Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Nice

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SURA YA TANO
SAFARI YETU YA JANGWANI
Tulikuwa tumeua ndovu tisa, ikachukua kazi ya siku mbili kutoa pembe zao. Tulipokwisha kuzitoa tulizileta kambini tukachimba shimo chini ya mti mkubwa tukaziweka humo tukafukia shimo. Pembe zilikuwa nzuri kabisa, nadhani sijaona namna yake, maana zile za Yule mkubwa aliyemuua Khiva zilikuwa yapata ratili mia na sabini, kadiri tulivyoweza kukisia. Na marehemu Khiva tulimzika katika kaburi pamoja na sagai lake kama ilivyo desturi, yaani apate kujitetea katika safari yake ndefu kwenda ahera. Siku ya tatu tuliondoka tukafunga safari yetu tukitumaini kuwa tutarudi salama na kuchimbua pembe zetu. Baada ya safari ndefu ya kuchosha tulifika mji wa Sitanda karibu na mto wa Lukanga, na hapo kwa kweli ni mwanzo wa safari yetu. Nakumbuka sana siku ile tuliyofika huko.

Kwa upande wa kulia zilikuwa nyumba chache zimetawanyika pamoja na mazizi ya ng’ombe, na karibu na mto yalikuwapo mashamba ya wenyeji. Kupita mashamba hayo ni mwitu wenye majani marefu umejaa wanyama wa porini. Upande wa kushoto palikuwa jangwa lile kubwa. Hapo paonekana kwamba ni mwisho wa ardhi inayofaa kuoteshwa vitu, siwezi kujua kwa sababu gani, lakini ndivyo ilivyo.

Upande wa chini ya kambi yetu maji yalitiririka katika mto mdogo, na ng’ambo yamto palikuwa mteremko wenye mawe mengi. Huu ndio ulikuwa mteremko ule ule nilipomwona Yule Silvestre akitambaa kwa mikono na magoti miaka ishirini nyuma, yaani aliporudi katika safari yake ya kutafuta Mashimo ya Sulemani. Na kupita mteremko huo ni jangwa lile lisilo na maji, jangwa la ukiwa kabisa.

Tulipo piga kambi yetu ilikuwa ni jioni, na jua lilikuwa likizama, mfano wa mpira mkubwa mwekundu. Mishale ya nuru ya rangi mbali mbali ilitoka ikaenea jangwani. Bwana Henry na mimi tulimwacha Bwana Good atengeneze kambi, nasi tulipanda mteremko ule tukasimama tukitazama jangwa.

Mbingu zilikuwa nyeupe kabisa, na mbali sana tuliweza kuona milima ya Sulemani kama vivuli vikubwa, na wakati mwingine kuona theluji juu ya vilele vyake. Basi nikasema, ‘Kule ndipo upo ukuta unaozunguka Mashimo ya Sulemani, lakini anaejua kama tutaweza kuupita ni Mungu tu.’ Bwana Henry akasema, ‘Nadhani ndugu yangu yupo, na ikiwa yupo basi tutaonana, lazima.’ Nikasema, ‘InshaIlah.’

Tukageuka turudi kambini, nikaona kuwa sisi hatupo pekee yetu, maana nilimwona Umbopa amesimama nyuma yetu na macho yake ameyakodolea milima ile ya mbali. Umbopa alipoona tumemwona, akamwambia Bwana Henry, ‘Je, Inkubu, ile ndiyo nchi unayotaka kufika?’ (na jina la Inkubu ndilo jina walilomwita wenyeji, nadhani maana yake ni ‘ndovu’).

Basi Bwana Henry, akajibu, ‘Ndiyo ile nchi ninayokwenda.’ Umbopa akasema , ‘Inkubu, jangwa ni pan asana, tena hapana maji kabisa, milima ni mirefu sana na vilele vyake vimefunikwa na theluji, na mwanadamu hawezi kukisia kuna nini pale nyuma pale linaposhukia jua; utafika huko kwa njia gani, na kwa nini unataka kwenda?’

Basi nilimtafsiria maneno yale yote, na Bwana Henry akasema, Mwambie ya kuwa na kwenda kumtafuta ndugu yangu aliyenitangulia.’ Umbopa akasema, ‘Inkubu, ni kweli: maana njiani nilikutana na mtu mmoja kabila lake Hottentot akaniambia kuwa miaka miwili nyuma Mzungu mmoja alianza kuvuka jangwa amefuatana na mtumishi mmoja, nao hawakurudi.’ Bwana Henry akamuuliza, ‘Je, waona ya kuwa huyo ni ndugu yangu?’
Umbopa akajibu, ‘La, bwana sijui, ila nilipomuuliza Yule mtu yu wanamna gani, akajibu kuwa ana macho kama yako, lakini ndevu zake ni nyeusi, na tena amefuatana na mtumishi mmoja Mbechuana jina lake Jim.’

Basi nilipotafsiri maneno haya nikasema, ‘ Ndhani ‘ndiye bila shaka, maana mimi namjua Jim tangu zamani.’ Basi Bwana Henry akatikisa kichwa akasema, ‘Mimi nilijua hakika, maana ndugu yangu akitia nia yake kutenda jambo atalitenda. Ikiwa alitaka kuvuka milima ya Sulemani basi amekwisha kuivuka isipokuwa amezuiwa na jambo.

Na kwa hivi lazima tumtafute upande wa pili.’ Umbopa alifahamu Kiingereza ingawa hakukisema ila mara chache, akasema, ‘Inkubu, ni safari ndefu.’ Bwana Henry akajibu, ‘Ndiyo ni mbali, lakini hakuna jambo duniani asiloweza kufanya ‘mwanadamu ikiwa amedhamiria kulifanya.

Umbopa, ikiwa mapenzi yanamvuta mtu naye yu tayari kukosa maisha yake kama kwamba si kitu, hakuna jambo asiloweza kulitenda, hakuna milima asiyoweza kuipanda, hakuna jangwa asiloweza kulivuka, ila mlima mmoja na jangwa moja ambalo wewe hulijui.’ Nilipoyatafsiri maneno hayo , Umbopa alijibu, ‘Maneno makubwa, baba yangu, maneno yanapovuma kweli yanayostahili kusemwa na mwanaume. Umesema kweli, Inkubu baba yangu.

Sikiliza! Maisha ni kitu gani? Ni unyoya, ni mbegu ya majani, ikipeperushwa huko na huko, pengine huzaa na kujizidisha na ikisha kufanya hivyo hufa, pengine huchukuliwa mawinguni. Lakini ikiwa mbegu ni njema na nzito, huenda itasafiri kidogo katika njia ambayo inataka. Ni vizuri kujaribu kusafiri katika njia yako na kushindana na ajali. Kila mtu ameandikiwa kufa. Kama mambo yamezidi, basi hufa upesi kidogo zaidi tu. Baba yangu, nitafuatana nawe kuvuka jangwa na milima mpaka nitakapozuiwa na ajali njiani.’
 
Hapo alinyamaza kimya kidogo, na baadae akaendelea kutoa hotuba yake kama ilivyo desturi ya Wazulu. ‘Maisha ni kitu gani? Niambieni, Ee Wazungu, nyinyi wenye busara, nyinyi mjuao siri za dunia, na dunia ya nyota, na dunia iliyo juu na kuzunguka nyota; nyinyi mpelekao maneno yenu mbali bila kutumia sauti; niambieni, Ee nyinyi Wazungu, siri ya maisha yetu ni nini huenda wapi, hutoka wapi? Hamwezi kunipa jawabu; hamjui! Sikilizeni, nitawaambia. Maisha ni mkono tunaotumia kukinga mauti.

Ni kimulimuli kinachong’aa wakati wa usiku; ni kama pumzi nyeupe za ng’ombe zinazoonekana wakati wa baridi; ni kivuli kidogo kile kinachokimbia katika majani na kupotea katika jua hapo linaposhuka.’

Bwana Henry akasema, ‘Wewe Umbopa ni mtu wa ajabu.’ Umbopa akacheka kidogo akasema, ‘Huoni kuwa wewe na mimi tumefanana sana. Huenda hata na mimi nakwenda kuvuka milima ile ili kumtafuta ndugu yangu!; Nikamtazama sana nikamuuliza, ‘Je, maneno gani hayo, maana yake ni nini? Wewe unajua habari gani ya ile milima? Akajibu, ‘Kidogotu, kidogo sana.

Ni nchi ngeni kabisa, nchi ya uchawi na vitu vizuri; nchi ya watu hodari na miti na vilele vya theluji na njia nyeupe kubwa. Nimesikia habari zake, lakini iko faida gani kusema.? Sasa giza linashuka. Wale watakaoishi kuona wataiona.’ Nikamtazama tena, maana ilinibainika kuwa anajua habari zaidi. Alifahamu ninayoyafikiri, akasema, ‘Usiniogope, Makumazahn, mimi sitegi mitego upate kutegwa.

Mimi sifanyi hila. Ikiwa tutajaaliwa kuvuka milima ile iliyo nyuma ya jua, nitakwambia yote ninayoyajua. Lakini mauti yamekaa juu ya milima ile. Uwe na busara, urudi nyuma, nendeni mkawinde ndovu, mabwana. Nimesema.’

Na bila kusema neon jingine, aliinua sagai lake kutuaga akageuka akarudi kambini, na baadaye tulimkuta huko anasafisha bunduki kama wale watu wengine, Bwana Henry akasema, ‘Mtu huyu wa ajabu sana.’ Nikasema, ‘Ndiyo, nampenda kama simpendi.

Ajua neno lakini hataki kulisema. Lakini ya nini kugombana naye! Safari yetu ni ya ajabu na Mzulu wa ajabu hawezi kuzidisha ajabu yake.’ Siku ya pili tulifanya vitu vyote tayari kuanza safari yetu. Hatukuweza kuchukua bunduki nzito tukaziacha pamoja na vitu vingine kwa wapagazi wetu, tukafanya shauri kuwaacha katika nyumba ya mtu mmoja aliyekaa karibu.

Sikupenda kabisa kuviacha vitu hivyo, maana Yule mtu alivitazama kwa macho ya uroho sana, lakini nilifanya hila. Kwanza nilishindilia bunduki zote, nikaziweka tayari kupigwa, nikamwambia kuwa akizigusa hata kidogo, basi zitalia.

Yeye hakusadiki, na mara ile akashika moja, na kama nilivyomwonya, ikalia, na risasi ikampiga ng’ombe wake mmoja, na vile vile kishindo chake kikamwangusha chini. Akainuka upesi ameshtuka kabisa tena anaona uchungu kwa kupata hasara ya ng’ombe wake, akataka nimlipe, lakini hakutaka kabisa kugusa tena bunduki.

Akasema, ‘Weka shetani wale katika majani ya paa la nyumba au zitatuua sote.’ Nikamwambia kuwa tutakaporudi nikiona kuwa moja imepotea nitamuua yeye na watu wake wote kwa uchawi; na ikiwa haturudi naye akijaribu kuiba bunduki, basi vivuli vyetu vitakuja kumfuata na kuwatia wazimu ng’ombe wake, na kuharibu maziwa yao kabisa, mpaka maisha yake yatakuwa na udhia mtupu! baada ya hayo, akaapa kuwa atazitunza awezavyo.

Basi tukisha kuweka vitu vyetu salama, tulifunga mizigo midogo, tukawachagua Umbopa na Ventvogel wafuatane nasi, tukawa watano, yaani, Bwana Henry, Bwana Good, mimi na Umbopa na Ventvogel. Hatukuchukua vitu vingi, tulipunguza mzigo kadiri tulivyoweza. Tulichukua bunduki tano na bastola tatu, na viriba vya maji vitano, na mablanketi matano, na nyama kavu na shanga za kutoa zawadi, na dawa.

Tena tukachukua visu vyetu na vitu vidogo vidogo kama vile dira na vibiriti na tumbako. Basi vitu hivyo pamoja na nguo tulizokuwa tukivaa ndivyo tulivyo chukua, basi, Siku ya pili hatukufanya kitu, tulipumzika tu, na jua liliposhuka tuliamka tukala, tukafunga vitu vyote tayari, tukalala tena kungojea mbalamwezi.

Yapata saa tatu mwezi ukatoka ukaangaza nchi nzima na mbele yetu tukaona lile jangwa kubwa la kutisha sana. Tukaondoka, na baada ya dakika chache tukawa tayari, lakini hata sasa tulisita kidogo kama ilivyo desturi, ya kibinadamu ikiwa anaanza safari ya hatari. Sisi watu watatu tulisimama pamoja.

Umbopa akasimama mbele kidogo ameshika sagai lake mkononi na bunduki ameweka begani analitazama sana jangwa; na Ventvogel na watu watatu waliokubali kufuatana nasi kuchukua vibuyu vya maji kwa safari ya siku ya kwanza wakasimama pamoja nyuma yetu.

Basi Bwana Henry akasema, ‘Rafiki zangu, sasa tu tayari kuanza safari yetu ya ajabu. Labda hatutafaulu. Lakini sisi ni watu watatu, nasi tutashirikiana katika mambo mema na maovu mpaka mwisho, Na sasa kabla hatujaanza, na tumwombe Mungu anayeumba na kuandika ajali za wanadamu, ambaye tangu zamani amekwisha amuru njia zetu, atuongoze miguu yetu kama apendavyo.’

Akavua kofia yake na Bwana Good pia akavua yake, wakasimama kimya kwa muda. Mimi si mtu wa kuomba, nadhani wawindaji wachache sana huwa wa namna hiyo; wala sijamsikia Bwana Henry akisema namna hiyo lakini nadhani katika moyo wake ni mtu wa dini. Bwana Good vile vile ni mtu wa dini. Lakini siwezi kukumbuka hata siku moja niliyoomba kama nilivyoomba siku ile. Na lazima nikiri kuwa niliona faraja kwa kuomba hivyo.

Maana yaliyo mbele yetu hatukuyajua, na siku zote mambo yanayotisha na yasiyojulikana huvuta wanadamu wamkaribie Muumba wao. Kisha Bwana Henry akasema, ‘ Haya twendeni!’ Tukaanza safari yetu.

Hatukuwa na kiongozi ila milima ya mbali na ile ramani aliyoandika mzee Jose da Silvestre, na kwa kuwa iliandikwa na mtu aliyekuwa akifa juu ya kipande cha kitambaa miaka mia tatu iliyopita, haikuwa kiongozi cha kutia moyo sana.

Lakini hii ndiyo iliyokuwa tama yetu kufaulu. Tukikosa kuliona ziwa lile la maji machafu ambayo alama yake ilionyesha kuwa ni katikati ya jangwa, basi haikosi tutakufa kwa kiu.
Na nilifikiri kuwa bahati ya kuliona haiwezi kutumainiwa sana.

Na hata ikiwa Yule mzee da Silvestre alipima sawasawa na kufanya alama barabara katika ramani, je, baada ya miaka hii yote iliyopita sip engine limekauka,au labda wanyama wa porini wamekwisha kuyakanyaga maji mpaka yamekwisha, au labda yamekwisha kufunikwa na mchanga uliyopeperushwa na upepo? Basi tukaenda, tukaenda, usiku tukikanyaga mchanga na majani yale yaliyosokotana sokotana yalitunasa miguuni, na mchanga uliingia katika viatu vyetu ikawa mara kwa mara kusimama tupate kuutoa.

Basi hivi hivi tulisafiri, na Bwana Good alijaribu kututia moyo kwa kupiga mbinja, lakini sauti yake ilizidi kututia huzuni tu, akaacha. Baadae kidogo jambo lilitokea lililotushtua sana kwanza, lakini kisha lilituchekesha mno. Tulikuwa tukifuatana mmoja mmoja na Bwana Good ametangulia, mara nilisikia sauti yake inafifia kabisa, na tena tukasikia kelele na ghasia, na mkoromo na mguno na vishindo vya miguu. Katika giza tuliweza kuona kama vivuli vinakimbia vimefichwa kidogo kwa mavumbi ya mchanga.


Bwana Henry na mimi tulisimama tumeshangaa; na mshangao wetu ulizidi tulipoona Bwana Good anakwenda mbio kuelekea milima, juu ya kitu tulichodhani kuwa ni kama farasi, akipiga makelele moja kwa moja. Mara tulimwona ametupa mikono juu, tukamsikia akianguka chini kwa kishindo. Ndipo nilipotambua kuna nini; tulikuwa tumetokea kwenye kundi la punda milia waliokuwa wamelala, na Bwana Good alianguka juu ya mgongo wa mmoja ambaye aliamka akamchukua mgongoni mwake.


Nikawaambia watu wetu wasiogope, nikamkimbilia Bwana Good nikichelea kuwa labda ameumia, lakini nilifurahi nilipoona kuwa amekaa kitako juu, ya mchanga ameshangaa na kuogopa sana. Lakini hakuumia, Baada ya hayo tulikwenda bila ya kupatwa na jambo jingine mpaka saa saba hivi, tukapumzika kidogo tukanywa maji kidogo na baada ya kupumzika kwa muda wa nusu, ambaye mpaka sasa alikuwa akituchekesha mara kwa mara alinyamaza tu.


Basi ilipopata saa nane, tukafika kwenye kile kilima kidogo, tumechoka kabisa, na hapo tulikaa na kwa sababu kiu kilituzidi, tulimaliza maji yote. Tena hayakutosha . Basi tukalala, Nilipokuwa katika kusinzia, nilisikia Umbopa akisema peke yake, ‘Kama hatupati maji kesho kabla mwezi haujapanda mawinguni, basi tutakuwa maiti.’ Joto lilikuwa jingi sana, lakini hata hivyo nilitetemeka kama mtu aliyeshikwa na baridi. Maana kutarajia mauti si vizuri, na hasa mauti ya namna ile. Lakini hata fikira za mauti hazikuweza kunizuia nisipatwe na usingizi, nikalala.
 
Safiii. Ngoja niitafune taratibu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chief kama utapata na hadithi ya Alfu lela Ulela tuwekee pia.
 
[emoji39] [emoji39]
 
[emoji119] [emoji119]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…