Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

SURA YA SITA


Ilipopata saa kumi za usiku niliamka baada ya kulala kwa muda wa saa mbili tu, na sasa haja ya kwanza ya mwili, yaani kupumzika, imetimizwa. Maumivu yale mengine ya kiu yalianza kuniudhi, nami sikuweza kupata usingizi tena.

Kabla ya kuamka nilikuwa nikiota ndoto ya kuwa ninaoga katika mto wa maji mazuri yanayopita, na kando ya mto miti mizuri inaota, Kumbe! Niliamka kujiona katika jangwa la ukiwa, kavu kabisa, nakumbuka yale maneno aliyosema Umbopa kuwa kama hatupati maji leo tutakufa kifo kibaya. Hapana mwanadamu aliyeweza kuishi katika nchi ya joto kama lile jangwa bila maji ya kunywa.

Nilikaa nikasugua uso wangu uliokuwa mchafu kwa mikono yangu iliyokuwa mikavu kabisa. Midomo na kope zangu zilikuwa zimegandamana kabisa, nikaweza kuyafumbua macho kwa shida. Mapambazuko yalikuwa karibu, lakini baridi ile tunayozoea kuona asubuhi haikuwapo kabisa, na hewa ilikuwa nzito na nene jinsi nisivyoweza kueleza.
Wenzangu walikuwa wamelala.

Baadaye kukaanza kupambazuka, na ili nipate kusahau kiu yangu, nilitoa kitabu kidogo nilichozoea kuchukua mfukoni mwangu, nikaanza kusoma, na kwa bahati maneno niliyosoma yalikuwa haya: ‘Kijana mzuri ajabu alishika kombe la nakshi, Limejaa maji matamu na safi..’ Niliposoma maneno yale nilimeza mate au kwa kweli nilijaribu kumeza. Hata kufikiri maji kulitaka kunifanya niwe na wazimu.

Hapo nadhani nilishikwa na kichaa kidogo, maana nilianza kucheka, na sauti yangu iliwaamsha wenzangu, na wao wakaanza kusugua nyuso zao chafu, na kufungua midomo na kope zao zilizogandamana.

Mara tulipoamka kabisa tukianza kuzungumza juu ya shida yetu. Hapana hata tone la maji. Tulipindua viriba vyetu tukalamba kingoni, lakini wapi! Vikavu kabisa. Bwana Henry akasema ‘Tusipopata maji tutakufa.’ Nikasema, ‘Kama ile ramani ya Yule mzee ni sahihi, maji yapo karibu tulipo sasa.’ Lakini maneno yangu hayakufariji mtu, maana ilikuwa dhahiri kuwa hatuwezi kuitumai sana ile ramani.

Sasa ikaanza kuwa kweupe kidogo kidogo, tukakaa tunatazamana tu, nikamwona Ventvogel, Yule Hottentot, akiondoka na kuanza kwenda macho chini, na mara akafanya sauti kama ya kukoroma, akaonyesha chini katika mchanga.

Tukashtuka tukasema, ‘Nini, nini? Tukaondoka sote tukamwendea tukitazama chini. Akasema, ‘Wako wanyama wengi kama paa hapa. Tazameni nyayo zao.’ Nikamuuliza, ‘Je, hata kama paa ni wengi hapa hilo linatufaa nini? ‘ Akajibu, ‘Paa hawatembei mbali na maji.’

Nikasema, ‘Kweli, nilisahau, Alhamdulilahi.’ Basi jambo hilo lilitutia uzima tena; ni ajabu sana ya kuwa ‘kama watu wamo katika shida tama ya faraja hata ndogo huwafurahisha. Maana katika usiku wa giza hata nyota moja ni bora kuliko kutokuwa na nyota kabisa.
 
Huko nyuma Ventvogel alikuwa akiinua pua yake akinusa hewa ile yenye moto kama anavyonusa paa mzee anayeshuku hatari. Mara akasema, ‘Nasikia harufu ya maji.’ Ndipo tulipozidi kufurahi, maana tulifahamu namna watu walio zoea kukaa porini wanavyojua kutumia fahamu zao kwa jinsi ya ajabu.

Mara ile jua likatoka likaangaza pote kwa fahari likatufunulia shani iliyotusahaulisha kwa muda ile kiu kali iliyotusumbua. Mbele yetu kadiri ya maili arubaini au hamsini tuliona vilele vya milima viitwavyo, ‘Maziwa ya Sheba’ viking’aa kama fedha katika mianga ya jua la asubuhi, na kila upande, mpaka upeo wa macho kwa maili mia nyingi, mlima wa Sulemani ulienea.

Hapo nilipo sasa siwezi kueleza fahari na utukufu wa shani ile ya ajabu, maana maneno yananipotea kabisa.
Hata kuikumbuka hunitia ububu. Mbele yetu tuliona milima mirefu sana, na nafasi ya katikati ya milima ilikuwa kama mwendo wa maili kumi na mbili.

Milima hiyo ilifanana sana na maziwa ya mwanamke, na mara kwa mara ukungu na kivuli cha chini kilifanana na mwanamke aliyelala amefunikwa kwa namna ya ajabu katika usingizi wake.

Chini ya milima pameinuka kwa taratibu kutoka jangwa, na kutoka mbali huonekana kama juu yake imeviringana na laini; na juu ya kila mlima kiko kilima kidogo kilichofunikwa na theluji na umbo lake ni kama titi la ziwa la mwanamke.

Kwa muda mdogo mianga ya jua ikacheza juu ya theluji na ukungu uliokuwa chini, na mara mawingu na ukungu zikazidi kuwa kama pazia kubwa yakatufichia milima mpaka tukaweza kuona alama tu ya milima ikitokeza katika pazia la mawingu.

Mara yale maziwa ya Sheba yalipotoweka, tukakumbuka tena kiu na taabu yetu. Twaona vilele vya milima viitwavyo ‘Maziwa ya Sheba’ vinang’aa kama fedha.
Ni kweli ya kuwa Ventvogel alisema anasikia harufu ya maji, lakini kila mahali tulipotazama hatukuona hata dalili ya maji. Pote tuliona mchanga mkavu na majani yale ya jangwa mpaka upeo wa macho.

Tulitembea tukazunguka kilima tukitafuta kila upande, lakini hatukuona dalili ya ziwa wala kisima, wala chemchem. Nikasema, ‘wewe Ventvogel, wewe ni mpumbavu kabisa; hapana maji hata kidogo.’ Lakini yeye alizidi kuinua pua na kunusa hewa akasema, ‘Bwana, nasikia harufu ya maji. Najua maji yapo.’ Bwana Henry akapapasa ndevu zake akafikiri, akasema, ‘Labda maji yapo juu ya kilima.’ Bwana Good akasema, ‘Upuuzi tu,! Nani aliyewahi kusikia maji hukaa juu ya kilima!?’


Nikasema, ‘Haya twendeni tukatazame.’ Tukaondoka tukapanda kilimani na Umbopa akatangulia. Mara alisimama kama amepagawa, akaita, ‘Maji! Maji!Maji!’ Tulikwenda kwa haraka, na hakika tuliona maji yako katika shimo. Namna yalivyokuwa katika mahali pale hatukungojea kuulizana, wala hatukusita kwa sababu yalikuwa meusi. Mara tukayarukia tukaanza kunywa.

Lo!jinsi tulivyokunywa! Tulipokwisha kunywa, tukavua nguo zetu zilizokuwa zimekauka kabisa.

Baadaye kidogo tuliondoka tukiwa tume burudika kabisa, tukala nyama kavu, maana kwa muda wa saa ishirini na nne tulishindwa kula, tukashiba. Kisha tulivuta tumbako tukalala mpaka saa sita, kando ya maji yale yaliyotuponya.

Siku ile tulikaa tukapumzika karibu na maji, tukishukuru ya kuwa ilikuwa bahati yetu kuyaona. Maana ingawa si mazuri lakini yalitufaa. Wala hatukumsahau Yule marehemu Silvestre aliyeandika alama sahihi ya mahali pale juu ya kitambaa kile. Ni jambo la ajabu kuwa maji yale yalikaa hivi, nami nadhani kwamba haikosi iko chemchemi chini ambayo maji yake yanapanda juu.

Basi tulipokwisha shiba na kujaza viriba maji, nyoyo zetu ziliburudika, na mwezi ulipotoka tulianza safari yetu tena, usiku ule tulikwenda mwendo wa maili ishirini na tano, lakini hatukuona maji tena, ila mchana tulipata kivuli chini ya vichuguu. Jua lilipotoka tena tukaona Maziwa ya Sheba, na sasa yalikuwa mazuri kupita jana.

Jioni tuliondoka tukashika safari na kulipopambazuka tukaona tumefika kwenye mwinuko wa chini ya Ziwa la kushoto la Sheba, maana ndipo tulipoelekea kutoka mwanzo wa safari. Na sasa maji yametuishia tena, na kiu kimetushika, wala hatukuona mahali pa kupata maji mpaka kufika kwenye theluji ya juu.

Baada ya kupumzika muda wa saa moja, ilitubidi kwenda mbele tena kwa sababu ya kiu, tukazidi kupanda kwa kujikokota mlimani. Ilipopata saa tano tulikuwa tumechoka, nasi hali yetu ilizidi kuwa mbaya. Chini palikuwa kokoto nyingi na miguu yetu ilituuma mno, basi tulikaa chini ya mwamba mmoja tukiuguzana.

Tulipokuwa tumekaa hivi nilimwona Umbopa akiondoka na kujikokota kwenye mahali penye majani kidogo, mara nilimwona yeye aliyekwenda pole pole na kwa taratibu, akirukaruka na kupiga kelele kama mtu aliyeshikwa na wazimu, na huku anatikisa kitu katika mkono wake.

Tuliondoka kwa haraka tukamfuata upesi tulivyoweza, tukitumai kuwa ameona maji. Nikamwita, ‘Je, una nini, Umbopa, una nini?’ Akaitikia, ‘Ee Bwana Makumazahn, ni maji na chakula pia.’ Akazidi kutikisa kile kitu chenye rangi ya kijani kibichi.

Ndipo tulipoona amevumbua kitu gani. Lilikuwa tikiti, nae amegundua konde la matikiti mengi mno, nayo yote yalikuwa mabivu. Mara tukaanza kuyala. Nadhani kila mmoja alikula matikiti sita hivi! Lakini ingawa yalituliza kiu yetu lakini tuliona njaa ya chakula. Tukajaribu kula nyama kavu, lakiniilikuwa tumeikinai.
 
Hapo kwa bahati niliona kundi la ndege wakubwa wanaruka juu, nikaona kuwa ni namna inayofaa kuliwa. Nikatwaa bunduki yangu, na kwa bahati tena nilipiga mmoja. Sasa tukafanya moto kwa majani makavu ya matikiti tukamwoka ndege, tukala chakula namna tusiyokula kwa juma zima.

Tulikula ndege Yule wala hatukusaza kitu ila mifupa ya miguu yake na mdomo wake, tukaona nafuu.

Usiku ule mwezi ulipotoka tukaendelea katika safari yetu. Tulichukua matikiti kadiri tulivyoweza. Tulipopanda kidogo tuliona hewa inaanza kuwa baridi na tuliona raha, maana tulikuwa karibu kufika kwenye theluji, ulibaki mwendo wa maili kumi na mbili tu. Na hapo tuliona matikiti mengine, basi hatukuona taabu ya kiu, na tena tulijua kwamba mara tukifika kwenye theluji shida yetu ya maji itakwisha.

Lakini sasa mlima ulianza kwenda juu sana na kwa hivyo mwendo wetu ulikuwa wa kobe tu. Usiku ule tulikula nyama iliyobaki, na mpaka sasa hatujaona kiumbe chenye uhai ila wale ndege, wala hatujaona chemchemi wala mto wa maji, tukafikiri kuwa ni ajabu , maana theluji ikiisha yeyuka lazima maji yake yateremke mahali.

Lakini baadaye tulijua kuwa mito yote iliteremka kwa upande wa pili wa mlima. Sasa tulianza kufikiri habari za njaa. Tumenusurika kufa kwa kiu, lakini ilionekana kuwa tutakufa kwa njaa. Habari zilizotokea katika siku tatu za taabu zilizofuata zimeandikwa katika kitabu changu kama hivi:

21 Mei: ‘’Tulianza safari saa tano mchana, hewa ilikuwa baridi tukaweza kusafiri mchana huku tumechukua matikiti. Tulijikokota mpaka jioni lakini hatukuona matikiti mengine. Naona kama tumekwisha pita mahali yanapositawi. Hatukuona mnyama yeyote, Jua liliposhuka tulipumzika, na kwa kuwa hatujala kwa muda wa saa nyingi tulisumbuka sana. Na hasa kwa sababu ya baridi ya usiku.’

22 Mei: ‘Mara kulipopambazuka tulianza safari tena, lakini tulikuwa dhaifu sana. Safari ya kutwa ilikuwa mwendo wa maili tano tu.

Tuliona theluji kidogo kidogo tukaila, lakini hatukula kitu kingine, Tulifanya kambi yetu usiku chini ya mwamba. Baridi ni kali mno. Tulikunywa mvinyo kidogo tukajifunika na mablanketi yetu tusife kwa baridi. Sasa tumo taabuni kabisa kwa sababu ya baridi na njaa. Nilifikiri kuwa Ventvogel atakufa usiku.’

23Mei: ‘Mara jua lilipopanda tukashika safari tena, tukaota jua. Sasa tu taabani kabisa kabisa, nadhani ilikuwa ni safari ya mwisho tusipopata chakula.
Mvinyo umebaki kidogo sana. Bwana Good na Bwana Henry na Umbopa wanavumilia namna ya ajabu, lakini Ventvogel yu karibu kufa. Kama walivyo Hottentot wote, yeye hawezi kuvumilia baridi.

Maumivu ya njaa si mabaya sana, lakini naona kama tumbo limekufa ganzi. Wenzangu wasema hayo hayo, sasa tumefika juu yam lima ule unaoungamana na matiti ya Sheba na chini pote ni pazuri ajabu. Nyuma yetu jangwa linalong’aa katika jua limeenea mpaka upeo wa macho, na mbele yetu theluji inaonekana kwenda juu kwa taratibu mpaka kufika kwenye matiti ya Sheba.

Hapana kitu chenye uhai kinachooneka. Mungu atusaidie nahofu ya kuwa hatima yetu ipo karibu.’ Na sasa nitaacha habari zilizoandikwa katika kitabu nishike hadithi yangu tena. Siku ile ya 23 Mei, kutwa tulijikokota mbele tukapanda mwinuko ule wa theluji na mara kwa mara tulilala tukapumzika.

Nadhani watu wangalituona wangalifikiri tu watu wa ajabu, maana tumekonda, tumechoka na tulikuwa tunavuta miguu kwa shida sana, na macho yetu yana dalili ya njaa kali nayo yamekodoka mbele kabisa.


Siku ile tulikwenda maili saba tu, na jua lilipokuwa karibu kushuka tukajiona chini ya titi la kushoto la Sheba, nalo lilikwenda juu sana kama mlima mrefu wa theluji. Ingawa tulikuwa dhaifu sana lakini tuliyoyaona tulihisi ajabu na shani, maana mianga ya jua ilitia theluji rangi ya damu, na juu yake ilikuwa kama taji la theluji nyeupe inayong’aa.

Hapo Bwana Good alisema akitweta, ‘Nadhani tuko karibu na lile pango alilotaja Yule mzee katika hati yake.’ Nikasema, ‘Ndiyo, yaani iwapo pango liko.’ Bwana Henry akasema, ‘Haya, Bwana Quatermain, usiseme hivyo, mimi namwamini sana Yule mzee; hukumbuki namna tulivyoona yale maji? Haikosi tutaona na lile pango upesi.’ Nikasema, ‘Tusipoliona kabla ya giza kuingia, sisi ni maiti, hivi ndivyo ninavyojua mimi.’

Basi tulijivuta tulivyoweza mpaka kufika kwenye shimo na hakika tuliona kuwa ni kinywa cha pango, na haikosi ni pango lile alilotaja Yule mzee Silvestre katika hati yake. Kwa bahati tulifika kwa wakati unaofaa, maana mara tulipofika jua likatua na giza likaingia upesi sana.

Basi tukatambaa tukaingia katika pango na kila mtu alikunywa mvinyo kidogo ukaisha kabisa, tukasongana pamoja tupate kujitia joto, tukajaribu kusahau taabu zetu katika usingizi. Lakini kwa kuwa baridi ilikuwa kali mno hatukuweza kupata usingizi. Basi hapo tulikaa tukiona baridi inatuumiza, kwanza katika vidole, na tena miguu na usoni, Tulisongana pamoja , lakini wapi! Ilikuwa bure tu, maana miili yetu ilikuwa haina joto hata kidogo.

Mara kwa mara mmoja wetu alipata usingizi kwa muda kidogo, lakini mara aliamka tena, nami naona kuwa tungalipatwa na usingizi kamili hatungeamka tena, tungekufa pale pale. Nadhani iliyotuponya ilikuwa ni nia yetu tu.

Ilipokuwa karibu kupambazuka nilimsikia Ventvogel akiugua, na meno yake yaliyokuwa ya kitetemeka kwa baridi yakatulia. Nikafikiri kama ameshikwa na usingizi. Mgongo wake uliokuwa unaniegemea mimi ukazidi kuwa baridi mpaka ukawa kama barafu.

Baadaye kulianza kuwa kweupe kidogo na mishale ya jua ilikuwa kama mishale ya dhahabu ikipenya mote katika pango, imetuangaza, ikamwangaza na Ventvogel aliekaa katikati yetu, amekwisha kufa! Masikini, si ajabu ya kuwa mgongo wake ulikuwa baridi.
Nilipomsikia anaugua alikuwa ana kata roho, na sasa mkavu kabisa. Tulishtuka sana tukaondoka upesi tukamwacha pale amekaa na mikono yake imekumbatia miguu yake..

Ni ajabu namna wanadamu wanavyoona woga katika mahali penye maiti! Baadaye jua lilipanda kukawa kweupe kabisa ndani ya pango.

Mara nilisikia mmoja wetu akipaaza sauti yake kwa hofu, nikageuka nikatazama. Haya ndiyo niliyo yaoona: Pale mwisho wa pango niliona maiti mwingine, amekaa na kichwa chake kimeinamia kifuani,’ na tena nikaona kuwa maiti mwenyewe ni Mzungu. Na wenzangu pia wakamwona, na kuona kuliwatia woga sana. Kila mmoja akatoka pangoni upesi alivyoweza.
 
SURA YA SITA


Ilipopata saa kumi za usiku niliamka baada ya kulala kwa muda wa saa mbili tu, na sasa haja ya kwanza ya mwili, yaani kupumzika, imetimizwa. Maumivu yale mengine ya kiu yalianza kuniudhi, nami sikuweza kupata usingizi tena.

Kabla ya kuamka nilikuwa nikiota ndoto ya kuwa ninaoga katika mto wa maji mazuri yanayopita, na kando ya mto miti mizuri inaota, Kumbe! Niliamka kujiona katika jangwa la ukiwa, kavu kabisa, nakumbuka yale maneno aliyosema Umbopa kuwa kama hatupati maji leo tutakufa kifo kibaya. Hapana mwanadamu aliyeweza kuishi katika nchi ya joto kama lile jangwa bila maji ya kunywa.

Nilikaa nikasugua uso wangu uliokuwa mchafu kwa mikono yangu iliyokuwa mikavu kabisa. Midomo na kope zangu zilikuwa zimegandamana kabisa, nikaweza kuyafumbua macho kwa shida. Mapambazuko yalikuwa karibu, lakini baridi ile tunayozoea kuona asubuhi haikuwapo kabisa, na hewa ilikuwa nzito na nene jinsi nisivyoweza kueleza.
Wenzangu walikuwa wamelala.

Baadaye kukaanza kupambazuka, na ili nipate kusahau kiu yangu, nilitoa kitabu kidogo nilichozoea kuchukua mfukoni mwangu, nikaanza kusoma, na kwa bahati maneno niliyosoma yalikuwa haya: ‘Kijana mzuri ajabu alishika kombe la nakshi, Limejaa maji matamu na safi..’ Niliposoma maneno yale nilimeza mate au kwa kweli nilijaribu kumeza. Hata kufikiri maji kulitaka kunifanya niwe na wazimu.

Hapo nadhani nilishikwa na kichaa kidogo, maana nilianza kucheka, na sauti yangu iliwaamsha wenzangu, na wao wakaanza kusugua nyuso zao chafu, na kufungua midomo na kope zao zilizogandamana.

Mara tulipoamka kabisa tukianza kuzungumza juu ya shida yetu. Hapana hata tone la maji. Tulipindua viriba vyetu tukalamba kingoni, lakini wapi! Vikavu kabisa. Bwana Henry akasema ‘Tusipopata maji tutakufa.’ Nikasema, ‘Kama ile ramani ya Yule mzee ni sahihi, maji yapo karibu tulipo sasa.’ Lakini maneno yangu hayakufariji mtu, maana ilikuwa dhahiri kuwa hatuwezi kuitumai sana ile ramani.

Sasa ikaanza kuwa kweupe kidogo kidogo, tukakaa tunatazamana tu, nikamwona Ventvogel, Yule Hottentot, akiondoka na kuanza kwenda macho chini, na mara akafanya sauti kama ya kukoroma, akaonyesha chini katika mchanga.

Tukashtuka tukasema, ‘Nini, nini? Tukaondoka sote tukamwendea tukitazama chini. Akasema, ‘Wako wanyama wengi kama paa hapa. Tazameni nyayo zao.’ Nikamuuliza, ‘Je, hata kama paa ni wengi hapa hilo linatufaa nini? ‘ Akajibu, ‘Paa hawatembei mbali na maji.’

Nikasema, ‘Kweli, nilisahau, Alhamdulilahi.’ Basi jambo hilo lilitutia uzima tena; ni ajabu sana ya kuwa ‘kama watu wamo katika shida tama ya faraja hata ndogo huwafurahisha. Maana katika usiku wa giza hata nyota moja ni bora kuliko kutokuwa na nyota kabisa.
Ndo naigonga apa taratiibu. Ahsante mkuu
 
Hapo kwa bahati niliona kundi la ndege wakubwa wanaruka juu, nikaona kuwa ni namna inayofaa kuliwa. Nikatwaa bunduki yangu, na kwa bahati tena nilipiga mmoja. Sasa tukafanya moto kwa majani makavu ya matikiti tukamwoka ndege, tukala chakula namna tusiyokula kwa juma zima.

Tulikula ndege Yule wala hatukusaza kitu ila mifupa ya miguu yake na mdomo wake, tukaona nafuu.

Usiku ule mwezi ulipotoka tukaendelea katika safari yetu. Tulichukua matikiti kadiri tulivyoweza. Tulipopanda kidogo tuliona hewa inaanza kuwa baridi na tuliona raha, maana tulikuwa karibu kufika kwenye theluji, ulibaki mwendo wa maili kumi na mbili tu. Na hapo tuliona matikiti mengine, basi hatukuona taabu ya kiu, na tena tulijua kwamba mara tukifika kwenye theluji shida yetu ya maji itakwisha.

Lakini sasa mlima ulianza kwenda juu sana na kwa hivyo mwendo wetu ulikuwa wa kobe tu. Usiku ule tulikula nyama iliyobaki, na mpaka sasa hatujaona kiumbe chenye uhai ila wale ndege, wala hatujaona chemchemi wala mto wa maji, tukafikiri kuwa ni ajabu , maana theluji ikiisha yeyuka lazima maji yake yateremke mahali.

Lakini baadaye tulijua kuwa mito yote iliteremka kwa upande wa pili wa mlima. Sasa tulianza kufikiri habari za njaa. Tumenusurika kufa kwa kiu, lakini ilionekana kuwa tutakufa kwa njaa. Habari zilizotokea katika siku tatu za taabu zilizofuata zimeandikwa katika kitabu changu kama hivi:

21 Mei: ‘’Tulianza safari saa tano mchana, hewa ilikuwa baridi tukaweza kusafiri mchana huku tumechukua matikiti. Tulijikokota mpaka jioni lakini hatukuona matikiti mengine. Naona kama tumekwisha pita mahali yanapositawi. Hatukuona mnyama yeyote, Jua liliposhuka tulipumzika, na kwa kuwa hatujala kwa muda wa saa nyingi tulisumbuka sana. Na hasa kwa sababu ya baridi ya usiku.’

22 Mei: ‘Mara kulipopambazuka tulianza safari tena, lakini tulikuwa dhaifu sana. Safari ya kutwa ilikuwa mwendo wa maili tano tu.

Tuliona theluji kidogo kidogo tukaila, lakini hatukula kitu kingine, Tulifanya kambi yetu usiku chini ya mwamba. Baridi ni kali mno. Tulikunywa mvinyo kidogo tukajifunika na mablanketi yetu tusife kwa baridi. Sasa tumo taabuni kabisa kwa sababu ya baridi na njaa. Nilifikiri kuwa Ventvogel atakufa usiku.’

23Mei: ‘Mara jua lilipopanda tukashika safari tena, tukaota jua. Sasa tu taabani kabisa kabisa, nadhani ilikuwa ni safari ya mwisho tusipopata chakula.
Mvinyo umebaki kidogo sana. Bwana Good na Bwana Henry na Umbopa wanavumilia namna ya ajabu, lakini Ventvogel yu karibu kufa. Kama walivyo Hottentot wote, yeye hawezi kuvumilia baridi.

Maumivu ya njaa si mabaya sana, lakini naona kama tumbo limekufa ganzi. Wenzangu wasema hayo hayo, sasa tumefika juu yam lima ule unaoungamana na matiti ya Sheba na chini pote ni pazuri ajabu. Nyuma yetu jangwa linalong’aa katika jua limeenea mpaka upeo wa macho, na mbele yetu theluji inaonekana kwenda juu kwa taratibu mpaka kufika kwenye matiti ya Sheba.

Hapana kitu chenye uhai kinachooneka. Mungu atusaidie nahofu ya kuwa hatima yetu ipo karibu.’ Na sasa nitaacha habari zilizoandikwa katika kitabu nishike hadithi yangu tena. Siku ile ya 23 Mei, kutwa tulijikokota mbele tukapanda mwinuko ule wa theluji na mara kwa mara tulilala tukapumzika.

Nadhani watu wangalituona wangalifikiri tu watu wa ajabu, maana tumekonda, tumechoka na tulikuwa tunavuta miguu kwa shida sana, na macho yetu yana dalili ya njaa kali nayo yamekodoka mbele kabisa.


Siku ile tulikwenda maili saba tu, na jua lilipokuwa karibu kushuka tukajiona chini ya titi la kushoto la Sheba, nalo lilikwenda juu sana kama mlima mrefu wa theluji. Ingawa tulikuwa dhaifu sana lakini tuliyoyaona tulihisi ajabu na shani, maana mianga ya jua ilitia theluji rangi ya damu, na juu yake ilikuwa kama taji la theluji nyeupe inayong’aa.

Hapo Bwana Good alisema akitweta, ‘Nadhani tuko karibu na lile pango alilotaja Yule mzee katika hati yake.’ Nikasema, ‘Ndiyo, yaani iwapo pango liko.’ Bwana Henry akasema, ‘Haya, Bwana Quatermain, usiseme hivyo, mimi namwamini sana Yule mzee; hukumbuki namna tulivyoona yale maji? Haikosi tutaona na lile pango upesi.’ Nikasema, ‘Tusipoliona kabla ya giza kuingia, sisi ni maiti, hivi ndivyo ninavyojua mimi.’

Basi tulijivuta tulivyoweza mpaka kufika kwenye shimo na hakika tuliona kuwa ni kinywa cha pango, na haikosi ni pango lile alilotaja Yule mzee Silvestre katika hati yake. Kwa bahati tulifika kwa wakati unaofaa, maana mara tulipofika jua likatua na giza likaingia upesi sana.

Basi tukatambaa tukaingia katika pango na kila mtu alikunywa mvinyo kidogo ukaisha kabisa, tukasongana pamoja tupate kujitia joto, tukajaribu kusahau taabu zetu katika usingizi. Lakini kwa kuwa baridi ilikuwa kali mno hatukuweza kupata usingizi. Basi hapo tulikaa tukiona baridi inatuumiza, kwanza katika vidole, na tena miguu na usoni, Tulisongana pamoja , lakini wapi! Ilikuwa bure tu, maana miili yetu ilikuwa haina joto hata kidogo.

Mara kwa mara mmoja wetu alipata usingizi kwa muda kidogo, lakini mara aliamka tena, nami naona kuwa tungalipatwa na usingizi kamili hatungeamka tena, tungekufa pale pale. Nadhani iliyotuponya ilikuwa ni nia yetu tu.

Ilipokuwa karibu kupambazuka nilimsikia Ventvogel akiugua, na meno yake yaliyokuwa ya kitetemeka kwa baridi yakatulia. Nikafikiri kama ameshikwa na usingizi. Mgongo wake uliokuwa unaniegemea mimi ukazidi kuwa baridi mpaka ukawa kama barafu.

Baadaye kulianza kuwa kweupe kidogo na mishale ya jua ilikuwa kama mishale ya dhahabu ikipenya mote katika pango, imetuangaza, ikamwangaza na Ventvogel aliekaa katikati yetu, amekwisha kufa! Masikini, si ajabu ya kuwa mgongo wake ulikuwa baridi.
Nilipomsikia anaugua alikuwa ana kata roho, na sasa mkavu kabisa. Tulishtuka sana tukaondoka upesi tukamwacha pale amekaa na mikono yake imekumbatia miguu yake..

Ni ajabu namna wanadamu wanavyoona woga katika mahali penye maiti! Baadaye jua lilipanda kukawa kweupe kabisa ndani ya pango.

Mara nilisikia mmoja wetu akipaaza sauti yake kwa hofu, nikageuka nikatazama. Haya ndiyo niliyo yaoona: Pale mwisho wa pango niliona maiti mwingine, amekaa na kichwa chake kimeinamia kifuani,’ na tena nikaona kuwa maiti mwenyewe ni Mzungu. Na wenzangu pia wakamwona, na kuona kuliwatia woga sana. Kila mmoja akatoka pangoni upesi alivyoweza.
Daah, hii kitu ni kali.

Wabeja sana mkuu blackstarline
 
Hii hadithi mara ya kwanza nimepata kuisikia katika wimbo wa Kwanza Unit.

Kwanza Unit-Msafiri.

Nilitafuta kitabu nikafeli kukipata.

Shukran sana,

Nipo naifatilia Nukta mpaka Nukta.

Endelea kuweka Utamu wa Mashimo ya Mfalme Suleiman.

Safi sana kamanda wangu,Tupo pamoja.
 
Hii hadithi mara ya kwanza nimepata kuisikia katika wimbo wa Kwanza Unit.

Kwanza Unit-Msafiri.

Nilitafuta kitabu nikafeli kukipata.

Shukran sana,

Nipo naifatilia Nukta mpaka Nukta.

Endelea kuweka Utamu wa Mashimo ya Mfalme Suleiman.

Safi sana kamanda wangu,Tupo pamoja.
Poa mkuu
 
SURA YA SABA


Tulipofika nje ya pango tulisimama tumepumbaa. Bwana Henry akasema, ‘Mimi nitaingia ndani tena.’ Bwana Good akamuuliza kwa nini? naye akajibu, ‘Kwa sababu labda Yule tuliyemwona ndiye tunayemtafuta labda ni ndugu yangu.’

Basi tukaingia ndani tena ili tushuhudie. Tulipoingia kwanza hatukuweza kuona vizuri sababu ya kiwi cha macho kilichofanywa na mwangaza wa nje lakini tuliposimama mwisho wa pango niliona maiti mwingine amekaa, kichwa chake kimeinamia kifuani. Baada ya kuzoea giza tulimkaribia Yule maiti, na Bwana Henry akapiga magoti karibu naye akamtazama usoni, akasema, ‘Namshukuru Mungu, huyu si ndugu yangu.’

Basi ndipo nilipomkaribia mimi nikamtazama. Huyu marehemu alikuwa mtu mrefu, mtu mzima na pua ya upanga, na nywele zake zilianza kuwa na mvi, na alikuwa na masharubu marefu.

Ngozi yake ilikuwa imekauka kabisa nayo imetanda juu ya mifupa yake. Alikuwa hana nguo ila shingoni alifungwa msalaba wa pembe. Nikasema, ‘Marehemu huyu alikuwa nani?’

Bwana Good akasema, ‘Je, huwezi kubahatisha?’ Nikatikisa kichwa, akasema, “Huyo si mzee Jose da Silvestre’ Nikasema, ‘Haiwezekani, maana yeye alikufa miaka mia tatu iliyopita.’ Bwana Good akajibu, ‘Na hapa kuna nini cha kuzuia asikae bila kuoza kwa miaka elfu tatu? Maana ikiwa ni baridi mno, nyama inaweza kukaa bila kuoza kwa muda mrefu sana.

Na hapa joto la jua haliingii kabisa; Wala wanyama hawaji kumrarua na kumharibu. Haikosi Yule mtumishi wake aliyemtaja katika maandishi yake alimvua nguo na kumwacha hapa.

Tazama, huu ndiyo mfupa aliotumia kama kalamu kuandikia ile ramani yake.’ Akainama chini akaokota mfupa mdogo uliopasuliwa ncha. Tukatazama tumeshangaa, na katika kutazama ajabu hii tulisahau shida na taabu zetu.

Bwana Henry akasema, ‘Ndiyo kweli, na hapa ndipo mahali alipotoa wino wake.’ Akaonyesha kijeraha kidogo katika mkono wa Yule maiti.

Basi sasa hatukuwa na shaka tena, maana tumekwisha shuhudia. ‘’Huyu maiti ni Yule mtu aliyeandika yale maelezo vizazi kumi nyuma ambayo yametuongoza hapa. Huu mkononi mwangu ni mfupa ule aliotumia kuwa kalamu, na hapo shingoni upo msalaba alioubusu wakati alipokuwa akifa.’’

Baadaye kidogo Bwana Henry alisema, ‘Haya twendeni, lakini ngoja kwanza nimpe mwenzie akae pamoja naye.’ Akamwinua Yule marehemu Ventvogel akamweka karibu na maiti ya Yule mzee, kisha akainama akatoa ule msalaba katika shingo ya Yule mzee kuwa ni ukumbusho. Nadhani anao hata sasa.

Mimi nilichukua ule mfupa, ninao hata sasa napengine nautumia kama kalamu, Basi tuliwaacha wale maiti wawili pamoja, walinde zamu katikati ya theluji inayodumu milele, tukatoka katika pango na kuingia katika mwangaza wa jua.

Tukaendelea katika safari yetu tukiwaza mioyoni ni baada ya saa ngapi na sisi tutakuwa kama wao walivyo sasa. Tulipokwisha kwenda yapata nusu saa tulifika, kwenye ukingo wa mlima uliokuwa kama meza.

Yaliyokuwa mbele yetu hatukuona kwa sababu ukungu ulifunika nchi kama mawimbi ya bahari. Lakini ukungu ulipoinuka kidogo tuliona kwa mbele yetu yapata hatua mia tano mahali padogo penye majani mwisho wa theluji, na katika majani hayo tuliona mto wa maji unapita.

Wala hayo si yote, maana pale katika majani tuliona wanyama wakubwa kumi au kumi na tano wamekaa wanaota jua.
Hatukuweza kuona ni wa namna gani, lakini nyoyo zetu zilijaa furaha tena, tukafanya shauri la kuwapiga.

Basi nilitwaa bunduki na Bwana Henry na Bwana Good vile vile wakatwaa bunduki zao tukamwambia Umbopa atupe ishara na sote tukapiga pamoja. Basi tukajiweka tayari na Umbopa akasema ‘Piga’ na sote tulipiga pamoja, na moshi wa bunduki ulipoinuka tuliona mnyama mkubwa amekufa.

Tulipiga kelele za furaha kwa kuokoka, hatutakufa kwa njaa. Ingawa tulikuwa dhaifu sana tuliruka katika theluji mpaka pale penye mnyama na kabla haijapita dakika kumi temekwisha mkatakata mnyama.

Na moyo na maini yake yalikuwa yamewekwa mbele yetu. Lakini sasa tukatambua shida nyingine, maana hatuna kuni, na kwa hivi hatuwezi kukoka moto wa kupikia nyama. Basi tukatazamana katika shida yetu, Bwana Henry akasema, ‘‘Watu wenye njaa hawawezi kuwa wachaguzi, lazima tule nyama mbichi’’ basi hapakuwa na njia nyingine ya kutoka katika shida yetu, na njaa. Yetu ilikuwa kali mno.

Basi tulifukia moyo na maini katika theluji kwa muda kidogo ili kuyapoza, kisha tuliyaosha sana katika maji ya mto, tukayala mabichi.

Kwa kweli sijaonja nyama tamu kama ile nyama mbichi. Baada ya robo saa tulikuwa na hali nyingine kabisa, maana uzima wetu ulirudi pamoja na nguvu, na damu ilizunguka katika mishipa yetu.

Lakini hatukusahau habari za hatari ya kula sana, maana matumbo yetu yalikuwa dhaifu, tukaacha kula kabla ya kushiba. Bwana Henry akasema, ‘’Tushukuru Mungu, Yule mnyama ametuokoa maisha yetu. Je, Quatermain, ni mnyama gani?’

Niliondoka nikaenda kumtazama, lakini nilikuwa sina hakika. Baadaye nilikuja kujua kama watu wa huko walimwita Inko. Tulipokwisha kula tulikaa tukatazama pote. Palikuwa pazuri mno. Tulipokuwa tumekaa hivyo, Bwana Henry alisema, ‘Je, katika ile ramani haikuandikwa habari za Njia kuu ya Sulemani?’ Nikatikisa kichwa na nikaendelea kutazama ardhi mbele yetu.

Akaelekeza mkono upande wa kushoto akasema, ‘Basi, tazama, ni ile!’ Tukatazama tukaona njia pana uwandani imetambaa kama nyoka. Hatukusema mengi, maana tulianza kuzoe mambo ya ajabu. Bwana Good akasema, ‘’Nadhani si mbali; afadhali na tufuate njia, haya tuondoke.’’

Basi tulipokwisha nawa katika mto tuliondoka tena. Kwa mwendo wa maili moja tulisafiri juu ya miamba na theluji, na tulipokwisha panda kilima kidogo tuliona njia tukaifuata.

Njia ilikuwa imara ya ajabu mno, na upana wake ulipata kadiri ya hatua thelathini, lakini haikuendelea, maana tulitembea hatua mia moja tukaona imefifia kabisa, imefunikwa kwa miamba.
 
Bwana Henry akaniuliza, ‘Je, imekuwaje sasa?’ nikatikisa kichwa tu. Bwana Good akasema, ‘Mimi najua.

Nadhani njia ilipita huku lakini mchanga umepeperusha na kuifunika, na huko juu nadhani imefunikwa kwa mawe yaliyotoka juu mlimani.’ Basi tukaona kuwa labda maneno yake ni ya kweli, tukaanza kuteremka mlimani.

Sasa safari yetu ilikuwa nyepesi wala si kama ile ya kupanda mlima tulipokuwa tunaona njaa kali. Kama tungaliweza kuwasahau masikini Ventvogel na Yule mzee pangoni nadhani tunaliona furaha kabisa, ingawa hatukujua hatari inayoweza kutokea kwa mbele. Kila tukiteremka tuliona hewa inazidi kuwa nzuri, na nchi yenyewe ilikuwa nzuri kabisa.

Njia ilikuwa ya ajabu mno, pengine ilivuka misingi mirefu juu ya daraja yenye matao, na pengine ilipanda mlima kwa kuzunguka zunguka, na pengine ilipenya ndani yam lima wenyewe. Ukuta wa tundu lile lililopenya mlima ulichorwa picha.

Bwana Henry akazitazama akasema, ‘Watu wanaita njia hii njia ya Sulemani lakini mimi nafikiri kama ni kazi ya watu wa Misri walipofika hapa kabla ya watu wa Sulemani. Maana, kazi hii kama si kazi ya Wamisri, nadhani imefanana sana nayo.’

Ilipopata saa sita tulikuwa tumekwisha teremka na kufika mahali penye miti mingi. Mara Bwana Good akasema, ‘Ah! Hapa tunaweza kupata kuni; na tukae hapa kidogo tuchome nyama iliyobaki; maini yale mabichi yamekwisha shuka tumboni.’

Basi tuliacha njia tukaenda kwenye mto wa maji safi tukakaa, na upesi tuliwasha moto. Sasa tulikata nyama ya Inko tuliyoleta tukaioka. Tulipokwisha shiba, tukavuta tumbako tukaaa tumefurahi, na raha yetu tulipoilinganisha na taabu iliyotupata ilikuwa kama ni raha ya peponi.

Baadaye kidogo sikumwona Bwana Good, nikatazama kuona umekwenda wapi. Nikamwona amekaa karibu na mto amekwisha oga. Sasa amevaa shati lake tu na tabia yake ya umaridadi ikadhihirika; maana amekunja suruwali na koti, naye anatikisa kichwa kwa kuona namna zilivyoraruka kwa miiba ya njiani. Kisha akatwaa viatu vyake akavisugua kwa majani, kisha akatwaa kipande cha mafuta ya nyama akaanza kuvisugua kwa mafuta.

Kisha akavitazama kwa miwani yake, maana alivaa siku zote miwani yenye kioo kimoja tu, akavivaa. Sasa alitoa kioo kidogo na kitana akajitazama uso na tena akatikisa kichwa, akachana nywele zake, lakini hakuwa radhi.

Akapapasa ndevu zake, maana hakuweza kunyoa kwa muda wa siku kumi, akatwa kile kipande cha mafuta akakiosha katika maji, kisha akasugua ndevu zake kwa mafuta, akatwaa wembe katika mfuko wake akaanza kunyoa ndevu zake.

Lakini niliona akiumia sana, maana niliweza kumsikia akiguna, nikacheka sana. Maana niliona kuwa ni ajabu kuwa mtu anakubali kuvumilia maumivu ya kunyoa kwa mafuta katika mahali tulipo sisi, yaani porini pasipo na watu. Basi alizinyoa ndevu zilizokuwa nyingi sana, kwa upande wa kulia wa uso wake, na mara nilishtuka sana nikaona mshale wa nuru unampitia kichwani.
 
Bwana Good akaruka ameshtuka sana, na mimi vile vile nikaruka nikatazama, na haya ndiyo niliyoona.

Pale yapata hatua ishirini kutoka nilipokuwa nimesimama mimi, na hatua kumi kutoka alipokuwako Bwana Good, niliona watu wamesimama. Wote walikuwa warefu na weusi, lakini wekundu kidogo kama rangi ya shaba nyekundu, na wengine walivaa manyoya marefu meusi na ngozi za chui; basi haya ndiyo niliyoona kwanza.

Mbele niliona kijana mwenye umri wa miaka kumi na saba amesimama kama ndiyo kwanza autupe mkuki. Mshale ule wa nuru niliouona ulikuwa mwangaza uliomulikwa na mkuki alioutupa.

Nilipokuwa nikitazama, mzee mmoja aliyekuwa kama askari akaja mbele akamshika mkono Yule kijana akasema naye, kisha wote wakatujia.
Bwana Henry na Bwana Good na Umbopa wote walishika bunduki zao wakaelekeza. Lakini wale watu wakazidi kutujia.

Basi niliona kuwa hawa kujua bunduki ni kitu gani, maana wangalijua wasingezi dharau hivyo. Basi nikawaambia waweke bunduki zao chini, maana watambue kuwa usalama wetu u katika kutafuta suluhu.


Wakafanya nilivyotaka, kisha nikaenda mbele kuonana na wale watu, nikamwambia Yule mzee kwa Kizulu. Maana nilibaatisha tu, lakini nilipoona kuwa wanafahamu maneno yangu nilistaajabu.

Yule mzee akaitikia, lakini maneno yake yaliachana kidogo na maneno ya Kizulu ila si sana, na mimi na Umbopa tuliweza kuyafahamu mara. Yule mzee akauliza, ‘Mmetoka wapi? Nyinyi ni nani? Kwa nini sura za nyinyi watatu ni nyeupe na huyu wanne ni kama sura zetu?’


Akapeleka mkono kumwonyesha Umboka. Nikamtazama Umbopa na nikajua kuwa anasema kweli. Sura yake ilikuwa kama sura za watu wale waliokuwa wamesimama mbele yetu, na maungo vile vile yalifanana nao. Nikamjibu, ‘sisi ni wageni tumekuja kwa amani, na mtu huyu ni mtumishi wetu.’
Akasema, ‘’Unasema uwongo, wageni hawawezi kuvuka ile milima.

Lakini uwongo wenu utafaa nini? Ikiwa nyinyi ni wageni lazima mtakufa, maana wageni wowote hawana ruhusa kuishi katika nchi hii ya Wakukuana. Hii ndiyo amri ya Mfalme. Basi mjiwekeni tayari kufa, e nyinyi wageni’’ Niliposikia maneno hayo nilifadhaika, na hasa nilipoona mikono ya wale watu inashuka na kushika visu vikubwa vilivyofungwa viunoni mwao. Bwana Good akauliza, ‘Je, mtu huyu anasema nini?’ Nikamjibu, ‘Anasema kuwa tutauawa .’

Bwana Good akaghumia, na kama ilivyokuwa desturi yake anapokuwa kwenye shida yeyote, alitia vidole kinywani akashika meno yake akayavuta chini, kisha akayaacha yarudi juu tena kwa kishindo. (Maana alikuwa ametiwa meno yaliyotengenezwa, kwa kuwa meno yake yameng’olewa).

Jambo hilo lilituokoa, maana mara walipoona hivyo, wale watu wakashtuka wakapiga kelele kwa hofu, wakaruka nyuma hatua mbili tatu. Nikasema, ‘Je, kuna nini?’ Bwana Henry akaninong’oneza akasema, ‘Ni meno ya Bwana Good nadhani alipoyavuta chini; wale watu wameona ni ajabu.

Haya, Bwana Good, yatoe kabisa.’ Basi akayatoa akayaficha upesi katika mkono wa shati lake.

Basi wale watu sasa walishikwa na udadisi wakasahau hofu yao kidogo, wakaja mbele, sasa ile habari ya kutuua waliisahau.

Yule mzee akaelekeza mkono wake kumwonyesha Bwana Good, naye amesimama amevaa shati na viatu tu, na tena amenyoa upande mmoja tu wa uso wake, akasema, ‘Ee nyinyi wageni, imekuwaje kuwa huyu mnene amevaa nguo maungoni ila miguu ni mitupu, na pia ndevu zaota kwa upande mmoja tu wa uso wake, naye, analo jicho moja ambalo linapenya nuru? Imekuwaje anaweza kuyatoa meno yake nakuyarudisha apendavyo?’


Nikamwambia Bwana Good, ‘Funua kinywa chako.’ Akafunua midomo yake kama mbwa mkali, wakaona kuwa hana meno kabisa, waliouona ni ufizi tu. Basi wale watu wakashtuka sana, wakasema, ‘Meno yake yako wapi sasa? Tulioyaona kwa macho yetu sasa hivi!’

Basi Bwana Good akageuza kichwa chake kidogo akainua mkono wake akayaweka meno ndani kwa siri, kisha akacheka. Kumbe! Kinywa chake kimejaa meno tena. Basi walipoona hivyo, Yule kijana alijiangusha chini akalia kwa hofu; na magoti ya Yule mzee yaligongana kwa kuogopa, akasema, na sauti yake ilitetemeka.

‘Naona kuwa nyinyi ni mizuka, maana hapana mtu aliyezaliwa na mwanamke mwenye ndevu upande mmoja tu wa uso, wala jicho moja linalopenya nuru, wala meno yanayotoweka na kuonekana tena. Ee mabwana, mtuwie radhi.’

Basi nikaona kama ni bahati yetu tena, nikamjibu kwa sauti kali, ‘Basi, msiogope; nitawataarifu habari za kweli. Sisi ni wanaume kama nyinyi lakini tumetoka katika ile nyota kubwa inayozidi kung’aa usiku.

Tumekuja kukaa pamoja nanyi kwa muda kidogo na kuwaleteeni neema. Mnaona rafiki zangu, nimejifunza lugha yenu ili niwe tayari.’

Wakaitika, ‘Ni kweli, ni kweli.’ Nikaendelea nikasema, ‘Na sasa, rafiki zangu, labda mnaogopa, mnafikiri kuwa tutamuua Yule kijana aliyemtupia mkuki huyu mwenzetu mwenye meno yanayotoka na kurudi tena. Maana mmetupokea vibaya baada ya safari ndefu tuliyoifanya ili kufika hapa.’

Yule mzee akasema, ‘Mabwana, mtusameheni nawasihi, maana yeye ni mwana wa mfalme na mimi ni mjomba wake. Akidhurika lazima mimi nitauawa.’ Yule kijana akaitikia, akasema, ‘Ndiyo, hayo ni kweli kabisa.’

Nikasema, ‘Labda mnafikiri kuwa hatuna nguvu za kujilipiza kisasi, lakini nitakuonyesheni. Haya wewe (nikamwita Umbopa kwa ukali sana) nipe mwanzi wangu wa uchawi unaosema.’ (Nikamwashiria anipe bunduki yangu).

Umbopa alitambua mara moja niliyotaka, akanipa bunduki yangu huku akiinamisha kichwa, na akasema, ‘Ni huu, bwana wa mabwana.’ Basi kabla sijamwambia anipe bunduki niliona swala amesimama juu ya mwamba kadiri ya mwendo wa hatua mia moja, nikanuia kumpiga.

Basi niliwaonyesha huyo swala, nikasema, ‘Niambieni kama yupo mtu aliyezaliwa na mwanamke anayeweza kumuua Yule mnyama kwa mshindo tu!
Yule mzee akajibu, ‘Hapana mtu, wala haiwezekani kabisa.’ Nikajibu, ‘Lakini mimi nitamuua.

Nikaelekeza bunduki yangu, Yule mnyama alikuwa mdogo lakini nilijua kuwa ni lazima nimpige. Nikavuta pumzi nikakaza mtambo wa bunduki kwa taratibu. Yule swala alisimama kimya kabisa. Bunduki ikalia, na mara Yule swala akaruka juu, akaanguka juu ya mwamba amekwisha kufa.


Basi, hapo wale watu waliguna kwa hofu, nikasema, ‘Haya, mkitaka mnyama nendeni mkamchukue huyo.’ Yule mzee akamwashiria mtu mmoja, na akaenda akamleta mnyama, wakamzungukia wakatazama tundu iliyoingia risasi.

Nikasema, ‘Kama hamsadiki hata sasa, basi mtu mmoja asimame mwambani nimfanye kama nilivyomfanya huyo swala. Hapo mtafahamu kuwa mimi sisemi maneno ya bure.’
Hapana aliyetaka kufanya hivyo mpaka Yule mwana wa mfalme aliposema, ‘Umesema vema. Wewe, mjomba wangu, nenda ukasimame mwambani, Uchawi ule umeua mnyama tu, hauwezi kumuua mtu.’

Lakini Yule mzee hakupenda shauri lile, akaudhika, akasema, ‘Hapana! Hapana! Macho yangu ya kizee yameona mambo ya kutosha. Watu hawa ni wachawi wa kweli kweli. Tuwachukue kwa mfalme.

Lakini ikiwa mmoja wenu anataka ushuhuda zaidi, basi na yeye asimame mwambani na ule mwanzi wa uchawi utasema naye.’

Hapo wote wakaanza kukataa. Na mmoja akasema, ‘Hapana, uchawi wa namna hiyo usipotee bure kwa ajili yetu. Sisi tumeridhika. Uchawi wote wa watu wetu hauwezi kufanya jambo kama hilo.’

Yule mzee akasema, ‘Ni kweli. Bila shaka ni kweli. Na sasa nyinyi watoto wa nyota, sikilizeni, nyinyi watoto wenye macho yanayong’aa, meno yanayotoweka, nyinyi mnaonguruma kwa ngurumo inayoweza kuua kwa mbali. Mimi ni Infadus, mwana wa Kafa, aliyekuwa mfalme wa watu wa Kukuana.


Huyu kijana ni Skraga, mwana wa Twala aliye mfalme mkuu wa Kukuana, Mlinzi wa Njia Kuu, Mtishaji wa adui zake, Mwenye elimu ya uchawi, Jemedari wa askari mia elfu, Twala mwenye chongo, Mweusi, Mtishaji.’

Nikasema kwa maneno ya dharau, ‘Mn, basi na tuongoze kwa Twala. Sisi hatutaki kusema na watu wanyonge na wadogo.’

Yule mzee akajibu, ‘Vema, mabwana wangu. Sisi tunawinda muda wa siku tatu kutoka mji wa mfalme, lakini mabwana muwe na subira na sisi tutawaongozeni.’ Nikajibu, ‘Vema, wakati wote upo mikononi mwetu, maana sisi hatufi.

Tu tayari mtuongoze. Lakini wewe Infadus, na wewe Skraga, angalieni! Msitudanganye, msijaribu kututega, maana tutatambua fikra zenu duni kabla hazijaingia katika akili zenu, na hatutakosa kujilipiza kisasi.

Nuru ile inayotoka katika jicho la Yule mwenye miguu mitupu na ndevu upande mmoja tu wa uso, itakuaribuni, itapita katika nchi yenu. Meno yake yanayotoweka yatajibana mikononi mwenu na yatakuleni nyinyi na wake zenu na watoto wenu; mianzi ya ajabu itasema nanyi kwa sauti na itawafanyeni kuwa kama takataka.

Angalieni.’ Basi maneno yangu yaliwatisha sana, na yule mzee alijibu, ‘Koom! Koom!’
Baadaye nilipata kufahamu ya kuwa yale maneno ndiyo wanayoyatumia kwa kumwamkia mfalme.

Akageuka akawaamuru watu wake, na mara upesi wakashika vitu vyetu ili wavichukukue, ila bunduki hawakushika, maana waliziogopa. Hata na nguo za Bwana Good wakazishik, naye alipoona hivi akataka kuzitwaa, ‘Ee, Bwana mwenye jicho linalong’aa na meno yanayoyeyuka, usitwae nguo, maana watumishi wako watazichukua.’

Bwana Good akasema kwa Kiingereza, ‘Ndiyo, lakini nataka kuziva.’ Umbopa akatafsiri maneno yake, na Infadus akajibu, ‘Hapana Bwana, usifiche miguu yako mizuri iliyo meupe tusiione tena? Tokea sasa lazima uvae shati na viatu na miwani yako tu basi.’

Na mimi nikaongeza, ‘Ndiyo, na tena lazima uache ndevu upande mmoja tu wa uso wako. Ukijibadili kwa namna yoyote watu hawa watafikiri kuwa tunawadanganya. Nakusikitikia, lakini kweli, lazima ufanye hivyo. Kama wakishuku habari hizi si za kweli, basi maisha yetu yatapotea kabisa.’

Bwana Good akasema, ‘Je, unasema kweli?’ Nikamjibu, ‘Ndiyo, nasema kweli kabisa, maana miguu yako meupe mizuri na miwani yako imekuwa ni umbo lako na lazima uvumilie tu.’ Akavumilia lakini hakuzoea, mpaka baada ya kadiri ya siku kumi, kwenda akivaa nguo chache hivi.
 
SURA YA SABA


Tulipofika nje ya pango tulisimama tumepumbaa. Bwana Henry akasema, ‘Mimi nitaingia ndani tena.’ Bwana Good akamuuliza kwa nini? naye akajibu, ‘Kwa sababu labda Yule tuliyemwona ndiye tunayemtafuta labda ni ndugu yangu.’

Basi tukaingia ndani tena ili tushuhudie. Tulipoingia kwanza hatukuweza kuona vizuri sababu ya kiwi cha macho kilichofanywa na mwangaza wa nje lakini tuliposimama mwisho wa pango niliona maiti mwingine amekaa, kichwa chake kimeinamia kifuani. Baada ya kuzoea giza tulimkaribia Yule maiti, na Bwana Henry akapiga magoti karibu naye akamtazama usoni, akasema, ‘Namshukuru Mungu, huyu si ndugu yangu.’

Basi ndipo nilipomkaribia mimi nikamtazama. Huyu marehemu alikuwa mtu mrefu, mtu mzima na pua ya upanga, na nywele zake zilianza kuwa na mvi, na alikuwa na masharubu marefu.

Ngozi yake ilikuwa imekauka kabisa nayo imetanda juu ya mifupa yake. Alikuwa hana nguo ila shingoni alifungwa msalaba wa pembe. Nikasema, ‘Marehemu huyu alikuwa nani?’

Bwana Good akasema, ‘Je, huwezi kubahatisha?’ Nikatikisa kichwa, akasema, “Huyo si mzee Jose da Silvestre’ Nikasema, ‘Haiwezekani, maana yeye alikufa miaka mia tatu iliyopita.’ Bwana Good akajibu, ‘Na hapa kuna nini cha kuzuia asikae bila kuoza kwa miaka elfu tatu? Maana ikiwa ni baridi mno, nyama inaweza kukaa bila kuoza kwa muda mrefu sana.

Na hapa joto la jua haliingii kabisa; Wala wanyama hawaji kumrarua na kumharibu. Haikosi Yule mtumishi wake aliyemtaja katika maandishi yake alimvua nguo na kumwacha hapa.

Tazama, huu ndiyo mfupa aliotumia kama kalamu kuandikia ile ramani yake.’ Akainama chini akaokota mfupa mdogo uliopasuliwa ncha. Tukatazama tumeshangaa, na katika kutazama ajabu hii tulisahau shida na taabu zetu.

Bwana Henry akasema, ‘Ndiyo kweli, na hapa ndipo mahali alipotoa wino wake.’ Akaonyesha kijeraha kidogo katika mkono wa Yule maiti.

Basi sasa hatukuwa na shaka tena, maana tumekwisha shuhudia. ‘’Huyu maiti ni Yule mtu aliyeandika yale maelezo vizazi kumi nyuma ambayo yametuongoza hapa. Huu mkononi mwangu ni mfupa ule aliotumia kuwa kalamu, na hapo shingoni upo msalaba alioubusu wakati alipokuwa akifa.’’

Baadaye kidogo Bwana Henry alisema, ‘Haya twendeni, lakini ngoja kwanza nimpe mwenzie akae pamoja naye.’ Akamwinua Yule marehemu Ventvogel akamweka karibu na maiti ya Yule mzee, kisha akainama akatoa ule msalaba katika shingo ya Yule mzee kuwa ni ukumbusho. Nadhani anao hata sasa.

Mimi nilichukua ule mfupa, ninao hata sasa napengine nautumia kama kalamu, Basi tuliwaacha wale maiti wawili pamoja, walinde zamu katikati ya theluji inayodumu milele, tukatoka katika pango na kuingia katika mwangaza wa jua.

Tukaendelea katika safari yetu tukiwaza mioyoni ni baada ya saa ngapi na sisi tutakuwa kama wao walivyo sasa. Tulipokwisha kwenda yapata nusu saa tulifika, kwenye ukingo wa mlima uliokuwa kama meza.

Yaliyokuwa mbele yetu hatukuona kwa sababu ukungu ulifunika nchi kama mawimbi ya bahari. Lakini ukungu ulipoinuka kidogo tuliona kwa mbele yetu yapata hatua mia tano mahali padogo penye majani mwisho wa theluji, na katika majani hayo tuliona mto wa maji unapita.

Wala hayo si yote, maana pale katika majani tuliona wanyama wakubwa kumi au kumi na tano wamekaa wanaota jua.
Hatukuweza kuona ni wa namna gani, lakini nyoyo zetu zilijaa furaha tena, tukafanya shauri la kuwapiga.

Basi nilitwaa bunduki na Bwana Henry na Bwana Good vile vile wakatwaa bunduki zao tukamwambia Umbopa atupe ishara na sote tukapiga pamoja. Basi tukajiweka tayari na Umbopa akasema ‘Piga’ na sote tulipiga pamoja, na moshi wa bunduki ulipoinuka tuliona mnyama mkubwa amekufa.

Tulipiga kelele za furaha kwa kuokoka, hatutakufa kwa njaa. Ingawa tulikuwa dhaifu sana tuliruka katika theluji mpaka pale penye mnyama na kabla haijapita dakika kumi temekwisha mkatakata mnyama.

Na moyo na maini yake yalikuwa yamewekwa mbele yetu. Lakini sasa tukatambua shida nyingine, maana hatuna kuni, na kwa hivi hatuwezi kukoka moto wa kupikia nyama. Basi tukatazamana katika shida yetu, Bwana Henry akasema, ‘‘Watu wenye njaa hawawezi kuwa wachaguzi, lazima tule nyama mbichi’’ basi hapakuwa na njia nyingine ya kutoka katika shida yetu, na njaa. Yetu ilikuwa kali mno.

Basi tulifukia moyo na maini katika theluji kwa muda kidogo ili kuyapoza, kisha tuliyaosha sana katika maji ya mto, tukayala mabichi.

Kwa kweli sijaonja nyama tamu kama ile nyama mbichi. Baada ya robo saa tulikuwa na hali nyingine kabisa, maana uzima wetu ulirudi pamoja na nguvu, na damu ilizunguka katika mishipa yetu.

Lakini hatukusahau habari za hatari ya kula sana, maana matumbo yetu yalikuwa dhaifu, tukaacha kula kabla ya kushiba. Bwana Henry akasema, ‘’Tushukuru Mungu, Yule mnyama ametuokoa maisha yetu. Je, Quatermain, ni mnyama gani?’

Niliondoka nikaenda kumtazama, lakini nilikuwa sina hakika. Baadaye nilikuja kujua kama watu wa huko walimwita Inko. Tulipokwisha kula tulikaa tukatazama pote. Palikuwa pazuri mno. Tulipokuwa tumekaa hivyo, Bwana Henry alisema, ‘Je, katika ile ramani haikuandikwa habari za Njia kuu ya Sulemani?’ Nikatikisa kichwa na nikaendelea kutazama ardhi mbele yetu.

Akaelekeza mkono upande wa kushoto akasema, ‘Basi, tazama, ni ile!’ Tukatazama tukaona njia pana uwandani imetambaa kama nyoka. Hatukusema mengi, maana tulianza kuzoe mambo ya ajabu. Bwana Good akasema, ‘’Nadhani si mbali; afadhali na tufuate njia, haya tuondoke.’’

Basi tulipokwisha nawa katika mto tuliondoka tena. Kwa mwendo wa maili moja tulisafiri juu ya miamba na theluji, na tulipokwisha panda kilima kidogo tuliona njia tukaifuata.

Njia ilikuwa imara ya ajabu mno, na upana wake ulipata kadiri ya hatua thelathini, lakini haikuendelea, maana tulitembea hatua mia moja tukaona imefifia kabisa, imefunikwa kwa miamba.
Umetisha mkuu, acha niifaidi taratiiibu
 
Back
Top Bottom