Hafizi Konkoni afukuzwe na viboko 30

mwehu ndama

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2019
Posts
630
Reaction score
2,151
Kila nikilitizima hili striker la boli HAFIZI Konkoni kutoka nchini Ghana linalokipiga ndani ya Yanga napata wasiwasi juu ya uwezo wake wa kutuvusha Yanga sc kutoka hapa tulipo kutupeleka hatua inayofuata.

Mimi ni muumini wa kuheshimu maamuzi ya makocha na inapofikia hatua kocha au benchi la ufundi halimuamini mchezaji kiasi cha kumpa dakika 7 za mwisho tena katika baadhi ya mechi, huku uwezo wake katika hizo dakika kiduchu anazopewa hazitendei haki jumlisha mapungufu kibao ya, kimsingi kama ball control na passing, moja kwa moja mchezaji huyo huwa ninamuona ni wa ovyo tu kama ilivyo kwa HAFIZI Konkoni

YANGA tunapaswa kuachana na tapeli hili la soka toka Ghana na ikiwezekana AFUKUZWE kambini leo hii, na achapwe VIBOKO 30, kwa udanganyifu sababu huyu si mwanasoka bali ni mcheza kamali toka Ghana.

 
Jamaa alipata kama clear chances 2, alichofanya mamaaeeee. Umbo nyumba uwezo kisoda.
 
Asitimiliwe tatizo ni kocha mdau mkereketwa mwenye vision ya soka aliona tatizo lipo wapi
 
Mimi naona hapewi muda sana kama vipi apewe mechi nzima
 
Alipewa gemu dhidi el mareikh ya Sudan jamaa alicheza hovyo sana, bora hata ditram nchimbi kuliko hili jangili
Anapewa muda kama huu tu dakika ya 82 sasa hapo tutamlaumu bure apewe mechi nzjma kama kina skudu
 
huyu nadhani amekuwa frustrated, anahitaji kusaidiwa kama alivyosaidiwa yule rasta wa simba ili arudi. kwa sasa pale anaonekana hajui kitu kabisa hadi arudi kwenye hali yake. shida ni nani wa kumsuribi sasa wakati tunamlipa mshahara acheze vizuri. hata sub yake haikuwa na faida yeyote kabisa.
 
Alicheza ni sawa na kuwa na timu pungufu, afadhali muwe pungufu mtabanana kuliko kukaa na hilo flop.
 
Naskia kaitwa kikosi Cha taifa Ghana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…