Haitoshi, Job Ndugai ajiuzulu na ubunge pia!

Gharama za India atalipiwa na Vicoba?

Kwa maradhi yanayomsibu siku hizi tuna wataalam watamtibu hapa hapa hospitali ya Mzena!!! Kwenda India ulikuwa mradi wake wa kupiga hela hakukuwa na ulazima
 
😀😀😀😀😀
 
Hawezi kuwa na msaada Kwa watu wa Kongwa kutokana na pride yake hivyo nashauri ajiuzulu!
Ndugai ataweza kweli kuomba dk 10 kuelezea kero za Kongwa???
 
alijitangaza kuwa ana faili milembe je kwanini agombee tena badala ya kurudi kutibiwa kwanza? Au anadhani tumesahau? au kwa kuwa bwana yule alinadi anawapenda vichaa kama yeye? Huu sasa ni wakati wa vichaa na waliojitia ukichaa kung'atuka ili nchi iende na tutafute namna ya kupata katiba mpya ambayo haitawaleta vichaa meza kuu
 
Kweli kabisa mkuu Bulesi kama kweli anataka kulinda credibility yake kisiasa akae pembeni kwanza ausome mchezo. Akiwa bench ndipo atausoma mchezo vizuri zaidi kuliko kubakia ndani ya ulingo huku akibakia kuwa mnyonge.
 
Mbona kwenye taarifa yake amewaaga na wananchi wa jimbo lake la kongwa?hawezi akaendelea kuwa mbunge tena!!
Basi akifanya hivyo atakuwa amefanya jambo la busara mno ✍️ 👏👏👏👏👏👏👏👏
 
Ugumu pekee atakaopata ni kurudi bungeni mle kama mbunge wa kawaida na kutakiwa kufuata taratibu zote kwa mujibu wa sheria na maagizo ya spika/naibu spika. Kiutaratibu inawezekana, ila kiubinadamu ni ngumu kidogo
 
Ugumu pekee atakaopata ni kurudi bungeni mle kama mbunge wa kawaida na kutakiwa kufuata taratibu zote kwa mujibu wa sheria na maagizo ya spika/naibu spika. Kiutaratibu inawezekana, ila kiubinadamu ni ngumu kidogo
Shida ni kwamba ni Mbunge wa CCM yani atakuwa zoba wa karne😅 maana hata kumtia spana mama hawezi atabakia kuskilizia posho tu!
 
Shida ni kwamba ni Mbunge wa CCM yani atakuwa zoba wa karne😅 maana hata kumtia spana mama hawezi atabakia kuskilizia posho tu!
Hili ndilo tatizo la wabunge wachumia tumbo. Yupo tayari kudhalilika ndani ya bunge ilmradi mkono uende kinywani. Uchumia tumbo haujawahi kumuacha mchumiaji salama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…