Pep
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 2,338
- 5,488
Mkuu blackstarline umetulaza njaa leo mkuu wangu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa hapa sina mkuuUnavyo vitabu vyake?
Kwa hapa sina mkuuUnavyo vitabu vyake?
Mkuu kesho mapema sana natupia mzigoMkuu blackstarline umetulaza njaa leo mkuu wangu
Kesho mapema sana na tupia mzigoWrite your reply... Lete nondo zaidi mkuu
Ndo naigonga apa taratiibu. Ahsante mkuuSURA YA SITA
Ilipopata saa kumi za usiku niliamka baada ya kulala kwa muda wa saa mbili tu, na sasa haja ya kwanza ya mwili, yaani kupumzika, imetimizwa. Maumivu yale mengine ya kiu yalianza kuniudhi, nami sikuweza kupata usingizi tena.
Kabla ya kuamka nilikuwa nikiota ndoto ya kuwa ninaoga katika mto wa maji mazuri yanayopita, na kando ya mto miti mizuri inaota, Kumbe! Niliamka kujiona katika jangwa la ukiwa, kavu kabisa, nakumbuka yale maneno aliyosema Umbopa kuwa kama hatupati maji leo tutakufa kifo kibaya. Hapana mwanadamu aliyeweza kuishi katika nchi ya joto kama lile jangwa bila maji ya kunywa.
Nilikaa nikasugua uso wangu uliokuwa mchafu kwa mikono yangu iliyokuwa mikavu kabisa. Midomo na kope zangu zilikuwa zimegandamana kabisa, nikaweza kuyafumbua macho kwa shida. Mapambazuko yalikuwa karibu, lakini baridi ile tunayozoea kuona asubuhi haikuwapo kabisa, na hewa ilikuwa nzito na nene jinsi nisivyoweza kueleza.
Wenzangu walikuwa wamelala.
Baadaye kukaanza kupambazuka, na ili nipate kusahau kiu yangu, nilitoa kitabu kidogo nilichozoea kuchukua mfukoni mwangu, nikaanza kusoma, na kwa bahati maneno niliyosoma yalikuwa haya: ‘Kijana mzuri ajabu alishika kombe la nakshi, Limejaa maji matamu na safi..’ Niliposoma maneno yale nilimeza mate au kwa kweli nilijaribu kumeza. Hata kufikiri maji kulitaka kunifanya niwe na wazimu.
Hapo nadhani nilishikwa na kichaa kidogo, maana nilianza kucheka, na sauti yangu iliwaamsha wenzangu, na wao wakaanza kusugua nyuso zao chafu, na kufungua midomo na kope zao zilizogandamana.
Mara tulipoamka kabisa tukianza kuzungumza juu ya shida yetu. Hapana hata tone la maji. Tulipindua viriba vyetu tukalamba kingoni, lakini wapi! Vikavu kabisa. Bwana Henry akasema ‘Tusipopata maji tutakufa.’ Nikasema, ‘Kama ile ramani ya Yule mzee ni sahihi, maji yapo karibu tulipo sasa.’ Lakini maneno yangu hayakufariji mtu, maana ilikuwa dhahiri kuwa hatuwezi kuitumai sana ile ramani.
Sasa ikaanza kuwa kweupe kidogo kidogo, tukakaa tunatazamana tu, nikamwona Ventvogel, Yule Hottentot, akiondoka na kuanza kwenda macho chini, na mara akafanya sauti kama ya kukoroma, akaonyesha chini katika mchanga.
Tukashtuka tukasema, ‘Nini, nini? Tukaondoka sote tukamwendea tukitazama chini. Akasema, ‘Wako wanyama wengi kama paa hapa. Tazameni nyayo zao.’ Nikamuuliza, ‘Je, hata kama paa ni wengi hapa hilo linatufaa nini? ‘ Akajibu, ‘Paa hawatembei mbali na maji.’
Nikasema, ‘Kweli, nilisahau, Alhamdulilahi.’ Basi jambo hilo lilitutia uzima tena; ni ajabu sana ya kuwa ‘kama watu wamo katika shida tama ya faraja hata ndogo huwafurahisha. Maana katika usiku wa giza hata nyota moja ni bora kuliko kutokuwa na nyota kabisa.
Daah, hii kitu ni kali.Hapo kwa bahati niliona kundi la ndege wakubwa wanaruka juu, nikaona kuwa ni namna inayofaa kuliwa. Nikatwaa bunduki yangu, na kwa bahati tena nilipiga mmoja. Sasa tukafanya moto kwa majani makavu ya matikiti tukamwoka ndege, tukala chakula namna tusiyokula kwa juma zima.
Tulikula ndege Yule wala hatukusaza kitu ila mifupa ya miguu yake na mdomo wake, tukaona nafuu.
Usiku ule mwezi ulipotoka tukaendelea katika safari yetu. Tulichukua matikiti kadiri tulivyoweza. Tulipopanda kidogo tuliona hewa inaanza kuwa baridi na tuliona raha, maana tulikuwa karibu kufika kwenye theluji, ulibaki mwendo wa maili kumi na mbili tu. Na hapo tuliona matikiti mengine, basi hatukuona taabu ya kiu, na tena tulijua kwamba mara tukifika kwenye theluji shida yetu ya maji itakwisha.
Lakini sasa mlima ulianza kwenda juu sana na kwa hivyo mwendo wetu ulikuwa wa kobe tu. Usiku ule tulikula nyama iliyobaki, na mpaka sasa hatujaona kiumbe chenye uhai ila wale ndege, wala hatujaona chemchemi wala mto wa maji, tukafikiri kuwa ni ajabu , maana theluji ikiisha yeyuka lazima maji yake yateremke mahali.
Lakini baadaye tulijua kuwa mito yote iliteremka kwa upande wa pili wa mlima. Sasa tulianza kufikiri habari za njaa. Tumenusurika kufa kwa kiu, lakini ilionekana kuwa tutakufa kwa njaa. Habari zilizotokea katika siku tatu za taabu zilizofuata zimeandikwa katika kitabu changu kama hivi:
21 Mei: ‘’Tulianza safari saa tano mchana, hewa ilikuwa baridi tukaweza kusafiri mchana huku tumechukua matikiti. Tulijikokota mpaka jioni lakini hatukuona matikiti mengine. Naona kama tumekwisha pita mahali yanapositawi. Hatukuona mnyama yeyote, Jua liliposhuka tulipumzika, na kwa kuwa hatujala kwa muda wa saa nyingi tulisumbuka sana. Na hasa kwa sababu ya baridi ya usiku.’
22 Mei: ‘Mara kulipopambazuka tulianza safari tena, lakini tulikuwa dhaifu sana. Safari ya kutwa ilikuwa mwendo wa maili tano tu.
Tuliona theluji kidogo kidogo tukaila, lakini hatukula kitu kingine, Tulifanya kambi yetu usiku chini ya mwamba. Baridi ni kali mno. Tulikunywa mvinyo kidogo tukajifunika na mablanketi yetu tusife kwa baridi. Sasa tumo taabuni kabisa kwa sababu ya baridi na njaa. Nilifikiri kuwa Ventvogel atakufa usiku.’
23Mei: ‘Mara jua lilipopanda tukashika safari tena, tukaota jua. Sasa tu taabani kabisa kabisa, nadhani ilikuwa ni safari ya mwisho tusipopata chakula.
Mvinyo umebaki kidogo sana. Bwana Good na Bwana Henry na Umbopa wanavumilia namna ya ajabu, lakini Ventvogel yu karibu kufa. Kama walivyo Hottentot wote, yeye hawezi kuvumilia baridi.
Maumivu ya njaa si mabaya sana, lakini naona kama tumbo limekufa ganzi. Wenzangu wasema hayo hayo, sasa tumefika juu yam lima ule unaoungamana na matiti ya Sheba na chini pote ni pazuri ajabu. Nyuma yetu jangwa linalong’aa katika jua limeenea mpaka upeo wa macho, na mbele yetu theluji inaonekana kwenda juu kwa taratibu mpaka kufika kwenye matiti ya Sheba.
Hapana kitu chenye uhai kinachooneka. Mungu atusaidie nahofu ya kuwa hatima yetu ipo karibu.’ Na sasa nitaacha habari zilizoandikwa katika kitabu nishike hadithi yangu tena. Siku ile ya 23 Mei, kutwa tulijikokota mbele tukapanda mwinuko ule wa theluji na mara kwa mara tulilala tukapumzika.
Nadhani watu wangalituona wangalifikiri tu watu wa ajabu, maana tumekonda, tumechoka na tulikuwa tunavuta miguu kwa shida sana, na macho yetu yana dalili ya njaa kali nayo yamekodoka mbele kabisa.
Siku ile tulikwenda maili saba tu, na jua lilipokuwa karibu kushuka tukajiona chini ya titi la kushoto la Sheba, nalo lilikwenda juu sana kama mlima mrefu wa theluji. Ingawa tulikuwa dhaifu sana lakini tuliyoyaona tulihisi ajabu na shani, maana mianga ya jua ilitia theluji rangi ya damu, na juu yake ilikuwa kama taji la theluji nyeupe inayong’aa.
Hapo Bwana Good alisema akitweta, ‘Nadhani tuko karibu na lile pango alilotaja Yule mzee katika hati yake.’ Nikasema, ‘Ndiyo, yaani iwapo pango liko.’ Bwana Henry akasema, ‘Haya, Bwana Quatermain, usiseme hivyo, mimi namwamini sana Yule mzee; hukumbuki namna tulivyoona yale maji? Haikosi tutaona na lile pango upesi.’ Nikasema, ‘Tusipoliona kabla ya giza kuingia, sisi ni maiti, hivi ndivyo ninavyojua mimi.’
Basi tulijivuta tulivyoweza mpaka kufika kwenye shimo na hakika tuliona kuwa ni kinywa cha pango, na haikosi ni pango lile alilotaja Yule mzee Silvestre katika hati yake. Kwa bahati tulifika kwa wakati unaofaa, maana mara tulipofika jua likatua na giza likaingia upesi sana.
Basi tukatambaa tukaingia katika pango na kila mtu alikunywa mvinyo kidogo ukaisha kabisa, tukasongana pamoja tupate kujitia joto, tukajaribu kusahau taabu zetu katika usingizi. Lakini kwa kuwa baridi ilikuwa kali mno hatukuweza kupata usingizi. Basi hapo tulikaa tukiona baridi inatuumiza, kwanza katika vidole, na tena miguu na usoni, Tulisongana pamoja , lakini wapi! Ilikuwa bure tu, maana miili yetu ilikuwa haina joto hata kidogo.
Mara kwa mara mmoja wetu alipata usingizi kwa muda kidogo, lakini mara aliamka tena, nami naona kuwa tungalipatwa na usingizi kamili hatungeamka tena, tungekufa pale pale. Nadhani iliyotuponya ilikuwa ni nia yetu tu.
Ilipokuwa karibu kupambazuka nilimsikia Ventvogel akiugua, na meno yake yaliyokuwa ya kitetemeka kwa baridi yakatulia. Nikafikiri kama ameshikwa na usingizi. Mgongo wake uliokuwa unaniegemea mimi ukazidi kuwa baridi mpaka ukawa kama barafu.
Baadaye kulianza kuwa kweupe kidogo na mishale ya jua ilikuwa kama mishale ya dhahabu ikipenya mote katika pango, imetuangaza, ikamwangaza na Ventvogel aliekaa katikati yetu, amekwisha kufa! Masikini, si ajabu ya kuwa mgongo wake ulikuwa baridi.
Nilipomsikia anaugua alikuwa ana kata roho, na sasa mkavu kabisa. Tulishtuka sana tukaondoka upesi tukamwacha pale amekaa na mikono yake imekumbatia miguu yake..
Ni ajabu namna wanadamu wanavyoona woga katika mahali penye maiti! Baadaye jua lilipanda kukawa kweupe kabisa ndani ya pango.
Mara nilisikia mmoja wetu akipaaza sauti yake kwa hofu, nikageuka nikatazama. Haya ndiyo niliyo yaoona: Pale mwisho wa pango niliona maiti mwingine, amekaa na kichwa chake kimeinamia kifuani,’ na tena nikaona kuwa maiti mwenyewe ni Mzungu. Na wenzangu pia wakamwona, na kuona kuliwatia woga sana. Kila mmoja akatoka pangoni upesi alivyoweza.
Poa mkuuHii hadithi mara ya kwanza nimepata kuisikia katika wimbo wa Kwanza Unit.
Kwanza Unit-Msafiri.
Nilitafuta kitabu nikafeli kukipata.
Shukran sana,
Nipo naifatilia Nukta mpaka Nukta.
Endelea kuweka Utamu wa Mashimo ya Mfalme Suleiman.
Safi sana kamanda wangu,Tupo pamoja.
Umetisha mkuu, acha niifaidi taratiiibuSURA YA SABA
Tulipofika nje ya pango tulisimama tumepumbaa. Bwana Henry akasema, ‘Mimi nitaingia ndani tena.’ Bwana Good akamuuliza kwa nini? naye akajibu, ‘Kwa sababu labda Yule tuliyemwona ndiye tunayemtafuta labda ni ndugu yangu.’
Basi tukaingia ndani tena ili tushuhudie. Tulipoingia kwanza hatukuweza kuona vizuri sababu ya kiwi cha macho kilichofanywa na mwangaza wa nje lakini tuliposimama mwisho wa pango niliona maiti mwingine amekaa, kichwa chake kimeinamia kifuani. Baada ya kuzoea giza tulimkaribia Yule maiti, na Bwana Henry akapiga magoti karibu naye akamtazama usoni, akasema, ‘Namshukuru Mungu, huyu si ndugu yangu.’
Basi ndipo nilipomkaribia mimi nikamtazama. Huyu marehemu alikuwa mtu mrefu, mtu mzima na pua ya upanga, na nywele zake zilianza kuwa na mvi, na alikuwa na masharubu marefu.
Ngozi yake ilikuwa imekauka kabisa nayo imetanda juu ya mifupa yake. Alikuwa hana nguo ila shingoni alifungwa msalaba wa pembe. Nikasema, ‘Marehemu huyu alikuwa nani?’
Bwana Good akasema, ‘Je, huwezi kubahatisha?’ Nikatikisa kichwa, akasema, “Huyo si mzee Jose da Silvestre’ Nikasema, ‘Haiwezekani, maana yeye alikufa miaka mia tatu iliyopita.’ Bwana Good akajibu, ‘Na hapa kuna nini cha kuzuia asikae bila kuoza kwa miaka elfu tatu? Maana ikiwa ni baridi mno, nyama inaweza kukaa bila kuoza kwa muda mrefu sana.
Na hapa joto la jua haliingii kabisa; Wala wanyama hawaji kumrarua na kumharibu. Haikosi Yule mtumishi wake aliyemtaja katika maandishi yake alimvua nguo na kumwacha hapa.
Tazama, huu ndiyo mfupa aliotumia kama kalamu kuandikia ile ramani yake.’ Akainama chini akaokota mfupa mdogo uliopasuliwa ncha. Tukatazama tumeshangaa, na katika kutazama ajabu hii tulisahau shida na taabu zetu.
Bwana Henry akasema, ‘Ndiyo kweli, na hapa ndipo mahali alipotoa wino wake.’ Akaonyesha kijeraha kidogo katika mkono wa Yule maiti.
Basi sasa hatukuwa na shaka tena, maana tumekwisha shuhudia. ‘’Huyu maiti ni Yule mtu aliyeandika yale maelezo vizazi kumi nyuma ambayo yametuongoza hapa. Huu mkononi mwangu ni mfupa ule aliotumia kuwa kalamu, na hapo shingoni upo msalaba alioubusu wakati alipokuwa akifa.’’
Baadaye kidogo Bwana Henry alisema, ‘Haya twendeni, lakini ngoja kwanza nimpe mwenzie akae pamoja naye.’ Akamwinua Yule marehemu Ventvogel akamweka karibu na maiti ya Yule mzee, kisha akainama akatoa ule msalaba katika shingo ya Yule mzee kuwa ni ukumbusho. Nadhani anao hata sasa.
Mimi nilichukua ule mfupa, ninao hata sasa napengine nautumia kama kalamu, Basi tuliwaacha wale maiti wawili pamoja, walinde zamu katikati ya theluji inayodumu milele, tukatoka katika pango na kuingia katika mwangaza wa jua.
Tukaendelea katika safari yetu tukiwaza mioyoni ni baada ya saa ngapi na sisi tutakuwa kama wao walivyo sasa. Tulipokwisha kwenda yapata nusu saa tulifika, kwenye ukingo wa mlima uliokuwa kama meza.
Yaliyokuwa mbele yetu hatukuona kwa sababu ukungu ulifunika nchi kama mawimbi ya bahari. Lakini ukungu ulipoinuka kidogo tuliona kwa mbele yetu yapata hatua mia tano mahali padogo penye majani mwisho wa theluji, na katika majani hayo tuliona mto wa maji unapita.
Wala hayo si yote, maana pale katika majani tuliona wanyama wakubwa kumi au kumi na tano wamekaa wanaota jua.
Hatukuweza kuona ni wa namna gani, lakini nyoyo zetu zilijaa furaha tena, tukafanya shauri la kuwapiga.
Basi nilitwaa bunduki na Bwana Henry na Bwana Good vile vile wakatwaa bunduki zao tukamwambia Umbopa atupe ishara na sote tukapiga pamoja. Basi tukajiweka tayari na Umbopa akasema ‘Piga’ na sote tulipiga pamoja, na moshi wa bunduki ulipoinuka tuliona mnyama mkubwa amekufa.
Tulipiga kelele za furaha kwa kuokoka, hatutakufa kwa njaa. Ingawa tulikuwa dhaifu sana tuliruka katika theluji mpaka pale penye mnyama na kabla haijapita dakika kumi temekwisha mkatakata mnyama.
Na moyo na maini yake yalikuwa yamewekwa mbele yetu. Lakini sasa tukatambua shida nyingine, maana hatuna kuni, na kwa hivi hatuwezi kukoka moto wa kupikia nyama. Basi tukatazamana katika shida yetu, Bwana Henry akasema, ‘‘Watu wenye njaa hawawezi kuwa wachaguzi, lazima tule nyama mbichi’’ basi hapakuwa na njia nyingine ya kutoka katika shida yetu, na njaa. Yetu ilikuwa kali mno.
Basi tulifukia moyo na maini katika theluji kwa muda kidogo ili kuyapoza, kisha tuliyaosha sana katika maji ya mto, tukayala mabichi.
Kwa kweli sijaonja nyama tamu kama ile nyama mbichi. Baada ya robo saa tulikuwa na hali nyingine kabisa, maana uzima wetu ulirudi pamoja na nguvu, na damu ilizunguka katika mishipa yetu.
Lakini hatukusahau habari za hatari ya kula sana, maana matumbo yetu yalikuwa dhaifu, tukaacha kula kabla ya kushiba. Bwana Henry akasema, ‘’Tushukuru Mungu, Yule mnyama ametuokoa maisha yetu. Je, Quatermain, ni mnyama gani?’
Niliondoka nikaenda kumtazama, lakini nilikuwa sina hakika. Baadaye nilikuja kujua kama watu wa huko walimwita Inko. Tulipokwisha kula tulikaa tukatazama pote. Palikuwa pazuri mno. Tulipokuwa tumekaa hivyo, Bwana Henry alisema, ‘Je, katika ile ramani haikuandikwa habari za Njia kuu ya Sulemani?’ Nikatikisa kichwa na nikaendelea kutazama ardhi mbele yetu.
Akaelekeza mkono upande wa kushoto akasema, ‘Basi, tazama, ni ile!’ Tukatazama tukaona njia pana uwandani imetambaa kama nyoka. Hatukusema mengi, maana tulianza kuzoe mambo ya ajabu. Bwana Good akasema, ‘’Nadhani si mbali; afadhali na tufuate njia, haya tuondoke.’’
Basi tulipokwisha nawa katika mto tuliondoka tena. Kwa mwendo wa maili moja tulisafiri juu ya miamba na theluji, na tulipokwisha panda kilima kidogo tuliona njia tukaifuata.
Njia ilikuwa imara ya ajabu mno, na upana wake ulipata kadiri ya hatua thelathini, lakini haikuendelea, maana tulitembea hatua mia moja tukaona imefifia kabisa, imefunikwa kwa miamba.