Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

SURA YA KUMI NA SITA


Giza lilikuwa limekwisha ingia siku ya tatu tulipofika mahali pa kupiga kambi chini ya ‘Vichawi Vitatu’ yaani ile milima mitatu iliyokuwa mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani.

Katika safari yetu tulikuwa sisi watatu, na Foulata, na Infadus, na Gagula aliyechukuliwa katika machela, ambaye daima tulimsikia akitukana na kuguna, na askari wachache pamoja na viongozi na watumishi.

Siwezi kusahau milima ile namna ilivyokuwa katika mwangaza wa jua la asubuhi; ilikwenda juu sana hata kufika mawinguni.


Tulipotazama juu tuliona Njia Kuu ya Sulemani inakwenda moja kwa moja mpaka kilele cha katikati, mwendo wa kiasi cha saa mbili.


Afadhali nisijaribu kueleza mambo tuliyokutana nayo katika safari hii, msomaji na akisie mwenyewe.

Lakini sasa tunakaribia mashimo yale ya ajabu ambayo ndiyo sababu aliyofia Yule mzee Mreno zama za miaka mia tatu nyuma, na tena Yule mjukuu wake aliyekuwa rafiki yangu, na tena, labda hata na ndugu yake Bwana Henry.


Je, ajali yetu itakuwa ya namna hiyo hiyo? Wao walipatwa na maovu kama alivyosema Yule kichawi Gagula; na sisi je? Tulipokuwa tukienda katika ile njia nzuri sikuweza kujizuia nisiwe na hofu. Na tena nadhani Bwana Good na Bwana Henry vile vile walikuwa na hofu.


Kwa muda wa saa moja na nusu tulikwenda kwa miguu upesi upesi tukivutwa na tamaa, hata wale waliochukua machela waliona shida kufuatana nasi, na Gagula akatoa kichwa chake katika machela akasema, ‘Nendeni pole pole nyinyi watu weupe, nyinyi mtafutao hazina, mbona mnakwenda mbio kuonana na maovu ?’

Akacheka kicheko cha uhabithi kilichochukiza sana na kufanya mwili kunisisimka, na kwa muda kidogo tulipunguza mwendo wetu.


Basi tuliendelea kwenda mpaka tuliona shimo kubwa lililokwenda chini sana mbele yetu, katikati ya mahali tulipo na kile kilele. Nikamuuliza Bwana Henry, ‘Je, unajua shimo hili ni la nini?’

Yeye na Bwana Good wakatikisa vichwa vyao. Nikawaambia, ‘Ni dhahiri kuwa hamjapata kuona mahali panapochimbwa almasi.


Nadhani shimo hili ni shimo la kuchimba almasi.’
Basi tulifuata njia ili tupate kutazama vitu vitatu tulivyoona kutoka mbali kidogo, na tulipokaribia tuliona kuwa ni Wale Watatu Walio Kimya, wanaoogopwa na Wakukuana. Lakini hatukutambua vema ukubwa wao mpaka tulipofika karibu kabisa.


Hapo tuliona masanamu matatu, na baina ya kila sanamu na mwenzake ilikuwa nafasi ya hatua ishirini, na wote wanatazama uwanda wa Loo. Masanamu mawili yalikuwa ya wanaume na lile la tatu lilikuwa la mwanamke.


Basi tulisimama tukatazama sana masanamu yale, na baadaye kidogo Infadus akatujia, akainua mkuki wake kuyaamkia yale masanamu, akatuuliza kama tunataka kuingia Mahali pa Mauti sasa hivi, au tutangoja mpaka kwisha chakula cha mchana.
Afadhali nisijaribu kueleza mambo tuliyokutana nayo katika safari hii, msomaji na akisie mwenyewe. [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Ikiwa tunataka kwenda sasa hivi, basi Gagula yu tayari kutuongoza.

Kwa kuwa ilikuwa saa tano tu, nasi tulikuwa na hamu sana kupatazama mahali penyewe, tulisema kwamba tunataka kwenda sasa hivi, nami nikatoa shauri kama afadhali tuchukue chakula pamoja nasi, maana labda tutakawia katika mahali penyewe.
Basi machela ya Gagula ikaletwa, akatoka ndani.


Huko nyuma Foulata aliweka nyama na vibuyu viwili vya maji katika kikapu. Gagula alipotoka katika machela akacheka na akajikongoja kushika njia. Sisi tulimfuata, mpaka kwenye mlango wa pango.


Hapo Gagula akasimama akatungojea, na hata hivi sasa akicheka kicheko cha uhabithi. Akasema, ‘Sasa watu weupe waliotoka katika nyota, mashujaa wenye busara, mtayari?


Tazama mimi nipo hapa kufanya aliyoniamuru bwana wangu mfalme, yaani kuwaonyesheni hazina na mawe meupe yanayong’aa.Ha!Ha!Ha!’
Nikajibu, ‘Sisi tu tayari.’


Akasema, ‘Vema! Vema! Jipeni moyo mpate kuvumilia mtakayo yaona. Nawe Infadus, utakuja, wewe uliye mhaini bwana wako?’


Infadus akakunja uso kwa hasira, akajibu, ‘La, mimi siji, hayanihusu. Lakini wewe, Gagula, utawale ulimi wako, wangalie pia mabwana zangu.


Mimi ninawatia katika mikono yako, na ukiudhuru hata unywele mmoja, wewe Gagula, utakufa, hata ukiwa mchawi wa namna gani! Umisikia?’


Gagula akajibu, ‘Nasikia Infadus. Lakini usiogope, mimi maisha nafuata amri za mfalme tu. Mimi nimefuata amri za wafalme wengi Infadus, lakini mwisho wao walifuata amri zangu mimi.

Ha!Ha! Nakwenda kutazama nyuso zao mara moja tena, na vile vile nitatazama uso wa Twala. Haya twendeni, twendeni.’


Akachukua kibuyu cha mafuta akatia utambi kama taa. Bwana Good akamuuliza Foulata, ‘Unakuja, Foulata?’ Akajibu, ‘Naogopa, bwana wangu.’ Akasema, ‘Basi nipe kikapu.’

Akajibu, ‘La, bwana wangu, uendako nami nitakwenda.’ Basi Gagula hakungoja zaidi, akaingia katika ule mlango, tukaona kuwa ni kinjia cha kutosha watu wawili kwenda pamoja, tena giza tupu.

Tukamfuata Gagula huku tukiogopa na kutetemeka; tukasikia kishindo cha mbawa, na mara Bwana Good akauliza, ‘Je, nini kile, kitu kimenipiga usoni?’ Nikasema, ‘Haya twendeni, alikuwa ni popo tu.’


Basi tukaenda mbele na tulipokuwa tumekwisha kwenda kadiri ya hatua hamsini tuliona kuwa giza linapungua, na halafu tukajiona katika mahali pa ajabu.
[emoji39] [emoji39]
 
Tumo katika pango kubwa lililo kwenda juu sana, hata kwa juu lilikuwa kadiri ya hatua mia moja. Kutoka pango hilo mapango madogo yaliingia katika mlima.

Basi tulitaka kutazama kila mahali, lakini Gagula hakutupa nafasi, yeye alikwenda mbele mpaka mwisho wa pango kubwa, tukamfuata.

Tulipofika huko tuliona mlango mwingine na Gagula akatugeukia akauliza, ‘Mko tayari kuingia katika Mahali pa Mauti?’

Tukajibu, ‘Haya tu tayari.’
Bwana Henry akasema, Mambo yanaanza kutisha sasa.’ Basi wakanipa nafasi mimi nitangulie, lakini katika roho yangu niliogopa, mpaka Bwana Good aliposema, ‘Haya, twende rafiki, au kiongozi wetu mzuri atatupoteza.’


Basi kuambiwa haya, nikaanza kuingia katika kinjia, na baada ya hatua ishirini hivi, nilijiona katika pango lingine.

Lilikuwa giza kidogo, lakini nilipozoea giza niliona meza ndefu na mwisho wa meza sanamu jeupe kubwa imekaa, na kuzunguka meza masanamu meupe mengine yenye kimo cha mtu.

Tena nikaona katikati sanamu jingine jeusi kidogo, na macho yangu yalipozoea giza nilitambua masanamu yale ni nini, nikageuka nikakimbia kutoka pango lile kadiri nilivyoweza kwenda mbio.


Kwa kawaida mimi siyo muoga sana, wala siogopi mambo ya kishetani, lakini nakiri kuwa niliyoyaona yalinitisha sana, na Bwana Henry asingalinizuia ningetoka pangoni upesi, na nisingekubali kuingia tena, hata kwa almasi zote zilizopo duniani.


Lakini Bwana Henry alinikamata baraabara, na kwa hivyo nilisimama, Lakini, mara na yeye macho yake yalizoea giza na yeye aliona yale niliyoyaona mimi, mara akaniacha akaanza kujifuta jasho usoni.


Bwana Good akashangaa kabisa, na Foulata akamkumbatia huku akilia tu. Gagula tu ndiye aliyecheka sana.

Mambo tuliyoyaona yakawa ya kutisha mno. Maana mwisho wa meza ile ndefu tuliona mifupa ya mtu mrefu sana, urefu wa futi kumi na tano au zaidi, naye ameshika mkuki mkononi, akawa kama sanamu za hayo Mauti yenyewe.

Nikasema, ‘Je, hi! Ni nini?’ Na Bwana Good akaonyesha wale waliokuwa wamekaa mezani akasema, ‘Na hawa ni nani?’


Na Bwana Henry akaonyesha Yule mweusi kidogo akauliza, ‘Na huyu ni nani?’
Gagula akacheka, ‘Hee!Hee!Hee! Maovu yanawajia wote waingiao Mahali pa Mauti. Hee! Hee!Hee!Ha!Ha! Njoo Ndovu, wewe uliye shujaa katika vita, njoo mtazame Yule uliyemuua.’


Na kizee huyu akamshika kwa vidole vyake vyembamba akamwongoza kwenye meza. Sisi tukafuata. Alipofika akasimama akamwonyesha Yule mweusi kidogo, Bwana Henry akastuka akarudi nyuma.

Maana pale mezani maiti yaTwala ilikuwepo, mfalme wa hivi karibuni wa Wakukuana, alikaa na kichwa chake amekipakata.

Na maiti huyo alifunikwa chumvi; tukasikia matone ya maji yakidondoka, tukafahamu kuwa maiti ya Twala inageuzwa kuwa jiwe, yaani kwa dawa iliyomo katika yale maji yanyodondoka.


Tukatazama masanamu yale mengine na tukafahamu Maiti za wafalme wa zamani zimekaa kuzunguka meza, na maiti ya mfalme Twala imekaa juu ya meza imepakata kuwa wale ni maiti wafalme wa zamani, na sasa wamekwisha geuka kuwa masanamu ya mawe kwa ile dawa.

Tukahesabu masanamu ishirini na saba, na ile ya mwisho ilikuwa sanamu ya baba yake Ignosi, na kila moja limegeuka jiwe.

Tukaona kuwa desturi hii ya kuweka maiti za wafalme hapa ni ya zamani sana. Lakini sanamu ile kubwa iliokaa mwisho wa meza tuliona kuwa ni kazi ya mikono ya watu wale waliochonga Wale Watatu Walio Kimya.
Daaah, hii kitu ni kali mazee
 
SURA YA KUMI NA SABA

Wakati ule tulipokuwa tukitazama kila kitu katika Mahali pa Mauti. Gagula alikuwa akifanya kazi yake. Alipanda mezani akaenda karibu na maiti ya Twala, na tena akampitia kila maiti akafanya kama anaongea na maiti.

Alipokwisha fanya hivyo akakaa kitambo kidogo chini ya ile sanamu kubwa akaanza kusema maneno mengi kama anasali.

Basi nikasema, ‘Haya Gagula, tuongoze katika chumba.’ Yule kizee akaondoka, akanitazama usoni, akasema, ‘Mabwana zangu hamuogopi?’
Nikajibu, ‘Tuongoze.’

Akasema, ‘Vema, mabwana zangu.’ Akazunguka nyuma ya ile sanamu ya Mauti, akasema, ‘Chumba kiko hapa. Afadhali uwashe taa kwanza.’


Akasimama ukutani. Basi nikawasha taa nikatazama nione mlango uko wapi, nisiuone; niliona ukuta tu. Gagula akacheka sana akasema, ‘Njia ni ile, mabwana zangu. Ha!Ha!Ha!’ nikasema, ‘Usifanye udamisi.’


Akajibu, ‘Mimi sifanyi udamisi, mabwana zangu, tazameni!’
Akatuonyesha ukuta. Tuliinua taa na alipokuwa akituonyesha, ukuta, kumbe ule mkubwa ulianza kupanda juu na kuingia katika sehemu ya juu ya pango.

Namna alivyo fyatua mtambo ulioinua ukuta ule, sisi hatukuona, maana alifanya hila za kutuficha.


Vile ukuta ulipanda pole pole mpaka ukaingia kabisa, tukaona mlango wa kuingilia katika pango la ndani. Sasa hatukuweza kusubiri tena, maana tupo hapo kwenye hazina, lakini mimi nilianza kuogopa na kutetemeka, sijui wenzangu walikuwaje.


Je, itakuwa ni hila tu, au yale maneno ya Da Silvestre yatatokea kuwa ya kweli? Kweli katika pango zimo hazina nyingi sana hata kutufanya kuwa matajiri kupita wote duniani? Punde tutajua.


Gagula akasema, ‘Haya ingieni nyinyi watu weupe mliotoka katika nyota, lakini kwanza msikilizeni mtumishi wenu, kizee Gagula.


Mawe yanayong’aa mtakayoyaona yalichimbuliwa katika shimo lile kubwa lililo chini ya Watatu Walio Kimya, nayo yaliwekwa hapa sijui na nani.

Mahali hapa pameingiliwa mara moja tu tangu wakati ule walipotoka kwa haraka sana wale walioyaweka mawe haya wakayaacha.

Habari za hazina zilijulikana na watu, maana zimekuwa zikipokezana kizazi baada ya kizazi, lakini hapana aliyejua chumba kiko wapi wala siri ya mlango wa chumba hicho.


Lakini mtu mweupe alitokea, akafika nchi hii kwa kuvuka milima ile, sina habari kama yeye alitoka katika nyota, akapokewa vizuri na mfalme wa wakati ule. Ilisadikika kuwa mwanamke mmoja wa nchi hii alisafiri pamoja naye, na Yule mwanamke akapata kujua siri ya ule mlango.


Basi Yule mtu mweupe aliingia pamoja na Yule mwanamke, wakaona mawe, akajaza mawe katika kifuko kidogo cha ngozi ya mbuzi alichokichukua Yule mwanamke ili kuwekea chakula chao.


Alipokuwa akitoka chumbani akainama achukue jiwe moja jingine lililokuwa kubwa, akalishika mkononi.’

Hapa Gagula akanyamaza . nikamuuliza, ‘Yapi yaliyompata Da Silvestre?’
Yule kizee akashtuka mno, akaniuliza, ‘Umejuaje jina la mtu huyo aliyekufa?

Hapana mtu anayejua yaliyotokea; lakini ilikuwa dhahiri kuwa Yule mtu mweupe aliogopa sana, akatupa kifuko kile cha mawe akatoka chumbani mbio huku kachukua jiwe moja tu.’
Jiwe lenyewe ni lile ulilolifungua wewe Makumazahn, katika paji la uso wa Twala.’ Nikamuuliza, ‘Je, hapana aliyepata kuingia tokea wakati huo?’


Akajibu, ‘Hapana, mabwana zangu. Lakini siri ya mlango ilisitirika na kila mfalme amefungua mlango, lakini hapana aliyethubutu kuingia.


Imesemwa kuwa atakayeingia katika chumba hiki atakufa katika muda wa mwezi mmoja, kama mtu Yule mweupe alivyokufa katika pango mlimani pale ulipomwona wewe Makumazahn, na kwa hivyo wafalme hawaingii.

Ha!Ha! maneno yangu ni ya kweli kabisa.’

Basi kusikia maneno hayo, tukatazamana, ghafula nikaona baridi na kuchafukwa na moyo. Kizee huyu alijuaje habari hizi zote?

Basi akasema, ‘Haya ingieni, mabwana zangu. Ikiwa nimesema kweli mtaona kifuko kile cha ngozi ya mbuzi kilichojaa mawe kimetupwa chini, na ikiwa ni kweli kuwa wale watakaoingia watakufa, basi haya mtapata kuyajua halafu!Ha!Ha!Ha!’
 
Akaingia mlangoni huku kachukua ile taa lakini lazima nikiri kuwa nilisita tena.
Bwana Good akasema, ‘Mimi nitaingia, hiki kishetani hakiwezi kunitisha mimi, ‘Akaingia na Foulata akamfuata na sisi tuliwafuata upesi.


Gagula alisimama mbele kidogo anatungoja, akasema, ‘Tazameni, mabwana zangu, wale walioweka hazina hapa walikimbia kwa haraka, wakafikiri kulinda siri, isijulikane na watu wengine lakini hawakupata nafasi.’

Akatuonyesha mawe makubwa yaliyoletwa tayari kusudi kuziba ile njia.
Basi tulikwenda mbele na Foulata akazidi kuogopa akasema kuwa hawezi kuendelea, basi tukamwambia akae atungojee, tukaweka kikapu karibu naye, tukaendelea.


Tulipokwisha kwenda kadiri ya hatua kumi na tano, tuliona mlango wa mbao umekaa wazi.

Yule aliyekuwa wa mwisho kutoka alikuwa amesahau kuufunga au labda alitishwa na kitu. Na pale mlangoni tuliona kifuko cha ngozi ya mbuzi kimejaa mawe! Gagula alicheka akasema, ‘Hee!Hee!


Watu weupe, niliwaambia nini? Sikusema kuwa Yule mtu weupe alifika hapa, akakimbia kwa haraka, akatupa kile kifuko cha mwanamke? Kitazameni!’

Bwana Good akainama akakiokota, akakiona kizito na akasema, ‘Lo! Kimejaa almasi.’
Bwana Henry akasema, ‘Haya twendeni mbele; nipe taa wewe kizee.’

Akatwaa ile taa akaingia chumbani, na sisi tulimfuata karibu na mara tukajiona katika chumba cha hazina za Sulemani.

Tulipozoea giza tuliona chumba kimechimbwa katika mlima. Tukaona pembe za ndovu nyingi sana, yapata mia nne au mia tano. Pembe hizi peke yake zilikuwa zinatosha kumfanya mtu kuwa tajiri maisha yake yote.

Katika upande mwingine wa chumba tuliona masanduku madogo yaliyo pakwa rangi nyekundu, nikasema, ‘Hizi ni almasi, lete taa.’


Bwana Henry akaleta taa akaiweka karibu na sanduku ambalo mbao zake za juu zilikuwa zimevunjika ; nikaingiza mikono yangu na kuitoa imejaa, si almasi bali sarafu za dhahabu. Basi nilirudisha dhahabu ile nikasema, ‘Hatutarudi mikono mitupu.’


Basi Gagula alitwambia, ‘Mabwana zangu mkitaka almasi na muende pale pembeni mtaona makasha matatu, mawili yametiwa muhuri na moja tayari limefunguliwa.’


Kabla sijatafsiri maneno haya kuwaambia Bwana Henry na Bwana Good, nilifikiri moyoni jinsi alivyopata kujua habari hizo huyu Gagula, yaani ikiwa hapana aliyeingia humu tangu Yule mtu mweupe alipoingia zamani, vizazi vingi nyuma.


Gagula alitambua mawazo yangu, akasema kwa maneno ya kunidharau, ‘Ah! Makumazahn, wewe unayekesha usiku, nyinyi mkaao katika nyota, hamjui kuwa wapo wanaoweza kuona hata ndani ya majabali? Ha!Ha!Ha!’

Lakini Bwana Good alikuwa amekwisha ona zile almasi, akasema, ‘Haya jamani, njooni mtazame.’ Tukaenda kwa haraka, tukaona pembeni makasha matatu, mawili yametiwa muhuri na moja limefunguliwa.

Tukatazama tukaona kuwa zimejaa almasi, nikasema kwa sauti ndogo, ‘Sisi ni matajiri kupita watu wote duniani.’

Bwana Henry akasema, ‘Ndiyo, lakini lazima tuzichukue kwetu kwanza!’ Tukasimama tunatazamana, na mara tukamsikia Gagula anacheka tena; Hee!Hee!Hee! Hayo ndiyo mawe meupe mnayopenda; yachukueni, myale, na myanywe, ha!ha!h!’


Basi hapo nilipomsikia akisema maneno hayo, nikaona ni maneno ya kuchekesha tu! Maana nani aliyesikia mtu akila na akinywa almasi! Nikaanza kucheka, na wenzangu nao wakaanza kucheka vile vile; tukacheka sana.


Gagula akasema, ‘Haya, mabwana zangu, chukueni kadiri mnavyotaka.’
Basi tukazidi kutazama almasi zile huku tumefurahi lakini hatukuona jinsi Gagula alivyotoka pole pole katika kile chumba na sasa anakaribia ule ukuta mkubwa wa jabali.

Mara tukashtuka sana kwa kusikia sauti ya Foulata.’Lo!Lo!Lo! Mwamba unaanguka!’
 
Tukasikia sauti ya Gagula, ‘Niachilie wewe! Niachilie. Na tena sauti ya Foulata, ‘Aa!Aa! Amenichoma kisu!’ lakini sasa tulikuwa tunakwenda mbio na tulipofika karibu, mwangaza wa taa ulituonyesha hivi:

Ukuta ule ukirudi pole pole katika mahali pake, na sasa nafasi iliyobaki kwa chini ni kadiri ya futi tatu tu.
Pale karibu na mwamba Foulata na Gagula wamekamatana wa kiviringishana. Damu ilikuwa ikimtoka Foulata, lakini hakukubali kumwacha kile kichawi kilichokuwa kikipigana kama paka wa mwituni.

Ah! Amemtoka! Foulata ameanguka chini na Gagula anatambaa chini ya ukuta wa jabali kama nyoka. Yupo chini sasa! Lo! Amechelewa! Amechelewa! Ukuta unamponda naye analia kwa maumivu. Chini, chini, ule ukuta mzito unazidi kumponda.

Analia vilio tusivyosikia maishani mwetu, kisha, tulisikia namna ukuta ule ulivyombinya mifupa yake, na mara tukafika kwenye ukuta, tumekwisha chelewa, tumekwisha fungiwa ndani!

Sasa tulimtazama Foulata, tukaona kuwa amechomwa kisu maungoni, naye yumo katika kukata roho.

Akasema, ‘Ah! Bwana wangu, nakufa! Gagula alikuwa akinyatia; sikumwona kwanza maana hakukuwa na mwangaza wa kutosha, na ukuta ukaanza kurudi chini; alirudi nyuma ili atazame mara ya pili, nikamwona, nikamshika, akanichoma kisu, na sasa nakufa!’

Basi akafa, na Bwana Good akasimama na machozi yakimtiririka, akasema, ‘Amekufa! Amekufa!’

Bwana Henry akasema, ‘Basi nawe usijisumbue rafiki, maana karibu utaweza kumfuata alipo. Maana huoni kuwa sisi tumezikwa tungali hai?’

Nadhani mpaka Bwana Henry aliposema maneno hayo, hatukutambua kwa hakika hatari itakayo tupata. Lakini sasa tulifahamu.

Jabali lile lililoshuka chini limekwisha kutufungia ndani ya chumba, na aliyejua siri ya kulifungua amekwisha kufa! Amepondeka chini yake! Kwa muda tulipigwa na mshangao, ikawa kama nguvu zimetuisha, na Bwana Henry akasema, ‘ Haya, tutafute siri ya mtambo unaoendesha huu ukuta, upesi.’


Tukapapasa papasa kila mahali tukijaribu kutafuta huo mtambo hatukuona hata alama. Nikasema, ‘Mimi naona kuwa mtambo haupo upande huu; kama ungekwepo kwa nini Gagula alijitia katika hatari ya kutambaa chini apate kutoka kabla ukuta haujashuka?
Alijaribu kutambaa chini kwa sababu alijua kuwa hapana njia nyingine ya kutoka katika chumba.’


Bwana Henry akasema, ‘Lakini Mungu amemlipa upesi, maana kufa kwake kulikuwa kubaya sana. Hatuwezi kuinua ukuta. Basi naturudi katika chumba cha hazina.’


Tukarudi na tulipokuwa tukimpita Foulata niliona kapu lile lenye chakula na vibuyu vya maji, nikalichukua katika chumba. Tukakaa juu ya makasha yale ya hazina, na Bwana Henry akasema, ‘Tugawanye hicho chakula tukitunze kadiri tunavyoweza.’


Tukakigawanya. Chakula kilikuwa cha kutosha kadiri ya siku mbili tu. Tulipokwisha kula kidogo tukaondoka tukatazama kila mahali kutafuta njia ya kutokea tusiione.


Taa ikaanza kuzimika, na mafuta yalikuwa karibu kwisha. Bwana Henry akauliza, ‘Je, Quatermain, sasa saa ngapi?’ Nikatazama saa yangu nikamwambia kuwa ni saa kumi na mbili, nasi tuliingia pangoni saa tano, nikasema, ‘Infadus atatukumbuka, na kama hatatutafuta leo, basi kesho ni lazima atatutafuta.’


Bwana Henry akajibu, ‘Ndiyo, lakini anaweza kututafuta bure. Yeye hajui siri ya kuinua ukuta huu, wala hana habari ya mlango ulipo.

Ni mtu mmoja tu alijua, naye ni Gagula, na hapana mtu mwingine anayejua. Hata akiuona, yeye hawezi kuvunja jabali lile, hata akileta jeshi zima la Wakukuana.

Rafiki zangu, mimi naona hatuna la kufanya ila kujiweka katika mikono ya Mungu. Kutafuta utajiri kumewaangamiza wengi; nasi tutazidisha hesabu yao.’

Hapo taa ikazidi kuzimika. Na mara moja ilipanda juu tena na tukaona pembe zote na makasha ya almasi naya dhahabu, na kifuko kile cha ngozi, na tukamwona maiti Foulata. Kisha taa ikazimika kabisa.
 
Tukasikia sauti ya Gagula, ‘Niachilie wewe! Niachilie. Na tena sauti ya Foulata, ‘Aa!Aa! Amenichoma kisu!’ lakini sasa tulikuwa tunakwenda mbio na tulipofika karibu, mwangaza wa taa ulituonyesha hivi:

Ukuta ule ukirudi pole pole katika mahali pake, na sasa nafasi iliyobaki kwa chini ni kadiri ya futi tatu tu.
Pale karibu na mwamba Foulata na Gagula wamekamatana wa kiviringishana. Damu ilikuwa ikimtoka Foulata, lakini hakukubali kumwacha kile kichawi kilichokuwa kikipigana kama paka wa mwituni.

Ah! Amemtoka! Foulata ameanguka chini na Gagula anatambaa chini ya ukuta wa jabali kama nyoka. Yupo chini sasa! Lo! Amechelewa! Amechelewa! Ukuta unamponda naye analia kwa maumivu. Chini, chini, ule ukuta mzito unazidi kumponda.

Analia vilio tusivyosikia maishani mwetu, kisha, tulisikia namna ukuta ule ulivyombinya mifupa yake, na mara tukafika kwenye ukuta, tumekwisha chelewa, tumekwisha fungiwa ndani!

Sasa tulimtazama Foulata, tukaona kuwa amechomwa kisu maungoni, naye yumo katika kukata roho.

Akasema, ‘Ah! Bwana wangu, nakufa! Gagula alikuwa akinyatia; sikumwona kwanza maana hakukuwa na mwangaza wa kutosha, na ukuta ukaanza kurudi chini; alirudi nyuma ili atazame mara ya pili, nikamwona, nikamshika, akanichoma kisu, na sasa nakufa!’

Basi akafa, na Bwana Good akasimama na machozi yakimtiririka, akasema, ‘Amekufa! Amekufa!’

Bwana Henry akasema, ‘Basi nawe usijisumbue rafiki, maana karibu utaweza kumfuata alipo. Maana huoni kuwa sisi tumezikwa tungali hai?’

Nadhani mpaka Bwana Henry aliposema maneno hayo, hatukutambua kwa hakika hatari itakayo tupata. Lakini sasa tulifahamu.

Jabali lile lililoshuka chini limekwisha kutufungia ndani ya chumba, na aliyejua siri ya kulifungua amekwisha kufa! Amepondeka chini yake! Kwa muda tulipigwa na mshangao, ikawa kama nguvu zimetuisha, na Bwana Henry akasema, ‘ Haya, tutafute siri ya mtambo unaoendesha huu ukuta, upesi.’


Tukapapasa papasa kila mahali tukijaribu kutafuta huo mtambo hatukuona hata alama. Nikasema, ‘Mimi naona kuwa mtambo haupo upande huu; kama ungekwepo kwa nini Gagula alijitia katika hatari ya kutambaa chini apate kutoka kabla ukuta haujashuka?
Alijaribu kutambaa chini kwa sababu alijua kuwa hapana njia nyingine ya kutoka katika chumba.’


Bwana Henry akasema, ‘Lakini Mungu amemlipa upesi, maana kufa kwake kulikuwa kubaya sana. Hatuwezi kuinua ukuta. Basi naturudi katika chumba cha hazina.’


Tukarudi na tulipokuwa tukimpita Foulata niliona kapu lile lenye chakula na vibuyu vya maji, nikalichukua katika chumba. Tukakaa juu ya makasha yale ya hazina, na Bwana Henry akasema, ‘Tugawanye hicho chakula tukitunze kadiri tunavyoweza.’


Tukakigawanya. Chakula kilikuwa cha kutosha kadiri ya siku mbili tu. Tulipokwisha kula kidogo tukaondoka tukatazama kila mahali kutafuta njia ya kutokea tusiione.


Taa ikaanza kuzimika, na mafuta yalikuwa karibu kwisha. Bwana Henry akauliza, ‘Je, Quatermain, sasa saa ngapi?’ Nikatazama saa yangu nikamwambia kuwa ni saa kumi na mbili, nasi tuliingia pangoni saa tano, nikasema, ‘Infadus atatukumbuka, na kama hatatutafuta leo, basi kesho ni lazima atatutafuta.’


Bwana Henry akajibu, ‘Ndiyo, lakini anaweza kututafuta bure. Yeye hajui siri ya kuinua ukuta huu, wala hana habari ya mlango ulipo.

Ni mtu mmoja tu alijua, naye ni Gagula, na hapana mtu mwingine anayejua. Hata akiuona, yeye hawezi kuvunja jabali lile, hata akileta jeshi zima la Wakukuana.

Rafiki zangu, mimi naona hatuna la kufanya ila kujiweka katika mikono ya Mungu. Kutafuta utajiri kumewaangamiza wengi; nasi tutazidisha hesabu yao.’

Hapo taa ikazidi kuzimika. Na mara moja ilipanda juu tena na tukaona pembe zote na makasha ya almasi naya dhahabu, na kifuko kile cha ngozi, na tukamwona maiti Foulata. Kisha taa ikazimika kabisa.
Barikiwa mkuu
 
Back
Top Bottom