Hadithi: Penzi la Kiziwi

Hadithi: Penzi la Kiziwi

Daah watoa hadithi wote wangekuwa kama wewe,ingekuwa safi sana. Umeshusha vipande bandika bandua mpaka raha yani. Big up sana Jon woka hauna lawama. Siku yoyote ukipata nafasi utatuwekea sizoni two.
Usijali kaka karibu
 
Episode 14 (mwisho msimu wa Season 0ne)

Nilihema juu juu, sikuamini kile ambacho nakiona mbele yangu. Ni kweli yule alikuwa ni Jane ama mwingine. Naye alinitazama huku akiwa na hasira mno, macho yake yaliingia ndani. Binti ambaye alikuwa anakimbia sasa alirudi na kumkumbatia Jane katika mapaja yake.

Sikuwa na jinsi ilinibidi nijishushe kwa Jane, nilijilalamisha ili aweze kunisamehe na kupata kuzungumza ili kujua nini ambacho kimetokea. Hatima ya mimba yake ni ipi? Mtoto ambaye alikuwa amembeba ni wa nani? pamoja na maswali mengine mengi ambayo nilikuwa nayo.

Nashkuru Mungu, Jane alinipa uhuru huo. Basi, nilimchukua na kwenda naye kwenye moja ya hotel kisha tuliweka makazi hapo. Tukaanza kuzungumza kwa kutumia maandishi, kila mmoja alikuwa anamtumia meseji mwenzake maana nilimpatia moja ya simu yangu.
“Mtoto yupo wapi?”
“Huyu ambaye unamuona anakula chakula” nilimtazama yule binti.

Sura yake ilikuwa ya Jane kabisa, walitofautiana vitu vichache sana. Jane alimwambia aje kuniamkia kwa kumuoneshea ishara, naye alifanya hivyo. Aliniamka kwa kuweka mkono kichwani kabla ya kurudi sehemu alipokuwa mwanzo.
“Mbona hajaongea?”
“Bubu”
“Bubu?”
“Ndio”
“Kwanini?”
“Acha tu”
“Kipi kilitokea nieleze?”
“Shangazi alinifuatilia tena miaka mitatu nyuma”
“Ikawaje?”
“Alinikuta nikiwa na huyu mtoto, aliamua kumkata ulimi”
“Mungu wangu! Kwanini anafanya haya?”
“Sijajua”
“Kwahiyo anaitwa nani?”
“Jessica”
“Umempa jina nzuri, na baba je?”
“Siwezi kufuta ukweli kuwa huyu ni damu yako, anaitwa Jessica Jack”
“Ahsante! Halafu huyo ambaye umembeba mgongoni ni mtoto wa nani?”
“Janeth”
“What! Inamaana Janeth ana mtoto?”
“Ndio”
“Yupo wapi mwenyewe?” swali langu lilimfanya Jane kuangua kilio.

Alitoa picha ya Janeth katika mkoba mdogo ambao alikuwa ameubeba kisha alinikabidhi. Niliitazama ile picha vizuri, ilimuonesha Jane akiwa ametobolewa macho. Nilipatwa na huruma kama sio hasira. Nilishika tena simu na kumtumia meseji.
“Amepatwa na nini?”
“Ndivyo alivyokuwa hivi sasa”
“Inamaana upo naye?”
“Ndio, naishi naye”
“Wapi?”
“Kwangu”
“Ok, unatakiwa kunipeleka na hili la shangazi yako kama yupo hai tutajua nini la kufanya” nilisisitiza.

Kiukweli nisiwe muongo katika siku ambayo moyo wangu uliumia ni hii, niliteseka sana moyoni kuona watu ambao nilikuwa nawapenda wakiwa katika mateso. Basi, tuliondoka na Jane hadi nyumbani kwake ambako alikuwa anaishi. Ilikuwa ni kwenye ghofu ambalo liliandikwa NYUMBA HAIUZWI EPUKA MATAPELI. Alikuwa akiishi hapo.

Tuliingia ndani na kumkuta Janeth akiwa amelala, muonekano wake ulikuwa tofauti kabisa. Maumivu ndani ya mwili wake yalikuwa mengi. Janeth alikonda, Janeth alikosa furaha, Janeth hakuwa na mvuto kama hapo awali.
“Huyu ndio Janeth wangu, natamani hata kumuua lakini naogopa dhambi. Lakini hana ambalo analijua, haoni furaha katika huu ulimwengu” niliisoma hii meseji huku machozi yakinitoka.
“Nani ndio baba wa huyu mtoto wake?”
“Sijui maana hata mimi nilimkuta mbezi akiwa na ujauzito wake”
“Nani ambaye alimsafirisha kutoka Dodoma hadi hapa?”
“Sijajua maana Mama alishafariki”
“Mama amekufa?”
“Ndio”
“Mungu wangu! Ilikuwaje?”
“Mungu aliamua kumtesa”
“Kwahiyo wewe unaishije?”
“Bado natafutwa ili kuuawa na Shangazi, bado maisha yangu yapo sehemu mbaya. Natoka jioni kutafuta riziki na mchana natumia kulala nikiwa na familia yangu” aliniambia Jane.

Siku hii tulizungumza mambo mengi sana, akaniulizia kuhusu familia yangu. Naendeleaje na maisha na mambo mengine kadha wa kadha ambayo nilimjibu, mwisho niliaga na kurudi nyumbani ambako nilimkuta Judy akiwa ni mwenye hasira maana nilikuwa nimechelewa kurudi.
“Ulikuwa wapi?”
“Kuna jambo nataka tuongee hata kabla ya kujua nilikuwa wapi?”
“Jambo gani?”
“Unakumbuka kama kuna mtu anaitwa Janeth”

“Usiniambie ulienda kwa Jane?”
“Kwanini unakuwa mkali hivyo?”
“Inamaana hadi leo unamfuatilia si ndio?”
“Hapana ila nilikutana naye njiani ikanilazimu nisimame. Tazama sasa hivi Janeth alivyo” nilitoa picha na kumuonesha Judy.

Nilimtazama Judy akiwa anatazama ile picha, macho yake yalianza kutoa machozi. Nikajua kwamba tayari kuna kitu kinamsumbua katika moyo wake, tayari alikuwa na huruma dhidi ya kile ambacho amekiona.
“Janeth anateseaka, Janeth hana macho, hasikii pia”
“Nani amefanya haya yote?”
“Ni yule ambaye alitaka kuwaua”
“Shangazi?”
“Ndio, binafsi nakuomba tuwasaidie hawa watu maana Dada yake anatafuta pesa ili kumpatia matibabu ndugu yake. Tuwasaidie hata kama watashindwa kuona ama kusikia lakini iwe kuwe na urahisi kimaisha. Jane anategemea Mbila ili kupata hela ya kuendesha maisha yake, hana ambalo analifahamu kwa sasa zaidi ya kunusa maumivu. Anahitaji msaada wetu” nilimwekea kituo hapa Judy.

Naye alivuta pumzi ndefu na kuiachia, macho yake yalikuwa yanaendelea kudondosha machozi huku akiwa anatetemeka na ile picha.
“Then baada ya kuwapa msaada nini kitaendelea?”
“Maisha yao yakiwa mazuri tu inatosha hayo mengine watapambana wenyewe”
“Hautarudiana naye?”
“Siwezi”
“Sawa! Nitafanya hilo” Judy alinipa uhakika nami nilimani kuwa ni kweli angeweza kufanya hili…... ITAENDELEA

Mwisho wa msimu wa kwanza, usikose kujua nini haswa kiliendelea katika msimu wa pili ambao utakujia hivi karibuni……….
Natamani kuendelea kuona mwendelezo
 
Back
Top Bottom