Hai, Kilimanjaro: Komandoo Adamoo na wenzake wazawadiwa ng’ombe dume kila mmoja

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426

Makomandoo hao ambao ni Walinzi wa Freeman Mbowe kwa kinachoitwa ( VIP PROTECTION ), waliokamatwa na kuwekwa Gerezani kwa miezi mingi, leo wamefika Hai Mkoani Kilimanjaro pamoja na Mtuhumiwa mwenzao Mbowe, aliyeenda huko kutoa Sadaka ya Shukrani kwenye Kanisa la KKKT Nshala Machame.

Pamoja na kuzawadiwa ng'ombe dume wakubwa kabisa kila mmoja, pia wamepewa BAHASHA NZITO NZITO SANA kila mmoja , ambazo ndani yake haifahamiki mmewekwa nini.

Zawadi hizo zote zimetolewa na Wazee wa Machame kama sehemu ya Shukrani zao kwa Makomandoo hao kwa Uaminifu wao kwa Mbowe kutokana na kinachoitwa Kukataa kutoa Ushahidi wa Uongo ili ionekane Mbowe ni Gaidi hata baada ya kuteswa sana kuliko karibia kifo , uaminifu wa Makomandoo hawa umewapa heshima kubwa sana mbele ya Jamii.
 
Komandoo na zawadi ya ng'ombe haya acha Leo tuweke akiba ya maneno. Niko machine tools hapa nasubiri usafiri nikale pombe za tambiko
 
Mungu arudishe haki na upendo miongoni mwa jamii ya watanzania bila kujali itikadi za vyama.
Wengine wamezoea dhuluma kiasi kwamba haki ikitendeka wao wanaona ndio kama wamedhulumiwa!!
 


wengine wamekipigania chama tawala ila leo hii wananyang'anywa mijengo yao waliopewa kama zawadi dah!!

Bora kuipigania chadema, unapewa ng'ombe mzima unamla anaisha na hela unaendatumia unavyojua. Zawadi zao hazinyang'anyiki
 
Komandoo na zawadi ya ng'ombe haya acha Leo tuweke akiba ya maneno. Niko machine tools hapa nasubiri usafiri nikale pombe za tambiko
Tena ukanywee kwenye masale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…