Hadithi: Viumbe Hatari (Dangerous Creatures)

Hadithi: Viumbe Hatari (Dangerous Creatures)

8
“Tafadhali Jimmy usiongee kitu, najua umenikasirikia sana na ndio maana sikutaka hata kukupigia kuwa nakuja, najua una maswali mengi sana kujua hapa nimefikaje, na kwanini nimekuja na kwanini siku ile nilikataa tusionane Arusha, yote haya utayajua tu,” alianza hotuba yake mrembo Angel huku akisogea sehemu aliyokuwepo na kuja kukaa mapajani, hebu fikiria mwenyewe nilikuwa na hali katika muda huo!
“sikia angel, we need to talk before anything, nilimwambia sasa huku nikimtoa pale mapajani,
“unakunywa nini?” nilisema huku nikisogea kwenye friji
“chochote ulicho nacho dear” alijibu
Nilienda kwenye friji na kutoa juisi ya tropical na glass mbili kisha nikaminina tukaanza kunywa pole pole
“umepajuaje hapa?” nilimuuliza huku nikiwa namaanisha
“well, uliniambia mwenyewe unapoishi , kumbuka mwenyewe, nilichokuwa sijui ni namba ya nyumba tu, kwahiyo nipofika niliulizia hapa na kwa bahati nzuri nilimkuta Oscar na ndie aliyenielekeza kwamba unaishi hapa baada ya kumuonyesha picha yako,
“Angel, sijawahi kukuelekeza kwangu , naamini hivyo kuwa mkweli!” nilijaribu kukumbuka kama niliwhi kuongea nae kuhusu sehemu ninayoishi lakini niliona wazi ni kama angel anadanganya,
“siku ile ulipokuja Arusha, sikuwa katika siku nzuri, na tumbo lilikuwa linaniuma sana, nisingeweza kuonana nawe katika hali ile!” alianza Angel
“mhh uongo mwingie huu” nilijaribu kuwaza na nikaona siwezi kufanya lolote kwani inaonekana ni kazi bure tu kubishana na mwanamke aliyejipanga! Kwahiyo nikaamua kumsikiliza tu
“juzi wazazi wamerudi , na mimi nikaona nitumie fursa ya kwena tena Gairo kwa dada, ila nilimpanga tu kuwa nakuja kwako in case wazazi wakiuliza,
Tumalize weekend Pamoja, jumatatu nitarudi Gairo kwa sister”
Alisema Angel
Basi, sikuwa na namna zaidi ya kujiona nina bahati sana, pengine kuliko wanaume wote kwa siku ile, hebu jaribu kufikiria mwanamke unayempenda aje mwenyewe bila hata kutumiwa nauli!! Tena ukae nae zaidi ya siku tatu ! bahati gani hiyo!
Kwa hivi nikamuingiza chumbani Angel ambapo alienda kuoga na kubadili nguo zake tukarudi sebuleni
Kwana nilitoa hoja ya kutoka out ili turudi jioni , lakini ANGEL ALIKATAA!
“mimi nataka tukae ndani tu siku zote hizi, nunua kila kitu tutapika humu baba!” alisema Angel sasa akipekua huko jikoni
“baba, kumbe wewe ni bachela mzoefu, sioni dalili ya kupikwa humu!” alisema angel akicheka
“sikia, jiko lipo kila vyombo vipo tatizo vya kupika ndio hamna, hebu subiri
Nilisema , kisha nikaingia ndani na kutoa kalamu na karatasi
“haya Andika mazaga hapa vitu vya siku tatu”
Nilisema nikimpa Angel, aliandika kisha nikachukua simu yangu na kuagizia vile vitu ambavyo alikua amependekeza,
Baada yah apo tulihamia chumbani kwa ajili ya mechi ya ufunguzi!
Tulikuja kushtuliwa baada ya kampuni ya vyakula mtandao kuwa wameleta zile bidhaa tulizoagiza,
Nilitoka nje na kuingiza mizigo ndani, baadae nikatoa kadi yangu nikakwangua kwenye kifaa chake kwa ajili ya malipo halafu nikarudi ndani kuendelea na kipindi cha pili! Niseme kwamba mtoto Angel alikuwa fundi, kitandani nilijikuta najiwekea mwenyewe ahadi ya kumuoa! Na kummiliki jumla kabisa!
Mpaka saa tatu usiku ndipo tulitoka chumbani na kuelekea jikoni kwa ajili ya kupika. Na kwa hivi naweza kusema hivi ndivyo siku ya kwanza ilivyokwenda baina yanu na Angel,
Kama ungepata nafasi ya kuniuliza kama nilikuwa nimefuta namba yake, hivi karibuni ningeweza kukukatalia kabisa!
Tuliendelea kula bata ile jumamosi na na jumapili yote , safari zilikuwa ni kulekea sehemu tatu tu,
Chumbani, jikoni na sebuleni!
 
9
Jumapili usiku , tayari ilikuwa ni usiku wa kuagana mimi na Angel,
Pamoja na mambo mengine Angel hakutaka mambo mengi, alitaka nimlipie nauli tu, na “nisihangaike sana” kwani yeye tayari ni mpenzi wangu, Pamoja na hayo tulipanga kuendelea na hatua nyingine zaidi huko mbeleni,
Kwakweli sikutaka kabisa Angel arudi, lakini niliona bora aende kwanza ili nijipange vizuri kumchukua mazima.
Jumatatu mapema nilimsindikiza mpaka kwenye ofisi za treni za mwendokasi, akaenda zake na mimi nikaunanisha zangu kazini.
Kwa muda sasa nilikuwa nikiongea na huyo aliyesema ni dada yake huko Gairo na kwa ufupi mambo yalikuwa burudani.
Basi tuliendelea na mapenzi yetu kwa furaha na amani, nilijaribu kumwambia mambo ya kufunga ndoa kama vipi, lakini alisema yeyey hakuwa na mpano huo kwasasa labda baada ya miaka mitano mbele kwani alikuwa na ndoto zake za kutimiza kwanza! Basi niliona haikuwa jambo jema kwa mimi kukazana na mambo ya ndoa, kama nilikua na uhakika wa kunywa maziwa kwanini nilazimishe kufua ng’ombe?
Basi nakumbuka baada ya mwezi mmoja hivi nilianza kumchukulia kama mchumba kabisa na hivi hata alipokuwa akiniuliza mambo ya kazini nilijaribu kumshirikisha baadhi ya mambo ambayo niliona ni ya kawaida tu, ikiwemo jinsi tunavyofanya kazi, nafasi yangu kazini, ratiba ya chakula kazini ,na kadhalika.
Kama mnavyojua ofisi za chakula za taifa mbali na kununua mazao pia ilifanya biashara ya kuuza mazao kwa wafanyabiashara wakubwa na kampuni mbali mbali za ndani na nje ya nchi, kwahiyo ofisi yetu ilikuwa na shughuli nyingi kila wakati, na pale nilipopata nafasi ya kupumzika basi nilichati au kumpigia simu mpenzi wangu angel.
Basi siku hiyo angel aliniomba nimtumie laki tatu alikua na matumizi binafsi na kadi yake ilikuwa imezuliwa kwakuwa hakuifanyia miamala zaidi ya siku 35, na kuwa nikishamtumia atarudisha baadae ,
Basi mimi nilicheka sana na kumwambia hajawahi kula pesa yangu hii ni nafasi pekee kwahiyo asirudishe, akawa anasema atarudisha kweli
Basi niliangalia akiba yangu na nikamtumia laki tatu na nusu, ilikuwa ni majira ya saa tano asubuhi , nikaendelea na kazi huku nikiamini hawezi kurudisha ile pesa! Hata hivyo majira ya jioni saa 9 akanirudishia laki tatu na nusu vile vile!
Hakika nilishangaa sana kitendo kile, kwa mwanamke wa kibongo tena ametoka chuo, sidhani..
“huyu sio dem wa kawaida” nilikuwa najaribu kuwaza kila saa
Niliamua kumpigia simu kumuuliza kwanini amerudisha pesa lakini nae akanijibu kwa kuniuliza maswali vile vile
“kwani wakati nakuomba nilisemaje”?
Kwahiyo sikuwa na jinsi yoyote ya kumjibu nikaishia kucheka tu yakaisha
Ilikuwa ni kawaida yetu kuonana kila baada ya wiki mbili Angel alikuja Dar na mwishowe akaniambia anaerejea ARUSHA kwani anajiandaa na maandalizi ya graduation ya chuo mwezi wa 11 na hivi kuna ratiba za chuo za kufanya na dada yake tayari alishapata msichana wa kazi!
Kwahiyo aliondoka Kwenda ARUSHA, huku tukiahidi kuwasiliana zaidi, na binafsi nilipanga kumfanyia surprise ya kumvalisha pete ya uchumba siku ya mahafali yake! Kwahiyo nilimshirikisha dada yangu na rafiki yangu Isaka,
Dada yangu hakuwa na kipingamizi chochote baada ya kusikia sifa za Angel! Alinihakikishia kwa jinsi alivyowajua wanawake, huyo Angel alikuwa na sifa zote na kwahiyo mdogo wake “nisilaze damu” katika hili jambo!
 
Endelea basi jamani Ila weka ndefu ndefu
 
CK Ebu njoo uendelee jamaniii mwanzo ushaanza arosto
 
10
Miezi ilikatika na hatimaye nilijaribu kufuatilia tarehe ya mahafali chuoni kwa akina Angel, nikaangalia na ratiba zangu za kazini nikaona naweza kuziweka vizuri tu, kwahiyo nikampanga sister Pamoja na Isaka, na dada yake wa Korogwe, tukaona tunaweza kuwa na surprise nzuri kabisa kwa ajili yake, tayari nilishanunua pete nzuri ya kumvalisha, kwa ajili ya kusimika rasmi uchumba wetu, kwa hivi nilimtanguliza Isaka na Dada yake wa korogwe siku moja kabla ili wakaandae mazingira ikiwemo kupata sehemu ambapo tungefanya “after party” mara baada ya Angel kuvaa Joho,
SIKU YA TUKIO
Basi chuo kikuu cha Uhasibu Arusha ambapo zamani kilijulikana kama TIA,
Kilikuwa kimepewa hadhi ya kuwa chuo kikuu cha kimataifa mwaka 2028 ambapo course mbali mbali zilitolewa kwa wanafunzi ndani na nje ya nchi, na kwakuwa walitoa course maalum ya uhasibu wa kidigatili na kwa nchi za afrika mashariki ni chuo hicho pekee ambacho walikuwa na course hiyo, kwa hivi mahafali ya chuo hiyo yalikuwa kama mahafali ya kitaifa kutokana na idadi ya wahitimu kutoka nchi mbali mbali , wahitimu pekee ndio waliokuwa ukumbini lakini waeni waalikwa walikuwa nje ya chuo kwenye uwanja mkubwa wakifuatilia kwa njia ya televisheni zilizokuwa kila pembe ya uwanja huo,
Kila mara nilijaribu kuangaza huko na huko kumuona angel lakini sikuweza, kumuona, kumbuka kulikuwa na umati mkubwa wa watu kwahiyo ingekuwa vigumu kumuona,
Basi tulisubiri mambo ya protokali yamalizike kisha baadae wahitimu walianza kutoka na ilikuwa ni zaidi ya Kariakoo.. kila mtu alikuwa anasubiri mhitimu wake, kuna waliokuja na matarumbeta, ngoma, wengine walishona sare n.k ili mradi kuonyesha tofauti
“haya wapi mwali wetu?” dada yanu Jeni aliniuliza
“soon tutakuwa nae” nilijibu kwa kujiamini
Na tulianza kusogea mpaka sehemu tuliyokuwa tumepaki gari letu na kisha nilichukua simu kumpigia Angel , simu iliita tu bila kupokelewa,
Mwanzo nilidhani ni kwasababu ya kelele za watu na muziki pale ndio maana kwahiyo nilisubiri dakika kadhaa tena lakini majibu yalikuwa yale yale simu haikupokelewa!
“UKO WAPI BABY, NIPO HUKU NYUMA YA JUKWAA KUU LA VIP” Nilituma ujumbe mfupi kwa angel,
“NJOO MPAKA GETI KUU KABISA LA KUTOKA NJE”
Hatimaye alijibu
“tuelekeeni kule kwenye geti kuu!” na sote tuliingia kwenye ari na kuelekea kule ambapo Angel alielekeza ,
Mbele yetu kulikuwa na parking kubwa ya magari na wageni waalikwa walikuwa wanatoka wakiwa na wahitmu wao, na kwa haraka zilikuwa ni purukushani na heka heka za kutoka nje ya chuo
‘yule pale!” nilisema nikiwaonyesha wenzangu
Tayari nilishamuona Angel akiwa amesimama akiongea na watu ambao sikuweza kuwaona vizuri,
Nilishuka na wenzangu na kusogea pale walipokuwa akina Angel
Na ni kama Angel aliwahi kuniona akakimbilia nilipo tukakumbatiana..
“hey usiniambie ushavua joho tayari?” nilimuuliza huku tukishikana mikono na kusogea kule walipokuwa wale wazee
“ah kitambo, ujue jina langu ni A so kwalienda kwa alphabet nilitoka mapema..”
Alisema Angel huku akiwa kama anatazama chini kwa aibu Fulani hivi
Basi tulisogea mpaka pale walipokuwa wale jamaa, Isak na dada yake Pamoja na dada yangu walisogea tu kama kondoo kuelekea kule tulipokuwa tunaelekea mimi na Angel
“walikuwepo wanaume wawili na mama mmoja nilihisi labda wanaweza kuwa wazazi wake Angel ingawa sikuona dalili ya “kufanana” hata kidogo
Tulisalimiana kisha ni kama mzee mmoja alimgeukia Angel ili aeleze kuhusu sisi
“aah ,
Jimmy, this is my Father, na huyu ni Baba yangu mwingine I can say that.. na huyu ni mke wake, mama amebaki nadhani anaandaa sherehe huko nyumbani
“ooh karibu sana Jimmy John Lukas, binti yangu alituambia kidogo kuhusu wewe!”
Alisema , nilistuka sana yule mzee kuweza kutaja majina yangu yote matatu, kitu ambacho hata Angel hajawahi kufanya!
“nashukuru sana mzee , nashukuru sana, huyu ni dada yangu anaitwa JENI, na huyu ni rafiki yangu anaitwa ISAKA , Na yule ni dada yake anaitwa Grace! Nimefurahi kukufahamu mzee!” nilisema huku nikimpa mkono na nilishangaa jinsi mikono yake ilivyokuwa imekomaa na yule mzee aliniangalia machoni bila wasi wasi wowote!
 
11
“ kama mpo tayari basi tunaweza kuondoka nadhani mama mtu atakuwa anasubiri kwa hamu huko” alisema yule mama ambaye wakati wote alikuwa kimya.
“Sisi tumefurahi kumuona baba mzazi wa Angel” isaka hatimaye alisema.
Ilibidi nisogee pembeni na Angel ili kujua ratiba zikoje maana tayari hali ilishaanza kuwa tete
“Jimmy kwa mila za kwetu, hamuwezi kuja kwenye sherehe ya nyumbani, mzee wangu ni mtata sana, hapa kwenyewe amekubali kukusalimia kwasababu ya yule anti pale…”
“Angel, nimekuandalia sherehe sehemu pia , umeona nimekuja na “watu” kwa ajili yako D” nilimkatisha
“hapo ndio unakosea dear, hii ni siku kubwa sana kwangu unadhani wazazi wangu watakubali kirahisi hivyo hii siku ichukuliwe na mtu mwingine?”
Nielewe dear, niruhusu leo wazee wafurahi then soon nakuja Dar kwa ajili yako unifanye utakavyo!
Alisema angel huku akirudi nyuma taratibu kuelekea kule walipokuwepo wazee
“haya wifi, SHEM ISAKA, tutawasiliana ngoja sisi tywahi huko maana bi mkubwa keshaanza kusumbua” alisema Angel na kisha tukapeana mikono na wale wazee wakaingia kwenye gari moja ya kifahari iliyokuwepo mbele yao kisha wakaondoka!
“KAKA HII FAMILIA HII hahahahah! ” alisema dada yangu JENI huku akiangua kicheko
Basi hatukua na jinsi isipokuwa kucheka tu!
“aisee mbona kama MAJINI!” Grace alisema na sasa tukazidi kuangua kicheko,
Nami kukoleza zaidi nikatoa ile pete na sasa kila mtu akacheka mpaka watu wakaanza kutushangaa
“hey kumbukeni kuna ukumbi na vyakula kule tumetoa hela!” hatimaye ISAKA alisema
Na hapo nikawa kama nimekumbuka ,
Kwakuwa bado shughuli zilikuwa zinaendelea kule ndani niliwaomba wanipe dakika kadhaa na mimi nikarudi kule ndani mbio..
Niliangaza huko na huko kutafuta ambacho nilikuwa natafuta! Baada ya kuona nakosa wazo lilinijia na kuingia ndani kabisa ya chuo kule ukumbini ambapo wahitimu walikuwa wamekaa
Niliingia na kukuta wengine wakiwa wanaendelea kupiga picha kwenye mabango mbali mbali , wengine wakiwa wanatoka na baadhi wakiwa wanachati na simu zao..
Haraka niliruka mpaka alipokuwa MC wa ile shughuli nilimnong’oneza sikioni kwa dakika kadhaa kisha akaniruhusu kuchukua kipaza sauti! Tayari niliashaanza kutengeneza hali Fulani tulivu pale ndani kwani hata wale ambao walikuwa wanatoka walisimama kwanza kusilikizia tangazo gani linakuja..
“mabibi na mabwana!
Naitwa Jimmy John Lukas! Nilianza huku nikiwa sijui nasema nini,
“Niko hapa kufurahi na ninyi hivi leo! Hongereni sana kuhitimu! Niko hapa kushare hadithi fupi kuhusu Maisha yangu mimi binafsi na kwanini nimechukua kipaza sauti hiki sasa!
Mwaka 2016 nilikuwa mhitimu wa chuo kikuu , katika nchi mojawapo ya afrika mashariki, wazazi wangu hawakuwa na kipato kikubwa cha kuweza kusafiri kuja katika mahafali yangu, kwa hivi siku ile wakati wenzangu wanashangilia na kuruka ruka na wazazi wangu na ndugu zao mimi nilikuwa peke yanu kwenye pembe moja ya ukumbi nikilia!
Kwahiyo naamini leo kati yenu hapa kuna mtu mmoja au wawili ambaye anapitia hali hiyo leo, nimekuja kumtia moyo! Pengine mwingine hana wazazi kabisa kwa maana sio inshu ya kipato kama ilivyokuwa kwangu, lakini ni kwamba hawezi kabisa kufika, kwa maana hata iweje hawawezi kuwa hapa,
Lakini kuna wale ambao ni inshu ya kipato wameshindwa kufika…
Wakati naendelea na hotuba yangu niliona akina ISAKA wakiingia na sasa walikuwa wamepigwa na mshangao kuniona nahutubia pale “bila sababu za msingi”
“kwahiyo mimi na rafiki zangu tumeandaa kitu kidogo cha kufurahi na watu kama hao siku ya leo,
Ndugu zangu kama hamtajali tunaomba watu watano ambao kwa namna moja ama nyingine hawana ndugu au wazazi au rafiki wa kufurahi nao kwenye siku hii muhimu basi naomba tufuatane nasi sasa” nilisema huku nikiinamisha kichwa kwa staili ya kutoa heshima kwa kijapani.
Na sasa ukumbi mzima walipiga makofi na kushangilia,
“waoo that’s my brother” alisema Isaka huku akinipongeza
Ni kweli walisogea pale tulipokuwepo wadada watatu na mvulana mmoja na badala ya watano walikuwa wanne!
Tulisalimiana nao huku tukiwapa maneno ya Faraja na kisha tukafuata hatua zote muhimu ikiwemo kuacha nakala ya vitambulisho vyetu kwa uongozi wa chuo kisha tukaondoka nao!
Tulifika sehemu ambayo tayari ilikuwa imeandaliwa maalum kwa ajili ya “angel” lakini ikapata “ANGELS” wengine
Kwahiyo tukapata chakula kizuri na hakika kila mmoja wetu alifurahia na kusahau lile Sakata la Angel kwa muda
“sasa tunawaachaje hawa madogo” ISAKA aliuliza
“nadhani tukisema tuwasikilize story zao tutakesha hapa” nilisema
Hivyo tulitoa maneno kadhaa ya kuwashukuru kwa kukubali mualikowetu na wao walifurahi sana hakika siku yao ilikuwa imekwenda vizuri kabisa,
Baada ya kumaliza harakati zote siku ile tulipumzika kisha kesho yake tukaianza safari ya kurudi dar!
 
11
“ kama mpo tayari basi tunaweza kuondoka nadhani mama mtu atakuwa anasubiri kwa hamu huko” alisema yule mama ambaye wakati wote alikuwa kimya.
“Sisi tumefurahi kumuona baba mzazi wa Angel” isaka hatimaye alisema.
Ilibidi nisogee pembeni na Angel ili kujua ratiba zikoje maana tayari hali ilishaanza kuwa tete
“Jimmy kwa mila za kwetu, hamuwezi kuja kwenye sherehe ya nyumbani, mzee wangu ni mtata sana, hapa kwenyewe amekubali kukusalimia kwasababu ya yule anti pale…”
“Angel, nimekuandalia sherehe sehemu pia , umeona nimekuja na “watu” kwa ajili yako D” nilimkatisha
“hapo ndio unakosea dear, hii ni siku kubwa sana kwangu unadhani wazazi wangu watakubali kirahisi hivyo hii siku ichukuliwe na mtu mwingine?”
Nielewe dear, niruhusu leo wazee wafurahi then soon nakuja Dar kwa ajili yako unifanye utakavyo!
Alisema angel huku akirudi nyuma taratibu kuelekea kule walipokuwepo wazee
“haya wifi, SHEM ISAKA, tutawasiliana ngoja sisi tywahi huko maana bi mkubwa keshaanza kusumbua” alisema Angel na kisha tukapeana mikono na wale wazee wakaingia kwenye gari moja ya kifahari iliyokuwepo mbele yao kisha wakaondoka!
“KAKA HII FAMILIA HII hahahahah! ” alisema dada yangu JENI huku akiangua kicheko
Basi hatukua na jinsi isipokuwa kucheka tu!
“aisee mbona kama MAJINI!” Grace alisema na sasa tukazidi kuangua kicheko,
Nami kukoleza zaidi nikatoa ile pete na sasa kila mtu akacheka mpaka watu wakaanza kutushangaa
“hey kumbukeni kuna ukumbi na vyakula kule tumetoa hela!” hatimaye ISAKA alisema
Na hapo nikawa kama nimekumbuka ,
Kwakuwa bado shughuli zilikuwa zinaendelea kule ndani niliwaomba wanipe dakika kadhaa na mimi nikarudi kule ndani mbio..
Niliangaza huko na huko kutafuta ambacho nilikuwa natafuta! Baada ya kuona nakosa wazo lilinijia na kuingia ndani kabisa ya chuo kule ukumbini ambapo wahitimu walikuwa wamekaa
Niliingia na kukuta wengine wakiwa wanaendelea kupiga picha kwenye mabango mbali mbali , wengine wakiwa wanatoka na baadhi wakiwa wanachati na simu zao..
Haraka niliruka mpaka alipokuwa MC wa ile shughuli nilimnong’oneza sikioni kwa dakika kadhaa kisha akaniruhusu kuchukua kipaza sauti! Tayari niliashaanza kutengeneza hali Fulani tulivu pale ndani kwani hata wale ambao walikuwa wanatoka walisimama kwanza kusilikizia tangazo gani linakuja..
“mabibi na mabwana!
Naitwa Jimmy John Lukas! Nilianza huku nikiwa sijui nasema nini,
“Niko hapa kufurahi na ninyi hivi leo! Hongereni sana kuhitimu! Niko hapa kushare hadithi fupi kuhusu Maisha yangu mimi binafsi na kwanini nimechukua kipaza sauti hiki sasa!
Mwaka 2016 nilikuwa mhitimu wa chuo kikuu , katika nchi mojawapo ya afrika mashariki, wazazi wangu hawakuwa na kipato kikubwa cha kuweza kusafiri kuja katika mahafali yangu, kwa hivi siku ile wakati wenzangu wanashangilia na kuruka ruka na wazazi wangu na ndugu zao mimi nilikuwa peke yanu kwenye pembe moja ya ukumbi nikilia!
Kwahiyo naamini leo kati yenu hapa kuna mtu mmoja au wawili ambaye anapitia hali hiyo leo, nimekuja kumtia moyo! Pengine mwingine hana wazazi kabisa kwa maana sio inshu ya kipato kama ilivyokuwa kwangu, lakini ni kwamba hawezi kabisa kufika, kwa maana hata iweje hawawezi kuwa hapa,
Lakini kuna wale ambao ni inshu ya kipato wameshindwa kufika…
Wakati naendelea na hotuba yangu niliona akina ISAKA wakiingia na sasa walikuwa wamepigwa na mshangao kuniona nahutubia pale “bila sababu za msingi”
“kwahiyo mimi na rafiki zangu tumeandaa kitu kidogo cha kufurahi na watu kama hao siku ya leo,
Ndugu zangu kama hamtajali tunaomba watu watano ambao kwa namna moja ama nyingine hawana ndugu au wazazi au rafiki wa kufurahi nao kwenye siku hii muhimu basi naomba tufuatane nasi sasa” nilisema huku nikiinamisha kichwa kwa staili ya kutoa heshima kwa kijapani.
Na sasa ukumbi mzima walipiga makofi na kushangilia,
“waoo that’s my brother” alisema Isaka huku akinipongeza
Ni kweli walisogea pale tulipokuwepo wadada watatu na mvulana mmoja na badala ya watano walikuwa wanne!
Tulisalimiana nao huku tukiwapa maneno ya Faraja na kisha tukafuata hatua zote muhimu ikiwemo kuacha nakala ya vitambulisho vyetu kwa uongozi wa chuo kisha tukaondoka nao!
Tulifika sehemu ambayo tayari ilikuwa imeandaliwa maalum kwa ajili ya “angel” lakini ikapata “ANGELS” wengine
Kwahiyo tukapata chakula kizuri na hakika kila mmoja wetu alifurahia na kusahau lile Sakata la Angel kwa muda
“sasa tunawaachaje hawa madogo” ISAKA aliuliza
“nadhani tukisema tuwasikilize story zao tutakesha hapa” nilisema
Hivyo tulitoa maneno kadhaa ya kuwashukuru kwa kukubali mualikowetu na wao walifurahi sana hakika siku yao ilikuwa imekwenda vizuri kabisa,
Baada ya kumaliza harakati zote siku ile tulipumzika kisha kesho yake tukaianza safari ya kurudi dar!
IPO vizuri
 
Back
Top Bottom