Haji Bin Manara. Ni nini Kinamsibu?

Haji Bin Manara. Ni nini Kinamsibu?

Haji ataendelea kuwepo sana kwenye mpira kwakua anaupenda na unampa rizki. Huu upepo utapita na ata huu uongozi utaondoka na yeye ataendelea na kazi zake...
Umeandika upuuzi tupu.....

Haji ni nani katika soka la nchi mpaka ifike kipindi sheria ziwe juu yake?acheni kudekadeka ,nyie ndio mnamharibu huyo mpuuzi.

Soka la nchi hii limepitia kipindi kigumu sana huko nyuma mpaka kuitwa KICHWA CHA MWENDAWAZIMU sababu ni watu kama hao kina haji maneno maneno mengi fitna kibao ilimradi kurudishana nyuma,leo hii kipindi cha KARIA timu zetu zimepiga hatua kubwa sana kuanzia ngazi za vilabu mpaka taifa kwa soka la kiume mpaka la kike.

Anayemsapoti huyu amphibia mimi namuona mpuuzi kama wapuuzi wengine. Ulaya hakuna watu wapuuzi kama hao kina haji katika soka lao na ndio maana wanaendelea kila siku,

Haji ni kirusi tupa kule
 
Moja Kati Ya Interviews za ajabu ambazo amewahi kufanya ni hii ambapo amefikia hatua Kusema kuwa Yeye Hawezi tena Kuizungumzia Taifa Stars......
Kigogo aliwahi kumchafua hiyo jamaa!

Kama alichomchafua ni sahihi basi ana depression yenye kina kirefu from childhood trauma!!!
 
Haji atabaki kua Haji iwe unataka au hutaki iwe ana kuudhi au kukufurahisha.

Hatma ya binadamu haijawahi kuwa mikononi mwa binadamu.

Hai kwasasa amefungiwa ila ukweli ulivyo baada ya karia kuondoka ata mwacha haji katika soka ni swala la muda tu.

Kuhusu Tanzania kuwa kichwa cha chizi ilo litabaki kuwa hivyo kwakua hakuna mkakati wa serikali kujiondoa uko.
Wachezaji wa michezo yote wana andaliwa mashulaeni na waalimu wana andaliwa kwa bajeti ya serikali.

Serikali inatakiwa ivi support vituo vichache vilivyopo vya michezo kwa fedha na rasilimali ya watu wenye ujuzi.

Matokeo ya hivi vilabu vikubwa kufanya vizuri ni fedha za watu binafsi na wakijiondoa soka letu linabaki kama lilivyo kwakua halina uti wa mgongo.

Punguza Mbumbumbu na kutambua hivi vitu vidogovidogo ivi vilabu havina capital ya kujiendesha.
 
Haji ataendelea kuwepo sana kwenye mpira kwakua anaupenda na unampa rizki. Huu upepo utapita na ata huu uongozi utaondoka na yeye ataendelea na kazi zake...
Umeongea ukweli Sana na naamini Karia na genge lake wataondoka na Haji atarudi juu zaidi maana jamaa ana ushawishi mkubwa kuliko wao so chuki na wivu ndo vinawatesa Tu Ila mpaji ni Mungu
 
Haji awe na subira ao jamaa hawana muda wataondoka na maisha yake katika soka yatarejea.
Yaani Haji asubiri hadi akina Ali Kamwe waondoke, sasa si atakuwa ameshazeeka?
 
Umeongea ukweli Sana na naamini Karia na genge lake wataondoka na Haji atarudi juu zaidi maana jamaa ana ushawishi mkubwa kuliko wao so chuki na wivu ndo vinawatesa Tu Ila mpaji ni Mungu
Atarudi wapi? Ihefu? Maana hata pale Ihefu kuna dogo anakimbiza balaa.
 
Haji Jua Linazama....

Maji ya Jioni.....

Kukimbizana na Kina Ahmed Ally na Ally Kamwe hataweza....
Na hicho ndicho kinamtia hofu
 
Tuwapeleke watoto shule ili wasiwe kama manara
Antonia nugaz kafanyiwa fitna na manara ila hajawahi kulalamika popote kwenye media kuhusu kuondoka kwake yanga

Hasani bumbuli yupo zake CRDB anakula hela

Jerry muro alikula ukuu wa wilaya sasa taka dini anajiona yeye ndio kila kitu amebakia kutukana na kulalamika tu manara tv imefeli kwa mdomo wake mchafu mpaka wanasiasa wanamuogopa alienda dodoma akapata kura moja akakimbia siku hyo hyo kabla ya majibu kukwepa aibu kiufupi takadini amekwama simba hawezi kurudi yanga kashaharibu AZAM hawamtaki amechanganyikiwa waswahili wanasema ujanja mwingi mbele kiza.
 
Haji atabaki kua Haji iwe unataka au hutaki iwe ana kuudhi au kukufurahisha.
Hatma ya binadamu haijawahi kuwa mikononi mwa binadamu...
Kwa karia si ndio alimfungulia manara baada ya kupigwa mvua leo hii karia amekuwa mbaya kwa manara kweli binadamu hawana shukran tatizo la manara anaona kila mtu anamuonea
 
T
Moja Kati Ya Interviews za ajabu ambazo amewahi kufanya ni hii ambapo amefikia hatua Kusema kuwa Yeye Hawezi tena Kuizungumzia Taifa Stars...!

Taifa Stars...! Nini tena atazungumzia?

Akaisemee Kenya? Uganda? UK? au USA..?

Wapo Watu Wanatafuta nafasi Waizungumzie Nchi yao Kupitia Stars, bado Hawajaipata.

Kwamba yeye Sio Mtanzania tena hajali Tanzania yupo Kundi gani, kapangwa na nani makundi AFCON haimuhusu.

Kwanini haya maneno Yanamtoka Kipindi hichi?

Najaribu kumtafakari.

Yawezekana kuna kitu anakiona kwa Sasa. Bila Shaka baada ya Kupumzishwa kwa Kufungiwa alikuwa na Mategemeo kuwa Vitengo vya habari vya Vilabu alivyovihudumu Vitapwaya. Na atakumbukwa sana na Watu
Kum miss, lakini haijawa hivyo. Maisha yameendelea, Na Soka La Bongo ndo Kwanza Linazidi Kupanda.

Mazingira ya Sasa yamebadilika Kabisa..! Vijana waliopewa mikoba Yake , Sio tu Viatu VimewaTOSHA bali Wamepitiliza Matarajio Kwa Kuwa Wabunifu Zaidi yake.

Hamasa Kipindi chake Zilikuwa Zinaishia Kutoa Slogans na kufanya Media tours Kwenye Vituo Viwili vitatu vya Media.

Hawa madogo wa Vitengo vya habari vya Simba na Yanga Media tours Wanazifanya, Lakini Wanaingia Mitaani na Vispika, Kubrand Wachezaji, Beach soka baina ya Matawi, kampeni za Kibegi...nk. zote hizo Zimeeeenda mbaya..!

Halafu Manara Akizingatia Umri Unamtupa Mkono, Wakati madogo ndo Kwanza Wanaanza Carrier zao...! Usipagawe We nani?

Huyu Mzee kaona anasahaulika, Kwanini asipaniki?

Wadau wanajiuliza Haji Bin Manara ni nini Kimemsibu?
Tuwekee clip yake!! Si kila mmoja ameiona!!
 
View attachment 2786043

Kila niliangalia Hii picha Huwa namtafakari sana Haji
..
IMG-20231028-WA0000.jpg
 
Huyu jamaa hakufaa kabisa kuwa msemaji wa timu.

Anaongea pumba sana mfano alivyosema kombe la looser ni pumba ya mwisho kabisa.

Kilichombeba ni jina la familia na sio kingine
 
Back
Top Bottom