Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Hebu nii'pasue taratiiibu
 
Aisee[emoji39] [emoji39] [emoji39]
 
Dah, foulata aisee dah
 
Bwana Henry alikuwa mtu mwema sana! Hata tungalikuwa watoto wawili naye ni mlezi wetu, nadhani asingaliweza kutufanyia wema zaidi.
 
SURA YA KUMI NA TISA

Baada ya siku kumi kutoka asubuhi ile tuliyookoka kwa namna ya ajabu, tulikuwapo tena nyumbani mwetu katika mji wa Loo; na kwa bahati hatukudhurika kwa mambo yaliyotupata, ila nywele zangu zilikuwa zimeingia mvi zaidi, na Bwana Good hali yake haikuwa kama zamani.

Nadhani alihuzunika sana kwa kifo cha Foulata. Nadhani sina haja kusema hatukuenda tena katika chumba cha hazina za Sulemani.

Lakini baada ya kupumzika kwa muda wa siku mbili tulishuka tena katika shimo lile refu tukitumai kuona kinjia kile tulichotokea, tusikione.

Maana mvua ilikuwa imenyesha na nyayo zetu zilifutika; na tena mteremko wa shimo ulijaa vitundu na vinjia vya wanyama. Ikawa haiwezekani kutambua kinjia kipi tulichotokea.

Siku ile kabla ya kuanza safari yetu ya kurudi Loo tuliingia tena katika Mahali pa Mauti tukatazama kila mahali.

Tukatazama tena ule ukuta wa jabali ulioshuka ukatufungia ndani ya chumba cha hazina, tukazikumbuka hazina zilizomo nyuma ya ukuta huo, na kile kizee cha ajabu kilichobonyezwa na ukuta, na Yule mwanamwali mzuri ambaye amezikwa ndani.

Tuliutazama sana tusione hata dalili ya namna unavyoinuliwa, ingawa tulijaribu sana kwa muda wa saa nzima. Kwa kweli siri yake ilisitirika sana, na kazi yake ilikuwa ya watu mastadi sana.

Mwisho tukaacha kutafuta kwa hasira, lakini naona kuwa hata ungaliinuliwa mbele ya macho yetu, hatungalidhubutu kuingia ndani tena, hatungalidhubutu kukiruka kiwiliwili cha Yule kizee Gagula, ingawa ilikuwa yamkini kupata almasi nyingi kupita kiasi.

Lakini niliona uchungu kuacha mali hiyo yote isiyomfaa mtu. Labda katika zama zijazo, msafiri mmoja atavumbua siri ya jabali hilo, lakini nadhani halitovumbuliwa. Naona kuwa hiyo mali itakaa pamoja na maiti ya Foulata mpaka mwisho wa dunia.


Basi tulianza safari yetu kurudi mji wa Loo. Msomaji atakumbuka kuwa mimi kwa bahati nilijaza mifuko yangu almasi, na kwa hiyo hatukuwa na haki ya kuona uchungu sana, Ijapokuwa nyingine zilitoka mfukoni nilipokuwa nikiporomoka katika shimo, lakini kwa thamani ya almasi ilivyo, nilikuwa na mali ya kutosha kutufanya matajiri sana.

Tulipofika Loo Ignosi alifurahi sana, naye alikuwa hajambo, akijaribu kutengeneza tena nchi yake, maana iliaribika sana katika vile vita.

Alisikiza habari zetu kwa makini na tulipomwambia habari za kufa kwake Gagula alianza kufikiri, akamwita mzee mmoja wa baraza lake, akamuuliza, ‘Wewe mzee sana, sivyo?’

Yule mzee akajibu, ‘Ndiyo. Bwana wangu mfalme! Babu yako na mimi tulizaliwa siku moja.’ Akamuuliza, ‘Niambie, wewe ulipokuwa mdogo ulikijua kile kizee kichawi Gagula?’

Akajibu ‘Nalimjua, mfalme wangu.’ Akamuuliza, ‘Wakati huo alikuwaje? Alikuwa kama wewe ulivyokuwa?’

Akajibu, ‘La, mfalme wangu! Alikuwa kama alivyo sasa na kama alivyokuwa siku za babu yangu kabla ya wakati wangu; alikuwa kizee wa kuchukiza amekauka na kujaa uovu.’

Ignosi akamwambia, ‘Basi, hayupo tena,’ tayari amekufa.’ Yule mzee akasema, Kweli Ewe mfalme! Basi na nchi imeondolewa baa kuu.’

Basi Ignosi akampa ruhusa naye akajibu, ‘Koom! Na kwenda, Ewe mfalme.Koom!’
 
Ingosi akatugeukia akasema, ‘Mnaona, ndungu zangu, huyo alikuwa kizee wa ajabu, nami nimefurahi kuwa amekufa.

Yeye alitaka nyinyi mfe katika pale Mahali pa Mauti na giza, na labda angalivumbua njia ya kuniua mimi vile vile kama alivyopata njia ya kumuua baba yangu na kumweka Twala, mahali pake.

Haya sasa, niambieni zaidi juu ya safari yenu; kwa hakika hapajatokea safari kama hiyo!’ basi nilipokwisha mwambia yote, nilimuuliza namna ya kutoka katika nchi ya Wakukuana.

Nikasema, ‘Na sasa, Ignosi, wakati wa kuagana nawe umewadia tupate kurudi katika nchi tuliyotoka.

Tazama, Ignosi, wewe ulikuja hapa ukitutumikia, na sasa tunakuacha hapa ukiwa mfalme mkubwa. Ikiwa unatushukuru basi tutendee kama ulivyoahidi.

Kutawala kwa haki, kushahi sheria, kutomuua mtu bila sababu ya haki, ndivyo utakavyo stawi. Kesho kutakapo pambazuka, Ignosi, twataka utupe walinzi wataotuongoza kuvuka milima tena. Sivyo mfalme?’

Ignosi akafunika uso wake kwa mikono yake kwa muda, akakaa kimya, kisha akasema, ‘Moyo wangu ni mzito sana; maneno yako yamenitia ufa moyoni, yameupasua katikati.

Nimewafanyia nini, ewe Ndovu na Makumazahn, na Boungwan hata mnataka kuniacha mpweke? Nyinyi mlioniunga mkono siku za vita, mnaniacha katika siku za amani na neema?

Mnataka nini! Je, ni wake? Chagueni katika wanawali wote! Mahali pa kukaa? Tazameni nchi hii ni yenu mpaka upeo wa macho yenu! Nyumba za Kizungu?

Mtawafundisha watu wangu nao watazijenga! Ng’ombe wa chakula na ng’ombe wa maziwa?

Kila mtu aliyeona atakuleteeni ng’ombe dume au ng’ombe jike! Mnataka kuwinda wanyama? Ndovu hawatembei katika mapori yangu?

Viboko hawalali katika matope kingoni mwa mito yangu? Mnataka kufanya vita? Majeshi yangu yanangoja amri zenu. Kama yapo mengine mnayotaka, hayo nitawapa .’

Nikajibu, ‘Sivyo, Ignosi, hatutaki kitu chochote katika vitu vyote ulivyotaja, tunataka kwenda kwetu tu.’ Ignosi akajibu kwa uchungu, ‘Sasa nimefahamu. Mnapenda mawe yale yanayong’aa kuliko mnavyonipenda mimi rafiki yenu.

Tayari mmepata mawe; sasa mnataka mwende kuyauza muwe matajiri kama ilivyo tamaa yenu watu weupe. Kwa ajili hiyo, mawe hayo meupe nayaangamie na aangamie pia atakayeyafuata.

Mauti yatamkabili atakayekwenda katika Mahali pa Mauti ili kuyafuata. Watu weupe, mnayo ruhusa ya kwenda.’

Basi niliweka mkono wangu juu ya mkono wake, nikasema, ‘Ignosi, twambie, wewe ulipotembea tembea katika nchi ya Amazulu, na miongoni mwa watu weupe huko Natal, moyo wako haukutamani nchi ile aliyokusimulia mama yako, yaani nchi ile uliyozaliwa, ulipocheza ulipokuwa mtoto, nchi ambayo ni kwenu?’
 
Akajibu, ‘Ndiyo, nilitamani sana, Makumazahn.’ Nikasema, ‘Ndivyo, Ignosi, mioyo yetu inavyotamani kwetu, nchi yetu.’

Basi, akakaa kimya kwa muda, kisha akasema, ‘Sasa nimefahamu kuwa maneno yako yana maana, nayo ni ya busara kama yalivyo siku zote.

Wale warukao hewani hawapendi kutambaa chini; watu weupe hawapendi kukaa wanavyokaa watu weusi.

Haya, kama lazima mwende, nendeni, mniache na moyo mnyonge, kwa sababu mkisha kwenda mtakuwa kwangu kama mliokufa, maana sipati habari zenu tena.

Infadus, mjomba wangu, atawachukueni na yeye mwenyewe pamoja na jeshi lake atawaongozeni. Nimesikia kuwa ipo njia nyingine ya kuvukia milima, naye atawaonyesheni.

Kwa herini, ndugu zangu, watu weupe mashujaa. Msinitazame tena, maana sina moyo tena.

Tazameni, natoa amri nayo itatangazwa kutoka milima mpaka milima, majina yenu, Ndovu, na Makumazahn, na Bougwan yatakuwa mwiko kutajwa tokea hivi leo, kama yanavyokuwa majina ya wafalme wanaokufa.

Atakayeyataja, atakufa, hivyo ndivyo majina yenu yatakavyo kumbukwa daima katika nchi hii.

‘Nendeni sasa machozi yasije yakanimiminika kama mwanamke.

Kila mkikumbuka mambo yaliyopita kumbukeni namna tulivyopigana bega kwa bega katika vita vikubwa ulivyoviongoza wewe, Makumazahn, au namna wewe ulivyokuwa mwisho wa askari wale waliozunguka upande wakalishinda jeshi la Twala, wewe Bougwan, au namna ulivyokaa katikati ya Wajivu na watu wakaanguka kama mavuno mbele ya shoka lako, wewe Ndovu; na namna ulivyozivunja nguvu za fahali Twala, ukakivunja na kukizika kiburi chake.

Kwaaherini, kwa heri milele, Ndovu na Makumazahn na Bougwan, rafiki zangu.’
Basi Ignosi akatutazama kimya kwa muda kidogo. Kisha akavuta ngezi ile aliyovaa akajifunika kichwa kujificha uso, Tukatoka kimya.

Kulipopambazuka tulitoka mji wa Loo, na rafiki yetu Infadus, naye vile vile moyo wake ulikuwa na huzuni kwa kuagana nasi.

Ingawa tuliondoka mapema sana, njia zote zilijaa watu, wakituamkia kwa maamkio ya kifalme tulipokuwa tukipita, na wanawake wakatushukuru kwa sababu tulimwondoa Twala, wakatutupia maua.

Tulipokuwa tukisafiri, Infadus alitwambia kuwa ipo njia nyingine ya kuvukia milima. Baada ya kusafiri kwa muda wa siku nne mwendo wa taratibu tulifika tena kwenye milima inayopakana na nchi ya Wakukuana na lile jangwa.


Hapa tuliagana na Infadus, askari shujaa, akatutakia mema katika safari yetu, na akawa karibu ya kulia kwa huzuni; akasema, ‘Mabwana zangu, macho yangu hayataona tena watu kama nyinyi.’

Nasi tuliona huzuni kuagana naye. Basi, baada ya kutazama kuwa chakula na maji na kila kitu cha safari yetu kiko sawa, tulipeana mikono na kuagana na Infadus, nasi tukaanza kushuka mlima. Ilikuwa kazi ngumu, lakini tulifika chini salama.

Asubuhi tulianza safari yetu ya taabu ya kuvuka lile jangwa, lakini tulikuwa na maji ya kutosha yaliyochukuliwa na wapagazi watano.
Saa sita, siku ya tatu tulifika kwenye mahali penye majani na miti.
 
Mambo ni moto chief nakuelewaga sanaaa... MzeeBabaa
 
SURA YA ISHIRINI

Na sasa nitasimulia habari zilizo za ajabu kupita zote za safari yetu, nazo labda zitaonyesha namna mambo yanavyotokea kwa ajali. (mambo yote hutokea kwa sababu)

Nilikuwa nikitembea pale tulipofika penye majani na miti, na mara niliona mambo ya kustajabisha. Mbele yangu, kadiri ya hatua ishirini, niliona banda limejengwa chini ya mti.

Nikasema kimoyomoyo, ‘Je, banda hili limekujaje hapa?’ Na mara niliona mtu mweupe anachechemea akitoka bandani amevaa ngozi, naye ana ndevu nyeusi ndefu.

Kwanza nilifikiri kuwa labda nimeshikwa na homa na nimo njozini. Maana, ilikuwa haimkiniki.

Hapana mwindaji aliyepata kufika hapa na hakika hapana mtu aliyepata kujenga nyumba hapa na kupafanya kwake.

Nikatazama tazama, na hapo Bwana Henry na Bwana Good wakaja, nikawaambia, ‘Haya jamani, huyu ni mtu mweupe au labda nimeshikwa na wazimu?’

Bwana Henry akatazama, na Bwana Good akatazama, ndipo Yule mtu mweupe alipotuona akatupigia kelelena akaanza kutujia anachechemea. Alipofika karibu, akaanguka kama kwamba amezimia.

Mara Bwana Henry upesi akamwinamia, akasema, ‘Alhamdulilahi! Ni ndugu yangu George!’

Kusikia kelele, mara mtu mwingine amevaa ngozi vile vile akatoka bandani kachukua bunduki, akatujia mbio.

Aliponiona, akasema, ‘Makumazahn, hunijui, bwana? Mimi ni Jim, mwindaji. Barua ile uliyonipa nimpe bwana wangu ilinipotea nasi tumekaa hapa hapa kwa muda wa miaka miwili.’

Na pale pale akaanguka penye miguu yangu akagaagaa na kupiga kelele kwa furaha. Nikasema, ‘Ee wewe, mzembe! Unastahili kupigwa sana.’

Huku nyuma Yule mtu mweupe akazinduka tena, akasimama, na yeye na Bwana Henry wakashikana mikono kwa nguvu kimya! Hawakuweza kusema hata neno. Ule ugomvi wa zamani ulisahauli kabisa.

Baadaye Bwana Henry akapata kauli akasema, ‘Mpenzi ndugu yangu, nilifikiri kuwa umekwisha kufa. Nimevuka milima ya Sulemani ili kukutafuta, na sasa ninakuona unakaa jangwani kama kunguru!’

Yule mtu akajibu, ‘Mimi nilijaribu kuvuka milima miaka miwili nyuma, lakini nilipofika hapa jabali liliniangukia likanivunja mguu, nami nikakaa hapa, sikuweza kwenda mbele wala kuru nyuma .’

Ndipo nilipokaribia mimi, nikasema, ‘Hujambo, bwana Neville? Unaweza kunikumbuka?’
Akanitazama akasema ‘Kumbe, Quatermain, na wewe Bwana Good vile vile. Ngojeni, rafiki zangu, naona kizunguzungu tena. Mambo haya ni ya ajabu na ya furaha tupu na hasa kwa mtu aliyekwisha kata tamaa.
 
Asante mkuu
 
Siku ile usiku Bwana George alitusimulia habari za safari yake. Kwa uchache ilikuwa hivi: miaka miwili nyuma alitoka mji wa Sitanda kujaribu kufika milima ya Sulemani.

Ile barua niliyompa Jim hakuipata, wala hakupata habari zake mpaka leo hivi. Lakini alisikia habari kwa wenyeji wengine.

Hakujaribu kufika kwenye maziwa ya Sheba bali alifuata njia ile nyingine tuliyorudia sisi, yaani njia iliyo bora kuliko ile iliyoandikwa katika ramani ya mzee Silvestra.

Yeye na Jim walipata taabu nyingi katika jangwa lile, lakini kwa bahati walifika hapa pahali penye majani na maji, ndipo Bwana George alipopatikana na ajali. Siku moja alikuwa kakaa kando ya mto na Jim alipanda juu kujaribu kutafuta asali.

Alipokuwa akifanya hivi, jiwe kubwa lililegea likaporomoka likamwangukia likamvunja mguu vibaya sana.

Basi tokea siku ile hakuweza kwenda vizuri, ikawa hawezi kwenda mbele wala kurudi nyuma, akaazimia kukaa pale pale.

Waliweza kupata chakula cha kutosha, maana walikuwa na risasi nyingi na wanyama huja penye majani na maji yale usiku usiku kila siku. Basi huwapiga wanyama, nakula nyama, na ngozi walizitengeneza ziwe nguo zao.

Basi Bwana George akamaliza kusimulia hadhithi yake, akasema, ‘Basi hapa tumekaa kwa muda wa karibu miaka miwili tukitumai kuwa labda wenyeji watapita na kutusaidia, lakini hawakuja.

Hivi jana usiku tulifanya shauri kuwa Jim aniache hapa naye ajaribu kufika mji wa Sitanda na kupata watu watusaidie. Tulikata shauri kuwa aondoke kesho, lakini hakika sikutumai kuwa ataweza kurudi tena.

Na sasa wewe, ambaye katika watu wote duniani sijakutumainia kabisa, wewe niliyekufikiri kuwa umenisahau na kukaa Uingereza kwa raha, umekuja bila ya kukutarajia.

Ni jambo la ajabu, tena bahati sana.’
Basi alipokwisha kusema, Bwana Henry akaanza kusimulia habari za mambo muhimu katika safari yetu, tukakaa sana usiku ule tukizungumza.

Nikamwonyesha almasi zile nilizopata, akasema, ‘Lo! Kweli mmepata kitu katika taabu zenu, si kama mimi nisiyestahili hata kuhesabiwa sasa.’

Bwana Henry akacheka, akasema, ‘Almasi hizi ni mali ya Quatermain na Good. Hivyo ndivyo tulivyopatana, ya kuwa watagawana mali yoyote tutakayo ipata.’

Basi, maneno yale yalinitia katika fikra, na nilipokwisha kumshauri Bwana Good, nilimwambia Bwana Henry kuwa sisi sote wawili tunataka hata na yeye ashirikiane nasi katika kugawanyana zile almasi, na kama yeye hakubali, basi sehemu yake tutampa ndugu yake aliyevumilia taabu nyingi kuliko sisi katika kujaribu kuzipata.

Mwisho akakubali namna tulivyopatana, lakini Bwana George hakupata habari mpaka baada ya siku nyingi. Basi, hapo nadhani nitamaliza hadithi yangu.

Safari yetu ya kuvuka jangwa mpaka mji wa Sitanda ilikuwa safari ya taabu nyingi, hasa kwa sababu ilitupasa kumsaidi sana Bwana George ambaye mguu wake wa kulia ulikuwa dhaifu sana, na ukamfanyia matata.

Lakini tulivuka, na kusimulia habari zake ingekuwa kukariri hadithi ile niliyokwisha isimulia.

Tulifika Sitanda, tukaona bunduki na vyombo vyetu vingine vipo salama, lakini nadhani Yule mzee aliyekuwa akivitunza hakupenda kutuona tena.

Baada ya miezi sita tulifika kwangu, katika mji wa Durban, na ndipo ninapokaa sasa na kuandika habari hizi. Na sasa nakupeni Kwaherini nyote mliosafiri pamoja nami katika safari hiyo ndefu na ya ajabu kuliko zote nilizosafiri.

MWISHO.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…