Jackal
JF-Expert Member
- Apr 10, 2012
- 9,971
- 13,608
- Thread starter
-
- #61
NITAKUPATA TU
SEHEMU YA 045
Ukimya ukachukua nafasi maeneo yale.
Hakuwa akisikia tena ile minong'ono.
Akausogelea mlango katika aina fulani
ya ukimya. Hata alipoufikia mlango
bado hapakuwa na kizuizi chochote.
Masimba akajaribu kutizama huku na
huko, lakini bado hapakuwa na kizuizi.
Bado hapakuwa na mtu. Mkono wake
ukashika kitasa na kukizungusha,
mlango ukamtii kama mfano wa mbwa
anapomtii chatu. Bastola ilikuwa
imetangulia Mbele tayari kumuondoa
mtu yoyote. Akaufungua zaidi kisha
kuingia. Alipoingia ndani alipokewa na
ukimya tena. Kuingia kwake tu hata ile
miguno ikapotea. Akaikamata bastola
zaidi na zaidi. Kidole bado kilisubiri
kuifanya kazi yake. Kazi ya kutoa tiketi
na hata usafiri. Usafiri wa kuwapeleka
watu kuzimu. Alitaka wakapumzike
sambamba na mama yake na hata Dee.
Alitaka wakajibu mashtaka yake mbele
ya Asteria na Familia yake. Kuingia
hapo akapokewa na harufu ya mipira
ya kiume. Harufu ya condom ilikuwa
imetawala katika nyumba ile.
Akaongeza hatua mbele kuwatafuta
wasafiri. Akaipita sebule bila kukutana
na kizuizi chochote. Aliposogea mbele
akasikia vishindo vya mtu vikionyesha
mtu kusogea kule alipo. Punde
akamuona mwanamume akitokea
katika giza lile. Giza ambalo alishindwa
kutambua kwa nini limeachwa
kutawala pale ndani. Mwanaume yule
akatembea na kupita karibu na
Masimba bila kumuona. Masimba
akamuacha apite, alivyopita
akamtokea kwa nyuma na kumkata
karate ya Shingo. Mtu yule akaanguka
kama mzigo. Baada ya kuhakikisha mtu
yule hayupo hai, akamsachi mifukoni.
Akamkuta na Bastola mbili sambamba
na vitamburisho kadhas. Vyote
akavichukua na kuvisunda mifukoni.
Baada ya kumaliza vyote akamshika na
kumuweka pembeni. Akasogea pale na
kuanzs kutembea kuingia ndani
alipotokea yule mtu. Wakati
anaukaribia mlango akasikia watu
wakiongea kwa ndani. Katika
mazungumzo yao akahisi walikuwa
watatu kutokana na mchanganyiko wa
Sauti zao.
"Mbona Fred harudi? Richie hembu
muangalie inawezekana amezima.
Aliisikia sauti ikitokea ndani. Masimba
akajua kuna mtu anakuja. Hivyo
akajibanza pembeni. Mara akauona
mlango ukifunguliwa kisha mtu tena
akatokea. Masimba akamuacha asogee
mpaka usawa wake. Hata alipoufika
usawa ule akajikuta akiguswa na kitu
cha barifi. Kisha sauti nzito ya
mwanaume ikanguruma. "Tulia kama
Ulivyo, ukifanya chochote sitasita
kukusafirisha kuzimu." " mtu yule
hakutarajia lile, akahamanika na kutaka
kupiga kelele. Masimba akamuwahi
kwa pigo moja ya kidogoni, mtu yule
akaanguka kama furushi. Masimba
akamuwahi na kumshindilia ngumi
kama tano. Mtu yule akatepeta kama
mlenda. Alimpekuwa mifukoni. Huyu
hakuwa na Silaha yoyote zaidi ya
paketi tano za condom. Akamuacha
sasa alikuwa akizama ndani kuwakabili
watu ambao walikuwa ndani.
Aliusukuma mlango taratibu na
kuchungulia kwa ndani. Watu wawili
walikuwa wamepakatana miguuni.
Kilichomshangaza huku ndani taa
hafifu zilikuwa zikiwaka. Nuru hiyo
ndio iliyofanya macho yake kutua kwa
watu wale wawili. Mwanaume na
mwanamke. Akaufungua mlango tena
na kupiga mluzi. Yule mwanaume
aliyekuwa amempakata mwanamke
akamuomva mwanamke asimame
kisha yeye kusogea pale mlangoni
huku akiuliza.
"Richie kuna nini? Aliuliza mtu yule
huku akiufungua mlango pasipo na
tahadgari. Akajikuta akikutana na
mapigo matatu ya kung fu. Mtu yule
akapepesuka na kwenda kumuangukia
mwanamke yule. Masimba hakuitoa
nafasi hiyo kwa mtu yule kuinuka.
Akawawahi wote pale chini huku
mdomo wa Bastola ukiwatizana sawa
sawia. Wote walikuwa wakitweta kwa
hofu. Kila mmoja alikuwa ameyatoa
macho yake akimtizama Masimba. Hofu
ilikuwa ikionekana machoni mwao.
Hofu ambayo haikufanana na
uonekanaji wa watu hawa. "Nimekuja
na tiketi zenu za kuzimu, nimekuja na
usafiri wa kuwapeleka huko. Lakini
mkinijibu maswali yangu naweza
kufikiria kuwaacha." Aliongea masimba
Akiwatizama watu wale pasipo
kuonyesha utani. "Usituue tutakujibu
maswali yako." Aliongea mwanamke
yule akitetemeka.
"Jimmy na suresh wako wapi? Akauliza
masimva.
"Mimi sijui unauliza nini. Alijibu yule
mwanaume akimuangalia masimba
usoni. "Narudia tena wako wapi Jimmy
na Suresh? Aliukiza tena safarii hii
akiuinua mkono ulioshika bastola.
"Unataka nikujibu mara ngapi?
Nimesema sijui.. akajibu tena yule
mwanaume. Muda ule ule mlipuko
mdogo ukatokea, bastola ya nasimba
ilikuwa imekohoa. Risasi ikatua
kwenye paja lake la kushoto. Akapiga
yoweee kubwa sana. "Utasema
hutasema? Akauliza masimba huku
bado bastola yake ameielekeza kwa
mtu yule aliyekuwa akigumia kwa
maumivu. Wakati mtu yule akiharibu
kujibu mlango ukasukumwa kwa
nguvu huku risasi kama mvua
zikimiminwa mle ndani. Masimba
akajivingirisha chini kisha kuchupa na
kuangukia pembeni. Risasi zikapita
muda ule ule akasikia yowee kutoka
pale alipowaacha wale majambazi.
Baada ya muda wa dakika tano. Risasi
zikakoma ukimya ukatawala Eneo lote.
Masimba Bado alikuwa amejificha pale
akiwaangalia wale watu. Hata wao
walionekana wakitafuta kitu. Hapo
akajua walikuwa wakimtafuta yeye.
Hakutaka kuwachelewesha, bastola
yake ikakohoa tena mfululizo. Watu
wanne walikuwa wakianguka mithili
ya magunia. Walikuwa tayari kwenye
safari ya kuzimu. Baada ya kuhakikisha
amewamaliza wote akainuka na
kusogea pale. Hapo akagundua hata
yule mateka wake wakiume alikuwa
ameuawa. Lakini kilichomshangaza ni
kutokumuona mwanamke yule. Wakati
akiendelea kutafuta akasikia kilio
kutoka chini ya kiti kikubwa . Punde
akamuona msichana yule akiinuka
huku akitetemeka. Bastola ya masimba
tayari ilikuwa ikimtizama. Lakini
alipomuangalia vizuri usoni..
Akajisemea malaika huyu hapaswi
kufa. "Nifuate tuondoke hapa kabla
polisi hawajaja." Aliongea Masimba
Huku akimvuta yule msicgana
waondoke mle ndani.
******
Walikuwa wawili tu ndani ya chumba
cha hoteli ile. Bastola ilikuwa bado
mkononi kwa masimba akuendelea
kumuangalia mwanadada yule
aliyekuwa akitetemeka kwa hofu.
"Unaitwa nani? Akauliza masimba
akiendelea kumtizama.
"Nani.!!!? Mimi au... aliuliza Binti huku
akitetemeka.
"Kwani hapa tuko wangapi?" Akauliza
Masimba akimuangalia tena.
"Tupo wawili." Akajibu tena Hofu
ikionekana machoni.
"Basi tambua nakuuliza wewe..
naomba unijibu kabla sijabadili
maamuzi." Aliongea Masimba.
"Naitwa SALHA ....." akajibu msichana
yule. "Umefikaje pale kwenye ile
nyumba na nani amekufikisha? Aliuliza
Masimba akiendelea kumuangalia.
"Nimeletwa pale na Jimmy. Wakati
ananileta aliniambia kuwa
amenitafutia kazi, lakini nilipofika
aliniweka pale kama Msimamizi wa
Biashara yao. Alijibu yule msichana. "JE
ni Biashara gani inafanywa pale? Na
kwa nini ulipogundua kazi ulioambiwa
haipo, wewe ukaendelea kukaa? Binti
yule akamuanglia Masimba kisha kwa
sauti yake ya upole akajibu. "Naogopa
kukwambia wataniua..... Maana
nishatishiwa kupigwa bastola. Baada ya
kumuuliza kwa nini ana muogopa mtu
mmoja aitwaye masimba.". " kwahiyo
una muogopa Jimmy lakini huniogopi
mimi? Tambua mimi ni israil nikiamua
ufe haufikishi sekunde moja. Naomba
nijibu maswali yangu kabla sijakupa
tiketi yako." Alinguruma Masimba
akimuangalia binti yule. Salha akainua
uso na kumwangalia masimba kisha
kwa Sauti dhaifu akasema ....
ITAENDELEA
SEHEMU YA 045
Ukimya ukachukua nafasi maeneo yale.
Hakuwa akisikia tena ile minong'ono.
Akausogelea mlango katika aina fulani
ya ukimya. Hata alipoufikia mlango
bado hapakuwa na kizuizi chochote.
Masimba akajaribu kutizama huku na
huko, lakini bado hapakuwa na kizuizi.
Bado hapakuwa na mtu. Mkono wake
ukashika kitasa na kukizungusha,
mlango ukamtii kama mfano wa mbwa
anapomtii chatu. Bastola ilikuwa
imetangulia Mbele tayari kumuondoa
mtu yoyote. Akaufungua zaidi kisha
kuingia. Alipoingia ndani alipokewa na
ukimya tena. Kuingia kwake tu hata ile
miguno ikapotea. Akaikamata bastola
zaidi na zaidi. Kidole bado kilisubiri
kuifanya kazi yake. Kazi ya kutoa tiketi
na hata usafiri. Usafiri wa kuwapeleka
watu kuzimu. Alitaka wakapumzike
sambamba na mama yake na hata Dee.
Alitaka wakajibu mashtaka yake mbele
ya Asteria na Familia yake. Kuingia
hapo akapokewa na harufu ya mipira
ya kiume. Harufu ya condom ilikuwa
imetawala katika nyumba ile.
Akaongeza hatua mbele kuwatafuta
wasafiri. Akaipita sebule bila kukutana
na kizuizi chochote. Aliposogea mbele
akasikia vishindo vya mtu vikionyesha
mtu kusogea kule alipo. Punde
akamuona mwanamume akitokea
katika giza lile. Giza ambalo alishindwa
kutambua kwa nini limeachwa
kutawala pale ndani. Mwanaume yule
akatembea na kupita karibu na
Masimba bila kumuona. Masimba
akamuacha apite, alivyopita
akamtokea kwa nyuma na kumkata
karate ya Shingo. Mtu yule akaanguka
kama mzigo. Baada ya kuhakikisha mtu
yule hayupo hai, akamsachi mifukoni.
Akamkuta na Bastola mbili sambamba
na vitamburisho kadhas. Vyote
akavichukua na kuvisunda mifukoni.
Baada ya kumaliza vyote akamshika na
kumuweka pembeni. Akasogea pale na
kuanzs kutembea kuingia ndani
alipotokea yule mtu. Wakati
anaukaribia mlango akasikia watu
wakiongea kwa ndani. Katika
mazungumzo yao akahisi walikuwa
watatu kutokana na mchanganyiko wa
Sauti zao.
"Mbona Fred harudi? Richie hembu
muangalie inawezekana amezima.
Aliisikia sauti ikitokea ndani. Masimba
akajua kuna mtu anakuja. Hivyo
akajibanza pembeni. Mara akauona
mlango ukifunguliwa kisha mtu tena
akatokea. Masimba akamuacha asogee
mpaka usawa wake. Hata alipoufika
usawa ule akajikuta akiguswa na kitu
cha barifi. Kisha sauti nzito ya
mwanaume ikanguruma. "Tulia kama
Ulivyo, ukifanya chochote sitasita
kukusafirisha kuzimu." " mtu yule
hakutarajia lile, akahamanika na kutaka
kupiga kelele. Masimba akamuwahi
kwa pigo moja ya kidogoni, mtu yule
akaanguka kama furushi. Masimba
akamuwahi na kumshindilia ngumi
kama tano. Mtu yule akatepeta kama
mlenda. Alimpekuwa mifukoni. Huyu
hakuwa na Silaha yoyote zaidi ya
paketi tano za condom. Akamuacha
sasa alikuwa akizama ndani kuwakabili
watu ambao walikuwa ndani.
Aliusukuma mlango taratibu na
kuchungulia kwa ndani. Watu wawili
walikuwa wamepakatana miguuni.
Kilichomshangaza huku ndani taa
hafifu zilikuwa zikiwaka. Nuru hiyo
ndio iliyofanya macho yake kutua kwa
watu wale wawili. Mwanaume na
mwanamke. Akaufungua mlango tena
na kupiga mluzi. Yule mwanaume
aliyekuwa amempakata mwanamke
akamuomva mwanamke asimame
kisha yeye kusogea pale mlangoni
huku akiuliza.
"Richie kuna nini? Aliuliza mtu yule
huku akiufungua mlango pasipo na
tahadgari. Akajikuta akikutana na
mapigo matatu ya kung fu. Mtu yule
akapepesuka na kwenda kumuangukia
mwanamke yule. Masimba hakuitoa
nafasi hiyo kwa mtu yule kuinuka.
Akawawahi wote pale chini huku
mdomo wa Bastola ukiwatizana sawa
sawia. Wote walikuwa wakitweta kwa
hofu. Kila mmoja alikuwa ameyatoa
macho yake akimtizama Masimba. Hofu
ilikuwa ikionekana machoni mwao.
Hofu ambayo haikufanana na
uonekanaji wa watu hawa. "Nimekuja
na tiketi zenu za kuzimu, nimekuja na
usafiri wa kuwapeleka huko. Lakini
mkinijibu maswali yangu naweza
kufikiria kuwaacha." Aliongea masimba
Akiwatizama watu wale pasipo
kuonyesha utani. "Usituue tutakujibu
maswali yako." Aliongea mwanamke
yule akitetemeka.
"Jimmy na suresh wako wapi? Akauliza
masimva.
"Mimi sijui unauliza nini. Alijibu yule
mwanaume akimuangalia masimba
usoni. "Narudia tena wako wapi Jimmy
na Suresh? Aliukiza tena safarii hii
akiuinua mkono ulioshika bastola.
"Unataka nikujibu mara ngapi?
Nimesema sijui.. akajibu tena yule
mwanaume. Muda ule ule mlipuko
mdogo ukatokea, bastola ya nasimba
ilikuwa imekohoa. Risasi ikatua
kwenye paja lake la kushoto. Akapiga
yoweee kubwa sana. "Utasema
hutasema? Akauliza masimba huku
bado bastola yake ameielekeza kwa
mtu yule aliyekuwa akigumia kwa
maumivu. Wakati mtu yule akiharibu
kujibu mlango ukasukumwa kwa
nguvu huku risasi kama mvua
zikimiminwa mle ndani. Masimba
akajivingirisha chini kisha kuchupa na
kuangukia pembeni. Risasi zikapita
muda ule ule akasikia yowee kutoka
pale alipowaacha wale majambazi.
Baada ya muda wa dakika tano. Risasi
zikakoma ukimya ukatawala Eneo lote.
Masimba Bado alikuwa amejificha pale
akiwaangalia wale watu. Hata wao
walionekana wakitafuta kitu. Hapo
akajua walikuwa wakimtafuta yeye.
Hakutaka kuwachelewesha, bastola
yake ikakohoa tena mfululizo. Watu
wanne walikuwa wakianguka mithili
ya magunia. Walikuwa tayari kwenye
safari ya kuzimu. Baada ya kuhakikisha
amewamaliza wote akainuka na
kusogea pale. Hapo akagundua hata
yule mateka wake wakiume alikuwa
ameuawa. Lakini kilichomshangaza ni
kutokumuona mwanamke yule. Wakati
akiendelea kutafuta akasikia kilio
kutoka chini ya kiti kikubwa . Punde
akamuona msichana yule akiinuka
huku akitetemeka. Bastola ya masimba
tayari ilikuwa ikimtizama. Lakini
alipomuangalia vizuri usoni..
Akajisemea malaika huyu hapaswi
kufa. "Nifuate tuondoke hapa kabla
polisi hawajaja." Aliongea Masimba
Huku akimvuta yule msicgana
waondoke mle ndani.
******
Walikuwa wawili tu ndani ya chumba
cha hoteli ile. Bastola ilikuwa bado
mkononi kwa masimba akuendelea
kumuangalia mwanadada yule
aliyekuwa akitetemeka kwa hofu.
"Unaitwa nani? Akauliza masimba
akiendelea kumtizama.
"Nani.!!!? Mimi au... aliuliza Binti huku
akitetemeka.
"Kwani hapa tuko wangapi?" Akauliza
Masimba akimuangalia tena.
"Tupo wawili." Akajibu tena Hofu
ikionekana machoni.
"Basi tambua nakuuliza wewe..
naomba unijibu kabla sijabadili
maamuzi." Aliongea Masimba.
"Naitwa SALHA ....." akajibu msichana
yule. "Umefikaje pale kwenye ile
nyumba na nani amekufikisha? Aliuliza
Masimba akiendelea kumuangalia.
"Nimeletwa pale na Jimmy. Wakati
ananileta aliniambia kuwa
amenitafutia kazi, lakini nilipofika
aliniweka pale kama Msimamizi wa
Biashara yao. Alijibu yule msichana. "JE
ni Biashara gani inafanywa pale? Na
kwa nini ulipogundua kazi ulioambiwa
haipo, wewe ukaendelea kukaa? Binti
yule akamuanglia Masimba kisha kwa
sauti yake ya upole akajibu. "Naogopa
kukwambia wataniua..... Maana
nishatishiwa kupigwa bastola. Baada ya
kumuuliza kwa nini ana muogopa mtu
mmoja aitwaye masimba.". " kwahiyo
una muogopa Jimmy lakini huniogopi
mimi? Tambua mimi ni israil nikiamua
ufe haufikishi sekunde moja. Naomba
nijibu maswali yangu kabla sijakupa
tiketi yako." Alinguruma Masimba
akimuangalia binti yule. Salha akainua
uso na kumwangalia masimba kisha
kwa Sauti dhaifu akasema ....
ITAENDELEA