Tresor Mandala
JF-Expert Member
- Aug 20, 2010
- 40,905
- 86,203
Sitoki hapa,Nina version ya kingereza ,ahsante sana na hongera kwa kutuletea uhondo huuKaribu sana mkuu! Old is gold
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sitoki hapa,Nina version ya kingereza ,ahsante sana na hongera kwa kutuletea uhondo huuKaribu sana mkuu! Old is gold
Pamoja mkuuSitoki hapa,Nina version ya kingereza ,ahsante sana na hongera kwa kutuletea uhondo huu
Angalia tu usijegeuka kuwa spoiler tu...Unanikumbusha mbali sana, mbele huko malkia wawili ndugu ,Niko sitoki nimeweka kambi
Ah mzee simba unajua mahali pa kushika na wakati wa kushika! ndio makumazahn vita vitakuwa vyema.Karibu sana mkuu! Old is gold
Naaaam mkuu, wacha niifaidi apa kwa uzuriSURA YA TATU
Tulifunga mtumbwi wetu pamoja na mtumbwi ule mwingine kwa kipande cha kamba kilichobaki, tukakaa tukingojea mapambazuko, na kufurahi kwa vile tulivyookoka.
Baada ya kukesha sana, kukapambazuka, nami sijapata kupendezwa kuuona mwangaza kama nilivyopendezwa kuuona siku ile, ingawa uliangaza juu ya kitu cha kutisha ndani ya mtumbwi wangu.
Maana, pale chini katika mtumbwi Yule maskini askari alikuwa amelala na sime imesimama kifuani mwake, na ule mkono uliokatwa ungali umeishika sime.
Sikuweza kuvumilia kumtazama zaidi, basi, nililivuta ndani lile jiwe lililokuwa nanga yetu, nikamfungia Yule askari aliyeuawa, nikamtumbukiza majini, akazama mpaka chini.
Kisha, tulitoa mtu mmoja katika mtumbwi mwingine tukamweka katika mtumbwi wangu, tukaendelea tena katika safari yetu, wote tumeshikwa na majonzi, wala hatukuweza kuona raha kwa kufikiri juu ya mambo ya mbele yetu, ila tulitumaini kufika misioni kabla ya kuingia usiku.
Hapo mambo yalizidi kuwa mabaya, maana jioni ilipokaribia, ilianza kunyesha mvua tukalowa kabisa, tena ikawa lazima pengine kukumba maji katika mitumbwi, na kwa kuwa upepo ulitulizwa na mvua, matanga hayakufaa kitu, ikawa lazima tupige kafi kadiri tulivyoweza.
Saa tano tulishuka mahali pa wazi kando ya mto kwa upande wa kushoto, na kwa kuwa mvua ilipungua kidogo, tulivua samaki tukazibanika motoni. Hatukuthubutu kwenda kutafuta wanyama.
Saa nane tuliondoka tena, tukachukua akiba ya samaki wa kuchoma na baada ya kitambo ilianza kunyesha tena mvua nyingi kuliko kwanza.
Tena, tulianza kuona shida zaidi kwenda mbele mtoni kwa sababu ya miamba mingi, na mafungu ya mchanga, na nguvu ya mkondo wa maji ilizidi, basi, ilikuwa dhahiri ya kuwa hatutawahi kuifikia nyumba ya Bwana Mackenzie kabla usiku haujaingia na habari hizi zilizidi kutusumbua.
Ingawa tulivuta kafi kadiri tulivyoweza, lakini hata hivyo hatukuweza kwenda mbele zaidi ya maili moja kwa saa moja, na ilipofika saa kumi na moja jioni, tulikuwa tumechoka taabani, na kwa kadiri tulivyoweza kukisia, nyumba ya misioni ipo mbali mwendo wa maili kumi.
Basi, tulianza kutengeneza mambo kadiri tulivyoweza tayari kwa usiku.
Baada ya mambo yaliotokea jana, hatukuthubutu kufanya kambi nchi kavu, na hasa kwakuwa kingo za mto Tana zimefunikwa na vichaka vinene vya kutosha Wajivuni elfu tano kujificha humo wasionekane, na kwanza tulifikiri tutakuwa hatuna budi kukaa tena katika mitumbwi.
Lakini kwa bahati, tuliona kisiwa kidogo, kadiri ya upana na urefu wa yadi kumi na tano, katikati ya mto. Basi, tulipiga kafi mpaka kufikia, tukaiegesha mitumbwi yetu, tukashuka na kutengeneza mambo kadiri tulivyoweza.
Mvua ilizidi kunyesha, tukaona baridi hata ndani ya mifupa yetu, wala hatukuweza kukoka moto.
Lakini mvua ilitufariji kwa neno moja, yaani Wakazi walituambia kuwa Wajivuni hawata tushambulia wakati wa mvua kwa sababu inawasumbua sana. Tulikula kipande cha samaki kilicholowa maji, isipokuwa Umslopogaas, maana yeye kama Wazulu wote, hali samaki.
Ndipo ulipoanza usiku wa taabu kupita zote ninazozikumbuka, isipokuwa taabu ya usiku ule ambao sisi watu weupe watatu tulivumilia pamoja tulipokuwa karibu kuangamia kwa baridi na theluji juu ya Ziwa la Sheba katika safari yetu ya kuiendea nchi ya Wakukuana.
Usiku ulikuwa kama hauna mwisho, na mara mbili tatu nilifikiri labda askari wetu wawili watakufa kwa maji na baridi na taabu. Bila shaka wangalikufa kama tusingaliwapa divai mara kwa mara.
Niliweza kuona ya kuwa hata Yule mzee shupavu Umslopogaas naye pia anaona maumivu, ingawa alikaa kimya tu, wala si kama wale Wakazi waliolalamikia hali zao bila kunyamaza. Mambo yalizidi kuwa mabaya kwenye saa saba ya usiku tuliposikia tena mlio wa bundi.
Basi, tukajifanya tayari kujitetea kama tukishambuliwa, lakini nadhani tungalishambuliwa wakati huo, tungalishindwa upesi.
Lakini labda mlio ulikuwa wa bundi hasa, au labda Wajivuni nao waliona taabu hata hawana moyo kutushambulia. Kwa vyo vyote hatukuwaona kabisa.
Hatimaye kulipapazuka na ukungu ukatambaa juu ya uso wa maji, na kulipokuwa kweupe, kukatakata, na mvua iliacha kunyesha, ndipo jua tukufu lilipochomoza, tukajivuta miguu, tukaenda tukasimama katika joto la jua, tukashukuru.
Hahaah poaNaaaam mkuu, wacha niifaidi apa kwa uzuri
Poa mkuuMkuu shukurani kwa kazi safi. Uwe unatushitua ukiweka.
Pamoja mkuuNext unitag niko nangojea uhondo huu si mchexo
Tater sijakuona mtaa huu
Naam [emoji39] [emoji39]Naweza kufahamu kwa nini watu wengine wasiostarabika huliabudu jua, na hasa kama hali ya maisha yao huwalazimisha pengine kuvumilia mvua na baridi kali.
Baada ya kupita nusu saa, tulikuwa tukiendelea tena vizuri kwa msaada wa upepo mzuri. Mioyo yetu ilichangamka kwa kuuona tena mwanga wa jua, tukawa tayari kuzicheka shida na hatari zilizotuelemea jana.
Basi, hivyo tuliendelea kwa furaha mpaka kadiri ya saa tano, na hapo tulipoanza kufikiri kushuka kama ilivyokuwa desturi yetu ili tujaribu kuwinda wanyama tupate kula, mara mto ulipinda, tukaona nyumba imara ya Kizungu iliyozungukwa na baraza imesimama vizuri juu ya mwinuko.
Nyumba ilikuwa imezungukwa na boma la mawe, na handaki nje ya boma.
Karibu na nyumba palikuwa na mti mrefu sana, namna ya msunobari.
Mimi nilikuwa wa kwanza kuiona ile nyumba, nami sikuweza kujizuia nisipige ukelele wa furaha, na wenzangu nao na watumishi wetu pia wakapiga ukelele kadhalika.
Sasa hatukuwa na nia ya kusimama tena. Tukasukuma mbele kwa nguvu, lakini ingawa nyumba ilionekana kama I karibu, ilikuwa mbali kwa kuufuata mwendo wa mto, wala hatukuifikia mpaka saa saba.
Ndipo tulipojiona chini ya mwinuko iliposimama ile nyumba.
Tuliisogeza mitumbwi, yetu mpaka kando ya mto, tukashuka, tukawa katika kuikweza nchi kavu ndipo tulipoona watu watatu waliovaa mavazi ya Kizungu wanatujia kwa haraka wakipita katikati ya miti.
Bwana Good aliwachungulia kwa rodi yake, akasema, ‘’Bwana mmoja, na Bibi mmoja na mtoto mwanamke mmoja, wanakuja kistaarabu karibu na bustani ya kistaarabu kutulaki katika mahali kama hapa kweli hili ni jambo la ajabu kupita yote!’’
Basi, walitukaribia. Yule Bwana Mckenzie alikuwa mtu mwembamba, mwenye mvi, na uso wake ulikuwa wa kupendeza, akasema, ‘’Mhali gani mabwana, natumaini hamjambo?
Watu wangu waliniambia tangu saa moja ya kuwa waliona mitumbwi miwili inakuja mtoni, basi, tumekuja kuwalaki.’’ Na Yule bibi, akasema, ‘’Tumefurahi sana kuonana tena na watu weupe.’’
Tukavua kofia zetu kuwaamkia, tukawajulisha tu nani. Kisha, Bwana Mackenzie akasema, tumefurahi sana kuwaona. Mwaka mzima umepita tangu alipofika hapa mtu mweupe wa mwisho aliyetujia.’’
Huku nyuma tulikuwa tukiupanda ule mwinuko ambao sehemu ya chini yake ni mashamba ya mahindi na maboga na viazi, na vyakula vinginevyo.
Wenyeji wengine, watu wa misioni walikuwa wamejenga nyumba zao katika mashamba hayo.
Katikati ya mashamba palikuwa na barabara, na kando yake ilikuwapo michungwa mingi iliyojaa machungwa.
Tokea hapo nimependa sana bustani, na nilipoiona ile ya Bwana Mackenzie nilifurahi sana, nikasema, ‘’Lo, bwana, tazama jinsi ilivyo nzuri bustani yako’’.
Akajibu, ‘’Kweli, ni bustani nzuri sana, wala si ajabu kwa sababu nimefanya kazi nyingi humo, lakini pamoja na hivyo tabia ya nchi hii ni nzuri, na miti huota vizuri sana.’’
Basi, tukaendelea, tukafika kwenye ile handaki ambayo upana wake ulikuwa futi kumi, imejaa maji, na ng’ambo yake palikuwa na boma la mawe urefu wa kwenda juu futi nane, lina vitundu huko na huko vya kupitishia bunduki.
Na juu yake pametapakaa mawe makali na vigae vilivyosakafiwa katika mgongo wa ukuta.
Bwana Mackenzieakalielekezea kidole chake, akasema, ‘’Hii ndiyo kazi yangu iliyo kubwa, au tuseme hii pamoja na kanisa lililojegwa nyuma ya nyumba.
Ilichukua mimi na wenyeji ishirini muda wa miaka miwili kuichimbua ile handaki, na kulijenga boma, lakini kabisa sikuweza kuona ni salama, mpaka kazi zilipokwisha.
Sasa ninaweza kujitetea juu ya watu wakali wote wa katika nchi ya Afrika, maana chemchem inayojaza handaki maji imo ndani ya boma juu ya mwinuko, nayo hububujika siku zote, nami kila mara ninayo akiba ya chakula nyumbani cha kutosha miezi minne.’’
Barikiwa mkuuChakula kilipokuwa karibu kwisha, niliomba ruhusa niondoke mezani. Nilitaka kwenda nje, nikafikiri juu ya mambo.
Nikaenda barazani, nikakitia moto kiko changu, nikakaa katika kiti karibu na mwisho wa baraza.
Nilikuwa nimeketi muda wa dakika sita saba, nikafikiri nimesikia mlango wa ukuta wa boma unafunguliwa, Nikatazama huko nisione kitu, nikafikiri ni mawazo yangu tu, Ulikuwa usiku wa giza, na mwezi haujapanda juu bado.
Baada ya kupita dakika moja tena, kitu kama tufe kilianguka juu ya sakafu ya baraza, kikaviringika kikapita mahali nilipokuwa nimekaa.
Kwanza sikuondoka, nilikaa nikifikiri ni kitu gani. Kisha nilifikiri labda ni mnyama mdogo. Ndipo wazo jingine likanijia, nikaondoka hima.
Kile kitu kilikuwa kimelala mbali kidogo, nikaunyosha mkono wangu karibu nacho, kisijongee, basi ni dhahiri si mnyama. Nikakigusa. Kilikuwa laini chenye uvungu na kizito. Nikakitwaa kwa haraka, nikakiinua katika mwangaza wa nyota. Kilikuwa ni kichwa cha mwanadamu ndio kwanza kimekatwa!
Mimi ni mtu aliyezoea mambo mengi, wala sichafukwi na moyo upesi, lakini lazima nikiri ya kuwa nilipokitazama kichwa kile, moyo wangu ulielea, nikataka kutapika. Kilifikaje hapa? Cha nani? Nilikiweka chini nikaukimbilia ule mlango mdogo.
Sikuweza kuona kitu wala kusikia mtu. Nilianza kutoka na kwenda katika giza nene, lakini nilikumbuka ya kuwa nikifanya hivyo nitakuwa ninajiweka katika hatari ya kuchomwa mkuki.
Nikarudi, nikaufunga mlango, nikatia komeo. Kisha, nilirudi barazani, nikamwita Sir Henry kwa sauti ambayo nilijaribu kuifanya kama hakuna jambo lililotokea.
Lakini naona sikuweza, maana si Sir Henry tu aliyetoka, ila Bwana Good na Bwana Mackenzie, wote wakaondoka mezani wakaja nje mbio. Bwana Mackenzie akauliza, ‘’Kuna nini?’’ Basi, ikawa sina budi kuwaambia.
Rangi ya uso wa Bwana Mackenzie ilibadilika, ikawa kama ya mfu. Tulikuwa tumesimama nje ya mlango wa sebule, na humo ndani mlikuwamo taa.
Akakishika kile kichwa kwa nywele zake, akakiinua ili akione vizuri, akasema, ‘’Ni kichwa cha mtu mmoja katika wale waliofuatana na Flossie.
Namshukuru Mungu si chake!’’ Sote tulisimama tukatazamana, tumetunduwaa, lakini tufanyeje! Hapo mlango ukabishwa, na sauti ikalia, ‘’Fungua baba, fungua!’’
Basi, tuliufungua mlango, na mtu alijiingiza amejaa hofu. Alikuwa mmoja wapo wa watu wale tuliowatuma kupeleleza habari.
Akasema, ‘’Baba yangu Wajivuni wanatujia! Jeshi kubwa limepita kuzunguka mwinuko, na sasa linaliendea lile boma la mawe la zamani la ng’ombe lililoko karibu na mto. Baba yangu, ujikaze moyo! Katikati yao nilimwona Yule punda mweupe na juu yake amekaa bibi Flossie.
Mjivuni mmoja alikuwa anamwongoza punda, na yaya alikuwa anatembea ubavuni analia. Sikuwaona wale watu waliofuatana nao asubuhi.’’
Bwana Mackenzie aliuliza kwa sauti iliyopwaya ‘’Mtoto yu hai?’’
Yule mtu akajibu, ‘’Ni mweupe kama theluji, lakini hakudhurika, baba yangu. Walipita karibu sana nami, nikauona uso wake.’’
Bwana Mackenzie akaguna, akasema, ‘’Mungu amsaidie yeye na sisi pia.’’
Nikauliza, ‘’Wako Wajivuni wangapi?’’
Akajibu, ‘’Zaidi ya mia mbili na hamsini.’’
Tukatazamana tena, tukaulizana kimoyo moyo, ‘’Tufanyeje?’’
Ndipo tuliposikia sauti inalia kwa uthabiti nje ya mlango. Ikasema, ‘’Fungua mtu mweupe, fungua mlango! Nimetumwa kusema nawe.’’
Umslopogaass alikimbilia ukutani, akainyosha mikono yake mirefu akajiinua aweze kutazama juu ya ukuta, akasema, ‘’Namwona mtu mmoja tu. Anazo silaha, tena amechukua kapu mkononi mwake.’’
Nikasema, ‘Fungua mlango,’’ Umslopogaas, akatwae shoka lako ukasimame hapa karibu na mlango. Mwache mtu mmoja tu apite ndani, mwingine akijaribu kuingia, muue.
Basi, mlango ulifunguliwa. Katika kivuli cha ukuta Umslopogaas alisimama ameliinua shoka lake juu tayari kupiga.
Hapo mwezi ukaangaza. Kukawa kimya muda kidogo, kisha, Mjivuni mmoja akaingia amevaa mavazi ya vita kama yale niliyoeleza, tena, amechukua kapu kubwa.
Mwezi uliung’arisha mkuki wake alipokuwa akijongea. Alikuwa mtu mshupavu, mwenye umri upatao miaka thelathini na mitano.
Alipofika karibu alisimama, akaliweka lile kapu chini, akaukita mkuki wake katika ardhi. Ukasimama wima. Akasema , ‘’Tuongee, Tarishi wa kwanza tuliye mtuma hakuweza kuongea,’’ akaonyesha kile kichwa kilicholala barazani kitu cha kutisha katika mwangaza wa mwezi.
‘’Lakini ninayo maneno ya kusema kama ninyi mnayo masikio ya kuyasikia. Tena, nimeleta zawadi.’’ Akaonyesha lile kapu, akacheka kwa ufedhuli na kiburi kisichoweza kuelezeka, na hata hivi hatuna budi kumsifu, hali amezungukwa na adui.