoni na kuibuka na
pingu. "Wanataka wanifunge pingu?
Lilikuwa swali la kwanza kujiuliza.
Lakini kabla hajakaa sawa akakisikia
kitu kizito kikitua kisogoni. Akaliona
giza likiingia machoni mwake, akataka
kujizuia asianguke, lakini haikuwa
hivyo, muda mfupi alikuwa yupo chini.
Hakujua tena kilichoendelea.
*******
Alihisi maumivu makali kichwani hasa
upande wa kisogoni. Maumivu makali
sana ambayo yalikifanya kichwa chake
kionekane kizito. Akataka kuuasogeza
mkono wake aguse sehemu ile, lakini
alijikuta akishindwa, hakushindwa kwa
kuwa mikono haikuwa na nguvu, bali
alishindwa kwa kuwa mikono yake
ilikuwa imefungwa pingu. Hilo
likamfanya atulie kwanza kuiruhusu
akili yake ifanye kazi. Akavuta
kumbukumbu ya nini ambacho
kimetokea kabla ya kufikishwa pale.
Akajaribu kwa muda lakini hakuweza
kwa wakati ule. Hakutaka kushindwa
katika hilo, akaendelea kukumbuka,
punde taswira ya picha ya mtoto
mwenye matundu mawili ya risasi
ukiwa umelala sakafuni, ikamjia usoni.
Taswira ambayo ilimkumbusha mengi
sana. Kifo cha Asteria, kifo cha
mwamvua, kifo cha dada wa asteria,
mumewe pamoja na mwanawe. Maiti
za watu wote watano zilikuwa zikipita
kichwani mwake. "TEDDY nitakupata
tu. Risasi yangu kutoka kwenye bastola
yangu lazima ikifumue kichwa chako.
Aliwaza huku sauti ya marehemu
Asteria Ikiendelea kujirudia. Hapo
akakumbuka pale alipowaona Askari
wa kikosi maalum wakiingia.
Akakumbuka wakati akitizamana na
yule Luteni Kanali. Kufikia hapi
akakumbuka kila kitu. Akatambua kwa
nini yuko pale. Kwa mara ya kwanza
akafumbua macho, cha kwanza
kukiona baada ya kufumbua ni uzuri
wa chumba alichomo. Kilikuwa
chumba kizuri sana, chumba chenye
upana wa kutosha. Kilikuwa na dirisha
kubwa la kioo, dirisha ambalo halikuwa
linaonyesha nje. Akageuza shingo
akiendelea kukichunguza chumba kile.
Macho yake yakanasa kitu mfano wa
flash kikiwa kimewekwa juu ya Dirisha.
Hakikuwa kitu kigeni kwa mpelelezi
kama yeye. Alitambua kuwa zilikuwa
camera ambayo ilikuwa ikichukua
picha kutoka mle chumbani na kurusha
sehemu fulani katika jengo lile. Bado
akaendelea kuangalia tena na tena
kujua jengo aliyomo liko sehemu gani.
Haikuchukua muda kugundua kuwa
alikuwa katika chumba cha siri ndani
Ya Makao Makuu Ya idara ya usalama
wa taifa yaliyopo Kijitonyama. Kwa nini
ameletwa hapa? Ina maana hata hawa
wenzake wanaamini kwamba
amefanya mauaji? Hilo
likamchanganya, hilo likamfanya
atamani kuonana na kiongozi wake.
Lakini hata kama angeonana naye
angemwambia nini wakati kazi hii
alikuwa akiifanya kwa siri bila
kuihusisha Idara? Hapo akauona
ugumu, hapo akaiona hatari ya
kushtakiwa na kupewa kesi ya mauaji.
Akatulia akifikiria nini akifanye.
Dakika kumi baadae akauona mlango
ukifunguliwa, kisha watu watatu
wakaingia. Hawakuwa wageni kwake.
Bali uingiaji wa watu hawa ulizidi
kumtia hofu na kumtisha zaidi.
Sekunde mbili alikuwa akiangalia na
Mkurugenzi Wa idara ya usalama wa
Taifa Kanali Godliving Kimaro pamoja
na maafisa wawili wa ngazi za juu wa
Polisi.
"Masimba Muuaji umezinduka?
Lilikuwa swali kutoka kwa mzee yule
ambaye hakuonyesha kutokuwa na
utani. Masimba bado alikuwa ametulia,
bado alikuwa akihisi yupo katika ndoto.
Alishakuwa masimba muuaji,
alishakuwa msaliti. Kama bosi wake
mkuu naye anaamini ni Muuaji, nani
ambaye atamuamini? Wakati akiwaza
hilo sauti ya mkurugenzi Ikamzindua
kutoka huko.
"Licha ya taifa kupoteza pesa nyingi
kukusomesha katika mataifa
mbalimbali, lakini leo umeamua
kuisaliti nchi yako, umeamua kuisaliti
nchi kwa sababu ya kuwatetea wauza
madawa ya kulevya. Unaua watu kwa
sababu ya kuahidiwa fedha? Umeitia
aibu System nzima, umeitia aibu Idara
hii. Mtu ambaye unategemewa kama
wewe leo unafanya huu upuzi?
Kuanzia leo idara inakufukuza kazi na
utakabiliwa na kesu ya mauaji na pia
utaishi katika kizuizi mpaka ukweli wa
hili utakapo kuwa mwingine."
Yalikuwa maneno ambayo yaliusisimua
mwili wa masimba, sio mwili tu bali
hata moyo na roho yake. Alitambua
jimmy Lambert na washirika wake
walikuwa wamemuwahi. Walikuwa
wamemuwahi na kummaliza kabisa.
Macho yake ya kazi yakamtizama mzee
kimaro usoni. Sasa walikuwa
wakiangaliana kwa muda. Macho yao
pekee ndio yalikuwa yakiongea.
Masimba akamlazimisha mzee
aendelee kumtizama. Wakatizamana
tena na tena. Kisha Bila kuongea kitu
mzee kimaro akabonyeza kitufe fulani
mle ndani, sehemu nne zikafunguka
kisha wakaonekana watu wanne
wakiingia.
No photo description available.

 
Duh! Watu huw mnapata wapi muda wa kuandika haya yote🤔,??

Mtoa mada zingatia matumizi ya Aya katika uandishi wako.
Hongera lakini.
 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 015
Walikuwa watu watatu, watu ambao
hawakuonekana kuwa na masihara
yoyote. Bado masimba hakuwa
akiamini. Akili yake haikuwa
ikikubaliana na kile kinachoendelea
pale. Hakuamini kama idara
aliyoifanyia kazi inaweza kuja
kudanganyika kwa urahisi kiasi kile.
Walikuwa wakimjua vizuri katika
majukumu mazito yote aliyowahi
kushiriki, alinusurika mara tatu katika
matukio ya hatari. Lakini leo hii
alikuwa amewekwa kizuizini. Tena
akipewa kesi ya kuhusika na mauaji ya
Godfrey Maboba na familia yake. Idara
kubwa yenye wajuzi wa hali ya juu
katika masuala ya ujasusi leo ilikuwa
ikidanganywa na watu. Watu ambao
wanaiharibu jamii ya Tanzania kwa
kuuza madawa ya kulevya. Yalikuwa
mawazo na fikra zilizozidi kuipandisha
hasira. Akaziangalia pingu ambazo
ziliifunga mikono yake. Alizitazama
kwa muda bila kuongea kitu. Kwa mara
nyingine akainua kichwa chake na
kumuangalia Mkurugenzi Mr Godliving
Kimaro. Aliyagandisha macho yake
usoni na kutaka kuongea kitu. Lakini
machozi yake yakashuka mashavuni
pasipo kutarajia.. hilo halikutarajiwa na
wote waliokuwepo pale, kwa mara ya
kwanza toka amjue Masimba ndio
alikuwa akilishuhudia chozi lake. Ndio
alikuwa akimuona Masimba akilia.
Bado macho yake yalikuwa usoni kwa
Chief. Lakini haukupita muda mrefu
watu wale wakamuinua juu na kuanza
kumkokota kutoka ndani ya chumba
kile. Bado macho yake yalikuwa kwa
Chief, aliendelea kumuangalia mpaka
alipotelewa kabisa ndani ya Chumba
kile. Safari yao ikaishia kwenye gari
moja ambayo ilikuwa imepaki nje.
Kufika pale mlango ukafunguliwa kisha
ishara ya kimtaka aingie ikifuatia.
Bastola zilikuwa zikimtizama huku
wanaume waliovalia suti nyeupe
wakiwa makini naye. Hakubisha na
hakutaka kufanya rabsha yoyote. Akatii
na kuingia ndani ya gari. Aliwekwa
katikati huku bado midomo ya bastola
ilimtizama. Watu waliomuweka
hawakujishughulisha naye, hawakuwa
wakiongea chochote. Walikuwa watu
wa kazi, watu ambao kukuondoa kwao
ni suala la kawaida. Hawakuwa wao tu,
ndani kulikuwa na watu wengine
wanne ambao nao walikuwa ni mfano
wa hawa watatu. Hapo bado akauona
ugumu wa kulianzisha. Hakutaka
kufanya mapema kiasi kwa kuogopa
kuharibu mipango yake. Akaendelea
kutulia, punde akamuona mmoja
akiishika mikono yake, ufunguo
ukapita, punde pingu zikajiachia.
"Usione tunakufungua ukajaribu kuleta
ujanja. Ukifanya hivyo risasi itakuwa
halali kichwani kwako." Alinguruma
mmoja kati ya watu wale. Masimba
hakuwa amemsikia, mawazo yake
hayakuwa pale, alikuwa akimuwaza
Teddy, alikuwa akimuwaza mwanamke
huyu, mwanamke ambaye alitokea
kuchukua sehemu kubwa katika
maisha yake. Alimpenda Teddy,
alimuamuni na kumheshimu. Hakuwahi
kuwaza kama itakuwepo siku teddy
angekuwa mnyama. Hakuwahi kuwaza
kama angeweza kuja kumgeuka.
Hakuwa na mashaka juu ya kukamatwa
kwake, alitambua kinachofanywa ni
kushurutishwa ili ataje wapi
alipoyapeleka madawa ambayo
ameyachukua kwa Jimmy. Bado
aliendelea kukaa kimya huku gari
ikiendelea kutembea. Alikuwa tayari
kumuua mtu yoyote. Bado sauti ya
Asteria ilikuwa ikijirudia kichwani
mwake. Asteria binti mzuri, binti
ambaye amekufa akiuomba msaada
kutoka kwake, hata pale
alipoukimbuka mwili wa mtoto yule
alihisi kuwa na deni kubwa. Alitaka
kumtafuta mwamvita, alitamani
kuonana naye kwa vyovyote. Lakini
kwa muda ule haikuwezekana tena.
Lakini alitamani na aliipenda staili ya
mwanamke yule. Punde akasikia kitu
kama mfano wa geti likifunguliwa.
Sekunde kumi baadae gari ilikuwa
ikisimama. Milango ikafunguliwa kisha
Masimba akatakiwa ashuke. Akatii
huku midomo ya bastola na mitutu
kutoka kwa walinzi wa Jumba lile
ikimsindikiza.
***********
Alikuwa amelala kitandani akiitizama
picha ambayo walipiga na masimba
mwanzoni mwa mahusiano yao.
Ilikuwa picha ambayo ilimkumbushe
mengi sana katika maisha yake.
Ilikuwa siku ya kwanza kukutana kwao,
ilikuwa siku ambayo Teddy alikuwa
amepata pass maalum. Akaitizama
picha ile kwa muda mrefu sana.
Alikuwa akiuvuta muda kumsubiri
masimba. Bado moyo wake ulikuwa
ukipambana na mapenzi, bado moyo
wake haukutaka umuache masimba. Ni
kweli aliitaka pesa, ni kweli aliipenda
pesa, lakini pesa hii haiwezi
kusababisha akamuacha masimba.
Akaiweka ile picha pembeni na
kuchukua nyingine. Hii ni picha
ambayo ndio ilikuwa na kumbukumbu
mbaya na nzuri kwake. Ilikuwa picha
iliopigwa nchini Urusi wakiwa
sambamba na wapelelezi wa shirika la
kijasusu la Nchi hiyo, FSB zamani
likijulikana kama KGB. ni picha ambayo
walikuwa katika oparesheni moja
katika mji moja katika nchi ya Syria. Ni
misheni hiyo ambayo kama sio umakini
na uwezo wa masimba basi angerudi
jina. Lilikuwa tukio baya kukumbukwa
lakini ni Masimba huyu huyu aliejitolea
kuhatarisha maisha yake sababu yake.
Kumbukumbu ya tukio nzima ilikuwa
ikijirudia. Ni wakati akiliwaza hilo ndio
mawazo yake yalipopitea baada ya
kuusikia mchakato wa viatu vya mtu.
Akajiinua kitandani mkononi akiwa
ameikamita bastola yake. Akatembea
akihisi labda alikuwa masimba, lakini
utofauti wa siku ile ndio ulimpa
wasiwasi wa kuhisi labda mtu huyu
hakuwa masimba. Siku zote alitambua
masimba hakuwa akiingia kwa kupitia
mlangoni. Akaendelea kutembea
akielekea kwa nje. Hakupitia mlango
wa kawaida bali aliamua kutumia
mlango wa siri ambao huwa unatokea
moja kwa moja mpaka nje. Macho yake
yalikuwa yakipita na kuingia hapa na
kutokea pale. Muda wote masikio yake
yalikuwa yamesimama mithiri ya
sungura akitaka kunasa hiki na kile.
Dakika mbili alikuwa nje ya nyumba
yao akiangaza huku na huko. Palikuwa
na giza sambamba na miti ambayo
iliizunguka nyumba yote na
kutengeneza kivuli. Akatulia kwanza
akiangaza macho yake huku na kule.
Punde akamuona mtu akichupa kutoka
kwenye mmoja kati ya miti ile na
kutumbukia kwa ndani. Mwili
ukamsisimka. Japokuwa palikuwa na
giza lakini mtu yule hakuwa Masimba
kutokana na umbo lake. Akaipa muda
akili yake kuwaza na kulitafuta jibu.
Alikuwa nani katika nyumba yao na
alikuwa akitaka nini? Hakuweza kupata
jibu kwa wakati ule, lakini kwa mbali
alianza kuhisi kuwa wenzake walikuwa
wakimgeuka. Ingawa hayakuwa
mawazo ya asilimia mia, lakini hakuna
mtu mwingine ambaye angeweza
kufika pale. Akaendelea kutulia
akitizama zaidi na zaidi, kwa mara
nyingine akamuona mtu wa pili naye
akichupa na kutua ndani. Huyu wa pili
alimsisimua zaidi kutokana na
muonekano wake. Alikuwa ni
mwanamke, tena mwanamke mwenye
ujuzi.
Teddy hakutaka kusubiri, sekunde ile
ile akarudi ndani kwa kupitia mlango
ule ule wa siri. Muda wote alikuwa
akijiuliza juu ya watu hawa. Akatokea
kwa ndani kisha kutulia.. aliangaza
macho kwa muda punde akakiona
kama kivuli kimepita hatua hamsini
kutoka pale alipotulia, sekunde ile ile
akakiona kivuli cha pili pili kikipita.
Muda ule ule akawaona watu
walewale wawili wakichupa kutoka nje
ya nyumba yao. Teddy akaduwaa.
Kuduwaa kwake sio kuduwaa bure
lakini alitambua watu hawa walitumwa
na Jimmy kumchunguza yeye ama
wametumwa na Idara ya Usalama wa
Taifa kunfuatilia. Wazo la idara ya
usalama hakuwa na mashaka nalo,
lakini kuhusu Jimmy alikuwa na
Uhakika nalo kwa kuwa ni siku hii
mchana ambayo walimtishia kwa
bastola, na sasa walituma watu ambao
hakujua ni kina nani na wamekuja pale
kwa sababu gani.
No photo description available.

 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 016
Hisia za kwamba watu wale
walitumwa na idara ya usalama wa
taifa zilikuwa ndogo sana ukilinganisha
na hisia kuhusu Jimmy. Ulikuwa
mchana tu walipomtisha kwa bastola,
lakini muda huu alikuwa
akiwashuhudia watu wakiuruka uzio
wa nyumba yao, watu ambao
waliuonyesha kile ambacho
kilimthibitishia kuwa watu
waliomtembelea walikuwa na uwezo
mkubwa sana, kutokana na namna ya
utokaji wao. Hilo likampa wasiwasi,
wasiwasi ambao hakuwa nao hapo
mwanzo. Kwa nini watu hawa
wamekuja hapa? Wametumwa na nani
na kwa sababu ipi? Hilo likampa
utimamu wa akili, utimamu wa
kutokurupuka. Alitaka kuujua ukweli
kuhusu watu hawa ambao bado
walikiumiza kichwa chake. Kwa mara
ya kwanza aliutamani uwepo wa
Masimba. Kwa mara ya kwanza
alimkumbuka masimba, hakuogopa
kuhusu kujua kwake, muda ule
alimhitaji kama msaada na mtu wa
pekee katika hili. Lakini masimba
hakuwepo na hakujua wapi alipo
mpaka muda huo. Hata hilo
lilimchanganya pia, kwa nini mpaka
muda ule masimba hajarudi? Ama
amekufa katika tukio la kulipuliwa kwa
gari yao? Hilo likamfanya teddy aamue
kurudi sehemu ya tukio. Alitaka
kumsaka masimba ajue wapi alipo. Hilo
likamrudisha mpaka ndani, macho yake
yakiangaza huku na kuangalia kule,
alitaka kujua kama watu wale
wamefanya chochote. Ni kweli alikiona
kile ambacho alikiwaza. Watu wale
walikuwa wamepekua sebuleni mpaka
chumbani kwa utaalam wa hali ya juu,
kitu ambacho kwa macho ya mtu wa
kawaida hawezi kugundua. Aliangalia
kwa muda na kuchunguza kila kitu
chake. Alipogundua kipo salama,
alibadili mavazi yake, akachukua
bastola zake mbili na kuzichomeka
sehemu tofauti ndani ya mavazi yake.
Akaurudisha mlango, safari ya kuelekea
Mjimwema ikaanza. Alikuwa
ameshakijenga kisasi na chuki juu ya
Jimmy na washirika wake. Alijiapiza
endapo kweli Jimmy yupo nyuma ya
matukio haya, basi atahakikisha
anampoteza.
******
Alishuka sehemu ya tukio na
kupokelewa na askari waliovaa
magwanda sambamba na utepe wa
kuonyesha kwamba sehemu haikuwa
salama. Akatembea mpaka pale
akisalimiana na baadhi ya askari, lakini
alipotaka kuingia ndani ya eneo
lililozungushiwa utepe akazuiwa na
makachero wa polisi waliovalia mavazi
ya kiraia. Teddy hakuongea wala
kujitambulisha kwa chochote, bali
alimuangalia kachero yule kama
sekunde mbili, kachero yule
hakumuangalia tena teddy. Alitoa
ruhusa kwa teddy kupita. Alipoingia
akajikuta akitizamana na miili ya watu
watatu ambayo ililazwa chini
kuonyesha kuwa haikuwa na uhai.
Akatembea akiiona hofu moyoni
mwake, hofu kuwa masimba alikuwa
ameuawa, hofu ya kumpoteza mpenzi
wake na hofu ya kutishwa na watu.
Ingawa hakuwahi kuogopa, lakini hili
lilimtia hofu. Mikono yake iliokuwa
akitetemeka sasa taratibu ilikuwa
ikishuka tayari kwa kufunua shuka.
Hatimaye akaikamata kisha kuifunua,
moyo wake ukachanua kwa tabasamu,
tabasamu mwanana baada ya
kugundua kati ya miili ile mitatu,
hapakuwa na mwili wa masimba.
Akairudisha shuka, akainuka akitoka
nje ya utepe wa polisi. Macho kadhaa
yalikuwa yakimtizama katika aina ya
maswali. Hilo halikumfanya aogope,
bado alitembea macho yake
yakitizama kila sura za makachero
waliokuwwpo pale kwa chati. Alitaka
kujua nani ambaye alikuwa akimtizama
kwa hila. Tokea alipowaona watu wale
kule nyumbani kwake, hakutaka
kuamini kama hakuwa akitembea na
macho ya watu ama kutembea
sambamba na watu. Aliamini kuwa
kama watu wamediriki kuingia ndani
ya nyumba yake, kisha kuifanyia
upekuzi katika muda usiozidi dakika
moja, hakuamini kama wanaweza
kumuacha atembee peke yake. Lazima
watakuwepo watu ama mtu ambaye
anaifanya shighuli ya kumfuatilia.
Lakini macho yote aliotizamana nayo
bado hayakuonyesha hila. Yalikuwa
macho ya kawaida japokuwa palikuwa
na giza.
********
Jumba lilikuwa na walinzi wenye silaha
nzito, wote walikuwa katika suti nyeusi
kuonyesha kuwa walikuwa watamu
katika medani ya kimapigano. Wote
walikuwa wameizunguka gari huku
midomo ya silaha zao zikielekezwa
ilipo simama ile gari. Hata mlango
ulipofunguliwa watu wale hakuongea
chochote zaidi ya kumpa ishara
masimba ashuke. Masimba akatii huku
bado midomo ya bastola sambamba na
bunduki za walinzi zikimtizama.
Alitembea akiwa amewekwa kati. Kila
hatua yake na uchezaji wa mikono
yake, ulikuwa ukiangaliwa kwa
ukaribu. Kila mguu wake ulipokuwa
ukipiga hatua na kutua chini, macho ya
Walinzi wale nayo yalikwenda
sambamba. Wakaufikia mlango mmoja
mkubwa wa vioo. Kufika hapo tu
mlango ukajifungua na wote wakaingia
ndani wakiwaacha walinzi nje. Kutoka
hapo wakaongoza mpaka ndani ya lifti
ambayo iliwapaleka mpaka ghorofa ya
saba. Wakashuka na kupokewa na
watu wengine, hawa ndio
waliomchukua masimba huku wale
waliokuja naye wakirudi na ile lifti.
Bado akili ya masimba ilikuwa haipo
katika utimamu wake. Alitambua
sehemu alipo, aliitambua kwa kuwa
hata yeye alikuwa jasusi. Lakini kitendo
cha kuletwa ndani ya jengo hilo
akichanganya na maneno ya Chief,
alitambua kuwa lazima kuna jambo
kubwa nyuma ya pazia. Akajiambia
asubiri, alikuwa akiamini subira tu ndio
ingeweza kumfanya ajue kile
kinachoendelea. Watu hawa
waliomuongoza kwa mara ya pili,
walikuwa zaidi ya watu, hawa
hawakuwa hata na tabasamu. Kila
mmoja alikuwa akiatizama kila
kinachotokea. Macho yao yalikuwa
yakizunguka kama kinyongo.
Yalimtizama na kumchunguza,
yalimuangalia kwa kina. Hata pale
macho yao yalipokuwa yakitizamana,
kila mmoja alimtambua mwenzake.
Wakaufikia mlango mwingine, mlango
huu haukufanana na kote walikopita,
mlango huu haukuonekana kama
ulikuwa mlango, lakini kule kukanyaga
sehemu ya nje kuukaribia,
kukaonekana kitu mfano wa shimo.
Masimba akasita kuingia, akataka
Kurudu nyuma. Hakufanikiwa hilo, kitu
kizito kikatua tena kichwani. Akakiona
kiza mbele yake. Akajaribu kupambana
na giza lile, lakini akashindwa.
Akaruhusu Macho Yake Kuingia giza. NI
KWELI YAKAINGIA GIZA. HAKUJUA
KILICHOENDELEA.
No photo description available.

 
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 017
Alipambana akikataa giza kuuchukua
mwanga wa mboni za macho yake,
lakini haikusaidia kitu. Akakubali giza
liyafunike macho yake. Na kweli
ndivyo ilivyokuwa.
Alikuja kushtuka baada ya masaa
mawili na kujikuta katika chumba
kidogo. Chumba ambacho hakikuwa na
kitanda isipokuwa maji tu. Tena maji ya
baridi kupindukia. Mwanzo wakati
anapatwa na fahamu alidhani labda
alikuwa pembezoni mwa bahari ya
hindi kutokana na maji yale.
Akafumbua macho zaidi na zaidi,
akayaona mazingira yale. Akahisi
kukata tamaaa. Aliyajua matumizi ya
chumba kile. Hakuna mtu ambaye
aliwahi kutoka akiwa hai kati ya wote
walioingizwa. Akainua kichwa chake na
kuangalia juu, akakumbuka mengi
aliowahi kulifanyia taifa lake,
akakumbuka aliponusurika vifo mara
kadhaa kwa sababu ya usalama wa
taifa lake. Lakini yote yamesahaurika,
lakini yote yalisahaulika kwa sababu ya
watu wachache. Hata yeye alipelekwa
ndani ya chumba kile ambacho
hutambulika kama kuzimu. Alitakiwa
naye afe, alitakiwa naye asirudi akiwa
hai. Bado maji yaliendelea kumtesa na
kumsulubu. Akainua macho na
kutizama mwisho kabisa wa chumba
kile. Aliamua kujaribu bahati yake,
hakutaka kamwe kufa kikondoo,
hakuamini kama angeshindwa kutoka
pale. Aliamini atatoka tena atatoka
akiwa salama. Akauvaa ujasiri na
kuutoa uoga na ukataji tamaaa.
Akainuka kutoka pale chini, akasimama
kwa muda akiendelea kutupa macho
yake kila pembe ya chumba kile.
Akaunyoosha mwili wake kuupima
kama una nguvu, aliporidhika akaanza
sasa kutembea ndani ya kichumba kile.
Kwa kuwa maji yalikuwa yamejaa
mpaka kiunoni, hakuwa akiona chini
alipokuwa akitembea. Alipokuwa
akipiga hatua nyingine akajikuta
akijikwaa kwenye kitu mfano wa mwili
wa binadamu. Hilo likamfanya asite
kuendelea kutembea, alikuwa
amesimama akijishauri kitu.
Alishaamua kufanya chochote, akili
yake ikahitaji kufanyakazi mara mia
zaidi ya kawaida yake. Hakutaka
kushughulika na kitu mfano wa mwili
wa binadamu aliyoukwaa. Alihitaji
kufanya kitu kikubwa cha kumuondoa
pale ndani. Akajaribu tena kutembea
lakini safari bado alikikanyaga kile kitu
mfano wa mwili wa binadamu. Kitu
kama hisia kikamjia kichwani, hisia ya
kwamba mtu huyu anaweza
kumsaidia. Kwa kuwa siku zote
aliziheshimu hisia zake, Masimba
akainama na kuanza kutafuta chini ya
maji. Kweli mikono yake ikagusa mwili
wa binadamu. Baada ya kuugusa,
akahakikisha mikono yake inaukamata
ule mwili na kuanza kuusimamisha.
Alipambana kwa muda na
alipofanikiwa kuusimamisha
akashangaa kumuona mtu anayemjua.
Mwili wa mtu yule ulikuwa ni wa
mmoja kati ya vijana ambao walikuwa
wakimsaidia katika kazi yake.
Hilo hakulitegemea, kengele za hatari
zikakigonga kichwa chake. Mmoja kati
ya vijana waliokuwa wakimsaidia kazi
kuuawa, alijua ilikuwa ni mbinu ya
watu waliomfikisha pale. Alitambua
vijana wote aliokuwa anasaidiana nao
watauawa iwapo kama yeye
ataendelea kuwepo pale mahabusu ya
kuZimu. Akaendelea kuutizama wili wa
kijana yule, hasira zikaonekana usoni.
Kuuawa kwa maafisa usalama wa taifa
kwa sababu ya manufaa ya watu
wachache kulimpa sana hasira.
Aliitambua hizi zilikuwa hila za Jimmy
Lambert na maafisa waandamizi wa
serikali. Alijua wote hawa walikuwa
wakishinikizwa kusema wapi ulipo
mzigo wa madawa ya kulevya
aliouchukua nyumbani kwa Jimmy. Hilo
likamfanya aihisi hatari hata kwa
teddy, alihisi hata yeye ipo hatari
atageukwa na kitakachofuatia ni yeye
kupotezwa kama walivyofanya kwake.
Kwa mara ya kwanza alitamani
amuone teddy amwambie, kwa mara
ya kwanza alitaka kumwambia teddy
hatari iliombele yake. Alitaka
kumwambia ukweli wa mambo. Lakini
angetokaje wakati yupo kuzimu,
alitokaje wakati muda mfupi ujao
atakuwa maiti. Masimba akasonya
huku akikifanya kitu ambacho hakuwa
amekiwaza. Mikono yake ilizama
kwenye mavazi ya marehemu yule.
Akahisi kukigusa kitu katika mavazi ya
marehemu yule. Akaongeza kasi ya
mikono punde akakitoa kitu kile
ambacho kilikuwa mfano wa golori.
Tabasamu likachanua usoni mwake.
Kilikuwa kitu maalum cha kufungulia
sehemu zisizowezekana. Kitu ambacho
hutumiwa sana na mashirika makubwa
ya Kijasusi Hasa CIA na M15 pamoja na
M16 ya Uingereza. Akakitizama kwa
muda, harafu akakiwasha na kuanza
kukizungusha kwa mikono yake
akikielekeza kila upande. Sekunde
kumi hazi kufika, maji yote yakapotea
kisha chini kwa pembeni pakaachia.
Mlango mkubwa ukaonekana mbele
yake. Hakutaka kusubiri kwa kuwa
alitambua huwa kuna muda maalumu.
Sekunde ya kumi na mbili alikuwa nje
ya chumba kile akitembea kuifuata
korido ambayo ilikuwa akielekea kama
Chini ya ardhi. Hakuwa na bastola,
hakuwa na silaha ya aina yoyote, lakini
alikuwa tayari kwa lolote. Jengo
lillikuwa kimya kanakwamba
hapakuwa na mtu ndani yake. Macho
yalikuwa yakiangalia kila kona ya
Jengo. Muda mfupi alikuwa ameibukia
sehemu ambayo haikuwa kimya. Sauti
za watu zilikuwa zikisikika kwa umbali
mfupi kutoka mahala aliposimama.
Wakati akifikiria nini afanye akavisikia
vishindo vya mtu akisogea mahala
pale. Akajiandaa kumkabili kwa mikono
yake. Punde akamuona mtu akipita,
alikuwa mwanamke. Alionekana na
mlinzi wa Jengo lile. Alikuwa na
Bunduki aina ya Oxcelf SG mkono.
Alikuwa akitembea akiangalia huku na
huko. Masimba akaona ulikuwa muda
sahihi wa kufanya kitu. Alichokifanya ni
kumtokea yule msichana kwa nyuma
na kumpigia mluzi. Msichana yule
akageuka akidhani aliitwa na
mwenzake. Lakini alijikuta akikutana
na flying kicks kutoka kwa masimba.
Kwa kuwa hakutarajia kitendo kile,
mwanamke yule akajikuta akishindwa
kuzuia mapigo yale, na kuruhusu
mateke yale kumtupa chini kama
furushi.
May be an image of 1 person

 
Back
Top Bottom