Hadithi: Time Travel

Hadithi: Time Travel

IMG-20220425-WA0000.jpg
 
MUDA

SEHEMU YA SITA.


“Basi mwanangu naomba upumzike kesho njoo utakuta nimeongea nae”
Baada ya maneno hayo Anitha alipangusa machozi na kusimama akisaidiwa na mama Nelson.

“Naomba unisindikize mama nimeacha gari kule barabarani,”
Waliongozana huku mama Nelson akimpa maneno ya kumfariji. Walipofika Anitha aliingia ndani ya gari na kutoa kiasi flani cha fedha na kumkabidhi mama Nelson.
“Simulizi langu linaitwa”
“ Mimi na wewe”
Vijana wawili walikutana kwenye ukumbi wa mziki msichana alipenda kunywa sana kileo ila mvulana alipenda tu kusikiliza mziki wali...........”
Inatosha Meneja alimkatisha yule kijana
“ Leo jioni njoo usimulie ila jaribu kuweka hisia si ulikuwa unamsikiliza mwenzako aliyeondoka”
Moyo wa Meneja ulikuwa na mashaka ila hakutaka kumuangusha mtu aliyempatia kiasi cha fedha.
“Endelea kufanya mazoezi nitakufuata baada ya kipindi”.
Aliongea yule mwanamme aliyekuwa mkuu wa shule ya akina Nelson.
“ Ndugu wasikilizaji leo tutaendelea na kipindi cha simulizi kila mtu aliisogelea Redio yake wengine waliweka spika zao za maskioni tayari kwa kusikiliza Anitha mwenyewe alikuwa amewasha Redio yake kupunguza hisia za maumivu cha ajabu kufika tu katikati mwa mda wa simulizi wengi walishasahau kama Redio imewashwa wengine walikuwa wakisonya.
Ni kama mtu amezoea kula wali maua gafla unaletewa bokoboko tena lililozidishiwa maji Anitha aliirudisha redio ile na kujigonga kwenye mguu wa meza na kuifanya izime bila kupenda. Mda wote Anitha alikuwa akiitazama saa yake iliyoko mezani kama kiwango cha mwendo wa muda .

Usingizi haukumjia mda wote alikuwa akiiwaza safari ya Mtoni Mtangoni. Saa kumi na moja alfajiri. Anitha alikuwa mezani kwake mbele ya kioo kikubwa kinachoilemba meza hiyo akijipodoa (kujilemba) kwa manukakato tofauti.
Baada ya kumaliza alichukua saa yake ya mkononi na kuivaa mkono wa kushoto aliitazama vyema wakati inasukuma mishale yake.
“Kati ya vitu unavyopaswa kutunza maishani mwako ni saa hii ninayokupatia”
aliikumbuka sauti ya daktari wake aliyeponesha maisha yake.
“Ukijua kuitumia vizuri saa hii maisha yako yatabadilika sana, maana utakuwa na uwezo wa kufanya chochote nje na ndani ya mda”.
Bado maneno ya daktari yaliendelea kumjia. Baada ya kumaliza alichukua funguo zake za gari na kufungua friji yake alitoa chupa moja ya mvinyo na kuiweka ndani ya gari, kisha aliwasha gari lake na safari mtangoni ilianza.
Alikuwa ameazimia moyoni mwake ikiwa Nelsoni atamkimbia tena atahakikisha anakunywa mvinyo yote hiyo ili asihisi maumivu yamtawale kama ilivyokuwa. Anita alipofika Mwenge alisimama na nkuanza kuzunguka huku na kule, alikuwa akitafuta batiki nzuri na yenye mwonekano mzuri, alitaka kumzawadia mama Nelson kama atamsaidia aweze kuongea naye.
Katika mzunguko wote hakuweza kupata, hivyo aliliwasha gari lake mpaka Kaliakoo. Aliweza kuipata batiki moja ilikuwa na mchanganyiko wa bluu na mawingu ya mvua, kusema kweli batiki ile ilpendeza sana. Hapo moyo waAnitha ulilidhika na aliingiza katika gari lake na kuondoka.
Nelson alikuwa amelala bado, akiwa kitandani aliendelea kuesabu mda wa dakika thelathini uliotosha kuaribu maisha yake.
“huu mda ni nini?”
Alionekana kujiuliza
“ Dakika tu chache mfumo mzima wa maisha unabadilika”
Hivi hakuna njia yoyote ya kubadili makosa uliyoyafanya bila kupoteza mda mwingine?.
Hivi nikibadili maisha yangu na kuyafanya yawe bora nitakuwa nimeondoa dosari ya awali? Naona hiyo itakuwa kama kuanza safari ya kwenda mji A. Napata changamoto ya usafiri badala ya kurekebisha unaamua kupanda mwingine unaokufikisha mji B. Eti kwa sababu yote ni miji hivi siwezi kufanya jambo lolote au ni.......”

Nelson aligunduliwa na mama yake mdogo aliyemuomba aje sebuleni ana shida naye kubwa.

Nelson alisonya kimoyo moyo kwani aliona mda wake unaendelea kupotea lakini alitambua kuwa yule ni sawa na mama yake mzazi hangekuwa na kibali cha kumkatalia jambo lolote lile. Alinyanyuka na kuelekea sebuleni ambako alimkuta Anitha akiwa amekaa huku chai ya kila aina ikiwa imetapakaa mezani.
“Njoo”
Mama yake alimwita kwa hisia.
Nelson alijivuta kwa unyonge na kukaa mahali pale. Moyoni mwa Anitha kulikuwa kunarindima hisia za shangwe. Mdomo wake ulianza kucheza cheza bila mpangilio.

“Nisamehe mwanangu mpendwa kuna hadithi mbaya kati yangu mimi na wewe ninaona hadi haibu ya kukusimulia hadithi hii”.
Alipotamka maneno hayo machozi yalianza kumtoka mfululizo.
“ Nelson mimi ndiye mama yako mzazi yule uliyekuwa unaishi nae ni mama mkubwa, yaani ni dada yangu mimi, nikiwa kidato cha pili nilipendana na mwalimu wangu wa masomo ya sayansi maana mimi pia nilikuwa napenda masomo hayo, alikuwa bado kijana tena ni mzuri kama wewe, kwa kuwa yule mwalimu alikuwa ni wa kujitolea aliitajika kwenda masomoni nje ya nchi.
Nilimwimiza tupime kabla ya yeye kuondoka ili kila mmoja ajue anabaki akiwa katika hali gani. Kumbe mimi nilitaka nijue afya yangu, maana nilikuwa sijielewi kabisa katika mwili wangu. Tulipopima niligundulika mjamzito mwalimu wangu aliogopa sana akawa anatetema tu bila kuongea chochote.
Nilienda nyumbani huku nimemuaidi mwalimu wangu atafakari jinsi ya kufanya, lakini kesho yake hakutokea aliamua kuondoka kimya kimya, hali niliyopitia ilikuwa ngumu sana nilifukuzwa shule na baba yangu aliwekwa ndani miezi miwili kwa kutonitunza vizuri.
Kwa kweli akili yangu ilivurugika kila nilipomuona mama yangu analia, toka siku hiyo niliapa nitatoa mimba yako au nitakutupa endapo ningefanikiwa kukuzaa.

Dada yangu aliujua huo mpango wangu, alinifungia ndani kwa uwangalizi wake mpaka nilipojifungua, alikuchukua na kuniambia niko tayari kufanya lolote ninalotaka kufanya.
Toka siku hiyo sijawahi kuonana na mwalimu wangu ambaye ndiye baba yako. Kwa kweli mpaka leo sijawahi kusikia taarifa yake yoyote.

Alitua kidogo na kuvuta pumzi nzito, alipokwisha kuitoa alisema
“wewe pia unataka kupitia hali yangu , usiruhusu hilo mwanangu, muhurumie Anitha pia”,

Alipomaliza kusema hayo Nelson alinyanyuka huku kilio cha kwikwi kikimuandama, alitoka nje na kuanza kupambana nayo. Anitha alimfuata naye alikuwa akilia kwa uchungu.
“Pole Nelson, mimi pia napitia hali kama yako”.
Alimtuliza huku akimpapasa mgongoni.
“Njoo mwanangu”.
Mama Nelson aliwaita.
Baada ya kukaa, waliongea mambo mengi na wote walionekana wakinywa chai kwa pamoja.
“Hizo saa mlinunua wapi?”
Aliuliza mama Nelson baada ya kuona saa zao zanafanana. Kila mmoja alinyanyua mkono na kuitazama saa yake zote zilihesabu saa sita kamili mchana, hata hivyo hakuna aliyejibu swali hilo zaidi ya wote kutabasamu kwa mshangao.

Anitha alinyanyuka haraka kama mtu anayefukuzwa na baada ya mda kidogoa alirudi na mzigo mkononi, alimkatia mama Nelson na kumwambia akajaribu huko ndani kwake.
“Acha wee! Mama lakee”
alitamka Nelson baada ya kumuona mama yake kapendeza na batiki limemkaa sawasawa katika mwili wake. Mama Nelson alianza kuruka ruka kwa staili ya tajiri wa kikongo maarufu pedejyee. Ni kama kumkuna anayewashwa, Anitha na mziki alikwisha ingia na kuanza kukatika.

Wakati hayo yakiendelea Nelson alikuwa akiukagua mda kuona ni matokeo gani na yanaweza kuchukua mda gani yanayoletwa na furaha. Baada ya staili hizo zisizo na hara yoyote ya mziki, wote walionekana kuwa wamoja katika mapatano.
Hapo Anitha alimuomba Nelson waende pamoja nyumbani kwake.
Kwa furaha waliyokuwa nayo Nelson asingependa kuikatiza alikubali mara moja. Na mama Nelson aliwasindikiza mpaka kwenye gari. Mama Nelson alirudi nyumbani huku moyo wake ukihisi furaha kubwa.
Wakati mama akisherehekea Anitha pia moyo wake ulikuwa mweupe kabisa. Aliliwasha gari lake na kuanza safari ya kuelekea Tegeta nyumbani kwake.
Alipofika Mtangoni kwa Azizi Ally, alikuta foreni ndogo na aliamua kufungua mziki huku mawazo yake yakimuona mama Nelson akicheza kwa staili yake. Kadiri mziki ulivyomuingia ndivyo Anitha alivyoanza kujitupatupa kwa mbwembwe.

Foleni iliruhusiwa na Anitha alikanyaga mafuta kwa fujo.
Ni Nelson aliyekuwa wa kwanza kumuona mtoto aliyekuwa anamkimbilia mama yake mzazi aliyekua ameishavuka bara bara.
“mama wee!”
Alitamka Anitha huku akikanyaga breki gafra.
“Sio kweli hii ni ndoto.”
TUKIO LA AJABU

Alijipiga piga kichwani kuakikisha kama amelala usingizi au ni mzima wa afya, ukweli ni kwamba ni mzima kabisa tena hana hata alama ya mchubuko.
Nelson hakuwa akijishangaa mwenyewe hapana, pia kundi la vijana waliokuwa wanacheza mpira walimzunga kwa mshangao wa aina yake.
“Wewe nani na umefikaje hapa?”
Alianza kapteni wa timu hiyo, kilichowashangaza wakati wanajiandaa kuanza mazoezi hakukua na mtu yeyote uwanja wote waliukagua.
Sasa imekuaje aonekane mtu katika eneo hilo?
Hayo maswali walijiuliza sana.
“Unaitwa nani?”
Mchezaji mmoja alimuuliza
“Mimi naitwa Nelson! Hapa niko wapi?”
Nelson nae aliuliza
“Unaitwa nani?
Alistaajabu yule kapteni, maana kila alipomtazama yule mtu alikuwa na sula ya baba yake, tofauti ni kwamba baba yake ni mkubwa kiumli ukilinganisha na mtu huyu.
“Umetoka wapi?”
Aliuliza yule kijana mchezaji wa mpila.
“Tumegonga mtoto na gari,nilikuwa na Anitha sijui yeye yuko wapi, tulikuwa Mtoni kwa Azizi Ally .
“Anitha?”
Kijana yule alioji kwa mshangao,
“Wewe ni Nelson,alafu ulikuwa na Anitha!”
Alizidi kuchanganyikiwa yule kijana .

“Mlikuwa mnatoka wapi?”
Alizidi kuhoji, Tunatoka Mtangoni kwa mama yangu mzazi.
“Kwa mama yako mzazi! Anaitwa nani?”
Kijana alizidi kuchanganyikiwa zaidi
“Joanita”
Alijibu kwa ufupi Nelson.

Yule Kijana alimsogelea na kumkaba kabali,
“Acha utani hebu nijibu ninachokuuliza”
Alionyesha kughadhabika.
Hata hivyo kijana mwingine alimshika na kumuondoa Nelson
“Wewe Robi mbona huna heshima hebu mtazame mtu huyu mbona anafanana na babayetu?”
Alihoji huyo kijana mwingine aliyekuwa amefanana sawasawa na Robi.
“Baba yenu yuko wapi?”
Aliuliza Nelson.
“Umesema unaitwa Nelson?”
Aliuliza yule kijana mwingine.
Mimi naitwa Fobi, huyu ni ndugu yangu pia Baba yetu anaitwa Nelson, mama yetu nae anaitwa Anitha, hata bibi yetu alikuwa anaitwa Joanitha ila amekufa miezi michache iliyopita.
Maelezo hayo yalimchanganya kichwa zaidi Nelson alianza kuwabembeleza wampeleke nyumbani kwao ili awaone hao wanaoitwa Nelson na Anitha.
Na kwakweli vijana wote waliweka mpira chini na kumpeleka Nelson nyumbani kwao.
Nelsoni Alistaajabu sana alimuona Anitha akiwa amepalalaizi miguu akiwa kwenye kiti cha kutembelea matairi, huku yeye mwenyewe akiwa anamkokota Anitha katika kigari hicho. Tofauti ni kwamba Nelson na Anitha walikuwa wanaelekea uzeeni.
“Wewe Mama ulikuwaje?”
Aliuliza Nelsoni, swali lililo wafanya Robi na Fobi kutikisa kichwa kwa pamoja kama ishara ya kusikitika.
“Gari letu lilimgonga Mtoto, alikuwa akivuka barabara wakati huo mke wangu Anitha ndiye aliyekuwa anaendesha Gari hilo, Mshtuko ule ndio uliomfanya hivi mke wangu”

Nelson alishtuka kisha akauliza
“ni eneo gani hilo?”
Pale vijana wanapochezea mpira kipindi hicho kulikuwa na Barabara ya raundi (Mzunguko)Lakini Rais mpya aliyeingia baada ya yule mama,
Alibadilisha barabara na kujenga Barabara za juu pale pembeni na zile za magari ya mwendo kasi. Baada ya kutamka maneno hayo Nelson alitambua jambo akanyoosha mkono uitazama Saa yake iliyokuwa mkononi na yule mzee pamoja na Anitha walisema kwa pamoja
“ Hizi si ndio Saa tulizowapa Robin a Fobi?”
“Hebu nizione Saa hizo”
Robi na Fobi waliingia chumbani na kuleta zile saa,
Saa zenyewe zilikuwa zimebonyea kidogo na upande wa mkanda zimechubuka,
Mzee akasema
“Hapo ni kwasababu ya lile tatizo la kugonga”
 
MUDA
SEHEMU YA SABA.





TUKIO LA AJABU KWA ANITHA

Wakati Nelson Akiangaika huku Anitha amechanganyikiwa mno, haelewi afanye nini
“Ni wapi hapa mzee wangu?”
Aliuliza Anitha Hata hivyo Mzee yule hakumjibu, mzee alikuwa bize akiudumia watu chai na maandazi.

Anitha alihisi labda Mzee yule amekataa kwasababu hakununua chochote kwake.
Anitha alichomoa noti ya elfu tano na kumpa mzee yule,
“Hii shilingi ya wapi?”
Aliuliza Mzee yule kwa Kiswahili kibovu.
Hata hivyo Anitha hakushangaa kwani rangi yake na mwonekano wake ulimwonyesha kuwa sio Mtanzania wa Asili. Alikuwa Mtu wa Asia hasa kutoka Masati.
Wateja walijikusanya kuona ile fedha ni ya nchi gani kusema kweli ilikuwa ya Tanzania ila ilitofautiana na pesa walio nayo.
“Leta kama hii”
Alisema yule Mzee, Anitha alipoitazama ilikuwa shilingi (50 ya zamani) Wakati Anitha anazidi kushangaa , Gari aina ya landrova iliyopakia Watu na Mizigo kwa pamoja ilisimama na konda alisema “kwa Azizi,Tumefika kwa Azizi Ally”
“Kwa Azizi Ally! Aliongea kwa mshtuko, Anitha Hali ya Hewa ilikuwa nzuri Hapakuwa na joto kali kama Eneo alilokuwepo majumba yalikuwa machache sana, tena ya hali ya chini ni kwa Azizi Ally tu ndiko kulikuwa na nyumba inayoeleweka, hakukuwa na kipande cha Barabara kinachotoka Temeke kuingia Barabara kuu,Barabara ilikuwa moja nayo ilikuwa ya vumbi ila ilionekana vizuri.


Anitha aliitazama Saa yake ya mkononi, ilikuwa inawaka mwanga wa Zambarau na mshale wake ulikuwa ukicheza chezasana kana kwamba imeishiwa moto kwenye Betri toka nipewe miaka nane iliyopita sasa imekuwaje? Anitha alijiuliza kisha akatumia kile kitufe cha ile saa kurudisha ule mshale sehemu yake.
Ajabu nyingine ilitikea alijikuta sebleni kwa Mama Nelson kilichomshangaza zaidi alijiona yeye akicheza Mziki na Mama Nelson.

Alibaki amewatazama huku ameduwaa bado hakuwa anaelewa chochote Mama Nelson na Anitha yule waliacha kucheza Walimgeukia na kumuuliza “Wewe ni nani?”Hakujibu chochote alikuwa amemtazama Nelson aliyekuwa amewatazama wanaocheza mziki usio sikika.
“Mimi ni .......Alishtushwa na Mtu aliyemshika mkono na kumburuta kwa nguvu. Alipo hamaki alimuona Nelson aliyekuwa akimvuta mkono kwa nguvu
“ Mbona sielewi!”
Alilalamika Anitha, Usijari wewe nifuate nimeshaelewa kinachoendelea.”

Alilalamika Nelson huku akimvuta kwa nguvu.
Walienda kwakukimbia mpaka lilipo Gari la Anitha , Anitha aliingia akiwa wa kwanza kwa woga kisha Nelson aliingia na kukaa upande wa pili wa Gari hilo. Anitha Aliwasha lile Gari walipofika mbele kidogo Nelson alitamka Anitha asimame naye Anitha alitii akiegesha lile Gari pembeni kisha waligeuka kutazama nyuma kwa maelezo ya Nelson.

Baada ya mda walimuona Nelson, Anitha na mama Nelson wakija lilipokuwa Gari walipofika walianza kuhamaki kwa kutoiona Gari , Hapo Nelson aliye kwenye Gari alibonyeza kitufe cha saa yake mpaka sehem flani kisha akimwambia Anitha afanye hivyo nae Anitha aliitazama Saa ya Nelson na kuona ule mshale uko wapi.

Alikibonyeza kitufe cha Saa yake na kupeleka mshale mpaka eneo lilelile kama la Nelson. Hapo walijikuta eneo lile walimpungia Mama yao mkono nae mama yao alirudi nyumbani huku akifurahia.
Bado Anitha alikuwa hajaelewa jambo lolote, Anitha aliwasha Gari na kuondoka alipofika Mtoni kwa Azizi Ally alikuta foleni aliamua kuwasha Mziki hata hivyo Nelson alimkataza. Anitha aligeuka na kumtazama lakini alipomuona Nelsoni amekunja uso aliogopa kumkwaza tena, aliamua kuuzima Foleni iliruhusiwa, yeye kabla hajafikiwa “Nelson alimuona mama fulani akikimbia kuvuka Barabara alikuwa amemshika Mtoto mkononi ila Mtoto yule aliogopa Gari lililokuwa limeanza kuitawala Barabara, Aliuachia mkono wa Mama yake na kubaki nyuma , Hapo Nelson alimwambia Anitha “Mtazame mtoto yule ,Mama yake ni waajabu sana amemuacha peke yake”

Anitha alizima breki na kuwasha taa kama ishara ya kumruhusu apite, Mtoto yule alikimbia kwa woga lakini alifanikiwa kuvuka.
Aliushikilia Mtandio wa mama yake kwa nguvu. Baada ya Anitha kujihakikishia hilo aliruhusu Breki na kukanyaga mafuta na gari lilivuka sehemu ile kwa usalama,Anitha aligeuka na kumtazama Nelson , Nelson alikuwa na Tabasamu usoni mwake, Hapo Anitha nae alitabasamu pia Tabasamu lililo tafsiri huba,
Yote hayo yalitokea wakati anapiga kona ya uhasibu kuelekea Barabara ya kwenda Tazara.
Mkono wa Anitha ulikuwa ukiwashwa washwa kuwasha mziki ila alipogeuka kumtazama Nelson na kumuona yuko bize na kusoma alama zilizokuwa kwenye Saa yake aliacha na kuongeza mwendo.
Walifanikiwa kufika salama pale nyumbani kwa Anitha, Anitha alianza kumuita Jeni mfanyakazi wake, Jeni alitoka chumbani kwake kwa furaha na kumkumbatia Anitha “Ulikuwa wapi Dada? Ujue niliogopa siku zote hizo unaniacha peke yangu kazini kwenu wameisha kutafuta kila siku wanakuja hapa” Aliendelea kumwagia maneno bila kupumzika.
Ila kitu kilichomshangaza Anitha ni kuambiwa amemuacha Jeni kwa muda mrefu.

Yeye aliona ni Tukio la Saa chache lakini Jeni aliongea kana kwamba amemaliza mda mrefu, Tena sio wa Saa moja tu bali Siku kadhaa.
Ndipo alipoamua kumuuliza Jeni “Kwani sikuwepo kwa mda gani?” Hata sijui nisemeje Dada ila ni kama aah” Alionyesha kushindwa kuhesabu mda huo.
Hapo Nelson alimuomba amuonyeshe sehemu ya kuwashia Redio. Alipomuonyesha Nelson alisogea na kuwasha Redio hiyo, Mziki mtamu uliokuwa na mwendo wa Taratibu ulianza kusikika
“Tucheze basi”
Nelson alisema huku anajitikisa tikisa. Anitha alianza na Nelson alimfuatisha na hiyo ilikuwa Burudani ya bure kwa Jeni aliyekuwa amemzoea Anitha kwa staili zake.
Wakati wakiendelea kucheza taratibu Nelson alisema
“kuna kitu hujagundua bado”
“Kitu gani?
Aliuliza Anitha.
Baada ya kumkosakosa Mtoto mara ya kwanza ulijikuta wapi?
“Hata sielewi watu wenyewe haweleweki mavazi yao, hakukuwa na nyumba wala Barabara ya lami, ila nilisikia wakisema et kwa Azizi Ally! Alifafanua kwa mshangao Anitha.
“Bila shaka wewe ulirudi nyuma Anitha”
“Nilirudi nyuma?
Unamaanisha nini Nelson”
“Ndio! Wakati wewe unasema ulikuwa huko usipopafahamu, Mimi nilienda mbali kabisa, Mbele kabisa ya hapa tulipo ila Nyumba ilikuwa hii hii.
Wewe utakuwa na watoto mapacha wanaofanana sana. Hilo nililiona.”

Nelson alisita kumwambia kuwa kuwa ndiye atakuwa Baba wa wa Watoto hao. Aliziona wazi hisia za Anitha , hivyo kama angesema jambo hilo lingemfanya hashindwe kutimiza jambo Jipya lililokuwa akilini mwake.
“Sasa hilo liliwezekanaje?
Aah, halafu ulimuona Baba wa Watoto hao?
“Anitha aliendeleza maswali”
“Itazame Saa yako Anitha!”
Anitha alinyanyua mkono wake na kuitazama ilikuwa ikihesabu kawaida mda wake, aligeuza kichwa na kutazama iliyokuwa mkononi mwa Nelson, nayo vile vile, ilikuwa kama yake.
“Hii ndiyo inayofanya mambo yote, Mimi nilienda kununua Saa, Tukio flani lilitukia na kila kitu kilisimama, ila saa hii pekee ndio iliendelea kehesabu Wakati, Wewe hiyo uliipataje?
Aliuliza Nelson huku akiutazama uso wa Anitha uliokuwa umegubikwa na mshangao.
“Nilipewa Saa hii miaka nane ilyopita, Nilikuwa nimelazwa pale Hospitali ya Misseny, kipindi kile iliitwa Bunazi nadhani na sasa hivi inaitwa hivyo kama sijakosea, Daktari mmoja wa kiume ndiye aliyenipata Saa hii, Tena nayakumbuka maneno yake , alisema “Kati ya vitu ninavyopaswa kuvitunza Maishani mwangu ni Saa hii”
Tena aliongeza kuwa “Nikijua kuitumia Saa hii maisha yangu yatabadilika, tena nitakuwa na uwezo wa kufanya chochote nje na ndani ya mda” Ila mimi sikuelewa na wala sijawahi kuelewa maana ya maneno yake, nilichoamua kufanya ni kuitunza vizuri Saa hii.”
Alitua kidogo na kumtazama Nelson aliyekuwa akitetemeka kama mtu mwenye woga.
“Kila ninapoiona saa hii inanikumbusha kuwa nisije nikatamani kujiua tena”
Wakati anaongea maneno hayo machozi yalikuwa yakimlengalenga machoni mwake.
Bila kutarajia Nelsoni alimvuta kwa nguvu na kumkumbatia huku akisema .
“Kumbe ni wewe niliyekuokoa kwa Dakika 28?”
“Na hapo ndipo maisha yangu yalikoharibikia”
Alilalamika Nelson kwa uchungu huku akiruhusu machozi kutiririka Mashavuni.
“Nilijua ni wewe tu niliposikiliza simulizi lile, ni wewe Nelson, Neli ni wewe, nakumbuka unaniuliza , Tatizo nini? Bas niambie nitakusaidia,

Nilikuwa nimejichukia kuliko kitu kingine chochote hapa Duniani, sikutaka niishi tena , ni Daktari yule , Mwenye huruma kama wewe, ndiye aliyenisaidia kurudisha Akili yangu na alinisaidia nijione mwenye thamani tena.”
Wakati anaongea maneno hayo vilio vya kusigina vilikuwa vikisikika pale Sebleni.
Hapo Jeni alitoka chumbani kwake na kuja kuchungulia sebuleni , aliwaona wakilia huku kila mmoja akijaribu kumpoza mwenzake lakini kila mmoja alipouona uchungu uliokuwa usoni mwa mwenzake, kila mmoja ilishindwa kuzuia machozi yake.

Kila mmoja aliachia kifua cha mwenzake na kuanza kumfuta machozi mwenzake.Wakati Nelson
Ana yafuta machozi ya Anitha, Anitha aliachia kicheko chenye mchanganyiko wa kilio, hapo Nelson aliwaza
“Huyu analia ama anacheka?”
Na jambo hilo lilimfanya kuachia kicheko kikavu na wote walikuwa wamerudia furaha yao ya awali.

Jeni alibanwa na kicheko baada ya kuona hali hiyo, Aliziba mdomo wake kwa nguvu na kukimbilia chumbani kwake aliofika aliufungua mlango wa chumba chake ili aweze kucheka , ila kicheko hicho hakikuwepo tena, aliishia Tabasamu tu.
Hata hivyo anitha alisikia mchakato wa mbio za Jeni na kutambua kuwa Jeni alikuwa akiwachungulia.

Sasa naomba unisikilize Anitha uliona nilichokifanya pale Mtangoni nilitumia Saa hizi tulizo nazo kuurudisha Wakati nyuma ,ili nirekebishe makosa tuliyoyafanya mpaka tunamgonga Mtoto na Madhara ya hilo, Wewe ungepalalaizi miguu na kutembelea kigari cha magurudumu Maisha yako yote. Lakini tulirekebisha na ndio maana tulipita salama, na mpaka sasa tuko hapa.

Mimi nafarijika kuuona uwepo wako mbele yangu ukiwa salama salimini. Aliongea hivyo huku akiipapasa miguu ya Anitha, Anitha alihisi mshtuko moyoni mwake na kuanza kucheka cheka bila mpangilio.
“Unajua nini Anitha , Tunapaswa turudi pale hospitalini ulikolazwa ili tukutane na yule Daktari, iliatufafanulie maana ya Saa hizi na kuna madhara yoyote yanayotokana na kuuchezea huu mda?

Anitha alinyanyua mkono wake na kuanza kugusa kile kitufe cha saa ili autafute mwako ule ukiwa hospitalini, hata hivyo Nelson alimzuia
“Unataka kufanya nini wewe?”.
Aliongea kwa kufoka hadi Anitha alishtuka.
“Si umesema turudi nyuma miaka nane?”
Sio hivyo Anitha ukirudisha mda nyuma utakuwa hapa hapa ila wakati wa nyuma, vipi ikiwa kutakuwa hakukuwa na usafiri imara wa kwenda Mkoa wa Kagera tena wilaya ya Missenyi,eeh! Inabidi tusafiri mpaka pale harafu tuweze kurudisha Wakati nyuma”

Anitha alifurahi sana na kuanza kuruka ruka kama mcheza Mziki aina ya Amapiano.
“Nina wazo sasa”
Alisema Anitha aliyekuwa amegubikwa na shangwe, Twende miaka kumi mbele alafu tuone usafiri yawezekana gharama za ndege zimeisha shuka, labda ni kama mabasi au treini za umeme zitakuwa zimeboreshwa, itakuwa rahisi kwetu kufika kule tunakotaka kwenda.”
Nelson alikuwa akimtazama Anitha aliyekuwa akionyesha shauku ya aina yake.
“Nikimzuia tena atajisikia vibaya acha nikubaliane nae tu, ila sio vizuri ni kutumia uwezo ulio nao bila sababu maalumu”.
Nelson alimkubalia na alimuomba waende miaka ishirini mbele , akilini mwake alitaka awaone Fobi na Robi kuna tatizo lolote litawapata, walikubaliana wote na kurudisha mshale wa Saa zao mpaka miaka ishirini ijayo, Rangi yenye mchanganyiko wa zambarau na njano ilianza kuonekana kwenye Saa hiyo.
Walipobonyeza walijikuta kwenye Nyumba kubwa yenye gholofa tatu kwenda juu, madirisha yote yalikuwa vioo vitupu walipotupa macho nje waliona Magari yamepangana yenye rangi za aina mbili tu. Wakati wakiendelea kustaajabu, Walisikia kelele za ugovi kule gholofa ya juu, Mara moja Nelson alimshika mkono Anitha na kuanza kumvuta waelekee huko juu kadri walivyosonga ndivyo kelele zilvyozidi kuongezeka.

Kuingia tu ndani Fobi na Robi walikuwa wamekamatana kabala ya nguvu huku maneno
“Ni wangu! Ulijua ni wa kwangu!”
Yalikuwa yakiendelea.
Huku Baba yao akiwa anajaribu kumnyanyua Mama yao ambaye alikuwa amesukumwa kwa nguvu na kujigonga kwenye sakafu baada ya kuingilia ugomvi ule.

“Mnafanya nini Rafiki zangu?”Mama yenu mnakaribia kumuua nyie bado mnaendelea na ugomvi?
Alitamka Nelson.
“ Ni huyu Robi na ugomvi wake, amempiga Mama yangu”Aliongea kwa kufoka Fobi”Bas achianeni Rafiki zangu” Alizidi kusisitiza Nelson, Hawakumshangaa Nelson wanamfaham ila mshangao ulikuwa kwa Anitha, kwani kitendo cha kujua Mtoto wake atampiga kiasi hicho, kilimfanya afadhaike sana.
“Tatizo nini wanangu”?
Alihoji kwa masikitiko Anitha,Lakini ni kama swali lake lilihamsha asira zao.Kusema kweli hawakuweza kuona utofauti wowote kati yao na mtu huyo anaye waita wanae.
“Wewe ni nani hadi utuhite sie wanao?”
Alihoji Robi,Kusema kweli Robi alikuwa mtu anaye ongozwa na hasira katika maamuzi yake.
“Unataka kuleta balaa linguine Robi”?
Alitamka yule mzee aliye kuwa akijitahidi kumnyanyua mke wake aliye kuwa akiugulia maumivu makali.
“Niambie tatizo lenu tafadhari,tumesikia purukushani zenutukasemezana,ngoja tuwasaidie” Aliongea kwa kusihi Nelson.
Fobi alisogea na kuanza kufafanua kwa hisia yenye uchungu.
“Rafiki zetu, matatizo yote yanasababishwa na Robi,Mimi nina mchumba wangu na tunaendana sana. Ila Robi amekuwa akitumia kigezo cha kufanana na mimi na kumchanganya mchumba wangu. Hii leo nimemuona akimlaghai na kumpeleka katika hoteli bora hapa jijini.Nimemuo nimemuona kwa macho yangu”
Alitua Fobi huku kifua chake kikipanga na kushuka mithili ya gari la Suzuki la kizamani.
“Eti umefanyaje Robi?”
Alihoji kwa hasira Nelson.
“Tatizo siyo mimi ni yeye na mama yake,Wao wamekuwa wakinitenga hawaendezwi na mafanikio yangu.Kila mara wanazungumza wao wenyewe,Ila mimi uniona kama kivuruge tu ninaye wavuruga. Hemu mpigie msichana huyo aje hapa!”Aliamrisha Nelson, na Fobi alinyanyua simu yake na kumpigia . Haikuchukua mda aligonga kengele ya nyumba yao Fobi na Robi walinyanyua sim zao na kuzitazama walimuona msichana huyo akiwa mlangoni, Fobi alibonyeza namba fulani katika simu yake na milango ilifunguka kwa kufuatana na yule msichana aliingia ndani .

Alionesha kustaajabu kwa mshangao mkubwa “Usiogope Dora we sogea tu hapa”
Dora alikuwa akiona kama maajabu ndani ya jumba hilo la kifahari. Alimtazama Fobi na Robi wanavyofanana utadhani ni mtu mmoja, ila jambo lililomshangaza zaidi ni kumuona Nelson na Anitha huku Baba yake Fobi na Mama yake nao wakiwa wamekaa ni umri tu ulio watofautisha.
“Sasa Fobi ni yupi?”
 
Back
Top Bottom